freemason thang
DESCRIPTION
ulimwenguTRANSCRIPT
![Page 1: Freemason Thang](https://reader035.vdocuments.mx/reader035/viewer/2022082201/5695d09d1a28ab9b02932df6/html5/thumbnails/1.jpg)
UTAWALA WA FREEMASONS KATIKA
BIBLIA TAKATIFU
Somo 1 UTAWALA WA FREEMASONS
KATIKA BIBLIA TAKATIFU ALFAJIRI, kuamkia Jumamosi, Desemba
30. mwaka 2006,mtawala wa nchi uliko Mto mkubwa, Frati,Saddam Hussein,
akanyongwa kwa kamba hadi kufa.
Mahali walipomnyonga, panaitwa Camp Justice; walimnyonga kwa makosa ya
ubinadamu,huko Kaskazini mwa Baghdad.
Saddam alinyongwa mbele ya Wairak wachache, na dunia ilishuhudia tukio hilo katika
televisheni; akina Mouwafik al-Rubaie,Mshauri
wa Usalama wa Irak, alikuwepo Camp Justice. Nataka msomaji atambue jambo muhimu na
la msingi sana. Kwamba, Marekani kuivamia
Irak na kumpindua Saddam Hussein mwaka 2003,
wakang‟oa sanamu yake jijini Baghdad, ilikuwa
kutimiza unabii muhimu sana. Sababu zote walizosema juu yake kwamba alikuwa na silaha za kuangamiza,ulikuwa
umbeya mtupu- mengi wanayosema Marekani
dhidi ya viongozi wanaohitilafiana nao ni uongo tu; utaona hapa chini.
Ilikuwa kuashiria kuanguka kwa Dola lenye nguvu huko Mashariki, na kando ya mito
miwili ya Tigris na Euphrates.Lilikuwa jambo
muhimu katika historia ya dunia.
Kunyongwa kwa Saddam mbele ya kamera za
televisheni,ilikuwa kuwaambia magamngwe wachache wasiotii mamlaka za Magharibi,kwamba dawa yao ni
kitanzi,risasi na kifo!
Siku ya mauti yake,Saddam alikabidhi kitabu chake cha Koran alichokumbatia kifuani,
akasali, wakamsomea sababu za kifo chake kwamba aliwaua Washia 148 huko Dujail
mwaka 1982; akakubali kusalimu amri na kufa kistaarabu!
Ndivyo zilivyokoma enzi za Saddam ambazo
wao waliziita, The Dark Period. Gaddafi naye ameuliwa baada ya kusalim amri,akapigwa risasi huku akiomba
msamaha,utadhani aliwakosea hao wauaji peke
yao! Feburuari mwaka jana, ikatangazwa kwamba
Osama bin Laden ameuliwa huko Pakistan,juzi
tukaona kwenye televisheni nyumba aliyoishi ikabomolewa na matingatinga,ili mahujaji
wasifululize kwenda kuhiji mahali hapo! Naam. Juzi tukatazama katika televisheni,ya
kwamba eti mwaka 1988 huko Lockerbie, Scotland, siyo maofisa Usalama wa Libya, akina
Megrahi waliolipua ile ndege ya Marekani ya
Pan American Airways! Nilimwona Al-Megrahi katika kitanda cha mauti
anapougulia maumivu ya Saratani baada ya kuachiwa huru akisema, alifungwa kwa
uonevu tu-Hao ndiyo Marekani Bwana!
![Page 2: Freemason Thang](https://reader035.vdocuments.mx/reader035/viewer/2022082201/5695d09d1a28ab9b02932df6/html5/thumbnails/2.jpg)
Hata Syria watashinda,maana imeandikwa Marekani na washirika wake wataushinda
Ulimwengu,kwa kuwa husaidiwa na Freemasons, Illuminanti na Ibilisi
mwenyewe,Mfalme wa Dunia hii. Dola la Kisovieti(USSR) lilishashindwa kusimama kijeshi kama dola kuu la dunia,
akina Mikail Gorbachev walishajikabidhi
Washington kitambo-Urusi imebaki kwa akina Putin watu
dhaifu. Nataka nikwambie msomaji. Dikteta wa
zamani wa Yugoslavia,Slobodan Milosevic aliondoka
kitini mwa enzi kwa „Nguvu ya Umma‟ mwaka
2000, akamwachia kiti Vojislav Costunica huko Serbia ya sasa.
Marekani na washirika wake walimpeleka Milosevic huko Hague kujibu mashitaka ya
uhalifu wa vita na haki za binadamu. Amini usiamini,ndani ya kampeni kali ya Haki za
Binadamu, Ibilisi anaongoza harakati dunia nzima=haki za mashoga, haki za akina
mama hata kuwachapa makonde akina baba, kampeni
za kunyimana unyumba, n.k Watawala wa nchi za „Mrengo wa Kushoto
waliopinduliwa na Marekani,ni wengi sana akina Noriega huko Amerika Kusini.
Korea Kaskazini,haitashambuliwa tena kijeshi.
Bada ya kifo cha Kim Jong Il, akaingia mtoto,”Chekechea” Kim Jong Un katika siasa za
Ulimwengu, bila shaka Korea itaacha kutengeneza Nyuklia kwa kupewa mafuta na
fedha taslim,na itaachana na kuabudu miungu
yao na kujiunga na „Dini Maalum‟ basi,hakutakuwa na maneno tena.
Tatizo ni Iran. Juma lililopita,tuliona kitisho cha
vita huko Iran ikizidi kuishupalia Israeli na kukomaza shingo yake kukabiliana na Marekani
na Washirika wa Magharibi. Tumejifunza katika makala zilizotangulia
kwamba Marekani na washirika wake na Israeli, Vatican wanaandaa mfumo mpya wa
utawala na ibada(Soma Ufunuo wa Yohana 17:1-17).
Mataifa yenye nguvu duniani, yatakuwa yanabeba mgongoni mwake madhehebu Fulani
ya kidini,ambayo kila mtu analazimika kuyakubali mafundisho yao na falsafa yao
ya kumpinga Mungu muumbaji. Turejee katika unabii wa Ufunuo wa Yohana
13:1-10.Kuna wasomaji wananiuliza Dini itabadilikaje na kuwa mamlaka ya siasa?
Ufalme wa mwisho duniani, baada ya Marekani kuitiisha dunia nzima kwa kushirikiana na
iliyokuwa dola ya Rumi, ni ule unaomkufuru
Mungu. Kumkufuru Mungu ni binadamu kujiita Mungu; ni mamlaka ya ibada,kuabudu dini
Fulani na mtu Fulani anayesema yeye siyo mwakilishi wa MUNGU tu,bali ni Mungu.
Shetani mwenyewe ataipa dini hii mamlaka yake (Ufunuo13:2).Freemasons,Illuminanti
wataipa nguvu Marekani na washirika wake,Ulaya
na Israeli, watampa mfalme wa kidini mamlaka yao
yote na viti vyao vya enzi na uwezo mwingi na
dunia itashangaa kwa mamalaka na uwezo wake.
![Page 3: Freemason Thang](https://reader035.vdocuments.mx/reader035/viewer/2022082201/5695d09d1a28ab9b02932df6/html5/thumbnails/3.jpg)
Katika Unabii wa Biblia,mnyama ni ufalme,mamlaka Fulani na siyo mtu binafsi.
(Danieli 7:17),mnyama huyu anayezungumzwa
na manabii Yohana na Danieli atainuka Ulaya,mahali palipokaliwa na watu wengi tangu
zama za Yohana mwaka 96 AD. Marekani na washirika wake, wakipewa
nguvu na nguvu za giza za Ibilisi, Freemasons,Illuminanti n.k watampa
mamlaka yao mfalme ajaye, baada ya Marekani
kuitiisha dunia na kuondoa demokrasia kwa Sheria – NEW World Order (Ufunuo 13:13).
Ajenda ya hawa wote ni kumpinga Mungu muumbaji wa dunia. Tabia ya ufalme huu
ujao duniani imezungumzwa vizuri kabisa. Ufalme huu wa Ufunuo 13:2 UNASEMWA
kwamba ulikuwa mfano wa CHUI, huyu chui
alikuwa na miguu ya DUBU, kichwa chake kilikuwa cha SIMBA na aliwabeba madikteta 10
ambazo ni mihimili 10 za mataifa ya Ulaya leo,
katika eneo lile la dola ya Rumi ya kale. Turejee katika ndoto ya Mfalme Dikteta Nebuchadnezzar, zama za Nabii Danieli
katika sura ya Pili na Saba ya kitabu cha Danieli.
Kuna historia ya dunia,zamani hata siku hizi. Nabuchadnezzar alioneshwa njozi kwamba
baada yake kungekuja falme nyingine nyingi.
Kwa mhtasari, sura ya saba ya kitabu cha Danieli,tunaambiwa kwamba mnyama SIMBA ni
ufalme wa Babeli(603-538 BC). Ufalme huu wa Babeli (siku hizi Irak)
ulipinduliwa Oktoba 13,mwaka 539 na Cyrus The
Great, unaweza kusema Koreshi. Ufalme wa Pili baada ya
Nebuchadnezzar,ulikuwa UMEDI na UAJEMI
waliunda serikali ya mseto, na wanafananishwa na DUBU aliyejiinua upande mmoja wa
mshirika wa utawala huu wa mseto.Wakawashinda
wafalme watatu ndizo mbavu tatu mdomoni mwa dubu huyu mkali, ulianza kutawala 538 hadi 331 BC.
Ufalme unaofananishwa na CHUI ni Ugiriki ya
sasa iliyoitwa Uyunani. Siku hizi Ugiriki ni dhaifu inayochangiwa fedha na ukanda wa Euro
zone, ili wasifilisike. Ugiriki ilianza kutawala
dunia mwaka 331 wakati wa Alexanda Mkuu, wakaja kupinduliwa na Rumi Oktoba
13,mwaka 168 BC.
Dola ya Rumi inafananishwa na MNYAMA wa ajabu!! Alikula na kuponda kwa mkono wa
chuma, na ulianza kutawala dunia Januari 22 mwaka 168 BC hadi kupinduliwa na
kugawanyika katika falme ndogo 10 za Ulaya leo, na nitazitaja. Ulikuwa mwaka 476 AD.
Dola hii ilitawala kwa karne zaidi ya sita. Soma
pia Danieli 2:41. Baada ya hapa,tumeona akina Napoleon
Bonaparte ,Julius Caesar, Adolf Hitler na wenzao
wakijaribu kuiunganisha Ulaya,na dunia nzima wakashindwa vibaya.Tumeona vita vya
dunia juma lililopita.
Sasa, tutazame tabia za falme hizi nne za Nabii
![Page 4: Freemason Thang](https://reader035.vdocuments.mx/reader035/viewer/2022082201/5695d09d1a28ab9b02932df6/html5/thumbnails/4.jpg)
Danieli ambazo yule Mfalme wa Ufunuo 13:1-10
ana nasaba nazo. Mfalme wa Ufunuo 13 ana fanana na CHUI,
ana tabia ya ufalme wa Ugiriki ama Uyunani. Tunawajua Wagiriki, sifa yao ni
FALSAFA.Wale “Great Thinkers” wametokea Ugiriki.
Socrates, Plato, Aristotle(384-322, BC) hawa wametuachia
maarifa ya sayansi. Masomo kama Biology, Chemistry, Geology, Zoology, Physics,
Psychology, Astronomy n.k yametoka kwao. Kwa hiyo, Mfalme huyu wa Ufunuo 13:1-10 ana
vaa „ngozi‟ tabia za CHUI-Ugiriki, sayansi,usomi,falsafa,ujanja ujanja.
Wagiriki, wanajulikana kwa academy zao na ibada ya masanamu. Eti kulikuwa na miungu 391
iliyoishi katika kilele cha Mlima Olympus. Socrates akaipinga hiyo miungu,akasema
kulikuwa na Mungu mmoja Mbinguni, wakampa sumu ainywe baada ya kukataa kutubu.
Socrates alikufa kwa kuipinga miungu ya mlima
Olympus! Yako mengi Ugiriki, michezo ya Olimpiki hiyo
itakayochezwa London Juni mwaka huu,na mbio
za Marathon. Siku nyingine nitaandika juu ya hili,leo niliache.
Mfalme ajaye atakuwa na mwenendo kama Ugiriki, ataleta maarifa na falsafa na ibada
ya miungu nitakayotaja kitambo. Atakuwa na miguu(mwendo) kama wa
UMEDI na UAJEMI, serikali ya mseto iliyoanzisha
duniani SHERIA.Sheria za kwanza zimetungwa
na Wamedi na Wajemi na hazikubadilika (Danieli 6:15,17)na pia ibada ya sanamu
iliyomtupa Danieli katika tundu la samba wakali
wenye njaa. Mfalme huyu atakuwa na kinywa kama na kinywa kama SIMBA, atanena kama
BABELI, kutengeneza masanamu na kulazimisha kila
mtu kuyasujudia. Masanamu ni kinyume cha Amri ya
Pili ya Mungu. Danieli 3 na 6 KUNA HADITHI ya Ibada
ya masanamu. Mfalme wa Ufunuo 13:1-10 atakuwa na
tabia za Rumi ya kale. Tuujadili kidogo ufalme wa
Rumi. Ibada ya sanamu na miungu iliyorithiwa kutoka
Babeli,Umedi, Misri,Ugiriki n.k. Baadhi ya miungu ya Rumi, Aphrodite ambaye ni
VENUS. Mfumo wa sayari,nyota na mwezi viliabudiwa
na Warumi. Mars ndiye Ares kwa Wagiriki, Artemy ndiye Diana, chimbuko la
kumwabudu Bikra Maria siku hizi. Athena, Saturn,Pluto,Mercury,Uranus,Zeus ndiye
Jupiter kiongozi wa miungu-orodha ni ndefu.
Kila mungu alipewa siku maalum ya ibada. Saturday, ni kwa ajili ya mungu Saturn, Sunday
ni siku ya mungu Jua yaani Sun‟s day! Ibada ya jua ni Mithras, Isis wa
Misri,Demeter wa Ugiriki,orodha ya miungu ni ndefu. Mfalme huyu wa Ufunuo 13:1-10 atapewa
mamlaka na shetani, atapewa kiti chake cha enzi
na uwezo mwingi, soma fungu la pili. Sasa, Urusi
![Page 5: Freemason Thang](https://reader035.vdocuments.mx/reader035/viewer/2022082201/5695d09d1a28ab9b02932df6/html5/thumbnails/5.jpg)
ama Iran watatawala wapi dunia? Tumejifunza kuhusu „donda la
mauti‟kupona Feburuari 10 mwaka 1929 na kwamba
utawala huu uliwahi kutiwa jeraha Feburuari 11 mwaka
1798 wakati wa maasi ya Wafaransa. Dunia nzima itashangaa kuona mfalme ajaye
anasujudiwa kama Mungu kwa lazima na hakuna demokrasia tena na uhuru wa dini- Religious Liberty.
Ufalme wa kidini utaongoza dunia na kutoa amri(sheria kali) wale wasiosujudu sanamu
wauawe ufunuo 13:15,17. Sitafsiri unabii kama nipendavyo,tusome Danieli 7:17 hadi 24.
Mnyama huyu atamkufuru Mungu-kumkufuru
Mungu ni mwnadamu kujiita Mungu Danieli 17:17,18 NI „Pembe Ndogo‟ ya Danieli ambayo ni
mamlaka hii ya ufunuo 13:1-10. Pembe yenye
macho(Intelligence) na mdomo wa kumkufuru Mungu yaani utawala wa dini.
Mataifa ya Ulaya yanayosemwa kuwa ni vichwa
saba yaani falme saba ni Anglo-Saxons (Uingereza),Alemanni(Ujerumani),Visigoths (Hispania),Franks
(Ufaransa),Lombards(Italia),Suevi(Ureno) na
Heruli, Ostrogoths na Vandali, walipinduliwa na utawala wa 538 hadi 1798 AD, YAANI
MIEZI 42, SIKU 1260, Wakati nyakati mbili na nusu
wakati. Usikose toleo lijalo uone AJENDA YA SIRI ya
Ulaya,Marekani kuunda Dola la mseto wa dini na
serikali duniani kwa ufadhili wa Freemasons,Illuminanti na Ibilisi.