kimetolewa na kuchapishwa na: bilal muslim mission … wa uislam… · haj sayyid saeed akhtar...

100
Kimeandikwa na: Kimetafsiriwa na: Mallam Dhikiri U.M. Kiondo Kimetolewa na Kuchapishwa na: BILAL MUSLIM MISSION OF TANZANIA S.L.P. 20033, Dar-es-salaam Tanzania

Upload: ngominh

Post on 12-Feb-2018

369 views

Category:

Documents


10 download

TRANSCRIPT

Kimeandikwa na:

Kimetafsiriwa na: Mallam Dhikiri U.M. Kiondo

Kimetolewa na Kuchapishwa na: BILAL MUSLIM MISSION OF TANZANIA

S.L.P. 20033, Dar-es-salaam Tanzania

BILAL ALLAMAH RIZVI

2

Haki ya Kunakili Imehifadhiwa na: Bilal Muslim Mission of Tanzania

ISBN 9976 956 38 x

Toleo la Kwanza 1980: Nakala 2,000 Toleo la Pili 1983: Nakala 5,000 Toleo la Tatu 1985: Nakala 2,500 Toleo la Nne 1998: Nakala 2,000 Toleo la Tano 1989: Nakala 2,000 Toleo la Sita 1995: Nakala 2,000 Toleo la Saba 1999: Nakala 2,000 Toleo la Nane 2002: Nakala 2,500

Kimetolewa na kuchapishwa na:

BILAL MUSLIM MISSION OF TANZANIA S.L.P. 20033

DAR-ES-SALAAM TANZANIA

MUNGU WA UISLAMU

3

YALIYOMO

1. Dibaji 5 2. Utangulizi 6 3. Historia Fupi ya Mtunzi wa kitabu Hiki 7

Sehemu ya Kwanza 4. Sura ya 1: Imani ya kuwepo Mungu 13 5. Sura ya 2: Kuwepo au kutokuwepo 14 6. Sura ya 3: Chanzo cha ulimwengu 16

7. Sura ya 4: Sifa za kitu cha milele 18 8. Sura ya 5: Jauhari ni kitu cha milele 22 9. Sura ya 6: Jauhrari ina mwanzo na mwisho 23 10. Sura ya 7: Dhana mbili 26 11. Sura ya 8: Jauhari si chanzo cha uhai 28 12. Sura ya 9: Imani ya Mungu mmoja dhidi ya Ulahidi 29 13. Sura ya 10: Mazungumzo 31 14. Sura ya 11: Dini dhidi ya mawazo ya Bwana Darwin 33 15. Sura ya 12: Jinsi watu wenye fikara za Bwana Darwin walivyopotea 37 16. Sura ya 13: Hoja za Bwana Rusell 40 17. Sura ya 14: Ulimwengu uliumbwa kwa bahati tu bila ya muumba? 46 18. Sura ya 15: Njia ya usalama kwa Muaginosi 57 19. Sura ya 16: Huu ulimwengu ni ushahidi

wa kuwepo kwa Mungu mmoja 60

BILAL ALLAMAH RIZVI

4

20. Sura ya 17: Sababu saba zioneshazo kuwa mwanasayansi anamwamini Mungu 66

Sehemu ya Pili Sura ya 18: Maana ya moja 76 21. Sura ya 19: Mwenyezi Mungu hawezi

kuwa zaidi ya mmoja 79 22. Sura ya 20: Maana ya Shirk 81 23. Sura ya 21: Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)

anazungumzia kuhusu "Tawhid" 84 24. Sura ya 22: Uislamu na Uyahudi 85 25. Sura ya 23: Umoja wa Mungu na Utatu 88 26. Sura ya 24: Umoja wa Mungu

na Ufarisayo 90 27. Sura ya 25: Umoja wa Mungu na ibada ya masanamu 91 28. Sura ya 26: Tawhiid ya Uislamu 96 29. Sura ya 27: Sifa za Mwenyezi Mungu 98 30. Sifat Thubutiyyah 99 31. Sifat Salibiyah 101 32. Sura ya 28: Majina ya Mwenyezi Mungu 103 33. Sura ya 29: Al-Asmaul-Husna

(majina mazuri ya Mwenyezi Mungu) 105 34. Sura ya 30: Sifa za asili na za matendo 109

DIBAJI

MUNGU WA UISLAMU

5

Tunamshukuru Allãh (s.w.t.) na kwa baraka za Mtukufu Mtume (s.a.w.a.) na Ahlul~Bayt (a.s.) kwa kutujaalia kuweza kufanikisha juhudi zetu hizi katika kuchapisha toleo la nane la kitabu hiki “Mungu wa Uislamu”.

Kitabu hiki kilochopo mikononi mwako ni tafsiri ya moja ya vitabu vya Al-Marhum Ayatullah Allamah Al-Haj Sayyid Saeed Akhtar Rizvi, Muasisi wa Tabligh ya Uislamu wa kweli katika Bara la Afrika, na kimetafsiriwa na Shaikh Dhikiri U.M. Kiondo kwa lugha ya Kiswahili kutoka lugha ya Kiingereza.

Mission inatoa shukurani zake za dhati kwa wale wote ambao kwa juhudi zao kitabu hiki kinawafikia wasomaji wetu. Tunamuomba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) awalipe malipo mema hapo Duniani na baadaye huko, Akhera.

Wamaa Tawfeeqi Illah Billah BILAL MUSLIM MISSION OF TANZANIA

UTANGULIZI

(Kwa maneno ya Mfasiri)

BILAL ALLAMAH RIZVI

6

Bismillahir Rahmanir Rahim, Allahuma Swalli alaa Muhammadin wa Aali Muhammad.

Kitabu hiki "Mungu wa Uislamu" ni tafsiri ya kitabu kiitwacho "God of Islam" kilichoandikwa na Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi, kikiwa ni sehemu ya pili ya Kozi ya I.C.C.

Katika kitabu hiki Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi anauzungumzia hatua kwa hatua, Mzizi wa kwanza wa Uislamu (Umoja wa Mungu). Anaanza kwa kuzungumzia kihoja sababu zitufanyazo tuamini kuwepo kwa Mungu, kisha anazipinga hoja za wanasayansi zipingazo kuwepo kwa Mungu; anatoa hoja za imani yetu (ya Umoja wa Mungu) na anamalizia kwa "Maana ya Umoja wa Mungu."

Bila shaka kitabu hiki kitawasaidia sana ndugu Waislamu na kitatoa mwanga kwa ndugu zetu wasio waislamu pia, Insha Allah.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujaalie sisi sote elimu ya kupambanua mema na mabaya na uongo na kweli. Tuwe wasikivu wa maneno yake, tuzitii amri Zake na Atujaalie mema hapa duniani na kesho Akhera pia - Amin.

Mallam Dhikiri U.M. Kiondo

MUNGU WA UISLAMU

7

HISTORIA FUPI YA MTUNZI WA KITABU HIKI

5TH JANUARI 1927 / 20TH JUNI 2002

Ra’isu ‘l-Muballighin Ayatullah Allamah Al-Muhaqiq Al-Faqih Al-Haj As-Sayyid Saeed Akhtari Rizvi, alizaliwa katika Familia ya Maulamaa mwezi Mosi Rajab 1345 A.H. (5th Januari 1927 M.) katika mji wa Ushri Khurd, Wilaya ya Siwan, Bihar, India. Mzazi wake Marehemu Ustadul Ulamaa Sayedul Hukama Maulana Al-Haj Sayyid Abul Hassan Rizvi (radhi za Mwenyezi Mungu Zimshukie) alikuwa Mmoja wa Maulamaa wakubwa wa India. Allamah Rizvi alianza masomo yake katika mji wa Gopalpur makazi ya jadi yake na kuendelea huko Patna na Banaras. Alifaulu Shahada ya juu katika mtihani wa lugha za Kiarabu, Kiajemi na Kiurdu kutoka (Chuo Kikuu cha) Allahabad Board, U.P., na akafanikiwa kupata Shahada ya juu zaidi ya elimu ya dini –“Fakhru 'L-Afadhil” kutoka chuo cha Jami'ul 'Uloom Jawadia, Banaras.

Kuanzia ujana wake, alikuwa akijishughulisha kikamilifu katika jamii, elimu na kuinua dini ya Jumuiya. Katika mwaka wa 1948, alichukuwa nafasi ya baba yake kama Imamu wa Jumuiya huko Hallaur katika wilaya ya Basti, U.P. na akaendelea na nafasi hiyo hadi mwaka wa 1951. Kuanzia 1952 - 1959 alifanya kazi kama Mwalimu wa Urdu na Kiajemi katika shule ya Sekondari ya juu ya Husainganj (huko) Husainganj, Siwani.

BILAL ALLAMAH RIZVI

8

Muda wa miaka yote hii alitumia likizo zake na wakati wake katika shughuli za Jumuiya kama kuendeleza shughuli za Anjumani Wazifa-e-Sadat-wa Momineen na Anjuma-e-Tarraqi-e-Urdu. Katika Mwezi Desemba 1959, alikwenda Tanzania (wakati huo ikijulikana kama Tanganyika) ambako alihudumia kama Imam wa Jumuiya huko Lindi (1959-1962) Arusha (1963-1964) na Dar es Salaam (1965-1969). Baada ya juma moja tu kuwasili kwake Afrika, alianza kujifunza lugha ya Kiswahili na kuangalia hali ya nchi kwa mtazamo wa kubalighisha Uislamu wa kweli miongoni mwa jamii ya wazawa (wa asili). Katika nyakati hizo kulikuwa hakuna Shia-Ithna-asheri hata mmoja mwenye asili ya Kiafrika katika bara lote. Katika mwaka wa 1962 alitayarisha mpango kwa ajili ya tablighi na akaupeleka kwa sekritariati ya Halmashauri Kuu ya Khoja Shia Ithnaasheri wakati huo ikiwa Arusha. Katika mwaka wa 1963 mpango huu ulijadiliwa kwa urefu. Katika hatua hiyo haukuweza kutekelezwa kama ilivyoshauriwa, lakini mwelekezo wa taratibu uliwekwa katika utekelezaji. Katika mwaka 1964 Sekritariati ilitayarisha taarifa (memorandum) iliyotegemea juu ya msingi wa taratibu yake ambayo iliwekwa katika agenda ya mkutano wa tatu wa mwisho wa mwaka wa muungano wa Jamati za Khoja Shia Ithna-asheri za Afrika (Federation of Khoja Shia Ithna-Asheri Jamaats of Africa) uliofanyika Tanga. Hivyo Bilal Muslim Mission ilizaliwa. Kuanzia siku hiyo, Allamah Rizvi alitumia muda wake katika shughuli za Tabligh. Katika mwaka 1963

MUNGU WA UISLAMU

9

Bilal Muslim Mission of Tanzania ilisajiliwa. Wakati kazi ilipoongezeka, Marehemu Ayatullah Al-Uzma Sayyid Muhsin Al-Hakeem (Najaf, Iraq) aliamuru Halmashauri Kuu ya Khoja Shia Ithna-asheri ya Afrika kumtoa katika majukumu ya Jamaat, na kuanzia hapo gharama zote za Allamah Sayyid Rizvi zilichukuliwa na marehemu Ayatullah Al-Uzma Sayyid Muhsin Al-Hakeem na baada yake zikachukuliwa na marehemu Ayatullah Al-Uzma Sayyid Abul Qasim Al-Musawi Al-Khu'i. Kwa juhudi zake ya Mission hii makumi ya maelfu ya Waafrika wamekubali imani ya Shia pole pole kupitia mafundisho, maandishi na masomo kwa njia ya Posta, sasa Jumuiya ya Shia imestawi nchini Guyana chini ya Bwana Lateef Ali ambaye amefanikiwa kueneza ujumbe mpaka Trinidad na Tobago. Mission ina kituo kwa ajili ya kufundishia Mubalighina mjini Dar es Salaam ambacho vile vile kina Bweni lenye nafasi. Kuna shule za chekechea, Msingi, Secondary na Madrasah ya Qur’ãn na Misikiti. Kwa nyongeza, Mission inaendesha masomo aina nne kwa njia ya Posta ambayo kwayo mwanga wa Ushia umefika mbali kwa mapana. Mission imechapisha vitabu zaidi ya miamoja na ishirini kwa Kiingereza na Kiswahili, sehemu kubwa ikiwa ni ya vitabu vya Allamah Rizvi au tarjuma yao. Kuna Bilal Muslim Mission nchini Kenya (imeanzishwa sawia na Misheni ya Tanzania) Burundi, Malagasy, Congo, Ruanda na Msumbiji. Yakitiwa moyo na Bilal Muslim Mission of Tanzania, Mashirika yenye majina kama haya yameanzishwa nchini Seneghal, Naijeria, Ghana, Sweden na Marikani.

BILAL ALLAMAH RIZVI

10

Katika mwaka wa 1963 alifanya ziyara ya Jamati zote za Khoja Shia Ithna-asheri za Afrika na kuwahimiza kuanzisha madarrasa kwa ajili ya vijana na watoto waweze kupata elimu za kidini, kwa utaratibu huo kila sehemu zimeanziswa Madrasa na vile vile vipindi vya dini katika shule pia yameanzishwa, masomo hayo yaliyotayarishwa na Allamah. Katika mwaka wa 1978 alirudi na kukaa nchini India ambako alianza kuandika tarjuma ya Kiingereza ya Tafsir al-Mizan cha Marehemu Allamah Sayyid Muhammad Husayn at-Tabataba'i. Juzuu kumi na mbili za tarjuma hii zimekwisha chapishwa na World Organization For Islamic Service (WOFIS) Tehran Iran. Mwezi Desemba 1980, alikwenda London kwa mualiko wa (Shirika la) Imam Sahebuz Zaman Trust. Kule London alikua pamoja na marehemu Hujjatul Islam Al-Mujahid Sayyid Mhadi al-Hakeem katika kuanzisha World Ahlul-Bayt (A.S.) Islamic League (WABIL) ni mmoja wa wadhamini watatu wa Shirika hili. Alikuwa Mkurugenzi wa Kamati ya maandalizi ambayo ilirasimu katiba ya WABIL na ilipanga mkutano wake wa kwanza wa katiba. Mkutano huu ulifanyika mwezi Augosti 1983 ambao kwayo wajumbe 80 kutoka nchi 30 walishiriki. Katika mkutano huo alichaguliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika hilo. Alirudi Tanzania mwaka 1986 kuendeleza shughuli za Bilal Muslim Mission of Tanzania na sasa hugawanya wakati wake kati ya Tanzania, India, na Canada. Mwaka wa 1991 Ilianzishawa Ahlul~Bayt (A.S.) World Assembly (ABWA) Tehran, Iran na Allamah Rizvi

MUNGU WA UISLAMU

11

alichguliwa moja wawana kamati ya Halmashuri kuu na mjube. Na vile vile ni Muasisi na Mwenyekiti wa Ahlul~Bayt (A.S.) Assembly of Tanzania (ABATA).

Mwaka wa 1993 ameanzisha Bilal Charitable trust of India, Gopalpur. Hadi sasa zaidi ya Misikiti 25 na Hussaeinia zimejengwa na zaidi ya 30 Nyumba za kuishi kwa watu ambao hawana makazi na vile vile shule za chekechea, Msingi, Secondary na teknolojia imeanzishwa na Tasisi hii. Allamah Rizvi ameanzisha Madrasa nyingi za Kidini na kufungua Markazi za Tablighi katika sehemu mbalimbali ulimwenguni, kati ya sehemu hizo ni India, Marakani, Uingereza, Canada, na nchi za Kiafrika. Allamah Rizvi ameandika zaidi ya vitabu 150 kwa lugha ya Kiingereza, Kiurdu, Kiarabu, Kifursi na Kiswahili. Baadhi ya vitabu vyake vimetafsiriwa kwa lugha za Ki-Japan Ki-Indonesia, Ki-Thai, Ki-Burma, Ki-Urdu, Ki-Hindi, Ki-Gurjati, Ki-Sindhi, Ki-Ajemi, Ki-Swahili, Ki-Hausa, Ki-Shona, Ki-Taliani, Ki-Faransa, Ki-Swidish, Ki-Bosni, Ki-Arabu, Ki-Holanzi.

Vile vile amefanya kazi na baadhi ya Maulama wa Qum kuweka vizuri na kusahihisha Adh-Dhariah fi Tasanif As-shia, Kitabu kikubwa cha habari za vitabu na watungaji wake kilichoandikwa na marehemu Ayatullah Agha Buzrg at-Tehrani.

Amepewa Ijazat (Mamlaka) na Ma-Ayatullah wakongwe Ishirini na Moja wa Najaf (Iraq) na Qum (Iran) kwa simulizi ya hadithi (riwayah) kwa mambo ya hukumu kwa Shariah na vile vile kushughulikia suala lolote ambalo kwayo ruhusa ya Mujtahid ni muhimu. Na

BILAL ALLAMAH RIZVI

12

vile-vile Allamah Rizvi amewapa Ijaza ya riwayah kwa Ma-Ulama wengine. Allamah Rizvi alikuwa nimtaalam wa lugha. Huandika, huzungumza na kutoa mihadhara kwa Ki-Urdu, Ki-Arabu, Ki-Ingereza, Ki-Swahili na Ki-Ajemi. Vile vile alikuwanayo elimu (ya maandishi) ya Ki-Hindi na Ki-Gujarati. Mbali na ukubwa na upana (wa eneo) alioshughulikia, na ziara za mara kwa mara ndani ya Afrika Mashariki, alizuru kama nchi 45 za Asia, Afrika, Ulaya na Marekani.

SEHEMU YA KWANZA

SURA YA 1

IMANI YA KUWEPO MUNGU

Ni silika ya kimaumbile.

Imani ya kuwepo Mwenyezi Mungu ni silika ya kimaumbile kwa mwanadamu sawa na silika nyinginezo. Malahidi (mtu asiyesadiki kuwa yupo Mungu) mmoja alimuomba Imam Jaffar As-Sadiq (a.s.) amdhihirishie kuwepo kwa Mwenyezi Mungu. Imamu (a.s.) akijua kuwa mtu yule alikuwa kesha safiri safari fulani fulani baharini, alimuuliza , "Je uliwahi kupatwa na dhoruba kali ambayo ilikufanyeni mpotee njia na matanga yenu yapasuke na kufanya kuelekea kwa jahazi yenu kuwa kwa kukatisha tamaa? Jibu lilikuwa, "Ndiyo". Kisha Imamu akamuuliza: "Na wakati mwingine pengine hata ile jahazi inayovuja ilianza kuzama na ninyi mkiwa mmechoka na mkiwa katika hali

MUNGU WA UISLAMU

13

ya kukata tamaa na mkiwa mnakabiliwa na mawimbi makali. Tena jibu lilikuwa 'Ndiyo'.

Kisha Imamu aliendelea kuuliza: "Je, halikuwepo tumaini katika moyo wako japokuwa dogo sana ulipokuwa katika hali hiyo ya kukatisha tamaa kuwa nguvu fulani isiyojina na isiyojulikana ingeliweza kukuokoa? "Baada ya Bedui huyu kukubali, Imamu alisema: "Nguvu hiyo ndiyo Mungu."

Mlahidi yule alikuwa mwenye busara. Aliweza kutambua ukweli alipouona.

SURA YA 2

KUWEPO AU KUTOKUWEPO

Mara nyingi huwa tunafikiria maelfu na maelfu ya vitu. Tunamfikiria farasi. mwanadamu, ndege ulaya, dunia, gari moshi, na kitabu. Tunaziona picha za vitu hivi katika fikara zetu.

Kuwepo kwa vitu vya aina hii huitwa "Kuwepo kidhana" (Wajudi - i - Dhihni).

Na vile vile farasi, mwanadamu, ndege ulaya, dunia, gari moshi au kitabu vinakuwepo kwa nje ya fikara zetu. Kuwepo huku kunaitwa, "Kuwepo nje ya dhana". Huku ndiko kuwepo halisi. (Wujud-i-Khariji).

Wakati mwingine huwa tunafikiria mawazo ambayo hayawezi kupatikana nje ya dhana zetu. Tunaweza kufikiria kuwa 2+2=5. Lakini je, inawezekana 2+2 kuwa 5 katika kuwepo halisi? Hapana. Tunaweza kudhania kuwa kitu fulani kinakuwepo na vile vile hakipo katika sehemu fulani na wakati fulani. Je jambo hili

BILAL ALLAMAH RIZVI

14

linawezekana kuwepo kweli? Kwa hakika - HALIWEZEKANI.

Fikara hizi za kimawazo ambazo haziwezi kuwepo hata kidogo, huitwa "Muhali". (Mumtaniul - Wujud).

Pia huwa tunadhania kuwa mtu fulani anatembea wakati fulani. Je hii inawezekana kuwepo hasa? Sasa hebu ondoa mawazo mengine toka akilini mwako. Hebu tazama ile picha ya yule mtu anayetembea katika muda maalum tu. Sasa hebu jiulize je, ni lazima kuwa mtu yule awe anatembea katika muda ule maalum? Au kwa upande mwingine, ni muhali kwa mtu huyo kuwa anatembea wakati ule? Jibu la maswali hayo mawili hapo juu ni "Hapana". Kwa nini? Kwa sababu sio lazima wala si muhali kwa mtu kutembea katika muda maalum. Anaweza akawa anatembea; na vilevile anaweza akawa hatembei. Kwa vyovyote vile sababu na hoja zihusikavyo katika suala hili, kutembea kwake na kutotembea kwake vinawezekana. Vinawezekana, laini sio lazima.

Maoni haya ya kifikara yenye uhusiano ulio sawa wa kuwepo na kutokuwepo huitwa ("Wamkinul - Wujud) . Uwezekano" au wa muda. Yanaweza kuwepo hasa, na vilevile yanaweza yakawa hayapo hasa. Hakuna haja katika asili yao ya kudai lolote katika hayo mawili. Kwa vitu hivyo, kuwepo au kutokuwepo yote ni sawa, kwa kutegemeana na asili ya vitu hivyo.

Mpaka hapo tumeona uhusiona wa aina mbili kati ya wazo la kifikara kuhusu kitu fulani na kuwepo kwake hasa:

MUNGU WA UISLAMU

15

1) Wazo hilo liwapo na uhusiano ulio sawa kati ya kuwepo na kutokuwepo, kitu hicho kiwaziwacho kinaweza kuwepo na pia kinaweza kutokuwepo.

2) Iwapo wazo hilo halina uhusiano kabisa na kuwepo kwa kitu hicho, basi kitu hicho kwa asili hakipo.

Kutokana na maelezo tuliyoyatoa hapo juu, itaonekana wazi wazi kuwa ni lazima iwepo aina ya tatu ya wazo, ambayo itakuwa ni kinyume cha "Muhali" (Mumtaniul Wujud) tuliyoitaja katika nambari (2) hapo juu.

3) Aina hii ya tatu ni wazo lisilo na uhusiano kabisa na kutokuwepo. Kulifafanua zaidi, wazo la aina hii huitwa, kuwepo kusiko na mwanzo wala mwisho. Wazo la aina hii huitwa (Wajibul Wujud) kuwepo kuliko Muhimu "Kuwepo Halisi."

Mpaka hapa picha kamili ya wazo hili imekamilika.

SURA YA 3

CHANZO CHA ULIMWENGU

Kuna kutoafikiana sana kuhusu maoni ya Walahidi na wale waaminio kuwepo kwa Mwenyezi Mungu muumba wa huu ulimwengu. Hata hivyo liko oni moja likubaliwalo sana na pande zote mbili hizo.

Pande zote, mbili zinakubaliana kuwa chanzo au kisababisho cha awali sana cha huu ulimwengu ni cha milele - yaani hakina mwanzo wala mwisho; kilikuwepo na kitakuwepo milele. Kwa msemo mwingine ni kuwa, si kiumbe "Wajib -ul - Wujuud."

BILAL ALLAMAH RIZVI

16

Sababu ya fikara hizi ni rahisi sana. Kwa sababu kila kitu katika huu ulimwengu kimo mwenye mkumbo ule wa vitu. "Viwezekanavyo kuwepo" (Mumkinul - Wujud) yaani kina uwezekano ulio sawa kati ya kuwepo na kutokuwepo. Hapo mwanzoni vitu hivi havikuwepo; hivi sasa vipo, na siku fulani baadaye vitatoweka. Kwa kutegemeana na asili yao, haviwezi kudai kuwepo au kukoma kuwepo. Hivyo basi, NI LAZIMA kuwepo na chanzo au kisababisho cha kuvifanya viwepo au kukomesha kuwepo kwao.

Na (ni jambo muhimu sana kwa) hicho chanzo au kisababisho chenyewe lazima kisiwe " Kiishicho kwa Muda tu" au sivyo nacho kitahitaji chanzo au kisababisho cha kukifanya kiwepo. Na nyororo hii ya visababisho na matokeo ni LAZIMA iishilizie kwenye kisababisho ambacho hakihitaji chanzo kingine kisicho hicho hicho chenyewe, kwa ajili ya kuwepo kwake. Hii ina maana kuwa chanzo au kisababisho hicho cha mwisho kilichoufanya huu ulimwengu uwepo, ni lazima chenyewe kiwe kijitoshelezacho katika kuwepo kwake.

Ni ajabu kuwa hata Walahidi wanakubaliana na wazo hili kwa sababu wanasema kuwa hakuna chochote kiwezacho kupatikana kutokana na "bure". Hivyo basi, chanzo asili cha kuwepo kwa vitu vyote ni lazima kiwe kiishicho milele. Kilichokuwepo milele na kitakachodumu milele.

Sasa inafuatia tofauti ya kwanza. Walahidi wanasema kuwa, hicho chanzo cha milele ni Jauhari (Matter). Waaminio kuwepo kwa Mungu wanasema kuwa hicho chanzo cha Milele ni"Mwenyezi Mungu."

MUNGU WA UISLAMU

17

Tutalizungumzia zaidi jambo hili baadaye, hapa itatosha tu kama tukijenga msingi wa imani ikubaliwayo na vikundi vyote viwili, nayo ni imani ya kuwa chanzo asili cha ulimwengu huu ni cha milele - hakina mwanzo wala mwisho.

SURA YA 4

SIFA ZA KITU CHA MILELE

KIKitu cha milele ni lazima kiwe na sifa hizi zifuatazo:-

1) Kwa kutegemeana na ufafanuzi wa neno hilo, kitu cha milele ni kitu kijitoshelezacho katika kuwepo kwake. Hakiwezi kuwa na muda fulani ambao hakikuwepo wala hakiwezi kukomeshwa kuwepo. Kwa maneno mengine ni kuwa, hakina mwanzo. Maana iwapo tutafikiria kuwa kilikuwa na mwanzo, basi hatuna budi vile vile tufikirie kuwa hakikuwepo kabla ya kuanza kuwepo kwake. Lakini tunafahamu haiwezekani kuwa hakikuwepo.

Hivyo ni lazima tukubali kuwa kitu cha milele hakina mwanzo kinaishi milele na milele.

2) Kwa sababu hizo hizo tulizozitaja hapo juu, kitu hicho hakiwezi kuwa na mwisho. Kinaishi milele kwa sababu hakiwezi kuwa kisicho kuwepo.

3) Kitu cha milele ni lazima kijitosheleze chenyewe kwa maneno mengine ni kuwa, ni lazima kiwe kisichohitaji chochote; kwa sababu, iwapo kitahitaji kitu fulani, basi kitakuwa ni chenye

BILAL ALLAMAH RIZVI

18

kukitegemea kitu hicho. Lakini kutokana na ufafanuzi wa kitu cha milele hakitegemei kitu chochote kingine maana ni chenye kujitosheleza. Kwa maneno mengine ningelisema kuwa, kitu cha milele ni lazima kiwe na utimilifu kamili.

4) Kitu cha Milele hakiwezi kuwa Muungano au mchanganyiko wa vitu.

Kuwepo kwa Muungano au mchangyiko kunategemea kuwepo kwa sehemu za mchanganyiko huo. Kwa vile tulishakubali kuwa kitu cha milele ni lazima kijitosheleze chenyewe kuhusu kuwepo kwake, hatuwezi tukakubali kuwa kuwepo kwa kitu hicho cha milele kunaweza kutegemea kuwepo kwa sehemu za muungano au mchanganyiko wake.

Zaidi ya hapo, hebu utazame muungano au mchanganyiko wa vitu, utaona kuwa sehemu za muungano au mchanganyiko huo zilikuwepo kabla ya kuwepo kwa huo muungano au mchanganyiko wenyewe. Kwa sababu kitu cha milele hakina mwanzo, hatuwezi kusema kuwa kitu fulani kilikitangulia; au sivyo, itatupasa tufikirie kuwepo kwa chanzo cha kitu hicho cha milele, jambo ambalo litakuwa kosa kubwa.

5) Kitu cha milele hakiwezi kuwa kitu chenye kiwiliwili wala uso wa juu wa kitu, wala si mstari wala si nukta.

Kitu chenye kiwiliwili kwa asili yake, huhitaji nafasi ya kukalia. Kama tulivyoona, kitu cha milele ni lazima kisiwe mhitaji hivyo, tuna maana ya kuwa kitu cha milele hakiwezi kuwa kitu chenye kiwiliwili.

MUNGU WA UISLAMU

19

Kuwepo kwa uso wa juu wa kitu huhitaji kuwepo kwa kitu chenye kiwiliwili. Mstari huhitaji kuwepo kwa uso wa juu wa kitu. Nukta nayo huhitaji mstari, Kitu cha milele si mhitaji wa chochote kile. Hivyo basi, kitu cha milele hakiwezi kuwa uso wa juu wa kitu, mstari wala nukta, wala hakiwezi kuwa kitu chochote kipatikanacho kwenye kitu chenye kiwiliwili kama vile ukubwa, rangi, harufu, uelekeo, hali au vitu vingine kama hivi ambavyo huitwa, "vitu visivyo na umbo la wazi (Aradh) katika lugha ya kifilosofia, kwa sababu kuwepo kwa vitu hivi hutegemea kuwepo kwa vitu vyenye maumbo ya wazi. Vyenyewe havijitoshelezi katika kuwepo kwao.

6) Kitu cha milele kisiingiliwe na mabadiliko, maana kama mabadiliko hayo yatakuwa kwa ajili ya kukifanya kitu hicho kiwe kizuri zaidi, itakuwa na maana kuwa kitu hicho cha milele hakikukamilika kabla ya hapo, yaani kilikuwa kikihitaji kitu fulani. Lakini tumekwisha eleza kuwa kitu cha milele hakihitaji chochote.

Na iwapo mabadiliko hayo ni kwa kukifanya kiharibike, itakuwa na maana kuwa kitu hicho cha milele sasa kinahitaji kitu fulani cha kukifanya kiwe kamili zaidi, na kama tulivyoeleza hapo mwanzo, kuwa jambo hilo haliwezekani.

Na iwapo mabadiliko hayo hayakifanyi kitu hicho kuwa kizuri wala kuwa kibaya, basi nini faida ya mabadiliko hayo?

Ukweli ni kuwa, mabadiliko yanaweza kutokea katika (kitu chenye umbo la kuonekana, jauhari) au katika sifa zake zisizo na maumbo ya wazi kama vile

BILAL ALLAMAH RIZVI

20

rangi, ukubwa, n.k. Lakini nimeeleza hapo awali kuwa kitu cha milele hakiwezi kuwa kitu chenye umbo la wazi wala sifa isiyo na umbo la wazi.

7) Kitu cha milele ni lazima kiwe chenye uhai. Kwa sababu imekubalika kuwa kitu hicho cha milele ndicho chanzo na kisababisho cha kuwepo kwa Ulimwengu. Na vile vile imekubalika kuwa hakuna chochote kiwezacho kutokea kutokana na "bure". Sasa kwa sababu tunaona vitu vingi sana vyenye uhai katika huu ulimwengu, hatuna budi tukubali kuwa chanzo cha vitu hivi vyenye uhai ni lazima kiwe chenye uhai. Kisingeliweza kuhuisha, iwapo chenyewe hakingelikuwa na uhai.

8) Kitu cha milele ni lazima kiwe kijuacho mambo yote. Mpango mgumu wa "atom" (sehemu ndogo sana ya kitu isiyogawanyika kikemia) inaonyesha hekima kamili iliyofanyika ndani yake. Mpango wa huu ulimwengu ambao umekamilika na ambao unahitaji kazi ngumu, hautoi hata kipengo kwa shaka yoyote kuwa, yeyote yule au chochote kile kiwacho chanzo au kisababisho cha Ulimwengu, ni lazima kiwe kinachojua mambo yote.

9) Kwa sababu hiyo hiyo tuliyoitaja hapo juu (Nambari 8) ni lazima tuamini kuwa chanzo cha milele cha ulimwengu huu ni LAZIMA KIWE chenye uwezo juu ya kila kitu.

SURA YA 5

JAUHARI NI KITU CHA MILELE

MUNGU WA UISLAMU

21

Walahidi wanasema kuwa Jauhari ndicho chanzo cha Ulimwengu. Haihitaji hekima nyingi zaidi ili kugundua kuwa Jauhari haina hata moja ya sifa zile za kitu cha milele tulizozitaja katika sura iliyopita.

Jauhari ina umbo, na hivyo inahitaji nafsi, Inagawanyika, hivyo imetengenezwa kwa sehemu nyingi mbalimbali. Na inaendelea kubadilika mara kwa mara.

Lakini walahidi wanashikilia kuwa jauhari haina mwanzo wala mwisho na hivyo basi ni ya milele.

Lakini maelezo ya hivi karibuni kuhusu jauhari yanayapinga maoni haya mawili ya ulahidi.

SURA YA 6

JAUHARI INA MWANZO NA MWISHO

"Jauhari" ni kitu gani? Jauhari ni kitu ambacho kinatumika kutengenezea vitu vyenye maumbo ya kuonekana. Au kitu chochote chenye sifa ya kuchukua nafsi na sifa za ukubwa na uzito.

Kabla hatujaendelea zaidi ni lazima tutaje jambo moja muhimu, kuwa katika kila tawi la sayansi kuna mawazo fulani fulani ambayo hayana uhusiano na kuwepo kwao halisi. Lakini hata hivyo, vinachukuliwa kuwa kwa hakika vipo ili kuwarahisishia wanafunzi wa somo hilo kuweza kuzielewa zaidi hoja za somo hilo.

Chukulia mfano wa somo la 'Elimu ya maumbo'(Geometry). Katika somo hili waalimu wanawafundisha watoto kuwa, 'nukta' ni kitu kisicho na

BILAL ALLAMAH RIZVI

22

urefu wala upana wala kina, kitu kama hicho hakina kuwepo halisi (yaani hakipo). Pia wanafundisha kuwa, "mstari" ni kitu chenye urefu tu lakini hakina upana wala kina. Kitu hiki vile vile hakina kuwepo maalum. Ukweli ni kuwa, ni kwa kuchukua kitu (chenye maumbo yote matatu ya kuonekana kama vile urefu, upana na kina) na kukigawanya kimawazo tu, ndio tunaweza kulielewa wazo la uso, mstari na nukta.

Hata hivyo wanafunzi wa "'Elimu ya maumbo' wanafundishwa kana kwamba vitu hivi vinapokuwepo kirahisi. Haifanywi hivyo ili kuwadanganya wanafunzi bali kuwafanya waelewe kwa urahisi zaidi.

Hali kadhalika katika somo la 'Kemia' (Chemistry), mwanafunzi anafundishwa kuwa jauhari haiwezi kutengenezwa wala kuharibiwa. Lakini mafundisho haya ni kwa kumfanya mwanafunzi huyo aweze kuzielewa hoja zingine.

Pia, ni kwa sababu hii kuwa wanafunzi wa Kemia wanafundishwa uhifadhi wa pekee wa jauhari na nguvu.

Lakini hebu visome vifungu hivi vifuatavyo:- "Katika somo la 'Maarifa ya kutumia nguvu za

mashine ' (mechanics), uzito na nguvu vinachukuliwa kuwa vinabadilishwa kitofauti tofauti. Katika nguvu za atomiki na niuklia, jauhari inaweza kugeuzwa na kuwa nguvu, na nguvu inaweza kugeuzwa na kuwa jauhari ... Kwa kadri kemia ihusikavyo, utaratibu wa kuigeuza jauhari (yaani utaratibu ule usemao kuwa jauhari haiwezi kutengenezwa wala kuharibiwa) unaweza kuchukuliwa kuwa ni ukweli.

MUNGU WA UISLAMU

23

Hivyo unaona kuwa maelezo yasemayo kuwa jauhari ni ya milele (haitengenezeki wala haiwezi kuharibiwa) ni dhana tu iliyowekwa ili kuwarahisishia wanafunzi somo la kemia.

Ni kweli kuwa 'Jauhari' hubadilika na kuwa "Nguvu". Hivyo, jauhari si kitu cha milele wala si kitu kisicho badilika. Hivyo tutaona kuwa jauhari haifaulu mtihani wa kitu cha milele. Si kitu kisicho na mwisho wala si kitu kisicho badilika. Na kwa sababu inafikiriwa kuwa "nguvu" inaweza kubadilishwa na kuwa jauhari, itakubalika kuwa jauhari ina mwanzo. Hivyo si kitu cha milele - si kitu kisicho na mwanzo.

Inafikiriwa kuwa 'Jauhari' ibadilikapo kuwa 'nguvu hubakia kuwa hiyo 'nguvu' na hivyo basi wanajaribu kuthibitisha kuwa jauhari inaishi milele.

Lakini 'nguvu' ni nini? 'Nguvu' ni uwezo wa jauhari wa kufanya kazi kutokana na msogeo wake au nafasi yake kuhusiana na nguvu inayoisogeza". Hivyo basi, 'nguvu'. si kitu chenye kuwepo kwa kibinafsi. Ni kitu kisicho na eneo la wazi - yaani inategemea jauhari au kitu fulani kwa kuwepo kwake. Kutokana na ufafanuzi wa 'nguvu' inaonekana kuwa haipatikani ila katika jauhati tu. Kwa sababu "nguvu" ni kitu kitegemeacho kingine, haiwezi kuwa kitu cha milele.

SURA YA 7

DHANA MBILI

BILAL ALLAMAH RIZVI

24

Sasa ni lazima tutaje hapa kuwa zipo dhana mbili, yaani wazo la kujaribia, katika sayansi kuhusu viumbe au chanzo cha Ulimwengu (Ulimwengu ni vitu vyote vilivyoumbwa au vilivyopo). Ya kwanza kabisa ni dhana ya maendeleo na mabadiliko. Dhana hii inasema kuwa, vitu vyote vilivyopo hapa duniani vilikuwa hapo mwanzoni katika aina fulani ya 'atom' ya zamani (ya kwanza) kabisa; kuwa Ulimwengu uliumbwa siku fulani; na kuwa siku fulani utakufa.

Kama wazo hili litachukuliwa kuwa ni sahihi, basi ile "atom" haiwezi kuchukuliwa kuwa ni kitu cha milele. Kitu kifaacho au kikomacho, hakiwezi, kwa makisio yoyote yale, kuwa kinachoishi chenyewe na cha milele.

Dhana ya pili inaitwa dhana ya "hali imara". Dhana hii inasema kuwa Ulimwengu ulikuwepo na utakuwepo milele, na kuwa 'jauhari' mpya inaendelea kuumbwa. Hivyo wanaamini kuwa Ulimwengu ni mkusanyiko wa jauhari; na wanaamini kuwa jauhari inaendelea kuumbwa. Kwa usemi mwingine ni kuwa ulimwengu ni mchanganyiko wa viumbe. Jinsi mchanganyiko wa viumbe unavyoweza kuitwa "kitu cha milele" (kisicho na mwanzo) ni kitu kisichoweza kuaminika.

Hivyo ni wazi kuwa, kwa maoni yoyote yale mtu awezaye kuichukulia jauhari, haiwezekani kuthibitishwa kuwa kitu cha milele (kisicho na mwanzo wala mwisho).

Sasa inaaminwa kuwa jauhari mpya inaendelea kuumbwa, kuwa jauhari inabadilika na kuwa "nguvu", kuwa jauhari inahitaji umbo na mahali, kuwa jauhari inaweza kugawanyika, na kuwa jauhari kila mara

MUNGU WA UISLAMU

25

inabadilika. Je inawezekana kusema kuwa jauhari ni kitu cha milele ambapo sifa zake ni sawa na zile za kitu cha muda tu?

Walahidi watano walifanya mazungumzo na Mtume (s.a.w) na mwisho wa mazungumzo hayo Mtume (s.a.w) aliwaambia:-

"Huu ulimwengu upo katika hali ya kuwa baadhi ya sehemu zake zinategemea sehemu nyingine; sehemu hizo haziwezi kuwepo bila ya sehemu hizo nyingine, sawa kabisa na sehemu fulani fulani za jengo zitegemeavyo sehemu nyingine kwa nguvu na kuwepo kwao. Na huu ulimwengu wote ni kama lile jengo. Sasa hebu, niambieni, kama sehemu ile (ambayo inazitegemea sehemu nyingine kwa ajili ya nguvu na kuwepo kwake) ni ya milele japokuwa ni yenye kutegemea na kuhitaji , basi zingelikuwaje sifa zake kama kitu hicho kingelikuwa ni chenye kuishi kwa muda tu ( ni chenye kuweza kuwepo, si cha milele).

Ndio. Waache Walahidi waseme vile ambavyo ingelikuwa kama jauhari isingelikuwa ya milele.

SURA YA 8

JAUHARI SI CHANZO CHA UHAI

Sasa, tunazirudia zile sifa tatu za mwisho tulizozitaja katika Sura ya 4. Tumekwisha ukubali msemo ule wa walahidi usemao kuwa hakuna chochote kiwezacho kupatikana kutokana na "bure". Sasa tunapoutazama Ulimwengu tunaona usanii na kielelezo cha kihekima sana na ulinganifu ulio sawasawa kabisa

BILAL ALLAMAH RIZVI

26

katika mpango huu usio kifani. Na vile vile tunaona ukimiminika uhai ndani yake. Na tunakubali kuwa jauhari haina uhai; na hivyo basi haina uwezo wala ujuzi.

Kama jauhari ingelikuwa kisababisho au chanzo cha ulimwengu, bila shaka huu Ulimwengu usingelikuwa na vitu vyenye uhai. Usingelikuwa na utaratibu wowote ule, kwa sababu jauhari isingeliweza kuupa ulimwengu kitu isichokuwa nacho. Je! ipo haja tena ya kusisitiza kwa maneno mengi kuwa haiwezekani kuifikiria jauhari kuwa ndicho chanzo cha Ulimwengu?

SURA YA 9

IMANI YA MUNGU MMOJA DHIDI YA ULAHIDI

Ninatoa tafsiri ya majadiliano kati ya Mtukufu Mtume (s.a.w) na Walahidi, ambayo sehemu yake tumeitaja hapo mwanzoni.

Mtume (s.a.w,) aliwauliza: Ni sababu gani inayokufanyeni muamini kuwa Ulimwengu hauna mwanzo wala mwisho na kuwa vitu hivi ni vya tangu na tangu na vitakuwepo milele na milele?

MUNGU WA UISLAMU

27

Walahidi: Tunaamini kile tu tukionacho. Kwa vile hatukukiona chanzo cha Ulimwengu ndio maana tunasema kuwa ni wa tangu na tangu, na kwa sababu hatukuuona mwisho wake, tunasema kuwa utabaki milele.....

Mtume (s.a.w): Vizuri, je mmewahi kuona kuwa Ulimwengu hauna mwanzo wala mwisho?.

Walahidi: Hapana , hatujawahi kukuona kule kutokuwa na mwanzo kwake; wala kule kutokuwa na mwisho kwake.

Mtume (s.a.w): Basi vipi mnauamini utangu wake? na kwa nini maoni yenu yapendelewe kuliko ya mtu yule aaminiye kuwa Ulimwengu ni kitu cha muda tu, kwa sababu hajauona ukiwa bila mwanzo wala bila mwisho?

Kisha baada ya mabishano mengine zaidi, Mtume (s.a.w) aliwauliza akisema "Je! mnaweza kuniambia kama siku (muda) zilizopita katika hii dunia ni zenye idadi maalum au si zenye idadi maalum? Kama mnasema kuwa siku zilizopita hazikuwa na kiwango maalum, basi vipi muda mpya uliingia iwapo ule wa zamani haukupita?

"Kama mnasema kuwa muda huo ulikuwa na kiwango maalum, basi hamna budi mkubali kuwa si wa tangu na tangu.

Walahidi: Ndio, ni wenye kikomo maalum.

Mtume (s.a.w): Haya, mlikuwa mkisema kuwa Ulimwengu ni wa tangu na tangu haukuumbwa wala hauna kikomo. Mnatambua ni nini maana halisi ya

BILAL ALLAMAH RIZVI

28

kukiri kwenu kuwa muda una kikomo maalum? Mlikuwa mnakataa nini? Sasa Mnakubali nini?

Walahidi walikubali kuwa imani yao haikuwa sahihi. Matokeo ya hoja alizozitoa Mtume (s.a.w)

yanaonyesha kuwa muda una uhusiano na jauhari ambao hautengeki. Kama haikuwa hivyo Mtume (s.a.w) asingeligusia habari za asili ya "muda" katika mazungumzo haya yanayohusu jauhari. Uzuri wa mambo haya unakubalika bila taabu yoyote kwa watu wale ambao wamejifunza elimu ya Uwiano.

SURA YA 10

MAZUNGUMZO

Hoja rahisi sana za watu wa zamani sana kuhusu jambo hili bado zinatumika, licha ya maendeleo makubwa ya kisayansi tuliyonayo siku hizi.

Mwanamke kizee mmoja alikuwa akisukuma gurudumu la kusokotea nyuzi. Mtu mmoja alimuuliza ni kwa nini anaamini kuwa yupo Mungu? Aliondoa mkono wake katika lile gurudumu na mara tu pia ya gurudumu ikasimama. Akasema "Unaona, hata hii pia rahisi sana inahitaji mkono wa kuifanya izunguke. Je! unaweza kufikiria kuwa jua hili, mwezi huu, nyota hizi, ulimwengu huu wote unasogea bila ya kuwepo mkono wa kuongoza."

Hadhrat Ali bin Abi Talib (A.S) aliombwa kutoa uthibitisho wa kuwepo kwa Msanii wa hii dunia. Alijibu: Kinyesi cha ngamia na cha punda humfanya mtu

MUNGU WA UISLAMU

29

aamue kuwa wanyama hao wamepita katika ile njia. Alama za wayo wa mtu huonyesha kuwa mtu kapita. Je! Ulimwengu huu mkubwa kiasi hiki na maajabu yake yote haya na sehemu yake hii ya chini (Ardhi), na ugumu wake hauonyeshi kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, Mtukufu na Mjuzi wa yote

Siku moja, Mlahidi mmoja aliyeitwa Abu Shakir Disani alimjia Imam Jaafar Sadiq (A.S) na akamuomba amuongoze kwenye kumtambua "Bwana Mungu wangu". Imam Jafaar (A.S) alimuomba akae, mara baada ya Abu Shakir Disani kukaa tu, alikuja mtoto aliyekuwa kashika yai mkononi. Imam (a.s) akalichukua lile yai toka mkononi mwake yule mtoto na kisha akamwambia Abu Shakir Disani, "Ipo ngome ya siri ndani ya hili kaka gumu, ambalo ndani yake uko utando mweroro ambao huifunika fedha iliyoyeyuka (ute wa yai) na dhahabu iliyoyeyuka (kiini cha yai). Ile dhahabu iliyoyeyuka haiharibiki thamani yake kwa kuchanganyika na ile fedha iliyoyeyuka, wala ile fedha iliyoyeyuka haichanganyiki na ile dhahabu iliyoyeyuka. (Ingawa zote zipo katika hali ya umajimaji na ni haki zingelichanganyika wakati yai hilo lisogezwapo au litikiswapo). Kila mara miyeyuko hii huuhifadhi ule mtengano wao. Hakuna hata msanii mmoja aliyejitokeza kudai kuwa amefanya mabadiliko fulani fulani katika yai, wala hakuna kitu chenye kuharibu kinachoingia ndani yake ili kuliharibu. Wala haijulikani kama limetayarishwa kwa ajili ya kutoa kifaranga cha kiume au cha kike. Ndege wenye rangi nyekundu kutoka ndani yake. Je! unafikiri linae msanii (Muumba, mjuzi wa kila kitu)?. Ni nani aliyeweka rangi mbalimbali

BILAL ALLAMAH RIZVI

30

katika sehemu hizi tofauti tofauti zilizoko ndani yake na vipi kifaranga kinatokea?. Nani msanii wa rangi hizi mbalimbali, manyoya, sehemu za mwili, rangi, miguu, mdomo, mabawa, macho, masikio, pua, matumbo, umio (gole), viungo n.k., kuhakikisha kuwa hakuna mtu yeyote aingiaye humo? Kutegemeana na hadithi hiyo, Abu Shakir Disani alizamisha kichwa kufikiria sana kwa muda mrefu na ghafla akasema kwa sauti kubwa, "Ninathibitisha kwamba hapana mola ila Mwenyezi Mungu mmoja tu, ambaye hana mshirika, na ninathibitisha kuwa Muhammad (s.a.w) ni mtumwa na mtume wake, na kuwa wewe (Imamu Ali a.s) u Imamu na Uthibitisho wa Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake, na najifarakisha na mawazo yangu ya kale.

SURA YA 11

DINI DHIDI YA MAWAZO YA BWANA DARWIN

Bwana Darwin alipoandika makala yake "Origin of Species (asili ya jamii ya vitu vyenye asili moja)" mnamo mwaka 1859 Miladiyya, alisababisha upinzani mkali sana kutoka vikundi vya kidini.

Upinzani wa kidini ulitoa hoja kuhusu mambo mawili:-

1) Bwana Darwin amethibitisha - kwa kutoa hoja zikubalikazo kuwa Ulimwengu haukuumbwa katika siku sita, (6) kama inavyoelezwa katika Biblia, bali umeumbwa katika muda mrefu sana na kuna hatua nyingi sana kati ya hali hiyo ya kwanza na hali hii ya sasa, na

MUNGU WA UISLAMU

31

2) Amekanusha na kusema kweli, bila ya sababu za maana, haja ya kuwepo Muumba (Mungu) katika haya matengenezo ya huu Ulimwengu.

Wayahudi na Wanasara wa siku zile waliamini kuwa dunia iliumbwa katika muda wa siku sita kutokana na maandishi ya vitabu vyao, nao hawakuweza kuikubali kirahisi fikara ya kuumbwa dunia katika muda mrefu. Na hivyo basi malumbano baina ya Wanasara na Sayansi yakafikia kiwango cha juu sana katika nusu ya pili ya karne ya kumi na tisa.

Lakini Waislamu je!

Qur'ani inasema kuwa, mbingu na ardhi viliumbwa katika "Ayyam" sita (Quran 11:7). Neno "Ayyam" lina maana mbili (i) siku (ii) nyakati. Wafasiri wa Qurani wa Kissuni, kwa ujumla, humfuata Bwana Kaabul - Ahbar, mtu aliyekuwa wa dini ya Kiyahudi na ambaye alisilimu katika zama za Khalifa wa pili Bwana Umar bin Khattab (r.a.). Hivyo ilikuwa ni jambo la kawaida kwa Bwana Kaab al Ahbar kuzitafsiri aya za Qurani kufuatana na imani yake ya zamani. Hivyo, Bwana huyu aliweka kila aina ya mapokeo ya Kiyahudi katika Uislamu. Ingawa Qurani haikutoa maelelzo yoyote kwa kirefu kuhusu aya hizi, Waislam walizitafsiri aya hizo katika hali ya kuwa kila maelezo ya "Mwanzo" (Kitabu cha Biblia) yalikuwa yameshirikishwa katika tafsiri za Qurani na hivyo basi yakawa sehemu ya mafundisho ya Kisunni.

Lakini wafasiri wa Kishia wamelikataa wazo la kuumbwa kwa Ulimwengu katika siku sita, tangu siku za mwanzoni mwa Uislamu. Kufuatana na tafsiri yao,

BILAL ALLAMAH RIZVI

32

"Ayyam" katika aya hizo lina maana ya "Nyakati" wala si "Siku". Kwa mfano, hebu tazama tafsiri ya Quran ya Bwana Ali bin Ibrahim Qummi (aliyefariki mara tu baada ya mwaka 919 Masihiyya) na Bwana Muhsin Faiz (aliyefariki mnamo mwaka 1680 Masihiyya). Vile vile tazama kamusi ya Qur'ani na Hadith iliyotungwa na Sheikh Fakhruddin Tarihi (aliyefariki mnamo mwaka 1676 Masihiyya). Kufuatana na tafsiri zao, Qur'ani inasema kuwa mbingu na ardhi viliumbwa kwa nyakati sita. (Au tuseme katika "hatua sita").

Hivyo basi, sisi Shia, hatuna wazo lolote lipingalo wazo la kuwa Ulimwengu uliumbwa kwa hatua hatua, wazo ambalo ndilo lililomo katika mafundisho ya mabadiliko na Maendeleo. Zaidi ya hapo, tafsiri yetu si jaribio la kutaka kuitafsiri tena dini yetu - kama wafanyavyo ndugu zetu Wanasara siku hizi, ili kuficha kushindwa kwa Ukristo na Sayansi. Sisi tulikuwa tukilifikiria vivyo hivyo miaka elfu moja kabla ya Bwana Darwin.

Lakini ni lazima tutaje hapa kuwa, kukubali kwetu kuumbwa Ulimwengu kwa hatua hatua, sio kuwa ndio tunaikubali dhana ya Mabadiliko na maendeleo. Watu wenye fikara za Mabadiliko na Maendeleo wanadai kuwa, (1) vitu vyenye uhai hubadilika kizazi hadi kizazi vikitoa vizazi vyenye tabia tofauti na zile za wahenga wao. (2) Mabadiliko haya yametoa vikundi vyote na aina zote za vitu viishivyo siku hizi na vingine ambavyo siku hizi vimepotea. (3) vitu hivi tofauti tofauti viishivyo, vina husiana vyenyewe kwa vyenyewe.

MUNGU WA UISLAMU

33

Lakini kama tulivyosema katika "Faida za dini", hakuna hata ushahidi mmoja wa mabaki ya viumbe vilivyoishi zamani, uonyeshao kuwa viumbe vya namna ya chini viliendelea hadi kufikia namna ya juu. Ni kwa sababu hii kuwa Dakta T.N.Tahmisian (mtaalamu wa mambo ya viumbe vyenye uhai wa Tume ya Nguvu za Atomiki) alisema, "Wanasayansi waendao huko na huko na kufundisha kuwa maelezo kuhusu mabadiliko na maendeleo ni ukweli wa maisha uliothibitika, ni wadanganyifu wakuu na hadithi watoazo kuyaeleza mabadiliko na maendeleo' zaweza zikawa zisizo na ukweli hata kidogo ndani yake. Katika kuyaeleza mabadiliko na maendeleo hakuna ukweli hata kidogo".

Ni tofauti kusema kama tusemavyo (na ushahidi utokanao na mabaki ya viumbe vilivyoishi zamani na makubaliano ya wanasayansi yanatuunga mkono) kuwa Mwenyezi Mungu aliumba ulimwengu huu kwa hatua na aliumba vitu na viumbe vyenye uhai hapa duniani kimoja baada ya kingine kwa nafasi katikati, na kusema kama wasemavyo watu wenye mawazo ya Bwana Darwin au watu wenye mawazo ya kisasa ya Bwana Darwin (na wala hawana ushahidi wowote kuthibitisha hivyo) kuwa vitu vyenye uhai hapa duniani vilitokana na vitu visivyo na uhai na kuwa kiumbe chenye "Cell" (chembe iliyo kama sega la nyuki ya mmea au mnyama iliyo asili ya kitu chenye uhai) moja kama vile "plakton" kiliendelea hatua kwa hatua hadi kuwa mwanadamu.

BILAL ALLAMAH RIZVI

34

SURA YA 12

JINSI WATU WENYE FIKARA ZA BWANA DARWIN WALIVYOPOTEA

Kuna sababu nyingi sana zilizousababisha ule msingi wa kwanza kabisa wa malumbano baina ya dini na wanasayansi. Sasa tuje katika msingi wa pili wa malumbano hayo, ambao ni kule kumkana Mwenyezi Mungu kuhusu kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, sisi Shia na dini nyinginezo (na wanasayansi wengi wa kizazi hiki) hatuafikiani kabisa na fikara za Bwana Darwin. Zifuatazo hapa chini ni sentensi chache zihusuzo maoni yetu.

Mazungumzo yote yaliyotolewa kuhusu "Mabadiliko na Maendeleo" hujaribu kujibu swali lihusulo "Jinsi gani Ulimwengu ulipata kuwa? Lakini hayagusi hata kidogo lile swali jingine kubwa lisemalo, "Na uliumbwa na nani?". Bali Bwana Darwin na wafuasi wake walisema kuwa kwa sababu waliweza kuueleza utaratibu wa kuumbwa kwa Ulimwengu na jinsi utaratibu huo ufanyavyo kazi, hivyo wamethibitisha moja kwa moja kuwa hakuna Mungu. Kusema hivyo ni sawa na kusema kuwa, "Kwa vile ninaweza kueleza jinsi gari lifanyavyo kazi, na naweza kubuni utaratibu wa utengenezaji wake, hivyo moja kwa moja nimethibitisha kuwa hakuna mtengenezaji wa gari hilo.

Inaweza kuonekana kuwa ni upumbavu mtupu kutokana na maandishi haya. Lakini jinsi uendeleavyo kuusoma mkanusho wao wa kuwepo kwa Mwenyezi

MUNGU WA UISLAMU

35

Mungu, ndio jinsi utakavyoweza kuuona udanganyifu huo katika hoja zao:

Sasa hebu ngoja tuutazame udanganyifu mwingine zaidi wa ulahidi. Tumeeleza tayari katika sura zilizopita. Lakini tunarudia kuueleza tena udanyifu huu ili kukupa sura kamili ya jambo hili. Wanadai kuwa "Kitu" hakiwezi kutokea kutokana na "bure". Hivyo basi, kufuatana na msemo wao huo, ni kosa kusema kuwa Mungu ameuumba Ulimwengu huu kutokana na "bure". Ni lazima kuwe na chanzo cha kila kitu. Kwa sababu hiyo wanaamini kuwa jauhari ni kitu cha milele, na kila kitu ni maendeleo ya hiyo jauhari ya milele.

Mstari huu wa hoja huenda moja kwa moja hadi kufikia mahali ambapo palianzia kitu kiitwacho "Uhai". Hakuna hata mtu yeyote aliyefaulu kulitatua fumbo la "uhai". Hakuna mtu ajuaye chanzo cha uhai. Walahidi wakiwa wamekwisha mkana Mwenyezi Mungu, wamelazimika kusema kuwa, hatujui, bali ni lazima kuwa chanzo cha uhai ni hiyo jauhari". Lakini jauhari haina uhai. Kama "Kitu" hakiwezi kupatikana kutokana na "Bure", basi vipi uhai unaweza kupatikana kutokana na kitu "Kisicho na Uhai?"

Si hivyo tu, hebu ngoja tuendelee. Kama wasemavyo kuwa, kila kitu ni lazima kiwe na chanzo. Na kama tujuavyo sote, Jauhari ni kitu. Sasa nini chanzo cha jauhari?

Mambo haya ya ulimwengu hayawezi kuelezwa bila ya kukoma mahali fulani, na kuamini kuwa Ulimwengu ulianza kutokana na mahali hapo. Walahidi husema

BILAL ALLAMAH RIZVI

36

kuwa Jauhari ndio hicho chanzo. Lakini Jauhati haina Uhai. Hivyo, kuwepo kwa uhai hakuwezi kuelezwa kwa njia hiyo. Na Jauhari haina akili. Kuwepo kwa akili na hekima katika wanyama na binadamu hakuelezeki kwa njia hiyo.

Hivyo basi, ikiwa tunataka kupata njia itoshelezayo katika kukueleza kuwepo kwa huu Ulimwengu kwa ujumla ni lazima tukubali kuwa yupo Muumba wa Tangu na tangu ambaye yu Chanzo cha kuwepo kwa huu Ulimwengu. Chanzo cha Uhai, an Chanzo cha Hekima. Naye huyo ni Mwenyezi Mungu.

SURA YA 13

HOJA ZA BWANA RUSELL

Kitabu kiitwacho "Why I am not a Christian (kwa nini mimi si Mkristo)" ni mkusanyiko wa maandishi ya Bwana Bertrand Rusell kuhusu "dini na mambo mengine yenye kuhusiana nayo. " Edita wa Kitabu hicho Profesa Paulo Edwards, anasema kuwa maandishi hayo, pengine ndiyo maandishi yatiayo nguvu zaidi na kutoa mawazo, kuzuri sana kwa mwanafikara aliye huru kutoa mawazo yake tokea zama za mabwana Hume na Voltaire.

Maneno haya yaliyosemwa na Bwana Rusell, yalitosha kumlazimisha mtu kujifunza kitabu hicho kwa

MUNGU WA UISLAMU

37

mategemeo makubwa ya mambo ya Kitaalamu na hoja, kuhusu dini. Jinsi mategemeo hayo yawezavyo kuthibitishwa, inaweza kuonekana kutokana na maelezo haya machache yaliyotolewa hapo chini:

Jambo la kwanza kuja machoni (mwetu) ni kule kutoafikiana kwa hoja hizo. Bwana Russell anajiita mwanafikara huru, na wakati wa majadiliano baina yake na Padre F.C. Copleston alisema kuwa yeye hakuwa kafiri bali alikuwa 'Aginosti" (Aginosti ni mtu aaminiye kuwa sisi wanadamu hatuna habari za Mwenyezi Mungu wala hatuwezi kuzipata).

Maoni ya Makafiri ni kuwa, kutokuwepo kwa Mungu kunaweza kuthibitishwa. Wale waaminio kuwa wanadamu hatuna habari za Mungu wala hatuwezi kuzipata, (maaginosti) wanasema kuwa, mwanadamu hajui na hawezi kujua kuwepo kwa roho katika viumbe, iwe ya Mungu au mwanadamu wala iliyopo katika hali ya baada ya kufa. Wanasema kuwa mwanadamu anaweza kutambua yale ya Ulimwengu huu wa kuonekana (yaani ulimwengu huu uwezao kujulikana kwa mmoja wa milango mitano ya maarifa). Kufatana na maoni yao, haina maana kuwa haiwezekani kuwepo kitu cha kimaarifa (yaani kitu kitambulikacho kimawazo tu) au roho juu ya ulimwengu huu wa kuonekana.

Maaginosti wanazikana hata hoja zile za kikafiri au za watu wasiosadiki kuwepo kwa roho na ulimwengu wa kiroho kwa kusema kuwa mambo hayo ni mafundisho ya kushikilia (yasiyo na msingi wowote) tu. Wanasema kuwa kama huwezi kujua kitu fulani, huna haki ya kukikataa. Jibu la pekee la Maaginosti kwa maswali

BILAL ALLAMAH RIZVI

38

yote yahusuyo roho, Mungu au kuwepo kwa mtu au kitu katika hali ya kiroho hadi sasa ni kuwa, "Sisi hatufahamu na hadi sasa hakuna misingi itoshelezayo hoja zetu itufanyayo tuamini kuwa tutafahamu daima. Kwa maneno mengine ni kuwa, mwanadamu, akiwa mtu wa muda tu, huwezi kuyaelewa mambo ya tangu na tangu na yadumuyo milele.

Padre Copleston alimuuliza Bwana Rusell mwanzoni mwa mahojiano yao (mnamo mwaka 1948 Masiyyah). "Labda utaweza kunieleza kama maoni yako ni sawa na yale ya Uaginosti au yale ya ukafiri. Maana yangu ni kuwa, je, utasema kuwa huko kutokuwepo kwa Mwenyezi Mungu kunaweza kuonekana? Bwana Rusell alijibu: "Hapana, sisemi hivyo; maoni yangu ni kama yale ya aginosti."

Kama Bwana Russell aliuamini 'Uaginosti' basi jibu lake kwa maswali yote yanayomhusu Mwenyezi Mungu, au maisha ya baada ya kufa ni lazima liwe "Sijui". Lakini badala yake, mwanzo kabisa mwa kitabu hicho anaamua, "Ninaamini kuwa nitakapokufa nitaoza na hakuna chochote kitakacho salia kuhusu nafsi yangu."

Mfano mwingine Bwana Rusell anasema mwanzoni kabisa mwa Utangulizi wa kitabu chake:

"Nafikiri dini zote kubwa za ulimwenguni, - Budha. Dini ya Kibaniani, Ukristo, Uislamu na Ukomunisti zote hazina ukweli na ni zenye madhara. Ni dhahiri kutokana na hoja zetu kuwa, kwa sababu dini hizo haziafikiani zenyewe kwa zenyewe si zaidi ya moja yao tu inayoweza kuwa ya kweli."

MUNGU WA UISLAMU

39

Baada ya kusema hivi, kila mtu atategemea kuona kuwa mwandishi huyu anazichunguza dini hizo na kuona ni kwa nini hakuna hata moja yao iliyokuwa ya kweli. Lakini hakuhisi kuwa yu wajibiwa katika maandishi yake yoyote yale kuzileta hoja zake katika mwishilizo wa kihoja. Alisema tu kuwa, "Kwa sababu haziafikiani zenyewe, si zaidi ya moja yao tu inayoweza kuwa ya kweli" na kisha kwa maamuzi yake yeye mwenyewe bila ya kanuni maalum, aliamua kuwa hakuna hata moja kati ya dini hizo iliyokuwa ya kweli.

Upumbavu huu unaendelea toka maadishi haya hadi yale na msomaji humaliza kukisoma kitabu hicho akiwa bado yuna mawazo ya kuwa, kama maandishi haya yangeliandikwa na mtu mwenye elimu ndogo (kuliko yeye Bwana Rusell), bila shaka watoa habari wasingelijishughulisha kuzitoa habari hizo.

"Labda hoja iliyorahisi sana kuielewa ni ile ya 'kisababisho cha kwanza'. (Imethibitishwa kuwa kila kitu tukionacho katika hii dunia kina kisababisho chake na kwa kadri urudivyo nyuma zaidi na zaidi katika mfululizo wa hivyo visababisho bila shaka utakifikia kisababisho cha kwanza kabisa na kile kisababisho cha kwanza mnakipa jina la Mungu)... Ninaweza kusema kuwa nilipokuwa kijana nilikuwa nikihoji vikali sana kichwani mwangu kuhusu maswali haya. Kwa muda mrefu sana niliikubali hoja ya kisababisho cha kwanza, hadi siku moja nilipokuwa na umri wa miaka 18, nilisoma maandishi ya Bwana John Stuart Mill na katika maandishi hayo nilikuta sentensi hii isemayo "Baba yangu alinifundisha kuwa, swali la "Nani aliyeniumba?" Haliwezi kujibiwa kwa sababu linamfanya mtu afikirie

BILAL ALLAMAH RIZVI

40

swali jingine la, "Nani aliyemuumba Mwenyezi Mungu? Sentensi ile rahisi sana imenionyesha, kama ninavyofikiria hadi sasa, hoja ya udanganyifu iliopo katika hoja ya kisababisho cha kwanza."

Sasa labda Bwana Rusell amezinakili hoja za wenye kuamini kwa kukosea tu bila ya yeye mwenyewe kupenda. Ili kujikumbusha, msomaji anaombwa asome tena sura ya 2 na ya 3 ya kitabu hiki. Katika sura hizo atakuta sentensi hizi:-

"Kwa sababu kila kitu katika huu ulimwengu kimo mwenye mkumbo ule wa vita vya Muda (Mumkinul - Wujud), kina uhusiano wa kawaida na kuwa au kutokuwa. Hapo mwanzoni vitu hivi havikuwepo, hivi sasa vipo; na siku fulani baadaye vitatoweka. Kwa kutegemeana na asili yao, haviwezi kudai kuwepo au kukoma kuwepo."

Na kisha hufuatia jambo muhimu sana ambalo Bwana Rusell amelikosea. Jambo hilo ni kuwa, chanzo au kisababisho kile, ni lazima chenyewe kisiwe cha muda tu, na sivyo chenyewe nacho kitahitaji chanzo au kisababisho cha kukifanya kiwepo. Na mfululizo huu wa Visababisho na athari LAZIMA ukomee katika kisababisho ambacho hakihitaji chanzo au kisababisho kingine kisicho hicho chenyewe, kwa kuwepo kwake. Imamu maana ya kuwa, chanzo au kisababisho cha mwisho cha huu ulimwengu ni LAZIMA kiwe kijitoshelezacho chenyewe katika kuwepo kwake.

Kama mtu akizilinganisha hoja za Kiislamu za kisababisho cha kwanza (kama zilivyoelezwa katika

MUNGU WA UISLAMU

41

kitabu hiki) na zile za Kanisa kama vilivyotolewa na Bwana Rusell mwanzoni, mtu anaona tofauti mbili kubwa:

Anasema: "Kila kitu tukionacho katika hii dunia kina kisababisho." Lakini ni haki angelisema: "Kila tukionacho katika hii dunia ni cha muda tu, nacho ni lazima kiwe na kisababisho cha kukifanya kiwepo."

Tena anasema, "Jinsi urudivyo nyuma zaidi na zaidi katika mfululizo huu wa visababisho ni lazima utakifikia Kisababisho cha Kwanza." Lakini ni lazima angelisema: "Ni lazima utakifikia kisababisho kisicho cha muda tu, chenye kujitosheleza kwa kuwepo kwake (ambacho asili yake ni huko kuwepo kwenyewe)."

Yasome maelezo haya na marekebisho haya, na tazama jinsi ukanusho wake unavyopoteza kila nguvu yake.

Bwana Rusell aliona kuwa itatosha kuidhihaki hoja hii kwa haraka tu. (Anasema): "Ninaweza kukieleza kile ambacho kwangu mimi kinaonekana kama hoja za kidanganyifu (za wenye kuamini). Kila mtu ambaye hivi sasa yuaishi, anaaye mamie na mimi nionavyo ni kuwa, hoja (zao) ni kuwa kwa hiyo, asili ya mwanadamu ni lazima iwe na mamae, lakini ukweli ni kuwa asili ya mwanadamu haina mama."

Ninaona, ni yeye huyu Bwana Rusell ambaye anajitia katika udanganyifu. Ameshindwa kugundua kuwa waaminio hawasemi kuwa, "kila kitu cha muda kina kisababisho cha muda, hivyo basi, ulimwengu mzima ni lazima uwe na kisababisho cha muda.

BILAL ALLAMAH RIZVI

42

Hoja zetu ni kuwa, kwa kuwa kila kilichomo katika huu Ulimwengu ni cha muda tu, na kwa vile mkusanyiko wa mabilioni ya vitu vya muda bado yatabaki kuwa vitu vya muda tu, Ulimwemngu mzima bado ni wa muda tu, na hivyo basi ni lazima uwe na kisababisho kingine kisicho huo Ulimwengu wenyewe cha kuufanya uwepo. Na kisababisho hich ni lazima kijitosheleze chenyewe katika kuwepo kwake. Na kwa sababu yuajitosheleza kwa huko kuwepo kwake, swali, Nani aliyemuumba Mungu? Haliwezi kutokea hata kidogo.

SURA YA 14

ULIMWENGU ULIUMBWA KWA BAHATI TU BILA YA MUUMBA?

Bwana Rusell aliendelea kuandika hivi: "Kama inawezekana kuwepo kitu bila ya kisababisho, ingeliwezekana pia Ulimwengu kuwa kama Mwenyezi Mungu".

Sababu ya Ulimwengu kutoweza kuwepo bila ya kisababisho ni kuwa vitu vilivyomo humo wakati fulani huwapo na wakati mwingine hukoma kuwepo. Hivyo hakuna chochote katika hali yao na katika asili yao kudai kupasika kuwepo. Kama vipo, ni kwa sababu ya mkono (fulani) ulioinua mizani ya kuwepo. Kama vikikoma kuwepo ni lazima iwe ni kwa sababu ule mkono umeinamisha upande wa kutokuwepo.

Bwana Rusell (anasema): "Wala hakuna sababu kwa nini (Ulimwengu) usiwe wa tangu na tangu".

MUNGU WA UISLAMU

43

Dai la kuwa huenda ulimwengu ulikuwepo tangu na tangu unakanushwa na fafanuzi za sayansi tulizonazo siku hizi. Hii ni tofauti kabisa na ukweli uliopo kuwa vitu vyenye kuwepo kwa muda tu haviwezi kuishi milele.

Msomaji anaombwa kuisoma tena sura ya 7 ambayo itamweleza kuwa maoni yoyote yale mtu ayachukuayo, jauhari haiwezi kuthibitishwa kuwa ni ya milele (bila ya mwanzo wala mwisho).

Kisha anasema tena: "Hakuna sababu kwa nini Ulimwengu usiweze kuwepo bila ya kisababisho."

Kabla ya kuendelea zaidi kuhusu sensenti hii, ngojea ninakili maneno yake (kutoka katika makala hayo hayo ambapo alilikanusha wazo la kuwa kuna sheria 'fulani' ya kiasili. Anasema:-

"Kama tujuavyo sote kuna sheria kuwa, kama ukitupa dadu utapata upande wenye dati sita mara mbili tu katika (kila) mara thelathini na sita (upatazo) na wala hatuyachukulii matokeo haya (ya mchezo wa dadu) kuwa ni ushahidi kuwa kuanguka kwa dadu kunarekebishwa na ule usanii. Kinyume na hayo, kama zile sita mbili hutokea kila mara ni lazima tufikirie kuwa kulikuwa na usanii.

Hapa Bwana Rusell anakubali kuwa, kama tukio linatukia mfululizo tena na tena itathibitika kuwa kulikuwa na usanii. Sasa, mtu atashangaa kuona ni kwa nini Bwana Rusell hakutumia hata muda Kidogo tu kuichunguza misogeo iliyotengenezwa vizuri sana na iliyofanywa vizuri sana ya 'magalaksi' (makundi ya nyota

BILAL ALLAMAH RIZVI

44

zisizopambanulika kwa macho matupu), nyota, sayari na miezi?

Hebu natufikirie kuwa yupo mtu fulani katika anga la juu ambaye hajawahi kusikia habari za dunia au wanadamu. Siku moja atakapoiona roketi ikipita na baada ya muda kidogo nyingine tena inapita kisha nyingine tena inapita. Hakika, njia na mielekeo yao si mmoja, na muda baina ya mitokeo yao si ya utaratibu mmoja ili kwamba uweze kupimwa na kukisiwa kabla. Lakini anajua kuwa kila roketi ina maelfu ya sehemu mbalimbali ambazo zinaungwa pamoja na zote kwa pamoja zinafanya chombo hicho kiwe kizuri sana.

Je, vipi Bwana Rusell atamfikiria mtu huyo kama angeliamua kuwa hizo roketi zimekuwepo bila ya mtengenezaji?

Na angeliulaumu vikali kiasi gani ufidhuli wa mtu huyo wa angani, kama roketi zote zingelirekebishwa vizuri sana katika njia zao na mfululizo wao?

Na kumbuka kuwa hizo roketi hazihusiani zenyewe kwa zenyewe. Zilinganishe hizi roketi na huu Ulimwengu wenye mamilioni ya 'magalaksi' yasiyo hesabika na kila 'galaksi' likiwa na mamilioni ya majua, na kila jua likiwa na sayari nyingi zilizunguukalo, na kila sayari ikiwa na miezi kadhaa n.k.

Na vyote hivyo 'Vimeshikana' pamoja katika nyororo ya nguvu na uvutano, kila kimoja kikimvuta kwake jirani yake na hicho nacho kikivutiwa na huyo jirani yake. Na kisha hebu fikiria kuwa Bwana Rusell anasema kuwa,

MUNGU WA UISLAMU

45

kuwa hivyo hakuwi uthibitisho wowote wa kuwepo kwa usanii fulani.

Profesa Frank Allen aliyekuwa Professa wa fizikia wa Chuo Kikuu cha Manitoba nchini Canada aliandika hivi katika makala yake, "Asili ya Ulimwengu, Ni kwa Bahati tu au kwa Usanii'.

"Kama mwanzoni mwa maisha hakukuwa na usanii, basi vitu vyenye kuishi ni lazima vingelitokea kwa bahati tu. Sasa bahati, au kuyumkinika kama kunavyoitwa ni tawi lilioendelea sana la somo la kihesabu ambalo huhusika na ile elimu pana sana ambayo hatuwezi kuwa na uhakika nayo kabisa. Tawi hili la elimu hutupatia kanuni zikubalikazo sana ambazo kwazo tunaweza kuupambanua ukweli na uongo na kutafuta uwezekano wa kutokea na aina ya tukio fulani."

Protein ni sehemu muhimu ya seli zinazoishi, nazo zina vitu vitano ndani yake, kaboni, hewa ya haidrojeni hewa ya naitrojeni, hewa ya oksijeni na kiberiti (dawa) kwa kipimo cha karibuni atom 40,000 katika kila molekiu (kipande kidogo sana cha kitu chenye tabia za kitu hicho). Kwa vile, kikemia kuna vitu vya kiasili (elements) 92 katika ulimwengu zilizotapakanywa kila mahali, bahati iliyovifanya vitu hivi vitano vikutane na kufanya molekiu; kiasi cha jauhari ambacho lazima kila mara kinatikiswa na kiwango cha muda uhitajikao kwa kumalizia kazi hii, vyote vinaweza kukadiriwa. Mwana hesabu wa Kiswisi, Bwana Charles Eugen Guye (ambaye maneno yake yamenakiliwa na Bwana V.H. Mottran katika makala yake ("Ushirikiano wa Viungo") iliyotokea katika gazeti la Liner, la tarehe 22 April 1948)

BILAL ALLAMAH RIZVI

46

alifanya hesabu na akagundua kuwa matukio hayo 10160 kwa 1 au katika 10160, yaani 10 ukizidisha kwa yenyewe mara 160, nambari iliyo kubwa zaidi kiasi cha kutostahili kuelezeka kwa maneno (kuiandika namba hii ni lazima baada ya kuandika 1 uongeze sifuri 160). Kiasi cha jauhari kihitajikacho kutikiswa ili kitoe molekiu moja ya 'Protein' ni ukubwa wa mamilioni ya hii jauhari yote iliyoko Ulimwenguni hivi sasa. Kwa ajili ya jauhari hii kutokea tu katika dunia, itahitaji miaka mingi sana, karibuni mabilioni ya miaka (10243) (ili kuipata nambari hii andika 1 na kisha andika sifuri 243). Protein zinatengenezwa kutokana na nyororo ndefu iitwayo 'aminedcides'.

Jinsi hizi 'aminedcides' zinavyopangwa ni jambo muhimu sana. Ikiwa zitakaa vibaya, hazitaweza kuuruhusu uhai kubakia katika kiumbe hicho na pia zinaweza kuwa aina fulani fulani za sumu. Profesa J. B. Leathes (wa Uingereza) amefanya hesabu na kugundua kuwa viungo vya nyororo ya hizi 'aminedcides' katika protein ya kawaida tu inaweza kuwekwa katika mamilioni ya aina (1048) (yaani baada ya kuandi 1 uweke sifuri 48 mbele ya hiyo moja). Ni vigumu sana kwa bahati hizi zote kutokea ili kuweza kuijenga molekiu ya protein.

Lakini tunaona kuwa kuna mabilioni yasiyohesabika ya molekiu za protein katika mwili wa mwanadamu, achilia mbali dunia nzima.

Hizi 'aminedcides' zinaendela kutengenezwa tena kwa utaratibu fulani, na vivyo bado Bwana Rusell anashikilia utartibu wake wa 'Bahati'.

MUNGU WA UISLAMU

47

Profesa Frank Allen anaendela kusema:-

"Lakini protein zikiwa katika hali ya kemikali (dawa) hazina uhai, ni baada ya kupata uhai ndipo huanza kuishi. Ni Akili ya Milele tu (yaani Mungu) Ambayo ilijua kabla kuwa molekiu hiyo itakuwa maskani ya uhai; na ndiyo ambayo ungeliweza kuitengeneza na kuihuisha."

Bwana Rusell amejitahidi sana kuipinga hoja hii, kwa maneno haya:-

"Nyote mwajua hii hoja ya (kuwa Ulimwengu unatokana) na usanii: Kila kitu katika huu Ulimwengu kimetengemezwa ili kiweze kuishi hapa duniani, na kama Ulimwengu ungelikuwa tofauti japo kidogo tu na hivi ulivyo sasa, tusingeliweza kuishi ndani yake. Hivyo ndiyo hoja itolewayo kuhusu kuwepo usanii. Wakati mwingine hoja hii huchukua umbo la ajabu, kwa mfano, watu husema kuwa sungura wana mikia miyeupe ili waweze kupigwa risasi (au kufumwa) kwa urahisi. Sijui fikara hizi zitakuwaje katika mawazo ya hao sungura wenyewe. Ni hoja rahisi sana kuiga kwa ajili ya kuwachekesha watu. Ninyi nyote mwajua maneno ya Bwana Voltaire, kuwa kwa hakika pua ilitengenezwa kuwa hivyo ili ifae kwa miwani. Maneno haya ya kuchekesha yamegeuka na kuwa karibuni si yenye kusikika sana kama ambavyo yangelipaswa kuwa katika karne ya kumi na nane, kwa sababu tangu zama za Bwana Darwin tunajua vizuri sana kwa nini viumbe vyenye uhai vinapatana na mazingira yao. Sio kuwa mazingira yao yalitengenezwa ili yafae kwa viumbe hivyo, bali viumbe hivyo vimekuwa ili vifae kwa hayo mazingira, na huo ndio msingi wa upatano wa viumbe

BILAL ALLAMAH RIZVI

48

hivyo na mazingira yao. Hakuna ushahidi wowote kuhusu usanii wa jambo hilo."

Hebu na tuchukulie tu kuwa viumbe vyenye uhai vimejifanya vipatane na mazingira yao. Lakini, je Rusell alikuwa kipofu kuhusu ukweli kuwa muda mrefu sana kabla ya kuwepo "viumbe vyenye uhai" ilitokea hii dunia kwanza. Hii dunia hewa yake, Umbo lake lote, pamoja na uhusiano wake na jua na sayari zingine na mwezi "umetengenezwa" katika hali ya kuwa kuwepo kwa maisha kuwezekane kila wakati. Je, Bwana Rusell anatutaka tuamini kuwa viumbe vyenye uhai, yaani wanyama na wanadamu, kabla ya kuwepo kwao, viliushawishi mpango wote wa Ulimwengu kwa ujumla na kule kuwepo kwa hii dunia hasa, ili ziweze kuwepo hapa kwa mamilioni yasiyoelezeka ya miaka baadaye?

Bwana Frank Allen ameandika katika makala hayo hayo hivi: Marekebisho ya dunia hadi kutokea uhai ni mengi sana kiasi cha kutostahili kuwepo kwa bahati tu.

Kwanza dunia ni tufe (mviringo) lililosimikwa angani katika mzunguko wa kila siku, katika mhimili wake, ukitoa mabadiliko ya mchana na usiku, na katika mzunguko wa mwaka kulizunguka jua. Misogeo hii huimarisha kule kuiweka sawa hii dunia katika anga, na ukishirikiana na mwinamo (nyuzi 23) wa mhimili kuelekea katika sehemu ya mzunguko wake (njia ya jua angani), hutoa utaratibu wa majira, hivyo huufanya kuwa maradufu ile sehemu ya dunia iliyokaliwa na watu na kutia tofauti nyingi katika maisha ya mimea kuliko vile ambavyo dunia isiyozunguka ingeliweza kufanya.

MUNGU WA UISLAMU

49

Pili, hewa inayofaa kwa maisha ya viumbe, ina tabaka kubwa la kutosha (karibuni maili 500) na ni nene vya kutosha kuifunika dunia ili kuihifadhi, kutokana na mgongano mbaya sana kati yake na vimondo milioni ishirini ambavyo huangukia duniani kila siku kwa mwendo wa karibuni maili thelathini kwa nukta. Miongoni mwa kazi nyingine nyingi zifanywazo na hewa, vilevile hewa hurekebisha hali ya hewa kuwa katika hali ya usalama kwa maisha ya viumbe; na huchukua pamoja nayo kiasi cha kutosha cha unyevunyevu wa maji matamu ndani barani kabisa kutoka baharini na kuinywesha ardhi ambayo bila ya kuweko hivyo, ardhi ingelikuwa jangwa lisilo na uhai. Hivyo basi, kwa hewa hiyo tunapata magurudumu ya kuurekebishia ulimwengu.

"Sifa nne kubwa za maji, nguvu yake ya kufyonza kiasi kikubwa cha oksijeni katika hali ya hewa yenye joto dogo sana, ujoto wake wa juu sana katika nyuzi 4 centigrade juu ya mgando wa maji, ambapo maziwa na mito hubakia katika hali ya umaji maji, uzito mdogo wa barafu kuliko ule wa maji ili kuwa hiyo barafu ibakie juu a maji na nguvu ya kutoa joto jingi inapoganda, inahifadhi maisha (ya viumbe) katika bahari, maziwa, na mito katika muda mrefu wa kipupwe".

"Nchi kavu inafaa kwa maisha ya kidunia." udongo hutupa madini ambayo maisha ya mimea huyatumia na kuyabadili kuwa chakula kifaacho kwa wanyama. Kuwepo kwa madini yenye asili ya chuma karibuni na uso wa ardhi huufanikisha ustarabu.

BILAL ALLAMAH RIZVI

50

Udogo wa dunia ukiulinganisha na ukubwa wa anga pengine inakatisha tamaa sana kulizungumzia jambo hilo (maana dunia huwa ndogo sana). Kama dunia ingelikuwa ndogo kama mwezi: kama ingelikuwa na kipenyo cha moja kwa nne (robo) ya kipenyo chake cha sasa; kama nguvu yake ya uvutano(ingelikuwa moja kwa sita ya ile ya dunia) hivi sasa, ingeshindwa kushikilia hewa na maji na joto lingelikuwa kali sana. Kama kipenyo chake kingelikuwa maradufu ya hiki cha hivi sasa, huo uso wa dunia ungelikuwa na ukubwa wa mara nne ya huu wa sasa na mara mbili ya ile nguvu yake ya uvutano ya hivi sasa. Tabaka la hewa lingelipunguka sana na kusababisha hatari kwa viumbe vyenye uhai na msukumo wa hewa (air pressure) ungeliongezeka toka ratili 15 hadi ratili 30 kwa kila eneo la nchi ya mraba, uzito ambao ungeliharibu uhai hapa duniani. Eneo la bonde lingeongezeka sana na ukanda uliokaliwa na watu ungelipungua sana. Jamii za wanadamu zingelitengwa sana, safari na mawasiliano vingelikuwa taabu sana na karibuni visingeliwezekana.

"Kama hii dunia yetu ingelikuwa na ukubwa kama wa jua, lakini ikabakia na uzito huu huu, nguvu ya uvutano ungelikuwa mara 150 ya hii ya sasa; tabaka la hewa lingelikuwa na unene wa maili nne tu, kuyeyuka kwa maji na kuwa mvuke kusingeliwezekana, na uzito wa hewa ungeliongezeka na kuwa zaidi ya tani moja katika kila eneo la inchi ya mraba. Mnyama aliye na uzito wa ratili moja, angelikuwa na uzito wa ratili 150, na wanadamu wangepungua ukubwa na kuwa na ukubwa kama ule wa kindi (sindi au sidiri). Kuwepo kwa akili kusingeliwezekana kwa viumbe kama hao."

MUNGU WA UISLAMU

51

"Kama ardhi ingelisogezwa na kuwa mara dufu ya umbali huu toka juani, joto ilipatalo lingelipungua na kuwa robo tu ya hili la sasa; mwendo wake katika kujizungusha yenyewe (katika mhimili wake) ungelikuwa nusu tu ya huu wa sasa; urefu wa majira ya kipupwe ungelikuwa mara mbili ya huu wa sasa, na kila kitu chenye uhai kingelikufa kwa baridi. Kama umbali wake kutoka juani ungelikuwa nusu ya huu wa sasa joto ambalo tungelipata lingelikuwa mara nne ya hili tupatalo sasa. Mwendo wake katika kujizungusha yenyewe (katika mhimili wake) ungelikuwa maradufu; majira yangelikuwa na urefu wa nusu tu ya haya ya sasa. Kama mabadiliko yangeliweza kuathiriwa na sayari hii (Dunia) ingeliunguzwa sana kiasi cha kutoweza kuweka kiumbe chenye uhai ndani yake. Kwa ukubwa (huu wa sasa) na umbali (huu wa sasa) kutoka juani, na mwendo wake (huu wa sasa) katika kujizungusha yenyewe (mwenye mhimili wake), dunia inaweza kuuhifadhi uhai ndani yake ili kuwa mwanadamu aweze kupata maisha ya furaha kimwili, kiakili na kiroho kama ilivyo hivi sasa.

SURA YA 15

NJIA YA USALAMA KWA MUAGINOSTI

Kama ilivyoelezwa hapo mwanzoni, Bwana Rusell alidai kuwa yu muaginosti. Kama tukilichukulia dai lake kama lionekanavyo, basi njia nzuri na ya usalama kwa Bwana Rusell ingelikuwa ni kuamini kuwepo kwa Muumba na siku ya Hukumu.

BILAL ALLAMAH RIZVI

52

Kuna hadithi ya Imamu wetu wa sita Hadhrat Jaafat as-Sadiq (a.s) isemayo kuwa:-

Ibn Abil Awja na Ibn Muqaffa walikuwa wamekaa katika Masjidul Haram wakati wa Hija pamoja na baadhi ya makafiri wenzao. (walijifanya Waislamu ili kujihifadhi na madhara, lakini walikuwa kila mara wakibishana kuhusu imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu). Ibn Muqaffa aliashiria kwa kidole chake kwenye sehemu karibu na Kaaba: "Unaliona hili kundi la watu? . Hakuna yeyote pale awezaye kuitwa mtu ila yule mzee (yaani Imam Jaafar as-Sadiq (A.S). Hao wengine ni kama ng'ombe na wanyama tu".

Ibn Abil Awja alimuuliza vipi alithubutu kusema hivyo.

Ibn Muqaffa akasema: "Kwa sababu nimeona kuwa yuna (uadilifu na elimu) ambavyo sikupata kuviona popote pale".

Ibn Abil Awja akasema "Sasa ni lazima nijaribu na kuona kama usemavyo ni kweli".

Ibn Muqaffa alijaribu kumshauri asifanye hivyo. Lakini Ibn Awja alimwendea Imamu (A.S). Baada ya muda fulani alirudi na akasema:- Ewe Ibn Muqaffa, yeye si mwanadamu tu. Kama katika Ulimwengu huu kuna kitu cha kiroho... ambacho hugeuka na kuwa kitu chenye umbo la kuonekana kipendapo kuwa hivyo, na kugeuka tena katika hali ya kiroho kipendapo kuwa hivyo, basi kitu hicho ni yeye (mtu huyu).

Ibn Muqaffa akasema: Vipi?

MUNGU WA UISLAMU

53

Ibn Abil Awja akasema: Nilikaa karibu naye. Watu wote walipoondoka, alianza kusema (bila ya mimi kumuuliza chochote) kuwa:-

"Kama ukweli ni kama waaminivyo, naye (Mwenyezi Mungu) yu kama wasemavyo (Mahujaji), basi wataokolewa nanyi mtakuwa taabuni. Na kama ukweli ni kama ninyi (walahidi) msemavyo, na sio kama wasemavyo wao (mahujaji), basi ninyi na wao nyote mtakuwa sawa (na hakuna dhara litakalomuangukia yeyote yule).

Nilisema, "Mwenyezi Mungu naakuwie radhi ni nini kile wasemacho? Imani yangu na imani yao ni moja tu".

Imam (a.s) alisema "Vipi imani yako na imani yao yaweza kuwa moja? Wao wanasema kuwa kutakuwepo na ufufuo, na thawabu na adhabu, na wanaamini kuwa kuna Mungu. (Na ninyi hamuamini hivyo).

Imamu (a.s) alikuwa na maana kwamba, kama kweli hakuna Mungu na hakuna siku ya Kiama, kama Ibn Awja alivyosema, basi waaminio na makafiri watakuwa katika hali moja baada ya kufa. Wote watapotea kabisa na hakuna yeyote atakayeadhibiwa kwa imani yake au kutoamini kwake. Kwa upande mwingine, kama yupo Mungu na siku ya Kiama, kama wasemavyo wale waaminio, basi baada ya kufa, wale waaminio wataokolewa na watabarikiwa, na Walahidi na makafiri wataadhibiwa. Hivyo basi itakuwa ni busara nzuri kumwamini Mungu na siku ya Kiama ili kujiokoa

BILAL ALLAMAH RIZVI

54

kutokana na uwezekano wa kuwepo laana na adhabu ya milele.

Msomaji anaombwa kusoma tena Sura ya 5 ya kitabu chetu kiitwacho: "Faida za Dini", inayohusu "Hoja ijulikanayo kama 'Hoja ya Pascal".

SURA YA 16

HUU ULIMWENGU NI USHAHIDI WA KUWEPO KWA

MUNGU MMOJA

Mpango wa ajabu wa huu Ulimwengu unazidi kuonekana kutokana na maendeleo ya Sayansi. Ulikuwepo wakati ambao, dunia ilifikiriwa kuwa ndio kitovu (senta) cha ulimwengu.

Imamu wetu wa tano Hadhrat Imam Muhammad Baqir (a.s) aliwaelezea wafuasi wake kuwa kuna Ulimwengu nyingi sana mbali na ule walioujua. Lakini ni ajabu kuwa, Waislamu waliyakataa mafundisho yake na wakawafuata mafilosofia wa kikafiri kama vile, Ptolomy aliyefikiria na kufundisha kuwa dunia imetulia na sayari za angani zinaizunguka dunia. Matokeo yake ni kuwa, lango la elimu lilibakia katika hali ya kufungwa kwao kwa muda wa zaidi ya miaka elfu moja. Baadaye ulifika wakati ambao watu waliugundua huu utaratibu wa Ulimwengu kwa masaada wa darubini. Hivyo wakalipa jua heshima hiyo waliyokuwa wakiipa dunia. Siku hizi tunajua kuwa Ulimwengu wetu ni jamii kidogo sana ya sayari nyingi na kuwa hii jamii ya ulimwengu wetu iko

MUNGU WA UISLAMU

55

ukingoni mwa galaksi kubwa sana ambalo tunaliita "Milky Way".

Tunauona mwezi ukizunguka dunia, kama vile afanyavyo mtoto mwenye furaha akicheza kwa furaha kumzunguka mama yake. Kuna sayari 8 zinginezo, ukiiacha hii dunia yetu, katika jamii ya hili jua letu, na 5 kati ya hizo zina sayari zao (miezi) ndogo. Mars na Neptune zina miezi miwili kila mmoja. Jupitor ina miezi 12, na visayari vidogodogo vingine. Saturn ina miezi 9 na Uranus in miezi 5. Miezi hiyo na visayari vidogodogo vyote hivyo vinazizunguka sayari zao. Na hizi sayari zote zinalizunguka jua, ambalo tunaweza kuliita 'Mkuu wa Jamii'.

Sasa hebu, tuzirudie zile hatua zetu kabla ya kuendelea zaidi.

Nyota zote hizi, Sayari na miezi midogo midogo vimetengenezwa kwa 'Atom' na hiyo Atom yenyewe ni picha ndogo ya jamii ya jua. Hapo zamani iliaminiwa kuwa hizi atom ni vitu visivyo gawanyika, lakini siku hizi inajulikana kuwa 'atom' zina sehemu nyingi, Imani ya kutoweza kugawanyika kwao imekomeshwa. Atom ina 'neucleus' na 'electron' kadhaa. Neuclius imejengwa kwa sehemu rahisi sana: neutrons na protons. Neucleaus iko katikati ya atom na imezungukwa na electrons. Ni lazima tueleze hapa, ili kuifanya picha hii eleweke zaidi, kuwa neucleus ya atom ni sehemu ya kinusu kipenyo (radius) kidogo sana, lakini yenye uzito mkubwa kupita kiasi. Kwa maneno yaliyowazi zaidi, aina zote za uzito wa kiatom (ila sehemu ndogo iwezayo kubeuliwa) uko katika neucleus, na ukubwa wa

BILAL ALLAMAH RIZVI

56

hiyo neucleus ni mdogo kuliko moja ya laki moja ya ukubwa wa atom. Na usisahau kuwa zaidi ya atom 100,000,000 zinaweza kuwekwa kwa kupangwa katika urefu wa sentimeta moja. Sasa, kama tulivyoeleza hapo mwanzoni, atom pekee ni Ulimwengu mzima. Protons na Neutrons zinaonekana kama kwamba zinazunguuka katika mihimili yao, kama ncha inayozunguka. Mzunguko wao unaonyesha (kuwepo kwa) mzunguko wa ndani.

Hivyo, tunaona kuwa upo muundo mmoja wa kazi, tangu sehemu hiyo iliyo "atom" ndogo, hadi kwenye ulimwengu mzima.

Lakini bado, huu si mwisho wa hadithi hiyo.

Kama tulivyokwisha kutambua kuwa, Jua, pamoja na jamii yake yote, liko katika ukingo wa galaksi la Milky Way, "Kama tunao uwezo wa kulitazama galaksi la Milky Way kwa mbali na kuliona lote zima, tungeliweza kuona kitu kama gurudumu la nyota lililosawa. lenye mkono wa kuzungushia kama vile macheche ya fataki (au kiberiti cha mchezo). Milky Way ina mamilioni ya nyota kama vile hili Jua letu. Mfano huu wa nyota umeungwa pamoja kwa nguvu ya uvutano na husogea angani kwa pamoja. Usanii huu huitwa 'Galaksi'.

Kama tukifikiria kuwa usanii huu wa jamii ya jua letu ni jamii ya nyota, basi galaksi ni lazima liitwe kabila kubwa sana, lililo na mamilioni ya jamii hizo.

Kuwepo kwa magalaksi mengi kulifahamika tangu zamani. Mnamo mwaka 1920 hivi, ilidhaniwa kuwa yapo magalaksi 500,000 hivi. Siku hizi, uchunguzi

MUNGU WA UISLAMU

57

uliofanyika kwa darubini zenye nguvu sana, idadi hii imeongezeka hadi kufikia 100,000,000 na inaongezeka kila siku. Kutegemeana na tuwezavyo kuona kwa kamera na darubini, kuna mafungu na mafungu ya magalaksi.

Ujuzi wa mwanadamu siku hizi, bado u katika hatua ya mwanzo kabisa. Hakuna ajuaye kilichoko nyuma ya haya magalaksi. Wala hatuna ujuzi mkubwa kuhusu hali ya hiyo misogeo yao. Qurani Tukufu inasema:-

Mwenyezi Mungu ameipamba (hii) mbingu ya karibuni (nanyi) kwa mataa (yaani hizi Nyota) (Quran 41:12).

Hivyo tunajua kuwa mpaka sasa bado hatujaona hata mwishoni mwa hili anga la kwanza. Na basi ni nani ayajuaye hayo maajabu yaliyojificha nyuma ya hili anga la kwanza! Mwenyezi Mungu anatuambia:-

"............... nanyi (wanadamu) hamkupewa elimu ila kidogo tu. (Quran 17:85)

Hivyo basi acha tuyakomeshe haya mazungumzo yetu katika hiki kiasi tujuacho. Tunajua kuwa sehemu za atom zinajizungusha zenyewe; visayari (miezi) vinazizunguuka sayari zao; sayari zinazizunguka nyota (jua) zao; na kila nyota na jamii yake nzima vinazunguka katika hayo magalaksi yao.

Imani yetu katika Umoja wa Mwenyezi Mungu inatokana na hali ya usanii wa huu Ulimwengu. Tumetoa thibitisho nyingi sana za Imani yetu katika karne zote 14 zilizopita. Sasa sayansi imeifungua njia mpya ambayo pia humuongoza mtu kwenye imani ya

BILAL ALLAMAH RIZVI

58

Umoja wa Mwenyezi Mungu. Imani yetu inaweza kufafanuliwa kwa ufupi sana katika maneno haya. "Huu usanii wa ulimwengu ulio sawasawa ni uthibitisho usiokanushika kuwa usanii wote huu umefanywa na Muumba mmoja tu.

Tunapoziona saa mbili zilizofanana hatuhitaji kuambiwa kuwa saa hizo zimetengenezwa katika kiwanda kimoja. Hivyo hivyo, tunapouona Ulimwengu katika hali ya mfano mmoja tu, sehemu zake zote zikitawaliwa na sheria ile ile na zote zikifanya kazi pamoja, silika zetu za kiasili zatuongoza kwenye imani ya kuwa Ulimwengu huu umetengenezwa na kutawaliwa na MUUMBA MMOJA TU.

Na hakika kuna tofauti kubwa kati ya saa na Ulimwengu. Saa zinaweza kuigwa au kurudifiwa na wadanganyifu na wenye kubunia. Lakini, kama wasemavyo wanasayansi kuwa, "Kiufafanuzi, uko ulimwengu mmoja tu. Mtu hawezi kutengeneza mwingine kama huo wala kufanya majaribio kwawo", hivyo hatuna haja ya kujishughulisha kuifikiria miungu mingine ya kimawazo tu. Kama huu Ulimwengu ambao ni kitu kilichotengenezwa - hauwezi kuwa zaidi ya mmoja, BASI VIPI MWENYEZI MUNGU MTENGENEZAJI anaweza kuwa zaidi ya MMOJA?

Sasa hebu tuvitazame hivi vitu vinavyoishi. Hapa vile vile tunaona usawa wa usawiri katika mjengo wa mifupa. Inashangaza sana kuona kuwa walahidi wameutumia usawa huu katika kuthibitisha kuwa hakuna Mungu.. Wanasema kuwa, "Kwa sababu viumbe vyote vyenye uhai vinaendelea kimabadiliko

MUNGU WA UISLAMU

59

kwa mpango, na kwa sababu, kwa mfano, mifupa ya Gibbons, Orang na Chimpanzee, Gorilla na Mwanadamu inafanana sana kimaumbile, inathibitisha kuwa hawakuumbwa na Muumba yeyote yule".

Kama hakukuwepo mpango maalum hapa Ulimwenguni, wala katika maumbile ya viumbe vyenye uhai na wao wakaitumia hali hiyo katika kupinga kuwepo kwa Muumba ingelileta maana akilini mwa mtu. Lakini inashangaza sana kuona kuwa wanautumia huu mpango maalum uliopo wa viumbe katika kupinga kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa yote na Mwenyezi. Kila mtu anaweza kuuona upuuzi wa hoja hii. Maana ukamilifu wa huu ulimwengu ni hoja isiyopingika kuwa huu Ulimwengu haukutengenezwa na asili pofu na isiyo na akili.

Kwa kweli, watu hawa wanaitumia hoja iliyo kinyume kabisa na dai lao hilo.

Watu wenye mawazo ya Bwana Darwin wanaweza kuutumia huu mfano wa maumbile dhidi ya wale wanaoamini kuwepo kwa Mwenyezi Mungu. Wanaweza vilevile kuutumia dhidi ya wale wasemao, kwa mfano kuwa, ng'ombe aliumbwa na muumba mwenye asili njema na nyoka aliumbwa na Mungu mwingine mwenye asili mbaya. Lakini vipi basi wataweza kuitumia dhidi ya Mwenyezi Mungu Muumba aliye Mmoja tu, Aliyeumba kila kitu kufuatana na mpango wake wenye utaratibu maalum?

Ni wazi kuwa Bwana Darwin alishindwa kuufikia mwisho wa mazungumzo yake. Hakuweza kuuona Ukweli wa Milele, ambao ushahidi wa hayo

BILAL ALLAMAH RIZVI

60

mazungumzo yake uliushabahia . Ushahidi uliokusanywa unapiga kelele kwa sauti kuu kuwa, viumbe vyote vyenye uhai na visivyo na uhai vimeumbwa na MWENYEZI MUNGU MMOJA TU, aliye mjuzi na Mwenyezi.

SURA YA 17

SABABU SABA ZIONESHAZO KUWA MWANASAYANSI ANAMWAMINI MUNGU

(Makala hii ya Bwana A. Cressv Morrison, Rais wa zamani wa "New York Academy of Science, iliyotokea mara ya kwanza katika gazeti liitwalo, Reader's Digest" katika mwezi wa Januari 1948; kisha kwa mapendekezo ya Professor G.A. Coulson, F.R.S; Profesa wa Hesabu wa Chuo Kikuu cha Oxford nchini Uingereza, ilichapishwa tena katika gazeti hilo la "Reader's Digest" la Novemba 1960 - Makala hii inaonesha jinsi sayansi iwalazimishavyo wanasayansi kuukubali ulazima wa kuwepo Muumba aliye Mkuu kabisa).

Bado tungali mwanzoni kabisa mwa karne ya sayansi na kila mwanga uongezekapo, unazidi kutupa nuru zaidi kuhusu huu usanii wa Muumba mwenye Hekima. katika muda wa miaka 90 baada ya Bwana Darwin tumepata ugunduzi mkubwa sana. Kwa moyo wa kisayansi na imani iliyojengwa katika msingi wa ujuzi tuupatao, huwa tunasogea karibu zaidi na kumtambua Mwenyezi Mungu.

Mimi binafsi, ninazihesabu sababu saba za kisayansi zinazoiunga mkono imani yangu:-

MUNGU WA UISLAMU

61

Ya Kwanza: Kwa sheria ya kihesabu isiyo na shaka yoyote, tunaweza kuthibitisha kuwa, ulimwengu wetu umetengenezwa na unatawaliwa na Mhandisi mwenye Hekima.

Kwa mfano hebu tia sarafu kumi zilizo na nambari moja hadi kumi, katika mfuko na kuzitikisa tikisa kabisa. Sasa hebu jaribu kuzichukua kwa taratibu kuanzia nambari moja hadi kumi, huku kila mara ukiirudisha ile sarafu na kuzitikisa zote kwa pamoja tena. Kihesabu tunafahamu kuwa nafasi yako ya kwanza kuchomoa nambari moja ni mara moja katika mara 10 ufanyazo hivyo. Na katika kuchomoa moja na mbili kwa utaratibu ni mara moja katika kila mara mia ujaribuzo kufanya hivyo. Na kuchomoa nambari moja, mbili na tatu kwa utaratibu, uwezekano wake ni mara moja katika mara elfu moja utakazojaribu na kuendelea. Uwezekano wako wa kuchomoa kwa utaratibu tangu nambari moja hadi kumi, utafikia nambari isiyoaminika ya mara moja katika mara millioni elfu kumi (10,000,000,000).

Kwa sababu hiyo hiyo hali nyingi sana zahitajika kuwepo hapa duniani ili kutoa maisha. Hali hizi haziwezi kuwa katika hali hii ya uhusiano mwema kwa bahati tu. Dunia inajizungusha katika mhimili wake, kwa mwendo wa maili elfu moja kwa saa. Kama itazunguka katika mwendo wa maili 100 kwa saa, siku zetu na mausiku yetu yangelikuwa na urefu wa mara kumi kuliko ilivyo hivi sasa, na joto la jua lingelichoma mimea yetu yote katika huo mchana mrefu na katika huo usiku mrefu kila kitu chenye uhai kingelikufa kwa baridi.

BILAL ALLAMAH RIZVI

62

Tena, hilo jua ambalo ndilo chanzo cha maisha, lina joto la usoni pake la nyuzi 12,000 za Fahrenheit, na dunia yetu iko mbali kiasi cha kutosha kuwa hili joto kali sana hutupa joto la kutosha tu wala si jingi sana. Kama jua likitupa nusu tu ya joto litupalo hivi sasa, tutakufa kwa baridi, na kama likitupa nusu zaidi ya hili la sasa,tutaungua na kufa.

Ule mwinamo wa dunia wa nyuzi 23 kuelekea kwenye jua hutupa majira yetu; kama isingeliinama hivyo, mvuke kutoka baharini ungelielekea kaskazini na kusini na kujenga mabara ya barafu. Kama mwezi wetu ungelikuwa, kwa mfano maili hamsini elfu badala ya umbali wake wa hivi sasa, mawimbi ya bahari zetu yangekuwa mengi sana kiasi ambacho mabara yetu yangelizama majini mara mbili kila siku, na baada ya muda kidogo, hata milima yetu ingelimegeka.

Kama tabaka la mwamba na ardhi lingelikuwa na unene wa futi kumi tu zaidi ya hivi ulivyo sasa, kusingelikuwemo hewa ya oksijeni, ambayo bila ya kuwepo kwake, wanyama wangelikufa.

Kama kina cha bahari kingelikuwa na urefu wa futi chache hivi, zaidi ya hiki cha sasa hewa yote ya Kaboni daioksaidi na oksijeni ingeliyeyuka katika maji na kusingelikuwa na mimea yoyote ile. Au kama tabaka ya hewa yetu lingelikuwa jembamba, baadhi ya vimondo ambavyo vinaungua angani kwa mamilioni kila siku, vengelipiga sehemu zote za uso wa ardhi yete na kusababisha moto kila mahali.

MUNGU WA UISLAMU

63

Kwa sababu hiyo na nyingine nyingi, hakuna hata uwezekano mmoja katika mamilioni, kuwepo maisha katika hii sayari yetu yametokea kwa bahati tu.

Ya Pili: Werevu uliopo katika maisha kuweza kutimiza shabaha yake, unadhihirisha kuwepo kwa Hekima iliyopo kila mahali.

Suala la kuwa uhai ni kitu gani hasa, mwanadamu bado hajaligundua. Uhai hauna uzito wala ukubwa. lakini una nguvu. Mzizi unaokuwa unaweza kuupasua mwamba. Uhai unayateka maji ya ardhi na hewa, na umevimiliki vitu vya asili na kuvilazimisha kuungana na kuunda miungano yao.

Uhai ni msanii, hukipa umbo lake kila kiumbe chenye uhai. Uhai ni msanii unasanii kila jani la mti na kulipa rangi kila ua. Uhai ni mwanamuziki, kila ndege yuaimba nyimbo za mapenzi. Vidudu huitana kwa muziki wa sauti zao nyingi. Uhai ni mkemia, huyapa matunda na viungo mionjo yao, na huyapa harufu nzuri mauaridi na kuyabadili maji na "carbonic acid" kuwa sukari na mti, na katika kufanya hivo huitoa hewa ya oksijeni ambayo wanyama wanaitumia kuivuta miilini mwao na kuweza kuishi.

Tazama tone la "protoplasm", ambalo linapenyesha nuru (angavu) na lililokaa katika hali ya halua (hali ya ute mzito), ambalo lina uwezo wa kusogea na linalokusanya nguvu kutoka juani. Hii seli moja, hili tone lipenyezalo nuru lililokua katika hali ya umande, lina mbegu ya uhai ndani yake, na linao uwezo wa kuugawa uhai huu kwenye kila kitu chenye uhai,

BILAL ALLAMAH RIZVI

64

kikubwa na kidogo. Nguvu za hili tone ni kubwa kuliko nguvu zote za mimea yetu yote, wanyama wetu na watu, maana maisha yote hutokana na tone hili, Maumbile hayakuumba uhai; lengelenge la moto na bahari za maji baridi visingeliweza kupata mahitaji yao.

Basi ni nani aliyeuweka uhai ndani ya hilo "protoplasm?

Ya Tatu: Hekima ya wanyama inaonyesha vizuri sana kuwepo kwa Muumba aliyeweka silika katika viumbe ambavyo kama si kwa kupewa silika, visingelikuwa na msaada wowote ule.

Solomon (namna ya samaki wanaozaliwa katika mito ya Umarikani ya Kaskazini kisha wakaishi baharini na kurudi kuzaa katika mito hiyo walimozaliwa na kufa huko) mdogo baada ya kuanguliwa katika mto fulani, hutumia miaka na miaka baharini, kisha hurudi tena katika mto wake, na kutembea upande ule ule wa tawi la mto huo ambako alizaliwa. Ni kitu gani kinachomrudisha sawa sawa kabisa bila ya kukosea? Kama ukimhamishia kwenye tawi lingine la mto atafahamu mara moja kuwa amepotea, na hivyo atarudi nyuma na kutafuta mto wake hadi aupate.

Na lililo gumu zaidi ni fumbo la mikunga (samaki wafananao na nyoka). Viumbe hivi huhama wakati vikuapo kutoka kila mahali katika mito na mabwawa. Wale mikunga watokao Ulaya husafiri maelfu ya maili katika bahari wote wakielekea kwenye kina kirefu kimoja karibuni na kisiwa cha Bermuda (Kusini Mashariki mwa mji wa Washington Amerika ya Kaskazini). Hapo hutaga mayai na kisha hufa. Wale

MUNGU WA UISLAMU

65

watoto ambao hawana njia yoyote ya kupatia ujuzi ila kuwa tu wako katika mbuga ya maji, pia nao hurudi, si kwenye mwambao walikotokea wazazi wao tu, bali vile vile kwenye mito, maziwa na au mabwawa kiasi ambacho kila fungu la maji huwa na mikunga. Hakuna mkunga wa Kimarikani aliyewahi kuvuliwa katika bahari za ulaya na wala hakuna mkunga wa Ulaya aishiye katika maji ya Amerika. Maumbile yamecheleweshwa kukua kwa mikunga wa Ulaya kwa muda wa mwaka au zaidi katika kufikia uwezo wa kusafiri hiyo safari ndefu. Hii nguvu imuongozayo mkunga kufanya hivyo inatoka wapi?

Duduvule atamkamata panzi, atatengeneza shimo ardhini, kisha atamchoma panzi msumari wake wenye sumu katika sehemu mahsusi ambayo itamfanya asife bali azimie tu na kubakia katika hali ya nyama iliyohifadhiwa. Kisha duduvule atataga mayai yake wakati huo ili watoto wake watakaoanguliwa waweze kumguguna panzi huyo kidogo kidogo bila ya kumuuwa. Kwa hao maduduvule nyama hiyo huwa mwisho. Mama duduvule, huruka na kwenda kufa. Hangojei kumuona mtoto wake. Ni kweli kuwa dudvule ni lazima afanye hivi vyote upesi sana tangu mwanzo, na kila mara huendelea kufanya hivyo hadi mwisho, au sivyo hapatakuwepo duduvule yeyote tena hapa duniani. Fumbo hili haliwezi kueleweka kwa kufikiria tu kuwa maduduvule yanafanya hivyo kwa kujichukulia tabia hizo kutokana na viumbe vingine; ni lazima tabia hizo ziwe zimetiwa katika miili ya maduduvule na Muumba (fulani) ajuaye yote.

BILAL ALLAMAH RIZVI

66

Ya Nne: Mwanadamu anacho kitu kingine zaidi ya silika za wanyama - nacho ni uwezo wa kufikiria.

Hakuna mnyama mwingine aliyeacha kumbukumbu ya kuhesabu mpaka kumi au hata kuelewa tu maana ya kumi. Kama tukizilinganisha silika na sauti moja ya firimbi iliyo nzuri, lakini yenye kikomo maalum, basi akili ya mwanadamu itakuwa na sauti zote za vyombo vyote vya muziki katika taarabu nzima. Hakuna haja ya kuipiga vita hoja hii ya nne. Nazishukuriwe fikara za mwanadamu, ambazo kwazo tunaweza kuufikiria uwezekano wetu wa kuwa hivi tulivyo. Tuko hivi kwa sababu tumepata cheche ya akili ijuayo kila kitu.

Ya Tano: Kupatiwa riziki kwa viumbe vyote vyenye uhai kunadhihirishwa katika hali ya ajabu tuijuayo siku hizi na ambayo Bwana Darwin hakuielewa - vitu kama maajabu ya "genes" (mambo yanayotawala tabia za kurithi kutoka kwa wahenga wa kiumbe). Hizi "genes" ni vitu vidogo sana kiasi cha kutoweza kuelezeka, ambavyo kama vile vyote vinavyohusiana na maisha ya wanadamu wote waliohai hapa Ulimwenguni vikikusanywa, zisingeliweza kuijaza kastabini. Lakini vivyo, hizi "genes" ndogo sana, na washirika wao waitwao "chromosomes (vitu vilivyo kama uzi vikaavyo katika seli na ambavyo ndani yake hukaa tabia za "kigene") wamo katika kila seli iliyo hai na ndiyo ufunguo mashuhuri kwa tabia za watu, wanyama na mimea. Kastabini ndio sehemu ndogo itoshayo kuwekea aina zote tofauti za tabia za watu millioni elfu mbili. Kwa vyovyote vile, ukweli uliopo hauwezi kukatalika. Basi, vipi sasa hizi "genes" zinavyoziweka

MUNGU WA UISLAMU

67

hizi tabia za kawaida za kurithi kutoka kwa wahenga wengi sana na kuhifadhi saikolojia ya kila mmoja wao katika hiyo sehemu ndogo sana kiasi hicho? Hapa hasa ndipo mahali hasa ambapo madabiliko na maendeleo huanza katika seli, kitu ambacho hushikilia na kuhifadhi "genes". Jinsi maelfu machache ya "atom" yanayoonekana kama sehemu ndogo sana ya "gene" yawezavyo kuvitawala vitu vyote hapa duniani ni mfano bora sana wa werevu mkubwa sana na riziki ambazo ni lazima zitoke kwenye ujuzi wa Muumba tu, hakuna njia nyingine tuwezayo kuitumia katika ufumbuzi wa jambo hili.

Ya sita: Kwa utajiri wa maumbile tunalazimika kutambua kuwa ni hekima ijuayo kila kitu tu, ambayo inaweza kutambua kabla na kutayarishwa kwa uangalifu wa kijanja wa namna hii.

Miaka mingi iliyopita namna fulani za miti ya jamii ya mipungate ilipandwa huko Australia kutumika kama wigo. Kwa vile Australia haikuwa na wadudu wowote waishambuliao miti hiyo, mara moja miti hiyo ilianza kukua kwa wingi sana; na miti hiyo iliendelea hadi ikachukua eneo lenye ukubwa wa England (Jimbo la Uingereza) nzima, ikiiwasonga wakazi wa huko, nje ya miji na vijiji, na kuharibu mashamba yao. Ili kupata kinga kutokana na madhara ya miti hii, wataalam wa elimu ya wadudu walifanya kila juhudi na mwishowe walimpata mdudu alaye sana mti huu na ambaye hali chochote kingine ila mti huu tu na ambaye vile vile huzaliana kwa urahisi, na ambaye hana maadui humo nchini Australia. Hivyo mara moja wadudu hao

BILAL ALLAMAH RIZVI

68

waliishinda mimea hiyo na siku hizi wadudu walao mimea hii ya jamii ya mipungate wamepungua, wote ila wamebakia kidogo tu watoshao tu kukiweka kiasi cha miti hiyo katika hali itoshayo siku zote.

Upunguzaji huo na mabaki umefanywa Ulimwenguni pote. Kwa nini wadudu wazaanao upesi sana wasiitawale dunia nzima? Kwa sababu hawana mapafu kama yale waliyonayo wanadamu; wanapumua kupitia mirija fulani waliyonayo. Lakini wadudu wakuapo, mirija yao haikui kufuatana na ukubwa wa mwili wa mdudu mwenyewe. Hivyo hakuwahi kuwepo mdudu mkubwa. Kuwepo kwa kiwango hiki cha kukua kumepunguaza idadi ya wadudu hawa.

Kama huku punguza idadi kwa kimaumbule kusingeliwekwa mwanadamu asingeliweza kuishi hapa duniani. Hebu fikiria kukutana na nyigu aliye mkubwa kama simba.

Ya Saba: Ukweli uliopo kuwa mwanadamu anaweza kulitambua wazo la kuwepo kwa Mwenyezi Mungu wenyewe ni uthibitisho usio na kifani.

Utambuzi wa Mungu unaibuka kutokanan na uwezo wa mwanadamu, ambapo haupatikani katika viumbe vingine - uwezo tuuitao dhana. Kwa nguvu ya uwezo huu, mwanadamu (na ni huyo mwanadamu tu) anayeweza kupata ushahidi wa Ulimwengu usio onekana. Sura ifunguliwayo na nguvu hiyo haina mipaka; Hakika kwa vile mwanadamu yu dhana thabiti, yuna ukweli wa kiroho. Anaweza kutambua kutokana na thibitisho zote za usanii na kutambua shabaha kubwa ambazo kwazo, mbingu ipo hapo ilipo na hivyo

MUNGU WA UISLAMU

69

ilivyo na kuwa Mwenyezi Mungu yu kila mahali na yu kila kitu. Lakini hakuna mahali popote palipo karibu sana kama ilivyo katika mioyo yetu.

Ni kweli kisayansi na kimawazo, kama alivyosema msoma-Viganja kuwa, Mbingu zinautangazia utukufu wa Mwenyezi Mungu na anga linaionyesha Sanaa Yake".

SEHEMU YA PILI

SURA YA 18

MAANA YA MOJA

Sasa mazungumzo yetu yatasimamia kwenye wazo la kuwa "Mwenyezi Mungu ni Mmoja tu". Ngoja tueleze waziwazi, tuna maana gani tusemapo 'MMOJA' katika sentensi hiyo hapo juu.

Neno "MOJA" katika mazungumzo yetu ya kila siku hutupa moja ya maana hizi:-

1)"Mtu" na "Farasi" ni kitu kimoja (kwa sababu wote wawili ni wanyama). Hapa neno "Moja" linaelezea kuwa mtu na farasi wote wamo katika kundi la jamii (genus) ya wanyama.

2) "Bakari" na "Smith"ni kitu kimoja. Hapa "Moja", huonyesha kuwa wote wamo katika jamii (species) moja ya mwanadamu.

3) Ukisema na huku unawaashiria seremala wawili kuwa wao ni kitu kimoja. Hapa neno "Moja" lina maana kuwa wote wawili wanafanya kazi moja, au (adjective) moja inaweza kutumika kwa wote hao wawili.

BILAL ALLAMAH RIZVI

70

4) Bwana Churchill alikuwa msemaji, mwandishi, askari na mtawala. Unaweza kusema kuwa usemaji wake, uandishi wake, uaskari wake na utawala wake vilikuwa kitu "kimoja", kwa sababu vyote viliunganika mwenye mwili wa mtu mmoja.

5)Painti moja ya maziwa na painti moja ya maji ni kitu "Kimoja" kwa sababu vyote vina kiasi hicho hicho.

6) Maziwa ya moto na maji ya moto ni kitu "kimoja" kwa sababu vyote vipo katika hali moja.

7) John na Smith wamesimama. Unaweza kusema kuwa wote ni kitu "kimoja" kwa sababu wote wapo katika hali hiyo hiyo ya kusimama.

8) Bwana Khalid ana wana wawili, Bakari na Umari. Bakari na Umari ni kitu "kimoja" kwa sababu wote wana uhusiano wa aina moja na Khalidi.

9) Mwili wa mwanadamu au kiti ni kitu "kimoja" kwa sababu viungo vyake au sehemu zake zimeungwa pamoja. (Lakini kama sehemu zake zikitenganishwa, hiki kitu "kimoja" kitakuwa mamilioni ya vitu).

10) Mtu au kitu kisicho kifani huitwa mtu au kitu "kimoja" kwa vile, kwa mfano, tunaweza kusema kuwa jua katika jamii yetu ya sayari ni "moja" kwa sababu halina kifani chake katika jamii hii.

LAKINI maana zote hizi za "UMOJA" zinatoa maana ya vitu viwili au vitu vingi, kwa sababu maana za neno "Moja" katika nambari 1 - 9 hapo juu huonyesha kuwa vitu "Viwili" au "Zaidi" ni "kimoja" katika hali fulani fulani. Hivyo mara kwa mara vitu "Viwili" au "zaidi" huitwa kwa maana hizi.

MUNGU WA UISLAMU

71

"Moja ikiwa kama mwanzo wa nambari au kuhesabu hufikiriwa kuwa kuna zaidi ya kitu kimoja.

Kitu kisicho kifani kinaweza kuitwa "kimoja" lakini ni matumizi ya kifumbo ya neno hili "Moja", ambayo hayana uhusiano hata kidogo na ukweli wake, kwa sababu kitu kile kisicho kifani kikiwa kimetengenezwa kwa jauhari, kina mamillioni ya sehemu mbalimbali wala si kimoja tu.

Tunaposema"Mwenyezi Mungu yu Mmoja", hatufikirii yoyote katika maana hizi. Umoja wa Mwenyezi Mungu una maana ya kuwa hana sehemu, hana viungo, haonekani hata kimawazo tu.

SURA YA 19

MWENYEZI MUNGU HAWEZI KUWA ZAIDI YA MMOJA

Mwenyezi Mungu hawezi kuwa zaidi ya mmoja. Kwa nini tuthibitishe hivi kwa nguvu? Zipo sababu nyingi. Zipo sababu mbili zaidi ya zile tulizozitaja hapo mwanzoni.

Uthibitisho wa kwanza: Imekwisha thibitishwa hapo mwanzoni kuwa, Mwenyezi Mungu yu wa Milele. Na pia imethibitishwa kuwa kitu cha milele hakiwezi kuwa muungano wa vitu vyenye asili tofauti au mchanganyiko, au kitu kilichochanganyika na kingine.

Sasa hebu fikiria kuwa zipo kalamu mbili zilizofanana sana. Zipo sawa katika umbo, ukubwa, rangi na kila sifa. Lakini vivyo hivyo zingali mbili, kila

BILAL ALLAMAH RIZVI

72

moja ikiwa na utambulisho wake tofauti na ule wa ile nyingine. Hivyo kila kalamu inasifa za aina mbili. Kwanza ni zile sifa ambazo ile kalamu ya pili pia inazo. Pili ni zile sifa ambazo huitofautisha kalamu moja na ile nyingine. Kwa maneno mengine ni kuwa, kila kalamu katika hiyo seti ni muungano wa machangnyiko wa sifa nyingi za aina hizi mbili.

Hii hutokea kila mara vinapokuwepo pamoja vitu viwili vifananavyo. Kwa hakika ingelitokea hivyo hivyo kama vitu viwili vya milele vingelikuwepo pamoja.

Ina maana kuwa, kama vingelikuwepo vitu viwili vya milele, vingelikuwa muungano wa vitu viwili hivyo. Kila kimoja kingeli kuwa na sifa ambazo mwenziwe nae anazo, yaani ule Umilele, na sifa nyingine ambazo mwenzie hanazo ambazo hukipa kitu hiki umbo la kipekee. Hii itakuwa na maana kuwa, kitu hiki cha milele kitakuwa muungano. Jambo ambalo kila mara tulilithibitisha kuwa haliwezekani kuwepo kuhusu Mungu.

Hivyo basi, Mwenyezi Mungu akiwa yu wa Milele, hawezi kuwa zaidi ya Mmoja.

Uthibitisho wa Pili: Kwa mfano wangelikuwepo miungu miwili, je, ingeliwezekana mmoja wao kupinga maamuzi ya mwenzie? Kama jibu ni "ndiyo" basi yule wa pili atakuwa mnyonge ukimlinganiha na yule wa kwanza, na hivyo basi si mwenye nguvu zote, na hivyo hatakuwa mungu hata kidogo. Kama Jibu ni "hapana" basi wa kwanza atakuwa mnyonge kuliko wa pili na

MUNGU WA UISLAMU

73

hivyo basi, si mwenye nguvu juu ya kila kitu na hatakuwa mungu hata kidogo.

Na kama wote wawili hufikiria na kufanya kazi wote kwa pamoja sawa sawa, basi nini faida ya kufikiria kuwepo kwa miungu wawili? Mungu mmoja atatosha kuuendsha huu Ulimwengu.

SURA YA 20

MAANA YA SHIRK

Shirk maana yake hasa ni "Ushirika". Katika msemo wa Kiislamu neno hili linatumika kwa maana ya imani ya kuwepo "Miungu mingi" NA IMANI YA KUWA "Kila kitu katika hii dunia ni sehemu ya Mungu".

Imani ya kuwepo kwa miungu mingi inapatikana katika aina nyingi sana. Hapa tunatoa maelezo fulani fulani kuhusu jambo hili na mengi yao yamechukuliwa kutoka kitabu cha Kiurdu kiitwacho "Tawheed Aur Adl" (Umoja na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu) kilichoandikwa na Maulana Muhammad Mustafa Jauher wa Karachi (Pakistan):-

"Kuna tofauti fulani fulani kimaoni kuhusu "Umoja wa Mungu". Kwa mfano:-

1) Baadhi ya watu husema kuwa Mwenyezi Mungu si pekee katika Umilele wake; anao washirika wake katika huo Umilele wake. Kwa mfano Wakristo huamini kuwa Yesu Kristo na Roho Mtakatifu ni washirika wa Mungu katika Uungu wake na ni ushahidi kuwa

BILAL ALLAMAH RIZVI

74

wasingeliweza kuitwa washrika katika uungu ila tu kuwa wao nao waliaminiwa kuwa ni wa milele.

Na wale waaminio kuwa roho huhamishwa hamishwa toka mwili huu hadi ule, huamini kuwa jauhari na roho vyote viwili ni vya milele kama Mungu. Kama wakiitupilia mbali hii imani ya umilele wa jauhari na roho, itawabidi vile vile waitupilie mbali ile imani yao ya huku kuhamishwa hamishwa kwa roho.

2) Kutokana na imani tuliyoitaja hapo juu, tunapata imani ya kuwa wako washirika wa Mungu kisifa, kama vile Wakristo waaminivyo kuhusu Yesu kristo. Kwa sababu kama Yesu Kristo hakushiriki katika sifa za uungu, asingeliitwa Mungu.

3) Baadhi ya vikundi vinaamini kuwa wapo washirika wa Mungu katika matendo - yaani wao ni wasaidizi wake au washirika wake katika kuumba na kuutawala Ulimwengu, kama vile wanafalsafa wa Kiyunani walivyoamini kuwepo kwa "wenye hekima kumi" ambao waliumba huu ulimwengu mzima.

4) Baadhi ya watu huamini kuwa Mwenyezi Mungu hana mshirika katika umilele wake, sifa zake na matendo yake, lakini ana washirika katika kuabudiwa. Watu hawa kwa kawaida huitwa "Mushrik" (Washirikina)" katika Qurani.

"Mushrik" hawa walikuwa watu walioabudu masanamu wa Uarbuni na mawazo yao walifuatiwa vile vile na wenye kuabudu masanamu wa Uhindi na sehemu nyinginezo.

MUNGU WA UISLAMU

75

5) Kikundi cha mwisho ni cha wale wafikirio kuwa Mwenyezi Mungu hana mshirika katika umilele wake, sifa zake, matendo yake na katika kuabudiwa kwake, lakini wanaamini kuwa wao wako huru kabisa kutokana na Mwenyezi Mungu kuhusu matendo yao. Imani hii ndiyo imani ya "Qadariyya" katika Uislamu, ambao husema kuwa Mwenyezi Mungu hana nguvu zo zote juu ya matendo ya mwanadamu. Imani hii ina maana kuwa, mwanadamu hamtegemei Mwenyezi Mungu, ila yeye (mwanadamu) ana shiriki katika madaraka ya Mungu yahusuyo matendo yake"

Hivyo zipo aina tano za Shirk:-

1) Shirk katika asili na umilele wa Mungu. 2) Shirk katika sifa za Mwenyezi Mungu 3) Shirk katika matendo ya Mwenyezi Mungu 4) Shirk katika kumuabudu Mwenyezi Mungu 5) Shirk katika madaraka ya Mwenyezi Mungu.

Imani zote hizi zina kanushwa vikali sana na wazi wazi katika Qurani.

BILAL ALLAMAH RIZVI

76

SURA YA 21

MTUKUFU MTUME (S.A.W.A.) ANAZUNGUMZIA KUHUSU

"TAWHID"

Sura ya saba na ya tisa ya kitabu hiki zina majadiliano ya Mtukufu Mtume (s.a.w) na walahidi. Ni sehemu za majadiliano makubwa ambayo wawakilishi 35 wa dini 5 (Wayahudi, Wakristo, Walahidi, Mafarisayo na Washirikina) walimjia Mtume (s.a.w) na kujadiliana naye. Mwishoni mwa majadiliano hayo wote waliukubali ukweli wa Uislamu na wakasilimu.

Ni kwa sababu ya uzuri wa hoja alizozitoa Mtukufu Mtume (s.a.w) ambazo alizitumia kuyaelezea kinaganaga mambo ya kifalsafa ya hali ya juu sana katika lugha rahisi sana, ambayo hata mtu wa kawaida aliweza kuyaelewa. Ni kazi bora sana itokanayo na "Hekima na mafundisho mazuri".

Lakini, hata hivyo wapo watu wadaio kila siku kuwa Mtume (s.a.w) alijifunza kwa Wakristo na Wayahudi. Majadiliano haya yanayakanusha madai yao hayo. Basi watu hao na watoe hoja zingine zisizopingika kutokana na maandishi ya Wayahudi na Wakristo wa karne za mwanzoni mwanzoni kabla ya Uislamu.

Sitatoka nje ya mazungumzo haya kama nikieleza kuwa, hoja hizi rahisi sana bado zingali zinafaa hadi leo, na bado zinafaa sana sawa na vile zilivyokuwa miaka 1,400 iliyopita, Majadiliano haya yanatajwa na Imamu Hasan Askari a.s. (Imamu wa 11 wa Shia Ithnasharia)

MUNGU WA UISLAMU

77

katika Tafsiir yake, na vile vile Allama Tabrasi ameyanakili katika kitabu chake maarufu sana kiitwacho "Al-lhtijaj" Juzuu I; na majadiliano hayo yametafsiriwa (na kutiwa maelezo kidogo) katika lugha ya Kiurdu na Maulana Muhammad Mustafa "Jauher" wa Karachi (Pakistan) na kitabu hicho kimetolewa mara mbili. Vitabu vyote hivi ninavyo katika maktaba yangu.

Mtukufu Mtume(s.a.w) alianza majadiliano yake na Wayahudi kisha alijadiliana na Wakristo, Walahidi, Mafarisayo, na mwishoni alijadiliana na wenye kuabudu masanamu.

Kwa sababu ya mpango wa kitabu hiki, mahojiano yake na walahidi yalitolewa katika sehemu ya kwanza (Sura ya 7 na 11). Sasa tunazitoa zile sehemu nne zilizobaki.

SURA YA 22

UISLAMU NA UYAHUDI

Wayahudi wa Uarabuni katika zama za Mtukufu Mtume (s.a.w) walikuwa walishapoteza imani yao. Wakiwa wanaishi pamoja na wenye kuabudu masanamu na Wakristo, nao walianzisha imani ya Mungu kuwa na Mwana. Kwa vile Uzair (Ezra) aliandika upya Torati baada ya kupotea kwa karne nyingi, Wayahudi walimtukuza sana na wakaanza kudai kuwa Uzair alikuwa mwana wa Mungu.

Mtukufu Mtume (s.a.w) aliwauliza ni sababu gani iwafanyayo wawe na imani hiyo. Walisema kuwa Uzair aliwaandikia upya Wana wa Israeli Torati baada ya

BILAL ALLAMAH RIZVI

78

kupotea, na tendo hili linaonyesha kuwa Uzair alikuwa Mwana wa Mungu.

Mtukufu Mtume akawauliza, kwa nini Uzair alikuwa mwana wa Mungu na Musa hakuwa mwana wa Mungu, ambapo Musa alilera Torati mara ya kwanza kabisa, na kuileta Torati kwa mara ya kwanza ni muhimu kuliko kuiandika upya?

Zaidi ya hapo, Musa alifanya miujiza mingi ambayo Uzair hakuifanya. Hivyo, kama Uzair alikuwa mwana wa Mungu kwa sababu tu kuwa Mungu alimpa heshima ya kuiandika upya Torati basi Musa yu mbele zaidi katika kustahili kuwa mwana wa Mungu.

Pia, nalichukulia jambo hili kuwa, kwa kusema "Mwana wa Mungu" hamna maana ya ule uhusiano udumuo wakati mtoto anapozaliwa kutoka katika tumbo la uzazi la mama yake baada ya wazazi wake kuingiliana kinyumba.

Wayahudi walithibitisha wakisema kuwa, waliposema kuwa Uzair alikuwa mwana wa Mungu, hawakuwa na maana ya mwana wa kuzaa, bali kwa sababu ya heshima yake mbele ya Mwenyezi Mungu. Neno hilo lina maana sawa kabisa na ile ya waalimu wengine wengi wanapowaita wanafunzi wao wawapendao "mwanangu".

Mtukufu Mtume (s.a.w) alisema kuwa alikwisha wajibu hoja hiyo aliposema kuwa kwa cheo hicho Musa alistahili zaidi kuitwa mwana wa Mungu.

MUNGU WA UISLAMU

79

Na kwa vyo vyote vile mfano wa mtu mzima kumuita kijana asiye na uhusiano naye "mwanangu" uhusikavyo, hebu na tuchunguze matumizi haya zaidi.

Bila shaka mmekwishaona kuwa mtu mzima huyo, anapoonyesha heshima kwa mwanachuoni mkuu humuita "ndugu yangu" au "kaka yangu" au "chifu wangu" au hata "baba yangu".

Ukitumia matumizi hayo hayo, unaweza kusema kuwa Musa (aliyekuwa na heshima zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko Uzair) ni lazima aitwe "Ndugu wa Mungu" au "Kaka wa Mungu" au"Chifu wa Mungu"?

Wayahudi hawakuweza kujibu swali hili na baada ya kushauriana sana wakasilimu.

SURA YA 23

UMOJA WA MUNGU NA UTATU

Wakristo waliieleza imani yao waziwazi kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja pamoja na Yesu na kuwa Yesu yu Mwana wa Mungu.

Mtukufu Mtume (s.a.w) aliwauliza nini maana yao wanaposema kuwa Mwenyezi Mungu wa Milele yu mmoja pamoja na mwanawe Yesu?

BILAL ALLAMAH RIZVI

80

Je, mna maana ya kuwa Mwenyezi Mungu wa milele alikuwa kiumbe awajibikiwaye na kifo, kama alivyokuwa Yesu.

Kama mnasema hivyo, hiyo ni muhali kwa kitu cha milele kisicho na mwanzo wala mwisho kuwa kitu cha muda chenye mwanzo na mwisho. Au mna maana ya kuwa Yesu aliyekuwa na mwanzo na mwisho alikuwa wa milele kama Mungu alivyo?

Lakini jambo hili nalo ni muhali kwa sababu vipi kitu kilichoumbwa baada ya kutokuwepo, kitaweza kuwa cha milele?

Au kwa sentensi hii (isemayo kuwa Mungu ni mmoja na Yesu) mna maana kuwa Mungu alimpa heshima Yesu, ambayo hakumpa mtu yeyote yule mwingine?

Kama ni hivyo, basi hamna budi mkubali kuwa Yesu hakuwa wa milele, kwa maana aliumbwa, na kuwa usawa wake katika huko kupata heshima kutoka kwa Mwenyezi Mungu vile vile si wa milele, kwa maana aliipata baada ya kuumbwa kwake. Na katika hali hiyo, Yesu hawezi kuwa mmoja pamoja na Mungu, kwa maana kitu cha milele na cha muda haviwezi kuungana.

Wakristo wakasema kuwa, wakati Mwenyezi Mungu alipoonyesha miujiza mingi sana kwa mkono wa Yesu, Alimfanya mwanawe kwa heshima.

Mtukufu Mtume(s.a.w) aliwajulisha tena zile hoja alizowapa Wayahudi kuhusu Uzair na kuwa kwake mwana wa Mungu, na akazirudia tena hoja hizo.

Kisha baada ya mashauriano zaidi, mmoja wao akasema kuwa maandishi matakatifu yanaeleza kuwa

MUNGU WA UISLAMU

81

Yesu alisema, "Ninakwenda kwa baba yangu" (Hoja hii imesimama katika msingi wa kuwa, Yesu mwenyewe alidai kuwa Mungu alikuwa baba yake, na kwa sababu Mtukufu Mtume (s.a.w) alimkubali Yesu kuwa yu Mtume wa kweli, dai lake haliwezi kuwa na kosa.)."

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema kuwa maneno aliyoyasema Yesu ni, "Ninakwenda kwa baba yangu na baba Yenu". Hii ina maana kuwa watu wote waliokuwepo pale wakimsikiliza walikuwa wana wa Mungu katika maana hiyo hiyo ambayo Yesu alikuwa mwana wa Mungu.

Zaidi ya hapo, maneno haya mliyoyanakili yanalikanusha dai lenu kuwa Yesu alikuwa mwana wa Mungu, kwa sababu ya heshima kubwa sana aliyokuwa nayo mbele ya Mwenyezi Mungu, kwa sababu kufuatana na imani yenu hiyo, hakuna yeyote kati ya wasikilizaji wake aliyekuwa na heshima hiyo na vivyo waliitwa wana wa Mungu.

Baada ya mashauriano fulani fulani walisilimu.

SURA YA 24

UMOJA WA MUNGU NA UFARISAYO

Mafarisayo wanaamini kuwa nuru na giza ni waumba na watawala wa huu ulimwengu. Mtukufu Mtume (s.a.w) aliwauliza sababu za imani yao hiyo.

Wakasema: Tunaona mambo ya aina mbili hapa ulimwenguni mazuri na mabaya. Kila kimoja cha vitu hivi ni kinyume cha kingine, hivyo tunaamini kuwa

BILAL ALLAMAH RIZVI

82

muumba wa mazuri hawezi kuwa muumba wa mabaya na muumba wa mabaya hawezi kuwa muumba wa mazuri. Vitu hivi viwili haviwezi kuwa pamoja.

Je, huoni kuwa theluji haiwezi kutoa joto na moto hauwezi kupoza. Hivyo ndiyo sababu itufanyayo tuamini kuwepo kwa waumba wawili tofauti wa mazuri na wa mabaya na wanawakilishwa na nuru na giza na wote hao ni wa milele.

Mtukufu Mtume(s.a.w) akasema: Hebu niambieni, je hamjaziona rangi mbalimbali hapa ulimwenguni- nyeusi, nyeupe, nyekundu, njano, kijani, samawati? Je, si kweli kuwa hakuna yo yote kati ya rangi hizi inayoweza kuwa pamoja na rangi nyingine mahali pamoja wakati mmoja?

Mafarisayo: Ndio. Haiwezekani kwa rangi mbili zo zote zile kati ya hizi kuwa mahali pamoja kwa wakati mmoja.

Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w) aliwauliza kuwa nuru na giza vikiwa vitu viwili tofauti, vipi basi vilitokia kuungana pamoja katika kuumba na hali viumbe vyao (mazuri na mabaya) vyote vipo katika huu ulimwengu mmoja? Je, hii haina maana kuwa ipo Nguvu kubwa iliyovileta pamoja vitu hivi wiwili tofauti?

Walizifikira sana hoja hizi kwa muda mrefu na mwishowe wakasilimu.

SURA YA 25

UMOJA WA MUNGU NA IBADA YA MASANAMU

MUNGU WA UISLAMU

83

Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w) aliwauliza wenye kuabudu masanamu kwa nini wanaabudu masanamu badala ya kumuabudu Mwenyezi Mungu Mmoja.

Wakasema: Twatafuta kuwa karibu zaidi na Mungu kwa kupitia haya masanamu.

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema. Masanamu haya yanasikia? Je, masanamu haya ni viumbe wamchao Mungu na kumtii? Vipi mnaweza kuutafuta ukaribu na Mungu kwa kupitia kwao?

Wenye kuabudu Masanamu wakasema: Hapana. Hayasikii.

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema. Ukweli ni kuwa, ninyi wenyewe mmeyachonga masanamu haya kwa mikono yenu. Hivyo, kama masanamu haya yangelikuwa na uwezo wa kuabudu, yangeliwajibikiwa kukuabuduni (maana mu muumba wao) wala si kuwa ninyi muyaabudu.

Zaidi ya hapo, Mwenyezi Mungu hakukuruhusuni kuabudu masanamu (basi vipi mtaweza kumkaribia Mwenyezi Mungu kwa kupitia haya masanamu, bila ya amri ya Mwenyezi Mungu)?

Baada ya kuisikia hoja hii, wenye kuabudu masanamu wakagawanyika makundi matatu:-

Kundi moja likasema: Masanamu haya ni mifano ya wale watu ambao Mungu alijidhihirishia. Hivyo tunamuabudu Mungu kwa njia hii ya kuyaabudu masanamu ya hawa watu waliokuwa mdhihiriko wa Mungu.

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema:-

BILAL ALLAMAH RIZVI

84

1) Imani yenu ya kuwa Mwenyezi Mungu alijidhihirisha kwa umbo la mtu fulani ni kosa kabisa kwa sababu mmefanya Muumba kuwa kama kiumbe chake. Je, hamuoni kuwa Mwenyezi Mungu hawezi kujidhihirisha kwa umbo lolote lile mpaka kile kitu kimzunguke Mungu? (Lakini vipi basi kitu cho chote kile kitaweza kumzunguka Mungu?)

2) Pia, vipi itakuwepo tofauti kati ya Mungu na vitu vingine vyenye maumbo ya kuonekana (kama vile rangi, muonjo, harufu, ugumu au ulaini, uzito au wepesi). Sifa zote hizi zapatikana katika vitu vingine, na havina kuwepo kwa kibinafsi. Je, Mungu nae ni kama vitu hivi?

3) Mwisho, unapompa Mwenyezi Mungu sifa (ya kudhihirika) ambayo ni sifa ya kitu cha muda tu, (sifa za kitu kilichoumbwa baada ya kutowepo kwake,) basi kwa nini hamuamini kuwa Mwenyezi Mungu anazo sifa zote za kitu cha Muda? Maana yangu ni kuwa, ni lazima muamini kuwa Mwenyezi Mungu hubadilika na kuoza na kufa kwa sababu mwili wa huo mdhihiriko wake huoza huharibika na kufa. Ni muhali kwa kitu kilichoko ndani ya mwili huo kutobadilika wakati hicho chombo chake kilimo kibadilikapo.

Mawazo yote haya huthibitisha kuwa ni muhali kwa Mwenyezi Mungu kuingia katika kitu cho chote kile.

Na mawazo haya ya kuwa Mwenyezi Mungu huingia ndani ya kitu yawapo kosa, hakubakii msingi wo wote wa imani yenu hiyo kuwa mwenyezi Mungu aliviingia badhi ya viumbe vyake ambavyo haya masanamu ni mifano ya watu wa aina hiyo.

MUNGU WA UISLAMU

85

Kikundi cha pili kilisema kuwa hao masanamu yalikuwa mifano ya watu wa kale waliokuwa wacha Mungu. "Tumechonga masanamu yao na kuyaabudu kwa nia ya kumtukuza Mwenyezi Mungu kwa njia ya kuyaabudu masanamu ya watu hao."

Mtukufu Mtume (s.a.w) akawauliza: Tafadhali hebu niambieni ni aina gani ya ibada mliyomfanyia Mwenyezi Mungu, mnapoyaabudu masanamu haya kwa kuyasujudia, mnapoyaomba, na mnapoweka vichwa vyenu juu yao? Je, hamjui kuwa ni haki ya Mwenyezi Mungu tu kuwa asifikiriwe kuwa yu sawa na Mtumwa Wake? Je, haitakuwa tusi kwa Mfalme kama ukimheshimu katika hali ile ile mumheshimuyo nayo mtumishi wake?

Wenye kuabudu masanamu wakasema ndio ni kweli.

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema: Basi, hamtambui kuwa kwa kuyaabudu masanamu ya viumbe, mnamtukana Muumba?

Kikundi cha mwisho kikasema: "Mwenyezi Mungu alimuumba Adamu na akawaamrisha malaika wamsujudie. Tuna haki kabisa ya kumsujudia Adamu (kwa sababu tu watoto wake). Kwa vile Adamu hayuhai siku hizi,tumechonga sanamu lake na kulisujudia na kutafuta ukaribu na Mwenyezi Mungu kwa ibada hiyo"

Mtukufu Mtume (s.a.w) aliwaambia: "Nakubali kuwa Mwenyezi Mungu aliwaamrisha malaika wamsujudie Adamu. Lakini je, alikuamrisheini kulisujudia sanamu la Adamu? Adamu na sanamu lake ni kitu kimoja. Mna

BILAL ALLAMAH RIZVI

86

uhakika gani kuwa Mwenyezi Mungu hachukizwi na kulisujudia sanamu la Adamu?

Hebu fikiria hivi, kama mtu akikuruhusu kuingia nyumbani mwake siku moja, je, unayo haki ya kuiingia nyumba hiyo kesho yake? Au kuingia nyumba yake nyingine siku hiyo hiyo?

Kama mtu anakupa zawadi ya moja ya nguo zake, au mmoja wa farasi wake, unayo haki ya kuichukua?

Wenye kuabudu masanamu wakasema: Ndio, tutaichukua.

Mtume Mtukufu (s.a.w) akasema kama huichukui ile nguo au yule farasi, utakuwa na haki ya kuchukua tena nguo yake nyingine au farasi wake mwingine bila ya ruhusa yake?

Wenye kuabudu masanamu wakasema: Hapana, kwa sababu katoa ile nguo au yule farasi wa kwanza, lakini sio ile nguo nyingine wala yule farasi mwingine.

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema: Ni nani aliye na haki zaidi kuwa mali yake haiwezi kutumika bila ya ruhusa yake, Mwneyezi Mungu au viumbe vyake?

Wenye kuabudu masanamu wakasema: Mwenyezi Mungu yuna haki zaidi katika kuona kuwa mali yake isitumike pasi na ruhusa yake.

Mtukufu Mtume (s.a.w) akasema: Kwa nini mwaugeuka msingi huu? Lini na wapi Mwenyezi Mungu alikuruhusuni muyaabudu masanamu?

Baada ya watu hawa kufikiria zaidi, wote walisilimu.

MUNGU WA UISLAMU

87

SURA YA 26

TAWHIID YA UISLAMU

Kutokana na majadiliano tuliyoyataja hapo juu, itaonekana jinsi Uiislamu, kwa mara ya kwanza katika historia ya dini, uliielezea "Tawhiid" (Umoja wa Mwenyezi Mungu) katika njia ambayo hakukuwepo kutoelewana tena baadaye.

Wayahudi walimwamini Mungu Mmoja, lakini Mungu wao hakuwa wa ulimwengu mzima, bali ni wa kabila moja tu. Na hata hivyo, walikwisha angukia katika shimo la kumpa za Uzair (Ezra) heshima ya kuwa "Mwana wa Mungu".

Ni matokeo ya mara moja yatokanayo na mafundisho ya Uislamu kuwa Wayahudi waliacha kumwita mtu "Mwana wa Mungu". Wakristo wanajaribu kuyatafsiri tena mafundisho ya Utatu: Wahindu walilazimika kugundua kuwa "Vedas" (Kitabu kitakatifu cha dini ya Kihindu) inafundisha Umoja wa Mungu na kuwa wenye kuabudu masanamu walikosea.

Sura ya Tawhiid ni mojawapo ya Sura fupi sana za Qurani Tukufu. Inadumisha imani sahihi kabisa ya Umoja wa Mungu, ikikataa kila aina ya "Shirk" kwa kusema hivi:-

"Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni mmoja. Mwenyezi Mungu asiyehitaji, ambaye wote wanahitaji Kwake. Hakuzaa wala hakuzaliwa. Wala Hana afananaye naye hata mmoja. (Qurani 112:1-4).

BILAL ALLAMAH RIZVI

88

Sentensi ya kwanza kabisa ya "Kalimah" ya Kiislamu yaani ile sentensi isemayo "Hakuna Mungu ila Allah" humwongoza Mwislamu katika maisha yake, si katika mambo ya dini tu bali vile vile katika tabia, za kijamii. Kifungu cha maneno kisemacho 'Hakuna Mungu" humwonyesha Mwislamu kuwa hakuna cho chote katika Ulimwengu kilicho bora kuliko yeye (mwanadamu). Qurani inaonyesha kuwa "Yeye (Mwenyezi Mungu) ndiye aliyekuumbieni hivi vyote vilivyomo humu duniani. Hivyo mwislamu anajua kuwa hakuna cho chote hapa duniani kipasikacho kuabudiwa. Si jiwe wala si mti, si wanyama wala watu; si Jua wala si Mwezi wala si Nyota viwezavyo kuabudiwa, kwa sababu kila kitu (kilichoko hapa duniani) kimeumbwa na kimeumbwa kwa faida yake (yeye mwanadamu). Hivyo, Mwislamu aikataapo kila aina ya udangayifu na kila wazo la ibada ya viumbe, ibada ya masanamu, na kuabudu watu, huwa tayari kuukubali ukweli ustahilio wa Umoja wa Mwenyezi Mungu. Kuamini kuwa yuko Mungu aliye Mkuu kabisa, hutufanya tuwe na shabaha maalumu katika maisha yetu na huyafanya matendo yetu kuwa na sababu maalum. Kama mwanadamu angeliachwa na fikara za kipotovu kuwa hakuna Mungu kabisa, maisha yake yasingelikuwa na shabaha yo yote ile, na maisha yasiyo na shabaha maalum ni hatari kabisa. Hivyo imeongezwa kuwa, hakuna Mungu "Ila Allah". Sentensi hii ina maana ya kukataa na kukubali pia. Maana zote hizo mbili ni zana za kujengea imani ya kuwa kila mtu yu sawa na mtu mwingine. Inapokuwa hakuna mtu aliye bora kuliko mwingine, hakutakuwa na mtu aliye duni. Hivyo basi, imani ya Umoja wa

MUNGU WA UISLAMU

89

Mwenyezi Mungu hukuza fikara za udugu na usawa na haki, kitu ambacho ni jambo jingine lililo muhimu sana katika Uislamu.

SURA YA 27

SIFA ZA MWENYEZI MUNGU

Sasa ni wakati wa kuielezea kwa kifupi ile imani yetu kuhusu Mwenye Mungu. Katika sura zilizotangulia, karibuni kila jambo lihusulo imani yetu limeelezwa wazi wazi. Bila shaka ilishaeleweka sasa kuwa zipo sifa nyingi sana ambazo ni za MUHIMU kwa Mwenyezi Mungu kuwa nazo, na kuwa zipo nyingine zilizo duni sana ambazo hazistahili cheo chake na ambazo hawezi kuwa nazo.

Hivyo basi, katika imani yetu, hizi sifa za mwenyezi Mungu zimegaiwa mafungu mawili, zile "zimstahilizo" na zile "Zisizomstahili".

SIFAT THUBUTIYYAH

(Sifa zimstahilizo Mwenyezi Mungu).

Zile sifa zimstahilizo Mwenyezi Mungu huitwa "Sifati Thubutiyyah". Sifa hizi ni nyingi lakini nane tu mara kwa mara hutajwa, nazo ni hizi:-

1) QADIIM: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu ni wa Milele yaani hana mwanzo wala mwisho.

2) QAADIR:

BILAL ALLAMAH RIZVI

90

Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye enzi zote, yaani ni mwenye uwezo juu ya kila kitu na kila jambo.

3) AALIM: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. Hakuna kilicho siri kwake.

4) HAI: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu yu hai na atakuwa hai milele.

5) MURIID: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu hufanya kila jambo kwa hiari yake. Hafanyi kitu au jambo lo lote kwa kulazimishwa.

6) MUDRIK: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu Anaona yote, As-Sami (Asikiaye yote), Basiir (Aonaye yote), Haazir (Aliyepo kila mahali). Mwenyezi Mungu huona na husikia kila kitu ingawa hana macho wala masikio.

7) MUTAKALLIM: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Bwana wa Ulimwengu, yaani anaweza kukifanya kitu chochote kiseme kama alivyoufanya mti uzungumze na Hadhrat Musa (a.s) na "Pazia la Nuru" lizungumze na Mtukufu Mtume wetu (s.a.w).

8) SADIQ: Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu yu Mkweli katika kauli na ahadi Zake.

MUNGU WA UISLAMU

91

Ni muhali kuweka kiwango cha sifa zake. Orodha ya sifa tulizozitoa hapo juu si kamili, bali ni wajibu wetu kuujua utukufu wa Mwenyezi Mungu. Sifa hizi za Mwenyezi Mungu si za kujipatia (kama vile mtu ajipatiavyo useremala n.k. kwa kujifunza na kujizoeza) bali ni za asili Yake.

SIFAT SALIBIYAH

(Sifa zisizomstahili Mwenyezi Mungu)

Sifa zisizomstahili Mwenyezi Mungu na ambazo Mwenyezi Mungu hanazo kwa sababu ni duni sana kwa cheo chake, zinaitwa "Sifat Salbiyyah". Sifa hizi ni nyingi, lakini kama "Sifat Thubutiyyah". nane tu hutajwa mara kwa mara, nazo ni:-

1) SHARIIK: Neno "Shariik" maana yake ni mwenzi au mshiriki. Mwenyezi Mungu hana mwenzi au mshiriki katika Uungu wake.

2) MURAKKAB: Neno hili maana yake ni Muungano wa vitu viwili au zaidi, au mchanganyiko wa vitu. Mwenyezi Mungu hakutengenezwa kwa kitu chochote cha umbo la kuonekana. Hawezi kugawanyika hata kimawazo.

3) MAKAAN: Maana yake ni "Mahali". Mwenyezi Mungu hayupo mahali fulani maalum maana hana 'JISM' (Mwili).

4) HULUUL: Maana yake ni "Kuingia". Hakuna kitu chochote kimwingiacho Mwenyezi Mungu wala Haingii katika

BILAL ALLAMAH RIZVI

92

kitu cho chote wala mtu yeyote. Kwa hiyo, imani ya kuwa Mungu anaweza kugeuka kuwa mtu au kitu chochote ni yenye kuchukiza sana mbele ya Mwenyezi Mungu.

5) MAHALI HAWADIS: Maana yake ni kitu chenye kubadilika. Mwenyezi Mungu habadiliki.

6) MAR-I: Maana yake ni kitu chenye kuonekana. Mwenyezi Mungu si mwenye kuonekana. Hajaonekana, haonekani, na hataonekana, kwa sababu hana umbo la kuonekana.

7) IHTIYAJ: Maana yake ni kitu chenye kutegemea kingine au kinachohitaji. Mwenyezi Mungu hana tofauti katika wema wowote. Hivyo si mhitaji wa kitu chochote.

8) SIFAT ZAID: Hii ina maana ya "Sifa zaidi". Sifa za Mwenyezi Mungu hazitengeki na Nafsi Yake. Kwa mfano tunasema kuwa Mwenyezi Mungu ni Alim, lakini haina maana kuwa Ujuzi wake ni tofauti na kuwepo kwake. Ukweli ni kuwa, haujawahi kutokea wakati ambapo Mwenyezi Mungu alipata kuwa na ujuzi kidogo na kisha akajipatia ujuzi zaidi. Ujuzi wake, Rehema Zake, Uadilifu wake, Wema wake wote na sifa Zake zote ni nafsi yake.

Hivyo basi itaonekana kuwa kutegemeana na Uislamu "ALLAH" ni jina la Mwenyezi Mungu kama lionekanavyo kutokana na nuru tuipatayo katika sifa

MUNGU WA UISLAMU

93

zimstahilizo Mwenyezi Mungu na zisizomstahili, ambazo tumezitaja. Kwa maneno mengine, ALLAH ni Muumba wa huu Ulimwengu,. Aishiye Milele, chanzo cha kila ukamilifu na aliyetakasika na kila upungufu.

SURA YA 28

MAJINA YA MWENYEZI MUNGU

Jina sahihi hasa ambalo Waislamu hulitumia kwa Mungu ni "ALLAH." Maana yake neno "ALLAH" ni Yule apasikaye kupendwa" na "Ambaye Kwake kila mmoja hukimbilia". Jina hili, kisarufi, halina kifani. Halina wingi wala muanathi (Uke). Hivyo jina hili hutoa mwanga wa ukweli kuwa, Mwenyezi Mungu ni MMOJA tu; hana mshiriki wala aliyesawa naye. Jina hili haliwezi kutafsiriwa vipasikavyo kwa neno Mungu" kwa maana neno Mungu linaweza kuwa Miungu, na Mungu mke.

Majina mengine mawili yanayotumika mara kwa mara ni 'Rahman' na Rahiim.

'Rahman' linaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu ni mwingi wa Rehma na kuwa Rehma Zake zimeizunguka kila kitu hapa ulimwenguni bila ya kujali ubora wa imani ya kitu hicho. Anatengeneza, anaumba, analisha kila kitu na kila mtu awe Mwislamu au Kafiri.

'Rahiim' linaonyesha kuwa Rehema za Mwenyezi Mungu katika Siku ya Kiama zitawazunguka wale wenye imani ya kweli tu, na kuwa makafiri na wanafiki wataachwa.

Inaonekana wazi kuwa majina yote haya mawili yanaonyesha Rehma za Mwenyezi Mungu zilizotukuka

BILAL ALLAMAH RIZVI

94

kabisa. Rehma zake katika hii dunia, kama zinavyoonyeshwa na neno, "Rahman" ni za kiujumla; na zile za hapo kesho huko Akhera kama zinavyoonyeshwa na neno Rahiim ni maalum.

Itashangaza kuona kuwa neno "Rahman" haliwezi kutumika kwa ye yote yule ila Mwenyezi Mungu tu; ambapo neno "Rahiim" linaweza kutumika kwa wengineo pia.

Ndio maana Imamu alieleza kuwa "Jina Rahman Ni jina lililohifadhiwa ambalo hutoa Rehma isiyohifadhiwa, na "Rahiim" ni jina lisilohifadhiwa ambalo hutoa Rehma Iliyohifadhiwa.

SURA YA 29

AL-ASMAUL-HUSNA (MAJINA MAZURI YA MWENYEZI MUNGU)

Ifuatayo ni orodha ya majina 99 yatumikayo kwa Allah katika Uislamu, pamoja na maana zao.

Na: JINA LA

MUNGU WA UISLAMU

95

MWENYEZI MUNGU MAANA YAKE: 1. Allah Jina maalum kwa Mwenyezi Mungu Mmoja tu. 2. Ar-Rahman Mwingi wa Rehema 3. Ar - Rahiim Mwingi wa Ukarimu 4. Al Malik Mfalme 5. Al Qudduus Mtakatifu 6. As Salaam Salama 7. Al-Mumin Mwenye Kuaminiwa 8. Al-Muhymin Mhifadhi 9. Al-Aziz Mwenye Nguvu 10. Al-Jabbaar Mwenye Nguvu zaidi 11. Al-Mutakabbir Mkubwa kabisa 12. Al-Khaaliq Muumba 13. Al-Baar Muumba (kutokana na bure) 14. Al Musawwir Msawiri 15. Al-Ghafaar Mwenye Kughufiria 16. Al-Qahhaar Mwenyezi, Mwenye kutiisha (viumbe vyote). 17. Al-Wahhab Mpaji 18. Ar-Razzaq Mwenye kutoa 19. Al-Fattah Mwenye kufungua 20. Al- Aliim Mwenye kujua yote 21. Al-Qaabith Mkusanyaji 22. Al- Baasitw Mwenye kupanua 23. Al-Khaafidh Mwenye kudhalilisha 24. Ar-Raafi-i Mwenye kuinua 25. Al Mudhill Mwenye kutiisha

(viumbe vyote). 26. Al-Muizz Mwenye kukweza (cheo) 27. As-Samii Mwenye kusikia yote 28. Al-Basiir Mwenye kuona yote 29. Al Hakam Msuluhishi

BILAL ALLAMAH RIZVI

96

30. Al-Adl Mwadilifu 31. Al-Latwiif Mwenye huruma 32. Al-Khabiir Mwenye kujua yote. 33 Al-Haliim Mwenye Huruma 34. Al-Adhiim Adhimu 35. Al-Ghafuur Mwenye kughufiria 36. Ash-Shakur Mwenye kushukuriwa 37. Al-Aliy Aali 38. Al-Kabiir Mkubwa 39. Al-Hafiidh Mhifadhi 40. Al-Muqiit Mwenye kulisha 41. Al-Hasiib Mhasibu 42. Al-Jaliil Jalali 43. Al-Karim Mkarimu 44. Ar-Raqiib Mlinzi 45. Al-Mujiib Mwenye kujibu (Dua za watu) 46. Al-Waasi-i Mwenye kutajirisha 47. Al-Hakiim Mwenye hekima 48. Al-Waduud Muhibu 49. Al-Majiid Mtukufu 50. Al-Maajid Mheshimiwa 51. Al Baaith Mwenye kufufua 52 Ash-Shahiidi Shahidi 53. Al-Haq Haki 54. Al-Wakiil Mdhamini 55. Al-Qawii Mwenye nguvu 56. Al-Matiin Imara 57. Al-Walii Walii (Liwali) 58. Al-Hamiid Mwenye Kuhimidiwa 59. Al-Muhswii Mhasibu 60. Al-Mubdii Mwenye kuanza Muumba 61. Al-Mujid Mwenye Kurudisha.

MUNGU WA UISLAMU

97

Mwenye kufufua 62. Al-Muhyii Mwenye kuhuisha 63. AL-Mumiit Mwenye kuleta kifo 64. Al-Hai Hai 65. Al-Qayyum Ajitoshelezaye katika kuwepo kwake. 66. Al-Waahid Aliye Mmoja tu 67. Al-Ahad Wa pekee, Asiye kifani 68. Asw-Swamad Mkamilifu; wa Milele 69. Al-Qaadir Mwenye Nguvu juu ya kila kitu. 70. Al-Muqtadir Mwenye Nguvu zote 71. Al-Muqaddim Mwendelezaji 72. Al-Muakkhir Mwenye kurudisha nyuma 73. Al-Al-Awwal Wa Kwanza 74. Al-Aakhir Wa Mwisho 75. Adw-dhwaahir Mwenye kuonekana 76. Al-Baatwin Aliyejificha 77. Al-Walii Walii (Liwali) 78. Al-Muta-aalii Mtukufu zaidi 79. Al-Barr Mkarimu 80. At-Tawwaab Mwenye kusamehe 81. Al-Muntaqim Mwenye kulipiza kisasi 82. Al-Afuw Mwenye kuafu. 83. Ar-Ra-uf Raufu 84. Maalik-ul-Mulk Mfalme na Ufalme

(Ulimwengu) 85. Dhul-Jalaali Mwenye Utukufu na wal Ikram Heshima 86. Al-Muqsitw Mwadilifu 87. Al-Jaami-i Mkusanyaji, Mwenye uwezo

BILAL ALLAMAH RIZVI

98

88. Al-Ghanii Tajiri, Mwenye Kujitosheleza 89. Al-Mughnii Mwenye kutajirisha 90. Al-Maanii Mwenye kukataza 91. Alw-Lwaarr Mwenye kuleta shari 92. An-Naafii Mkarimu 93. Al-Nuur Nuru 94. Al-Haadii Kiongozi 95. Al-Badii-i Mwenye kutengeneza (kwa mfano wa awali) 96. Al-Baaqii Wa Milele 97. Al-Waarith Mrithi 98. Ar-Rashiid Kiongozi 99. Asw-Swabuur Mwenye subira.

SURA YA 30

SIFA ZA ASILI NA ZA MATENDO

Swali: Moja ya majina ya Mwenyezi Mungu ni "Khaliq" yaani Muumba. Kwa vile Mwenyezi Mungu alikuwa Muumba wa tangu na tangu, je, hii haionyeshii kuwa kile kitu kilichoumbwa, yaani Ulimwengu, ni wa tangu na tangu?

Jibu: Mwenyezi Mungu hakuumba tangu na tangu. Kama utajifunza kwa makini utaona kuwa sifa za Mwenyezi Mungu, kama zilivyotajwa katika sura iliyotangulia zinaweza kugawanywa katika mafungu mawili kwa urahisi sana.

Kwanza, zipo sifa zile ambazo hazitengeki na wazo la Uungu. Kwa mfano, tunasema kuwa Mwenyezi Mungu ni Qaadir (Mwenye nguvu juu ya kila kitu) na Hai

MUNGU WA UISLAMU

99

(Aliye Hai). Hizi ni sifa zile ambazo haziwezi kutengwa na Mwenyezi Mungu, kwa maana haujakuwepo muda ambao Mwenyezi Mungu hakuwa Mwenye nguvu juu ya kila kitu, Mwenye kujua yote au kuishi. Alikuwa "Qaadir", "Aalim" na Hai tangu na tangu atabakia kuwa "Qaadir", "Alim" na "Hai" milele.

Sifa kama hizi zinahusu asili ya Mwenyezi Mungu, na hivyo basi zinaitwa "Swifaat-i-Dhat" (Sifa za asili ya Mwenyezi Mungu).

Pili, zipo sifa zielezeazo matendo ya Mwenyezi Mungu. Kwa mfano, tunasema kuwa Mwenyezi Mungu ni "Khaaliq" (Muumba) "Raaziq (Mwenye kuruzuku) n.k. hizi ni sifa zinazoelezea matendo ya Mwenyezi Mungu, na hivyo basi zinaitwa: Swifaat-i-Afaal (Sifa za matendo ya Mwenyezi Mungu).

Matendo haya si ya tangu na tangu na hivyo basi sifa hizi hazikutumika kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, tangu na tangu. Unajua kuwa Mwenyezi Mungu ni "Muriid". Anafanya jambo kufuatana na mipango Yake Mwenyewe, na Mapenzi yake Mwenyewe. Yeye si kama moto ambao unaunguza bila ya shabaha maalum au kupenda kwake yeye. Wala yeye si kama jua ambalo laendelea kutoa nuru na joto bila ya kusudio maalum wala bila ya kupenda kwake lenyewe. Mwenyezi Mungu hufanya kazi kwa mujibu wa mipango yake Mwenyewe. Huumba anapopenda na wala si kabla ya hapo.

Hii haina maana kuwa Mwenyezi Mungu hakuwa na uwezo wa kuumbia. Uwezo wa kuumbia ulikuwepo tangu na tangu; kwa sababu "Ule Uwezo" hautenganiki

BILAL ALLAMAH RIZVI

100

na Asili Yake. Lakini kutokea kwa uwezo ule, na kuutumia, si kwa tangu na tangu. Kifupi ni kuwa Mwenyezi Mungu alikuwa na uwezo wa kuumba.tangu na tangu, lakini hakuanza kuumba tangu na tangu na alipoumba aliitwa "Khaaliq", lakini si kabla ya hapo.

Hali kadhalika, Aliporuzuku Aliitwa "Razaaq" alipoghufiria Aliitwa "Ghaffaar", Alipolipiza kisasi, Aliitwa "Qahhar". Alipohuisha Aliitwa 'Muhyi' Alipofisha Aliitwa "Mumiit".

: MWISHO :