matangazo shrine of mary help of christians...
TRANSCRIPT
Wasaidizi wa misa Jumapili 13/01/ 2019
01.15 asubuhi: CMA
3.00 asubuhi: BL. MICHAEL RUA
05.30 asubuhi: GXT
11.30 Jioni: Wahusika
Masomo: 1. Is: 40: 1 –5.9 –11; Zab: 104
2. Ti: 2: 11—14; 3: 4– 7; Injili: Lk:3: 15—16. 21 -
Wasimamizi wa PPC 13/01/ 2019
Peter Kioko
Essau Muruye
Herman Joseph Kimani
Susan Wambui
SHRINE OF MARY HELP OF CHRISTIANS - UPPER HILL
Mandhari: “...akasema, shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto, na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili
mimi nami niende nimsujudie ; ...”
Mungu Baba wa mbinguni, tunasadiki na kukiri kuwa utabaki Mungu uliye
daima mwaminifu na kweli, unayerudisha na kuponya watu wako. Tunapoad-
himisha Jubilei ya miaka ishirini na tano, ya kutabarukiwa kanisa la hija la
Maria msaada wa wakristo, ambalo ni zawadi yako, tunakushukuru na kuku-
sifu wewe.
Ewe Bwana Yesu Kristo, uliyepakwa mafuta na kuteuliwa na Baba kuleta
habari njema kwa maskini, kuwahubiri wafungwa kufunguliwa kwao, vipofu
wapate kuona, waliogandamizwa wawe huru, na kutangaza mwaka wa Bwana
kwa watu wake, uturejeshe katika neema.
Uje Roho Mtakatifu na ukae katika jumuiya yetu, katika mwaka huu wa Jubi-
lei. Tunakuomba uunde ndani yetu familia kwa ajili yako, na kwa ajili ya utu-
kufu wa jina lako. Katika neema, upole na upendo wako, tuopoe kutoka yote
yawezayo kututenganisha na ibada ya kweli.
Ewe Utatu Mtakatifu, kwa maombezi yaWatakatifuYohane Bosko, Maria
Domenika Mazzarello, Dominic Savio na watakatifu wote, katika familia ya
Wasalesiani, na Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili, na aliye mlinzi na
msaada wetu, tunaweka nia yetu kwako (............) Kwa njia ya Kristo Bwana wetu…..
Amina.
Nakala ya Jumapili
EPIFANIA
6 January, 2019
Mwaka C
Sala ya Mwaka wa Jubilee
Unaombwa kuzima simu yako
Chukua nakala moja kwa kila familia.
Ubatizo wa watoto wachanga
1. Chukua na kujaza fomu ya Ubatizo kabla ya mtoto kuingizwa kwenye orodha ya wanaobatizwa. 2. Mafundisho kwa wazazi na wasimamizi wa watoto wachanga wa Ubatizo ni Jumatano tarehe 13 Februari, 2019, kwenye Ukumbi wa mkutano. Saa 11.30 jioni 3. Ritriti kwa watakaobatiziwa watoto itaku-wa Jumamosi tarehe 16, Februari, 2019, saa 3.30 asubuhi. 4. Ubatizo wa watoto utakuwa tarehe 24 Februari, 2019
MATANGAZO
1. Uchaguzi wa Uongozi Parish Pastoral Council (PPC) kwa miaka mitatu ijayo utaanza tarehe 13 Januari 2019, kuanzia na jumuiya. Ratiba ya uchaguzi na mipaka ya Jumuiya ziko kwenye Bul-
letin Insert.
2. Sikukuu ya St. John Bosco huadhimishwa tarehe 31 Januari kila mwaka. Mwaka huu, tutaadhimisha sikukuu tarehe 27 Januari. Hii ni maadhimisho ya siku yetu kama familia kama
parokia.
3. Ritriti ya kila mwezi iongozwayo na Fr. Selvam itakuwa Jumamosi tarehe 12 Januari, 2019, saa
2.30 asubuhi.
4. Usajili wa Mafundisho ya Ubatizo kwa watoto wa zaidi ya miaka mitano unaendelea katika ofisi ya
Shrine.
5. Mafundisho ya Katekesi (Watu wazima na wato-to) na Sunday school yatarejea tarehe 13 Januari,
2019.
6. Shajara zenye masomo ya Biblia ya 2019 zin-zuzwa kwenye Booshop; Kiingereza Ksh, 700,
Swahili, Ksh. 600 /-.
7. Toleo la Kipindi Krisimasi la Shrine Digest mwa-ka huu 2018 linazwa hapo nje ya kanisa na katika
bookshop. Tafadhali jichukulie nakala.
8. Shajara maalum za Mwaka wa Jubilee ya Kani-sa lute za 2019 zinapatikana kwa Ksh 700/-. Jipa-
tie shajara yako kutoka Bookshop.
9. Kwa Wanaume wote, Chama cha Kitume CMA Don Bosco, kinaanzisha Batalion ya 24 ya Man Enough Jumamosi 19 Januari, 2019 saa 1 asubuhi. Jisajili kwenye hema nje ya kanisa baada
ya Misa.
10. “Mothers of Sons” msimu wa 5 itaanza tarehe 12 Januari, 2019 kwenye Conference Hall 1:30 asubuhi hadi 3:30 asubuhi. Jisajili kwa kutuma
ujumbe mfupi kwa 0721469260.
11. Leo ni Epifania ya Bwana. Kanisa ulimwenguni huomba mchango ya kuunga mkono kazi za Baba Mtakatifu za “Pontifical Childhood”. Tunaombwa kutoa mchango wa pili Jumapili, 13 Januari kwa
ajili ya hili.
Salesians of Don Bosco, Upper Hill Road, P.O. Box 62322
00200,City Square, Nrb.Tel: 2714622,
Office No: 0722 331 662, E-mail:
Parish Priest/Shrine Director: 0716 876 680
Website www.donboscochurch.org,
Mpesa Pay bill: 331 662
Shrine of Mary Help of Christians
Je, umejiandikisha katika Parokia yoyote?
Jiandikishe kwenye Parokia mojawapo. Wale wa-
takaojiandikisha kama wanaparokia, wataanza
kupata huduma kama wanaparokia miezi 3 baada
ya kupata kadi.
MISA ZA JUMUIYA 12.30 jioni
Yatatolewa baadaye
SOMO LA KWANZA Isa.60: 1-6
Kwa kuliokoa Taifa la Israeli Mungu alilianga-
za liwe nuru kwa mataifa mengine ambayo
yatakuja na utajiri wao kuhiji Yerusalemu.
Somo katika kitabu cha Nabii Isaya.
Ondoka, ee Yerusalemu, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja na utukufu wa Bwana umekuzukia. Maana, tazama, giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu; Bali Bwana atakuzukia wewe, na utukufu wake utaonekana juu yako. Na mataifa wa-taijilia nuru yako, na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako. Inua macho yako, utaza-me pande zote; wote wanakusanyana; wanakujia wewe; wana wako watakuja kuto-ka Mbali, na binti zako watabebwa nyongani. Ndipo utakapoona na kutiwa nuru, na moyo wako utatetemeka na kukunjuka; kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia, utajiri wa mataifa utakuwasilia. Wingi wa ngamia utakufunika, ngamia vijana wa Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Sheba; wataleta dhahabu na uvumba; na kuzitangaza sifa za
Bwana.
Neno la Bwana.
Wimbo wa Katikati Zab. 72:
(K) Mataifa yote ya ulimwengu watakusujudia Ee Bwana
1. Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako. NaMwana wa mfalme haki yako. Atawaamua watu wako kwa haki, na watu
wako walioonewa kwa hukumu. [K]
SHANGILIO
Aleluya, aleluya! Tuliona nyota yake mashari-
ki, nasi tumekuja kumsujudia. Aleluya.
kwao kwa njia nyingine.
INJILI Mat. 2: 1 – 12
Watu wote tumepata nuru ya Kristo Mkom-
bozi. Mamajusi wanawakilisha watu wa ma-
taifa waliomtambua na kumkiri Kristo.
Somo katika Injili ilivyoandikwa na Mathayo.
Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uya-
hudi zamani za mfalme Herode, tazama,
mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu,
wakisema, Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfal-
me wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyo-
ta yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
Basi mfalme Herode aliposikia hayo, ali-
fadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.
Akakusanya wakuu wa makuhani wote na
waandishi wa watu, akatafuta habari kwao:
Kristo azaliwa wapi? Nao wakamwambia,
Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana
ndivyo ilivyoandikwa na nabii, Nawe Bethle-
hemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kam-
we katika majumbe wa Yuda, kwa kuwa
kwako atatoka mtawala atakayewachunga
watu wangu Israeli. Kisha Herode akawaita
wale mamajusi faraghani, akapata kwao
hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota,
akawapeleka Bethlehemu, akasema, shikeni
njia, mkaulize sana mambo ya mtoto;
2. Siku zake yeye, mtu mwenye haki
atasitawi, na wingi wa amani hata mwezi
utakapokoma na awe na enzi toka bahari hata
bahari, toka mto hata miisho ya dunia. [K]
3. Wafalme wa Tarshishi wa visiwa na walete
kodi, wafalme wa Sheba na Seba na watoe
vipawa. Naam, wafalme wote na wamsujudie;
na mataifa yote wamtumikie. [K]
4. Kwa maana atamwokoa mhitaji aliapo, na
mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi atamhu-
rumia aliye dhaifu na maskini, na nafsi za
wahitaji ataziokoa. [K]
SOMO LA PILI Efe 3: 2-3, 5-6
Ahadi ya kuletewa Mkombozi Yesu Kristo,
haikuwa kwa ajili ya Waisraeli tu, bali ni kwa
ajili ya mataifa yote hata sisi.
Somo katika waraka wa Mtume Paulo kwa
Waefeso.
Ndugu zangu: Ikiwa mmesikia habari ya
uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa
ajili yenu; ya kwamba kwa kufunuliwa nalijul-
ishwa siri hiyo. Siri hiyo hawakujulishwa
wanadamu katika vizazi vingine; kama
walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na
manabii zamani hizi katika Roho: ya kwamba
Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmo-
ja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja
nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu
kwa njia ya Injili.
Neno la Bwana.
na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili
mimi nami niende nimsujudie. Nao
waliposikia maneno ya mfalme, walishika
njia; na tazama, ile nyota waliyoiona
mashariki ikawatangulia, hata ikaenda
ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mto-
to. Nao walipoiona ile nyota, walifurahi fu-
raha kubwa mno. Wakaingia nyumbani,
wakamwona mtoto pamoja na Mariamu ma-
maye, wakaanguka wakamsujudia; nao
walipokwisha kufungua hazina zao,
wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na
manemane. Nao wakiisha kuonywa na Mun-
gu katika ndoto wasimrudie Herode,
wakaenda zao.
Injili ya Bwana