neno la uzima
DESCRIPTION
NENO LA UZIMA. Mei 2012. "Nimekuja kuwasha moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi!” (Lk 12:49). Katika maandishi ya kiyahudi moto unaashiria neno la Mungu lililotamkwa na nabii. Lakini pia linaashiria hukumu ya Mungu anayetakasa watu wake kwa kupita kati yao. - PowerPoint PPT PresentationTRANSCRIPT
NENO LA UZIMA NENO LA UZIMA
Mei 2012Mei 2012
"Nimekuja kuwasha moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi!”
(Lk 12:49).
Katika maandishi ya kiyahudi moto
unaashiria neno la Mungu
lililotamkwa na nabii. Lakini pia
linaashiria hukumu ya
Mungu anayetakasa
watu wake kwa kupita kati
yao..
Tunaweza kusema hivyo kwa neno la Yesu: linajenga, na kwa wakati huo huo linabomoa kila kisicho thabiti, kila kinachotakiwa kushuka, kila kilicho batili, na kuacha tu
ukweli ukisimama.
Yohani Mbatizaji alisema:
“Atawabatizeni kwa Roho
Mtakatifu na moto” (Lk 3:16), akitabiri ubatizo
wa Kikristo uliozinduliwa siku
ya Pentekoste kwa kushuka
Roho Mtakatifu na kuonekana
ndimi za moto (rej Mdo 2:3).
Hii ni kazi maalum ya
Yesu: kuwasha moto duniani, kuleta Roho Mtakatifu na
nguvu zake za kufanya upya na
kutakasa.Huo ndio utume wa Yesu: kutupa
moto duniani, kuleta Roho Mtakatifu pamoja na
nguvu yake ya kufanya yote upya na ya kutakasa.
"Nimekuja kuwasha moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi!”
(Lk 12:49).
Yesu anatupatia Roho. Lakini Roho Mtakatifu anafanyaje kazi?
Anatujaza upendo na anataka tutunze moto huu wa upendo ukiwaka mioyoni mwetu.
Je, ni aina gani ya upendo? Si wa kiulimwengu, upendo usio na kikomo. Ni upendo wa kiinjili.
Unaopenda wote kama Baba wa mbinguni anayewaangazia jua lake waovu na wema na
kuwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki, wakiwemo adui (rej Mt 5:45).
Ni upendo usiosubiri wengine wachukue hatua ya kwanza, bali unakuwa daima
wa kwanza kupenda.
Ni upendo unaojifanya mmoja na kila mmoja: unateseka na kufurahi pamoja nao, ukishiriki hofu na matumaini
yao. Na ikibidi, unagusika, kwa matendo. Kwa hiyo siyo tu upendo wa kihisia unaoelezwa kwa maneno matupu.
Ni upendo unaoongozwa na Kristo ndani ya jirani, kwa kuzingatia maneno yake: ‘Ulinitendea mimi” (Mt
25:40).Ni upendo unaopelekea upendano.
Kwa kuwa upendo huu unaonekana, ni udhihirisho wa maisha yetu ya kiinjili, unasisitiza na kushuhudia neno
- ushuhuda tunaoweza na tunaotakiwa kutoa ili kuinjilisha.
"Nimekuja kuwasha moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi!”
(Lk 12:49).
Upendo ni kama moto – cha muhimu ni kuutunza.
Na moto lazima uunguze kitu daima. Na zaidi ya yote lazima uunguze ubinafsi wetu, na
unafanikiwa kwa kuwa kwa kupenda tunaelekea nje yetu: aidha kuelekea Mungu kwa kufanya
mapenzi yake, au jirani kwa kuwasaidia.
Hata moto mdogo, ukiwashwa unaweza kuwa mlipuko – ule mlipuko wa upendo, amani na
undugu wa wote ambao Yesu alileta duniani.
"Nimekuja kuwasha moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi!”
(Lk 12:49).