mkoa wa simiyu · ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika mkoa wa simiyu. mkoa una jumla...

12
1 MKUU WA MKOA MH ANTHONY J MTAKA KATIBU TAWALA MKOA NDG. JUMANNE A SAGINI MKOA WA SIMIYU UTANGULIZI Mkoa wa Simiyu ulianzishwa kwa Tangazo la Serikali (GN) Na. 72 la tarehe 02 Machi, 2012, unapatikana Kaskazini mwa Tanza- nia, Kusini Mashariki mwa Ziwa Victoria. Mkoa upo kati ya longitudo 33°03” na 34°01” Mashariki ya mstari wa Griniwichi na latitudi 02°01” hadi 04°00” Kusini mwa Ikweta. Aidha, kwa upande wa Kaskazini, Mkoa wa Simiyu unapakana na Mkoa wa Ma- ra, Mashariki Mikoa ya Singida na Manyara, Kusini Mkoa wa Shinyanga na Tabora na upande wa Magharibi Mkoa wa Mwanza. ENEO LA UTAWALA Mkoa wa Simiyu una eneo la Kilomita za mraba 23,807.70. Kati ya hizo Km za mraba 11,479.10 zinafaa kwa shughuli za Kilimo na Ufugaji, Kilomita za mraba 11,723.60 ni eneo la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mapori ya Akiba ya Maswa, Kijereshi na Mwiba, Hifadhi za Jumuiya za Wanyama Pori (WMAs) Makao. Aidha, Kilometa za mraba 605 ni eneo la maji ya Ziwa Victoria. Mkoa una Wilaya 5 za kiutawala ambazo ni Bariadi, Busega, Itilima , Maswa na Meatu. Aidha, Mkoa una Halmashauri 6, majimbo 7 ya uchaguzi, Tarafa 16, Kata 130, Vijiji 471, Mitaa 92 na Vitongoji 2,659. Ufugaji Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351. Wanyama wengine ni nguruwe 7936, bata 17,795, punda 4,356 na mbwa 35,006. Ng’ombe wa kienyeji wanaopatikana Simiyu Shughuli za Uvuvi na Kilimo cha Pamba Mkoani Simiyu SHUGHULI KUU ZA UCHUMI Kilimo:- Kilimo na Ufugaji ni shughuli kuu za kiuchumi zinazofanywa na wakazi wa Mkoa wa Simiyu. Eneo la Km za mraba 11,479.10 sawa na asilimia 48.2 ya eneo lote la Mkoa linafaa kwa kilimo na ufugaji. Kilimo na ufugaji inachangia asilimia 75 ya pato la Mkoa na zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Mkoa huu ni wakulima na wafugaji. Viwanda na Biashara Mkoa una viwanda vya kati 14 vya kuchambua pamba na kusindika mafuta ya pamba na alizeti. Viwanda hivi vinafanya kazi wakati wa msimu wa zao la pamba. Ufugaji wa Nyuki Mkoa una jumla ya vikundi 91 vya ufugaji nyuki vyenye wanachama 2,589 na mizinga 4, 790 yenye uwezo wa kuzalisha lita 61,500 za asali na kilo 4,690 za nta kwa mwaka. Madini ya chumvi Chumvi inapatikana katika maeneo ya Mito-Minane na Mwagotolo katika kijiji cha Lukale, Wilaya ya Meatu. Madini haya huuzwa ndani na nje ya mkoa. Mazao ya Biashara Mazao ya biashara yanayolimwa Mkoa wa Simiyu ni pamba (inazalishwa kwa asilimia 47 ya pamba yote inayozalishwa nchini),. Mazao mengine ni alizeti, dengu na choroko. Mazao ya chakula Mazao makuu ya chakula ni mahindi, mtama, uwele, mpunga, viazi vitamu, mihogo, dengu,maharage na jamii nyingine ya mikunde. Uvuvi Shughuli za uvuvi zinafanyika katika Wilaya ya Busega ambayo ina eneo la Ziwa Victoria lenye km za mraba 605 na inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya wilaya, mkoa na Taifa kwa ujumla. IDADI YA WATU Kutokana na Sensa ya Taifa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012; Mkoa ulikuwa na jumla ya watu 1, 584,157 kati ya hao Wanaume walikuwa 759,891 na Wanawake 824,266. Wastani wa ongezeko la idadi ya watu ni asilimia 1.8 kwa mwaka, na wastani wa watu katika kaya ni 6.9. Aidha, hadi kufikia Desemba, 2015 Mkoa unakisiwa kuwa na wakazi wapatao 1,671,250, Wanawake wakiwa 869,582 na Wanaume 801,668.

Upload: others

Post on 10-Jan-2020

30 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

1

MKUU WA MKOA

MH ANTHONY J MTAKA

KATIBU TAWALA MKOA

NDG. JUMANNE A SAGINI

MKOA WA

SIMIYU

UTANGULIZI

Mkoa wa Simiyu ulianzishwa kwa Tangazo la Serikali (GN) Na. 72 la tarehe 02 Machi, 2012, unapatikana Kaskazini mwa Tanza-

nia, Kusini Mashariki mwa Ziwa Victoria. Mkoa upo kati ya longitudo 33°03” na 34°01” Mashariki ya mstari wa Griniwichi na

latitudi 02°01” hadi 04°00” Kusini mwa Ikweta. Aidha, kwa upande wa Kaskazini, Mkoa wa Simiyu unapakana na Mkoa wa Ma-

ra, Mashariki Mikoa ya Singida na Manyara, Kusini Mkoa wa Shinyanga na Tabora na upande wa Magharibi Mkoa wa Mwanza.

ENEO LA UTAWALA

Mkoa wa Simiyu una eneo la Kilomita za mraba 23,807.70.

Kati ya hizo Km za mraba 11,479.10 zinafaa kwa shughuli za

Kilimo na Ufugaji, Kilomita za mraba 11,723.60 ni eneo la

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mapori ya Akiba ya Maswa,

Kijereshi na Mwiba, Hifadhi za Jumuiya za Wanyama Pori

(WMAs) Makao. Aidha, Kilometa za mraba 605 ni eneo la

maji ya Ziwa Victoria.

Mkoa una Wilaya 5 za kiutawala ambazo ni Bariadi, Busega,

Itilima , Maswa na Meatu. Aidha, Mkoa una Halmashauri 6,

majimbo 7 ya uchaguzi, Tarafa 16, Kata 130, Vijiji 471, Mitaa

92 na Vitongoji 2,659.

Ufugaji

Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao

1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351.

Wanyama wengine ni nguruwe 7936, bata 17,795, punda

4,356 na mbwa 35,006.

Ng’ombe wa kienyeji wanaopatikana Simiyu

Shughuli za Uvuvi na Kilimo cha Pamba Mkoani Simiyu

SHUGHULI KUU ZA UCHUMI

Kilimo:- Kilimo na Ufugaji ni shughuli kuu za kiuchumi

zinazofanywa na wakazi wa Mkoa wa Simiyu. Eneo la Km za

mraba 11,479.10 sawa na asilimia 48.2 ya eneo lote la Mkoa

linafaa kwa kilimo na ufugaji. Kilimo na ufugaji inachangia

asilimia 75 ya pato la Mkoa na zaidi ya asilimia 80 ya wakazi

wa Mkoa huu ni wakulima na wafugaji.

Viwanda na Biashara

Mkoa una viwanda vya kati 14 vya kuchambua pamba na

kusindika mafuta ya pamba na alizeti. Viwanda hivi vinafanya

kazi wakati wa msimu wa zao la pamba.

Ufugaji wa Nyuki Mkoa una jumla ya vikundi 91 vya ufugaji nyuki vyenye

wanachama 2,589 na mizinga 4, 790 yenye uwezo wa kuzalisha

lita 61,500 za asali na kilo 4,690 za nta kwa mwaka.

Madini ya chumvi Chumvi inapatikana katika maeneo ya Mito-Minane na

Mwagotolo katika kijiji cha Lukale, Wilaya ya Meatu. Madini

haya huuzwa ndani na nje ya mkoa.

Mazao ya Biashara

Mazao ya biashara yanayolimwa Mkoa wa Simiyu ni pamba

(inazalishwa kwa asilimia 47 ya pamba yote inayozalishwa

nchini),. Mazao mengine ni alizeti, dengu na choroko.

Mazao ya chakula

Mazao makuu ya chakula ni mahindi, mtama, uwele, mpunga,

viazi vitamu, mihogo, dengu,maharage na jamii nyingine ya

mikunde.

Uvuvi

Shughuli za uvuvi zinafanyika katika Wilaya ya Busega

ambayo ina eneo la Ziwa Victoria lenye km za mraba 605 na

inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya wilaya, mkoa na

Taifa kwa ujumla.

IDADI YA WATU

Kutokana na Sensa ya Taifa ya Watu na Makazi ya mwaka

2012; Mkoa ulikuwa na jumla ya watu 1, 584,157 kati ya hao

Wanaume walikuwa 759,891 na Wanawake 824,266. Wastani

wa ongezeko la i d a d i y a watu ni asilimia 1.8 kwa

mwaka, na wastani wa watu katika kaya ni 6.9. Aidha, hadi

kufikia Desemba, 2015 Mkoa unakisiwa kuwa na wakazi

wapatao 1,671,250, Wanawake wakiwa 869,582 na Wanaume

801,668.

Page 2: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

2

HUDUMA ZA JAMII

ELIMU

Elimu ya Msingi:- Mkoa una jumla ya shule za Msingi 523

zenye madarasa ya awali, kati ya hizo 514 ni za Serikali na 9 ni

za binafsi na Taasisi za dini. Shule hizi zinazohudumiwa na

jumla ya walimu 6912 kati ya walimu 9448 wanaohitajika.

Elimu ya Sekondari:- Mkoa una shule za sekondari 148, kati

ya hizo 140 ni za Serikali na 8 ni za binafsi na Taasisi za dini.

Shule hizi zinahudumiwa na walimu 2,330 kati ya walimu 4317

wanaohitajika.

Vyuo:- Mkoa una vyuo vya ualimu 3 vinavyomilikiwa na watu

binafsi, vyuo 2 vya maendeleo ya Jamii na 1 cha ufundi stadi .

Elimu ya juu:- Mkoa una Chuo Kikuu Huria kinachotoa

mafunzo mbalimbali ya elimu ya juu.

AFYA:

Mkoa una zahanati 191, vituo vya afya 14 na hospitali 4

zinazomilikiwa na serikali, watu binafsi na Taasisi za dini.

Hospitali ya Somanda ni Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa.

Mkoa unatekeleza mpango wa utoaji elimu ya kinga kwa

magonjwa mbalimbali yakiwemo Malaria, Kifua Kikuu

UKIMWI.

MAJI

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika

mkoa ni wastani wa asilimia 46 ambapo mijini na asilimia 46.6

na vijijini ni asilimia 46. Serikali inaendelea kuboresha hali ya

upatikanaji wa maji safi na salama katika mkoa kupitia

programu ya maendeleo ya sekta ya maji. Aidha Serikali

inaendelea na mpango wa kuleta maji kutoka ziwa Victoria

katika miji ya Makao Makuu ya Wilaya.

FURSA UWEKEZAJI

Mkoa unazalisha asilimia 47 ya pamba ya Tanzania hivyo una

fursa kubwa ya uwekezaji katika viwanda vya kusokota nyuzi,

kutengeneza nguo na viwanda vya kutengeneza vitu

vitokanavyo na pamba kama mafuta, bandeji, pamba za

hospitali na pamba za masikioni. Aidha, Mkoa una idadi kubwa

ya ng‟ombe hivyo kuna fursa za viwanda vya kusindika mazao

ya ngo‟ombe kama maziwa, nyama na ngozi.

MALIASILI NA UTALII

Shughuli za Utalii na uwindaji wa Kitalii zinafanyika katika

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Pori la Akiba la Maswa na

Hifadhi za Jumuiya ya Wanyamapori (WMA) Makao.

Halmashauri zinazozunguka Pori la Akiba la Maswa zinapewa

asilimia 25 ya ruzuku inayotokana na uwindaji huo.

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Mkoa una mtandao wa barabara zenye urefu wa kilomita

4,730.95 ambazo zimegawanyika katika makundi yafuatayo:-

Barabara kuu Km 334.72, barabara za Mkoa Km 532.30,

barabara za Wilaya Km 2420.5 na barabara za Vijijini

1451.53; kati ya hizi Km 141.76 zina kiwango cha lami, Km

2453.59 kiwango cha changarawe na Km 2134.7 za kiwango

cha udongo. Kwa upande wa Mawasiliano, Mkoa

umeunganishwa na mitandao ya simu ya Airtel, Vodacom,

Tigo, Halotel na TTCL, huduma ya mawasiliano inapatikana

Mijini na Vijijini.

Daraja la Mto Simiyu linalotenganisha Wilaya ya Meatu na

Itilima

UTAMADUNI NA MICHEZO

Mila na desturi za wakazi wa Mkoa wa Simiyu kwa asilimia

kubwa ni za kabila la Wasukuma kwa kuwa ndilo kabila kuu.

Makabila mengine ni wataturu na wahadzabe wanaopatikana

katika wilaya ya Meatu karibu na Ziwa Eyasi.

Ngoma za asili katika Mkoa huu ni Mbina ambazo huchezwa

wakati wa msimu wa mavuno na huitimishwa tarehe 31 Mei ya

kila mwaka. Pia wenyeji (Wasukuma) wanapenda kushiriki

katika michezo mbalimbali ikiwemo mashindano ya mbio za

baiskeli na riadha.

Twiga katika Pori la Akiba la Maswa

Ujenzi wa Jengo la wagonjwa wa nje

Hospitali ya Mkoa (OPD)

Sehemu ya Ngoma ya Asili (Mbina) maarufu katika Mkoa wa

Simiyu

Page 3: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

3

Mkuu wa Wilaya

Mhe. Festo Kiswaga

HALMASHAURI YA WILAYA

BARIADI Mkurugenzi Mtendaji (W)

Ndg. Abdallah Malela

UTANGULIZI Wilaya ya Bariadi iko kati ya nyuzi 2015’ na 3010’ kusini mwa Ikweta na nyuzi 33040‟ hadi 350 10’ mashariki ya Greenwich.

Wilaya hii inaundwa na Halmashauri mbili; Halmashauri ya mji Bariadi na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na ina jimbo 1 la

uchaguzi (jimbo la Bariadi).

JIOGRAFIA

Halmashauri ya Wilaya Bariadi inapakana na Wilaya ya Busega

kwa upande wa magharibi, Mkoa wa Mara upande wa kaskazini,

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Pori la Akiba la Maswa upande

wa mashariki, Wilaya ya Maswa na Itilima upande wa kusini.

ENEO Halmashauri ina eneo la ukubwa wa Km za mraba 5,091.21 kati

ya hizo, Km 1,096.21 ni ardhi yenye udongo unaofaa kwa

shughuli za kilimo na ufugaji, Km 790 ni eneo la Pori la Akiba la

Maswa na Km 3,160 ni Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na eneo la

Km 45 ni maji, misitu na milima.

ENEO LA TAWALA Halmashauri ina tarafa 3 ambazo ni Mhango, Dutwa na Nkololo,

kata 21, vijiji 84 na vitongoji 555.

IDADI YA WATU: Kulingana na sensa ya Taifa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012,

Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ilikuwa na jumla ya watu

267,296 kati yao wanawake 139,426 na wanaume ni 127,870 na

ongezeko la asilimia 3 ya idadi ya watu kwa mwaka. Wastani wa

idadi ya watu kwa kaya ni 6.9.

SHUGHULI ZA KIUCHUMI: Katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi shughuli kuu za

kiuchumi ni Kilimo, Ufugaji na biashara ndogo ndogo.

Mifugo Halmashauri ina jumla ya ng‟ombe 262,835, mbuzi 113,013,

kondoo 54,328 na kuku 373,738. Asilimia kubwa ya wafugaji wa

wanafuga kienyeji.

Kilimo Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya

Bariadi wanategemea kilimo. Halmashauri ina eneo la hekta

185,729 linalofaa kwa kilimo kati ya hizo, hekta 102,151 ndizo

zinatumika kwa kilimo na eneo la hekta 63,348 linafaa kwa

kilimo cha umwagiliaji. Mazao makuu ya chakula yanayolimwa

ni mtama, mahindi, mpunga, viazi vitamu na mihogo. Mazao ya

biashara yanayolimwa ni pamba, alizeti, dengu na choroko.

HUDUMA ZA JAMII

ELIMU

Halmashauri ina jumla ya Shule za Msingi 73 zenye madarasa ya

awali na zinamilikiwa na serikali, shule za sekondari 23 kati ya

hizo 22 zinamilikiwa na Serikali na 1 ni ya mtu binafsi.

AFYA

Halmashauri ina zahanati 25, na vituo 2 vya afya

vinavyomilikiwa na Serikali, watu binafsi, na Taasisi za

Dini. Wilaya haina Hospitali ila wananchi wanapata huduma

katika Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa. (Somanda).

MAJI

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika

Halmashauri ni asilimia 42.

Kisima cha maji kijiji cha Mwauchumu

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Halmashauri ina jumla ya Km 727.6 za barabara. Kati ya

hizo Km 296.6 ni za Wilaya na Km 429.1 ni za Vijiji.

Halmashauri inapata huduma za mawasiliano ya simu

kupitia makampuni ya Vodacom, Airtel, Tigo, Halotel na

TTCL.

MALIASILI NA UTALII

Zaidi ya asilimia 41.8 ya eneo la Halmashauri ya wilaya ni

Hifadhi ya Taifa Serengeti na asilimia 8.4 ni Pori la Akiba

la Maswa. Hii inatoa fursa kubwa ya utalii na uwindaji wa

kitalii kuzunguka maeneo hayo.

UTAMADUNI

Wenyeji wa Halmashauri hii (Wasukuma) wana tamaduni

tofauti zikiwemo kucheza ngoma ya asili (Mbina), ngoma

hii huchezwa wakati wa msimu wa mavuno na mashindano

ya mbio za baiskeli. Pia wanaendeleza Utamaduni wa

kichifu (Utemi) .

FURSA ZA UWEKEZAJI

Kutokana na Wilaya kuwa na idadi kubwa ya Mifugo na zao

la Pamba, zipo fursa za uwekezaji katika kuongeza thamani

ya Bidhaa ya mazao yanayotokana na Pamba pamoja na

mifugo.

Page 4: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

4

HALMASHAURI YA MJI

BARIADI Mkurugenzi wa Mji

Ndg. Melkzedek Humbe

UTANGULIZI

Halmashauri ya Mji wa Bariadi ilianzishwa kwa tangazo la Serikali namba 278 la tarehe 24 Agosti, 2012. Halmashauri hii

iligawanywa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, na ndipo yalipo makao makuu ya Mkoa.

ENEO LA HALMASHAURI

Halmashauri hii ina ukubwa wa Km za mraba 876.71 ambazo

zinatumika kwa shughuli za kilimo, makazi ,biashara na

shughuli nyingine.

ENEO LA UTAWALA

Halmashauri hii ina Tarafa 3, Kata 10 na mitaa 92 na ni

sehemu ya jimbo la Uchaguzi la Bariadi.

IDADI YA WATU

Kutokana na Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, idadi

ya wakazi wa mji wa Bariadi ni 155,620. Kati yao wanawake

ni 81,772 na wanaume ni 73,848.

SHUGHULI ZA KIUCHUMI

Shughuli za kiuchumi katika Mji wa Bariadi ni Biashara,

Viwanda vidogo, Kilimo, Ufugaji na Ushirika.

Kilimo:- Halmashauri ina eneo lenye jumla ya hekta 87,671

ambapo hekta 77,850 zinafaa kwa kilimo. Mazao ya chakula

yanayolimwa ni pamoja na mahindi,mpunga, mtama, viazi

vitamu na mikunde. Mazao ya biashara ni Pamba, Alizeti,

mbaazi, choroko na dengu.

Sehemu ya shamba la Pamba na marobotaya pamba

Biashara:-Mji wa Bariadi una wafanyabiasha wadogo na

wakubwa wanaotoa huduma mbalimbali katika sekta ya

usafirishaji, viwanda vidogo, visima vya mafuta na huduma

nyingine za jamii. Takribani asilimia 95 ya wanyabiashara

katika mji wa Bariadi ni Wanyantuzu (wenyeji).

Ufugaji:- Ufugaji ni Shughuli kubwa ya kiuchumi

inayofanywa na wananchi wa mji wa Bariadi. Kutokana na

sensa ya mifugo iliyofanyika mwezi Aprili 2016 Halmashauri

ina jumla ya Ng‟ombe 66,699, , Mbuzi 40,302, Kondoo

23,575, Nguruwe 1,326 Kuku 102,901, Bata 9,345, Punda

306, Mbwa 8,968, paka 5,198 na Kanga 685

Viwanda:- Mji wa Bariadi una viwanda vitatu vya

kuchambua Pamba, ambavyo ni Nsagali Co. Ltd, NGS

Investment Co. Ltd na Vitreces Investment Co. Ltd.

Viwanda hivi vinamilikiwa na watu binafsi.

HUDUMA ZA JAMII

AFYA Halmashauri ya Mji Bariadi ina zahanati 18, kati ya hizo 8 ni za

serikali, 1 ni ya Jeshi la Magereza na 9 zinamilikiwa na watu

binafsi na Taasisi za Dini. Aidha, vipo vituo 2 vya afya vi-

navyomilikiwa na serikali na Hospitali 1 ambayo ni hospitali

Teule ya Mkoa .

ELIMU Halmashauri ina jumla ya shule 40 za Msingi zenye madarsa ya

awali, kati ya hizo 38 ni za Serikali na 2 ni za binafsi. Shule za

sekondari zipo 16 kati ya hizo 14 ni za Serikali na 2 ni za bi-

nafsi. Aidha, kuna Chuo kimoja cha Ualimu kinachomilikiwa

na mtu binafsi, chuo 1 cha Maendeleo ya Jamii kina-

chomilikiwa na Serikali na Chuo Kikuu Huria.

MAJI Upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Mji wa

Bariadi ni asilimia 42.5.Vyanzo vya maji ni visima vifupi 240

na visima virefu 27.

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Barabara:- Halmashauri ina mtandao wa barabara zenye

jumla ya km 398.55, kati ya hizo barabara za lami ni Km 6.66

changarawe Km 37.1 na za udongo Km 357.35.

Halmashauri ipo katika mradi wa uboreshaji miundombinu

katika miji (ULGSP) ambapo Km 4.85 zinaendelea kujengwa

kwa ufadhili wa Benki ya Dunia. Barabara hizi

zitakapokamilika zitakuwa na taa za barabarani, sehemu ya

watembea kwa miguu, mifereji na maegesho ya magari

kuzunguka soko.

Mawasiliano:- Mji wa Bariadi unapata huduma ya

mawasiliano kupitia makampuni ya simu ya Vodacom, Airtel,

Tigo, Halotel na Zantel. Usikivu na upatikanaji wake ni mzuri .

HUDUMA ZA FEDHA

Taasisi zinazotoa huduma ya fedha katika Mji wa Bariadi ni

Benki ya NMB,CRDB na Benki ya Posta. Pia zipo huduma za

fedha kwa kupitia mitandao ya simu ambayo ni M-Pesa, Tigo-

Pesa na Airtel money.

Mkuu wa Wilaya

Mhe. Festo Kiswaga

Page 5: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

5

Mkuu wa Wilaya

Mh. Benson Kilangi

HALMASHAURI YA WILAYA

ITILIMA Mkurugenzi Mtendaji (W)

Ndg. Mariano E Mwanyigu

UTANGULIZI Wilaya ya Itilima kwa upande wa Kaskazini inapakana na Wilaya ya Bariadi, Kusini Wilaya ya Meatu na Maswa, Magharibi

Wilaya ya Busega na Mashariki inapakana na Mkoa wa Arusha. Wilaya ina ukubwa wa Km za Mraba 2,647.7 ambapo Km2

1,938.7 sawa na 73.2% zinatumika kwa shughuli za kiuchumi, makazi na miundombinu, Km2 640 sawa na 24.17% ni Pori la akiba

la Maswa, Km2 69 sawa na 2.61% ni maeneo ya Mto Simiyu, vilima, misitu ya asili (ngitile) na mabonde.

ENEO LA UTAWALA

Wilaya ina Tarafa 4 ambazo ni Kanadi, Bumera, Itilima na

Kinang‟weli, Kata 22, Vijiji 102 na Vitongoji 597. Pia ina jimbo

moja la uchaguzi (Jimbo la Itilima).

IDADI YA WATU Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012,

Wilaya ilikuwa na jumla ya wakazi wapatao 313,900 kati yao

wanawake ni 165,398 na wanaume ni 148,502. Jumla ya Kaya ni

43,597, wastani wa idadi ya watu katika kaya ni 7. Ongezeko la

watu ni 1.8% kwa mwaka hivyo Kwa mwaka 2016 idadi ya watu

inakadiriwa kuwa 342,247.

SHUGHULI ZA KIUCHUMI NA UZALISHAJI

Uchumi wa Itilima unategemea zaidi kilimo na ufugaji.

KILIMO

Kilimo huchangia asilimia 85-95 ya pato la Wilaya. Eneo

linalofaa kwa kilimo ni hekta 193,170 na linalolimwa ni hekta

163,447. Zaidi ya asilimia 75 ya wakazi wa wilaya hii ni

wakulima.

Mazao makuu ya chakula:- ni mahindi, mtama, mpunga, viazi

vitamu, muhogo, maharage na kunde. Pia mazao ya mboga

mboga kama kabichi hulimwa katika baadhi ya maeneo

Mazao ya Biashara:- Pamba, ni zao kuu la biashara, mazao

mengine ni karanga, alizeti, dengu, mbaazi na choroko.

Wilaya imepiga hatua katika matumizi ya zana bora za kilimo

ambapo trekta kubwa zipo 80, ndogo 28, plau 13,031,

mikokoteni 1,188, majembe ya kupalilia 2,100, rippers 3,

majembe ya kupandia 5 na maksai 54,706. Elimu inaendelea

kutolewa ili kuongeza idadi ya wakulima wanaotumia zana bora

za kilimo.

MIFUGO

Wilaya ina zaidi ya ng‟ombe 296,322, kondoo 48,177, mbuzi

100,220, nguruwe 1,063, kuku 201,243, bata 4,843, mbwa

13,752 na punda 89. Shughuli za ufugaji hufanyika

sambamba na kilimo. Eneo la ardhi linalofaa kwa malisho ya

mifugo ni Km za mraba 1,938.7 sawa na hekta 193,870.

Mkulima akiwa katika Shamba la Pamba

Mkulima akilima shamba kwa trekta

Mkulima wa mbogamboga (Aina ya kabichi) katika kijiji cha

Mwabuki .

Page 6: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

6

MAENDELEO YA JAMII

Wilaya imesajili vikundi vya wajasiriamali 544 katika mwaka wa

fedha 2015/2016, vikundi hivi vinapewa Mikopo yenye riba na-

fuu ya 10% ya mapato ya ndani ya fedha zinazotengwa katika

bajeti ya Halmashauri. Pia kuna vikundi 41 vinavyojishughulisha

na “Village Community Bank” (VICOBA) kwa lengo la kujiletea

maendeleo.

ELIMU

Elimu ya Msingi:- Wilaya ina jumla ya shule 87 za msingi

zenye madarasa ya awali zinazomilikiwa na serikali. Shule hizi

zina jumla ya wanafunzi 78,688 kati yao wavulana ni 38,127 na

wasichana ni 40,561 na zinahudumiwa na walimu wapato 1,262

kati ya wlimu 1,608 wanaohitajika.

Jengo la darasa katika shule ya msingi Mwakimisha.

Elimu ya Sekondari;- Wilaya ina Shule 30 za sekondari, kati ya

hizo 29 ni za serikali na 1 ni ya Taasisi ya dini. Shule hizi

zinahudumiwa na walimu wapato 502 kati ya walimu 1,160

wanaohitajika.

AFYA

Wilaya ina jumla ya zahanti 29 kati hizo 26 ni za serikali na 3

zinamilikiwa na watu binafsi na Taasisi za dini, kuna vituo

vya afya 3, wilaya haina hospitali hivyo wananchi wanapata

huduma za Rufaa katika Hospitali Teule ya Mkoa (Somanda).

Wananchi wakipata huduma ya maji safi katika kijiji cha

Zanzui

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Wilaya ina mtandao wa barabara zenye urefu wa Km 692.3,

kati ya hizo Km 53.68 ni barabara za Mkoa, Km 227.9 ni

barabara za Wilaya (collector roads), Km 390.72 ni barabara

za Vijiji (feeder roads) na Km 20 ni barabara za vituo vya

biashara (urban roads). Barabara zote ni za kiwango cha

changarawe na udongo. Wilaya ina huduma ya mawasiliano

ya simu za mkononi ya mitandao ya Tigo, Airtel, Vodacom,

Halotel na TTCL.

HUDUMA ZA JAMII

UTAMADUNI

Wenyeji wa wilaya hii ni kabila la Wasukuma (Wanyantuzu),

jina hili lilitokana na muunganiko wa makabila mawili,

Wasukuma na Wanyaturu. Wenyeji hujihusisha na shughuli za

ufugaji wa kiasili, kilimo na shughuli za sanaa zikiwemo Muziki

wa asili, tiba asilia, ngoma, ususi, ufinyanzi, uchongaji na

matambiko. Jengo la kliniki ya mama na mtoto kituo cha afya Luguru

MAJI

Huduma ya maji safi na salama inapatikana kwa wastani wa

asilimia 45.2 ambapo wananchi wanapata maji umbali usiozidi

mita 400. Wilaya ina visima virefu na vifupi vinavyotoa

huduma 118, mabwawa 2, malambo 21 na matenki ya kuvunia

maji ya mvua 48.

Page 7: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

7

Mkuu wa Wilaya

Mhe

HALMASHAURI YA WILAYA

MASWA Mkurugenzi Mtendaji (W)

DKT. Fredrick D. Sagamiko

UTANGULIZI

Wilaya ya Maswa inapakana na Wilaya ya Meatu kwa upande Mashariki , Kaskazini na Kaskazini Magharibi

inapakana na Wilaya ya Itilima, Kusini inapakana na Wilaya ya Kishapu (Mkoa wa Shinyanga) na Magharibi

inapakana na Mkoa wa Mwanza.

ENEO LA WILAYA

Wilaya ni Km za mraba 3,398 kati ya hizo Km 2,475 zinafaa kwa

shughuli za kilimo na ufugaji, Km 77 ni hifadhi ya misitu na Km

846 ni miinuko ya mawe, vilima na misitu ya asili (ngitili).

ENEO LA UTAWALA

Kiutawala, Wilaya ina tarafa 3, Kata 36, Mamlaka ya Mji 1 yenye

Vitongoji 40, Vijiji 120, na Vitongoji 510. Aidha, kuna Majimbo

mawili ya uchaguzi, ya Maswa Mashariki na Maswa Magharibi.

IDADI YA WATU

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 idadi ya

watu inakadiriwa kufikia watu 344,125 kati yao wanawake ni

176,723 na wanaume ni 167,402. Kaya zinakadiriwa kufikia

52,942 zenye wastani wa watu 6.5 kwa kaya. Ongezeko la watu

linakadiriwa kuwa asilimia 1.8 kwa mwaka.

SHUGHULI ZA KIUCHUMI

Shughuli kubwa za uchumi kwa Wananchi wa Wilaya ya Maswa

ni kilimo na ufugaji. Shughuli zingine ni uvuvi,ushirika na

viwanda vidogo. Wilaya inategemea mapato yake kwa kiasi

kikubwa kutokana na mazao ya kilimo na mifugo. Kwa mujibu

wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 asilimia 80 ya

wakazi wanashughulika kilimo na ufugaji. Wastani wa pato la

mwananchi kwa mwaka inakadiliwa kuwa Tsh. 324, 843

Miundombinu ya Kilimo cha umwagiliaji katika kijiji

cha Kinamwigulu

FURSA ZA KIUCHUMI

Wilaya ina jumla ya ekari 10,576.5 kwa ajili ya uwekezaji

wa viwanda, shughuli za kilimo na ufugaji katika kata za

Shishiyu, Malampaka na Sukuma. Zipo fursa za kuongeza

thamani ya bidhaa zinazotokana na mazao ya pamba, alizeti

na mifugo.

ENEO LA KILIMO

Wilaya ina kilometa za mraba 3,398 kati ya hizo, Km 2,475

zinafaa kwa shughuli za kilimo na ufugaji na Hekta 52,375

zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Mazao ya chakula na

biashara yanayolimwa ni pamoja na Mpunga, Viazi vitamu,

Mahindi, Mtama, Ulezi, karanga na Mihogo. Zao kuu la biashara

ni Pamba, mazao mengine ni alizeti , dengu na choroko.

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Barabara;- Wilaya ya Maswa ina barabara zenye urefu wa

km 1,043.98 , kati ya hizo, km 302.27 ni za changarawe na

km 741.71 ni za udongo. Barabara hizi zinapitika kwa

asilimia 55 kwa mwaka mzima.

RELI;- Wilaya ina kituo kidogo cha reli Inayotoka Mwanza

kuelekea Dar Es Salaam katika mji mdogo wa Malampaka na

kuna kituo kidogo cha usafirishaji wa mizigo na abiria.

UFUGAJI

Idadi ya Mifugo katika Wilaya ni ng‟ombe 403,416 mbuzi

239,498, kondoo 182,284, kuku 1,441,648, punda 847, nguruwe

3405 na mbwa 12,286 . Huduma za kustawisha mifugo

zinatolewa kupitia majosho 44, mabwawa 33, malambo 31 Cliniki

1 ya mifugo na vituo 7 vya kutolea Ushauri wa mifugo. Zaidi ya

ekari 92,418 hurutubishwa kila mwaka kutokana na uzalishaji wa

tani 462,090 za mbolea ya samadi.

VIWANJA VYA NDEGE:-Wilaya ina viwanja vya

ndege vidogo viwili (air strips) ambavyo Vipo Maswa Mjini

na Malya.

SIMU: - Mawasiliano ya simu yanapatikana kwa wastani

wa asilimia 92 kupitia makampuni ya mawasiliano ya TTCL,

Vodacom, Airtel,Halotel na Tigo.

REDIO:- Kuna Stesheni 1 ya Redio Sibuka FM, ambayo

inamilikiwa na mtu binafsi. Wilaya hutumia redio hiyo ku-

tolea matangazo na taarifa mbalimbali muhimu kufikishwa

kwa Wananchi.

Page 8: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

8

Sehemu ya Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD) katika

Hospitali ya Wilaya ya Maswa

MAJI:- Asilimia 59.78 ya wananchi wanaoishi vijijini

wanapata huduma ya maji safi na salama. Kwa upande wa

mjini wananchi wanapata maji safi na salama kwa asilimia

83, chanzo kikuu cha maji mjini ni kupitia mradi wa maji wa

kitaifa Maswa.

HUDUMA ZA JAMII

Vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari

Nyalikungu vilivyojengwa kwa ufadhili wa SEDP II

AFYA:- Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ina jumla ya

vituo vya kutolea huduma ya Afya 46, Zahanati 42 kati hizo

Zahanati 2 zinazomilikiwa na madhehebu ya dini 2 na 2

zinamilikiwa na watu binafsi, vituo vya afya 3 na Hospitali

ya Wilaya.

HUDUMA ZA FEDHA

Wilaya ina jumla ya Taasisi za kifedha 2 zinazo toa

huduma kwa jamii nazo ni NMB na CRDB. Aidha kuna

Taasisi ndogo ndogo za fedha zinazotoa mikopo kwa

Wananchi ambazo ni BAYPOT, FINCA, ABC Bank,

VISION FUND.Wilaya ina jumla ya SACCOS 52

zilizosajiliwa. Tenki la kuhifadhia maji kijiji cha Lalago

Wananchi wakipata huduma ya maji katika kijiji cha

Sangamwalugesha

MAENDELEO YA VIJANA

Wilaya ina Vikundi vya vijana 256 vyenye jumla ya wanachama

2,662.Vikundi hivi hujishughulisha na kilimo, ufugaji, biashara

ndogondogo, ushonaji, ususi, ufinyanzi, ufyatuaji wa tofali, ujenzi

na uselemara, utengenezaji wa chaki pamoja na uendeshaji wa

bodaboda.Vikundi 08 vimeunda SACCOS na hadi sasa

vimepatiwa shilingi 38,000,000 toka Wizara yenye dhamana na

Maendeleo ya vijana.Fedha hizi zimetumika kuanzisha kiwanda

cha kutengeneza chaki zinazotambulika sokoni kwa jina la

„MASWA CHALKS‟ (nyeupe) na „JPM CHALKS‟ (za rangi).

HUDUMA YA UMEME

Huduma ya umeme wa gridi inapatikana katika maeneo ya vijiji

pamoja na makao makuu ya Wilaya. Jumla ya vijiji 67 kati ya

vijiji 120 vimeunganishiwa katika Mpango wa Umeme Vijijini

(REA).

iHUDUMA YA UMEME

Huduma ya umeme wa gridi inapatikana katika maeneo ya

vijiji pamoja na makao makuu ya Wilaya. Jumla ya vijiji 67

kati ya vijiji 120 vimeunganishiwa katika Mpango wa

Umeme Vijijini (REA).

ELIMU:- Wilaya ina jumla ya Shule za Msingi 123, kati

ya hizo shule 2 ni za binafsi na shule 121 ni za serikali,

shule za sekondari ziko 40 kati ya hizo 36 zinamilikiwa na

Serikali na 4 ni za watu binafsi na Taasisi za dini.

Vyuo;- Wilaya ina chuo 1 cha Ualimu kinachomilikiwa na

watu binafsi, chuo cha Maendeleo ya Wananchi 1

(Malampaka FDC) na chuo cha Ufundi Stadi 1 (Binza

VTC) vinavyomilikiwa na serikali.

Chaki zinazozalishwa na kikundi cha Vijana

Wilaya ya Maswa

Page 9: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

9

HALMASHAURI YA WILAYA

MEATU

MKUU WA WILAYA

Mh. Dkt.Joseph Chilonga

MKURUGENZI WA WILAYA

Ndg. Fabian Manoza

UTANGULIZI

Wilaya ya Meatu inapatikana katika latitudi 2057 na 409 kusini mwa Ikweta na longitudo 3408 na 34049 Mashariki mwa Grinwich.

Imepakana na wilaya ya Bariadi upande wa kaskazini, Ngorongoro na Karatu upande wa mashariki, Wakati upande wa kusini

inapakana na wilaya za Mbulu na Iramba na wilaya za Maswa na Kishapu zipo upande wa magharibi wa wilaya.

ENEO LA WILAYA

Wilaya ina ukubwa wa kilometa za mraba 8,835. Asilimia 49

ya eneo lote la Wilaya ni hifadhi za wanyamapori ambazo ni

Pori la akiba Maswa, sehemu ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti,

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi za Jumuiya ya

Taifa ya Wanyamapori (WMA) . Eneo lililosalia asilimia 51

linatumika kwa ajili ya makazi, shughuli za kijamii na kiuchumi

ENEO LA UTAWALA

Wilaya hii ilianzishwa Tarehe 01 Julai 1987 baada ya Wilaya ya

Maswa kugawanywa. Makao makuu ya Wilaya ya Meatu yapo

katika Mji wa Mwanhuzi. Wilaya ina Tarafa tatu:- ambazo ni

Kisesa, Kimali na Nyalanja na kata 25 ambazo zina jumla ya

idadi ya vijiji 100 na pia ina majimbo 2 ya uchaguzi ambayo ni

Jimbo la Kisesa na Meatu.

IDADI YA WATU

Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012,

Wilaya ilikuwa na jumla ya wakazi wapatao 299,619 kati yao

143,569 ni wanaume na 156,050 ni wanawake. Wastani wa

idadi ya watu katika kaya ni 7.4 na ongezeko la watu ni 1.9%.

Wilaya inakaliwa na kabila la Wasukuma ambalo lina idadi

kubwa ya watu ikilinganishwa na Makabila mengine ambayo

yanapatikana katika Wilaya ya Meatu, makabila hayo ni

Wanyaturu, Wanyiramba, Wanyisanzu na Wahadzabe

SHUGHULI ZA KIUCHUMI

Shughuli za kiuchumi zinazofanywa na Wilaya hii ni Kilimo na

Ufugaji. Shughuli za Uwindaji na upigaji picha za kitalii

unafanyika kwenye Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya

Makao na Pori la Akiba la Maswa. Aidha utengenezaji wa

chumvi unafanyika katika eneo la Ziwa Eyasi Tarafa ya

Nyalanja na biashara ndogondogo.

Uzalishaji wa chumvi katika kijiji cha Nyalanja

Uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara

Katika msimu 2015/16 Wilaya iliweka lengo la kuzalisha

jumla ya tani 121,365 za chakula. Katika utekelezaji jumla ya

tani 1,888,217 zilivunwa. Wilaya ya Meatu ni kame kwa

kipindi kirefu cha mwaka. Hivyo wananchi wanahimizwa

kulima mazao yanayostahimili ukame hasa mtama, uwele na

viazi vitamu. Mahindi pia hulimwa katika baaadhi ya maeneo.

Zao kuu la biashara ni Pamba, mazao mengine ya biashara ni

alizeti na vitunguu

UFUGAJI

Ufugaji ni shughuli kuu ya pili Kiuchumi baada ya Kilimo

kwa wananchi wa wilaya ya Meatu.Wilaya inakadiriwa kuwa

na Ng‟ombe 353,389, Mbuzi 385,252, Kondooo 137,297,

Nguruwe 884, Punda 3,114, kuku 457,362 na Bata 3,607.

UVUVI

Uvuvi hufanyika katika kata ya Bukundi, Mwamalole na

Mwabuzo. Shughuli hii hufanyika katika Ziwa Eyasi, Mto

Sibiti, Bwawa la Mwanyahina na Kitangiri. Aina ya samaki

wapatikanao ni perege,kambare,nembe,ningu na kamongo

ambao hutumika kwa ajili ya chakula na biashara.

KILIMO

Eneo la hekta 458,200 kati ya 883,500 ambalo ni eneo lote la

wilaya linafaa kwa kilimo. Eneo linalolimwa ni hekta 159,993

sawa na asilimia 35 za eneo linalofaa kwa kilimo. Eneo

lililobaki (425,300 ha) ni kwa ajili ya mifugo, makazi, hifadhi

ya wanyamapori ya Makao (WMA-Wildlife Management Area)

na Hifadhi ya wanyamapori ya Maswa (Maswa Game

Reserve).

MISITU

Sekta ya misitu imejikita katika utunzaji wa ngitili (Uoto wa

asili) ambapo eneo lenye jumla ya hekta 161,615.4 za ngitili

zilizohifadhiwa. Wilaya imejiwekea utaratibu wa kuanzisha

bustani ya miche ya miti ili kuratibu zoezi la upandaji miti kila

mwaka. Hii inatokana na hali ya kijiografia ya wilaya hii kuwa

kame.Uhamasishaji hufanyika kwa wananchi kutunza uoto wa

asili (ngitili) na kujenga tabia ya kupanda miti kila ifikapo

msimu wa mvua.

Page 10: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

10

MALIASILI NA UTALII

Wilaya ya Meatu ina eneo la hifadhi lenye ukubwa wa km za

mraba 3888. Eneo hili linaundwa na pori la akiba la Maswa (Km22094), eneo la hifadhi ya jamii ya Wanyamapori (WMA)

Makao(Km2768.9), Ngitili ya kijiji cha Makao (196.47km2),

Hifadhi ya ya Taifa Serengeti(694km2) na hifadhi ya Ngorongoro(Km2135). Kuwepo kwa maeneo haya yenye wanyama kama

tembo, twiga, simba, nyati n.k kumeongeza uwepo wa fursa za

utalii katika wilaya ya Meatu na kuchangia katika pato la wilaya

na Taifa kwa ujumla

Wanyama pori katika eneo la Hifadhi ya Makao Meatu

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

Wilaya ina jumla ya mtandao wa barabara wenye urefu wa Km.

1,032 ambapo urefu huu umegawanywa katika Barabara za

Mkoa (135 Km) ,Barabara za Wilaya (337.94 Km), Barabara za

Mjini (27.45 Km) na Barabara za Vijijini( 542.87 Km). Wilaya

imeunganishwa na barabara za changarawe na zenye tabaka la

udongo. Aidha, Barabara za Mjini Mwanhuzi zenye urefu wa Km

13 zimejengwa kwa kiwango cha lami. Wilaya ina mtandao wa

mawasiliano ya simu ya TTCL, VODACOM, AIRTEL, TIGO na

HALOTEL

Barabara ya lami km 13 mjini Mwanhuzi na ujenzi wa

barabara mpya Katani/Vijijini

ELIMU:-Wilaya hii ina shule za Msingi 111 zenye jumla ya

wanafunzi 59,332 kati yao wavulana ni 27,639 na wasichana

29,693. Mwaka 2016 wilaya iliandikisha jumla ya

wanafunzi 10,931 wa darasa la kwanza, kati yao wavulana

5467 na wasichana 5464 sawa na asilimi 102 ya lengo.

Elimu ya Sekondari:- wilaya ina jumla ya shule 22 za

sekondari kati ya hizo tatu (03) ni za Kidato cha Tano na

Sita.Wilaya pia inasimamia uendeshaji wa madarasa ya

Elimu ya Watu Wazima kwa lengo la kupunguza idadi ya

waisojua kusoma na kuandika kupitia mpango wa Elimu

masafa(ODL) na mpango wa uwiano kati ya elimu ya watu

wazima na jamii (MKEJA).

AFYA Wilaya ina zahanati 52, Vituo vya Afya 3 na Hospitali 1 ya

Wilaya na inatoa elimu ya kinga, chanjo kwa watoto, mama

wajawazito na tiba kwa wananchi. Hali ya upatikanaji wa

vifaa tiba ni asilimia 60.

Huduma za upasuaji Na jengo la hudumu Kwa wazee Hospitali ya wilaya ya Meatu

HUDUMA ZA JAMII

MAJI Hali ya upatikanaji wa maji ni asilimia 34 mjini na asilimia 42.2

vijijini .Vyanzo vikuu vya Maji katika Wilaya ya Meatu ni

Bwawa la Mwanyahina ambalo linahudumia wakazi wa Mjini

Mwanhuzi. Maeneo ya Vijijini vyanzo vikuu ni visima vifupi na

virefu.

MAENDELEO YA SEKTA VIJANA Idara ya maendeleo ya jamii kwa kushirikiana na idara ya

ushirika imetoa elimu ya ujasirimali, uanzishwaji na uende-

shaji wa SACCOS kwa vikundi 8 vya vijana. Vikundi hivyo

vimeungana na kutengeneza SACCOS 1 ya vijana ambayo

imekopeshwa kiasi cha Tsh. 31,000,000/= kutoka Wizara

yenye dhamana na Maendeleo ya vijana na kuanzisha ki-

wanda kidogo cha kusindika maziwa ya ng‟ombe wa kien-

yeji yanayotambulika sokoni kwa jina la “MEATU MILK”

UTAMADUNI

Wilaya ina jumla ya makabila matatu ambayo ni watindiga

(wahadzabe), wataturu na kabila kuu wasukuma, makabila yote

haya yamebaki katika asili zao hivyo kuwa kivutio cha utalii wa

utamaduni. Kuna jumla ya Vikundi vya burudani na sanaa 25

ambapo vikundi 6 vimesajiliwa na Baraza la Sanaa Tanzania

(BASATA) ambavyo ni Mshikamano House of Talent, Bomani

Sanaa Group, Nzobe Ngoma Group, Ngoma ya Wataturu, Mshi-

kamano Sanaa Group na Meatu Time Arts Group.

Kabila la Watindiga(Wahadzabe) wakisaga unga na kulia ni Kabila la

wataturu katika ngoma ya Asili inayoitwa “Nyangira”

Maziwa yanayotengenezwa na Kikundi cha Vijana Meatu

Page 11: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

11

HALMASHAURI YA WILAYA

BUSEGA

UTANGULIZI

Wilaya ilianzishwa Mwaka 2012 kwa Tangazo la Serikali (G.N) Na 73 la tarehe 02 Machi 2012, Wilaya hii ilianzishwa baada ya

kugawanywa kwa Wilaya ya Magu iliyoko Mkoa wa Mwanza. Kwa upande wa Kaskazini wilaya inapakana na Mkoa wa Mwanza,

Mashariki inapakana na Mkoa wa Mara, kusini inapakana na Wilaya ya Bariadi, Kusini-Magharibi inapakana na Wilaya ya Itilima,

na upande wa Magharibi inapakana na Wilaya ya Magu iliyoko Mkoa wa Mwanza.

ENEO LA KIUTAWALA Wilaya ina Jimbo 1 la uchaguzi, Tarafa 2, Kata 15 na Vijiji 59

vyenye jumla ya Vitongoji 334. Makao makuu yapo katika

Kata ya Nyashimo.

Jengo la ofisi ya Halmashuari linaloendelea kujengwa

IDADI YA WATU Idadi ya watu kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya

mwaka 2012 ni 216,059, kati yao wanaume ni 104,741 na

wanawake ni 111,318, ambapo ukuaji wa ongezeko la watu ni

2% kwa mwaka.

SHUGHULI ZA UCHUMI Shughuli kubwa za kiuchumi katika Wilaya ya Busega ni

Kilimo, Ufugaji na Uvuvi. Wilaya ina jumla ya Hekta

77,293.70 zinazofaa kwa kilimo na ufugaji na kilomita za

mraba 605 ni sehemu ya Ziwa Victoria ambayo inatumika kwa

shughuli za uvuvi.

Kilimo: Katika msimu 2015/2016 jumla ya hekta 36,7776

sawa na asilimia 47.6 za eneo linalofaa kwa kilimo zililimwa

mazao ya chakula na biasahra.

Mazao ya chakula ni pamoja na mahindi, mtama, viazi vitamu

na mihogo, zao kuu la biashara ni pamba.

Ufugaji: Wilaya ina jumla ya ng`ombe 186,054, mbuzi 68,364,

kondoo 35,127, nguruwe 1,258 na kuku 346,459. Eneo

lililotengwa kwa ajili ya malisho ni hekta 150,900.

Uvuvi: shughuli za uvuvi hufanyika katika mialo(Beach

Management Unit) ya Nyamikoma, Nyakaboja na Ihale.

Wilaya ina jumla ya wavuvi 3,926 ambao huvua samaki aina

ya sato na sangara kwa ajili ya kupeleka viwandani na kwenye

masoko ya kawaida ndani na nje ya wilaya hasa soko la

halmashauri ya Mji Bariadi yalipo makao makuu ya Mkoa

MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO Wilaya ina jumla ya kilometa 299.1 za barabara zinazojumuisha

barabara za wilaya Km. 172.9 na barabara za vijiji (Feeder

roads) Km.126.2. Jumla ya Km. 209.37 sawa na asilimia 70 ya

barabara zote za wilaya na vijiji, zinapitika majira yote ya

mwaka. Wilaya ina mawasiliano ya TTCL, Aitel, Vodacom,

Tigo, Halotel na Zantel.

MADINI Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na kampuni ya Twig Gold

mwaka 2011 ilibaini kuwa wilaya ina akiba ya tani milioni 11

za madini aina ya nickel katika mlima wa Ngasamo. Kampuni

ya Red hill nickel Limited imewezeka katika uchimbaji wa

madini hayo na ikokwenye hatua ya tathmini na upembuzi

yakinifu wa mzingira “Social Environmental Impact

Assessment” (SEIA).

HUDUMA ZA JAMII

ELIMU

Elimu ya Msingi: Wilaya ina jumla ya shule za msingi 91

kati ya hizo, 86 ni za serikali na 5 ni za watu binafsi. Shule

zote zina madarasa ya awali na zinahudumiwa na walimu

1,018 kati ya 1,328 wanaohitajika . Elimu ya sekondari: Shule za Sekondari ziko 21 kati ya

hizo 17 ni za Serikali na 4 ni za watu binafsi. Shule zote zina

maabara zilizojengwa kwa nguvu za wananchi na serikali kwa

ajili ya kuwezesha wanafunzi kujifunza masomo ya sayansi

kwa vitendo.

Jengo la Maabara Shule ya Sekondari Mkula.

Page 12: MKOA WA SIMIYU · Ufugaji ni shughuli kuu ya pili ya kiuchumi katika Mkoa wa Simiyu. Mkoa una jumla ya ng'ombe wa asili wapatao 1,568,715 mbuzi 946,649 kondoo 480,788na kuku 2,923,351

12

AFYA Wilaya ina vituo 2 vya afya vya serikali vilivyoko kata ya Igalukilo na Nyashimo na Zahanati 20 za serikali

zinazo toa huduma ya afya kwa wananchi . Kuna hospitali 1 ya Mkula inayotoa huduma kwa wananchi na

inamilikiwa na Taasisi ya dini (AIC), ipo katika kata ya Mkula. Halmashauri inatarajia kuingia mkataba na

kuifanya kuwa hospitali teule ya wilaya.

Jengo la Wodi ya mama wajawazito katika zahanati ya Nassa

MAJI

Huduma ya maji safi na salama inapatikana kwa asilimia 38.6 vyazno vikuu vikiwa ni miradi ya maji bomba,

visima vifupi na virefu.

Ujenzi wa Mradi wa maji katika kijiji cha Lukungu