toleo la 20 january—march banana investments ltd · ckht huandaa mafunzo ya awali, “orientation...

8
HALIUZWI Toleo la 20 January—March TOLEO NAMBA 20 HALIUZWI JANUARY— MARCH Banana Investments Ltd.

Upload: others

Post on 27-Dec-2019

17 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

TOLEO NAMBA 20 HALIUZWI JANUARY— MARCH

Banana Investments Ltd.

Page 2: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

2 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

Hili ni toleo la kwanza kutoka baada ya wahariri

kupatiwa mafunzo ya uandishi wa makala kwa

hiyo litakua na mabadiliko kidogo ambayo

tumeyafanya baada ya kupata utaalam zaidi.

Pia tunapenda kuchukua nafasi hii kuwatangazia

wasomaji wa jarida hili ikiwa ni pamoja na wasam-

bazaji wa bidhaa za BIL, wateja pamoja na marafiki

wote kwamba tunapokea makala mbalimbali kutoka

sehemu zote kwa hiyo wote wanaoweza kuandika

watume kwenye email ifuatayo: ba-

[email protected] au [email protected]. Pia

wanaweza kutuma kwa kupitia magari wa wasam-

bazaji au S L P 10123 Arusha. Kila makala ita-

kayochapwa mwandishi atapewa motisha ya kiasi

kidogo cha fedha ili aweze kuandika makala nyingi

zaidi.

Wote mnakaribishwa.

RAHA: BONGE LA LADHA KWA

BEI NAFUU.

KAMATI YA WAHARIRI YALIYOMO

Augustine S. Minja - Mwenyekiti 0715 451004

Beatha Anthony - Katibu 0717 350971

Philbert A. Mhindi - Mjumbe 0713 139052

Gerald Lyimo - Mjumbe 0754 380105

1. WAHARIRI WAPATA MAFUNZO YA UANDISHI WA HABARI ...2

2. PROMOTION YA TAJIRIKA NA RAHA YAFIKIA TAMATI……...3

3. MABORESHO KATIKA HUDUMA YA WATEJA…………….……3

4. MTANDAO WA USAMBAZAJI WA RAHA NCHINI TANZANIA..4

5. KIJUE CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA……………….…5

6. BANANA FOUNDATION WADHAMINI MAFUNZO YA VION-

GOZI WA SACCOS………………………………………….……….5

7. Y’S MEN TANZANIA WAFANIKISHA VUKA BODA BASH…....6

8. AJIRA MPYA, NGUVU MPYA KAMPUNI YA BANANA……......7

9. MATUKIO YA KUGAWA ZAWADI ZA TAJIRIKA NA RAHA…..8

WAHARIRI WA MBIU YA BANANA WAFANYIWA MAFUNZO

YA UBORESHAJI WA UASHISHI WA MAKALA

Baadhi ya washiriki wa Semina wakiwa ukumbini tayari kwa

kuanza masomo.

Mnano tarehe 12/10/2010 kampuni iliandaa semmina ya siku

moja kwa ajili ya kuwanoa wahariri wa Mbiu ya Banana.

Semina hii iliyoshirikisha wahariri kutoka mashirika mbalim-

bali wakiwepo AMCF na TCCIA iliendeshwa na wakufunzi

kutoka chuo cha Uandishi wa habari cha Arusha. Katika

mambo yaliyofundishwa kwenye hiyo semina ni pamoja na

upangiliaji wa

makala, jinsi ya kuandika makala bora na pia jinsi ya kupitia

makala.

SALAMU ZA MHARIRI

Page 3: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

3 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

Akampuni yaboresha huduma kwa watejaKutokana na kampuni kujali na kuwathamini wateja wetu, imeanzisha huduma

bora kwa wateja kwa saa 24 kwa njia ya simu:Huduma hii itakuwa kwaajili ya kuhakikisha kwamba wateja wanapata

yafuatayo:-

Kujibu maswali mbalimbali ya wateja.

Kuhakikisha wateja wetu wanapata huduma bila kukosa.

Kupata maoni na mahitaji mbalimbali kutoka kwa wanywaji/wateja.

Huduma hii itakuwa kwa kutumia meseji au kupiga simu na majibu yake yaweza kuwa ni kwa meseji au kupigiwa simu

na mteja atajibiwa hapo hapo au baadae. Namba za simu kwaajili ya huduma hii ni ; 0759 270508 na 0682 802283

WATEJA KWETU NI WAFALME, TUPO TAYARI KUWAHUDUMIAWATEJA KWETU NI WAFALME, TUPO TAYARI KUWAHUDUMIAWATEJA KWETU NI WAFALME, TUPO TAYARI KUWAHUDUMIAWATEJA KWETU NI WAFALME, TUPO TAYARI KUWAHUDUMIA

MABORESHO KATIKA HUDUMA KWA WATEJA.

Hivi karibuni kampuni yetu ilifanikiwa kufanya promotion kabambe ambayo ilianza mnamo tarehe 21.09.2010 hadi tarehe

09.12.2010.Kwa kipindi chote hicho wanywaji wetu waliweza kujipatia zawadi mbalimbali kama vile Raha ya bure, Fulana maalum

na pesa taslimu kuanzia shilingi 1,000/=, 2,000/= 5,000/= 10,000/= na 20,000/=

Hata hivyo haikuishia hapo tu, Shindano kubwa ilichezeshwa tarehe 12.12.2010 katika eneo la Sanawari maarufu kama stand ya

tax, ambapo washindi 8 walipatikana. Zoezi zima liliendeshwa chini ya usimamizi wa mwakilishi kutoka Bodi ya bahati na nasibu

Ndugu Humud Abdulhusein na waandishi wa habari kutoka sehemu mbalimbali. Washindi waligawanyika katika makundi matatu

ambayo kwa kundi la tatu walizawadiwa baiskeli 5 aina ya phonex, washindi wawili kwa kundi la pili walizawadiwa TV 2 aina SON

ya inchi 21 na Mashindi mmoja kwa nafasi ya kwanza alizawadiwa pikipiki aina ya Toyo 125CC.

ZAWADI HIZO ZILITOLEWA KAMA JEDWALI LINAVYO ONYESHA HAPA

PROMOTION YA TAJIRIKA NA RAHA YAFIKIA TAMATI, WENGI WATAJIRIKA NA VITU MBALIMBALI

DRO

NAM

BA

JINA LA

MSHINDI

ENEO

ZAWADI

SIMU

NAMBA.

980 DEUS FRANSIS NGARANARO BAISKELI 0757145298

1500 GENES JASTIN

MOSHI

OLORIENI BAISKELI 0753299738

1060 JOSEPH UWAWI SASI- DULUTI BAISKELI BOX 99

DULUTI

802 PIUS BENEDICT

MALLYA

MOSHONO BAISKELI 0759206692

514 MAIMU KI-

MARO

BABATI BAISKELI 0787866876

785 NESTO ED-

WARD KIMARO

NJIRO TV 0768614444

1046 DEVOTA LYIMO MIANZINI TV 0782459405

696 JOHN J.SHOO ESSO MOTORCY-

CLE

0753627459

0714439303

Baadhi ya washindi wakipokea zawadi zao maeneo

ya kiwandani.

Page 4: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

4 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

Tunawakaribisha wafanyabiashara kujiunga na Kampuni yetu ya Banana Investments Ltd kusambaza kinywaji chetu kwenye mikoa

ambayo RAHA haijafika. Hali ya sasa katika usambazaji wa mvinyo wa Raha upo kama unavyoonyesha hapo juu kwenye Ramani.

Page 5: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

5 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

CHUO Kikuu huria cha Tanzania, CKHT, ni chuo ki-

kuu cha umma hapa nchini. Chuo hiki hutoa elimu kwa

njia ya masafa kwa watu wa rika zote ambao hawana

muda wa kuhudhuria masomo darasani muda wote,

hivyo kutoa fursa kwa waajiriwa na wafanya biashara

kujiendeleza katika taaluma mbalimbali katika ngazi

za stashahada ,”certificate”, stashahada , “diploma” na

shahada “degree”. Elimu inayotolewa na Chuo Kiku-

kuu huria cha Tanzania ni elimu yenye ubora na inayo-

kubalika (Quality and affordable education) sawa na

vyuo vikuu vingine duniani Makao makuu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yako

Dar es Salaam, Sanduku la posta 23409, na tovuti ya

chuo ni www.out.ac.tz. Chuo kina vituo katika mikoa

yote ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kuna usemi kuwa

“CKHT kinawafuata wanafunzi popote walipo nchini

Tanzania” na si kinyume chake kama ilivyo kwa vyuo

vikuu vingine. Wanafunzi wanaojiunga na CKHT

husailiwa na Tanzania Commission of Universities,

TCU, sawa na wale wanajiunga na vyuo vikuu vingine

hapa nchini. CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-

gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu

kuendelea na elimu ya juu. Mwanafunzi hupata fursa

ya kujifunza taratibu za chuo na maelezo ya kina kuen-

dana na mafunzo aliyochagua. Katika kipindi hiki

mwanafunzi hupewa nafasi ya mwisho kubadilisha aina

ya mafunzo atakayochukua na CKHT.

Baada ya mwanafunzi kusajiliwa, chuo husaidia kutoa

elimu endelevu kwa njia ya majaribio na mitihani kwa

muda wote wa mafunzo. Mwanafunzi hupewa mihta-

sari,“course outlines” za masomo anayochukua pamoja

na vitabu husika, na ana uhuru wa kujisomea kwa wa-

kati wake mwenyewe ndani ya muda wa masomo

uliopangwa. Watu mbalimbali wamefanikiwa kujiendeleza kwa uta-

ratibu huu na kuhitimu mafunzo mbalimbali. Miongoni

mwa wafanyakazi wa Kampuni ya Banana waliofaulu

kupitia CKHT ni pamoja na Bwana Ally A. Massawe,

Mkurugenzi wa Fedha na Utawala ambaye alitunukiwa

Shahada ya Uzamili ya Biashara na Utawala, “ Master

of Business Administration” na Bi. Betty Mboya,

katibu muhtasi wa kampuni ya Banana, ambaye ame-

hitimu Astashahada ya Biashara na Utawala. Wote

walitunukiwa vyeti vya kuhitimu mwezi October, 2010.

Bi Betty Mboya amefaulu kuendelea kusomea Shahada

ya Biashara na Utawala , “Bachelor of Business Ad-

ministration” kwa mhula ulioanza 13 Novemba, 2010.

KIJUE CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA

Imeandikwa na Betty Mboya.

Faida kubwa za utaratibu wa masomo ya CKHT ni pamoja

na unafuu wa ada ukilinganisha na vyuo vingine, wanafunzi

kupewa fursa ya kujisomea kwa wakati wao nje ya eneo la

chuo na hivyo kuruhusiwa kuendelea kusoma na huku waki-

fanya kazi au biashara kwa wakati mmoja. Wanafunzi wana-

ruhusiwa kufanya mitihani sehemu yoyote nchini bara na

visiwani bila kujali mahali alipojiandikisha. Wahitimu wa

shule za sekondari, kidato cha IV na VI, ambao hawakucha-

guliwa kuendelea na masomo ya juu sasa wanaweza kupata

elimu ya juu kupitia CKHT na kuongeza kwa kiasi kikubwa

idadi ya wahitimu wa elimu ya juu hapa nchini.

BANANA FOUNDATION WADHAMINI MAFUNZO YA

VIONGOZI WA SACCOS.

Na. Beatha Anthony

Banana Foundation ni taasisi isiyo ya kiserikali inayojihu-

sisha na kutoa misaada mbalimbali katika jamii hasa kwa

watu au familia zisizojiweza.

Taasisi hii inapata ruruku zake kutoka Banana Investments

Ltd ambazo zinatumika kutoa misaada mbalimbali. Shughuli

ambazo Banana Foundation inafanya ni pamoja na kusaidia

kuinua kipato cha wanajamii hasahasa wajasiriamali

wadogowadogo. Na hii wanaifanya kupitia kwenye vyama

vya ushirika vya kuweka na kukopa (SACCOS). Mpaka sasa

banana Foundation imeshaingia mkataba na SACCOS za

UDEA, Kijenge RC, TCCIA na Banana. Ili waweze kuwa-

saidia kuinua vyama vyao na kutoa mikopo ya kutosha na

kwa wakati wa wajasiriamali. Msaada unaotolewa na Ba-

nana Foundation ni wa mafunzo mbalimbali ya kujenga

uwezo na sio fedha taslimu.

Ili kuhakikisha kwamba hilo linafanikiwa Banana Founda-

tion wakishirikiana na Benki ya CRDB waliandaa semina ya

siku moja iliyojumuisha viongozi wa SACCOS zote na ku-

toa mafunzo juu ya janga la mikopo ambalo limekua ni ta-

tizo sugu kwa SACCOS nyingi.

Akiendesha mafunzo hayo Bw Seuri kutoka CRDB alisisi-

tiza kwamba viongozi na watendaji wawe makini wakati wa

kutoa mikopo kwani hapo ndio makosa mengi hujitokeza.

Pamoja na hayo pia Banana Foundation hutoa msaada kwa

wanafunzi wanaoishi katika mazingira hatarishi hasa yatima

na wale wanaoishi katika hali duni. Wanafunzi wanaopata

hizi ruzuku ni wale wanaosoma katika shule zilizoko kata ya

Oloirien au wanaoishi Oloirien lakini wanasoma sehemu

nyingine. Pia wanafunzi hao wanatakiwa kuwa na uwezo wa

kimasomo darasani na sio ambao hawafanyi vizuri.

Pia tunakaribisha watu wote wanaoweza kutoa msaada an-

Page 6: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

6 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

Y’S MEN TANZANIA WAFADIKISHA VUKA BODA BASH NA: Beatha Anthony

Tamasha la Vuka Boda lililoandaliwa na wanachama wa Y’s

Men wa Arusha kuanzia tarehe 17 mpaka tarehe 20 Decemba

2010. Tamasha hili liliudhuriwa na wanachama kutoka Moshi,

Arusha, Nairobi South, Nairobi Central, Thika, CUEA na

KEMU.

Wanachama wote walifikia shule ya Trust St Patrick iliyopo mae-

neo ya Sakina ambapo walipatiwa malazi pamoja na usafiri kwa

muda wote waliokuwepo hapa Arusha. Katika Tamasha hili

lengo kuu lilikua ni kumpongeza kijana Vincent Gichamba wa

Nairobi Central kwa kuchaguliwa kuwa International Youth Rep-

resentative (IYP) wakati wa Convention iliyofanyika Yokohama

Japan mwezi wa August mwaka huu.

Katika tamasha hili kati ya mambo yaliyofanyika ni pamoja na

kuotesha miti katika maeneo ya moshono, pia kulikuwepo na

mafundisho mbalimbali ya uongozi bora katika viwanja vya ki-

talii vya Lake Duluti na kumalizia kwa kutembele kituo cha utalii

cha Snake Park kilichopo Arusha.

Y’s Men International imekua ikitoa kipaumbele kwa mafunzo

ya uongozi bora kuanzia ngazi ya familia, taifa na mpaka kima-

taifa kwani inaaminika kwamba Viongozi waaminifu na wenye

busara ndio wanaleta maendeleo endelevu.

PAP Hiyasinti Kilasara akielezea jambo wakati wa presenta-

tion katika ukumbi wa Lake Duluti.

Baadhi ya Washiriki wa Vuka Boda Bash wakiwa kwenye picha

ya pamoja maeneo ya Snake Park.

Wanachama wakiskiliza kwa makini baadhi ya mafundisho yali-

yotolewa katika ukumbi wa Duluti.

Kiongozi wa Y’s Yoth arusha akiwa na wanachana kutoka Nai-

robi Centrali walivyotembelea kituo cha utalii cha Meserani

snake park

Page 7: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

7 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

Elisante Makyao – Afisa Masoko

Bw. Elisante ana Stashada ya juu

katika maeneleo ya ustawi wa jamii

katika chuo cha Community Devel-

opment Training Institute (CDTI)

Tengeru Arusha mwaka 2010. Pia

ana cheti cha maendeleo ya jamii

katika chuocha CDTI Tengeru cha

mwaka 1992 pamoja na cheti cha elimu ya secondary

kidato cha nne katika shule ya secondari Majengo

moshi mwaka 1985. Ana uzoefu wa miaka zaidi ya

kumi katika taasisi mbalimbali.

AJIRA MPYA, NGUVU MPYA KAMPUNI YA BANANA

KIBWENZO

Zuhura Mmbaga – Accounts Technician

Bi Zuhura ana Diploma in Cooperative

and Accounting katika chuo cha

Moshi University Collage of coopera-

tive and business studies – 2010 pia

ana cheti cha kuhitimu elimu ya juu

katika shule ya secondari Shinyanga

Commercial Institute (SHYCOM) –

2008.

Steven Mvungi – Afisa Masoko Msaidizi Bw. Steven Mvungi ana Cheti cha

Accounts Technician – 2009, ana

Certificate ya Accounts Technician

NBAA pia ana cheti cha elimu ya

juu katika shule ya sekondari Ma-

kumira – 2001 pamoja na cheti cha

elimu ya sekondari kidato cha nne

Lembeni mwaka 1998.

Page 8: Toleo la 20 January—March Banana Investments Ltd · CKHT huandaa mafunzo ya awali, “orientation pro-gram”, baada ya wanafunzi kuchaguliwa au kufaulu kuendelea na elimu ya juu

8 HALIUZWI

Toleo la 20 January—March

Makao Makuu Kiwanja Na. 311, Kitalu jj Oloirien Village, P. O. Box 10123, Arusha TANZANIA S i m u : +255754224440,+255272506475 E-mail: [email protected] http:/www.banana.co.tz tz

Dar es Salaam Depot Ubungo Kibangu, S. L. P. 79407, Dar es Salaam TANZANIA Simu: +255 222 774 276, +255 756 707 983 Email: [email protected]

Tanga Depot Barabara ya 4, S. L. P. 5150, Tanga TANZANIA Simu: +255 272 646 134

Email: [email protected].

WASHINDI WA TAJIRIKA NA RAHA WAKIKABIDHIWA ZAWADI ZAO