kujenga mfumo imara wa ushirikiano wa ......ii kujenga mfumo imara wa ushirikiano wa masuala ya...

87
KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga na Kutekeleza Shughuli za Lishe Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania

Upload: others

Post on 25-Dec-2019

48 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

i

KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE

KATIKA SEKTA MBALIMBALI

Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga na Kutekeleza Shughuli za Lishe

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania

Page 2: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

ii

KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI:

Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga na Kutekeleza Shughuli za Lishe

Kwa maelezo zaidi wasiliana na: Mkurugenzi Mtendaji

Taasisi ya Chakula na Lishe 22 Barabara ya Barack Obama

S.L.P 977 Dar-Es-Salaam, Tanzania Simu: +255 22 2118137 Faksi: +255 22 2116713

Barua pepe: [email protected] Tovuti: www.tfnc.go.tz

Aprili 2018

Page 3: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

iii

Tahadhari:

Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri katika Kupanga na Kutekeleza Shughuli za Lishe umetayarishwa kwa ushirikiano na msaada kutoka kwa Taasisi ya Bill na Melinda Gates. Maelezo yaliyomo kwenye mwongozo huu yametayarishwa kwa ushirikiano wa wataalamu mbalimbali kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba cha Kilimanjaro, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Chuo Kikuu cha Sanyansi za Afya cha Muhimbili, Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Chuo Kikuu cha cha nchini Marekani, na washiriki wengine kutoka katika halmashauri za wilaya za Mvomero na Siha nchini Tanzania. Maelezo yaliyomo humu hayawakilishi moja kwa moja maoni ya mtu binafsi aliyeshiriki kuandaa mwongozo huu au taasisi yake anayofanyia kazi. Jina la Mwongozo huu: Taasisi ya Chakula na Lishe Tazania. 2018. Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano wa Masuala ya Lishe Katika Sekta Mbalimbali: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga na Kutekeleza Shughuli za Lishe. Dar es Salaam, Tanzania. Kwa maelezo ya ziada wasiliana na:

[email protected]

[email protected]

[email protected]

Luitfrid Peter Nnally Afisa Mtafiti Mwandamizi, Lishe Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dar es Salaam, Tanzania

Mary Vincent Mosha Mhadhiri Taasisi ya Afya ya Jamii Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba cha Kilimanjaro Moshi, Tanzania

Akwilina W. Mwanri Mhadhiri Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro, Tanzania

Page 4: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

iv

YALIYOMO

Maana ya Maneno Mbalimbali Yaliyotumika katika Mwongozo Huu ...................................................................... vi

Shukrani ................................................................................................................................................................ viii

Sehemu ya 1: Utangulizi - Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano Katika Usimamizi wa Shughuli za Lishe Katika Sekta Mbali Mbali ................................................................................................................................................... 1

1.1 Lengo la Mwongozo Huu ......................................................................................................................................... 1

1.2 Maelezo Mafupi Kuhusu Yaliyomo Katika Mwongozo Huu .......................................................................................... 2

1.3 Wanufaika wa Mwongozo Huu ..................................................................................................................................... 4

1.4 Kwa nini Mwongozo Huu Unahitajika ........................................................................................................................... 5

1.5 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda: – Chapisho la 1: Ushirikiano wa Sekta Mbalimbali katika Kuboresha Lishe ............................................................................................................... 9

Sehemu ya 2: Kujenga Uwezo wa Sekta Zinazohusiana na Lishe Katika Ngazi ya Wilaya kwa Kutumia Wakufunzi Washauri ..................................................................................................................................................... 11

2.1 Malengo ya Kutumia Wakufunzi Washauri Ili Kuwajengea Uwezo Watendaji ........................................................... 11

2.2 Muhutasari wa Mbinu ya Kujenga Uwezo Watendaji kwa Kutumia Mkufunzi Mshauri ............................................ 11

2.3 Akina Nani Wananufaika Katika Mbinu Hii? ............................................................................................................... 13

2.4 Umuhimu wa Mbinu Hii .............................................................................................................................................. 14

2.5 Hatua za Mafunzo kwa Kutumia Mbinu ya Mkufunzi Mshauri .................................................................................. 15

2.6 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda – Chapisho la 2: Maafisa Lishe WalioJengewa Uwezo Walitekeleza Mafunzo kwa Vitendo .................................................................................. 25

Sehemu ya 3: Kuimarisha Uratibu Kupitia Uainishaji wa Wadau wa Lishe Wilayani ................................................ 27

3.1 Sababu ya Kuainisha Wadau wa Lishe ........................................................................................................................ 27

3.2 Muhutasari wa Maelezo Kuhusu Uanishaji wa Wadau .............................................................................................. 27

3.3 Wanufaika wa Zoezi la Kuainisha Wadau ................................................................................................................. 28

3.4 Unainishaji Wadau Una Umuhimu Gani ..................................................................................................................... 29

3.5 Hatua za kufuata katika Uainishaji Wadau katika jamii .............................................................................................. 29

3.6 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda – Chapisho la 3: Kuainisha Wadau Katika Jamii Huimarisha Ushirikiano wa Kisekta Katika Utoaji wa Huduma za Lishe ............................................ 38

Sehemu ya 4. Kuimarisha Ushirikiano baina ya Sekta Mbalimbali Kupitia Warsha Shirikishi za Wadau wa Lishe ..... 40

4.1 Madhumuni ya Warsha Shirikishi ............................................................................................................................... 40

4.2 Muhtasari wa Warsha Shirikishi ................................................................................................................................. 40

4.3 Wanufaika wa Warsha Shirikishi ................................................................................................................................. 42

4.4 Msingi wa Warsha Shirikishi ....................................................................................................................................... 42

4.5 Hatua za Kuendesha Warsha Shirikishi ....................................................................................................................... 43

4.6 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda – Chapisho la 4: Warsha Shirikishi Yasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya Kuimarisha Mtandao wa Wadau wa Lishe ...................................................... 52

Page 5: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

v

Viambatanisho ...................................................................................................................................................... 54

Kiambatanisho 1.1 Dhana ya Kuboresha Lishe. ....................................................................................................... 54

Chanzo: The Lancet Series on Maternal and Child Nutrition, 2013 ......................................................................... 54

Kiambatanisho 1.2. Malengo ya Lishe ya Tanzania ambayo yanatarajiwa kufikiwa mwaka 2021. Mpango wa Lishe unaojumuisha sekta mbalimbali wa mwaka 2016-2021. ........................................................................................ 55

Kiambatanisho 2.1. Majukumu ya Afisa Lishe wa Wilaya ........................................................................................ 56

Kiambatanisho 2.2: Mtiririko wa kuwajengea uwezo watendaji katika ngazi ya wilaya ........................................ 57

Kiambatanisho 2.3: Mfano wa namna ya kutathmini hali halisi katika wilaya na kupanga shughuli ..................... 58

Kiambatanisho 2.4: Mfano wa mada na maswali ya kujadili wakati wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri .................................................................................................................................... 59

Kiambatanisho 2.5 Mfano wa fomu ya kurekodi majadiliano wakati wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri .................................................................................................................................... 61

Kiambatanisho 2.6 Mwongozo wa kuandika malengo MAKINI ............................................................................... 63

Kimbatanisho 3.1 Dodoso la kuainisha wadau wa lishe katika jamii ....................................................................... 65

Kiambatanisho 3.2 : Mfano wa kanzidata ya kutambua wadau iliyoridhiwa kutoka REACH .................................. 72

Kiambatanisho 3.3: Mfano wa Jedwali la Utambuzi wa Wadau ambalo limeshajazwa .......................................... 73

Kiambatanisho 4.1: Mbinu za kuwezesha Warsha Shirikishji .................................................................................. 74

Kiambatanisho 4.2: Mfano wa Ratiba ya Warsha Shirikishi kutoka Mradi wa Kujenga Mifumo imara ya Lishe Tanzania ................................................................................................................................................................................. 75

Kiambatanisho 4.3: Mapendekezo ya vitabu na machapisho ya rejea kwa ajili taarifa za ziada ............................ 76

Kiambatanisho 4.4. Mfano wa Fomu ya Tathmini ya Warsha Shirikishi .................................................................. 78

Kiambatanisho 4.5 Mfano wa mambo ya kujifunza katika Warsha Shirikishi ya Wadau wa Lishe: Kutoka mradi wa “Kujenga mfumo imara wa usimamizi wa huduma za Lishe” ................................................................................. 79

Page 6: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

vi

Maana ya Maneno Mbalimbali Yaliyotumika katika Mwongozo Huu Mradi wa Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe

Mradi wa Kujenga Mfumo Imara wa Usimamizi wa Masuala ya Lishe ni mradi uliotekelezwa kwa miaka miwili ambao ulilenga katika kuongeza ushirikiswaji wa wadau wa sekta mbali mbali zinazo tekeleza afua za lishe, kuwajengea uwezo watendaji katika ngazi ya wilaya ili kuboresha lishe ya wanawake na watoto wadogo na kusaidia Mpango wa Lishe wa Taifa ili kuonyesha kwa vitendo mbinu za kuwajengea uwezo watumishi, kuainisha wadau na kuendesha warsha ya ushirikishwaji wadau kutoka katika sekta mbali mbali wanaotekeleza afua za lishe. Mbinu hizi zinaweza kutumika katika mikoa au wilaya nyingine za Tanzania ili kuleta msukumo mpya katika upangaji na utekelezaji wa afua za lishe.

Kujenga Uwezo Ni mchakato wa kuendeleza na kuimarisha stadi, hisia, uwezo na raslimali ambazo mtu binafsi au taasisi inazihitaji ili kuendana na mazingira magumu na yanayobadilika kwa haraka. Lengo ni kuimarisha uwezo katika utendaji kazi, kutatua matatizo na kutimiza malengo ya mtu binafsi, taasisi na jamii.

Asasi za Kiraia Ni Vikundi au Taasisi zisizo za kibiashara zinazo fanya kazi katika ngazi ya Jamii kwa faida ya wanajamii bila kutaka kupata faida yeyote ile ya kibiashara. Lengo lake ni kutaka kujenga usawa katika upatikanaji wa huduma zote za msingi katika jamii kama vile huduma za afya, lishe, mazingira, elimu na upatikaji wa tekinolojia za kisasa n.k.

Ushirikiano Kupeana taarifa, kushirikiana katika kazi, kushirikishana raslimali na kuimarishana katika uwezo kwa faida ya pande zote mbili na kutimiza malengo ya pamoja.

Umahiri Ni uelewa, utaalamu au ujuzi unaohitajika ili kuweza kufanikisha utendaji wa kazi au shughuli maalumu.

Kamati ya Lishe ya Wilaya

Kamati hii inajumuisha wajumbe kutoka idara na sekta mbalimbali zinazo husiana na lishe katika Halmashauri. Wajumbe wengine ni kutoka katika asasi zisizo za kiserikali, mashirika ya dini na sekta binafsi.

Warsha ya Ushirikishwaji wadau

Ni warsha ambayo inajumuisha wadau mbali mbali pamoja ili kubadilishana utaalamu na ujuzi wao, kuainisha suluhisho la matatizo au changamoto zilizopo na kutumia ujuzi wa maafisa na utaalamu kutoka sekta na maeneo mengine ya kijiografia.Warsha hii inahamasisha ubadilishanaji wa mawazo, ujuzi na ubunifu ili kutatua matatizo kwa pamoja.

Kujenga Uwezo wa Watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri

Ni mbinu ya kujenga uwezo wa watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri ambayo inahusisha kanuni mbalimbali ikiwemo usawa, jumuishi, yenye mahusiano saidizi ya kujifunza ambapo yule ambaye anauzoefu katika kazi anafungua milango zaidi na kuwapatia uwezo ujuzi na stadi, fursa alizo nazo kwa moyo dhabiti kabisa watu anaowajengea uwezo. Watendaji wanaojengewa uwezo wanaimarishwa kiujuzi na kiuwezona hivyo wanaweza kuboresha utendaji wao hususani katika kuwasiliana na kushirikiana na wadau wengine ili kuweza kutimiza malengo ya kitaalamu waliyo jiwekea. Mkufunzi mshauri anapata uelewa mkubwa wa changamoto

Page 7: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

vii

zinazowakabili maafisa na watendaji anaowajengea uwezo na hivyo anapata fursa ya kuwasaidia katika kuvishinda vikwazo. Kujengewa uwezo kwa kutumia mkufunzi mshauri humwezesha mtendaji kuuliza maswali yenye tija, kujitambua zaidi yeye mwenyewe na kuweza kufanya maamuzi yenye kuleta ufanisi.

Wadau wa Sekta Mbali mbali Wanao Tekeleza Afua za Lishe

Hawa ni watu binafsi na Taasisi zinazo jishughulisha na utekelezaji wa afua za lishe katika ngazi ya jamii. Wadau wanaweza kuwa maafisa wa serikali, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Asasi za Kiraia zinazofanya kazi katika sekta ambazo zinatekeleza afua za lishe, Viongozi wa kijamii, watendaji wanaofanya kazi karibu zaidi na jamii kama vile Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii (WAJA).

Sekta Mbali mbali Zinazo tekelezaji Afua za Lishe

Ili kupata matokeo yanayo staili ya lishe kutokana na afya na maendeleo tunahitaji ushirikiano wa Sekta mbali mbali. Afua za lishe zinazolenga kukabiliana na sababu za moja kwa moja za utapiamlo (hususani ulaji duni na magonjwa) zina umuhimu mkubwa katika kuongeza kasi ya maendeleo. Hata hivyo, Afua za lishe zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo (mfano uhakika wa chakula katika kaya, matunzo ya makundi maalumu, na huduma za jamii ikiwemo afya, maji na usafi wa mazingira) zina umuhimu wake pia. Hivyo ni muhimu kushirikisha sekta nyingine kama vile kilimo, elimu na ustawi wa jamii, ili ziweze kujumuisha afua za na mikakati inayolenga kukabiliana na sababu zilizofichika za utapiamlo. Mbinu ya ushirikishaji wa kweli wa sekta mbali mbali italeta matokeo makubwa na kuwezesha huduma za lishe kuwafikia walengwa wengi kwa haraka, vilevile itasaidia miradi mingine kuweza kufikia malengo yake na hivyo kuonyesha ufanisi wa miradi hiyo.

Afua na Miradi ya Lishe Ambayo Inalenga kukabiliana na Sababu Zilizijificha za Utapiamlo

Ni shughuli, huduma au mikakati inayotekelezwa ili kukabiliana na sababu zilizojificha zinazochangia matatizo ya utapiamlo. Mfano ni masuala yanahusiana na sera, kukuza kipato na hali ya kijamii, uhakika wa chakula, makuzi na malezi ya mtoto, usafi wa mazingira na maji. Shughuli hizi zinalenga kuongeza wigo na ufanisi wa afua ambazo zina lenga kutatua sababu za utapiamlo za moja kwa moja.

Afua na Miradi ya Lishe Ambayo Inalenga kukabiliana na sababu za Moja kwa Moja za utapiamlo

Ni shughuli, huduma au mikakati inayotekelezwa ili kukabiliana na sababu za wazi za utapiamlo. Sababu hizo ni pamoja na ulaji duni na hali mbaya ya afya hususani magonjwa. Afua hizi zinajumuisha pia baadhi shughuli, huduma au mikakati inayotekelezwa ili kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo ikiwemo kuboresha matunzo ya makundi maalumu kama vile kukabiliana na taratibu duni za ulishaji watoto.

Page 8: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

viii

Shukrani Mwongozo huu ni matokeo ya mradi shirikishi unaoitwa “Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano katika Usimamizi wa Shughuli za Lishe: Utafiti Unaolenga Kupanua Wigo wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe” uliojumuisha taasisi mbalimbali za elimu ya juu na serikali ikiwemo Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba cha Kilimanjaro, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba cha Muhimbili, Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela,na Chuo Kikuu cha Cornell kilichopo katika jimbo la New York nchini Marekani. Mradi huu ulitekelezwa kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka 2017. Mwongozo huu unajumuisha mafunzo na uzoefu uliopatikana katika utekelezaji wa mradi kupitia kazi zilizofanywa na wadau wa mradi na washiriki wengine wakati wa mchakato wa kupanga na kutekeleza shughuli za Kuwajengea Uwezo Watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri, kazi ya kuwatambua wadau wanaotekeleza shughuli za lishe katika jamii, mikutano mbalimbali iliyofanyika katika halmashauri za wilaya zilizotekeleza mradi huu, na warsha za kubadilishana uzoefu zilizofanyika. Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa maofisa wa ngazi za Mikoa na Wilaya na wadau wengine walishiriki katika kazi hii kutoka katika wilaya mbili za majaribio, zilizotumika kuibua uzoefu huu na kuuhid=fadhi kama kumbukumbu muhimu. Shukrani mahususi zinatolewa kwa Maofisa Lishe wa Wilaya walioshiriki katika shughuli za kujenga uwezo wa kiutendaji kwa kutumia muda na uzoefu wao. Pia shukrani ziwaendee Wakufunzi Washauri waliosaidia wilaya za mfano kwa kuwapatia watendaji wa wilaya hizo mwongozo na msaada wa kitaalamu, maoni, ushauri na hatimaye kufanikisha uandishi wa Mwongozo huu: Hao ni pamoja na Mary Mosha na Rune Philemon (Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba cha Kilimanjaro); Akwilina Mwanri na Joyce Kinabo (Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine); Anna Kessy na Naomi Saronga (Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba cha Muhimbili); na Haikael Martin and Clara Mollay (Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela). Shukrani nyingi ziende pia kwa Joyceline Kaganda na Luitfrid Nnally (Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania), Sia Msuya and Rachel Manongi (Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba cha Kilimanjaro) kwa msaada wao mkubwa wa kitaalamu. Wengine ni Gina Chapleau, Christina Stark, Katherine Dickin, na Rebecca Stoltzfus (Chuo Kikuu cha Cornell) waliosaidia usanifu na utekelezaji wa mradi pamoja na kuandaa rasimu ya awali ya Mwongozo huu. Wafuatao pia walitoa mchango mzuri katika mapitio na uchambuzi wa kitaalamu wa rasimu ya kwanza ya Mwongozo huu: Walbert Mgeni, Freddy Lwoga, Maria Msangi, Laurent Mselle na Catherine Kimalando (Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania); Gwao O. Gwao (Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto); Happy Nkunda (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni – Mkoa wa Dar-es-salaam), na Janet Mzava (Afisa Lishe wa Mkoa wa Dar-es-Salaam). Tunamshukuru pia Christine Demmelmaier aliyetoa huduma ya uhariri na maoni ya kuboresha rasimu mbalimbali za Mwongozo huu. David Kyungu wa Matatizo Media Productions anastahili shukrani za pekee kwa kuandaa michoro iliyotumika katika Mwongozo huu.

Page 9: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

1

Sehemu ya 1: Utangulizi - Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano Katika Usimamizi wa Shughuli za Lishe Katika Sekta Mbali Mbali

1.1 Lengo la Mwongozo Huu Viashiria mbalimbali huchangia katika kuifanya Afya na hali ya Lishe ya mtu binafsi na jamii kuwa nzuri au mbaya. Usimamizi na utekelezaji wa wa Afua za Lishe kwa pamoja baina ya wadau unaweza kuitwa kuwa ni Ushirikiano baina ya sekta mbali mbali ili kuboresha hali ya lishe. Mwongozo huu unatoa ufumbuzi wa mbinu mbali mbali ambazo zinaweza kutumika katika kuimarisha utendaji wa wataalamu katika ngazi ya Wilaya ili kuboresha ushirikiano wa sekta mbali mbali na hivyo kuboresha hali ya Lishe. Mbinu mojawapo ya kuimarisha utendaji wa maafisa katika ngazi ya wilaya ili waweze kupanga, kuratibu na kutekeleza afua za lishe katika sekta mbali mbali ni kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri. Mbinu hii inahusisha ushirikiano baina ya Mkufunzi Mshauri na afisa anayejengewa uwezo, kusaidiana, kujenga mahusiano wezeshi ya kujifunza miongoni mwao kwa lengo la kuimarisha ufahamu, ujuzi na umahiri wa walengwa wa mafunzo hayo. Mwongozo huu unatoa maelezo jinsi Mkufunzi Mshauri anavyopaswa kuwa na matumizi ya mbinu hii katika kuwajengea uwezo watendaji. Madhumuni ni kuwawezesha watendaji kuimarisha ushirikiano wa kisekta, kupanga na kuingiza maswala ya lishe katika sekta mbali mbali zinazo tekeleza afua za lishe ili kuboresha hali ya lishe na kufikisha huduma kwa walengwa wengi zaidi. Katika siku za karibu kumekuwa na ongezeko la kasi ya ushirikishaji wa sekta mbali mbali katika kuratibu na kuimarisha utekelezaji wa afua mbali mbali za Lishe. Hata hivyo, kuna uhaba wa miongozo inayobainisha mbinu za kuratibu ushirikishwaji wa sekta mbali mbali katika utekelezaji wa afua za Lishe. Mwongozo huu unaainisha ujuzi na stadi wanazohitaji wasimamizi wa huduma za lishe ili waweze kuwajengea uwezo maafisa katika ngazi ya wilaya. Hali kadhalika, mwongozo huu unaainisha mifano, na hatua za kufuatwa katika kuwajengia uwezo watendaji katika ngazi ya wilaya kwa kutumia Mkufunzi Mshauri ili waweze kusimamia kwa ufanisi masuala ya Lishe katika maeneo yao ya kazi.

Mbinu Tatu Zinazo Tumika Katika Kujengea Uwezo Watendaji kwa Kutumia Mkufunzi Mshauri

Mwongozo huu unafafanua mbinu tatu ambazo zinaweza kutumika katika kuimarisha ushirikiano wa wadau kutoka sekta mbali mbali katika masuala ya Lishe na kufikisha huduma kwa walengwa wengi zaidi katika ngazi ya Wilaya nchini Tanzania. 1. Kujenga uwezo wa Watendati katika ngazi ya Wilaya kwa kutumia Mkufunzi

Mshauri. 2. Ushirikishwaji wa Jamii katika kuwatambua wadau mbalimbali wanatekeleza afua za

Lishe katika ngazi ya Wilaya. 3. Kuendesha Warsha Shirikishi kwa ajili ya kuongeza uelewa na kuimarisha

ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika utekelezaji wa Afua za Lishe.

Page 10: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

2

Mwongozo huu pia umejumuisha vitendea kazi na kuainisha njia mbali mbali zinazo weza kutumiwa na wadau wanaotaka kuongeza wigo wa ushirikishwaji na uwezo wa sekta mbali mbali zinazo husika na utekelezaji wa Afua za Lishe (Angalia kiambatanisho 1.1-4.5). Mwishoni mwa kila sura ya mwongozo huu, kuna maelezo mafupi kuhusu ushuhuda wa ufanisi wa mbinu zilizotumika wakati wa majaribio kwenye wilaya mbili za nchini Tanzania. Mradi shirikishi unaoitwa Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano katika Usimamizi wa Shughuli za Lishe: Utafiti Unaolenga Kupanua Wigo wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe, ulitumika kufanya uchambuzi wa jinsi ya kujenga uwezo wa Maafisa Lishe wa Wilaya wanaofanya kazi kwenye sekta ya afya na kuwasaidia kumarisha uhusiano wadau wa sekta nyingine. Mradi huu uliwashirikisha Wanataaluma, Watendaji wa Serikali, na Asasi za Kiraia ili kujifunza njia bora za kufanya kazi kwa pamoja na hivyo kuboresha ufanisi wa ushirikiana baina ya sekta mbalimbali katika utekelezaji wa afua za lishe. Ingawa Mradi huu uliwalenga Maafisa Lishe wa Wilaya, watendaji na wadau wengine katika wilaya na jamii pia walishirikishwa. Njia zilizotumika na mafunzo yaliyopatikana na kuainishwa yanaweza kutumika na watumiaji wengine zaidi ya waliotajwa katika mwongozo huu.

1.2 Maelezo Mafupi Kuhusu Yaliyomo Katika Mwongozo Huu Mpangilio wa Mwongozo Huu Mwongozo huu unafafanua njia tatu ambazoweza kutumika kuwajengea uwezo watendaji katika halmashauri kutokana na malengo yao ili kuimarisha ushirikiano wa sekta mbali mbali zinazotekeleza afua za lishe. Mwongozo huu umeundwa katika sehemu kuu nne, ambazo zimeandikwa kwa kifupi kutokana na shuhuda mbali mbali zinazojumuisha mawazo na fikra za washiriki mbalimbali ambazo zimejumuishwa katika kiambatanisho namba 17.

• Sehemu ya 1 ina maelezo yanayoutambulisha mwongozo huu, sababu za kutengenezwa, walengwa, muuondo wake, na maelezo mafupi ya mbinu ya kushirikisha sekta mbalimbali katika utekelezaji wa afua za Lishe.

• Sehemu ya 2 ina maelezo ya mbinu za kuwajengea uwezo watendaji ambazo zinaweza kutumika kuchochea msukumo mpya na kuleta matokeo makubwa katika sekta mbali mbali zinazotekeleza afua za lishe hususani katika kupanga mipango. Inajumuisha pia umuhimu wa kutumia mbinu hizo na hatua za kufuata wakati wa matumizi ya mbinu hizo. Hatua hizo zinajumuisha jinsi Mkufunzi Mshauri anavyoweza kuwajengea uwezo wadau wa sekta mbali mbali wanaotekeleza afua za lishe ili waweze kufanya tathimini isiyo rasmi ya hali ya lishe katika jamii yao, kujiwekea malengo, na kuainisha shughuli zinazowekwa kutekelezwa ili kufikia malengo waliyojiwekea, kuwatambua wadau wa lishe na jinsi ya kuendesha warsha shirikishi ya wadau wa sekta mbalimbali zinazohusiana na masuala ya lishe.

• Sehemu ya 3 ina maelezo yanayohusu hatua za kuwatambua wadau waliopo katika jamii. Pia inaainisha jinsi maofisa katika wilaya wanavyo weza kufanya zoezi la kuwatambua wadau, kukusanya taarifa zao ikiwa ni pamoja na kuainisha shughuli wanazozifanya na maeneo wanayofanyia kazi hizo, kuainisha changamoto na fursa zilizopo katika kuimarisha ushirikiano wa kisekta, na kujenga mahusiano imara yatakayowezesha kuboresha uhusiano wa wadau.

Page 11: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

3

• Sehemu ya 4 ina maelezo yanayohusu jinsi ya kuendesha warsha shirikishi za wadau. Sehemu hii inawasaidia watendaji katika ngazi ya wilaya kujifunza namna ya kushirikisha wadau waliopo katika jamii ili waweze kufahamu kwa undani maana ya ushirikiano wa kisekta katika masuala ya lishe, kuongeza hamasa, na kushirikiana katika kufikia maamuzi ya pamoja, na kuweka vipaumbele vya lishe na kuainisha hatua za utekelezaji kwa siku zinazofuata.

• Maelezo mafupi ya ushuhuda. Mwishoni mwa kila Sura ya mwongozo huu kuna maelezo mafupi kuhusu jinsi kujengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri, uainishaji wa wadau mbalimbali na uendeshaji wa warsha shirikishi ya wadau vilivyo fanyika katika wilaya mbili za majaribio na namna ambavyo uzoefu uliopatikana unaweza kutumika katika kuimarisha uhusiano miongoni mwa sekta mbali mbali ili kuweza kutatua tatizo la utapiamlo katika jamii.

• Viambatanisho vilivyowekwa vinasaidia kuonesha muundo wa mwongozo huu, vitendea kazi, na machapisho ya nyongeza ambayo yanaweza kuwasaidia wasimamizi ili waweze kuendesha zoezi la kuwajengea uwezo watendaji katika ngazi ya wilaya, kuainisha wadau mbali mbali na kuendesha warsha shirikishi ya wadau wa lishe. Miundo na vitendea kazi vilivyomo vilitengenezwa, kujaribiwa na kuboreshwa wakati wa utekelezaji wa mradi wa Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano katika Usimamizi wa Shughuli za Lishe: Utafiti Unaolenga Kupanua Wigo wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe. Viambatanisho vilivyomo vimejumuisha hatua za kufuatwa wakati wa mchakato wa kujenga uwezo wa watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri, Jinsi ya kuainisha wadau mbali mbali, vitendea kazi hivyo vinavyo tumika vimetoholewa kutoka mradi wa REACH (www.reachpartnership.org), nakala ya fomu ya tathimini ya warsha shirikishi ya wadau na viambatanisho vingine.

Mbinu tatu ambazo zimewasilishwa katika mwongozo huu zinaweza kuboresha utendaji kazi wa mtu binafsi, kuimarisha ushirikiano wa wadau, kuanzisha au kuimarisha mtandao wa wadau na kuwezesha kufikiwa kwa maamuzi ya pamoja baina ya wadau wa lishe. Jambo la muhimu la kuzingatiwa ni kwamba mbinu zilizo ainishwa zinaweza kutumika katika kuboresha mipango na utekelezaji wa afua za lishe miongoni mwa wadau mbali mbali na hatimaye kuboresha hali ya lishe na afya ya familia na Jamii kwa ujumla. Pia zinaweza kutumika kukidhi matakwa ya walengwa mahususi katika mazingira, maeneo na nyakati mbalimbali. Kila Sehemu ya mwongozo huu imegawanyika tena katika vipengele vidogo vidogo vifuatavyo:

• Lengo la mbinu husika • Muhtasari • Wanufaika wakuu • Umuhimu wake • Mwongozo wa hatua za kufuatwa katika matumizi ya mbinu husika • Maelezo mafupi kuhusu ushuhuda kwa vitendo, ambao unaeleza jinsi mbinu husika ilivyotumika

wakati wa utekelezaji wa mradi wa majaribio wa Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano katika Usimamizi wa Shughuli za Lishe: Utafiti Unaolenga Kupanua Wigo wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe 2015/16

Page 12: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

4

1.3 Wanufaika wa Mwongozo Huu Mwongozo huu unaeleza jinsi ya kutumia mbinu ya kujenga uwezo wa watendaji kwa kutumia Wakufunzi Washauri kwa lengo la kuimarisha uwezo wa wadau mbali mbali wanao tekeleza afua za lishe katika ngazi ya wilaya. Hata hivyo, zoezi la kuwajengea uwezo watendaji linaweza kubadilika wakati wowote kulingana na mahitaji na mazingira halisi ya eneo husika. Zoezi la kuwajengea uwezo watendaji linapaswa kuzingatia mahitaji mahususi ya walengwa na pia linazingatia mazingira mapana na mahitaji ya wadau wa lishe katika wilaya husika. Kadiri watendaji wanaojengewa uwezo wanavyo pata uelewa na stadi, wanapata uwezo wa kutumia zoezi hilo katika kutatua changamoto za maeneo na majukumu mapya ya kazi zao. Ifahamike kwamba, hakuna watu wawili wanao lingana kwa kila kitu au wanaoweza kujengewa uwezo kwa kufuata hatua zinazofanana. Watumiaji wanapaswa kutumia maelezo haya kama mwongozo. Hivyo wanapaswa kuwa wabunifu na kujitahidi kurekebisha zoezi la kujengea uwezo watendaji kulingana na mahitaji ya kila mtu na mabadiliko yanayo jitokeza. Watumiaji wa Mwongozo huu wanaweza kuwa wadau wa taasisi na ngazi mbali mbali kama vile Serikali za Mikoa na Wilaya, Sekta mbali mbali na watu wenye majukumu mbali mbali. Hata hivyo, mfumo imara wa wadau kutoka sekta mbali mbali zinazo jihusisha na utekelezaji wa Afua za Lishe, utawasaidia watu waweze kupeleka uelewa na stadi walizo nazo kutoka ngazi ya Mkoa hadi katika ngazi ya Jamii. Watumiaji wengine wakiwemo wadau kutoka katika Asasi za Kiraia zisizo za Kiserikali na Wasimamizi wa

Malengo ya Mwongozo huu Baada ya kuupitia mwongozo huu , tunatarajia watumiaji wataweza kuelewa yafuatayo:

• Dhana ya Kujenga uwezo wa watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri na hatua zake,

• Jinsi mkakati wa kujenga uwezo wa watendaji unavyoweza kuboresha mipango ya lishe inayotekelezwa na sekta mbali mbali na kufikisha huduma kwa walengwa,

• Manufaa na matokeo ya kujengea uwezo watendaji , ikiwa ni mbinu mbadala wa programu za mafunzo zilizo zoeleka hapo awali,

• Umuhimu wa vitendea kazi mbalimbali kwa mfano kitendea kazi kinachoainisha hatua za kuwatambua wadau wa lishe na hatua za kuendeshaji warsha shirikishi ya wadau ili kuimarisha ushirikiano wa sekta mbali mbali zinazo jihusisha na utekelezaji wa sfua za lishe,

• Hatua za kufuata katika mchakato wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri, uainishaji wa wadau mbali mbali na uendeshaji wa warsha shirikishi ya wadau wa lishe,

• Jinsi ya kutumia vitendea kazi wakati wa utekelezaji wa hatua zilizoainishwa katika Mwongozo huu na,

• Mambo muhimu ya kuzingatia katika utekelezaji wa mbinu hizi kama zilivyo ainishwa katika wilaya mbili za Majaribio.

Page 13: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

5

Watoa huduma za Afya Katika Ngazi ya Jamii wanaweza kufaidika na matumizi ya mbinu mbali mbali zilizopendekezwa katika Mwongozo huu. Watumiaji wa Mwongozo huu wanaweza kuwa na Stadi katika Usimamizi na Ujuzi katika kuratibu afua na huduma mbalimbali za Lishe, wanaohitaji kujiongeza ujuzi na kupanua upeo wa majukumu yao.Wengine wanaweza kuwa ni wageni kabisa katika utekelezaji wa huduma za lishe au ambao ni mara yao ya kwanza kutumia mbinu zilizoainishwa katika Mwongozo huu lakini wanahitaji kujifunza zaidi. Watendaji wanaojengewa uwezo wanaweza kutumia mwongozo huu kama zana ya kujifunzia na kutekeleza vizuri zaidi majukumu yao, pia wao wenyewe, wanaweza wakatumia Mwongozo huu na hatimaye kuwa Wakufunzi Washauri.

1.4 Kwa nini Mwongozo Huu Unahitajika

1.4.1 Changamoto za Afya na Lishe

Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye utulivu na mafanikio katika nchi za Afrika. Ukuaji wa uchumi umeifanya Tanzania kuendeleza uwekezaji katika taasisi na miundo mbinu. Serikali ya Tanzania imekuwa ikipata mafanikio katika kusimamia na kuboresha afya na lishe ya Jamii. Pamoja na mafanikio hayo bado Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi. Watu wengi Tanzania wanaishi vijijini na wanategemea kilimo cha kujikimu. Takribani nusu ya kaya zilizo vijijini hupata chini ya milo mitatu kwa siku na kati ya hizo asilimia 74 hawapati vyakula ina ya nyama na samaki (Tanzania-DHS-MIS 2015-16). Zaidi ya asilimia 22 ya kaya waliripoti kuwa hawana uhakika wa kupata chakula cha kutosha. Kushindwa kupata mlo ambao unakidhi mahitaji ya virutubishi katika mwili kunasababisha utapiamlo, hivyo kuwafanya watu hasa watoto kuwa katika hatari ya kupata magonjwa yanayoweza kusababisha vifo kama vile kuhara na kichomi, pia kuwa katika hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa mara kwa mara. Utapiamlo ni hali inayojitokeza kwa sababu ya kutokula aina mbalimbali za vyakula na chakula cha kutosha. Utapiamlo wa muda mrefu husababisha uwezo wa motto kujifunza kupungua na anapokuwa mtu mzima tija yake katika kazi hupungua pia.

Kuboresha Lishe ya Watoto Huwawezesha Kufikia Kiwango Bora cha Ukuaji

Watoto wakiwa na kimo kifupi ukilinganisha na umri wao (wakidumaa), hupata athari za kudumu zisizoweza kurekebishwa katika maisha yao yote. Nchini Tanzania, kuna watoto wapatao milioni 2.7 walio na umri chini ya miaka mitano ambao wamedumaa. Watoto hao wamekosa virutubishi muhimu tangu wakati mama zao walipokuwa wajawazito, na hali ya kukosa virutubishi muhimu iliendelea katika miaka miwili ya mwanzo wa maisha yao. Kwa sababu walikosa fursa katika umri huu muhimu, watoto hawa wanaweza kuwa na afya mbaya na uwezo mdogo kiakili ikilinganishwa na wenzao walio katika umri huo. Udumavu unaweza kuathiri uwezo wa kujifunza, tija katika kazi za uzalishaji na wa kipato wakati wa utu uzima.

Page 14: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

6

Madhara ya utapiamlo yana jitokeza katika mzunguko hatarishi. Utapiamlo huathiri afya ya mtu binafsi na kuongeza kasi ya magonjwa, kudhohofisha nguvu kazi ya taifa na hatimaye kuathiri uchumi. Utatuzi wa tatizo la utapiamlo ni mgumu kwani tatizo hili linatokana na sababu chache zilizo wazi na nyingine nyingi zilizofichika. Kutokana na ukweli huu utapiamlo bado ni tishio kubwa kwa nguvu kazi ya taifa.

Kutokuwa na chakula cha kutosha au aina sahihi ya chakula kunaweza kusababishwa na sababu mbalimbali zikiwemo hali ngumu ya uchumi, magonjwa ya mimea, tatizo la masoko ya uhakika na sababu nyingine nyingi. Familia nyingi nchini Tanzania ni za wakulima wadodo wadogo kilimo chao ni cha kujikimu, hivyo wanakuwa katika hatari ya ukosefu wa chakula wanapokosa mavuno ya kutosha. Familia inapotegemea kupata kipato kutokana na kuuza mazao inaweza kuamua kutumia ardhi na muda wote kuzalisha mazao ya biashara badala ya kulima mazao ya chakula yenye virutubishi kwa wingi. Hali hii inaweza ikasababisha utapiamlo sugu katika familia hiyo. Jjedwali lifuatalo linatoa muhtasari wa hali ya lishe ya wanawake na watoto nchini Tanzania.

Lishe Duni Huathiri Tija katika Taifa

Chanzo: Imetoholewa Kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO

Takwimu za Hali ya Lishe Nchini Tanzania

41 % ya Watoto wachanga chini ya miezi 6 hawakunyonyeshwa maziwa ya mama pekee

60 % ya Watoto (miezi 6 - 23) hawapati kiasi cha kutosha cha chakula.

70 % ya Watoto (miezi 6 - 23) hawapati chakula chenye mchanganyiko wa kutosha.

90 % ya Watoto (miezi 6 - 23) ulishaji wao ni duni kulingana na viwango vya ulishaji watoto.

34 % ya watoto wa umri chini ya miaka 5 wamedumaa.

45 % ya Wanawake wa umri kati ya miaka 15 mpaka 49 wana upungufu wa damu.

Chanzo: 2015-16 TDHS-MIS Key Findings. Rockville, Maryland, USA:MoHCDGEC, MoH, NBS, OCGS, and ICF

Maendeleo hafifu kimwili na kiakili

Kupungua kwa tija

Umasikini

Magonjwa, kukosekana kwa

uhakika wa chakula katika kaya

Utapiamlo

Page 15: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

7

1.4.2 Mahitaji ya Mbinu Madhubuti za Kukabiliana na Utapiamlo Ili kuvunja mzunguko hatarishi wa utapiamlo, tunahitaji kutumia mbinu madhubuti za kukabiliana na sababu za wazi na zilizojificha za utapiamlo (Kiambatanisho 1.1). Ingawa utapiamlo unasababishwa moja kwa moja na ulaji duni usiokidhi mahitaji ya virutubishi mwilini na magonjwa, utatuzi wa tatizo hilo hauwezi kupatikana kwa kutekeleza afua za zinazolenga sekta ya afya peke yake. Kuna ushahidi unao onesha kuwa utekelezaji wa afua zinazolenga kuongeza ulaji wa virutubishi pekee unaweza kupunguza udumavu kwa asilimia 20 tu (Bhutta ZA, na wenzake, Lancet 2013). Kwa kuwa utapiamlo unatokana na sababu mtambuka, afua za sekta ya afya zinazolenga kuboresha lishe ya jamii kwa kuimarisha na kulinda afya zinapaswa kutekelezwa kwa pamoja na afua za sekta nyingine. Pia ni muhimu kushirikisha wadau wengine katika hatua zote za kukabiliana na tatizo la utapiamlo. Mfumo wa utoaji wa huduma za lishe unaojumuisha wadau kutoka sekta mbali mbali unapaswa kujumuisha afua zinazo lenga kukabiliana na sababu za moja kwa moja za utapiamlo na sababu zilizojificha za tatizo hilo. Mfano wa afua zinazo lenga kukabiliana na sababu za moja kwa moja za utapiamlo ni pamoja na kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa watoto wachanga katika miezi 6 ya mwanzo wa maisha yao. Mfano wa afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizofichika za utapiamlo ni pamoja na mpango wa kusaidia kaya masikini ambao unaweza kuimarisha umiliki wa raslimali kwa wanawake, kuongeza uwezo wao katika kufuata ushauri wa lishe bora wanaopewa.

Sekta Zinazohusika Katika Kutatua Sababu Zilizofichika za Utapiamlo Zinaweza Kuchangia Kupunguza Utapiamlo kwa Kiasi kikubwa Endapo Zitatekeleza Afua za Lishe

Sekta hizo zinaweza :

1. Kuweka malengo ya kuboresha hali ya lishe. 2. Kujumuisha masuala yanayo husu afya moja kwa moja (kwa mfano kupambana

na udumavu) katika sera, vipaumbele na shughuli wanazotekeleza 3. Kubuni miradi inayojenga uwezo wa wanawake kufanya maamuzi binafsi na

kujitegemea. 4. Kuboresha miradi ya lishe ili kuwafikia walengwa sahihi wanaokusudiwa,

kuitekeleza katika wakati sahihi, na muda wa kutosha ili kuwanufaisha wanawake wajawazito na watoto walio na umri chini ya miaka 2.

5. Kutumia fursa zilizopo ili kuongeza kasi ya utoaji wa huduma za lishe. Kwa mfano huduma ya uwezeshaji wa kaya masikini kwa kuzipatia pesa inaweza kujumuisha huduma ya ushauri nasaha na elimu ya lishe ili fedha zinazo tolewa zitumike kwa usahihi.

Kuna msukumo na mwitikio mkubwa katika utoaji wa huduma za lishe unaojumuisha wadau kutoka sekta mbali mbali. Serikali ya Tanzania imeandaa Mpango Mkakati wa Lishe Unao Jumuisha Wadau Kutoka Sekta Mbali mbali ambao utatekelezwa kati ya mwaka 2016 hadi 2021. Mpango huu unatoa

Page 16: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

8

mwongozo unaolenga kuimarisha afua za lishe ili kukabiliana na sababu za moja kwa moja na zilizofichika za utapiamlo katika jamii. Ili Tanzania iweze kufikia Malengo ya Lishe na Maendeleo ya Binadamu (Kiambatanisho 1.2), inapaswa kuongeza na kuimarisha uwezo wa watendaji wanaohusika katika sekta zote zinazo husiana na masuala ya lishe. Hata hivyo kuna changamoto nyingi katika kutatua tatizo la utapiamlo. Kwa sababu hiyo sekta zote zinapaswa kufanya kazi kwa pamoja na kushirikiana bila kuchelewa. Suala hili linahitaji uongozi imara wenye uwezo wa kuunganisha wadau kutoka sekta mbali mbali. Jedwali lifuatalo lina orodha ya wadau muhimu wanaoweza kushirikiana katika utekelezaji wa afua za lishe.

Ingawa mkakati wa lishe madhubuti katika ngazi ya taifa unaweza kuleta matokeo mazuri, bado utekelezaji wa afua za lishe unakabiliwa na changamoto kubwa ya kujenga umoja na ushirikiano baina ya wadau katika ngazi mbalimbali. Kuna uhitaji mkubwa wa kuongeza uelewa wa wadau kuhusu tatizo la utapiamlo. Kwa mfano, wadau wanapaswa kufahamu kuwa utapiamlo ni tatizo linalohusu sekta mbali mbali, kuboresha mawasiliano baina ya sekta moja na nyingine, kuhakikikisha kuwa vipaumbele vya lishe katika ngazi ya taifa, mkoa na wilaya vinafanana, pamoja na kujenga uwezo wa taasisi na watendaji ili waweze kutekeleza na kusimamia shughuli za lishe kwa ufanisi. Changamoto hizi zinaweza kudhibitiwa iwapo wadau wataweza kufanya kazi kwa pamoja na sekta ya afya na kushirikiana katika matumizi ya rasilimali na vitendea kazi. Mwongozo huu unalenga kuchochea utekelezaji wa huduma za lishe (scalingupnutrition.org) kwa kutoa miongozo rahisi na vitendea kazi vinavyoweza kusaidia wadau kutoka sekta kupanga na kutekeleza afua za lishe. Mbinu tatu ambazo zimewasilishwa (Kujengea uwezo watendaji kwa kutumia wakufunzi washauri, Utambuzi wa Wadau na Warsha Shirikishi ya Wadau) ni mifano ya jinsi ya kujenga uwezo wa watendaji kutoka sekta mbali mbali wanao tekeleza afua za lishe katika ngazi ya wilaya, kwa lengo la jumla la kuimarisha ushirikiano wenye kuleta ufanisi katika kukabiliana na matatizo ya lishe.

Mpango Mkakati wa Lishe Nchini Tanzania Umezingatia Mahitaji ya Jamii na Kujumuisha Wadau wa Sekta mbali mbali

Mfumo wa Huduma za Lishe Unajumuisha: Sekta Mbali mbali

- Kilimo; afya; maji, Usafi wa Maji na Mazingira; elimu; Uwezeshaji Jamii za Watu Maskini.

Watendaji wa Ngazi Mbalimbali - Taifa – wizara, idara na Taasisi - Serikali za mitaa – Mkoa, wilaya, na jamii

Serikali, na Wadau Wengine - Serikali—Taifa, Mkoa, Wilaya, Kata - Wadau wa Maendeleo—Taasisi za Umoja wa Mataifa, Taasisi za Kimataifa - Asasi za Kiraia (AZAKI) —Mashirika yasiyo ya Kiserikali na Mashirika ya Kidini - Wanataaluma na Sekta binafsi

Imetoholewa Kutoka: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Utekelezaji Afua za Lishe Unaojumuisha Wadau kutoka Sekta Mbali mbali, 2016-2021.

Page 17: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

9

Utekelezaji wa afua za lishe katika sekta nyingi husaidia kufikia malengo kwa ufanisi kuliko sekta moja ikitekeleza afua hizo peke yake.”—Mkakati wa Lishe wa Tanzania Unaojumuisha Sekta Mbalimbali

Utapiamlo Husababishwa na ulaji duni usiokidhi au unaozidi mahitaji ya mwili, kutokula chakula sahihi, au mwili kushindwa kutumia virutubishi kutokana na Magonjwa

Ushirikishaji wa Wadau wa Sekta Mbalimbali ili kukabiliana na utapiamlo unahusu kujumuisha malengo na afua za lishe kwenye mipango na vipaumbele vya sekta muhimu.

Hali ya Lishe ya Watoto Wachanga na Wadogo Nchini Tanzania

Kiwango kidogo cha Unyonyeshaji wa maziwa ya

mama Taratibu za ulishaji watoto wachanga na wadogo zina

changamoto. Watoto wenye umri chini ya miezi wanahitaji

maziwa ya mama pekee— hawahitaji maji, vinywaji vingine

au chakula, kwani vinaweza kusababisha kuugua magonjwa.

41% ya watoto walio chini ya

umri wa miezi 6 hawanyonyweshwi maziwa ya

mama pekee

Kulishwa milo michache kwa siku

Mtoto anapotimiza umri wa

miezi sita anahitajika kupewa chakula cha nyongeza zaidi ya

maziwa ya mama. Vyakula vinapaswa kuandaliwa kwa kuzingatia usafi na usalama.

Pia mtoto alishwe mara nyingi kwa siku.

60% ya watoto wenye umri

wa miezi 6 hadi 23 wanalishwa milo michache

kwa siku

Kutolishwa chakula cha mchanganyiko

Ulaji wa chakula

mchanganyiko ni muhimu katika kuboresha lishe ya watoto. Kuna tofauti kati

ya chakula kinachozalishwa, kinachopatikana na kile

kinachohitajika kwa ajili ya mahitaji ya mwili .

74% ya watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 23

hawapati mlo kamili wenye chakula mchanganyiko

Ukuaji hafifu kimwili na kiakili

Udumavu husababishwa na ukosefu wa virutubishi kwa muda mrefu. Watoto waliodumaa huwa

na kimo kifupi ukilinganisha na umri wao na ubongo wao

huathirika kiasi cha kusababisha kupungua kwa uwezo wao wa

kujifunza, athari zinazodumu hadi wanapokuwa na umri wa mtu

mzima.

34% ya watoto wenye umri chini ya miaka 5 wamedumaa

Sababu Zilizojificha za Utapiamlo

Utapiamlo ni tatizo lenye sababu nyingi zilizomo katika mazingira anayoishi mtoto. Sababu za moja kwa moja ni pamoja na ulaji wa vyakula visivyokidhi mahitaji ya virutubishi na magonjwa, kuna sababu mbalimbali zilizojificha, pamoja na:

• Umasikini,na utegemezi kiuchumi • Kukosa elimu na rasilimali • Ukosefu wa maji safi na mazingira machafu • Ukosefu wa huduma za afya na matibabu • Ukosefu wa hamasa ya mabadiliko ya tabia • Uvunjifu wa haki za kijamii

Huduma za kuboresha hali ya lishe zinapaswa kutekelezwa na sekta mbalimbali

Utapiamlo ni tatizo pana— lisipofanyiwa kazi linaweza kuleta athari za kudumu

kwa waathirika binafsi na jamii yote

Kuunganisha nguvu ya

jamii

Kuimarika Uchumi

Uhakika wa chakula

Mfumo imara wa huduma

za afya

Mazingira wezeshi

1.5 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda: – Chapisho la 1:

Ushirikiano wa Sekta Mbalimbali katika Kuboresha Lishe

A

PRIL

I 201

8 |

TAN

ZAN

IA F

OO

D A

ND

NUT

RITIO

N C

ENTR

E

Page 18: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

10

Kuhusisha sekta mbalimbali ili kuongeza kasi ya huduma za lishe

Ya udumavu inaweza kupunguzwa kwa kuongeza ulaji wa vyakula vyenye virutubishi kwa wingi.

Ya udumavu inaweza kupunguzwa kwa kuboresha kilimo, miundombinu, elimu, maji na usafi wa mazingira, huduma za afya na kadhalika.

► Kujumuisha malengo ya kuboresha lishe; Kujumuisha vipaumbele mahususi vya afya (kwa mfano, udumavu) kwenye sera na shughuli zao.

► Kuboresha ufikishaji wa huduma kwa walengwa, muda wa kuanza na kipindi cha utekelezaji wa mradi; ili kuboresha lishe ya makundi ya waathirika.

► Kutilia mkazo uwezeshaji na lishe ya wanawake; Kubuni programu zinazolenga kuwajengea wanawake uwezo wa kufanya maamuzi na kujitegemea.

► Kutumia fursa zilizopo kuongeza mahitaji na upatikanaji wa huduma ; Mfano kuingiza elimu na ushauri wa lishe katika programu ya uwezeshaji kaya masikini.

Mikakati jumuishi ya kisekta: “Sekta yangu inawezaje kuboresha lishe?”

KILIMO

Boresha upatikanaji wa chakula, teknolojia za kuhifadhi chakula; toa elimu ya udhibiti wa wadudu waharibifu; hamasisha kilimo cha mazao mchanganyiko

ELIMU

Anzisha bustani za shule; toa elimu ya mapishi/jinsi ya kuhifadhi chakula; tumia mpango wa utoaji chakula shuleni kama jukwaa la kutolea elimu ya lishe

MIFUGO &

UVUVI

Hamasisha ufugaji samaki katika jamii, ufugaji bora wa kuku; ulaji wa nyama na mayai kwa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 24

MAENDELEO YA JAMII

Hamasisha wanaume washiriki kusaidia kuboresha ulishaji wa watoto wao; saidia program zinazolenga kuzuia mimba za utotoni; ingiza elimu ya lishe kwenye vikundi vya wanawake

MAJI & USAFI

WA MAZINGIRA

Hamasisha matumizi ya maji safi na salama, utakasaji maji katika kaya, toa elimu ya usafi na matumizi ya vyoo bora na udhibiti sahihi wa kinyesi cha watoto

AFYA

Toa huduma za lishe na ushauri kwenye kliniki ya wajawazito, chanjo, na uzazi wa mpango

Sekta ambazo hazilipa suala la lishe umuhimu zinaweza kusaidia kupunguza tatizo la utapiamlo iwapo zitajumuisha vipaumbele vya lishe katika kazi zao. Sekta hizo zinaweza:

A

PRIL

I 201

8 |

TAN

ZAN

IA F

OO

D A

ND

NUT

RITIO

N C

ENTR

E

Ushuhuda huu umeandaliwa na wadau wa mradi kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Chuo Kikuu cha Tiba cha Kikristo cha Kilimanjaro, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba cha Muhimbili, Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, na Chuo Kikuu cha Cornell University (New York, Marekani). Kwa maelezo zaidi kuhusu mradi huu tafadhali tembelea tovuti hii: [email protected]

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na mradi huu wasiliana na: Luitfrid Nnally, [email protected] Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dar es Salaam

Imetayarishwa kwa Uhisani wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation

Page 19: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

11

Sehemu ya 2: Kujenga Uwezo wa Sekta Zinazohusiana na Lishe Katika Ngazi ya Wilaya kwa Kutumia Wakufunzi Washauri

2.1 Malengo ya Kutumia Wakufunzi Washauri Ili Kuwajengea Uwezo Watendaji Afua zinazolenga kutatua sababu zilizofichika za utapiamlo zimeanza kupewa msukumo na kipaumbele katika sera za kitaifa na miradi mbalimbali. Ili kua na mwendelezo, ni vyema kujenga uwezo wa maafisa katika ngazi ya halmashauri ili kujenga uwezo wa idara mbalimbali kufanya kazi pamoja. katika maswala mtambuka ya lishe. Mbinu mpya za kujenga uwezo zinaweza kutumika pamoja na mbinu za jadi ambazo zimekuwepo awali. Kwa uzoefu uliopo, utoaji wa mafunzo ya kitaaluma mara nyingi husaidia kuimarisha uelewa na kubadili tabia. Hata hivyo, katika uhalisia kuna tofauti kubwa kati ya mabadiliko yanayotokea wakati wa mafunzo na umahiri wanaouonesha walengwa muda mrefu baada ya kujifunza. Mbinu ya kutumia Wakufunzi Washauri inaweza kutumika kama mbadala wa programu za mafunzo zilizo zoeleka katika jamii yetu. Mbinu ya kutumia Wakufunzi Washauri katika kuwajengea uwezo watendaji inawezesha walengwa wa mafunzo na wawezeshaji kubadilishana ujuzi kwa muda mrefu. Mbinu hii inatoa fursa ya mwezeshaji kuendelea kutoa msaada na elimu endelevu kwa walengwa wa mafunzo, hali inayosaidia walengwa kuzoea stadi wanazojifunza. Mbinu hii inasaidia Wakufunzi Washauri wenye ujuzi na uzoefu mkubwa kuwapa walengwa wa mafunzo msaada wa kiufundi kwa vitendo. Kupitia maelekezo ya Wakufunzi Washauri, walengwa wa mafunzo wanapata ujuzi endelevu wa kutatua changamoto halisi zilizopo kwa ufanisi mkubwa, ikiwemo kupata ujuzi wa kuimarisha ushirikiano baina ya sekta mbali mbali na uratibu wa utekelezaji wa afua za lishe. Maafisa Lishe wanao wajibu wa kuratibu mipango ya lishe ya wadau wa sekta mbalimbali katika ngazi ya wilaya. Afisa Lishe wa Wilaya anayejengewa uwezo anapata ujuzi na mbinu za kuimarisha ushirikiano wa wadau wa lishe wa sekta mbali mbali katika kupanga mipango, utekelezaji, ufuatiliaji, na utoaji wa taarifa za huduma zinazotolewa katika jamii. Ili kujenga ushirikiano imara baina ya wadau katika kukabiliana na tatizo tunahitaji kuboresha uratibu, uongozi, kufanya kazi kama timu, na mbinu za uhamasishaji. Kujengea uwezo wa watendaji kwa kutumia mbinu ya Wakufunzi Washauri ni mkakati sahihi unaoweza kuimarisha ujuzi na ushirikiano wa wadau katika utekelezaji wa afua za lishe. Vile vile mbinu hii inaweza kupunguza pengo lilipo katika kuwafikia walengwa na kuainisha fursa mpya kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizofichika za utapiamlo.

2.2 Muhutasari wa Mbinu ya Kujenga Uwezo Watendaji kwa Kutumia Mkufunzi Mshauri Mbinu hii inahusisha kujenga mahusiano ya karibu baina ya Mkufunzi Mshauri mwenye ujuzi na uzoefu mkubwa na mtendaji ambaye anayehitaji kujengewa uwezo. Kupitia mchakato huu mlengwa anapatawa fursa ya kujifunza kwa vitendo na kwa karibu stadi ambazo vinginevyo asingeweza kupata fursa bora zaidi ya kujifunza akiwa katika mazingira halisi ya kazi. Mkufunzi Mshauri anasaidia na kutoa miongozo

Page 20: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

12

ya kuimarisha stadi na uwezo wa mlengwa anayejengewa uwezo. Pia Mkufunzi Mshauri anapata fursa ya kuibua na kuboresha vipaji na kuhamasisha ubunifu wa mlengwa wa mafunzo. Kujengea uwezo mtendaji kwa kutumia mkufunzi mshauri kunahusu kujenga mahusiano yanayolenga kumsaidia mtendaji anayejengewa uwezo ili aweze kuuliza maswali ya msingi, aweze kujitambua yeye mwenyewe na aweze kufanya maamuzi yenye hekima katika wajibu na kazi anazozifanya. Mahusiano haya ya kujifunza ambayo yanaweza kubadilika kulingana na mahitaji yameonesha kuwa ni njia yenye kuleta ufanisi katika kongeza kiwango cha uelewa, ujuzi na umahiri katika utendaji kazi ili kusaidia kupata utatuzi wa changamoto za kiutekelezaji na uratibu wa huduma za lishe zinazotekelezwa katika sekta mbalimbali, pamoja na kuimarisha ushirikiano na mtandao wa wadau na wataalamu wa lishe. Hatima ya yote haya ni kuongeza tija katika juhudi za pamoja za wadau za kukabiliana na matatizo ya utapiamlo.

Mwongozo huu umetumia neno ‘kujengea uwezo watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri’ katika maana ambayo ni tofauti neno ‘usimamizi saidizi’. Usimamizi saidizi mara nyingi unalenga kutafuta makosa au kasoro za utekelezaji au utoaji wa huduma katika maeneo mbalimbali ikiwemo masuala ya kiutawala, ufuatiliaji wa wafanyakazi, utunzaji wa kumbukumbu, matumizi ya rasilimali mbali mbali ikiwemo rasilimali fedha na kadhalika. Kwa kawaida Wasimamizi hutembelea maeneo ya kazi kwa kufuata ratiba maalumu iliyopangwa. Lakini ‘kujengea uwezo watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri‘ ni mbinu inayohusu kujenga mahusiano shirikishi na ya kirafiki baina ya Mkufunzi Mshauri na Mtendaji anayejengewa uwezo ili kumwezesha mlengwa kujifunza kwa urahisi na hivyo kuboresha kiwango chake cha utendaji.

Nini maana ya kujengea Uwezo Mtendaji kwa Kutumia Mkufunzi Mshauri? Kujengea uwezo mtendaji kwa kutumia mkufunzi mshauri ni mbinu inayohusisha kujenga mahusiano endelevu baina ya Mkufunzi Mshauri na mlengwa wa mafunzo ili kumsaidia mlengwa kuboresha kiwango chake cha utendaji katika wajibu, majukumu na kazi zake za kila siku. Mkufunzi mshauri ni muwezeshaji ambae anafanya kazi ya kuinua kiwango cha uelewa, ujuzi na weledi wa mlengwa mmoja wa mafunzo (Mtendaji anayejengewa uwezo) au na kundi la walengwa (Watendaji zaidi ya mmoja wanaojengewa uwezo) katika kipindi kirefu kilichopangwa. Malengo ya mafunzo yanaweza kubadilika kutokana na hali halisi inayojitokeza kulingana na mahitaji ya walengwa. Mbinu hii inawezesha walengwa kujifunza kutoka kwa Mkufunzi Mshauri katika mazingira rafiki na halisi ya utendaji kazi, wakisaidiana na kuelekezana mbinu za kukabiliana na changamoto halisi za kiutendaji mahali pa kazi. Kwa kufanya hivyo, walengwa wa mafunzo wanapata uzoefu kutoka kwa Mkufunzi Mshauri aliye na kiwango cha juu cha ujuzi, umahiri na weledi katika fani husika. Pia walengwa wa mafunzo wanapata fursa ya kutekeleza kwa vitendo stadi na ujuzi walioupata, wanaongezea hekima katika utendaji, wanaongeza kiwango chao cha uelewa wa masuala ya lishe,na kupata uzoefu utakaowasaidia kukabiliana na changamoto za utekelezaji wa shughuli za lishe katika sekta mbalimbali. Jukumu la mkufunzi mshauri siyo kutatua matatizo ya kiutendaji yeye binafsi, bali ni kuwasaidia walengwa kutafuta suluhisho ambalo ni bora litakalosaidia kukabilana na changamoto wanazokabiliana nazo.

Imetoholewa kutoka: The United Republic of Tanzania. Training Programme for Nutrition Officers at Regional and District Levels. Module 4: Resource Mobilization, Advocacy & Capacity Building Skills

Page 21: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

13

2.3 Akina Nani Wananufaika Katika Mbinu Hii? Wanaonufaika wakuu wa mbinu hii ni watendaji wanaojengewa uwezo katika ngazi ya halmashauri au wilaya. Wengine ni Mkufunzi Mshauri na mtandao mpana waa wadau wa lishe katika mkoa na wilaya husika. Ikumbukwe kwamba Serikali katika ngazi ya Mkoa inawajibu wa kutoa msaada wa kiutaalamu na kuzisaidia wilaya katika kutafsiri sera za kitaifa kwa lengo la kufanikisha utekelezaji. Kwa hiyo utekelezaji na utoaji wa huduma hufanyika katika ngazi ya wilaya. Wilaya zinawajibu wa kupanga mipango inayozingatia huduma za lishe zinazopaswa kutekelezwa na sekta mbali mbali, uandaaji wa bajeti, kujumuisha vipaumbele vya lishe katika mipango, utekelezaji, ufuatiliaji na tathimini ya shughuli za lishe zinazotolewa kwa walengwa katika jamii. Maafisa Lishe wa Wilaya wanao wajibu wa kusimamia na kuratibu shughuli mbalimbali katika wilaya (kiambatanisho 2.1). Kuimarisha ushirikiano rasmi kati ya Maafisa Lishe wa Wilaya na watendaji wa sekta mbali mbali kunaweza kusaidia katika kuunganisha nguvu za pamoja za wadau wanao tekeleza Afua za Lishe. Katika wilaya kuna kamati ya lishe ya wilaya ambayo inaundwa na wajumbe kutoka sekta mbali mbali zinazo tekeleza Afua za Lishe. Wajumbe wengine wanatoka katika asasi za kiraia, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Taasisi za Kidini. Mojawapo ya majukumu ya kamati hii ni kupitia mipango na bajeti zinazolenga kuatua matatizo ya utapiamlo katika wilaya. Kwa hiyo ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli za lishe katika jamii, Maafisa Lishe wa Wilaya wanahitaji kuwa na uelewa wa kutosha, stadi, uwezo, na umahiri utakaowawezesha kuboresha usimamizi na uratibu wa sekta mbalimbali na wadau wa lishe katika wilaya. Kwa hiyo kuwajengea uwezo Maafisa Lishe wa Wilaya na baadhi ya Maafisa wa sekta mbalimbali ni njia mojawapo ya mfumo wa utekelezaji na uratibu wa shughuli za lishe katika wilaya. Wataalamu wanaopaswa kuwajengea uwezo watendaji wa ngazi ya wilaya wanaweza kuwa ni wabobezi wa tasnia ya lishe wenye weledi wa kutosha. Wataalamu hao wanaweza kuwa na uzoefu wa usimamizi wa huduma za lishe katika ngazi ya kimataifa, taifa, mkoa au wilaya. Pia wataalamu hao wanapaswa kuwa na umahiri wa kutosha katika utekelezaji wa afua zinazolenga kukabiliana na sababu za moja kwa moja na sababu zilizofichika za utapiamlo. Wakufunzi washauri wanaweza wakawa wafanya kazi rasmi walio ajiliwa na Taasisi mbalimbali kama vile Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Mashirika ya Kimataifa, Wizara na Idara za Serikali, Taasisi za Elimu ya Juu na Asasi za Kiraia, Mashirika ya Dini na sekta binafsi.

Manufaa ya Kujengea Uwezo Watendaji kwa Kutumia Wakufunzi Washauri Manufaa kwa watendaji waliojengewa uwezo:

• Wanapata ushauri na kutiwa moyo • Wanajenga Mahusiano Saidizi • Wanaimarishwa katika stadi za kutatua matatizo yao, Wanaweza kujitathimini

wenyewe na kujiamini zaidi • Wanaongeza weledi na Fursa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kitaalamu • Wanapata uwezo wa kuboresha ushirikiano miongoni mwa sekta mbali mbali

katika utekelezaji wa shughuli za lishe

Page 22: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

14

Manufa ya Kujengea Uwezo Watendaji kwa Kutumia Wakufunzi Washauri (inaendelea) Manufaa kwa wakufunzi washauri:

• Wanapata fursa ya kutathimini ujuzi, umahiri na weledi wanaoujenga kwa walengwa

• Wanajenga mahusiano ya kiutaalam • Wanaimarishwa katika kutambua na kuthamini utendaji wa wengine • Wanapata fursa ya kujiongezea uzoefu na utaalam na kuusambaza kwa wengine • Wanapata fursa ya kujiongezea upeo katika kufahamu jinsi wadau kutoka sekta

mbali mbali wanavyofanya kazi ya kutekeleza Afua za Lishe • Wanapata fursa ya kuridhika kutokana na kuwasaidia na kuwajengea uwezo

wetumishi wengine

Manufaa kwa wadau wa lishe kutoka sekta mbali mbali: • Wanapata hamasa ya kuimarisha ushirikiano baina yao na sekta mbalimbali na

kujitoa katika utekelezaji wa shughuli za lishe. • Wanapata fursa ya kuimarisha mtandao unaowezesha ushirikiano baina yao. • Wanajengewa utamaduni unaowasaidiaa kuridhishwa na utendaji wa kazi

wanazofanya • Wanaongeza tija katika utendaji kwa kuboresha matumizi ya rasilimali, kuepuka

kurudia kutoa huduma moja kwa walengwa wale wale na kushirkikishana uzoefu, channgamoto na mbinu bora za kukabiliana na vikwazo katika utoaji wa huduma.

• Wanapata fursa ya kuimarisha mawasiliano baina yao. • Kuongezeka kwa ubora na ufanisi wa afua zinazotekelezwa katika jamii

2.4 Umuhimu wa Mbinu Hii Mbinu ya Kujengea uwezo watendaji kwa kutumia mkufunzi mshauri imekuwa na ufanisi mkubwa katika kutatua changamoto za kiutendaji wanazokutana nazo katika mazingira ya kazi zao. Mbinu hii inapotumika inawezesha walengwa wa mafunzo kuibua mbinu na mikakati sahihi inayofaa katika kutatua changamoto katika mazingira halisi ya kazi na hivyo kuongeza tija katika utendaji. Katika fani ya Lishe, mbinu hii inaweza kuongeza kasi ya utekelezaji na hatimaye kusaidia kufikiwa kwa malengo ya Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Lishe Unao Jumuisha Wadau Kutoka Sekta Mbali Mbali hususani katika maeneo yafuatayo:

• Kuboresha mawasiliano baina ya wadau na kuimarisha mfumo wa utoaji taarifa. • Kuboresha mipango lishe kwa kujumuisha afua za kukabiliana na sababu zilizofichika za

utapiamlo katika sekta mbalimbali zinazohusika. • Kuratibu ushirikiano wa wadau wa lishe kutoka sekta mbali mbali ili wajumuishe vipaumbele

vilivyoainishwa kwenye Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Lishe. • Kuzijengea uwezo Taasisi na sehemu nyingine katika kuyaweka malengo katika vitendo. • Kuimarisha ushirikiano wa wadau wa lishe.

Page 23: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

15

Mbinu hii inaweza kutoa mchango mkubwa katika kuwasaidia watendaji wanaojengewa uwezo kuainisha upungufu katika utekelezaji wa afua za lisge na hicyo kufanikisha kufikiwa kwa malengo yaliyowekwa. Pia, mbinu hii inawapatia watendaji fursa ya kujifunza kwa vitendo stadi mbalimbali zinazowasaidia kuboresha utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Kupitia mbinu hii Mkufunzi Mshauri anapata fursa ya kutambua ujuzi na umahiri unaohitajika na watendaji katika Wilaya ili waweze kufanya kazi vizuri na wadau mbalimbali wakiwemo maafisa wengine katika wilaya, asasi za kiraia, na watoa huduma za afya wa kujitolea katika ngazi ya jamii hususani katika kupanga na kutekeleza shughuli za lishe. Mkufunzi Mshauri anapata nafasi ya kutambua changamoto na fursa zilizopo mapema na hivyo anakuwa katika nafasi nzuri ya kumsaidia mtendaji anayejengewa uwezo kuweza kugundua maeneo muhimu ya kupewa kipaumbele na mbinu za kukabiliana na changamoto na hivyo kuongeza tija na ufanisi katika kazi yake.

Kwa maelezo zaidi kuhusu mwongozo wa kuandaa mafunzo kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri, Angalia kiambatanisho 2.2. Kadiri mlengwa anayejengewa uwezo anavyoboresha kiwango chake cha ujuzi, umahiri na weledi katika eneo moja la kiutendaji, kipaumbele chaa mafunzo kinapaswa kubadilika ili kumjengea uwezo katika eneo linguine la kiutendaji. Katika kipindi chote cha mafunzo Mkufunzi Mshauri anapaswa kufuatilia kwa karibu jinsi mlengwa anavyoweza kuzoea na kutumia stadi aliyojifunza.

2.5 Hatua za Mafunzo kwa Kutumia Mbinu ya Mkufunzi Mshauri Mkufunzi Mshauri anaweza kupata umahiri iwapo atafanya mazoezi kwa vitendo na kujitathimini mwenyewe. Anaweza kutumia mbinu mbalimbali katika kuwajengea uwezo watendaji. Kwa mfano kutoaa kipaumbele katika kukabiliana na changamoto za kiutendaji zinazo jitokeza ambazo mlengwa anaona kuwa ni ngumu kuzitatua iwapo hatapata msaada wa kitaalamu. Au Mkufunzi Mshauri anaweza kuamua kuanza na changamoto nyepesi, au kumfundisha mlengwa stadi ambazo tayari anazifahamu angalao kwa kiwango kidogo. Hatua zifuatazo zinatoa mwongozo wa mchakato wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri. Vile vile unaweza zana zinazotumika kujengea uwezo watendaji zimeainishwa katika viambatanisho 2.1 hadi 2.7.

Mifano ya Mada na Stadi za Kuwafundisha Walengwa

1. Miongozo na zana za Ufuatiliaji: Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Utekelezaji Afua za Lishe Unao Jumuisha Wadau Kutoka Sekta Mbali mbali, Mwongozo wa Raslimali na Uwajibikaji wa Pamoja, Kadi ya Alama za Lishe, Mwongozo wa Mipango na Bajeti za Lishe Katika Halmashauri

2. Mafunzo kwa vitendo ili kuboresha stadi, ujuzi na umahiri: Mbinu za uwezeshaji na uendeshaji wa mafunzo, stadi za unasihi na mwasiliano, Mbinu za utafiti, Jinsi ya Kuzungumza katika hadhara, Kuaanda na kuongoza mikutano na warsha

3. Elimu mahususi ya lishe: Matibabu ya Utapiamlo wa ukondefu, Udhibiti wa tatizo la upungufu wa Vitamini na Madini mwilini, Kupanga na Kutekeleza tafiti za Lishe

4. Kujumuisha vipaumbele vya lishe katika mipango na kazi za sekta mbalimbali: Kuainisha na kuratibu wadau wa lishe, Kuhamasisha wadau wa sekta nyingine kujumuisha vipaumbele vya lishe katika mipango na bajeti zao, kuhimiza wadau wa sekta mbalimbali kuongeza kasi ya utoaji wa huduma za lishe katika jamii

Page 24: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

16

2.5.1 Hatua ya kwanza: Fanya Tathimini ya Hali Halisi Kujenga mfumo imara wa usimamizi wa masuala ya lishe kunahitaji ufahamu wa kina kuhusu mfumo wenyewe. Vile vile kunahitaji ufahamu wa mtiririko wa taarifa kutoka sehemu moja hadi nyingine, rasilimali, jinsi wadau mbali mbali wanavyobadilika na mchakato mzima wa ufanyaji maamuzi katika ngazi mbalimbali za serikali na kiutawala. Wakati Mkufunzi Mshauri anapokutana na walengwa kwa mara ya kwanza, watapaswa kupanga “muda maalum” wa kukutana na mlengwa mmoja mmoja. Wakati wanapokutana kwa mara nyingine katika hatua za awali, Mkufunzi Mshauri anapaswa kujifunza mazingira halisi ya wilaya husika na mahitaji halisi ya walengwa wa mafunzo. Hatua hii ya awali inajulikana kama ‘hatua ya kufanya tathimini ya hali halisi’. Mkufunzi mshauri ambaye anayafahamu kwa undani mazingira yake ya kufanyia kazi na jinsi yanavyo athiri shughuli na uwezo wa walengwa wa mafunzo anakuwa na fursa nzuri zaidi ya kutoa msaada wenye ufanisi. Mazungumzo ya awali yatamsaidia Mkufunzi Mshauri kujifunza na kuwafahamu kwa undani walengwa wa mafunzo, mtazamo wao, hamasa waliyo nayo na mahitaji yao. Pia husaidia kuainisha vikwazo na fursa zilizopo katika menejimenti na uratibu wa shughuli za lishe katika wilaya. Vilevile Mkufunzi Mshauri anapaswa kuzungumza na wadaau muhimu hususani Mganga Mkuu wa Wilaya na Maofisa wengine. Mazungumzo haya yatamsaidia Mkufunzi Mshauri kuelewa zaidi hali halisi ya masuala ya lishe kwa mtizamo mwingine, kuwashirikisha watendaji muhimu katika utendaji kazi na kwa kujenga hamasa ya kusaidiana. Kiambatanisho 2.3 kinaainisha mfano wa mwongozo wa ‘hatua ya kufanya tathimini ya hali halisi’. Mkufunzi Mshauri na walengwa wa mafunzo wanaweza kufuata hatua hizi ili waweze kutambua na kuandaa malengo ya mafunzo. Lifuatalo ni jedwali linalo onesha baadhi ya maswali ya mfano yanayoweza kutoa mwongozo na kumsaidia Mkufunzi Mshauri wakati anapo jiandaa kuwajengea uwezo walengwa wa mafunzo.

Maswali ya Mwongozo Wakati wa Maandalizi

Matarajio ya mafunzo • Je ni mada au stadi gani zinazopaswa kupewa kipaumbele wakati wa kumjengea

uwezo mlengwa? Je utawezaje kumshauri mlengwa kuhusu mada, stadi na mchakato wa kufuata wakati wa kumfundisha?

• Je mlengwa wa mafunzo anatarajia kukamilisha shughuli gani katika miezi 6 ijayo? • Je ni kwa kiasi gani mlengwa wako anaweza kujifunza yeye mwenyewe bila usaidizi

wa karibu? • Je wewe na mlengwa wa mafunzo mna tarajia nini baada ya mafunzo?

Mbinu za Mafunzo • Je utatumia mbinu gani katika kuwajengea uwezo walengwa? • Je ni jinsi gani utawashirikisha na kuwahamasisha walengwa katika mchakato wa

mafunzo? • Je utawezaje kufanya ufuatiliaji na tathimini ya mafunzo ili uweze kufahamu ufanisi

wa mbinu unazozitumia? • Je utawezaje kuboresha mafunzo kutokana na maoni ya walengwa?

Page 25: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

17

Mkufunzi Mshauri atahitaji kupanga mpango wa kuwatembelea walengwa ili aweze kukutana nao kwa mara ya kwanza na kujadiliana kuhusu mada muhimu zitakazo husika katika mafunzo shirikishi. Hii itamsaidia Mkufunzi Mshauri kutambua uzoefu wa walengwa na maboresho yanayohitajika katika kila mada iliyo ainishwa. Kiambatanisho 2.4 kimeainisha maswali yanayoweza kuulizwa katika kila mada.

Mada za kujadiliana wakati wa mafunzo shirikishi kwa kutumia Mkufunzi Mshauri • Jinsi ya kusimamia wadau wa sekta mbali mbali wanao tekeleza afua za lishe, wadau muhimu na

viongozi watoa maamuzi, makundi mengine ya wadau wanaoweza kushirikishwa • Mabadiliko ya mara kwa mara katika mahusiano na kusaidiana baina ya wadau • Jinsi ya kuongoza wadau wa sekta mbali mbali zinazo tekeleza afua za lishe, mawasiliano, kupeana

taarifa, kupanga mipango na matumizi ya raslimali • Ufahamu, uelewa, hamasa na mtazamo wa wadau wa sekta mbali mbali kuhusu lishe • Ushirikishwaji wa jamii katika huduma za lishe zinazotolewa na wadau wa sekta mbali mbali

Tunza kumbukumbu ya masuala yanayojitokeza katika ‘hatua ya kufanya tathimini ya hali halisi’ ikiwemo mitazamo ya walengwa wa mafunzo shirikishi, kiwango chaao cha uelewa na uzoefu. Mkufunzi Mshauri anaweza kufuatilia mchakato mzima wa mafunzo shirikishi kwa kutunza kumbukumbu katika kila hatua. Walengwa wa mafunzo shirikishi na Mkufunzi Mshauri wanaweza kushirikiana kujaza fomu ya kumbukumbu za mkutano inayonesha malengo, mada muhimu zilizojadiliwa, changamoto na hatua za kuchukua hapo baadaye (Kiambatanisho 2.5). Matokeo muhimu katika hatua hii ya awali, ni kuanzisha ushirikiano baina ya Mkufunzi Mshauri na walengwa wa mafunzo shirikishi. Kila moja anaanza kumwelewa mwenzake na hivyo wanaanza kuimarisha uhusiano wa kitaalama. Ni muhimu kuzingatia kuwa mlengwa wa mafunzo shirikishi anaweza asiwe na uelewa wa maswali ya kuuliza, raslimali au taarifa zipi zinahitajika, au wadau anaohitaji

Maswali ya Mwongozo Wakati wa Maandalizi (inaendelea) Msaada kutoka katika Jamii

• Je ni msaada au raslimali gani unazo hitaji ili uweze kuwa mkufunzi mshauri mwenye ufanisi?

• Je unafikiri kwamba kiongozi wako au maofisa wengine wanaweza kuwa watu wa msaada kwako wakati wa zoezi la kuwajengea uwezo walengwa wako?

• Je unaweza kuwajenga watendaji wengine katika ngazi ya mkoa na wilaya jamii ili wapate ujuzi wa kuwa Wakufunzi Washauri?

Mbinu za Kuimarisha Ushirikiano wa Wadau wa Lishe • Kwa nini ushirikiano wa Wadau na Sekta Mbali mbali ni muhimu katika kukabiliana

na matatizo ya utapiamlo? • Utawezaje kujenga mazingira yanayoruhusu walengwa wa mafunzo kuimarisha

ushirikiano na kufaidika kutokana na kufanya kazi kwa karibu na sekta nyingine? • Je utawezaje kutumia mbinu hii kubuni mafunzo yanayoweza kuimarisha

ushirikiaano wa wadau na sekta mbali mbali ili kuboresha Lishe ya jamii?

Imetoholewa kutoka: The Wisconsin Program for Scientific Teaching. Entering Mentoring: A Seminar to Train a New Generation of Scientists. 2005.

Page 26: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

18

kushirikiana nao katika kazi. Kwa kumfahamu mlengwa wa mafunzo shirikishi Mkufunzi Mshauri anapata fursa ya kutambua stadi, ushauri na taarifa zenye manufaa zinazohitajika na mlengwa. Kuna mbinu nyingi ambazo Mkufunzi Mshauri anaweza kuzitumia katika mafunzo shirikishi ili kuwajengea uwezo walengwa. Mbinu hizo ni pamoja na: kutoa mafunzo kwa mlengwa mmoja mmoja, kutoa mafunzo kwa walengwa wengi kwa pamoja, au kuwajengea uwezo watendaji au maafisa wa fani au sekta moja. Kuelewa mazingira na kuwafahamu walengwa wa mafunzo shirikishi humsaidia Mkufunzi Mshauri kuchagua mbinu anayoweza kuitumia kulingana na mazingira halisi yaliyopo na aina ya walengwa wanaopaswa kushiriki mafunzo shirikishi. 2.5.2 Hatua ya pili: Weka Malengo na Matokeo Unayoyataka Katika hatua ya pili, Mkufunzi Mshauri na walengwa wa mafunzo shirikishi wanapaswa kujadiliana na kuweka malengo na matarajio yanayoweza kufikiwa katika kipindi maalumu walicho jiwekea. Malengo yanapaswa kulenga hali halisi ya lishe katika wilaya na kuzingatia miongozo iliyopo katika Taifa na Wilaya. Kwa kuanzia miongozo ifuatayo inaweza kutumika katika kujiwekea malengo: Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Lishe Unaohusisha Wadau Kutoka Sekta Mbali mbali na Mwongozo wa Halmashauri kwa Ajili ya Kuandaa Mipango na Bajeti ya Lishe. Malengo yanayowekwa yanapaswa pia kuzingatia ujuzi, umahiri na weledi unaohitajika kuboreshwa. Jedwali lifuatalo limeainisha hatua tatu za kutathmini umahiri: Stadi, Ufahamu na tabia zinazohitajika na walengwa wa mafunzo shirikishi:

Umahiri wa Kufikiwa • Stadi- Uwezo wa mlengwa katika kufanya kazi: kwa mfano uwezo wa kutumia Komputa

kwa usahihi, ujuzi wa kufanya mawasiliano ya ana kwa ana, ujuzi wa kufanya mahesabu, au mbinu za kufanya ufuatiliaji na tathmini.

• Ufahamu- Uelewa wa masuala ya msingi ya lishe: Kwa mfano udumavu, Ushirikishaji Wadau kutoka Sekta mbali mbali katika shughuli za lishe, mbinu za kuwatambua wadau wa lishe waliopo katika wilaya, utafutaji wa raslimali fedha, upangaji wa bajeti za lishe, tathmini ya lishe, stadi za unasihi na usimamizi saidizi wa huduma za lishe

• Tabia- Sifa ambazo mtendaji lazima awe nazo katika utendaji kazi: Kwa mfano ubunifu, ushirikiano, uaminifu na utoaji wa mrejesho na kadhalika.

Kuna ukomo wa uwezo wa ushawishi wa Mkufunzi Mshauri kwa walengwa wa mafunzo shirikishi. “Muundo wa Hatua za Ushawishi” unaainisha hatua za kupitia wakati wa kumshawishi mlengwa wa mafunzo shirikishi kuhusu jambo linalolengwa katika mafunzo. Mkufunzi Mshauri anaweza kutumia “Muundo wa Hatua za Ushawishi” kama mwongozo wa kumwezesha mlengwa wa mafunzo shirikishi kufikiria na kutambua matarajio ya mafunzo. Hakikisha kuwa matokeo yanayoya tarajiwa yanapatikana katika muda maalum na yanayo endana na muda wa mafunzo. Hatua nyingine ni kuhakikisha kuwa mlengwa wa mafunzo shirikishi anatambua watendaji na wadau wengine wanaopaswa kumpa ushirikiano ili aweze kufikia matarajio yake. Mwisho, jadili hatua anazopaswa kuchukua mlengwa wa mafunzo shirikishi ili aweze kuwashawishi watendaji wengine na wadau muhimu ili aweze kufikia

Page 27: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

19

matarajio yake. Mlengwa wa mafunzo shirikishi anaweza kuwa na matarajio mbalimbali ambayo yatahitaji awashawishi watendaji na wadau wengi ili wampe ushirikiano kuyatimiza na kupanga mikakati mingi zaidi itakayomwezesha kufikia malengo yake. Kwa kutumia “Muundo wa Hatua za Ushawishi” Mkufunzi Mshauri anaweza kumsaidia mlengwa wa mafunzo shirikishi kupanga na kutekeleza kazi mbalimbali na hivyo kuboresha kiwango chake cha utendaji. Muundo wa Hatua za Ushawishi

Chanzo: EnCompass LLC. Innovative Approaches for Organizational Excellence. https://www.encompassworld.com/resource s/participatory-program-theory. Septemba 2017.

Malengo na hatua za utekelezaji zilizopangwa zinapaswa kulenga shughuli mahsusi, ufanisi wake uwe unapimika, zinazoweza kutekelezwa, na zioneshe muda maalum wa utekelezaji (Kiambatanisho 2.6). Mlengwa wa mafunzo shirikishi anaweza kupata uzoefu mkubwa na kujifunza kutoka kwa Mkufunzi Mshauri na kwa kufanya kazi kwa ushirikiano na wadau kutoka sekta mbali mbali ambapo wote wananufaika kwa ushirikiano huo. Mkufunzi Mshauri anaweza kusaidia mlengwa wa mafunzo shirikishi kuainisha wadau mbali mbali au kuwaandalia warsha shirikishi inayohusu utekelezaji wa afua za lishe. Shughuli hizo zitampa manufaa mlengwa wa mafunzo shirikishi na wadau wote wa lishe kutoka sekta mbali mbali waliopo katika ngazi ya wilaya. Maelezo ya kina kuhusu utambuzi wa wadau wa lishe katika wilaya soma sehemu ya 3 na 4 katika mwongozo huu. Shughuli za kufanya lazima ziongeze kiwango cha uelewa, uzoefu na mafundisho mapya na kuboresha utendaji wa walengwa katika kazi zao za kila siku. Kwa mfano Mkufunzi Mshauri anaweza kuelekeza walengwa wa mafunzo shirikishi jinsi ya kuainisha na kufanya uchambuzi wa wadau wa lishe katika wilaya na kuwasilisha matokeo ya zoezi hilo kwenye kikao cha Kamati ya Lishe ya Wilaya ili kusaidia katika utoaji maamuzi na upangaji wa vipaumbele vya lishe katika ngazi ya wilaya.

2.5.3 Hatua ya Tatu: Ongoza Utekelezaji wa Shughuli Mbali Mbali Baada ya kujiwekea malengo, kutambua matarajio ya mafunzo shirikishi na hatua za kufuata katika mchakato wa mafunzo shirikishi, Mkufunzi Mshauri anapaswa kutoa mwongozo wa utekelezaji wa shughuli zilizokubaliwa. Wakati hayo yanafanyika, Mkufunzi Mshauri anapaswa kujizuia na kuepuka kufanya shughuli hizo yeye mwenyewe. Badala yake, awaachie watendaji wanaojengewa uwezo wazifanye wao wenyewe. Mkufunzi Mshauri awe mwelekezaji kiongozi wa shughuli hizo na awape fursa walengwa wa mafunzo shirikishi wachangie mawazo yao pale panapotokea changamoto. Lengo la mbinu hii ni kuwafanya walengwa wa mafunzo shirikishi waongeze ufahamu kwa vitendo na kujifunza stadi mbalimbali kupitia uwezeshaji wa Mkufunzi Mshauri. Mbinu hii inawawezesha watendaji wanaojengewa

Mipango Hifadhi ya Jamii

Page 28: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

20

uwezo kujifunza kwa vitendo kwa kufanya shughuli mbali mbali wao wenyewe, na hivyo wanakuwa katika uwezekano mkubwa wa kuendelea kutunza ujuzi na stadi mpya ambazo wamezipata. Hakuna taratibu au tabia ambazo zinaweza kufaa kila mahali inapotumika mbinu hii ya kuwajengea uwezo watendaji. Hata hivyo uzoefu umeonesha kuwa kuna baadhi ya misingi inayotoa mwongozo wa mahusiano baina ya Mkufunzi Mshauri na Walengwa wa mafunzo shirikishi wakati mbinu hii inapotumika. Misingi hiyo ni pamoja na sifa nzuri anazopaswa kuwa nazo Mkufunzi Mshauri na mlengwa wa mafunzo shirikishi. Mkufunzi Mshauri anaweza kutumia orodha ya sifa hizi ili aweze kutathimini udhaifu wake na maeneo anayofanya vyema ili aweze kuweka mikakati ya kuboresha mafunzo.

Mkufunzi Mshauri Anaruhusiwa Kuyafanya Yafuatayo

Mkufunzi Mshauri Haruhusiwi Kuyafanya Yafuatayo

Kusikiliza , kujifunza na kuuliza maswali: Kuwa muwazi kwa matatizo na maoni ya walengwa wa mafunzo shirikishi. Eelewa kuwa changamoto zinatokana na sababu nyingi na nzito.

Kusaidia na kuwezesha: Wasaidie walengwa waweze kujenga mtandao wa wadau utakaowasaidia katika kazi zao, ili waweze kushirikiana na wadau wengine, wakiwemo maofisa wakubwa wa ngazi ya utoaji maamuzi kama vile Mganga Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri wa Wilaya n.k.

Kufanya Mapitio: Jadili miongozo mbali mbali ya kitaifa, hadibu za rejea, changamoto na fursa zilizopo na kuzitafsiri katika mazingira halisi yaliyopo.

Kuongeza wigo wa taarifa na raslimali: Wape wlengwa wa mafunzo shirikishi ufahamu wa mambo mapya na uwaelekeze mbinu za kutafuta rasilimali ili waweze kutimiza malengo yao na kufanya maamuzi ya hekima.

Kutia moyo na kuhamasisha: Wajenge walengwa wa mafunzo shirikishi waweze kujikubali, waongeze kiwango chao cha kujiamini kufanya makubwa zaidi ya waliyozoea, wape fursa ya kujifunza kupitia uzoefu na kupanua wigo wao wa kufikiri.

Kutatua matatizo: Usijihusishe na jukumu la kutatua matatizo ya walengwa wa mafunzo shirikishi.

Kufanya majukumu ya mlengwa: Usifanye kazi au kutekeleza shughuli ambazo walengwa wa mafunzo shirikishi wanaweza kuzifanya wao wenyewe

Kuweka Malengo: Usiwape walengwa wa mafunzo shirikishi malengo. Waruhusu wajiwekee malengo yao wenyewe.

Kulazimisha: Usiwalazimishe walengwa wa mafunzo shirikishi kuwa na mwelekeo moja au kuchagua jambo la kufanya.

Kulaumu: Kamwe usiwaambie walengwa wa mafunzo shirikishi kuwa wamekosea na usiangalie zaidi makosa yao.

Page 29: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

21

Mtendaji anayejengewa uwezo ni tofauti na Mkufunzi Mshauri kwa hiyo hawafanani. Wakati mwingine mtu anapata changamoto pale anapokutana na watu waliopitia mazingira na uzoefu tofauti, au wenye elimu tofauti na yeye, au wanaowasilisha maoni yao kwa namna tofauti. Mtu anaweza asiamini uwezo wa mwenzake kwa sababu hana ujuzi, stadi au sifa ambazo yeye anaziona kuwa zina thamani zaidi kwake. Mkufunzi Mshauri mzuri anapaswa kuwa na mbinu mchanganyiko, ujuzi, stadi, umahiri, weledi, na ubora wa pekee katika kazi. Uwezo wa kuwasaidia wateja kwa kuwajengea uwezo wa kujiamini ni sehemu muhimu katika kujenga mahusiano wakati wa zoezi la kuwajengea watendaji uwezo. Kuwatia moyo na kuwapa mrejesho chanya huwasaidia watendaji wanaojengewa uwezo kushinda na kufanikiwa hata wakiwa katika mazingira magumu. Hakuna njia moja pekee inayoweza kufanya zoezi la kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri kuwa nzuri. Mbinu za kuwajengea uwezo watendaji, mahitaji, tofauti za kiwango cha uelewa na ujuzi wa walengwa wa mafunzo shirikishi, malengo, changamoto na mazingira wanayofanyia kazi hutofautiana kwa kiasi kikubwa. Kutokana na tofauti hizo, walengwa wa mafunzo shirikishi katika maeneo yasiyofanana watakuwa na mahitaji, ushauri, taarifa na hata kuhamasishwa kwa namna iliyo tofauti. Baadhi ya walengwa wa mafunzo shirikishi wanaweza kuona haya, au kutokuwa tayari kuomba msaada. Mkufunzi Mshauri mzuri ni yule ambaye ni rahisi kuzoeleka, anayepatikana na anayeweza kuwahudumia watu wenye haiba na tabia za aina mbali mbali. Kwa maelezo ya ziada kwa Wakufunzi Washauri wapya, tazama Kiambatanisho 2.7.

Mlengwa Anaruhusiwa Kuyafanya Yafuatayo Mlengwa Haruhusiwi Kuyafanya Yafuatayo

Kuchukua hatua: Atambue anahitaji kujengewa uwezo, kuomba ushauri endapo unahitajika, kutoa ufafanuzi wa malengo aliyoyaweka na kutoa mrejesho.

Kupokea uzoefu : Lazima ajisikie kuwa na uhitaji wa kupokea uzoefu kutoka kwa wataalamu mbalimbali.

Kupokea Changamoto: Atambue kwamba kila kazi ina changamoto zake –ajaribu kujifunza kutokana na changamoto hizo

Aruhusu watu waje kwake: Aweze kujenga ukaribu na wadau na walengwa wa huduma za lishe, asiwe mtu ambaye hana ushirikiano na watu asiyeruhusu watu wanaotaka huduma yake kumkaribiamtandao na ushirikiano kwa njia ya kutembelea hospitalini, jamii na kuzungumuza na watu mbali mbali

Awe ni mwenye kujiongeza na aonyeshe ushirikiano: Atafute fursa za kushirikiana na watendaji wengine na kushirikishana uzoefu walioupata katika zoezi la mafunzo shirikishi kutumia Mkufunzi Mshauri.

Kuzuia Changamoto: Usikubali Mkufunzi Mshauri kutatua matatizo yako. Karibisha shughuli zinazo kufanya ujifunze kwa vitendo.

Kukaa katika eneo ambalo halina changamoto: Usione haya kupata uzoefu kutokana na kujifunza mambo mapya hata kama kuna changamoto.

Kutochangamana na watu: Tambua kuwa kila mtu (Msimamizi wako, watumishi wenzako,Viongozi wa kijamii) wanajambo ambalo wanaweza kukufundisha

Kutokuwa muwazi: Usiwe na wasiwasi kuomba ushauri jinsi ya kupata fursa na raslimali unazo zihitaji.

Imetoholewa kutoka: Bowling Green State University Mentoring Program. Do’s and Don’ts for Mentors and Mentees.

Page 30: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

22

2.5.4 Hatua ya Nne: Kutoa Msaada Endelevu wa Kiufundi Mkufunzi Mshauri, endelea kutoa msaada endelevu kwa walengwa wa mafunzo shirikishi, kujadili na kutunza kumbukumbu za changamoto na mafanikio mbali mbali ili zikusaidie kufanikisha mafunzo yako. Mlengwa wa mafunzo shirikishi, tekeleza kazi zote zinazotolewa wakati wa mafunzo shirikishi zinazolenga kushirikisha wadau wa sekta mbali mbali zenye uhusiano na lishe, au miradi inayolenga kuboresha lishe ya jamii, ukizichukuliwa kuwa zinakupa fursa inayosaidia kufanya tathmini ya mafanikio ya kazi hizo. Kwa kutumia vitendea kazi na miundo mbali mbali, kama vile muundo wa kufanya Ufuatiliaji na Tathmini na mapitio baada ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali unaweza kugundua njia nzuri ya kuboresha utendaji katika shughuli za baadaye. Maelezo ya vitendea kazi hivyo viwili yanapatikana hapo chini. Muundo wa Ufuatiliaji na Tathmini Sababu ya kufanya ufuatiliaji na tathmini ni kutaka kuainisha mafanikio na upungufu katika utendaji, utoaji wa huduma na uendeshaji miradi, ili kuboresha ubora na ufanisi. Mchakato huu unatoa fursa ya kuweza kugundua na kurekebisha matatizo katika utekelezaji kwa wakati sahihi na kuimarisha tija kwa nyakati zijazo. Jedwali lifuatalo ni muundo anaoweza kutumika kama mwongozo wakati wa kupanga shughuli za ufuatiliaji na tathmini. Mwongozo huu pia una muhtasari wa maswali yanayoweza kuulizwa kutokana na changamoto zinazoweza kujitokeza.

KIASHIRIA Nini kinachopimwa?

MAANA YAKE Jinsi ya kukokotoa na tafsiri yake

HALI YA SASA Je takwimu za sasa zikoje?

LENGO Lengo ni kufika wapi?

CHANZO CHA TAKWIMU Je takwimu hizi zinapatikana wapi?

ITAPIMWA MARA NGAPI Je itapimwa mara ngapi?

MUHUSIKA Nani atahusika kupima na kutoa takwimu hizo?

UTOAJI WA TAARIFA Taarifa zitapelekwa wapi?

Tathimini Baada ya Utekelezaji Mchakato wa Kufanya Tathmini Baada ya Utekelezaji unawawezesha Mkufunzi Mshauri na walengwa wa mafunzo shirikishi kuweka kumbukumbu ya yaliyotokea wakati wa mafunzo. Lengo kuu la kufanya tathimini baada ya utekelezaji ni kujifunza kwa kuzungumza na kufikiria juu ya kukamilisha kazi au mradi husika.Taarifa zinazopatikana zinaweza kutumika kutatua changamoto na kuboresha mchakato mzima katika siku zinazofuata.

Page 31: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

23

Kanuni za Msingi za Kufanya Mapitio Baada ya Utekelezaji 1. Lenga kutoa mrejesho wenye tija unaojenga. Tambua michango chanya kutoka kwa

wadau wote wanao husika. 2. Waone washiriki wote kuwa wako sawa 3. Kama kundi, zingatiene maswali yafuatayo:

• Nini kilitarajiwa kitokee? → Na kwa nini? • Nini kimetokea kwa sasa? → Na kwa nini? • Tofauti ni nini ? → Kwa nini? • Kipi kilifanyika vizuri? → Kwa nini ? • Nini kingeweza kufanyika vizuri zaidi? → Kwa nini? • Je tumeweza kujifunza nini?

Imetoholewa Kutoka: BetterEvaluation. Accessed Sept 2017

http://www.better evaluation.org/ en/ evaluation-options/after_action_review

Muda muafaka wa kufanya tathimini baada ya utekelezaji ni punde tu baada ya kukamilisha utekelezaji wa kazi husika. Hata hivyo, inawezekana kufanyika wakati wowote wa utekelezaji wa shughuli za mafunzo shirikishi. Zoezi hili linalengo la kupata kumbukumbu na tathimini ya mambo waliyo jifunza walengwa kabla hayaja sahaulika. Walengwa wote walioshiriki katika mchakato hawana budi kualikwa katika majadiliano. Kila muhusika yuko huru kushiriki katika majadiliano na kutunza kumbu kumbuku kulingana na jinsi anavyoona na mtazamo wake binafsi. Faidi na Umuhimu wa Kufanya Tathimini Baada ya Utekelezaji:

• Inaweza kutumika kwa shughuli yeyote ile baada ya kubadilisha malengo ya awali. • Inaweza kutumika mara tu ya kukamilisha kila hatua ya utekelezaji. • Inatoa nafasi kwa wadau binafsi kuweza kushirikisha mawazo yao na kuyafanya yasikike. • Inawawezesha watu kutambua kile ambacho wamejifunza. • Inajenga mazingira ya kujiamini katika kundi.

Kwa taarifa zaidi na rejea kuhusu Ufuatiliaji na Tathimini unaweza kusoma zaidi kwenye tovuti zifuatazo:

• BetterEvaluation: http://www.betterevaluation.org/ • Active Learning Network for Accountability and Performance in Humanitarian Action:

http://www.alnap.org/resources/ • International Initiative for Impact Evaluation:

http://www.3ieimpact.org/en/evaluation/resources/ • International Evaluation Partnership Initiative: https://www.evalpartners.org/toolkit • MEASURE Evaluation: https://www.measureevaluation.org/measure

Page 32: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

24

Kujengea Uwezo wa Watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri Mambo ya nyongeza

Maafisa Lishe wa Wilaya na watendaji wengine wanaofanya kazi katika sekta nyingine wanahitaji “stadi za kisasa” ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi. Hata hivyo, suala la kuwajenga uwezo wao ili kuimarisha stadi hizi mara nyingi limekuwa halipewi kipaumbele.

Kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri ni njia mojawapo ya kuwasaidia kujifunza “stadi za kisasa” kama vile ufuatiliaji wa miradi, stadi za kutathmini, stadi za mawasialiano, unasihi na jinsi ya kuwasilishaji mada katika mafunzo na mikutano, uundaji mitandao ya wadau, ushawishi na uhamasishaji wadau na jamii, na elimu ya matumizi ya programu za komputa. Wakati wa utekelezaji wa shughuli za kuwajengea uwezo watendaji, Mkufunzi Mshauri anaweza akatambua, akasaidia na akatumia muda wake katika kuwasaidia watendaji wote wanao ratibu na kutoa mchango katika utekelezaji wa afua za lishe wanaotoka katika sekta mbali mbali ili kupata matokeo yenye ubora wa hali ya juu. Mara nyingi watendaji wanaojengewa uwezo hupata fursa ya kuongeza stadi na ushirikiano katika utendaji wao wa kazi kupitia kwa Mkufunzi Mshauri na hatimaye kuna uwezekano wa walengwa hao wa mafunzo shirikishi kuwa wakufunzi washauri wa wenzao na hivyo kuendeleza suala la kujenga uwezo wa watendaji katika ngazi za chini katika jamii. Kama tujuavyo, serikali inaendelea kupeleka madaraka katika serikali za mitaa, kutafuta njia ya kuwasaidia watendaji wanao wasiliana moja kwa moja na wateja katika masuala ya lishe kunaweza kukaimarisha mipango ya wilaya na utoaji wa afua za lishe zinazotekelezwa na wadau kutoka sekta mbali mbali. Zoezi la kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri na usimamizi elekezi linaweza kuwanufaisha watendaji wengi katika majukumu yao muhimu katika ngazi ya wilaya na hata kusaidia kuwajengea uwezo Watendaji wa Afya ya Jamii (WAJA) waliofundishwa, Maafisa Ugani, au wawakilishi wa masuala ya lishe kutoka idara nyingine nje ya idara ya afya. Maafisa Lishe wa Wilaya ambao wamejengewa uwezo kwa kutumia Mkufunzi Mshauri wanakuwa katika nafasi nzuri ya wao wenyewe kuhitimu na kuwa wakufunzi washauri wa wenzao.

Page 33: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

25

Sera ya Lishe na Utekelezaji Wake: Kuziba Mianya

Nchini Tanzania kuna juhudi kubwa za kitaifa za kusaidia mapambano dhidi ya utapiamlo. Pia kunamsaada mkubwa katika kujumuisha sekta mbali mbali ili zifanye kazi kwa pamoja katika masuala ya lishe. Hata hivyo, kuna changamoto katika utekelezaji wa sera na mikakati ya lishe hasa katika ngazi ya wilaya. Maafisa Lishe wa Wilaya wana mchango mkubwa katika kuratibu sekta mbali mbali zinazo tekeleza masuala ya lishe katika ngazi ya wilaya. Maafisa hawa wanafanya kazi karibu na watoa huduma za afya ngazi ya jamii ili kuweza kuifikia jamii. Miradi yeyote ile muhimu ni lazima iifikie jamii kwa kuwa zaidi ya theluthi mbili (70%) ya Watanzania wanaishi vijijini. Serikali ya Tanzania inaendelea kupeleka madaraka katika serikali za mitaa. Serikali za Mitaa zinahitaji kuwa imara hususani katika masuala ya usimamizi, utawala na uratibu wa shughuli mbali mbali. Serikali ya Tanzania imeimarisha utekelezaji wa shughuli za lishe wilayani kwa kuajiri Maafisa Lishe wa Wilaya mnamo mwaka 2011. Mnamo mwaka 2015, Maafisa Lishe walipata mafunzo ya wiki mbili. Mafunzo hayo yaliratibiwa na kuendeshwa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania. Baada ya mafunzo hayo, Maafisa lishe wanahitaji msaada endelevu ili waweze kutumia ujuzi na stadi walizojifunza katika mafunzo hayo. Zipo fursa mbalimbali za mafunzo endelevu yatakayo saidia kuimarisha uwezo wa Maafisa Lishe kushirikiana na sekta mbali mbali ili kufikisha huduma za lishe kwa walengwa wengi wenye uhitaji. Mbinu ya kutumia Mkufunzi Mshauri ili asaidie kujenga uwezo wa kiutendaji wa Maafisa Lishe ni njia mojawapo inayoweza kusaidia kuboresha ujuzi, umahiri na weledi wa walengwa.

Wakufunzi Washauri waliimarisha uwezo wa kiutendaji wa Maafisa Lishe wa Wilaya

Programu za kuwajengea watumishi uwezo wakiwa kazini zinaweza kuimarisha utaalamu katika huduma za afya, kuimarisha weledi wa watumishi, kuongeza tija katika kazi na kuleta matokeo chanya katika huduma za afya. Nchini Tanzania ubora wa utoaji wa huduma za afya katika jamii uliimarika kutokana na utoaji wa mafunzo kazini kwa wafanyakazi wanao kutana moja kwa moja na wateja wakiwa kazini. Katika mradi wa

majaribio wa Kujenga Mfumo Imara wa Usimamizi wa Masuala ya Lishe, Wataalamu kutoka Taasisi za Elimu ya Juu wafanya kazi ya Ukufunzi Mshauri ili kuwajengea uwezo Maafisa Lishe wa Wilaya mbili kwa kipindi cha mwaka moja. Wakufunzi washauri walikutana na Maafisa Lishe kila mwezi na kutoa ushauri, unasihi,na kuwatia moyo. Vilevile waliwasaidia Maafisa Lishe kupata na kutumia ujuzi na raslimali ambazo zilizohitajika katika kuimarisha na kutekeleza majukumu yao vizuri zaidi. Mafunzo shirikishi kwa watendaji yalijumuisha upangaji wa malengo, kuainisha upungufu, kutatua changamoto na kupanga mikakati na mipango ya utekelezaji. Zoezi hili liliboresha uwezo wa Maafisa Lishe kufanya kazi kwa kushirikiana na sekta mbali mbali na kugundua shughuli mpya ambazo zilikuwa na mchango mkubwa katika kuboresha menejimenti na usimamizi wa masuala ya lishe.

Wakufunzi Washauri na Maafisa Lishe wa Wilaya walilenga maeneo muhimu yafuatayo:

1. Miongozo ya kitaifa. Maafisa Lishe wa Wilaya waliongeza kiwango chao cha uelewa kuhusu mipango ya kitaifa, hadidu za rejea na miongozo mbalimbali ya masuala ya lishe.

2. Raslimali. Maafisa Lishe wa Wilaya walipata vitendea kazi na machapisho mbali mbali ya elimu ya lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania. Vilevile walengwa wa mafunzo shirikishi walijifunza kupitia visa kutoka nchi nyingine.

3. Kuainisha wadau wa lishe katika wilaya. Maafisa lishe walifanya zoezi la kuainisha wadau mbali mbali. Zoezi hili lilisaidia kuwatambua wadau wanaotoa huduma za lishe katika jamii. Wadau hao waliweza kujumuishwa kwenye mtandao mpana wa wadau wa lishe katika wilaya.

4. Uendeshaji wa warsha shirikishi ya wadau. Maafisa lishe wa wilaya pia walindaa warsha ya siku moja ya wadau wa lishe waliopo katika jamii ili kujadili tatizo la utapiamlo, utendaji wa sekta mbali mbali na uainishaji wa vipaumbele kwa ajili ya ushirikiano wa baadaye

“Kujengewa uwezo kazini kulibadilisha mtizamo wangu kuhusu masuala ya lishe

kwa sababu nilitambua kuwa kumbe naweza kuanza kupanga mwenyewe

kwa kupitia miongozo ya lishe na machapisho mengine ya kitaifa .”

[Afisa Lishe wa Wilaya]

Maendeleo ya Jamii 2.6 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala

ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda – Chapisho la 2:

Maafisa Lishe WalioJengewa Uwezo Walitekeleza Mafunzo kwa Vitendo

APR

ILI 2

018

| TA

NZA

NIA

FO

OD

AN

D N

UTRI

TION

CEN

TRE

Page 34: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

26

Kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri katika wilaya nyingine Usimamizi saidizi na ushirikishwaji wa wakuu wa idara mbali mbali ni muhimu katika kuboresha uratibu wa shughuli za lishe. Hata hivyo bado kuna changamoto ya upatikanaji wa wataalamu kwa wakati na nguvu kazi. Mbinu ya kutumia Mkufunzi Mshauri ili kujenga uwezo wa Maafisa Lishe wa Wilaya wanaoratibu shughuli za lishe wilayani inaweza kusaidia kuboresha utendaji. Hivyo kuwatambua wakufunzi washauri waliopo ni jambo la muhimu. Mbinu mojawapo inaweza kuwa ni kujenga mahusiano mazuri kati ya wasimamizi na maafisa lishe wa wilaya. Kwa suala hili, mkufunzi mshauri anaweza kumshirikisha Waganga Wakuu wa Wilaya, Maafisa Lishe wa Mikoa, wataalamu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe, na kadhalika. Mbinu nyingine inayoweza kutumika ni kuwashirikisha Wakufunzi Washauri kutoka sehemu nyingine. Katika mbinu hii unaweza kuwatumia Maafisa Lishe wa wilaya ambao tayari wamejengewa uwezo ili washiriki kuwajengea uwezo Maafisa Lishe wengine katika mkoa husika. Maafisa lishe wa wilaya hawana watumishi walio chini yao ambao wanaweza kuwatumia. Suluhisho kwa hili ni kuongeza idadi ya Maafisa Lishe wa Wilaya, kutumia watumishi wanaofanya kazi za lishe kwenye sekta mbalimbali, maafisa ugani na watoa huduma za afya waliopo katika ngazi ya jamii waliopata ya lishe. Vilevile inawezekana kuwatumia watumishi wa Asasi Zisizokuwa za Serikali na watumishi wengine waliopo vijijini ili kuongeza nguvukazi. Mkakati huu unajulikana kwa jina la: “Mzunguko wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia Wakufunzi Washauri” ili kuongeza idadi ya watendaji wa masuala ya lishe.

“Mchakato wa kujenga uwezo wa watendaji ni endelevu. Juhudi za kubadili mawazo na

mtizamo wa mtu huchukua muda mrefu kuzaa matunda. Kwa hiyo, walengwa wa mafunzo

shirikishi kwa kutumia Mkufunzi Mshauri watahitaji fursa ya kupeleka mafunzo hayo kwa Maafisa Lishe wa wilaya nyingine. Hizi ni juhudi

zakuongeza ari na msukumo mpya katika masuala ya lishe.”

[Afisa Lishe wa Wilaya]

Maafisa Lishe wa Wilaya waliopata mafunzo haya walizingatia kwa makini kuhusu suala la wao kwenda kuwajengea uwezo Maafisa Lishe wengine katika mikoa yao. Maafisa Lishe wa Wilaya walihimizwa kuwashirikisha wadau wengine kutoka katika taasisi zilizo katika jamii. Kwa mfano, Maafisa Lishe wanaweza kutengeneza jumbe mbalimbali za lishe ili zijumuishwe katika shughuli za kilimo. Kwa upande mwingine, Taasisi za kijamii zinaweza kuendesha warsha zinazohusu mipango ya lishe kwa ajili ya wadau mbali mbali walio katika maeneo yao.

Hitimisho—Kujengea uwezo watendaji na msaada wa kitaalamu hoboresha utendaji

Maafisa Lishe wa Wilaya walichukulia zoezi la kujengewa uwezo kwa kutumia Mkufunzi Mshauri kwa mtizamo chanya. Walisema zoezi hili liliboresha ujuzi wao na liliwasaidia kwa kiasi kikubwa. Aidha, walichukulia kwamba wataalamu wa Taasisi za Elimu ya Juu ni chanzo cha kuaminika cha maarifa, ujuzi na raslimali. Hata hivyo, wote kwa pamoja Maafisa Lishe wa Wilaya na Wakufunzi Washauri kutoka Taasisi za Elimu ya Juu walikuwa na kazi nyingi wakati wa zoezi hili. Pia walipata changamoto ya kupanga ratiba ya safari na kuibua kazi mpya. Suala la kujenga uwezo wa watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri likijumuishwa katika mfumo wa elimu kazini kwa watumishi wa Serikali litasaidia na kuleta tija kwa watendaji mbalimbali wakiwemo Maafisa Lishe wa Wilaya. Baada ya kufanya zoezi la kuwajengea uwezo watendaji mara tatu, Maafisa Lishe wa Wilaya walitoa taarifa ya kuimarika kwa uwezo wao hususan kuongezeka kwa: • Ufahamu wao kuhusu lishe • Uelewa wao kuhusu mipango ya lishe ya kitaifa na ya

wilaya • Uwezo wa kuhamasisha jamii na stadi za utatuzi wa

matatizo • Kujiamini • Uwezo katika kufanya kazi zao

Zoezi la kuwajengea uwezo watendaji liliimarisha mahusiano kati ya watendaji wa sekta mbali mbali. Zoezi hili vilevile, liliongeza ushirikiano wa ufanyaji kazi kwa pamoja katika kupanga mipango ya lishe. Katika siku zijazo, Maafisa Lishe wa Wilaya, wataendelea kutafuta msaada utakaowasaidia kuanzisha ushirikiano mpya wakati wa kupanga shughuli za lishe .

Muhtasari wa mambo muhimu: ► Kuna mwitikio mkubwa wa kitaifa katika kupambana na

utapiamlo. Hata hivyo, shughuli mbalimbali zinaweza kufanyika ili kuweza kutambua uwezo wa Maafisa Lishe wa Wilaya katika kusimamia utendaji wa sekta mbalimbali katika wilaya.

► Wanataaluma waliwasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya katika wilaya mbili kwa kipindi cha mwaka moja. Lengo likiwa kuainisha vigezo ambavyo vinasaidia au kuzuia Maafisa Lishe wa Wilaya wasitumie stadi walizonazo.

► Katika kuwajengea uwezo Maafisa Lishe wa wilaya msisitizo maalumu uliwekwa katika kutumia mbinu ya kufanya kazi kwa pamoja kama timu. Waliendesha warsha kwa viongozi wa halmashauri na walifanya zoezi la kuainisha wadau mbalimbali walio katika jamii yao.

► Zoezi la kuwajengea uwezo liliwasaidia Maafisa Lishe kuimarisha stadi za msingi na kuwajengea uhusiano mpya ambao unahitajika katika kupanga na kuratibu shughuli za lishe za wadau wa sekta mbalimbali wilayani.

Jifunze Jifunze zaidi kuhusu kujengewa uwezo na mbinu nyingine za kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbali mbali zinazo tekeleza afua za lishe katika mwongozo wa kujenga mfumo imara wa Masuala ya Lishe Katika tovuti hii: www. tfnc.go.tz

Imetayarishwa kwa Uhisani wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na mradi huu wasiliana na: Luitfrid Nnally, [email protected] Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dar es Salaam

A

PRIL

I 201

8 |

TAN

ZAN

IA F

OO

D A

ND

NUT

RITIO

N C

ENTR

E

Page 35: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

27

Sehemu ya 3: Kuimarisha Uratibu Kupitia Uainishaji wa Wadau wa Lishe Wilayani

3.1 Sababu ya Kuainisha Wadau wa Lishe Hakuna njia moja ambayo inayoweza kutatua matatizo ya utapiamlo. Ili tuweze kutatua matatizo ya utapiamlo kunahitajika juhudi za pamoja za wadau waliopo katika ngazi ya wilaya ili tuweze kuimarisha hali ya kiuchumi na kijamii na kutumia fursa zilizopo ili kuboresha utoaji wa huduma za lishe. Utambuzi wa wadau wa lishe waliopo katika wilaya unatoa fursa ya kuweza kuelewa wadau waliopo, kutambua huduma na kazi wanazozifanya, kuwahamasisha na kujenga ushirikiano na umoja miongoni mwao. Vile vile husaidia katika kuboresha uratibu wa shughuli za lishe katika wilaya.

3.2 Muhutasari wa Maelezo Kuhusu Uanishaji wa Wadau Halmashauri za Wilaya zinaweza kuongeza kasi ya utoaji huduma za lishe kwa walengwa wengi zaidi kwa kuwahusisha wadau mbalimbali katika kutafsiri Sera na Mpango Mkakati wa Lishe Unaojumuisha Wadau wa Sekta Mbalimbali, na kupanga Mipango ya Lishe. Kwa hiyo Wilaya zinapaswa kuwafahamu wadau waliopo katika maeneo yao ili kuelewa maeneo wanayofanyia kazi (Tarafa, kata, mitaa na vijiji), kutambua iwapo afua wanazozitekeleza zinawiana na vipaumbele vya Mpango Mkakati wa Lishe wa Taifa na wilaya, na uelewa wao kuhusu mikakati ya kukabiliana na sababu za karibu, sababu zilichofichika na sababu za msingi za utapiamlo. Kwa kupitia mchakato wa kuainisha wadau Maafisa Lishe wa Wilaya wanaweza kutambua wadau wanaoweza kushirikiana nao na katika maeneo mbalimbali ya ushirikiano. Kuzifahamu kwa undani shughuli wanazofanya wadau na kujumuishamaoni yao katika mipango na vipaumbele vya wilaya na hivyo kuchangia upatikanaji wa mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya lishe.

Kwa nini ni Muhimu Kuainisha Wadau wa Lishe Waliopo Wilayani?

Uainishaji wa Asasi za Kijamii na Wasimamizi wa Asasi hizo husaidia:

• Kupata viongozi walio mstari wa mbele katika kuhamasisha masuala ya lishe, kuwajengea uwezo wadau, na kutafuta raslimali za kutekeleza afua za lishe wilayani.

• Kuimarisha ushirikiano wa wadau wa lishe wilayani na katika jamii hivyo kuongeza wigo wa wadau wa masuala ya lishe wilayani

• Kupata ushauri wa wadau wengine ambao ushiriki wao katika masuala ya lishe ni muhimu ili kuleta ufanisi

• Kuhimiza uwajibikaji, ushiriki na uratibu wa masuala ya lishe miongoni mwa wadau • Kufahamu changamoto na fursa zilizopo katika kuratibu na utekelezaji wa afua za lishe

miongoni mwa wadau mbalimbali • Kuainisha vipau mbele vya lishe ili kuongeza kasi mpya katika utekelezaji wa afua za lishe.

Page 36: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

28

Kuna zana na mbinu nyingi ambazo zinaweza kutumika katika uanishaji wa wadau. Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania siku za awali ilitumia mbinu ya REACH ili kuainisha wadau wanaotekeleza afua za lishe nchini Tanzania. Zana nyingi za kuainisha wadau, ikiwemo zana ya REACH, zinaweza kuboreshwa na kutumika kuainisha wadau kulingana na malengo ya mtumiaji. Zana ya REACH inalenga kutambua mambo makuu manne: Shughuli zinazotekelezwa na wadau, maeneo ya kijiografia zinapotekelezwa shughuli hizo, njia itatumika kutekeleza shughuli hiyo, na walengwa wa huduma zinazotolewa. Taarifa zaidi kuhusu REACH zinapatikana katika tovuti ifuatayo: http://www.reachpartnership.org/reach-countries/tanzania Pamoja na kutumia taarifa zinazokusanywa kwa kutumia zana ya REACH, uainishaji wa wadau unaweza kuwa na lengo la ziada lenye umuhimu – hususani – kuimarisha ushirikiano miongoni mwa wadau kupitia kufahamiana na kujenga au kuimarisha mtandao wa wadau baada ya kuwatambua. Kuimarisha ushirikiano miongoni mwa watendaji wa wilaya na watoa huduma wanaofanya kazi karibu zaidi na jamii ni fursa kwa serikali inayowezesha kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali na kujifunza. Zana ya kuainisha wadau ya REACH inajumuisha maswali yanayotoa mwanya wa kujieleza yanayosaidia kufahamu mtizamo na uzoefu wa kila mdau kuhusu uratibu na ushirikiano baina yao.

3.3 Wanufaika wa Zoezi la Kuainisha Wadau Wadau wanaotekeleza afua zinazolenga kutatua sababu za moja kwa moja au zilizofichika za utapiamlo katika sekta mbali mbali wilayani ndiyo wanufaika wa kwanza wa zoezi la kuainisha wadau. Kupitia zoezi hili, wadau hawa wanapata fursa ya kuimarisha ushirikiano na mtandao wao pamoja na kuwawezesha kubadilishana taarifa na raslimali. Uainishaji wa wadau vilevile unaisaidia jamii kujifunza jinsi ya kuratibu na kuendesha miradi ya lishe inayohitajika kwa wakati huo ambayo ina manufaa katika kuimarisha afya ya jamii. Uainishaji wa wadau unawasaidia wajumbe wa Baraza Kuu la Halmashauri ya wilaya ambao wana wajibu wa kupitisha bajeti na mipango ya maendeleo ya wilaya. Zoezi la uanishaji wadau linawasaidia wajumbe hao kuweza kuzitambua asasi za kiraia na watu binafsi wanaotekeleza miradi ya lishe katika wilaya. Pia kupitia zoezi hili wajumbe wa Baraza Kuu la Halmashauri wanaweza kutambua kazi zinazofanywa na wadau, uwezo wao, fursa walizo nazo, na changamoto wanazo kabiliana nazo wakati wa kupanga na kutekeleza afua za lishe.

Mdau Ni Nani?

Mdau ni mtu yeyote Yule, kundi au Taasisi ambazo zinamtazamo unaofanana. Kwa lengo la kujenga mfumo imara wa wadau wanaotekeleza Afua za lishe, Wadau hawa wanaweza kuwa:

• Maafisa Lishe wa Wilaya • Maafisa Wawakilishi wa masuala ya Lishe kutoka Sekta Mbali Mbali • Maafisa Ugani waliopo katika kata na vijijini • Asasi za Kijamii • Viongozi wa Asasi Zisizokuwa za Kiserikali (AZISE) • Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii (WAJA) • Viongozi wengine katika Jamii (Kwa mfano viongozi wa dini, wakuu wa shule , viongozi wa

serikali za vijiji n.k)

Page 37: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

29

3.4 Unainishaji Wadau Una Umuhimu Gani

Ni vigumu kufikisha huduma bora na kutekeleza afua za kupambana na tatizo la utapiamlo katika jamii iwapo watendaji katika ngazi ya wilaya watakuwa na uwezo mdogo wa kiutendaji. Mara nyingi imewahi kutokea kuwa Maafisa Lishe wa Wilaya wanakosa nguvu ya ushawishi katika mchakato wa kupanga mipango na utengaji wa bajeti na raslimali za miradi ya lishe. Sifa za mfumo imara wa usimamizi wa masuala ya lishe ni pamoja na kuwepo kwa ushirikiano mzuri baina ya wadau na sekta mbali mbali. Ushirikiano huo unawawezesha wadau kuimarisha uwezo wa jamii katika kukabiliana na utapiamlo, kuleta ufanisi katika matumizi ujuzi na stadi walizonazo watendaji pamoja na rasilimali zilizopo. Utambuzi na ushirikiano wa wadau wenye hamasa ya kutumia elimu na ujuzi walionao ili kukabiliana na matatizo mbalimbali ya lishe unasaidia kuleta ufanisi katika utekelezaji na utendaji. Mfumo imara wa usimamizi wa masuala ya lishe unaojumuisha wadau kutoka sekta mbali mbali unakamilika pale ambapo wadau hao wanakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa kuratibiwa kama kundi; pamoja na kazi zao kuongozwa kwa kufuata sera na mikakati ya kitaifa.

3.5 Hatua za kufuata katika Uainishaji Wadau katika jamii

Uainishaji Wadau ni kazi ambayo inaweza kufanyika kwa kufuata hatua kadhaa sambamba na majukumu mengine. Mchakato wa kuwatambua, kuwaainisha na uchambuzi wa wadau unaweza kuchukua wiki au miezi kadhaa, kutegemeana na upatikanaji wa wataalamu wanaoweza kufanya kazi hiyo. Kuna vitendea kazi mbalimbali vinavyoweza kutumika katika zoezi la uainishaji wadau. Vitendea kazi hivyo

Manufaa ya Zoezi la Uainishaji Wadau

Manufaa kwa Maafisa wa Wilaya: • Kujenga uhusiano wa karibu wa kiutendaji kazi na wadau wengine. • Kuimarisha uratibu wa shughuli na miradi mbalimbali. • Kuimarisha mfumo wa utendaji na ushirikiano na wadau mbalimbali wanao tekeleza afua za

lishe. • Kuongeza upatikanaji wa rasilimali ikiwemo rasilimali fedha na watu.

Manufa kwa wadau wa sekta mbalimbali: • Kujenga ufahamu mmoja kuhusu umuhimu wa lishe katika jamii. • Kujenga mahusiano mazuri baina yaon na maafisa waliopo wilayani. • Kuonesha mfano wa jinsi Serikali inavyotambua na kusaidia miradi inayotekelezwa. • Kuimarisha uhusiano miongoni mwa wadau. • Kuongeza fursa za kushirikiana, kusaidiana na kupeana ushauri wa kiufundi. • Kuongeza wigo wa kufikisha huduma za lishe katika maeneo mengi kwenye jamii.

Manufaa kwa jamii: • Kuimarisha na kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya lishe. • Kuhimiza ushirikishwaji wa jamii katika miradi • Kuongeza idadi ya walengwa wanaopata huduma kupitia utekelezaji wa miradi ya lishe • Kuongeza ushirikishwaji na mahusiano katika jamii. • Kuongeza ufahamu kuhusu raslimali zilizopo kwa ajili ya miradi ya afya na lishe.

Page 38: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

30

vimejumuishwa kwenye mwongozo huu katika viambatanisho 3.1-3.3. Mbinu ya uainishaji wadau ni pana, lakini kuna hatua kuu tano ambazo ni muhimu zikafuatwa ambazo ni:

Andaa bajeti na

muda wa kufanya zoezi

Tafuta raslimali Andaa mahitaji na

vifaa utakavyo tumia na fanya utambuzi wa wadau wa kufanya nao kazi

Andaa na fanya majaribio ya vitendea kazi ambavyo utavitumia kulingana na malengo yako

Andaa orodha ya

taasisi na wadau wengine utakaotafuta taarifa zao

Weka ahadi za kukutana na wadau wako

Ulizia kama kuna wadau wengine muhimu

Endelea kurekebisha orodha yako ya wadau

Fanya mahojiano na

wadau uliowaorodhesha

Rekodi mahojiano iwapo utapata ridhaa ya muhusika

Jenga uhusiano mzuri na wadau wako wakati wa mahojiano

Tunza taarifa zako na andika katika karatasi

Panga mpango wa ufuatiliaji wa baadaye

Ingiza taarifa zako

katika Komputa Fanya uchambuzi

wa taarifa zako ikijumuisha: Idadi ya watu, Vikwazo na wawezeshaji.

Tengeneza jedwali la kuonyesha Viashiria mbali mbali

Andika taarifa juu ya njia uliyotumia na matokeo yako na wasilisha matokeo yako

Orodhesha upungufu

na changamoto za wadau na jadiliana na wadau kuhusu matokeo ya zoezi hilo

Ainisha maeneo ya kipaumbele 2-3 ili kuboresha

Wasilisha matokeo ya zoezi hilo kwa wadau wengine katika njia shirikishi

Wahusishe wadau katika kufikia muafaka na wezesha upangaji mipango ya pamoja

3.5.1 Panga Mbinu Utakayotumia Fikiria Juu ya Muda na Raslimali Utakazo Zihitaji Zoezi la kutembelea na kufanya mahojiano na wadau linahitaji mipango thabiti, muda na raslimali watu na fedha. Kwa hiyo unahitaji kujua ukubwa wa zoezi lenyewe la kuainisha wadau: Je litajumuisha taasisi zote zilizopo katika wilaya au litajumuisha baadhi ya taasisi ulizozipatia kipaumbele? Je unatarajia kuhoji wadau wangapi? Je unatarajia dodoso lako litakuwa na maswali mangapi? Uwingi wa takwimu utakazo kusanya na idadi ya wadau utakaowafikia itategemea raslimali ulizo nazo. Timu ya wataalamu kutoka sekta mbali mbali ambayo itakashiriki katika zoezi la uainishaji wadau inaweza kusaidia kupanga mbinu itakayotumika katika zoezi lenyewe. Vilevile inaweza kusaidia katambua muda utakao tumika na kutathmini gharama na raslimali zitakazo hitajika katika zoezi. Mambo muhimu ya kuzingatia ni pamoja na: Muda Utakao Tumika: Zingatia muda utakaotumika kufanya zoezi la kuainisha na kuwashirikisha wadau mbali mbali. Wasiliana na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ili kuandaa orodha ya asasi na mashirika yatakayo husika katika mahojiano. Panga kutumia walau saa moja kwa kila mahojiano utakayo yafanya. Hakikisha kwamba wadau wanafahamishwa siku na muda utakao tumika katika mahojiano

Page 39: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

31

kabla ya zoezi lenyewe kufanyika ili waweze kujipanga. Utahitaji muda wa ziada kuingiza takwimu katika kompyuta na kuandaa taarifa ya zoezi la uainishaji wadau. Usafiri: Wadau unaowahitaji wanaweza kupatikana katika sehemu mbali mbali ndani na nje ya wilaya. Njia bora na sahihi ya kujifunza kazi wanazofanya ni kukutana nao ana kwa ana. Gharama za usafiri zinaweza kuchukua sehemu kubwa ya gharama zote. Pia unaweza kufanya mawasiliano ya awali kwa njia ya simu ili kuuliza maswali machache kuhusu kazi wazifanyazo wadau mbali mbali. Hii inaweza kusaidia kufahamu ni wadau wapi ambao utawapa kipaumbele kwa ajili ya kufanya nao mahojiano ya ziada. Andaa Ratiba: Ratiba ya mahojiano na wadau lazima itangulie kwanza ili waipate mapema, hasa kwa wadau ambao wako katika kata za mbali. Ni muhimu kuwa na bajeti kwa ajili ya gharama za mawasiliano kwa njia ya simu. Kufanya Mahojiano na Wadau: Hakikisha umeandaa dodoso la kukusanyia taarifa, ambalo linaweza kuwa katika mfumo wa karatasi au simu ya mkononi. Matumizi ya karatasi kama mwongozo wa mahojiano hutoa fursa ya kutosha kuandikia na kuchukua taarifa ya masuala muhimu yanayojitokeza wakati wa mahojiano. Endapo mdau ataridhia unaweza kurekodi mahojiano kwenye kifaa cha kurekodia sauti. Hii itakusaidia kusikiliza mahojiano hayo baadaye. Uchambuzi wa Takwimu: Shughuli hii inaweza kufanyika kwa ufanisi zaidi kwa kutumia kompyuta na programu zake (Kwa mfano programu za Microsoft, Excel n.k) na kwa kushirikiana na wataalamu wenye ujuzi wa uchambuzi wa takwimu. Zingatia upatikanaji wa vitendea kazi kama vile kompyuta na wataalamu waliopo katika wilaya kwa ajili ya kufanya kazi hii. Wataalamu hawa wanaweza kuwa maofisa wa halmashauri wenye ujuzi wa masuala ya takwimu. Mkufunzi Mshauri anaweza pia kutumia ujuzi wake kuwaelekeza watendaji wanaotekeleza zoezi hili jinsi ya kufanya uchambuzi wa takwimu kwa kutumia programu za komputa au anaweza kusaidia kuwaunganisha na mtaalamu mwenye ujuzi huo. Kuwa mbunifu katika kuongeza idadi ya wadau wa kushirikiana nao na jifunze kutoka kwa wengine mambo mazuri wanayo yafanya. Badala ya kompyuta unaweza ukatumia karatasi kubwa ya chati pindu kufanyia uchambuzi wa takwimu, kujumlisha na kuandaa muhtasari wa matokeo ya majibu yaliyotolewa na wadau kulingana na kata au sekta zao. Mkakati wa Kusambaza Matokeo ya Zoezi: Mkakati wa kusambaza matokeo ya zoezi la uainishaji wa wadau unajumuisha gharama za uchapishaji, undaaji wa taarifa fupi ya matokeo ya zoezi, hatima na matarajio kuhusu hatua zitakazofuata baada ya zoezi hilo kukamilika. Warsha shirikishi ya wadau kwa ajili ya kuwasilisha matokeo ya zoezi hili inaweza kutumia gharama ndogo. Hivyo njia hii inaweza kuwa yenye ufanisi nay a gharama nafuu ya kuwashirikisha wadau matokeo ya zoezi hilo pamoja na kupata fursa ya kubadilishana uzoefu na kujifunza kutoka kwa wenzao. Jibu Maswali Haya Wakati wa Maandalizi ya Zoezi Katika hatua za maandalizi, kuna maswali mengi ya msingi ambayo yanaweza kukuongoza katika zoezi la kuainisha wadau (Angalia jedwali lifuatalo hapo chini). Majibu ya maswali haya yatakusaidia katika mchakato wa uainishaji wa wadau hususani: jinsi ya kushirikisha wadau, jinsi ya kukusanya taarifa, uwasilishaji wa taarifa, matumizi ya taarifa katika uboreshaji wa ushirikiano na utekelezaji wa miradi. Fikiria kwa undani kuhusu maswali haya ya kukuongoza ili uweze kukusanya taarifa sahihi kutoka kwa wadau ambazo zitawasaidia kutimiza malengo yao ya muda mrefu.

Page 40: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

32

Kuandaa Zana za Kutumia Wakati wa Zoezi la Kuainisha Wadau Andaa au rekebisha zana za kuainisha wadau zilizopo, kamilisha maswali ya kumuuliza kila mdau. Kiambatanisho namba 3.1 kinaonesha mfano wa zana ya uainishaji wadau iliyoboreshwa kutoka katika mradi wa REACH. Ni muhimu kujumuisha maswali ambayo yatatambulisha vikwazo wanavyokutana navyo wadau na wawezeshaji pamoja na changamoto za kiutendaji katika sekta mbalimbali. Hili linaweza kufanikishwa kwa kujumuisha maswali ya kujieleza ambayo yatakusanya maoni na mitazamo ya ndani ya wadau. Pia, hamasisha kujenga mahusiano kwa kuuliza malengo, maoni na vikwazo vinavyowapa wasiwasi wadau na namna ya kuwapa msaada.

Maswali ya kukuongoza katika Maandalizi ya Zoezi la Uainishaji wa Wadau 1. Ni taarifa zipi zitakusaidia katika kudumisha uhusiano na kuimarisha utendaji? 2. Je unatarajia zoezi la uainishaji wadau litafika wapi au litakuwa la ukubwa gani?

Kwa mfano, Je unatarajia kuwalenga wadau wangapi, je unatarajia kuwashirikisha katika mipango ya baadaye?

3. Je ni viashiria gani ambavyo tayari vinafahamika na kuna upungufu gani wa ufahamu katika wilaya?

4. Je takwimu za uainishaji wadau zitajumuishwaje na viashiria vingine ambavyo vipo katika wilaya na taarifa zingine?

5. Je taarifa zitakazo patikana katika zoezi la uainishaji wadau zitatumikaje na zitaweza kuongeza thamani katika utendaji?

6. Je taarifa zitakazo patikana zitasambazwaje na kwa akina nani?

Imechukuliwa kutoka kwa: MEASURE Evaluation Manual, Mapping Community-Based Global Health Programs

Vigezo vya utambuzi wa wadau vinavyopendekezwa kutumika

Vigezo

Wadau Husika

Mifano (unaweza kuboresha orodha hii)

• Wahusika wa masuala ya lishe; Afisa Ugani ngazi ya Kata; Mashirika na Asasi za Kiraia, Watoa Huduma ya Afya ngazi ya jamii.

Shughuli • Mafunzo ya uzalishaji na usindikaji wa vyakula; programu za mikopo midogo kwa ajili ya kilimo cha viazi lishe, ufugaji wa wanyama, programu za huduma ya chakula kwa wanafunzi shuleni, bustani za jamii, taarifa za lishe na ushauri nasaha kwa wanafunzi shuleni

Eneo • Orodha ya kata zote ambazo shughuli zinafanyika

Page 41: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

33

3.5.2 Kuainisha wadau Uimarishaji wa mfumo wa utatuzi wa matatizo ya utapiamlo unahitaji ushirikishaji wa wadau wanaofanya kazi katika sekta mbalimbali. Tumia Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Lishe Unao Jumuisha Wadau Kutoka Sekta Mbali Mbali au miongozo mingine ya kitaifa na taarifa zilizopo katika halmashauri ili kuwatambua wadau wanaoweza kuleta matokeo chanya katika masuala ya lishe, kuwatambua wadau utakaowafikia na kutambua fursa au mchango watakaoutoa katika kukabiliana na matatizo ya utapiamlo. Zingatia shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na uamue kama zinamchango wowote katika lishe ikiwemo shughuli zinazolenga kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, maendeleo na ukuaji wa mtoto, masoko ya bidhaa za vyakula vya watoto wachanga na dawa, teknolojia mpya za kilimo na shughuli nyingine.

Vigezo vya utambuzi wa wadau vinavyopendekezwa kutumika (inaendelea)

Vigezo

Mifano (unaweza kuboresha orodha hii)

Jamii Iliyolengwa

• Jamii yote; watoto chini ya umri wa miaka 18; wakulima na familia zao; watu walioambukiizwa Virusi Vya Ukimwi; wanawake wa umri wa kuzaa miaka 15-49; watoto wachanga wenye umri wa miezi 0-6.

Njia ya kuwafikia

walengwa

• Shule za sekondari; makanisani na misikitini; ushirika wa wakulima; semina za umma; ujumbe wa radio; mashamba darasa.

Malengo • Ongezeko la asilimia 25 la walaji wa unga wa mahindi unaosindikwa katika mashine zinazo ongeza vitamini na madini ya nyongeza; kuboresha hali ya lishe ya watu walioambukizwa VVU

Mshikamano

• Orodhesha wadau wote wenye ushirikiano wa moja kwa moja na wadau wengine wanaojulikana na anayehojiwa

Changamoto

• Mabadiliko ya tabia nchi huathiri programu za kilimo na usafi na usalama wa maji na mazingira; rasilimali zisizotosheleza kufikia makundi yaliyolengwa; changamoto za tamaduni na tabia za ulaji na maandaalizi ya chakula; kukosekana kwa mawasiliano baina ya sekta mbalimbali

Mafanikio • Viongozi maarufu huongoza asasi za kiraia kuhamasisha utatuzi wa tatizo la utapiamlo katika jamii; mitandao isiyo rasmi ya wadau wakiwemo maafisa wa ngazi ya kata husaidia kufikia walengwa kikamilifu; viongozi wa kata wanaounga mkono juhudi za kupambana na utapiamlo.

Fursa za utendaji

• Wadau waliohamasika hujisikia kuwa shughuli za lishe wanazozitekelleza zina umuhimu lakini wanahitaji fursa za kushirikiana. Miradi ya mazao ya biashara na ufugaji wa wanyama inaweza kujumuisha ushauri na taarifa za lishe ikiwemo ulishaji wa watoto wadogo. Hii itasaidia kuongeza kiwango cha uelewa miongoni mwa wazazi na kuimarisha ushirikishaji wa wanaume na wanawake katika utoaji wa maamuzi wa pamoja katika familia ili kuboresha lishe ya familia.

Page 42: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

34

Tengeneza orodha ya wadau wakuanzia ikiwa na taarifa za majina, anwani na namba za simu. Idara ya Maendeleo ya Jamii ya Wilaya ina jukumu la kusajili na kuratibu shughuli za mashirika na asasi zisizokuwa za kiserikali zinazofanya kazi katika wilaya. Idara hii ni sehemu muhimu ya kuweza kupata taarifa za awali za Mashirika Yasiyo ya Serikali yenye uhai yaliyopo katika wilaya. Katika orodha ya kuanzia, ainisha mashirika yenye uwezo wa kujishughulisha na masuala ya lishe. Mashirika hayo yanaweza kuwa yamejumuisha utekelezaji wa shughuli za lishe katika mipango yao au yanaweza kuwa yanatoa huduma katika sekta nyingine za huduma za msingi za kijamii lakini yanajumuisha shughuli za lishe katika afua wanazozitekeleza. Mkakati wa kujumuisha masuala ya lishe katika shughuli za kila siku za sekta mbalimbali una upeo mpana. Ni mkakati ambao wadau wa sekta mbalimbali wanaweza kufanya kazi kwa pamoja kupitia sera na taratibu zilizopo ili ziwanufaishe katika malengo yao, hata kama suala la kuboresha hali ya lishe siyo lengo la msingi la mdau au taasisi husika. Tambua wadau ambao wameweza kutatua matatizo ya msingi ya utapiamlo. Maafisa Watendaji ngazi ya Kata wanaweza kuhusishwa katika kuainisha mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi katika maeneo yao. Baada ya kupata orodha ya awali ya wadau, wasiliana nao kwa njia ya simu na omba kuwafanyia usaili. Kama orodha ni ndefu, jaribu kutoa kipaumbele kwa wadau wenye uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na kutoa matokeo mazuri kwa wengine. Angalia jedwali lifuatalo kuhusu jinsi ya kuweka vipaumbele katika zoezi la kuainisha wadau.

Kabla ya kukutana na wadau, Jaribu kujifunza toka kwao. Endelea kutengeneza taarifa ya kila mdau kwa kutumia maswali yafuatayo.

• Nani yuko tayari kujihusisha na maeneo yenye kipaumbele? • Nani anaweza kuleta mabadiliko chanya katika mipango ya lishe ya sekta mbalimbali? • Nani ana utayari wa kufuata michakato yote, kama kuhudhuria mikutano, kukusanya taarifa,

pamoja na shughuli na taratibu zingine zitakazohitajika? • Nani ana sauti zaidi na anaweza kujitoka katika kuboresha hali za wanaoishi katika mazingira

hatarishi zaidi? • Nani anafahamu mazingira, hali halisi, na changamoto zinazowakabili watu wanaoishi katika

mazingira hatarishi zaidi? • Nani ana uhusiano na sekta mbalimbali na anaweza kuwa kiongozi mzuri wa kuimarisha

mshikamano?

Kuweka vipaumbele katika zoezi la utambuzi wa wadau

1. Tambua wadau wenye ushawishi na wanye utayari wa kufanya mabadiliko ili kwenda na wakati. Tafuta watu wenye nguvu ya kushawishi mabadiliko kwa haraka (kwa mfano vyombo vya habari na viongozi dini na wa kisiasa)

2. Tafuta watu ambao ni wahamasishaji wanoaweza kuwa mfano wa kuigwa katika jamii. Watu au vikundi ambavyo vinajitoa kwa uaminifu katika sekta husika ni muhimu kama sekta yenyewe ilivyo muhimu.

3. Tafuta mashirika yanayosaidia watu walio katika hatari ya kuathirika kutokana na tatizo la upungufu wa rasilimali watu, wenye dalili za kuathirika na utapiamlo na ambao tayari wameanza kupata athari za kiuchumi na jamii.

Imechukuliwa kutoka: Mainstreaming HIV and AIDS in Sectors and Programmes, UNAIDS, UNDEP, September 2005

Page 43: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

35

Ili kupunguza gharama, unaweza kuanza kuainisha wadau walio karibu. Endelea kufuatilia wadau waliopo katika kata za mbali zaidi kadiri muda na rasilimali zitakavyoruhusu. Uainishwaji wa kata chache utaleta matunda iwapo wahamasishaji wa msingi wameshapatikana katika maeneo ya karibu.

3.5.3 Usaili wa wadau Kusanya taarifa za wadau kwa kuwafanyia usaili wa kina. Usaili unawezesha kupata takwimu za namba na za maelezo yenye ufafanuzi wa kina. Mfano takwimu za namba ni “wadau wangapi wanatekeleza shughuli zinazozihitajika katika wilaya” na, mfano wa takwimu zamaelezo yenye ufafanuzi wa kina ni “wadau gani wanafikiria na wanathamini ushirikiano baina ya sekta mbalimbali katika kukabiliana na utapiamlo”. Kujenga mahusiano, kutunza kumbukumbu ya kile ulichojifunza, na kutengeneza mpango wa ufuatiliaji ni mikakati muhimu inayohitajika wakati wa kufanya usaili wa wadau. Jenga mahusiano

Uhusiano ni msingi muhimu wa kujenga ukaribu, kuaminiana na kufanya kazi kwa ushirikiano baina ya watu waliopatana. Hakikisha kuwa wewe mwenyewe unaendesha zoezi la usaili wa wadau kama itawezekana ili kuanzisha uhusiano. Uhusiano ukishaanzishwa, mdau ataweza kuhamasisha, kujifunza, na kuwa mwalimu wa wengine. Wadau wanaweza pia kuhamasisha wengine kukubali maoni, kutoa taarifa, na kutengeneza fursa mpya kwa pamoja.

Tunza kumbukumbu ya ulichojifunza

Ili kupata taarifa zote ulizoshirikishwa wakati wa usaili ni muhimu kuchukua taarifa za kutosha. Kuandika ni jambo muhimu wakati wadau wanapotoa majibu ya maswali ya wazi, taarifa za kina juu ya malengo yao, changamoto na mafanikio. Iwapo wadau wataruhusu, unaweza kurekodi usaili. Kurekodi kunatoa fursa ya kuweza kusikiliza tena majadiliano wakati wa kufanya uchambuzi. Kurekodi pia hujenga mahusiano na mdau na huongeza muda wa kumsilikliza kwa makini, kumuangalia, kuvutiwa na kukufanya ubaki katika majadiliano, bila kupoteza muda wa kuandika taarifa nyingi. Zingatia kuendesha usaili mkiwa wakusanya taarifa wawili. Hii itasaidia kunukuu na kutunza taarifa vizuri, kama mmoja kati

Namna ya kujenga mahusiano • Tafuta msingi wa pamoja wa kuanzia. Tambua mambo yanayopendwa na wadau,

mada, au maoni ambayo yanafanana na yako. Iwapo wadau watajisikia kuwa wana mitazamo inayoendana na yako au wana uzoefu unaofanana na wako huwa watulivu, watakuamini, na watajisikia huru kukushirikisha maoni yao

• Sikiliza kwa makini, kwa kujali na kuonyesha kuwa unavutiwa. Jaribu kuthamini mitazamo mbadala ya wadau na elewa wanachofikiria

• Jibu kwa uwazi, ukionesha kujali, na uaminifu. Mahusiano bora ni yale ambayo huwa yanaonyesha kweli unajali wengine

• Uliza maswali yanayotoa mwanya wa kujieleza. Wape wadau fursa ya kuzungumzia mambo wanayoyapenda, misingi, mahitaji, matakwa, changamoto na mafanikio.

Imechukuliwa kutoka: Mindtools: Essential skills for an excellent https://www.mindtools.com/pages/article/building-rapport-coaching.htm

Page 44: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

36

ya wanaoongoza usaili ataandika taarifa zinazotolewa. Kuendesha usaili mkiwa watu wawili kunaweza kusaidia pia kupata mitazamo kwa pamoja itakayowezesha kumtambua mdau, kupitia mambo ya msingi na kujenga mahusiano. Mara baada ya kukamilisha usahili, pitia taarifa ulizoziandika na jaza mapengo yeyote yaliyojitokeza. Tunza kumbukumbu ya uliyoyachunguza na namna majadiliano yalivyoenda, jinsi mdau alivyoonekana kutulia na kushiriki mazungumzo, na mtazamo wako juu ya ushirikiano aliokupa na shughuli anazofanya ambazo utazipa kipaumbele. Kamilisha maandalizi ya mpango wa ufuatiliaji Mpango wa ufuatiliaji unaweza kukukumbusha jambo ambalo mdau alilitaja unalotaka kulifuatilia ili upate taarifa zaidi; kusambaza taarifa ya matokeo ya zoezi la kuwatambua wadau; au kushirikisha wadau katika kupanga hatua inayofuata, mada za kujadili katika warsha shirikishi ya wadau, na utaratibu wa kupeana taarifa na kujifunza uzoefu baina yao.

3.5.4 Chunguza wadau Wakati wa uchunguzi wa wadau, taarifa zilizokusanywa na kuandikwa wakati wa usaili zinapangwa ili kuangalia mwenendo na tofauti baina yao. Jedwali linaweza kuwa na msaada mkubwa katika kupanga takwimu zote za idadi na maelezo yaliyokusanywa. Kuna njia nyingi za kuingiza na kupanga takwimu katika jedwali. Kwa mfano, unaweza kuingiza takwimu kwa kuzichukua taarifa zote za mdau katika mstari mlalo. Kwa taarifa za idadi, hizi zinaleta urahisi wa kupata jumla ya takwimu za kila mdau. Jedwali la uchambuzi wa takwimu ni mpangilio ambao humwezesha mtumiaji kufafanua au kueleza taarifa zilizokusanywa kwa urahisi zaidi. Jedwali la uchambuzi wa takwimu linaweza kusaidia kueleza mahusiano ya takwimu zilizopo ambazo zitafafanua kila kinachotokea katika sekta na eneo fulani. Pia, linaweza kuonesha wadau wenye malengo, mitazamo na shughuli zinazofanana. Mfano wa jedwali la uchambuzi wa takwimu unapatikana kwenye (Kiambatanisho 3.2) na (Kiambatanisho 3.3). Chunguza tawimu ili kupata muhtasari wa maelezo ya mada mbalimbali. Mhutasari wa maelezo unaweza kutengenezwa kwa kila mdau, ambapo utasaidia kutunza taarifa za hali ya shirika au idara hiyo. Maelezo juu ya aina ya shughuli, sekta husika, eneo, au walengwa ni muhimu sana wakati wa kuandaa muhtasari wa yaliyojitokeza katika taarifa ya mwisho. Kwa takwimu zinazotoa maelezo ya kina, kutengeneza jedwali la mwitikio wa wadau kunaruhusu watumiaji kusoma na kufafanua changamoto, fursa na mada nyingine za majadiliano miongoni mwa wadau. Kutengeneza majedwali ya namna hii kutasaidia kuvumbua maudhui muhimu na kuboresha mawasiliano na mpango wa ufuatiliaji unaoendana na misingi na changamoto za wadau.

Page 45: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

37

Afisa wa ngazi ya wilaya akiwashirikisha wadau kujadili matokeo ya zoezi la uainishaji wa wadau katika jamii

3.5.5 Shirikisha wadau Kuwakutanisha wadau pamoja ni hatua muhimu katika mchakato wa kuimarisha miradi ya lishe. Baada ya usaili, endelea kujenga mahusiano na kutengeneza fursa kwa ajili ya kuongeza mawasiliano na kushirikishana uzoefu miongoni mwa wadau. Wale walioshiriki zoezi la uainishaji wa wadau wanaweza kuandaa warsha shirikishi ya wadau ili kuwasilisha na kujadili matokeo ya zoezi hilo. Warsha shirikishi ni namna nzuri zaidi ya kuwasilisha matokeo na kufikia muafaka miongoni mwa makundi mbalimbali ya wadau.

Utambuzi wa wadau, Maelezo ya ziada Utambuzi na ushirikishwaji wa wadau husaidia kuwezesha upatikanaji wa taarifa nyingi. Iwapo kuna mpango makini ulioandaliwa vizuri unaoongoza zoezi la uainishaji wadau, majibu ya maswali yafuatayo yatapatikana:

• Je, wadau wa msingi ni akina nani? • Je, unashirikiana nao kwa kiasi gani? • Kitu gani sahihi unakifanya sasa kuwafikia wale uliowasahau? • Ni kwa njia gani mtafanya kazi kwa pamoja ili kuleta mwendelezo wa shughuli za

lishe zinazohusisha sekta mbalimbali ambazo wote mnazijali?

Page 46: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

38

Kuainisha wadau: Mbinu ya kupeleka huduma za lishe katika jamii

Ushirikiano baina ya sekta mbalimbali ni jambo la muhimu katika kuboresha umoja katika utoaji wa huduma. Ni muhimu kutathmini shughuli zinazohusiana na lishe zinazofanywa na sekta mbalimbali. Njia mojawapo ya kufanikisha hili ni “Kuainisha wadau”. Shughuli ya kuainisha wadau inasaidia kuboresha uratibu wa wadau wenye lengo linalofanana.

“Mdau” ni mtu, kikundi au taasisi zenye lengo linalofanana. Kwa muktadha wa mwongozo huu, wadau ni wale ambao wanatoa huduma zinachangia kuboresha hali ya lishe ya jamii. Wanajumuisha wafanyakazi wa sekta ya afya, elimu, kilimo na nyingine. Uainishaji wa wadau katika jamii ili kuwatambua unawezesha Maafisa Lishe wa Wilaya kufahamu na kuzishughulikia sababu za utapiamlo na kuzishughulikia kupitia utekelezaji wa sera na mpango mkakati wa lishe unaojumuisha sekta mbalimbali.

Maafisa Lishe wa Wilaya waliainisha wadau katika jamii kwa lengo la:

Kujenga uhusiano na wadau wa sekta zingine ili kushawishi ujumuishaji wa vipaumbele vya lishe katika mipango yao

Kuboresha upatikanaji wa takwimu za lishe na rasilimali pamoja na kuboresha uratibu mapambano dhidi ya utapiamlo

Kusaidia wadau wa lishe katika jamii na kuimarisha ushirikiano na asasi za kiraia

Kutambua sababu halisi za utapiamlo njia za kukabiliana nazo zinazokubalika katika jamii

Mnamo mwaka 2011, Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania ilitekeleza zoezi la kuainisha wadau wa lishe nchini kwa lengo la kutambua upungufu na changamoto za utekelezaji wa afua za lishe. Taasisi ilianza kwa kuainisha mikakati ya lishe katika ngazi ya Taifa. Zana iliyoandaliwa na mradi wa REACH ilitumika katika zoezi hilo. Kupitia mradi wa Kujenga Mfumo Imara Wa Ushirikiano Wa Masuala Ya Lishe Katika Sekta mbalimbali Wakufunzi

washauri waliwasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya mbili kufanya zoezi la kuainisha wadau. Wakisaidiwa na Wakufunzi Washauri, Maafisa Lishe wa Wilaya waliiboresha zana ya REACH na kuitumia kwa majaribio ili kuainisha wadau wa lishe katika wilaya zao. Zana ya REACH inasaidia kuwatambua wadau, kupata taarifa zao na kuimarisha ushirikiano katika kukabiliana na utapiamlo.

Maafisa Lishe wa Wilaya: 1. Waliweza kufahamu nguvukazi iliyopo katika utoaji wa

huduma za lishe. Walifahamu wadau waliopo, shughuli zao na maeneo wanayofanyia kazi.

2. Waliandaa mpango wa kuimarisha ushirikiano na uhusiano na wadau. Mpango huo ulilenga kuimarisha utekelezaji na kuingiza vipaumbele vya lishe katika kazi za wadau.

Maafisa Lishe wa Wilaya waliwafahamu wadau muhimu

Waliiboresha zana ya REACH iliyowasaidia taarifa muhimu. Waliweza kuwatambua wadau waliopo katika wilaya, shughuli za lishe wanazozifanya, walengwa na njia zinazotumika kufikisha huduma kwa jamii.

Maafisa Lishe wa Wilaya walifanya mazungumzo ya ana kwa ana na wadau mbalimbali. Pia walijifunza shughuli za lishe zinazotekelezwa ikiwemo unasihi kuhusu unyonyeshaji wa maziwa ya mama, pamoja na shughuli zinazotekelezwa katika sekta nyingine nje ya sekta ya afya.

Swali la msingi lililowawezesha Maafisa Lishe kupata taarifa hizo ni “Shirika lenu linatekeleza shughuli gani zinazoweza kuchangia ukuaji na afya ya watoto, na uchaguzi wa chakula kwa mama na mtoto mdogo?

Maswali kwa wadau yalenga maeneo matatu muhimu ambayo ni:

1. Changamoto na mafanikio katika kupanga na kufanikisha shughuli na miradi ya kijamii.

2. Jinsi wadau wanavyofanya kazi kwa ushirikiano ili kuoresha afya na lishe ya jamii. Kama hawana ushirikiano kuwaonesha umuhimu wa kushirikiana katika kazi wanazozifanya.

3. Mbinu mpya au zisizotumika mara kwa mara za kufanikisha toaji wa elimu na huduma zinazolenga kupunguza utapiamlo

3.6 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda – Chapisho la 3:

Kuainisha Wadau Katika Jamii Huimarisha Ushirikiano wa Kisekta Katika Utoaji wa Huduma za Lishe

APR

ILI 2

018

| TA

NZA

NIA

FO

OD

AN

D N

UTRI

TION

CEN

TRE

Page 47: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

39

Uainishaji wadau uliibua changamoto na fursa mpya

Maafisa Lishe wa Wilaya waliweza kutambua changamoto chache na namna ya kuzitatua. Halmashauri ziliazimia kusajili mashirika yote katika wilaya. Orodha ya wadau inaweza kuwasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya kutambua wadau waliopo. Orodha hiyo inajumuisha mashirika yasiyokuwa hai kiutendaji. Kuimarisha ushirikiano na usajili wa wadau utasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya kuwatambua wadau waliopo na kufanya nao kazi.

Zoezi la usaili wa wadau linahitaji muda na rasilimali fedha na watu. Watendaji wenye uzoefu wanaweza kukosekana wakati wa kurudia zoezi hilo kwa mara nyingine. Suluhisho mojawapo la changamoto hii ni kuanzisha kikundi cha maafisa 2 hadi 3 kutoka sekta mbalimbali watakaojengewa uwezo wa kuendesha zoezi hili. Kikundi kinaweza kutafuta rasilimali zinazohitajika na kushirikiana kuendesha zoezi la kuainisha wadau. Kikundi kinaweza kujumuisha Afisa Lishe wa Wilaya, Maafisa wa Idara nyingine wanaoshughulikia masuala ya lishe, watendaji wa ngazi ya kata au watoa huduma za afya katika ngazi ya jamii waliopatiwa mafunzo.

Zana ya REACH ya kuainisha wadau inaweza kuboreshwa ili kujumuisha malengo na viashiria vya idara na sekta nyingine (nje ya sekta ya afya) ili kutoa fursa ya kukusanya taarifa zitakazosaidia kila sekta.

Mpango wa kuwezesha wadau

Maafisa Lishe wa Wilaya waliwasilisha matokeo ya zoezi la kuainisha wadau kwa viongozi wa halmashauri na kuhamasisha ushirikiano wa wadau katika utekelezaji wa shughuli za lishe. Zoezi liliwasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya kuweka kumbukumbu na kuimarisha utekelezaji wa shughuli za lishe katika ngazi ya jamii. Kwa kutumia matokeo hayo Maafisa Lishe wa Wilaya waliongoza majadiliano, kushawishi wadau kuongeza masuala ya lishe katika shughuli wanazozifanya na kuboresha ushirikiano wa kisekta. Kutokana na takwimu walizozipata, Maafisa Lishe wa Wilaya waliandaa mpango unaoelekeza njia za kusaidia na ufuatiliaji wa wadau walio tayari kufanya kazi kwa pamoja.

Wadau walikuwa na shauku ya kushirikiana

Jambo moja la muhimu ambalo Maafisa Lishe wa Wilaya walijifunza ni uwepo wa idadi kubwa ya miradi katika jamii inayoweza kujumuisha elimu ya lishe. Mfano mmojawapo ni mradi wa kilimo cha bustani katika kaya, ambapo Maafisa Lishe wa Wilaya walipenda kujumuisha elimu ya maandalizi na uhifadhi wa mbogamboga unaowezesha kupunguza upotevu wa virutubishi.

Mfano mwingine unahusisha miradi ya kilimo cha mazao ya biashara ambapo Maafisa Lishe wa Wilaya waliona fursa ya kujumuisha elimu ya lishe kwa wanaume ili waweze kutumia kipato chao kununua chakula chenye virutubishi muhimu kwa wanawake wajawazito, watoto wachanga na wadogo na vijana balehe.

Wadau walipendezwa na suala la ushirikiano katika utendaji kazi. Walitaka kuyafahamu mashirika yanayofanya kazi kama zao katika jamii. Pamoja na hilo, mashirika yalitaka kujua jinsi ya kupata rasilimali na msaada wa kitaalamu. Karibu wadau wote waliona kuwa shughuli zao zina manufaa katika lishe. Wapo waliovutiwa na kufanya kazi na Afisa Lishe wa Wilaya ili kuweza kuongeza ufanisi wa kazi zao. Muhtasari wa mambo muhimu:

► Ingawa kuna mwitikio mkubwa wa masuala ya lishe katika ngazi ya Kitaifa, bado kuna Halmashauri ambazo zinahitaji msaada wa kuelekezwa namna ya kutekeleza sera na miongozo ya lishe kwa vitendo.

► Wakufunzi Washauri walifanya kazi na Maafisa Lishe wa Wilaya na kuwasaidia kuwatambua wadau waliopo katika wilaya, lengo likiwa ni kutathmini wadau muhimu na shughuli zinazofanywa na sekta mbalimbali.

► Maafisa Lishe wa Wilaya waliwadodosa wadau kuhusu shughuli wanazozifanya. Waliweza kuwauliza kuhusu changamoto na fursa zilizopo katika kufikia malengo yao na kufanya kazi katika sekta mbalimbali.

► Maafisa Lishe wa Wilaya waliandaa mpango wa kuwasaidia wadau wa sekta mbalimbali kuboresha lishe. Mpango ulilenga kuwasaidia wadau kuingiza malengo na shughuli za lishe katika miradi, kufanya ufuatiliaji, na kupanua wigo wa utekelezaji wa miradi katika jamii.

Jifunze Jifunze zaidi kuhusu kujengewa uwezo na mbinu nyingine za kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbali mbali zinazo tekeleza afua za lishe katika mwongozo wa kujenga mfumo imara wa Masuala ya Lishe Katika tovuti hii: www. tfnc.go.tz

Imetayarishwa kwa Uhisani wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na mradi huu wasiliana na: Luitfrid Nnally, [email protected] Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dar es Salaam

A

PRIL

I 201

8 |

TAN

ZAN

IA F

OO

D A

ND

NUT

RITIO

N C

ENTR

E

Page 48: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

40

Sehemu ya 4. Kuimarisha Ushirikiano baina ya Sekta Mbalimbali Kupitia Warsha Shirikishi za Wadau wa Lishe 4.1 Madhumuni ya Warsha Shirikishi Sehemu iliyopita ilieleza mbinu ya kuwatambua wadau muhimu. Hatua inayofuata ni kuwakutanisha wadau hawa pamoja. Warsha shirikishi inahusu kuwaleta pamoja wadau wanaofanya kazi zinazofanana ili kufanikisha kufikiwa kwa malengo yao. Katika warsha hiyo, wajumbe hushiriki majadiliano yanayohusu shughuli wanazozifanya na hivyo watapata fursa ya kutambua maeneo wanayoweza kushirikiana na kubadilishana maoni yanayolenga kuimarisha mikakati yao ya kukabiliana na matatizo ya utapiamlo.Warsha ni mwanzo wa kujenga uhusiano. Inaweza kuanzisha, uhai, mpangilio, kujitambua, ushirikiano wa muda mrefu wa wadau ambao wananufaika kwa pamoja kutokana malengo wanayoshirikiana katika kusaidia uboreshaji wa afya katika jamii.

Nini maana ya Warsha? Warsha ni semina yenye kutoa elimu au mfululizo wa mikutano inayotoa msisitizo wa kubadilishana taarifa miongoni mwa washiriki wachache. Tofauti na semina, warsha ni shughuli ambayo haina urasmi sana na inahitaji zaidi ushiriki wa waliohudhuria. Katika warsha, washiriki wanapata stadi na taarifa mpya kutoka kwa washiriki wenzao na kupitia mada zinazowasilishwa, kwa namna yenye kufurahisha na ambayo itakumbukwa na washiriki.

Chanzo: The United Republic of Tanzania. Training Programme for Nutrition Officers. Module Four: Resource Mobilization, Advocacy and Capacity Building Skills.

4.2 Muhtasari wa Warsha Shirikishi Overview Katika Warsha shirikishi, washiriki hujadili na kutathimini ushirikiano wa sekta mbalimbali katika shughuli za lishe. Wadau hupanga shughuli za lishe ili kuhamasisha ushirikiano baina yao. Wadau hujitahidi kuelewa malengo na iwapo shughuli wanazozifanya zinaingiliana au zinasaidiana pamoja na kutambua vipaumbele vinavyohitaji ushirikiano baina yao. Kupitia ushiriki wao katika warsha hiyo, wadau hupata fursa ya kutafakari mambo mbalimbali na uzoefu walio nao. Pia warsha shirikishi inatoa fursa kwa wadau kushirikishana, kutathimini, na kuboresha uelewa na ujuzi walio nao.

Warsha Shirikishi inaweza: • Kuimarisha mawasiliano na kutoa fursa ya mafunzo kwa wadau • Kuhamasisha na kuendeleza mabadiliko ya tabia zinazoathiri lishe katika • Kukusanya taarifa na uzoefu wa kuaminika • Kuimarisha na kuunganisha upya wadau wenye tabia ya kufanya kazi bila ushirikiano • Kuchochea utekelezaji wa sera za lishe katika maeneo wanayofanyia kazi • Kutambua fursa na mahitaji ya kujenga uwezo wa sekta muhimu ili kuimarisha juhudi za

wadau za kuboresha hali ya lishe

Page 49: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

41

Watu wazima hujifunza vema iwapo mafunzo yatatolewa kwa kutumia mbinu shirikishi. Warsha shirikishi huendeshwa kwa kutumia mbinu shirikishi ambapo wadau hekaa pamoja na kupata fursa ya kubadilishana ujuzi na kutatua matatizo. Mafunzo huunganishwa na uzoefu ambao washiriki wanaweza kuutumia, kujaribu ujuzi mpya na kupeana mrejesho. Ushirikishaji wa washiriki katika warsha husaidia:

• Kuongeza kiwango cha uelewa wa shughuli, vipaumbele na mbinu za kutatua matatizo katika halmashauri.

• Kuongeza msaada kwa miradi na mipango ya sekta mbalimbali zinazotekeleza afua za lishe • Kujifunza kutoka kwa wengine kupitia kushirikishana taarifa na uzoefu • Kuimarisha mawasiliano na ushirikiano miongoni mwa idara na sekta za serikali • Kubuni mbinu za kuboresha utekelezaji wa miradi kwa ufanisi zaidi • Kudhibiti matumizi ya rasilimali na kupunguza uwezekano sekta mbalimbali zinazotekeleza afua

za lishe kurudia kazi ambazo zilishatekelezwa na sekta nyingine. • Kuhakikisha kuwa maamuzi yanazingatia taarifa sahihi ambazo mara nyingine huwa

hazizingatiwi, ikiwa ni pamoja na mitazamo ya jamii au taarifa za idara moja tu. • Kuongeza wigo wa uchambuzi wa maoni na mitazamo katika utoaji wa maamuzi • Kuimarisha uwezo wa viongozi wa jamii na halmashauri

Sehemu hii ya mwongozo inalenga kutambua mipango ya ushirikishwaji inayofaa na mbinu za kuwasilisha, kuendesha majadiliano ya vikundi pamoja na vipengele vya namna ya kutatua matatizo. Mbinu hizi zitaongeza kujifunza na kuandaa msingi imara katika sekta mbalimbali zinazotekeleza afua za lishe katika wilaya. Mbinu shirikishi zinajumuisha kuandaa warsha shirikishi ya wadau inayowawezesha kujifunza na kujenga mahusiano baina yao. Mbinu hiyo ni tofauti na warsha isiyo shirikishi ambapo mtaalamu huwasilisha mada kwenye mhadhara bila kuwashirikisha washiriki.

Tofauti za msingi kati ya kuwezesha warsha na kutoa mhadhara

• Mwezeshaji anahimiza kujifunza kwa pamoja

• Kubadilishana ujuzi miongoni mwa watu

• Wanaojifunza wanahusika, wanaweka mipango na wanashirikishana ujuzi na maarifa

• Mhadhiri ni mtaalam

• Ujuzi hutoka kwa watu wachache kwenda kwa wengi

• Wanaojifunza hawahusiki katika mchakato wa kujifunza.

Tumia mbinu shirikishi kuruhusu wadau kushiriki na ili kuchochea kujifunza. Shirikisha wadau mbalimbali kutoka katika ngazi ya wilaya na jamii ili watu wenye uzoefu wa tofauti waweze kuchangia maarifa waliyonayo wakati wa kujifunza. Andaa warsha ili kujenga ushirikiano na kuwatambua wadau walio

Mwezeshaji

Washiriki wenye uzoefu unaofanana

Washiriki wanye uzoefu mbalimbali

Mhadhiri

Page 50: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

42

tayari na wenye hamasa ya kufanya kazi kwa kushirikiana na wengine. Kwa kutumia mbinu shirikishi, hatimaye wadau wote hupata fursa ya kudhibiti namna mafunzo yanavyotolewa na maamuzi yanayotolewa pamoja na kujifunza kutoka kwa wengine.

4.3 Wanufaika wa Warsha Shirikishi Wakuu wa idara katika halmashauri ndiyo wenye maamuzi kuhusu shughuli zinazotakiwa kupewa kipaumbele. Viongozi hawa watu muhimu katika kufanikisha ushirikiano baina ya sekta mbalimbali katika kutatua tatizo la utapiamlo. Hata hivyo, wana mahitaji na vipaumble mbalimbali vya utekelezaji kiasi kwamba wanaweza kukosa muda wa kutosha kushiriki kikamilifu katika shughuli za lishe. Kwa hiyo, inapaswa kujenga ushirikiano na maafisa wa ngazi ya chini ambao wana muda wa kutosha kufanya kazi kwa pamoja na Afisa Lishe wa Wilaya na watendaji wengine wanaotoa huduma za lishe kwa wateja katika jamii. Sambamba na hilo, ni muhimu kuwashirikisha na kuwapa taarifa Wakuu wa Idara hususan maoni na ujuzi uliopatikana. Utoaji wa taarifa toka ngazi za chini kwenda juu huboresha kiwango cha uelewa wa utekelezaji, changamoto na fursa zilizopo na hivyo kusaidia maandalizi ya mipango na bajeti. Hata kama Wakuu wa Idara ambao ni watoa maamuzi wa hawatahusishwa moja kwa moja, watajifunza kupitia ushiriki wao katika warsha shirikishi. Watapata uelewa wa mitazamo iliyopo ili kuielekeza katika mipango ya sekta mbalimbali zinazotekeleza afua za lishe. Warsha ya ushirikishwaji inahusisha wanufaika wa msingi ambao ni wadau wote watakaoshiriki katika warsha hiyo. Watanufaika kwa kujenga mahusiano mapya, kuimarisha ushirikiano, na matumizi ya miongozo ya kukabiliana na utapiamlo. Wanufaika wengine ni pamoja na wale wanaofanya kazi zinazohusisha utekelezaji wa afua za lishe ambao wako nje ya halmashauri. Wanufaika hawa ni pamoja na mashirika na taasisi zinazofanya kazi katika ngazi ya kimataifa, kitaifa au ya mkoa. Taasisi hizo zinaweza kujifunza vizuri kutoka katika mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe wa wadau katika wilaya na kuboresha mbinu zao katika maeneo mengine.

4.4 Msingi wa Warsha Shirikishi Suala la kutoa kipaumbele katika kukabiliana na utapiamlo linahitaji mshikamano wa hali ya juu wa wadau mbalimbali. Mshikamano ni ubalidilishanaji wa taarifa, kushirikiana katika shughuli zinazotekelezwa, kushirikiana katika matumizi ya rasilimali, kuwezeshana, kuhakikisha pande zote zinanufaika, na kufikia malengo kwa pamoja. Kuandaa warsha shirikishi ni mojawapo ya mbinu za kuwakutanisha wadau kwas lengo la kuimarisha mshikamano miongoni mwao. Wilaya zina viwango tofauti vya ufahamu kuhusu wadau waliopo na ushirikiano walio nao. Sehemu hii ya mwongozo inatoa ufafanuzi kuhusu jinsi ya kuendesha warsha shirikishi ili kuwawezesha wadau waelewe na kuutumia mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe pamoja na kuvitambua vipaumbele vya kufanyia kazi. Wakati warsha shirikishi inapoendelea, wadau hushirikiana katika kupanga shughuli ambazo zitaleta matokeo makubwa katika lishe, afya, na ustawi. Kwa kufanya kazi kwa pamoja, warsha inawasaidia washiriki kupanga mikakati ya kukabiliana na sababu za karibu, zilizojificha za msingi za utapiamlo. Lengo ni kuwa na warsha zinazoweza kuwasaidia watendaji mbalimbali kutekeleza majukumu yao kwa nguvu zaidi ili kukabiliana na utapiamlo.

Page 51: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

43

4.5 Hatua za Kuendesha Warsha Shirikishi Maandalizi na mipango mizuri ni mambo ya muhimu katika kufanikisha warsha shirikishi. Ni muhimu kuainisha hatua zote zinazohusika katika uendeshaji wa warsha shirikishi. Waandaaji wa warsha wataeleza malengo ya warsha, shughuli zilizopangwa kufikia malengo hayo, maudhui makuu ya warsha, na mbinnu za uwezeshaji ambazo zitawahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu katika majadiliano. Zifuatazo ni hatua muhimu zinazowezesha kuongoza mchakato wa maandalizi. Unaweza pia kupata mbinu zingine za kuendesha warsha shirikishi katika Kiambatanisho namba 4.1 – 4.5. 4.5.1 Hatua ya Kwanza: Panga Mbinu ya Kuwezesha Warsha Kuwezesha warsha kunahusisha kuongoza washiriki katika kushirikishana na kujifunza stadi mpya. Mwezeshaji mahiri wa warsha hujishusha kiasi cha kujiweka katika nafasi sawa na washiriki. Pia hutengeneza mazingira chanya ya kushirikishana ujuzi na kujifunza. Mwezeshaji anahitaji kuwa na uelewa wa maudhui na ujumbe muhimu wa warsha, lakini lililo la muhimu zaidi kwake ni kuwa na umahiri katika mbinu shirikishi za uwezeshaji. Kuongoza majadiliano ya wadau linaweza kuwa jambo gumu iwapo washiriki hawafahamiani au hawakubaliani katika mambo ya msingi. Mwezeshaji anapaswa kuchukua nafasi ya mwamuzi, anayetengeneza nafasi itakayowafanya washiriki wajisikie huru kutoa maoni yao. Mwezeshaji anapaswa kuhakikisha kuwa wasiwasi wa kila mshiriki umepatiwa ufumbuzi, hasa wale ambao wanaonekana kusita kutoa mitazamo yao. Kwa kutumia maswali yanayotoa mwanya wa kujieleza, mwezeshaji huwapa fursa washiriki wenye maoni tofauti na wenye maoni yanayofanana kueleza mitazamo yao. Mfano wa maswali yanayotoa fursa ya kujieleza ni:”Je, wengine wanafikiri nini?”, ”Ni changamoto gani zingine ambazo hatujaweza kuzijadili?” au “Je kuna mitazamo mingine tunayoweza kuizingatia?”.

Mambo 8 ya Msingi kwa Mwezeshaji 1. Omba mtu mwingine mshirikiane katika kuwezesha: Kuwezesha warsha ni jambo

linalochosha. Kuwa na mwezeshaji zaidi ya mmoja kunawapa washiriki fursa ya kujifunza kwa namna tofauti.

2. Tengeneza fursa ya kujifunza kwa vitendo, uvumbuzi na uchunguzi. 3. Badilisha kasi na mbinu za uwezeshaji ili kukuongeza shauku ya kujifunza. Watu wazima

hujifunza kwa ufanisi iwapo mbinu shirikishi zitatumika. Hii inamaanisha kuwapa fursa ya kufanya majadiliano, maigizo au kushiriki katika kazi za vikundi.

4. Andaa shughuli zitakazowawezesha washiriki kujifunza kutoka kwa wengine na ili waweze kujenga ujuzi wao wenyewe. Ujuzi si lazima upatikane kutoka kwa mwezeshaji.

5. Tumia uzoefu binafsi kama zana ya kujifunzia. Kama mada ni mpya, waache washiriki wafikiri juu ya uzoefu wao binafsi kwa kuanzia kujifunza na kuvumbua yaliyomo katika mada husika.

6. Tegemea kupata maoni tofauti: yakijitokeza vyema yatachangia katika kufikia uamuzi

7. Tilia mashaka juu ya makubaliano yaliyofikiwa kwa urahisi. Jaribu kuthibitisha Kama kweli wamekubaliana katika jambo hilo na kuona iwapo uamuzi wao ni wa msingi.

8. Wape washiriki machapisho yenye maelezo ya msingi ili kuimarisha ukusanyaji wa maoni na waombe washiriki watoe mifano yao binafsi wakati wa majadiliano.

Page 52: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

44

Andaa shughuli za warsha zitakazowaruhusu washiriki kuelewa vizuri sekta zingine (ikiwa ni pamoja na sera, malengo, lugha, maadili na vipaumbele). Kufanikisha hili, sisitiza kushirikishana uzoefu, ujuzi, na miongozo kwa vitendo baina ya washiriki wa sekta mbalimbali. Mbinu tofauti za uwezeshaji zitawawezesha washiriki kuungana na kutengeneza njia za kuwasiliana wao kwa wao. Mbinu moja ya uwezeshaji, ikiunganishwa na nyingine, itaongeza kiwango cha washiriki mbalimbali kushirikiana katika kujifunza (Angalia kiambatanisho 4.1). Kufanikisha lengo hili, andaa mada ya msingi ambayo itawasilishwa katika warsha na namna itakavyowasilishwa kwa washiriki. Toa fursa ya washiriki kujiongoza na kujifunza kutoka kwa wengine na namna ya kutekeleza mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe. Shughuli zilizoandaliwa zitategemea hali ya wilaya husika na wadau waliopo. Jedwali lifuatalo linatoa mifano ya aina za shughuli za warsha zinazoweza kuandaliwa. Vikao vya warsha vinaweza kurekebishwa kulingana na hali ya wilaya yoyote. Mfano wa ajenda, angalia kiambatanisho 4.2.

Mfano wa Shughuli za Warsha 1. Fanya mapitio ya mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe na miongozo

mingine ya lishe. 2. Tambua malengo yanayendana na maslahi ya washriki wa sekta mbalimbali.

3. Chunguza visa mkasa vinavyoonesha mifano ya “mikakati yenye ufanisi” wakati wa kujaribu kujumuisha shughuli za lishe katika sekta zingine.

4. Jadili changamoto na fursa za kutekeleza shughuli za lishe katika sekta mbalimbali.

5. Andaa vipaumbele vinavyoweza kutekelezwa na sekta mbalimbali ambavyo vinaendana na hali ya wilaya husika.

6. Fanya majaribio ya mikakati mbalimbali uone iwapo inatekelezeka kwa kuanisha taarifa, rasilimali, ujuzi, utayari wa wadau katika utekelezaji na msaada utakaohitajika.

7. Jadili hatua za utekelezaji zitakazofuata na njia za ufuatiliaji.

4.5.2 Hatua ya Pili: Andaa Malengo na Matokeo Warsha shirikishi za wadau wa sekta mbalimbali zinazotekeleza afua za lishe hutoa fursa kwa washiriki kujadili masuala muhimu ya sekta zinazotekeleza afua za lishe ikiwamo.

• Miongozo ya kitaifa na Mpango wa Kitaifa Wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe • Mwitikio wa halmashauri katika masuala ya utapiamlo • Kujumuisha masuala ya lishe katika sekta mbalimbali nje ya sekta ya afya • Changamoto za ushirikiano baina ya wadau

Kusaidia majadiliano, muandaaji wa warsha anaweza kutunga maswali mapema kwa ajili ya kuongoza mjadala. Kwa mfano:

• Je, shughuli gani kwa sasa zipo? • Ni kwa namna gani shughuli zilizopo kwa sasa zinagusa maeneo yenye kipaumbele ya mpango

wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe?

Page 53: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

45

• Ni kwa namna gani shughuli zilizopo kwa sasa zinaweza kuboreshwa au kubadilishwa ili kuleta matokeo mazuri ya lishe?

Jambo la muhimu katika kufanikisha warsha hii ni wadau kuwa na uelewa unaofanana wa malengo, matokeo yanayotarajiwa, na mchakato ulio wazi wa kuwezesha kufikia malengo hayo. Fanya maamuzi kwa umakini kuhusu dhumuni la warsha na kutambua mapema malengo na matokeo. Mwanzoni mwa warsha, washiriki wajadili matarajio yao katika warsha hiyo. Andika masuala hayo yote katika chati pindu ili kila mmoja aone. Kisha ongeza malengo mengine ambayo hayajayatajwa.

Mfano wa Malengo ya Warsha Shirikishi Baada ya warsha shirikishi washiriki wataweza:

1. Kuimarisha uelewa wa Mpango wa Kitaifa wa Utekelezaji wa Shughuli Za Lishe na maeneo yaliyopewa kipaumbele

2. Kuongeza kiwango cha uelewa kuhusu uhusiano wa lishe na sekta nyingine muhimu, pamoja na kutambua fursa na changamoto za ushirikiano

3. Kupata ujuzi kwa vitendo, kufanya mapitio na kujadili matokeo ya mikakati iliyofanikiwa na isiyoleta mafanikio katika kujumuisha masuala ya lishe

4. Kuainisha maeneo maalumu ya kipaumbele kwa wadau ili waweze kuendelea kufanya kazi pamoja.

Mfano wa Matokeo ya Warsha Shirikishi

Matarajio ya warsha hii ni:

1. Kuanzisha ushirikiano miongoni mwa wadau 2. Kufikia muafaka kuhusu vipaumbele 2 hadi 3 vya Mpango wa Kitaifa wa Utekelezaji

wa Shughuli za Lishe vinavyopashwa kuzingatiwa na wadau katika wilaya 3. Kupanga “hatua za kuchukua baada ya warsha” na kuainisha mambo muhimu ya

kutekeleza ikiwa ni pamoja na wahusika, mawasiliano na ufuatiliaji.

4.5.3 Hatua ya Tatu: Wezesha Wadau ili wawe na Uelewa Unaofanana Kuhusu Tatizo Lililopo Ili waweze kuwa wahamasishaji wazuri wa masuala ya lishe, ni jambo lenye manufaa zaidi iwapo wadau watakuwa na uelewa unaofanana kuhusu athari za utapiamlo, umuhimu wa kupambana na utapiamlo, na jinsi utapiamlo unavyoathiri jamii. Maneno yanayotumika katika masuala ya lishe kama vile ukondefu na udumavu hayafahamiki kwa usawa miongoni mwa watu wa sekta mbalimbali. Kwa mfano, athari mbaya za udumavu zinaweza zisieleweke kwa kuwa watoto waliodumaa wanaweza kuonekana kuwa wana afya nzuri. Walengwa wakielewa kuwa athari za utapiamlo ni pamoja na madhara ya kiafya, elimu, uchumi na ustawi wa jamii wanaweza kuhamasika zaidi na hii itasaidia kuongeza uelewa wa ukubwa wa tatizo katika jamii.

Page 54: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

46

4.5.4 Hatua ya Nne: Wezesha Wadau ili wawe na Uelewa Unaofanana Kuhusu Utatuzi wa Tatizo Lililopo Wadau wanaweza kunufaika wakifahamu shughuli zinazojumuishwa katika kutatua matatizo ya lishe. Mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe unaweza kusaidia kujenga mfumo imara wa usimamizi wa huduma za lishe. Mpango huo unatoa mwongozo unaoweza kusaidia katika kupanga

Shughuli za Warsha— Kuelewa maana ya Utapiamlo Ongoza majadiliano kuhusu tofauti zilizopo baina ya uzito pungufu, ukondefu, udumavu na upungufu wa wekundu wa damu. Waache washiriki watoe ujuzi wao wa namna hali hizi zinavyoweza kuathiri afya na tija. Michoro ya watoto wenye udumavu na ukondefu inaweza kutumika kuonesha na kujadili tofauti za aina za utapiamlo.

Ongeza kiwango cha uelewa wa hali ya lishe nchini, hususani katika halmashauri husika. Tumia takwimu za utafiti wa hali ya kidemografia na afya (http://dhsprogram.com au takwimu zingine katika halmashauri. Andika asilimia za ukubwa wa matatizo mbalimbali ya lishe katika chati pindu na uliza washiriki wataje asilimia zinazowiana matatizo mbalimbali ya lishe katika mkoa wao (mfano, udumavu, ukondefu, uzito pungufu, unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee)

Zoezi hili linaweza kuamsha mjjadala kuhusu wanaathirika wakuu wa utapiamlo katika jamii (mfano takwimu za mijini ukilinganisha na vijijini), na hivyo kusaidia kuwatambua walengwa wa afua za lishe. Katika zoezi hili, tawimu zingine kama za “Lives Saved Tool “(http://www.livessavedtool.org/) zinaweza kutumika kuonesha idadi ya vifo vinavyoweza kuzuiwa iwapo afua zinazopendekezwa zitaweza kufikia wanajamii.

Washiriki pia wanaweza kutumia takwimu kutoka katika sekta zao (mfano, takwimu za viwango vya umaskini, usalama na uhifadhi wa chakula, mbinu za kilimo, Usafi na Usalama wa Maji na Mazingira) ili kila mmoja ajifunze vigezo vya msingi miongoni mwa sekta mbalimbali vinavyoweza kuathiri utapiamlo.

Page 55: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

47

bajeti na shughuli za lishe katika wilaya. Unafafanua na kuhamasisha mbinu za ujumla za kuboresha mipango (mfano, kuhusisha sekta mbalimbali na wadau wengine) na kujumuisha malengo mahususi (mfano, kupunguza tatizo la upungufu wa wekundu wa damu kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa). Ingawa mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe unajumuishwa vyema katika mipango ya ngazi ya Taifa, maelezo na mikakati yake inakabiliwa na changamoto katika utekelezaji wake. Warsha shirikishi inatoa fursa kwa wadau kupitia vipengele muhimu vya mpango wa kitaifa wa utekelezaji wa shughuli za lishe, lakini pia inawezesha wadau kufanya mapitio na kujadili uzoefu uliopo na zana zinazoweza kutumika katika utekelezaji (angalia jedwali lifuatalo).

Warsha hutoa fursa ya kutathmini Mambo Yanayofahamika

Kumekuwa na miongozo, machapisho na makala nyingi zinazowaelekeza maafisa mipango jinsi ya kuhusisha sekta mbalimbali katika miradi (mifano katika Kiambatanisho 4.3). Kuongezeka kwa kiwango cha uelewa na majadiliano katika vikundi pamoja na machapisho hayo kutawasaidia wadau kuchukua hatua zinazofaa kukabiliana na utapiamlo katika wilaya. Matumizi ya mbinu shirikishi katika uendeshaji wa warsha kwa maofisa wa idara na wadau wengine kutoka sekta mbalimbali ni hatua ya kwanza na muhimu ya kuimarisha uongozi na usimamizi wa masuala ya lishe katika wilaya. Pia warsha shirikishi inaweza kusaidia kujenga maadili, ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wadau na hatimaye kubadili mwelekeo wa utekelezaji wa hatua za kukabiliana na utapiamlo kutoka katika sekta ya afya kuelekea katika sekta nyingine.

Uwezeshaji wa Warsha Shirikishi Kuhusu ya utambuzi wa Sekta Mbalimbali Zinazotekeleza Afua Za Lishe #1. Wapange washiriki katika makundi kwa sekta ili waweze kujadili na kuandika vipaumbele vya sekta katika chati pindu. Kisha zungushia vipaumbele vya kila sekta vinavyohusiana na utapiamlo na Mpango wa Kitaifa wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe. Shughuli hii inaonesha jinsi ambavyo kila sekta imeingia katika majukumu ya lishe. Pia Washiriki wataona jinsi uzingatiaji wa masuala ya lishe unavyoweza kusaidia kufikia malengo katika sekta zao.

Rasilimali za kulisha na kutunza familia (wajawazito na wanaonyonyesha, kaya na ngazi ya jamii)

Usalama wa chakula, ikiwa ni pamoja na uwepo wa chakula, uwezo wa kukinunua na matumizi ya chakula

Jinsi tunayojifunza: • Namna ya

kuboresha lishe kwa kushirikiana na sekta na wadau wengine.

• Jinsi ya kutekeleza shughuli zilizokubalika katika wilaya mbalimbali.

• Namna ya kushirikishana mbinu zinazofanya vizuri

Mapitio ya pamoja ya hali

ya utapiamlo na njia za utatuzi

zinazofahamika

Mambo tunayoyafahamu • Lishe bora

huboresha maisha na kujenga taifa lenye nguvu

• Tanzania hutanguliza masuala ya lishe katika ajenda za kisiasa.

• Shughuli mbalimbali zinazolenga kuboresha hali ya lishe

Page 56: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

48

#2. Pata mifano wa shughuli za lishe zilizofanikiwa kutoka kwa wadau wa sekta mbalimbali kwa kuwauliza maswali kuhusu shuguli hizo. Unaweza kutumia mfano wa shughuli iliyofanikiwa katika wilaya nyingine. Washiriki wajadili – Jambo gani limesababisha shughuli hii kufanikiwa? Jambo gani linaashiria kuwa shughuli hiyo ilihusisha ushiriki wa sekta mbalimbali? Maswali haya yatasaidia kuwafanya washiriki waielewe vyema dhana ya Mfumo Imara wa Usimamizi wa Masuala ya Lishe kwa Kujumuisha Sekta Mbalimbali. Wape washiriki fursa ya kufikiri jinsi watakavyofanya kazi kwa ushirikiano kukabiliana na changamoto za utapiamlo zinazowagusa wadau wote. #3. Washiriki watoe mifano ya namna ambavyo sekta mbalimbali zinaweza kujihusisha na masuala ya lishe. Toa mifano kwa kutumia miongozo ya kitaifa kama itahitajika. Washiriki wakitambua namna ambavyo Sekta Mbalimbali Zinazotekeleza Afua Za Lishe kwa ushirikiano zinavyofanya kazi, watoe mifano yao wenyewe kwa kueleza namna ambavyo idara na taasisi zao zitaweza kujumuisha masuala ya lishe katika vipaumbele vyao.

4.5.5 Hatua ya Tano: Kutambua Changamoto na Fursa za Ushirikiano Katika Vipaumbele vya Utekelezaji Kutambua changamoto na fursa za kufanya kazi kwa pamoja huusaidia kuimarisha ushirikiano baina ya wadau. Tumia mijadala katika vikundi vidogo vidogo vya washiriki kutambua changamoto zilizopo na mafanikio waliyoyapata katika kufanya kazi kwa kushirikiana na sekta na idara mbalimbali. Unda vikundi vya majadiliano kwa kuchanganya washiriki kutoka sekta mbalimbali. Kikundi kikikamilisha kazi ya kujadili changamoto na mafanikio, kiwasilishe matokeo ya kazi yao mbele ya washiriki wote ili kutambua mikakati ya kutatua changamoto zilizopo kwa manufaa ya wadau na sekta zote.

Kikundi cha washiriki wa warsha shirikishi kikijadili changamoto na fursa za kujenga ushirikiano baina yawadau na sekta mbalimbali

Page 57: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

49

Ushirikishaji wadau katika utoaji wa maamuzi huwasaidia kufikia muafaka juu ya mikakati inayowezesha wadau wa sekta mtambuka kufanya kazi kwa ushirikiano, kuimarisha mawasiliano baina yao, na kufanya ufuatiliaji wa mipango waliyokubaliana kuitekeleza kwa ushirikiano. Tumia maamuzi yaliyofikiwa kutambua maeneo yanayohitaji utekelezaji wa haraka na njia mahsusi ambazo washiriki wa warsha wataweza kushirikiana katika kufanya kazi. Panga vipaumbele vinavyohitaji utekelezaji wa haraka kulingana na mipango ya kitaifa na hakikisha kuna ushahidi wa kitaalamu kuwa vinaweza kuleta ufanisi. Washiriki watafakari kwa kina vipaumbele, mikakati ya kushirikiana, majukumu na wajibu wao, na hatua za ufuatiliaji. Washiriki wazingatie vipaumbele wanavyopenda kuanza utekelezaji wake, rasilimali zilizopo, ratiba na uwezekano wa wadau kushiriki katika shughuli zilizopangwa. Jadili namna ya kuimarisha mawasiliano endelevu na njia itakayotumika kupeana taarifa ili kujenga mshikamano endelevu baina ya wadau baada ya kukamilisha warsha shirikishi. Washiriki wajue kuwa wana muda wa kutafakari zaidi. Waulize ni kitu gani kingine wanahitaji kufahamu au kukifanya ili waweze kufanya maamuzi. Pima uelewa na jadili changamoto zingine zinazoweza kujitokeza katika kufanya maamuzi. Kwa kawaida hakuna njiia moja na ya pekee iliyo sahihi ya kuimarisha ushirikiano wa kisekta katika kukabiliana na utapiamlo. Maamuzi yatategemea uwezo wa kila mdau na uimara wa mtandao wao. Kushirikiana katika kufanya ni jambo la muhimu zaidi katika hali ambayo kuna vipaumbele vingi vya kushughulikia, au endapo shughuli za lishe zilizolengwa kutekelezwa na wadau wa sekta mbalimbali zinaweza kuleta matokeo tofauti kwa walengwa tofauti. Pia wakati wa kuandaa hatua zinazofuata, tafakari juu ya rasilimali fedha zinazohitajika, na jadili kuhusu rasilimali nyingine zilizopo kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zilizopangwa. Hata hivyo, usisubiri kupata fedha za nyongeza kabla ya kuanza utekelezaji wa mikakati iliyopangwa. Hatua nyingi za mwanzoni zinaweza kuanza kutekelezwa kwa gharama nafuu, mfano kutathimini mbinu za utekelezaji zitakazotumika, kuandaa mikutano na warsha za watendaji na wadau wapya zinazoweza kufanyika kwenye ofisi mahali pa kazi na kuandaa vitendea kazi vitakavyotumika katika uhamasishaji na utekelezaji wa afua za lishe katika sekta mbalimbali. Warsha huanza na majadiliano mengi ya msingi. Pamoja na shughuli mahususi ambazo washiriki wa warsha shirikisi wameziandaa, kuna hatua muhimu ambazo zinapaswa kuimarishwa (angalia jedwali lifuatalo).

Mambo Muhimu ya kuendelea Kuimarisha

1. Tenga muda na rasilimali kwa ajili ya kutafakari na kupanga shughuli za lishe 2. Inua kiwango cha uelewa wa manufaa ya shughuli za lishe zinazohusisha sekta mbalimbali. 3. Inua kiwango cha uelewa wa mfumo wa usimamizi wa masuala ya lishe unaohusisha sekta

mbalimbali miongoni mwa wadau muhimu 4. Tengeneza mfumo shirikishi na ubunifu katika kupanga na kuandaa bajeti ya lishe. 5. Jenga uongozi imara wa kamati ya lishe na time ya watendaji wanaotekeleza afua za lishe katika

jamii 6. Ongeza kiwango cha uelewa wa majukumu ya wadau: nani atahusika na fedha, mipango na

utekelezaji. 7. Saidia Maafisa Lishe wa Wilaya na asasi za kiraia kukabilana na changamoto za kifedha na kiutawala

ambazo zinazuia mipango na utekelezaji wa shughuli za lishe zinazotekelezwa na sekta mbalimbali.

Page 58: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

50

Mara baada ya kuanzisha msingi unaoonesha shughuli zipi zipewe kipaumbele na wadau gani wataongoza juhudi hizo, hatua inayofuata ni kuandaa na kutekeleza afua hizo. Suala hili la kuandaa mpango mkakati linaweza kuwa na changamoto na litahitaji ufuatiliaji wa wadau siku zinazofuata baada ya warsha. Kuna machapisho mbalimbali yanayoweza kusaidia kuandaa mpango mkakati wakati wa uendeshaji wa warsha shirikishi. Moja ya machapisho hayo ni Mwongozo wa Kutathimini Programu (http://www.a2zproject.org/pdf/PAG.pdf). 4.5.6 Hatua ya Sita: Fanya Tathimini ya Warsha na Jenga Mshikamano Baina ya Wadau Kabla ya kufika mwisho wa warsha shirikishi, ni muhimu kutathmini namna ambavyo mchakato mzima wa warsha ulivyoenda. Mara nyingi, ili washiriki waweze kuwa huru kueleza jinsi wanayojisikia ni muhimu kutumia maswali maalum ili waweze kujieleza kwa uhuru bila kutaja majina yao (mfano katika Kiambatanisho 4.4). Wape washiriki muda wa dakika 10 waweze kutafakari na kuandika maoni yao na yale waliyojifunza, yale yaliyowafanya wajisikie vizuri, na mambo ambayo yanaweza kuboreshwa. Zingatia kumalizia warsha kwa namna ya kujenga ujamaa na mshikamano. Usiache kasi ipungue. Wimbo, ukimya, kusimama katika mduara, kupeana mikono – kitu chochote kinachodhihirisha na kuhimiza hisia za kufungwa kwa warsha katika muda ambao kundi lilikaa kinaweza kusaidia. Wakati washiriki wanaanza kuondoka, fikiria kutoa chapisho lenye muhtasari wa maelezo yanayojumuisha mambo muhimu na zana zitakazowawezesha washiriki kushirikiana baada ya warsha. Maelezo hayo mafupi yanaweza pia kuwa na rejea muhimu za kujifunza zaidi juu ya mada iliyotolewa au namba za simu, anuani za barua au posta za maafisa na watendaji kama vile Afisa Lishe wa Wilaya. Kuwapa washiriki vitu vya kurudi navyo nyumbani, ikiwa ni pamoja na kijarida au maelezo ya mada zilizowasilishwa wakati wa warsha huwasaidia kuwakumbusha na kutumika kama rejea hapo baadae. Baada ya warsha, andaa muhtasari wa mambo muhimu yaliyojitokeza na maoni yaliyotolewa na washiriki. Wasilisha kwa wadau taarifa hiyo kwa Kamati ya Lishe ya Wilaya. Mfano wa jedwali la kuwasilisha malengo, changamoto, na fursa unapatikana katika Kiambatanisho 4.5.

Page 59: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

51

Mambo ya Ziada ya Warsha Shirikishi Warsha shirikishi huruhusu wadau kuandaa njia za kutatua matatizo pamoja, kubuni mbinu za kufanya kazi na wadau wenye taaluma mbalimbali, na kuleta pamoja serikali, asasi za kijamii, mashirika yasiyo ya kiserikali na wafanyakazi wengine wanaokutana na mteja moja kwa moja ili kuimarisha ufanisi wa miradi. Ni njia muafaka ya kuwahusisha na kujenga mshikamano wa wadau wanaofanya shughuli zinazoleta matokeo katika masuala ya afya na lishe. Kujenga mahusiano haya kunahitaji wadau kuelewa vipaumbele vya wadau mbalimbali na masuala yanayowapa mashaka. Baada ya warsha, mwendelezo wa kuimarisha mahusiano unahusisha namna ya kutafuta njia za kuwasaidia wadau kuimarisha ushirikiano na utekelezaji wa shughuli za lishe katika sekta mbalimbali. Kadri Wilaya inavyoimarisha mfumo wa usimamizi wa shughuli za lishe unaohusisha sekta mbalimbali, warsha nyingine zinaweza kufanyika ili kukamilisha uwasilishaji wa mada nyingine kama vile mpango mkakati, afua za lishe zenye ufanisi, na jinsi ya kutathmini utekelezaji. Wadau wanaweza kuhusishwa katika mchakato wote kuanzia kupanga hadi kufanya tathmini. Pia wanaweza kueleza jinsi wanayoelewa kuhusu afua zinazoweza kutekelezwa na ambazo haziwezi kutekelezwa kulingana na mitazamo yao. Kwa kuzingatia mrejesho wao, unaweza kurudia mchakato huo kutoka mwanzoni na washirikishe wadau katika kuandaa mipango ya ziada, kuboresha, na kuingiza shughuli nyingine wanazoona kuwa zina umuhimu. Kuhusisha wadau wa sekta mbalimbali kwa namna hii kunaweza kuleta utofauti wa hali ya juu na kufanikisha jitihada mbalimbali.

Page 60: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

52

Warsha imeonesha maana ya ‘mkakati jumuishi wa lishe’

Miongozo ya kitaifa inaelekeza jinsi sekta mbalimbali zinavyoweza kufanya kazi pamoja katika kuimarisha masuala ya lishe. Pia miongozo inatoa mifano ya namna washiriki wa sekta za afya, maji, elimu, na sekta zingine wanavyoweza kujumuisha masuala ya lishe katika shughuli zao za kila siku. Miongozo hiyo ni vitendea kazi vinavyowawezesha Maafisa Lishe wa Wilaya na watendaji wa Halmashauri kutekeleza afua za lishe kwa vitendo

Ushirikiano katika kufanya kazi kwa pamoja miongoni mwa sekta mbalimbali ni njia inayofaa iwapo wadau wakuu wanakusudio linaloeleweka kwa kuzingatia malengo yao na kile wanachokiamini kuwa ni muhimu kwao. Wanaweza kufanya kazi kwa pamoja, kutafuta mahali pa kuanzia na kuchukua hatua ya kuimarisha afya. Kwa kawaida katika wilaya kuna shughuli za wadau wa sekta mbalimbali zinazoweza kuleta matokeo chanya katika kuboresha hali ya lishe ya jamii. Lakini utekelezaji wa shughuli hizo unaweza kuwa na ufanisi zaidi iwapo serikali za mitaa zitasaidia kuziimarisha.

Njia mojawapo ya kuhamasisha ushirikiano wa wadau katika utekelezaji wa afua za lishe ni kutumia vyema Kamati za Lishe za Wilaya. Kamati hizi hukutana kila robo mwaka ili kuratibu sekta mbalimbali zinazohusika katika kukabiliana na changamoto za lishe. Kumekuwa na wito wa kuimarisha ufanisi wa kamati hizi ikiwemo kuandaa hadidu za rejea za kamati na mfumo wa kupeana taarifa.

Kwa kuongezea, Maafisa Lishe wa Wilaya wanaweza kuwahusisha maofisa wa sekta nyingine zinazotoa huduma za lishe moja kwa moja kwa walengwa. Maofisa hao wanaweza kujengewa uwezo kupitia ushiriki wao katika warsha shirikishi za wadau wa lishe katika halmashauri.

Mbinu Shirikishi huongeza umoja katika kazi

Mbinu shirikishi huwaleta watu pamoja ili waweze kubadilishana ujuzi na kutatua matatizo. Mbinu shirikishi zinaweza kuimarisha usimamizi wa miradi na kuimarisha umoja. Pia zinaweza kutumika kuanzisha mijadala inayosaidia kuboresha utoaji maamuzi. Nchini

Tanzania, matumizi mbinu shirikishi za mafunzo yamesaidia kujenga uwezo wa watoa huduma wanaofanya kazi kwenye vituo vinavyotoa huduma za afya.

Kama sehemu ya mradi wa Kujenga Mfumo Imara wa Ushirikiano wa Masuala ya Lishe Katika Sekta Mbalimbali, Maafisa Lishe wa Wilaya waliwaalika wajumbe wa Kamati za Lishe za Wilaya kutoka sekta mbalimbali na washiriki wengine kutoka katika mashirika na tasisi zinazotoa huduma ndani ya halmashauri.

“Kwa sababu ya warsha hii, sasa naweza kuona

uwezekano wa watu wa idara ya elimu wanavyoweza kufanya kazi na idara ya maji

katika masuala ya lishe mashuleni.” [Mshiriki wa warsha]

Kwanza, wawezeshaji wa warsha shirikishi waliongoza mjadala kuhusu lishe na changamoto za maendeleo nchini Tanzania. Mada hii iliwaongezea wajumbe wa warsha kiwango cha uelewa kuhusu changamoto za msingi za lishe na mbinu jumuishi za kukabiliana na matatizo ya lishe. Baadae washiriki kutoka sekta mbalimbali walifanya kazi katika vikundi wakishirikishana ujuzi na uzoefu pamoja na kueleza vipaumbele vya lishe katika sekta zao. Kila mmoja alishiriki kujadili changamoto na njia mpya za kufanya kazi kwa kushirikiana na sekta nyingine. Malengo ya Warsha Shirikishi:

• Kushirikisha na elimu ya lishe na kuimarisha uelewa wa uhusiano uliopo baina ya lishe na sekta mbalimbali.

• Kuongeza ufahamu, motisha na kukubalika kwa mfumo shirikishi wa usimamizi wa shughuli za lishe katika sekta mbalimbali.

• Kutambua changamoto na fursa zilizopo katika mipango na utekelezaji wa afua za lishe.

• Kuweka vipaumbele vya lishe kwa pamoja ili kuimarisha ushirikiano baina ya sekta mbalimbali.

4.6 “Kujenga Mifumo Imara ya Usimamizi wa Masuala ya Lishe” Maelezo ya Ushuhuda – Chapisho la 4:

Warsha Shirikishi Yasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya Kuimarisha Mtandao wa Wadau wa Lishe

A

PRIL

I 201

8 |

TAN

ZAN

IA F

OO

D A

ND

NUT

RITIO

N C

ENTR

E

Page 61: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

53

Viongozi wa wilaya walibadilishana maoni kuhusu mbinu za kuimarisha uratibu

Washiriki walilenga: • Kuimarisha mfumo wa mawasiliano baina yao,

kufafanua majukumu na uwajibikaji.

• Kutengeneza fursa ya kufanya mapitio ya miongozo na sera za kitaifa kwa pamoja.

• Kuongeza uelewa na ujuzi wa watendaji wanaotoa

huduma moja kwa moja kwa walengwa kuhusu huduma jumuishi za lishe.

• Kuhamasisha wajumbe wa Kamati za Lishe za

Wilaya kutenga rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa mipango na shughuli jumuishi za lishe.

Warsha shirikishi ilitoa fursa kwa Wakuu wa Idara na viongozi wa jamii kujadili namna ambavyo sekta wanazoziongoza zinaweza kufanya kazi kwa pamoja katika kusaidia utekelezaji wa mkakati jumuishi wa lishe. Wakati wa warsha, Maafisa Lishe wa Wilaya waliweza kuwatambua wadau waliohamasika na kutengeneza mahusiano chanya. Washiriki waliona umuhimu wa kufanya kazi kwa pamoja. Walichunguza njia za kuwezesha sekta zote kushirikiana na Afisa Lishe wa Wilaya katika kuimarisha shughuli na kupanga programu zitakazoweza kuisaidia jamii. Matokeo ya Warsha Shirikishi:

Jitihada endelevu zinahitajika ili kuhakikisha kuwa Maafisa Lishe wa Wilaya wanapata msaada unaohitajika katika kuboresha lishe. Washiriki walisema kuwa, warsha ziliwahamasisha na kuwapa ari mpya ya kujitolea zaidi katika masuala ya lishe. Kwa hiyo matumizi endelevu ya mbinu shirikishi ni njia mojawapo ya kuimarisha mpango jumuishi wa lishe unaozingatia hali halisi ya wilaya. Maafisa Lishe wa Wilaya wanaweza kutumia mbinu shirikishi kuhamasisha wadau wa lishe katika ngazi ya kata na vijiji, ambapo miradi inatekelezwa.

Muhtasari wa mambo muhimu:

► Miongozo ya kitaifa inajumuisha mifano muhimu ya namna ambavyo sekta zinaweza kujumuisha shughuli za lishe katika vipaumbele vyao.

► Wakufunzi Washauri waliwasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya kutoka katika wilaya mbili za majaribio kuongoza warsha shirikishi ya siku moja. Walipitia shuhuda na kujadili njia ambazo washiriki wanaweza kutumia katika kusaidia huduma za lishe katika sekta mbalimbali

► Kupitia warsha shirikisi, Maafisa Lishe wa Wilaya walijiongezea ufahamu kuhusu faida za shughuli za lishe zinazojumuishwa katika sekta mbalimbali.

► Warsha shirikishi ilitoa fursa kwa watendaji wa halmashauri kuwasaidia Maafisa Lishe wa Wilaya kuzishinda changamoto za usimamizi na uratibu wa huduma jumuishi za lishe wilayani.

Kujadili malengo na dhumuni la umuhimu wa kutenga muda na rasilimali katika mipango ya lishe.

Kuongezeka kwa ufahamu wa namna ya kupata na kuitumia miongozo ya kiserikali na mikakati jumuishi ya lishe

Kuimarisha uelewa wa namna ambavyo sekta zinaweza kuongeza malengo na shughuli za lishe katika mipango na vipaumbele vyao.

Kukusanya taarifa zinazofafanua changamoto zilizopo katika kujenga mshikamano wa wadau wa sekta mbalimbali na kutambua vipaumbele vya ushirikiano kwa ajili ya kufanya kazi kwa timu.

“Ni kwa nadra sana huwa tunakaa pamoja na kujadili juu ya afya na maendeleo ya taifa letu.

Muda huu umekuwa wa thamani katika kushirikishana changamoto na mafanikio na nini

kifanyike kuhusiana na masuala ya lishe.” [Mshiriki wa warsha]

Jifunze Jifunze zaidi kuhusu kujengewa uwezo na mbinu nyingine za kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbali mbali zinazo tekeleza afua za lishe katika mwongozo wa kujenga mfumo imara wa Masuala ya Lishe Katika tovuti hii: www. tfnc.go.tz

Imetayarishwa kwa Uhisani wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na mradi huu wasiliana na: Luitfrid Nnally, [email protected] Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dar es Salaam

A

PRIL

I 201

8 |

TAN

ZAN

IA F

OO

D A

ND

NUT

RITIO

N C

ENTR

E

Page 62: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

54

Viambatanisho Kiambatanisho 1.1 Dhana ya Kuboresha Lishe. Chanzo: The Lancet Series on Maternal and Child Nutrition, 2013

FAIDA ZA LISHE BORA KATIKA MZUNGUKO WA MAISHA Magonjwa na

vifo vya watoto

Maendeleo ya ukuaji wa akili, utambuzi na hisia

Ufaulu na uwezo wa kujifunza shuleni

Kimo katika utu uzima Kiribatumbo na magonjwa sugu yasiyoambukizwa

Uwezo wa kufanya kazi na tija

Afua na programu za lishe zinazo lenga kutatua sababu za moja kwa moja za utapiamlo • Afya na lishe ya vijana

balehe na kabla ya kupata ujauzito.

• Milo ya nyongeza kwa wajawazito na wanaonyonyesha

• Utoaji wa vidonge vyenye virutubishi vya nyongeza au uongezaji virutubishi kwenye vyakula

• Milo ya nyongeza kwa watoto

• Ulaji wa vyakula vya mchanganyiko

• Taratibu sahihi za ulishaji na uchangamshi wa watoto

• Matibabu ya utapiamlo mkali

• Kuzuia na kutibu magonjwa

• Afua za lishe wakati wa majanga

Ukuaji na maendeleo mazuri ya mtoto katika tumbo la uzazi wakati wa ujauzito

Ujuzi na ushahidi Siasa na utawala

Uongozi, uwezo na rasilimali fedha Hali ya kijamii, uchumi na mazingira

(Kitaifa na Kimataifa)

Kujena mazingira wezeshi

• Tashmini za kina • Mikakati ya uhamasishaji • Uratibu wa pande zote • Uwajibikaji, motisha,

kanuni na sharia • Mipano ya uongozi • Uwezo wa kuwekeza • Ukusanyaji wa rasilimali za

ndani

Afua na programu za lishe zinazolenga kutatua sababu zilizo fichika za utapiamlo

-Kiilimo na Usalama wa chakula -Hifadhi za kijamii -Makuzi na maendeleo ya mtoto -Afya ya akili kwa wanawake -Uwezeshaji wa wanawake -Ulinzi wa watoto -Elimu ya darasani -Usafi wa maji na mazingira -Afya ya uzazi wa mpango

Usalama wa chakula, ikiwa ni pamoja na uwepo wa chakula, uwezo wa kukinunua na matumizi ya chakula

Rasilimali za kulisha na kutunza familia (wajawazito na wanaonyonyesha, kaya na ngazi ya jamii)

Uwezo wa kupata na kutumia huduma za afya, usafi na usalama wa mazingira

Unyonyeshaji wa maziwa ya mama, vyakula vyenye virutubishi vingi na ratiba ya ulishaji

Taratibu za ulishaji na utunzaji, malezi na uchangamshi

Kupungua kwa magonjwa

Page 63: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

55

Kiambatanisho 1.2. Malengo ya Lishe ya Tanzania ambayo yanatarajiwa kufikiwa mwaka 2021. Mpango wa Lishe unaojumuisha sekta mbalimbali wa mwaka 2016-2021.

Malengo ya Taifa katika kuboresha Lishe ya

Wajawazito na wanawake Wanaonyonyesha, Watoto

Wachanga na Wadogo

1. Kupunguza udumavu miongoni mwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kutoka 34% mpaka 28%

2. Kudhibiti kiwango cha ukondefu chini ya 5% kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

3. Kupunguza tatizo la watoto kuzaliwa wakiwa na uzito pungufu toka 7% mpaka chini ya 5%

4. Kupunguza tatizo la upungufu wa wekundu wa damu kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa kutoka 45% mpaka 33%

5. Kupunguza tatizo la upungufu wa Vitamini A kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 kutoka 33% mpaka 26%

6. Kudhibiti wastani wa kiwango cha madini joto kwenye mkojo kati ya 100-299 μg/L kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa.

7. Kuzuia kuongezeka kwa tatizo la uzito uliozidi na kiriba tumbo kwa watoto na watu wazima.

Page 64: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

56

Kiambatanisho 2.1. Majukumu ya Afisa Lishe wa Wilaya

Majukumu ya Afisa Lishe wa Wilaya kama

Yalivyoainishwa katika Mwongozo wa Mpango wa Mafunzo

ya Maafisa Lishe

1. Kuwa katibu wa Kamati ya Lishe ya Wilaya

2. Kutoa msaada wa kitaalamu na kufuatilia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Utekelezaji wa Shughuli za Lishe

3. Kupokea, kutafsiri na kusambaza sera, mikakati,viwango, sheria, kanuni na miongozo

4. Kukusanya rasilimali fedha na kuhakikisha uwepo wake kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za lishe

5. Kuwashauri Wakurugenzi wa Halmashauri juu ya njia sahihi za kukabiliana na changamoto za kilishe

6. Kuandaa taarifa za lishe na masuala yanayohusiana na lishe kwa ajili ya vikao vya kila mwezi, robo mwaka na mwaka vya Kamati ya Lishe ya Wilaya

7. Kuandaa na kuwasilisha mipango na bajeti za shughuli za lishe kwa Kamati ya Lishe ya Wilaya.

8. Kuanzisha na kuimarisha mfumo wa pamoja wa taarifa za lishe

9. Kusaidia kujumuisha vipaumbele vya lishe katika sera, mikakati na programu.

10. Kutambua na kufanya kazi na wadau wanaotekeleza shughuli zinazohusiana na lishe katika wilaya.

Page 65: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

57

Kiambatanisho 2.2: Mtiririko wa kuwajengea uwezo watendaji katika ngazi ya wilaya

Lengo kuu: Kuboresha hali ya lishe kwa wanawake na watoto

Watendaji wa Wilaya waliojengewa uwezo kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri

Kujenga uhusiano katika:

• Sekta: kilimo, maji, elimu na nyinginezo katika ngazi za mkoa, wilaya, kata, vijiji na jamii

• Wadau: Taasisi za utafiti na vyuo vikuu, serikali, asasi za kiraia, Taasisi Zisizo za Kiserikali na sekta binafsi

• Hupata taarifa • Hujengewa kujiamini na kujifunza stadi mpya • Hupata ufafanuzi kuhusu wajibu wao na

uwajibikaji • Hufanya kazi ya kuainisha wadau waliopo

katika wilaya • Wahamasishaji katika wilaya • Huendesha warsha shirikishi za wadau wa

lishe • Wanaongeza uelewa wa umuhimu wa lishe

katika maendeleo ya wilaya

Mkufunzi Mshauri: • Chanzo cha msaada katika masuala ya lishe mkoani • Ufuatiliaji Saidizi na Wakuu wa Idara • Kamati hai za Lishe katika halmashauri • Ushiriki wa watendaji wanaojengewa uwezo katika mafunzo na fursa

nyingine za kujifunza • Watendaji na wawezeshaji wenye ari ya kucukua hatua

Huongeza uwezo wa: • Kupanga mipango • Kuongoza • Kushirikiana • Kuandaa • Kusaidia • Kufuatilia na kutathimini

afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo katika jamii

Vikwazo vya uwezeshaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri: • Upatikanaji wa muda wa kutosha • Ratiba na majukumu mengine • Uelewa kuhusu na upatikanaji wa miongozo, hadidu za rejea, machapisho,

rasilimali • Msaada kutoka taasisi mbalimbali • Ujuzi wa matumizi ya kompyuta na program muhimu • Uzoefu katika masuala ya sayansi ya jamii na njiambinu za utafiti

Page 66: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

58

Kiambatanisho 2.3: Mfano wa namna ya kutathmini hali halisi katika wilaya na kupanga shughuli

Mbinu ya kujenga uwezo wa watendaji kwa kutumia Mkufunzi Mshauri hufanikiwa zaidi iwapo mkufunzi na walengwa wanapanga lengo kwa pamoja na kushirikiana katika kazi au miradi mbalimbali ili kufikia lengo hilo. Mtiririko ufuatao unaweza kumsaidia Mkufunzi Mshauri na mlengwa wa mafunzo kupanga shughuli zinazoweza kuimarisha uwezo wa mlengwa katika kushirikisha wadau mbalimbali wanaotekeleza mipango na afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo. Mtiririko huu unaweza kutumika kuainisha mada za kujadili na shughuli zinazoweza kufanywa na mlengwa wa mafunzo, idara, taasisi na watendaji wengine wa ngazi za chini zaidi katika jamii. Mtiririko huu unaonesha mifano michache ya mikakati ya kuwajengea uwezo watendaji.

Uchambuzi wa hali halisi (1—3): Mkakati wa kujenga uwezo wa watendaji unaozingatia mahitaji (4—6):

Mab

adili

ko y

a

mtu

bin

afsi 1. Kuna uelewa gani

na je miongozo inapatikana?

• Elimu kuhusu udumavu na hatua zinazochangia kuboresha lishe

• Uelewa wa mpango wa kitaifa wa lishe • Uelewa kuhusu mpango na bajeti ya lishe wa

halmashauri

4. Pitia na jadili miongozo ya kitaifa na ya wilaya, oanisha malengo ya uwezeshaji na mpango wa lishe wa kitaifa.

Mab

adili

ko y

a ki

taas

isi 2. Je kuna kamati

katika wilaya inayounga mkono shughuli hizi?

• Kamati ya lishe katika halmashauri yenye ufanisi

• Ushirikiano kati ya sekta na idara mbalimbali • Uelewa wa majukumu, uwajibikaji na jinsi ya

kutoa mrejesho.

5. Tambua wadau na kuainisha afua / shughuli kuu wanazofanya, jenga uhusiano na tathmini changamoto na fursa zilizopo kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano wa wadau na sekta

mbalimbali.

Uha

mas

ishaj

i jam

ii ka

tika

ngaz

i za

chin

i

3. Je maafisa wa wilaya wana uwezo wa kuifikia jamii?

• Utaratibu wa kutumia mawazo, kutoka ngazi

za chini kwenda ngazi za juu katika mipango ya lishe.

• Wadau wa ndani wanajulikana na kushirikishwa mara kwa mara

• Takwimu za shughuli zinazochangia kuboresha lishe zinakusanywa.

6. Andaa warsha ya wadau waliopo kwa ajili ya kujifunza jinsi ya kutekeleza afua zinazolenga kuboresha lishe zinazotekelezwa na wadau na

sekta mbalimbali.

Page 67: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

59

Kiambatanisho 2.4: Mfano wa mada na maswali ya kujadili wakati wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri

Tumia mifano ya maswali yafutayo kama kigezo cha kupata taarifa na kujua maendeleo. Ili uweze kujadili mada zifuatazo utahitaji kuwatembelea watendaji mara kwa mara. Uliza maswali zaidi kadiri ya mjadala utakavyokuwa wakati wa mazungumzo badala ya kufuata orodha hii ya maswali kama ilivyo. Unaweza kulazimika kurudia mada katika mazungumzo ili kupata taarifa zote muhimu. Ni muhimu kuuliza maswali ya nyongeza yanayotoa mwanya wa kujieleza ili kuelewa mitazamo, uzoefu, malengo ya mtendaji anayewezeshwa. Mpatie mtendaji swali 1 au 2 kabla ya kumtembelea ili aweze kufikiria majibu sahihi kabla ya kujadiliana naye mada hiyo. 1. Dira na malengo la Lishe Taja mambo mazuri na vitu vinavyoendelea vizuri. Taja mapungufu na vitu vinavyohitaji maboresho. Nini kinahitajika ili kuimarisha mfumo unaoshirikisha sekta mbalimbali katika kutekeleza afua za lishe katika wilaya. Kama tungekuwa tumefika mwaka 2025, ungependa mfumo wa lishe uwe vipi? Wewe una ujuzi na ustadi katika maeneo gani? Ainisha malengo 3 na shughuli 3 halisia zinazoweza kufanikishwa ndani ya mwaka ujao. Anza kuandaa mpango kazi wa kufikia malengo yaliyoainishwa

2. Vipaumbele vya lishe katika wilaya Jikite kujua jinsi lishe inavyopewa kipaumbele. Vipaumbele vya lishe katika wilaya ni vipi? Vipaumbele hivi vimewezaje kutambuliwa? Nani alihusika kuvitambua vipaumbele hivyo? Ni Shughuli/kazi zipi zinapata fedha za kutekeleza? Kuna mikakati na mipango kazi ipi kwa ajili ya shughuli zinazohusiana na lishe? Nani anahusika kutengeneza mipango hiyo. Wewe binafsi unashirikishwaje katika kuandaa mpango huo. Nani anatumia mpango huo. Jinsi gani mpango huu au matumizi yake unaweza kuboreshwa.

3. Elimu na uelewa wa lishe Nani ana wajibu wa kutoa elimu ya lishe na kujua matokeo yake. Inatolewaje, takwimu gani zipo au zinaweza kupatikana? Wataalam / maofisa wanajuaje kuwa matatizo yanayohusiana na lishe yapo katika jamii mbalimbali kwenye wilaya yao? Taarifa na elimu ya lishe inatokaje kutoka ngazi ya taifa hadi kufika wilayani na jamii? Ni wapi taarifa na elimu hii haifiki kama inavyostahili? Pitia maneno na misamiati muhimu katika lishe mfano udumavu, afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo. Jadili uelewa wa maneno haya miongoni mwa watendaji wa wilaya.

4. Mpango wa lishe unaojumuisha sekta mbalimbali Mtendaji aliyejengewa uwezo na watendaji wengine wa wilaya wanahusika vipi katika kupanga na kushughulikia matatizo ya utapiamlo? Mchakato wa kupanga bajeti upoje? Kuna ushirikiano wowote kati ya sekta mbalimbali ili kuboresha lishe? Kama wanashirikiana wamefanya hivyo mara ngapi, toa mfano)? Mlengwa angependa kufanya shughuli gani kwa kushirikiana na watendaji wa idara zingine? Mulengwa ana mawasiliano yeyote na watu, taasisi au mashirika anayohitaji kushirikiana nayo? Uliza kuhusu mikutano ya kamati ya lishe ya halmashauri. Je, inafanyika mara ngapi? Nani wanahusika? Je mikutano hiyo ina tija? Nani anaiongoza na kufanya maamuzi, mikutano ya kamati ya lishe inawezaje kuboreshwa? Nini kifanyike ili kuimarisha mahusiano kati ya idara zinazohusiana na lishe.

Page 68: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

60

5. Ushiriki wa Jamii Je mtendaji aliyejengewa uwezo anafanya kazi na wanajamii moja kwa moja katika kutekeleza shughuli yoyote kwa sasa? Je mtendaji anafanya kazi na watoa huduma kama vile asasi za kiraia na wahudumu wa afya ngazi ya jamii? Afua zipi zinazohusiana na lishe zinatekelezwa katika jamii? Huduma za lishe zinawezaje kuifikia jamii vizuri? Fursa gani zipo ili watendaji waliojengewa uwezo wawasaidie watu wa asasi za kiraia, wahudumu wa afya ngazi ya jamii na wafanyakazi wa ugani?

6. Mahusiano na Msaada Kuna mahusiano na msaada gani kwa ajili ya mtendaji aliyejengewa uwezo? Mtendaji aliye jengewa uwezo anaweza kumuendea nani akihitaji ushauri au akiwa na swali? Msaada anaopata unasaidia? Nini cha ziada kinaweza kuwasaidia watendaji waliojengewa uwezo kufanya kazi zao? Jadili fursa ya mtendaji aliye jengewa uwezo ya kuongoza na kufanya maamuzi kuhusu afua za lishe katika sekta mbalimbali. Je, Watu au mashirika hutafuta ushauri kutoka kwa mtendaji aliyejengewa uwezo? Mtendaji aliyejengewa uwezo anajihusisha na shughuli gani? Anafanya kazi na nani kutekeleza shughuli hizo? Angependa kufanya kazi na nani mwingine na kwa nini?

7. Rasilimali na Taarifa Orodhesha taarifa / takwimu na rasilimali zilizopo. Rasilimali hizi zinatumikaje? Nini kingine kinahitajika kufanikisha majukumu na kazi zilizoorodheshwa kwenye Hadidu za rejea za mtendaji aliyejengewa uwezo. Vyanzo vya hizo rasilimali zingine ni vipi? Upatikanaji wa rasilimali hizo unamsaidiaje mtendaji aliyejengewa uwezo kufanya kazi yake?

Page 69: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

61

Kiambatanisho 2.5 Mfano wa fomu ya kurekodi majadiliano wakati wa kuwajengea uwezo watendaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi Mshauri _______________________________________________________________________________ Tathmini kilichojadiliwa wakati uliopita ili kupata pa kuanzia kwa wakati huu. Taarifa za jumla Aliyepo: ……………………..………………………………………………………………………………………………………………………………….

Tarehe: …………………………………………………………………..……………………………………………………………….…………………….

Mahali: …………………………………………………….……………………………………………………………………….……………………….….. Shughuli zilizopangwa na mafanikio yaliyopatikana tangu mkutano wa mwisho

Shughuli zilizofanywa Mafanikio yaliyopatikana

Malengo ya mkutano Malengo ya mkutano huu ili kuendeleza zaidi shughuli zinazopangwa:

1: …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..

2: ……………………………………………………………………………………………………………………………………………….…………………..

3: ……………………………………………………………………………………………………………………………………………….………………….. Mada za kujadili. Mada muhimu zilizojadiliwa:

1: …………………………………………………………………………………………………………………………………….…………………………..

2: …………………………………………………………………………………………………………………………………….…………………………..

3: …………………………………………………………………………………………………………………………………..…………………………….. Changamoto zinazofikiriwa na mikakati kuzikabili

Changamoto Hatua zilizochukuliwa

Page 70: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

62

Hatua za kuchukua Kazi mahsusi kwa mtendaji Kazi mahsusi kwa mkufunzi mshauri

Majukumu mengine Taja matukio yanayotarajiwa mbele, mafunzo, mipango, au majukumu ambayo wanatimu wanatarajia kufanya.

1: ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..

2: ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..

3: …………………………………………………………………………………………………………………………….…………………………………..

Majadiliano yajayo

Tarehe ………………………………..……………….. Muda ………………………………… Mahali………………………….…………. Maelezo: Mkufunzi mshauri Andika mambo yalivyoenda katika mkutano. Je wanatimu walionekana wamerithika, wamehamasika na kushiriki kikamilifu? Wanatimu wanahitaji kufanyia kazi mambo yapi kuwa bora zaidi? Elezea ulivyoiona timu hii na jinsi mkutano ulienda:

Page 71: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

63

Kiambatanisho 2.6 Mwongozo wa kuandika malengo MAKINI

Malengo MAKINI na Hatua za utekelezaji

1. Lengo liwe Mahususi Lengo linapaswa kuwa mahususi na linaloeleweka ili uweze kuelekeza nguvu zako sehemu sahihi na uhamasike kufikia malengo yako. Nahitaji kukamilisha nini? Kwanini lengo hili ni muhimu? Nani anahusika? Lengo hili lipo maeneo gani? Rasilimali zipi zinahitajika na kuna vikwazo au

ugumu gani?

4. Lengo liwe Linaendana na mmajukumu yako:

• Hakikisha lengo linahukuhusu- yaani linahusisana na malengo mengine yanayofanya kila mtu asonge mbele

• Linaonekana kuwa na thamani au linalipa?

• Huu ni muda muafaka? • Mimi ni mtu sahihi kulifikia hili lengo? • Je inawezekana kwa kuzingatia

mazingira ya sasa?

2. Lengo liwe Linapimika: Uwe na malengo yanayopimika ili uweze kufuatilia maendeleo, kukamilisha kwa wakati na uhamasike.

• Kiasi gani, vingapi? • Nitajuaje kama lengo limekamilika

3. Lengo liwe Linawezekana kufikiwa Weka malengo ambayo ni halisia - ambayo yanapanua uwezo wako lakini yawe yanazekana

• Nitalifikaije hili lengo? • Lengo hili ni halisia kwa kiasi gani

ukizingatia changamoto kama vile fedha na muda?

5. Muda wa utekelezaji: Panga shabaha na tarehe za kuzifikia ili kazi za kila siku zisichukuwe kipaumbele cha malengo ya muda mrefu.

• Naweza kufanya nini katika kipindi cha miezi 6 kuanzia sasa?

• Naweza kufanya nini katika kipindi cha wiki sita kuanzia sasa?

• Nini naweza kufanya leo?

Page 72: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

64

Kiambatanisho 2.7 Vidokezo kwa ajili ya Wakufunzi Washauri Wapya Mkufunzi mshauri mzuri anaweza kuongeza kiwango cha umahiri baada ya kufanya kazi hiyo kwa kipindi fulani lakini ufuatao ni mwongozo kwa yule anayeanza. 1. Jitambulishe – Wajue Watendaji unaowajengea uwezo.

2. Chunguza wanapenda nini – uliza maswali, hamasisha majadiliano na mazungumzo kwa kuwashirikisha historia au uzoefu wako.

3. Andaa taarifa – fanya mazungumzo yasiyo rasmi na walengwa unaowajengea uwezo. Pata muda na nafasi kwa ajili ya kujuana nao.

4. Uwe mchangamfu – jibu kwa ufasaha na pia wape taarifa mpya na machapisho au vitendea kazi na fursa za kufanya kazi na watu wengine.

5. Anzisha njia bora za mawasiliano – chagua kipi kinafaa kwenu nyote mapema na kuweka wazi mategemeo katika kila mkutano.

6. Tafuta wakufunzi washauri – Wakufunzi washauri wapya wanaweza kufaidika kutokana na maelekezo ya ziada kutoka kwa wale wenye uzoefu zaidi.

7. Kuwa makini na watendaji unaowajengea uwezo – tatizo au swali ambalo linaonekana la kawaida/dogo linaweza kuwa la muhimu sana kwa walengwa wako.

8. Sikiliza kwa makini na tafuta tatizo halisi – wape watendaji unaowajengea uwezo muda waseme jambo ambalo linaweza kuleta shida au linalokasirisha. Toa muda wa kutosha kusikiliza ili utambue mambo muhimu yatakayojitokeza.

9. Kuwa mkweli na muwazi – waoneshe walengwa wako uwezo nini unaweza au huwezi kuwapa wakati wa kuwajengea uwezo. Eleza upungufu ulioyoona na toa mapendekezo.

10. Msaidie mlengwa unayemjengea uwezo ajenge heshima yake – toa sifa / pongezi na mapendekezo ya kuboresha.

11. Wakaribishe wakufunzi washauri wengine – Elezea kuwa hakuna mtu mmoja anayeweza kukidhi mahitaji ya watendaji wote wanaojengewa uwezo

12. Fanya mikutano ya ana kwa ana – pendekeza mkutano ofisini kwa mtendaji ili afanye kazi katika maeneo yake.

13. Kuwa Mkufunzi Mshauri mwenye busara na anayeaminika – Ni muhimu uwe Mkufunzi Mshauri anayejali na anayepatikana kila anapohitajika. Kwa mfano kuzingatia muda wa mkutano, kuandika kumbukumbu wakati wa mkutano na kurejea hizo kumbukumbu katika mikutano itakayofuata.

14. Usiwe mtoa maagizo kupita kiasi – Toa mapendekezo mbalimbali lakini wape nafasi walengwa wako wachangue. Epuka kuwachagulia au kudhibiti tabia zao.

15. Uwe unakosoa kwa hoja ya kujenga – mrejesho unaolenga kujenga ni muhimu kwa ajili ya kukua na kufanya vizuri zaidi.

16. Sisitiza mrejesho – hakikisha unajua mahitaji ya watendaji unaowajengea uwezo ili uweze kusaidia. Uliza kama mrejesho unatosheleza au unahitajika zaidi.

17. Fanya mazungumzo muda unaofaa – Kama mtendaji anakuja kwako muda ambao haufai, pendekeza muda mwingine badala ya kumsikiliza kwa haraka haraka.

18. Kumbuka lengo – Lengo siyo kumpita/ kumshinda mtendaji anayejengewa uwezo bali kuwapa mwongozo na msaada ili waweza kazi yao. Sisitiza kujiamini, kufikiria wenyewe na kujitosheleza.

Page 73: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

65

Kimbatanisho 3.1 Dodoso la kuainisha wadau wa lishe katika jamii (Imetoholewa kutoka REACH) Kwa ajili ya kutathmini kazi za wadau, walengwa, njia za kutolea huduma, maoni kuhusu mafanikio na ushirikiano. Muonekano na lengo la dodoso Dodoso hili limeandaliwa kupitia mradi uitwao “Kujenga mifumo imara ya lishe” utelekezaji wa sayansi kwa msaada wa Scaling Up Nutrition”, wajumbe wa mradi waliridhia dodoso hili kutoka REACH (Nguvu mpya ya Kupambana na Tatizo la Njaa na Utapiamlo kwa Watoto) – iliyotengenezwa ili kuwatambua wadau wanaohusika katika afua za lishe (www.reach-initiative.org). Takwimu za msingi zilizokusanywa na REACH ni pamoja na kazi zinazofanywa na wadau, walengwa na mbinu wanazotumia kufikisha huduma zao kwa jamii. Dodoso hili linasaidia kuwezesha ukusanyaji wa taarifa muhimu kwa ajili ya maafisa lishe wa halmashauri ili waweze kutambua wadau wanaohusika katika afua za lishe zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo katika ngazi ya jamii. Taarifa zinazopatikana kupitia matumizi ya dodoso hili zinaweza kusaidia kuimarisha ushirikiano wa kisekta katika masuala ya lishe, kuhimiza majadiliano na kujenga uhusiano kati ya Afisa Lishe wa Wilaya na wadau katika jamii. Dodoso linajumuisha maswali yanayotoa mwanya wa kujieleza ili kuchochea majadiliano kuhusu ushirikiano kati ya sekta mbalimbali, changamoto katika kupanga na kutekeleza shughuli za lishe, jinsi ya kuboresha shughuli zinazohusiana na lishe na fursa zilizopo za kushirikiana. Dodoso hili limegawanyika katika maeneo makuu yafuatayo:

• Taarifa binafsi za mdau • Malengo ya mdau • Mfadhili mkuu wa taasisi / shirika la mdau • Ukubwa wa taasisi ya mdau • Shughuli za mdau zinazohusu afya, ukuaji na chakula kinacholiwa na wanawake na watoto • Mafanikio na changamoto za mdau katika kutekeleza kazi zake. • Ushirikiano na wadau wengine. • Fursa ambazo hazitumiki ipasavyo kuboresha lishe.

Dodoso hili la kutambua wadau linaweza kuwaleta pamoja na kusaidia watendaji wa serikali na wadau kuelewa hali ya lishe katika maenao yao. Watendaji wa halmshauri katika idara mbalimali wanaweza kutumia taarifa zitokanazo na matumizi ya dodoso hili kujua nani anafanya NINI na WAPI, pamoja na kujadili uratibu wa rasilimali, shughuli na kuendeleza afua zilizofanikiwa kwenye maeneo mengine. Dodoso hili lilifanyiwa majaribio katika wilaya mbili za Tanzania bara. Kwa hiyo majaribio zaidi yakifanyika dodoso hili linaweza kuboreshwa na litafaa kutumika katika mazingira na program nyingine.

Page 74: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

66

A: TAARIFA BINAFSI ZA MDAU 1. Namba ya usajili wilayani

2. Tarehe ya usaili (siku/mwezi/mwaka) 3. Jina la taasisi/kikundi

4. Aina ya taasisi (tiki moja) a. Asasi za kiraia b. Asasi za dini c. Serikali d. Mashirika yasiyo ya serikali e. Sekta binafsi f. Mengineyo (taja)…………………………………………………………..…………….

5. Makao Makuu ya Taasisi (anwani) 6. Jina mtu aliyefanyiwa usaili/ mahojiano

7. Cheo cha aliyefanyiwa usaili/ mahojiano

8. Namba yake ya simu 9. Anuani yake ya barua pepe

B: MALENGO YA MDAU 1. Lengo Kuu la taasisi ni nini?

(Andika malengo mengi kadiri yanavyotolewa na mdau. Uliza kama kuna kipeperushi, kitini au ripoti ambayo unaweza kupewa ili ukasoma zaidi kuhusu taasisi hiyo baada ya mahojiano).

1a. Lengo la 1: 1b. Lengo la 2: 1c. Lengo la 3:

C: WAFADHILI WA MDAU 1. Vyanzo vya fedha na ufadhili wa

taasisi hii ni wapi? (yote kama inafaa)

a) Fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo (taja)………………………………………… b) Fedha kutoka vyanzo binafsi (taja)……………………………………………………………. c) Fedha za halmashauri/wilaya. d) Michango ya watu binafsi e) Kikundi cha kuwezeshana kiuchumi f) Shughuli au matukio ya kukusanya michango g) Mikopo kutoka benki au taasisi za fedha h) Ada za uanachana i) Mapato ya ndani (shughuli za kuingiza kipato) j) Ada za huduma wanazotoa (mafunzo/shule) k) Kuuza vitu l) Mengineyo (taja)………………………………………………………………………………………

D: UKUBWA WA TAASISI YA MDAU 1. Kuna wafanyakazi wangapi wa kulipwa katika taasisi hii? (Andika majibu)

2. Kuna wafanyakazi wangapi kujitolewa katika taasisi hii? (Andika majibu)

3. Je, mnatekeleza shughuli zenu katika wilaya/mkoa mwingine zaidi ya huu? Mikoa/wilaya zipi?

(Andika majibu)

Page 75: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

67

E: KAZI ZA MDAU 1. Napenda kujua maeneo au mambo ambayo taasisi yako inahusika nayo kwa ujumla. Kwa sasa mnazo shughuli zinazohusiana na __________? (soma orodha kwa sauti na zungushia ndio au hapana kulingana na jibu lililotolewa).

a. Kilimo na Ufugaji 0. Hapana 1. Ndiyo

b. Kuzuia na kutibu magonjwa 0. Hapana 1. Ndiyo c. Shughuli za kiuchumi 0. Hapana 1. Ndiyo

d. Huduma za elimu 0. Hapana 1. Ndiyo

e. Uhifadhi wa mazingira 0. Hapana 1. Ndiyo f. Afya ya uzazi na uzazi wa mpango 0. Hapana 1. Ndiyo g. Afya ya mama mjamzito na anayenyonyesha na

mtoto 0. Hapana 1. Ndiyo

h. Ulinzi na ustawi wa jamii 0. Hapana 1. Ndiyo

i. Maji, usafi wa mazingira na usafi 0. Hapana 1. Ndiyo j. Mengineyo (taja):

………………………………………………………..……………… 0. Hapana 1. Ndiyo

2. Taasisi hii inajihusisha na shughuli gani ambazo zinagusa afya, ukuaji au chakula wanachokula mama, watoto wadogo au makundi mengine maalumu katika wilaya hii? (orodhesha majibu)

a. Shughuli ya 1:

b. Shughuli ya 2:

c. Shughuli ya 3:

d. Shughuli ya 4:

F: FOMU YA KAZI Fomu ya kazi Na: ……………………………………

Jaza fomu hii kwa kila shughuli aliyotaja mdau ambayo inahusiana na afya na ukuaji wa mama na watoto wadogo. Jaza fomu nyingi kadiri unavyohitaji ili kuandika kazi za mdau.

1. Napenda kujifunza zaidi kuhusu kazi hizi kwa undani zaidi. Kwa kuanzia na kazi ya kwanza uliyotaja, naomba uelezee kazi hii na vipengele vyake (Rejea kiambatanisho cha 1 kwa maelezo na mifano ya kazi).

Andika katika kundi la jumla (swali la E1 hapo juu) Mfano: Shughuli za kiuchumi

Andika katika kazi mahususi (swali la E2 hapo juu) Mfano: Kulima mwani kama zao la biashara ili kuboresha kipato cha kaya hivyo kuwa na uwezo wa kununua chakula.

a. SHUGHULI KUU: b. MAELEZO YA SHUGHULI:

2. Malengo ya shughuli hii ni nini? a. Lengo la 1:

b. Lengo la 2:

c. Lengo la 3:

3. Shughuli / kazi hii ilianza lini? (mwezi/mwaka) Mwezi: ……………….. Mwaka: …………………….

4. Shughuli/ kazi hii ina tarehe ya kuisha (tiki kimoja) Ndiyo: …………………. Hapana: ……………..……..

5. Kama ndiyo, kazi hii imepangwa kuisha lini (mwezi/mwaka) Mwezi: ……………….. Mwaka: …………………….

Page 76: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

68

6. Kazi hizi zinatekelezwa katika kata zipi? (Andika majina ya Kata kabla ya mahojiano).

Tafadhali tiki hapana au ndiyo kuonyesha kata ambazo kazi inatekelezwa.

a. 0 Hapana 1 Ndiyo b. 0 Hapana 1 Ndiyo c. 0 Hapana 1 Ndiyo d. 0 Hapana 1 Ndiyo e. 0 Hapana 1 Ndiyo f. 0 Hapana 1 Ndiyo

7. Walengwa wa kazi hii ni nani? (Usisome orodha hii. Tiki yote yatakayotajwa)

1. Kila mtu (hakuna walengwa mahsusi) 2. Kaya 3. Watoto (Taja umri): ………………………………………………………………………………………………………………………………………… 4. Wanafunzi (Taja umri): …….…………………………………………………………………………………………………………………………….. 5. Watu wazima (wanawake) 6. Watu wazima (wanaume) 7. Wanawake walio katika umri wa kuzaa (miaka 15-49). 8. Wanawake wenye watoto wa umri chini ya miaka 5 9. Watoto wa miezi 6-59 wenye ukondefu mkali 10. Watoto wa miezi 6-59 wenye ukondefu wa kadiri 11. Wakulima wadogo 12. Wazee (miaka 60 au zaidi) 13. Watoto yatima 14. Wajane 15. Watu wanaoishi na maambukizi ya VVU 16. Wanawake walioathirika na ukeketaji 17. Watu wenye ulemavu 18. Wengineo (taja): …………………………………………………………………………………………………………………………………..………..

8. Njia gani zinatumika kuwafikia walengwa (Usisome orodha. Tiki yatakayotajwa)

1. Wafanyakazi wa ugani (kilimo, afya, mifugo) Taja: ………………………………………………………………………………………. 2. Wahamasishaji wa mabadiliko katika jamii 3. Wahudumu wa afya ngazi ya jamii 4. Polisi jamii 5. Vituo vya kutolea huduma za afya 6. Shule 7. Taasisi za dini (Makanisa, Misikiti) 8. Vyombo vya habari (radio, magazeti, vipeperushi) 9. Wakala wa mikopo midogomidogo 10. Mashamba ya mfano (shamba darasa) 11. Semina / mafunzo 12. Viongozi wa jamii 13. Mikutano ya wazi / maonesho 14. Vyama vya ushirika vya wakulima 15. Vikundi vya watu (mfano watu wanaoishi na VVU, vikundi vya wanawake) Taja: ……………………………………………. 16. Kutembelea nyumba kwa nyumba 17. Maghala 18. Nyingine (Taja)…………………………………………………………………………………………………………………………………………………..

9. Mnatekeleza shughuli ingine inayogusa ukuaji, afya au vyakula vinavyoliwa na wanawake, watoto wadogo au makundi mengine maalum?

0 = Hapana 1 = Ndiyo

KUMBUKA: Kama mdau ana kazi zingine za kujadili, tafadhali jaza fomu ingine kwa kila kazi husika iliyotajwa.

Page 77: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

69

G. MAFANIKIO, CHANGAMOTO NA USHIRIKIANO

1. Napenda kujua kuhusu utoaji wa huduma katika ngazi ya jamii. Mafanikio gani wewe na taasisi hii umeyaona katika kutekeleza shughuli ulizonieleza. (Dodosa) Kipi kilifanikiwa?

(Andika majibu)

2. Changamoto gani wewe na taasisi hii mmepata wakati wa kupanga na kutekeleza shughuli hizo?

(Andika majibu)

3. Jamii mnazofanya nao kazi zina mtu anayeziwakilisha katika shirika? (Kama ndiyo) wawakilishi hao ni nani na wana cheo gani katika jamii? (Dodosa). Mnawashirikishaje katika kazi zenu?

(Andika majibu)

4a. Mnashirikiana na taasisi au wadau wengine katika kazi ulizonieleza? (Tiki moja)

0 = Hapana 1 = Ndiyo

4b. (Kama ndiyo) Taasisi zipi mnashirikiana nazo moja kwa moja? (Orodhesha jina la kila taasisi.)

1. 2. 3.

4c. Kuna taasisi au mdau mwingine mnajua anafanya kazi kama za kwenu katika wilaya hii ili niongee naye? (Kama ndiyo orodhesha majina ya taasisi.)

1. 2. 3.

5. Sekta gani ya serikali mnafanya nayo kazi moja kwa moja katika kutekeleza kazi ulizonieleza?

Tafadhali nieleze jinsi sekta hiyo imechangia katika shughuli zenu. (Mnafanya kazi na nani?) Wanafanya nini? Mnakutana mara ngapi? Ushirikiano huo una manufaa gani? Nini kinahitaji kuboreshwa?)

a. Kilimo na umwagiliaji O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: b. Habari na mawasiliano O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: c. Maendeleo ya Jamii O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: d. Elimu O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: e. Fedha O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: f. Afya O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: g. Mifugo na uvuvi O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: h. Lishe O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: i. Polisi na Idara ya Sheria O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: j. Sera na Mipango O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: k. Ustawi wa Jamii O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: l. Biashara O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: m. Maji O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu: n. Nyingine (taja) ------------------ O Hapana 1 Ndiyo Andika majibu:

6. Katika wilaya hii kuna ushirikiano kati ya sekta mbalimbali au wataalam ili kuboresha lishe? (kama ndiyo) Unafanyikaje? Nini kinaweza kuboreshwa? (Kama hapana) inawezekana au kuna umuhimu wa kuwa na ushirikiano? Kivipi?

(Andika majibu)

7. Fursa gani unaona ambazo zinaweza kusaidia utoaji wa huduma na elimu ya lishe?

(Andika majibu)

Hapa ni mwisho wa maswali niliyotaka nikuulize kwa leo. Nashukuru sana kwa kukubali kunipa uzoefu wako na muda wako. Nimejifunza mengi. Kuna kitu chochote ungependa kusema au kujadili kabla hatujafunga mazungumzo yetu?

-- Mwisho wa utambuzi wa Wadau --

Page 78: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

70

H. ORODHA YA TATHMINI YA WADAU

1. Taasisi hii inawafikia makundi maalum ambayo yana hatari kubwa ya kupata utapiamlo? O Hapana 1 Ndiyo

2. Malengo ya taasisi hii yanahusika na afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo? (Angalia maelezo na mifano kwenye Kiambatanisho Na. 1)

O Hapana 1 Ndiyo

3. Malengo ya taasisi hii ni mahususi kwa kukabiliana na sababu za wazi za utapiamlo? (Angalia maelezo na mifano kwenye kiambatanisho Na. 1)

O Hapana 1 Ndiyo

4. Taasisi hii inajihusisha na shughuli ambazo zinaongeza au zinaimarisha huduma za lishe? O Hapana 1 Ndiyo

5. Unadhani hii taasisi inafaa kushirikiana nayo?

O Hapana 1 Ndiyo

I: MAONI YA WACHUNGUZI

1. Nini mtazamo na maoni yako kuhusu taasisi hii / mdau huyu? (Andika majibu)

2. Ushirikiano na mdau huyu una manufaa? Kwa nini una manufaa au kwanini hauna maana? Kama ndiyo, mambo gani yanafaa zaidi kushirikiana naye? Kitu gani kinaweza kufanyika baada ya hapa?

(Andika majibu)

Fomu ya Kutambua Wadau – Kiambatanisho cha 1. Nini maana ya afua zinazolenga kukabiliana na sababu za wazi za utapiamlo na afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo?

Afua zinazolenga kukabiliana na sababu za wazi za utapiamlo: Ni zile zinazotekelezwa katika sekta ya afya ambazo zinalenga kukabiliana na vyanzo vya moja kwa moja vya utapiamlo kama vile ulaji duni, na baadhi ya sababu zilizojificha kama vile taratibu za ulishaji wa watoto na uwezo wa kupata chakula.

Afua zinazolenga kukabiliana na sababu zilizojificha za utapiamlo: Ni zile zinazotekelezwa katika sekta mbalimbali zikilenga kutatua sababu zisizo za moja kwa moja za utapiamlo kama vilr kuboresha uhakika wa chakula, kutenga rasilimali za kutosha kwa ajili ya huduma za uzazi, kaya na ngazi ya jamii, na upatikanaji huduma za afya, usafi na usalama wa mazingira na kujumuisha malengo mahususi ya lishe na hatua za kuchukua.

Kundi Baadhi ya mifano ya shughuli zinazohusiana na lishe 1. Kilimo na

ufugaji 1a. Matumizi ya mazao / mifugo yenye virutubishi kwa wingi kwa wakulima au wafugaji wadogo. 1b. Urutubishaji mazao kibailojia. Mfano kilimo cha mazao yaliyoboreshwa kwa kuongeza viwango vya virutubishi kwa njia ya kibaiolojia kama vile mahindi ya njano yenye vitamin A kwa wingi , maharage yenye madini chuma na zinki kwa wingi na viazi vitamu vyenye rangi ya manjano na vitamin A kwa wingi. 1c. Kuchambua mahindi na karanga ili kupunguza sumu kuvu na madhara mengine ya yatokanayo na hifadhi duni ya mazao baada ya kuvunwa. 1d. Mafunzo ya uzalishaji usindikaji na uhifadhi wa chakula.

2. Kuzuia magonjwa na huduma za afya

2a. Huduma ya kinga na tiba ya malaria. 2b. Huduma ya kupunguza maambukizi ya VVU/ UKIMWI, ushauri nasaha na matibabu kwa waathirika. 2c. Dawa za minyoo na za kutibu kuhara.

Page 79: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

71

3. Shughuli za kiuchumi

3a. Uuzaji wa bidhaa zilizolimwa au zilizosindikwa mfano mchanganyiko wa unga wenye protini kwa wingi kwa ajili ya uji wa watoto wadogo. 3b. Shughuli za kuongeza kipato mfano kilimo cha mazao ya biashara (ufugaji wa nyuki, kilimo cha vanila) 3c. Programu za mafunzo ya kazi na ufundi kwa ajili ya kuinua kipato.

4. Program za elimu

4a. Elimu ya lishe ili kuongeza ulaji wa vyakula vyenye virutubishi vinavyozalishwa na jamii. 4b. Kuongeza uelewa wa masuala ya lishe (mfano mashuleni, kliniki, kutembelea jamii katika kaya zao, elimu ya lishe kwa makundi rika) 4c. Kuwaunganisha wakulima katika jamii ili washiriki katika progtamu za huduma ya chakula kwa wanafunzi shuleni na kilimo cha bustani za mboga na matunda shuleni.

5. Uhifadhi wa mazingira

5a. Shughuli za kilimo zinazohifadhi mazingira ili kulinda afya ya udongo na kuongeza uzalishaji wa mazao yenye virutubishi kwa wingi. 5b. Kudhibiti matumizi yasiyo sahihi ya mbolea na dawa za kuuwa wadudu. 5c. Kupanda mimea inayorutubisha ardhi na kuhifadhi mazingira. 5d. Kuhamasisha matumizi ya majiko sanifu yanayookoa nishati na muda.

6. Uzazi wa mpango na afya ya uzazi.

6a. Huduma ya afya ya uzazi na ushauri nasaha. 6b. Uchunguzi wa afya, huduma ya uzazi, afya na lishe wakati wa ujauzito. 6c. Kujumuisha huduma za uzazi wa mpango katika program za lishe mfano wiki ya lishe, siku ya wakulima, na unasihi wa lishe.

7. Afya ya mama na mtoto

7a. Uhamasishaji wa unyonyeshaji maziwa ya mama pekee kwa miezi 6, uelimishaji na vikundi vya kusaidiana. 7b. Uhamasishaji wa ulishaji wa vyakula vya nyongeza, uelimishaji na vikundi vya kusaidiana. 7c. Kuzuia na kutibu utapiamlo. 7d. Uongezaji wa virutubishi kwenye vyakula na utoaji wa virutubishi vya nyongeza kwa makundi maalum.

8. Ustawi na ulinzi wa jamii

8a. Msaada wa kisheria, hatua za udhibiti na ulinzi kwa makundi maalumu. 8b. Program za kutoa ushauri kuhusu ukatili wa kijinsia. 8c. upatikanaji wa elimu na vifaa vya shule.

9. Upatikanaji na usafi wa maji. Mazingira, mwili na chakula (WASH)

9a. Kujenga au kuboresha mifumo ya huduma ya maji. 9b. Elimu ya kunawa mikono kwa maji na sabuni na kuzingatia nyakati muhimu za kunawa mikono. 9c. Taratibu za usafi na usalama wa chakula. 9d. Kuboresha taratibu za usafi wa mazingira mfano kufuga wanyama mbali na maeneo ya kuandalia chakula na mahali wanapocheza watoto. 9e. Kuboresha uhifadhi na utupaji taka ngumu. 9f. Uthibiti wa wadudu wanaoeneza magonjwa mfano inzi, mbu, mende na panya. 9g. Kuboresha miundombinu ya kuondoa maji ya mvua na utupaji salama wa vitu visivyotumika tena katika mashino yaliyofunikwa.

Page 80: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

72

Kiambatanisho 3.2 : Mfano wa kanzidata ya kutambua wadau iliyoridhiwa kutoka REACH

Mfano wa vipengele vya kufuatilia kazi ya kwanza ya mdau iliyotambuliwa. Kazi ya kwanza:

Utangulizi Kazi ya kwanza:

Malengo Kazi ya kwanza: Mahali/ kata inayotekeleza

kazi hiyo Kazi ya kwanza: Walengwa

Maelezo na vipengele vya kazi (Andika majibu)

Lengo la kazi ya 1 (Andika majibu)

Lengo la kazi ya 2 (Andika majibu)

Lengo la kazi ya 3 (Andika majibu)

Kata ya 1 Hapana =0 Ndiyo =1

Kata ya 2 Hapana =0 Ndiyo =1

Kata ya 3 Hapana =0 Ndiyo =1

Jumla ya walengwa Hapana =0 Ndiyo =1

Wanafunzi miaka 5-18 Hapana =0 Ndiyo =1

Watoto yatima Hapana =0 Ndiyo =1

Elimu ya VVU na Ukimwi shuleni na makundi rika

Kuongeza uelewa wa vijana kuhusu masuala ya VVU na UKIMWI.

Kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa vijana

Inalenga shule za msingi 59 na sekondari 19

1 0 1 0 1 0

Mfano wa kazi za wadau katika sekta mbalimbali Shughuli za Wadau

Kilimo USAFI Ustawi wa Jamii Udhibiti wa Magonjwa

Jina

la M

dau

Kilim

o ch

a M

atun

da

na m

boga

mbo

ga

Ufu

gaji

wa

mifu

go

Kilim

o ch

a bu

stan

i sh

ulen

i

Upa

ndaj

i kti

na

hifa

dhi y

a m

azin

gira

Elim

u ya

una

waj

i m

ikon

o na

usa

fi

Uvu

naji

maj

i ya

mvu

a

Mik

opo

mid

ogo

mid

ogo

Upa

tikan

aji w

a el

imu

na v

ifaa

vya

elim

u

Uka

tili w

a ki

jinsi

a

Daw

a za

kut

ibu

maa

mbu

kizi

ya

min

yoo

Prog

ram

u za

VVU

na

UKI

MW

I

Mat

ibab

u ya

kuh

ara

kwa

kutu

mia

ORS

1 x x 2 x x 3 x 4 x x x x 5 x x x 6 x x x 7 x

Page 81: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

73

Kiambatanisho 3.3: Mfano wa Jedwali la Utambuzi wa Wadau ambalo limeshajazwa

Shughuli mahususi Idadi ya Taasisi

Idadi ya Kata

Walengwa Mifumo/njia ya kutoa huduma

Ulishaji wa watoto

Vikundi vya kusaidia unyonyeshaji

2 10 Wanawake walio katika umri wa kuzaa (miaka 15-49)

Vikundi vya wanawake

Usindikaji na uhifadhi wa vyakula vya watoto.

2 4 Jamii yote Misikiti, makanisa, semina, vyama vya ushirika vya wakulima, mikutano katika jamii

Lishe

Utoaji wa vyakula vyenye rirutubishi kwa wingi.

5 17 Watoto na vijana balehe (miaka 0-18) msisitizo kwa watoto yatima na wenye maambukizi ya VVU, wazee.

Misikiti, makanisa, semina, vyama vya ushirika vya wakulima, mikutano katika jamii

Elimu ya lishe 3 17 Watu walioambukizwa VVU/ wenye UKIMWI, wanafunzi (miaka 5-18) wajane.

Shule, vikundi maalum

Kuzuia na kutibu magonjwa

Dawa za minyoo

2 3 Wanafuzi (miaka 5-18) Wanafunzi

Elimu ya VVU/UKIMWI, ushauri nasaha na upimaji

5 17 Wanafunzi / miaka (5-18), yatima, wajane, watoto wenye VVU / UKIMWI.

Makanisa, Misikiti, shule, semina, vikundi vya msaada, vyombo vya habari

Shughuli/taratibu za kilimo

Bustani za mboga katika kaya au shule

5 17 Wanafunzi (miaka 5-18) kwa kuwalenga watoto na wanawake walio katika mazingira magumu.

Shule, vyama vya ushirika vya wakulima, makanisa, misikiti, mikutano katika jamii

Ufugaji (kuku, mbuzi) 3 5 Makundi yasiyopewa kipaumbele, wanafunzi, jamii zinazoweza kuzalisha zaidi.

Shule, vyama vya ushirika vya wakulima, makanisa, misikiti, mikutano katika jamii

Upatikanaji na usafi wa maji na mazingira.

Elimu ya kunawa mikono.

12 13 Wanafunzi miaka (5-18) kwa kuwalenga watoto walio katika mazingra magumu, watu wenye VVU/UKIMWI, yatima, wajane na walemavu.

Shule, semina mikutano ya hadhara, vyombo vya habari, makanisa, misikiti, kutembelea kaya kwa kaya, wahamasishaji mabadiliko katika jamii.

Uvunaji wa maji ya mvua.

1 3 Wanafunzi miaka (5-18) kwa kuwalenga watoto walio katika mazingra magumu, watu wenye VVU/UKIMWI, yatima, wajane na walemavu.

Shule, semina mikutano ya hadhara, vyombo vya habari, makanisa, misikiti, kutembelea kaya kwa kaya, wahamasishaji mabadiliko katika jamii.

Afya na uzazi wa mpango

Huduma za msingi za afya na upimaji.

4 17 Watoto na vijana balehe (Miaka 0-18), wanawake, watu wenye VVU/UKIMWI, yatima na wazee.

Shule, semina, vikundi vya kusaidiana, viongozi, mikutano ya hadhara.

Uzazi wa mpango 1 15 Wanawake walio katika umri wa kuzaa (miaka 15-49), wanawake wenye VVU/UKIMWI.

Kutembelea kaya kwa kaya makanisa, misikiti.

Ustawi wa jamii na ulinzi.

Haki na msaada wa kisheria

4 17 Watu wenye VVU/UKIMWI, yatima, wajane, walemavu.

Kutembelea kaya kwa kaya, shule, makanisa, misikiti, mikutano ya hadhara, vikundi vya kusaidiana, vyombo vya habari wahamasishaji mabadiliko wa jamii.

Program zamikopo midogo midogo.

2 8 Jamii yote na kwa kuwalenga zaidi watu makundi yasiyopewa kipaumbele.

Vyama vya ushirika vya wakulima, wakala wa mikopo midogo midogo, mashamba darasa, kutembelea kaya kwa kaya, shule, makanisa, misikiti, vyombo vya habari, mikuktano ya hadhara, wahamasishaji mabadiliko wa jamii.

Page 82: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

74

Kiambatanisho 4.1: Mbinu za kuwezesha Warsha Shirikishji

Mbinu Shirikishi za Uwezeshaji

Andika mawazo ya washiriki

Waambie washiriki waandike mawazo yao kwenye chati pindu au karatasi za kuandikia zilizopo ukutani. Hii inasaidia kila mshiriki kujenga tabia ya kufikiri wakati wote wa warsha. Inasaidia pia kupitia na kuboresha mawazo yaliyotolewa mwanzo. Baada ya warsha, wawezeshaji wanaweza kukusanya chati pindu ili kupata mawazo yote yaliyotolewa.

Fanya kazi kwa vikundi vya ukubwa tofauti.

Wezesha majadiliano na kujifunza kupitia vikundi vidogo vidogo. Jumuisha washiriki wenye taaluma mbalimbali katika kila kikundi. Vikundi vya watu 5 au pungufu huongeza ufanisi wa kupata mawazo mbalimbali. Hata hivyo kama zoezi linahitaji washiriki waeleze uzoefu kwa kina, kufanya kazi kwa jozi (watu wawili) huwawezesha wote kuongea na kusikilizana. Badilisha vikundi vidogo vidogo kila wakati kwa siku ili kuhakikisha kuwa kila mtu anapata fursa ya kufanya kazi na washiriki tofauti.

Toa mrejesho Vikundi vidogo vidogo viwasilishe mrejesho wa kazi zao mbele ya washiriki wote ili kupata mawazo mazuri yaliyotolewa. Tenga muda wa kila kundi kuwasilisha ili kuepuka upotevu wa muda. Vinginevyo vikundi vichache vinaweza kuwasilisha halafu washiriki wengine waongezee mambo ambayo hayajasemwa kabisa.

Tumia uandishi wa kufikiria.

Tumia uandishi wa kufikiria kuwafanya washiriki wafikiri kuhusu mada zilizojadiliwa kwenye warsha. Kufikiria ni kusema kufafanua kwa mapana mada zilizojadiliwa na siyo kutoa maelezo. Zoezi hili linaweza kuonyesha upungufu, uzuri na mafanikio katika mada zilizojadiliwa. Uandishi wa kufikiria unaweza pia kuwasaidia washiriki kuweka mawazo yao vizuri kabla ya kutoa mrejesho kwa washiriki wote.

Wasilisha visa mkasa

Wape washiriki nafasi wachunguze kisa mkasa kuhusu uzoefu unaohusiana na mipango na utekelezaji wa shughuli za lishe katika sekta mbalimbali. Visa mkasa huelezea mtu, taasisi, tukio au hatua za kuchukua katika muda au mahali maalum. Vinaweza kusaidia kuleta mawazo na majadiliano. Chagua kisa chyenye mvuto, ambacho si cha kawaida, kinachoonyesha uzoefu au hali ya mazingira halisi.

Page 83: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

75

Kiambatanisho 4.2: Mfano wa Ratiba ya Warsha Shirikishi kutoka Mradi wa Kujenga Mifumo imara ya Lishe Tanzania

8.30-9.00

Kujiandikisha

9.00-9.10 MAKARIBISHO NA NENO LA UFUNGUZI WA WARSHA —Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri

9.10-9.30 Utambulisho wa washirika, matarajio, malengo na kanuni za warsha

9:30-10:30 Somo la 1: Utangulizi – Hadithi ya msukumo katika masuala ya lishe (Jinsi ya kufanya: Mapitio katika kundi rika, Simulizi na majadiliano)

• Madhara ya utapiamlo na hatua za kuchukuwa katika sekta mabalimbali. • Mpango wa Taifa wa Lishe wa miaka mitano • Changamoto na fursa za kushirikiana na sekta zote • Faida ya kujumuisha vipaumbele vya lishe katika sekta zingine.

10.30-10.45 Mapumziko na Kifungua Kinywa

10.45-12.45 Somo la 2: Kujifunza kwa pamoja changamoto na fursa za ushirikiano katika sekta mbalimbali (Jinsi ya kufanya: Bungua bongo, kazi za vikundi vidogo, kufikiri kwa kina katika kikundi)

• Vipaumbele vya sekta mbalimbali na uhusiano wake na masuala ya lishe • Changamoto na fursa za ushirikiano baina ya sekta mbalimbali • Faida ya kujumuisha vipaumbele vya lishe katika sekta zingine.

1.00-2.00 CHAKULA CHA MCHANA KWA WWASHIRIKI WA WARSHA SHIRIKISHI

2.00-3.30 Somo la 3: Fursa za kuimarisha huduma za lishe katika sekta mbalimbali (Jinsi ya kufanya: Bungua bongo na mjadala wa mabishano katika kundi kubwa)

• Kuandaa mikakati na jinsi ya kufanya kazi kwa ushirikiano • Kujadili na kujaribu kazi zinazoweza kutekelezwa kwa ushirikiano ili kutaa tatizo mahsusi • Kuorodhesha vipaumble vinavyolenga vipaumbele vinavyofanana vya wadau wa sekta

mbalimbali, hatua za kuchukua, na majukumu

3.30-3.50 Session 4: Workshop Conclusion (Approach: Next steps and feedback)

• Decide how to bring workshop learnings and plans to attention at the grassroots, district, and regional levels

• Workshop lessons learned, evaluation, and feedback for facilitators

Somo la 4 makubaliano ya warsha (Jinsi ya kufanya: Mambo ya kutekeleza na mrejesho baada ya warsha)

• Kuamua jinsi ya kupeleka mapendekezo na mafundisho yaliyopatikana katika warsha kwa wadau wengine katika ngazi ya jamii, wilaya na mkoa.

• Majumuisho ya warsha: mafundisho makuu yaliyopatikana, tathmini ya ufanisi wa warsha na mrejesho kwa wawezeshaji.

3.50-4.00 UFUNGAJI WA WARSHA—Mganga Mkuu wa Wilaya

4.00-4.15 Viburudisho

Page 84: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

76

Kiambatanisho 4.3: Mapendekezo ya vitabu na machapisho ya rejea kwa ajili taarifa za ziada

Tanzania

Tanzania National Multi-sectoral Nutrition Action Plan (NMNAP) – From Evidence to Policy to Action. United Republic of Tanzania (2016). http://docs.scalingupnutrition.org/wp-content/uploads/2017/09/NMNAP_Tanzania.pdf

Mpango wa taifa wa Lishe (2016-2021) ni mpango wenye uthibitisho na unaohusu sekta mbalimbali, unaolenga kupunguza viwango vya vya utapiamlo wa aina zote nchini Tanzania. Lengo Kuu la mpango wa Taifa wa lishe ni kupunguza udumavu kutoka 34% mpaka 28% itakapofika mwaka 2021, ambayo ni hatua muhimu kuelekea kufikia malengo ya MKUKUTA 20/25 na malengo ya lishe ya Baraza la Afya Duniani.

The 2015-16 Tanzania Demographic and Health Survey and Malaria Indicator Survey (2015-16) https://dhsprogram.com/publications/publication-FR321-DHS-Final-Reports.cfm

Ripoti ya Takwimu za afya na demografia ya watu ikiwa ni pamoja na taarifa mpya na kuaminika kuhusu viashiria vya demografia na afya kuhusu uzazi wa mpango, kasi ya uzazi, vifo vya wanawake, vifo vya watoto wachanga na wadogo, hali ya lishe ya watoto na wanawake, huduma kwa wanawake wajauzito, huduma za kujifungua, chanjo na magonjwa kwa watoto.

Guidelines for Councils on the Preparation of Plan and Budget for Nutrition – 2nd edition. Prime Minister’s Office, Tanzania (2012). 3rd edition coming soon.

Mwongozo huu umeandaliwa ili kusaidia halmashauri/wilaya kuainisha shughuli/afua za kujumuisha katika mipango na bajeti za mwaka ili kukabiliana na tatizo la utapiamlo. Kwa kuwa kuna sababu nyingi za utapiamlo, inabidi hatua zichukuliwe katika sekta zote ili kuhakikisha kujenga mazingira wezeshi ya kuboresha lishe. Hatua za kuboresha lishe zinajumuishwa katika sekta za afya, kilimo, maendeleo ya jamii, elimu, maji, mipango na fedha.

Nutrition Assessment, Counseling, and Support (NACS) Training Package for Facility-Based Service Providers. TFNC and FANTA (2011). https://www.fantaproject.org/tools/tanzania-nutrition-assessment-counseling-and-support-nacs-training-package-facility-based

Kitita cha mafunzo ya Tathmini Unasihi na Msaada wa Lishe kimeandaliwa kwa ajili ya kufundisha watendaji katika vituo vya kutolea huduma za afya kulingana na viwango vinavyokubalika duniani. Kitita hiki kinaashiria jitihada za Serikali ya Tanzania katika kujumuisha huduma bora za lishe kwenye taratibu za kila siku za utoaji huduma za afya na matibabu.

Nutrition Assessment, Counseling, and Support (NACS) Tools. TFNC and FANTA (2011). https://www.fantaproject.org/tools/tanzania-nutrition-assessment-counseling-and-support-nacs-tools

Vitendea kazi hivi vinatoa taarifa zinazohitajika kwa ajili ya kupanga mipango, kutekeleza, kufuatilia na kutoa taarifa kuhusu ujumuishwaji wa huduma bora za lishe katika utoaji wa huduma za afya kila siku. Vitendea kazi hivi ni pamoja na kitabu cha rejea, vitini vya kufundishia, mwongozo wa utekelezaji na fomu za aina mbalimbali kwa ajili ya matibabu ya utapiamlo na huduma ya chakula dawa.

Rejea za machapisho yanayohusu mikakati ya kukabiliana na sababu zilizo fichika za utapiamlo WASH and Nutrition Guidebook. ACF (2017). http://nutritioncluster.net/wash-nutrition-guidebook-acf-2017/

Kitabu kinachoonesha uhitaji wa mwongozo wa kivitendo kuhusu afya na usafi wa mazingira na kujumuisha lishe katika ngazi za kiutendaji. Kinaweza pia kutumia kama kitendea kazi kwa ajili ya wafadhili na taasisi (kama vile Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto) katika kutoa kipaumbele kwa mikakati na uwekezaji kupitia rasilimali fedha.

Compendium of Actions for Nutrition (CAN). REACH, UN Network for SUN (2016). http://www.reachpartnership.org/compendium-of-actions-for-nutrition

Hili ni andiko linalojumuisha mazingira ya hatua za kuboresha lishe katika sekta zote na kuelewa kwa upana hatua zinazohitajika kukabiliana na utapiamlo, kuwezesha majadiliano na sekta mbalimbali na kuongeza kasi ya utekelezaji wa shughuli zinazohusiana na sera na mipango ya lishe. Walengwa wa chapisho hili ni wadau wote wanaohusika na michakato ya kimamlaka na uratibu wa afua za lishe katika sekta mbalimbali.

Page 85: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

77

The Contribution of Agriculture and Social Protection to Improving Nutrition. SUN Movement Secretariat (2015). http://docs.scalingupnutrition.org/wp-content/uploads/2015/09/SUN-IN-PRACTICE-4-SOCIAL-PROTECTION-ENGLISH.pdf

Muhtasari mfupi wa jinsi kilimo na mfumo wa uwezeshaji wa kaya masikini unavyoweza kuchangia kuimarisha huduma za lishe katika nchi zinazotekeleza mpango wa kuongeza msukumu kwa masuala ya lishe (SUN) duniani kwa kuangalia visa mkasa kutoka nchi sita. Hatua za kuchukuwa na mambo ya kujifunza yamewasilishwa kwa muhtasari. Chapisho hili ni muhtasari wa nne katika mfululizo wa machapisho ya utekelezaji wa SUN.

Scaling Up Nutrition (SUN) – A Framework for Action. SUN (2011). http://scalingupnutrition.org/wp-content/uploads/pdf/SUN_Framework.pdf

Muhtasari huu wa kisera una madhumuni mawili ya msingi: kuto a mwongozo wa mambo muhimu ya kuwekewa mkazo, kanuni na vipaumbele kwa ajili ya hatua za kukabiliana na utapiamlo, na kuhamasisha upatikanaji wa msaada ili kuongeza uwekezaji kwa ajili ya utekelezaji wa afua za lishe katika sekta mbalimbali. Walengwa wa andiko hili ni watunga sera na viongozi wanaotoa maamuzi.

Rejea za machapisho yanayohusu mikakati ya kukabiliana na sababu za wazi za utapiamlo

Essential Nutrition Actions: Improving maternal, newborn, and infant and young child health and nutrition. WHO (2013). http://apps.who.int/iris/bitstream/10665/84409/1/9789241505550_eng.pdf?ua=1

Muhtasari wa muongozo wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu afua za lishe zinazolenga siku 1000 za maisha ya mtoto. Kwa kuzingatia kitita cha afua muhimu za lishe, watunga sera wanaweza kupunguza vifo vya watoto wadogo, kuboresha ukuaji kimwili na kiakili hivyo kuongeza tija.

The Community Infant and Young Child Feeding (IYCF) Counselling Package. UNICEF (2012). https://www.unicef.org/nutrition/index_58362.html

Machapisho yaliyoandaliwa kumwezesha mhudumu wa jamii kuhamasisha mabadilko ya tabia na kuwasaidia wazazi au walezi wengine kulisha watoto wao ipasavyo. Machapisho haya ni pamoja na mwongozo wa mipango, mwongozo wa kuridhia machapisho, mwongozo wa mkufunzi, vitendea kazi vya mafunzo, kitabu cha mshiriki, kadi za unasihi kwa ajili ya mtoa huduma wa jamii, kitabu cha ujumbe muhimu, vipeperushi vya aina mbalimbali, moduli ya ufuatiliaji saidizi na tathmini.

Rejea za machapisho yanayohusu Ufuatiliaji saidizi na kujengea uwezo watendaji kwa kutumia wakufunzi washauri Training Supervisors to Mentor Health Workers Who Provide Counselling on IYCF. SPRING/Kyrgyz Republic (2017). https://www.spring-nutrition.org/publications/training-materials/training-supervisors-mentor-health-workers-who-provide-counselling

Mwongozo huu humpatia mwezeshaji utaalamu na stadi anazohitaji ili kuwasaidia wasimamizi wawezeshe watoa huduma wa afya wanaotoa unasihi wa ulishaji wa watoto wachanga na wadogo. Ingawa mafunzo haya yanalenga ulishaji wa watoto, stadi za kuwawezesha watoa huduma zinaweza kutumika katika mambo mengine mbalimbali.

Supportive Supervision/Mentoring and Monitoring for Community IYCF. UNICEF (2013). https://www.unicef.org/nutrition/files/Supervision_mentoring_monitoring_module_Oct_2013(1).pdf

Muongozo huu unajenga stadi za msimamizi aweze kufuatilia utendaji wa wahudumu katika ngazi ya jamii na kusaidia kuimarisha utendaji wao kama kuna upungufu. Mafunzo yamepangwa katika malengo 7 ya kujifunza ikiwa ni pamoja na utangulizi wa dhana ya ufuatiliaji au usimamizi saidizi, mifano ya vitendea kazi na fomu za ufuatiliaji, fursa za kujaribu stadi ambazo ni muhimu na vitendea kazi vya kuandaa mpango kazi kwa kuzingatia hali halisi ya eneo husika.

A Manual for Comprehensive Supportive Supervision and Mentoring on HIV and AIDS Health Services. Ministry of Health and Social Welfare, United Republic of Tanzania (2010). https://www.jica.go.jp/project/tanzania/001/materials/pdf/common_03_01.pdf

Kitita kinachambua hali ya usimamizi saidizi na uwezeshwaji katika huduma za VVU/UKIMWI na jinsi ya kuandaa jaribio la awali. Kitita hiki kimeambatana na vitendea kazi sahihi kwa ajili ya mameneja, watu wanaopanga miradi, watekelezaji na mifumo ya watathimini wa usimamizi saidizi na wakufunzi wanaowajengea uwezo watendaji.

Page 86: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

78

Kiambatanisho 4.4. Mfano wa Fomu ya Tathmini ya Warsha Shirikishi Tarehe na Mahali: __________________________________________________________________ Kazi yako: _________________________________________________________________________ Muda uliotumikia cheo/nafasi uliyopo: _________________________________________________ Maelekezo: Tafadhali weka mduara katika majibu yako kwa sentensi zilizopo hapa chini. Thaminisha majibu yako kwa namba 1 mpaka 6.

Swali

Siku

bali

kabi

sa

Sisk

ubal

i

Siku

bali

kido

go

Nak

ubal

i ki

dogo

Nak

ubal

i

Siku

bali

kabi

sa

1. Malengo ya warsha yameeleweka 1 2 3 4 5 6 2. Warsha imeandaliwa kwa namna ambayo

washiriki wameweza kubadilisha mawazo na uzoefu.

3. Shughuli zilizofanyika kwenye warsha zimenifanya nishiriki kikamilifu kujifunza na kuamsha uwezo wangu wa kufikiri.

1 2 3 4 5 6

4. Mategemeo yangu kwa warsha hii yamefikiwa. 1 2 3 4 5 6 5. Mambo yaliyofanyika katika warsha hii

yanahusiana na kazi yangu. 1 2 3 4 5 6

6. Majadiliano na shughuli za warsha hii zimenihamasisha kuongeza ushiriki wangu na uwajibikaji kwenye masuala ya lishe.

1 2 3 4 5 6

7. Masomo/mada za warsha zimewasilishwa vizuri. 1 2 3 4 5 6 8. Mpangilio wa warsha hii ulikuwa njia nzuri

kwangu kujifunza zaidi jinsi ya kujumuisha lishe katika sekta zingine.

1 2 3 4 5 6

9. Nafikiri nimeweza kusikika na kueleza mawazo yangu kupitia warsha. hii

1 2 3 4 5 6

Maswali ya majibu mafupi 1. Mada gani zilikuwa na umuhimu mdogo sana kwako? Na kwa nini? 2. Mada zipi zilikuwa za muhimu mkubwa sana kwako? Na kwa nini? 3. Ushauri gani unatoa ili kuboresha warsha kama hii? 4. Shughuli gani ambazo zinahusiana na lishe wewe unahusika nazo? 5. Jinsi gani warsha hii imebadili mawazo yako kuhusu kusaidia na kuimarisha mfumo wa ushirikiano

wa sekta zote katika wilaya katika kutekeleza masuala ya lishe? 6. Kitu gani umejifunza katika warsha hii ambacho kimekufurahisha sana? Ni kwa jinsi gani utatumia

mambo uliyojifunza kutoka katika warsha hii? 7. Kwa kuzingatia ushirikiano wako na watu wengine katika warsha hii, kuna mtu umepanga kuendelea

kuwasiliana naye? Je ni nani na kwa nini? 8. Una maoni gani mengine kuhusu warsha hii?

Page 87: KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA ......ii KUJENGA MFUMO IMARA WA USHIRIKIANO WA MASUALA YA LISHE KATIKA SEKTA MBALIMBALI: Mwongozo wa Kuimarisha Uwezo wa Halmashauri Katika Kupanga

79

Kiambatanisho 4.5 Mfano wa mambo ya kujifunza katika Warsha Shirikishi ya Wadau wa Lishe: Kutoka mradi wa “Kujenga mfumo imara wa usimamizi wa huduma za Lishe”

Malengo Changamoto kuu Njia zinazoweza kusaidia

Uongozi wenye msaada na wa kuaminika.

• Kukosa uongozi kamili au uliothibitishwa huzuia uwezo wa kupanga na kukamilisha ajenda za lishe katika sekta mbalimbali.

• Kutoa mafunzo na msaada kwa watumishi wapya na wale waliopo kwenye nafasi muhimu ili kuwepo na mwendelezo.

• Wajumbe wanahudhuria mikutano ya kamati za lishe wanabadilika mara kwa mara. Wajumbe halisi huwatuma wawakilishi wasiokuwa na mamlaka ya kutoa maamuzi.

• Kutofautisha mpango / bajeti na utekelezaji wa kuanzisha timu za kusaidia vyote viwili.

• Mategemeo makubwa yamewekwa kwa Maafisa Lishe wa Wilaya ambao hawajawezeshwa vya kutosha kuongoza afua ya lishe katika wilaya nzima.

• Kuongeza usaidizi au kujengewa uwezo na fursa kwa afisa lishe aweze kushirikiana na sekta zote.

Uhusiano thabiti na malengo ya pamoja.

• Ushirikiano mdogo kati ya idara mbalimbali hupunguza nguvu za pamoja katika masuala ya lishe.

• Kuongeza fursa za kujua vipaumbele vya sekta zote na faida za masuala ya lishe kwa wote.

• Uhusiano dhaifu kati ya Afisa Lishe wa Wilaya na Waratibu wa Lishe waliopo kwenye idara mbalimbali.

• Kuvunja vikwazo na kufanya bidii kujenga mahusiano mapya.

Elimu ya lishe na mbinu za kutumia.

• Uelewa mdogo wa utapiamlo na athari zake nchini Tanzania, mikakati ya kuongoza mipango na hatua za kuchukua.

• Kuumia warsha shirikishi na mapitio ya pamoja kujadili miongozo, takwimu, mambo mapya, mafanikio, na kuweka vipaumbela vya kufanyia kazi.

Rasilimali za uhakika na uratibu au usimamizi.

• Uhamasishaji na utetezi hafifu, kutotengwa rasilimali za kutosha kwa ajili ya masuala ya lishe katika idara zingine.

• Kuonyesha mchango wa afua zinazosaidia kuboresha lishe, uwepo wa mwongozo wa kuridhisha kwenye mikutano ya halmashauri / wilaya.

• Kukosa njia/namna ya kushirikishana takwimu na taarifa kati ya idara na wadau.

• Kujenga uwezo wa kupeana taarifa (mfano kanzidata, warsha, na mihutasari ya miongozo, mikakati na sera) na kutafsiri elimu, taarifa mpya kwa kuzingatia afua za lishe katika sekta mbalimbali.

Uwezo wa kuhudumia jamii

• Kutokujua afua za lishe zinazotekelezwa katika jamii na kukoosa ushirikiano na asasi za kiraia.

• Kuainisha wadau ili kuongeza ushirikiano na kuimarisha miradi/program.

Mipango Aprili 2018

Jifunze Jifunze zaidi kuhusu kujengewa uwezo na mbinu nyingine za

Aprili 2018 TANZ

Janu

i

Aprili 2018 TANZ

Kujenga uhusiano katika:

• Sekta: kilimo,

Vikwazo vya uwezeshaji kwa kutumia mbinu ya Mkufunzi

Huongeza uwezo wa:

• Kupanga mipango

• Kuongoza

Mkufunzi Mshauri:

• Chanzo cha

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na mradi huu wasiliana na: Luitfrid Nnally

Mipango

I Kwa maelezo zaidi kuhusiana na mradi huu wasiliana na: Luitfrid Nnally

Mipango