kanisa linahitaji kujua (swahili)

83
Umeka wakati tuyazungumzie mambo kadhaa ya msingi waziwazi ili Wakristo watambue ya kwamba Bwana ana mambo mazuri zaidi kwa ajili yao! Miki Hardy LINAHITAJI KUJUA KANISA

Upload: ctmi-church-team-ministries-international

Post on 17-Aug-2015

288 views

Category:

Spiritual


14 download

TRANSCRIPT

Page 1: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Umefika wakati tuyazungumzie mambo kadhaa ya msingi waziwazi ili Wakristo watambue ya kwamba

Bwana ana mambo mazuri zaidi kwa ajili yao!

Miki Hardy

LINAHITAJI

KUJUA

KANISA

Page 2: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

10

Hakimiliki © 2013 na Church Team Ministries International (CTMI) Kanisa Linahitaji Kujua na Miki Hardy. Imechapishwa na Church Team Ministries International (CTMI) Toleo la kwanza: Julai 2015 Jalada limebuniwa na: Idara ya Habari ya CTMI Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu ya chapisho hili inayoweza kunakiliwa, kusambazwa,au kutolewa kwa namna yo yote ile isipokuwa kwa ruhusa ya mchapishaji.

Vifungu vya Biblia vimetolewa katika Biblia, Swahili – Union Version, 1962.

Machapisho mengi ya Church Team Ministries International yanapatikana kwa gharama nafuu ikiwa yananunuliwa kwa jumla kwa ajili ya kutangaza, kuchangisha fedha, kugawa bure, na kwa kuelimishia.

Kwa maelezo zaidi, tuandikie: Media Dept., CTMI, Trianon, Mauritius; au tuma baruapepe kwa: [email protected]

Tembelea tovuti yetu: www.ctmi.org

ISBN 978-99949-0-181-4

Page 3: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Yaliyomo

I. Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka 5

II. Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo? 15

III. Mkristo na Pesa 23

IV. Mungu na Muziki 31

V. Vita ya Rohoni 39

VI. Mahusiano Kabla ya Ndoa 47

VII. Barabara ni Nyembamba 55

VIII. Kanisa Litakabiliwa 65

IX. Yesu Anaita Tena 75

...................................

..........................

.......................................................................

......................................................................

...........................................................................

.......................................................

........................................................

................................................................

.....................................................................

3

Page 4: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

4

Page 5: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Sura ya I

Moyo wa MunguJuu ya Ndoa na Talaka

5

Page 6: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

Wakristo wengi leo wanaweza kukumbuka wakati ambapo suala

la talaka kwa mchungaji au kiongozi wa Kanisa lilikuwa ni jambo la

aibu isiyoneneka. Hapakuwepo na uwezekano kwa mtu wa jinsi hiyo

kuendelea katika utumishi. Zaidi na zaidi, leo tunaona wachungaji

wakitoa talaka, wakioa upya na kuendelea na huduma kana kwamba

hakuna jambo zito lililofanyika. Ninaamini haya ni matokeo ya anguko

na udini ambavyo vimechukua nafasi ya fundisho la uzima na Kweli

ya Kibiblia ndani ya Kanisa. Hili ndilo chimbuko la hii hali ya mambo.

Sasa, ikiwa mchungaji anaweza kumpa mkewe talaka na akaendelea

kuwaongoza watu wa Mungu, je! waumini wanapata mfano wa jinsi

gani wa kuiga?

Labda maswali tunayopaswa kujiuliza ni, “Ni kwa nini Wakristo wawili

waliojazwa Roho Mtakatifu washindwe kutatua tofauti zao” na, “Je!

kuna uhalali wo wote kwa haya matatizo kutotatulika, au kwa wawili

hawa kuachana?” Ama liwe linamhusu mchungaji, au mshirika wa

kanisa, ninaamini suala la kutengana, kutoa talaka, na kufunga ndoa

mara ya pili hufanyika kwa sababu hawa watu hawajui wajibu wao

kamili mmoja kwa mwingine katika ndoa. Tunaona kwenye Maandiko

ya kuwa mume ana wajibu mkubwa mno: kumpenda mkewe kama

Kristo anavyolipenda Kanisa. Vivyo hivyo, mke naye ameitwa amtii

mumewe. Kama wawili hawa wasipouchukua msalaba wao, na

kumruhusu Roho wa Mungu awavunje na kuwabadilisha, hilo kamwe

halitakuja kutokea… Mungu peke yake ndiye anayeweza kulifanya hili

mioyoni mwao. Hakuna mbinu inayoweza kulifanya hili… ni matokeo

ya kazi ya Msalaba maishani mwao!

6

Page 7: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Sijaona popote kwenye Maandiko kinachonielekeza kuamini ya

kuwa ni mapenzi ya Mungu kwa wanandoa Wakristo, achilia mbali

mchungaji, kutoa talaka. Hii ni kwa sababu Mungu, kwa njia ya

Msalaba, ameleta njia ya kurejesha upendo na umoja kati yao. Hebu

sasa tuangalie Neno la Mungu linavyotufunulia kuhusu suala la ndoa

na talaka…

Siku hizi, watu wengi hawaoni shida kwa Wakristo wanandoa

kuachana kwa sababu tu mmoja wao hapatani na mwenzake; au

kwa kuwa tu hawana mtazamo mmoja kuhusu mambo mbalimbali au

hawana tena maono mamoja!

Hakika hili ni eneo ambalo Kanisa limekubali kuathiriwa si tu na njia

za ulimwengu usioamini, bali pia na viongozi wa Kikristo ambao

wameandika vitabu, wakihalalisha matendo yao ya kibinafsi sana na

ambao, kwa kuamua kuchukua njia ya talaka wamefungua mlango

kwa waumini kufanya vile vile. Ninaamini ya kwamba badala yake,

tunapaswa tuuangalie mtazamo wa Mungu juu ya suala hili.

Ndoa Kwenye Agano Jipya

Kwenye kitabu cha Mwanzo, Mungu aliianzisha ndoa. Baada ya yale

Yesu aliyokamilisha Msalabani, ndoa ya kwenye Agano la Kale, yenye

wake wengi na hati za talaka, haiwezi tena kulinganishwa na ndoa

chini ya Agano Jipya.

Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka

7

Page 8: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

Mpango wa Mungu kwetu sisi, kama Wakristo tuliozaliwa mara ya pili,

ni kuishi na waume zetu na wake zetu hadi ‘kifo kitakapotutenganisha’.

Katika Marko 10:2, kwa kuwa Yesu alikuwa akiwahoji Mafarisayo

juu ya mtazamo wao wa kisheria katika masuala mengi, walimjaribu

kwa kumwuuliza: “Je, ni halali kwa mtu kumwacha mkewe?” Yesu

akawaonyesha ya kuwa, chini ya Musa na Torati, Mungu ‘aliruhusu’

talaka kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao (Marko 10:5); lakini

katika Agano Jipya, mambo yangekuwa tofauti. Katika Mathayo 5:32,

anazungumzia waziwazi juu ya kile kinachotarajiwa kwa waamini

wote wa Agano Jipya: “Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye

mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi;

na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.” ‘Isipokuwa kwa habari ya

uasherati’ bila shaka haimaanishi pale mwenzi mmoja anapoanguka

katika dhambi na kufanya tendo moja la uasherati au la kukosa

uaminifu. Inazungumzia mtu ambaye amerudi nyuma na anaishi

katika dhambi, na aliyedhamiria kuendelea kuishi katika dhambi. Kwa

kuiruhusu talaka katika mazingira hayo maalum, Yesu hajaondoa

ukweli kwamba yule aliyekosewa bado anatakiwa kunyenyekea na

kusamehe. Hili linaweza kufanyika kwa dhati pale tu tunapoikubali njia

ya Msalaba. Kwa hivyo, Biblia iko wazi: kwenye Agano Jipya, hakuna

uhalali wowote wa kutoa talaka isipokuwa katika maeneo maalum

sana… vinginevyo itapunguza kile Yesu alichokifanya Kalvari!

8

Page 9: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Injili Zisizokuwa Na Uweza

Nina hakika utakuwa umegundua ya kuwa Kanisa limepoteza

mwelekeo katika hili eneo, na linaenenda kama vile Injili ni kitu

kinachobadilika kwa kutegemea nyakati. Katika miongo michache

iliyopita, Kanisa, kwa kujumuisha wachungaji na viongozi, kwa usahihi

kabisa, halikukubaliana na talaka, lakini leo hii talaka imekubalika

makanisani. Ni nini kilichofanyika? Bila shaka ni kwa sababu injili

inayohubiriwa leo hii imebadilika na haina uwezo wa kushughulika

na mambo ya jinsi hiyo. Haina nguvu tena ya kuihakiki dhambi kama

mwanzoni. Mfano mzuri ni injili ya ‘Mafanikio’ inayovuta mioyo ya

watu kuyaandamia mambo ya mwilini badala ya kutafuta makuzi ya

rohoni. Haijengi, na hakika haina uwezo wa kukabiliana na mambo

ya ndani ambayo Wakristo wanapambana nayo leo. Hii ndio maana

ni muhimu turejee kwenye injili ya ufunuo wa Msalaba ikiwa tutataka

kuona familia za Kikristo zenye umoja pamoja na kupungua kwa

kiwango cha talaka Kanisani.

Siku hizi Wakristo mara nyingi wanataka njia rahisi ya kutatua matatizo

yao ya ndoa, mlango rahisi wa kutokea. Wanaachana kwa sababu

nyepesi kama vile: “Mke wangu hanitii”; “Mume wangu si mtu wa

rohoni,” au mbaya zaidi, “Hatupatani tena, maono yetu na matarajio

yetu yamebadilika…” Watu wa jinsi hii bila shaka hawajaisikia injili

sahihi, kwani injili sahihi itawaongoza katika kuwajibika kila mmoja

kwa mwenzake.

Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka

9

Page 10: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

Nafasi Ya Mume

Niruhusu nifafanue juu ya ufunuo wa ajabu Paulo aliopewa kuhusu

ndoa kwenye Waefeso 5. Uhusiano wa mume na mke ndio tu

uliolinganishwa katika Agano Jipya na uhusiano Yesu alio nao na

Kanisa lake. Paulo anatamka kwa ujasiri ya kuwa, “KAMA Kristo naye

alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake VIVYO HIVYO mume naye

anapaswa kumpenda mke wake.” Yesu alijinyenyekeza, akachukua

sura ya mwanadamu, akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

Hiyo ndiyo hali ya moyo Yesu anayoagiza mume awe nayo kwa mke

wake. Huo ndio wajibu wa mume: kama Yesu, yeye naye anaitwa

apoteze haki zake na autoe uhai wake kwa ajili ya mke wake. Huu

ndio ufunguo wa ndoa yenye mafanikio.

Utaratibu Wa Mungu Kwenye Ndoa

Nafasi ya mke imefananishwa na ile ya Kanisa. Paulo anatamka ya

kuwa “KAMA vile Kanisa limtiivyo Kristo, VIVYO HIVYO mke naye

anapaswa kumtii mumewe.” Kwa hivyo, Kanisa – wewe na mimi –

linapoelewa kile Yesu alichofanya msalabani kwa ajili yetu; kwa

maneno mengine, upendo aliouonyesha, sisi nasi tunaweza kumpenda

pia. Isingewezekana tumpende Yeye kabla ya kuujua upendo wake

kwetu. Je, unaweza ukaona utaratibu wa mambo hapa?

10

Page 11: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Ni wazi, basi, kwamba mume ana wajibu mkubwa zaidi kuliko mke

katika ndoa, kwani huduma yake inalinganishwa na ya Kristo, ilhali

ya mke imefananishwa na ya Kanisa. Ikiwa mume atakuwa tayari

kuchukua hatua ya kwanza, katika kuutii wito wake, kama Kristo

alivyofanya, moja kwa moja atavuna hali ya utii kutoka kwa mke

wake. Katika mazingira ya kawaida, hatutarajii kwamba utii wa

mwanamke kwa mumewe utakuwa wa moja kwa moja; lakini msingi

sahihi unapokuwepo, mume anaweza akatarajia ya kuwa mkewe

atamnyenyekea. Hata hivyo, hata kama mke hatafanya vile, mume

anapaswa aendelee kuyatoa maisha yake kwake, na amtegemee

Mungu kufanya muujiza moyoni mwa mkewe. Mwishoni mwa kifungu

hiki, Paulo ananukuu andiko kutoka katika Agano la Kale, “Kwa sababu

hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na

mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.” Moyo wa Mungu kwa

ajili ya ndoa ni mume na mke wadumu katika umoja maisha yao yote.

Tunapozitii amri za Mungu, yeye ni mwaminifu na hutenda miujiza.

Mume Wa Mke Mmoja…

Yapo mambo mengi sana yahusuyo ndoa ambayo hayajatajwa katika

Biblia. Kanisani mwetu penyewe tumeshuhudia matukio mengi

tofauti katika miaka hii mingi, na tumejifunza kuyatatua kila moja kwa

namna yake, katika neema na kweli. Mahali ndugu wa kiume au wa

kike alipoichukua njia ya Msalaba, na kuiruhusu toba kufanya kazi

11

Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka

Page 12: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

moyoni mwake, tumeshuhudia urejesho na ushindi maishani mwao

na katika utumishi wao kwa Bwana. Na hebu niongeze kusema

ya kwamba Mungu si Mungu anayetoa nafasi ya pili au ya tatu ya

kujaribisha mambo. Mpango wake sikuzote ni kwa mume kuwa na

mke mmoja, na ametuwezesha katika hilo kwa kumtuma Yesu katika

mfano wa mwanadamu, afe Msalabani na kuishinda dhambi katika

mwili. Ni juu yetu kuyatoa maisha yetu yawe dhabihu ili miili yetu

isulubiwe. Mwanamume anayemwacha mkewe halafu akaendelea

katika utumishi kana kwamba hakuna kilichofanyika, hawezi kutarajia

kuendelea kubeba upako ule ule katika utumishi wake kwa Bwana, na

hasa ikiwa ameoa tena, hadi atakapoacha kuhalalisha uamuzi wake

huo na kutubu.

Ufunguo Unaoleta Matengenezo

Si mpango wa Mungu kwa mtu yeyote kumwacha mwenzi wake.

Mungu anachukia talaka; lakini hawakatai wale walioachana – au

waliooa ama kuolewa mara ya pili – ikiwa watatubu. Ikiwa nimegusa

eneo linalokuhusu, hujachelewa. Mungu anaweza kukurejesha,

pamoja na utumishi wako kama uko kwenye huduma, ikiwa utakuwa

tayari kukiri ya kuwa haukuenenda sawasawa na moyo wala Neno la

Mungu, bali ulifuata tamaa za mwili wako; na ya kuwa, inawezekana

ulijiingiza katika mahusiano yasiyo sahihi.

12

Page 13: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Ikiwa ni hivyo, ni lazima umrudie Bwana kwa toba ya kweli; kulingana

na maongozi ya Roho Mtakatifu, na ukiwa na utayari wa kufanya lolote

atakalokuagiza kufanya... hata kama itakulazimu kumrudia mwenzi

wako wa mwanzo. Kumbuka ya kwamba Bwana hahitaji sababu au

maelezo kuhusu mwenzi wako, au kuhusu yale aliyoyafanya. Yeye

huuangalia moyo wa mtu.

Katika kila jambo, Mungu anatamani tuwe na moyo safi, mnyenyekevu,

uliojaa msamaha, na ulio na toba. Inawezekana yakawepo

mahusiano ambayo pengine hayawezi kurekebishika; ila, mengi zaidi

yanarekebishika, ikiwa tuko tayari kujikana nafsi zetu na kuuchukua

msalaba wetu. Msalaba ndilo suluhisho la Mungu kwa ndoa yenye

mafanikio!

13

Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka

Page 14: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

14

Page 15: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Sura ya II

Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo?

15

Page 16: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

Katika safari zangu barani Afrika katika miaka 25 iliyopita, swali moja

limekuwa likijitokeza mara kwa mara: “Je, inawezekana kwa Mkristo

aliyezaliwa mara ya pili kupagawa mapepo?” Hili jambo mara nyingi

huhusishwa na maisha aliyoishi mhusika huko nyuma, au kibaya

zaidi, linahusishwa na mambo waliyoyafanya mababu zake.

Inanihuzunisha kuona kwamba kuna Wakristo wengi wanaoamini

ya kwamba wao, au ndugu zao wa kiume na wa kike katika Kristo

wanaweza kupagawa mapepo baada ya kupokea wokovu. Sote

tunakubali ya kuwa kazi za mapepo na roho chafu zipo. Lakini je!

inawezekana kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kuhitaji kufunguliwa

kutokana na nguvu za mapepo? Ninaposoma Maandiko, jibu langu

kwa swali hili ni “Hapana!” yenye nguvu. Biblia iko wazi kuhusu hili

suala: tunapozaliwa mara ya pili, tunaokolewa kutoka katika nguvu

za giza na kuingizwa katika Ufalme wa Yesu Kristo. Roho Mtakatifu

anakuja kuishi ndani yetu na nuru haiwezi kukaa pamoja na giza.

Hakuna jinsi kabisa ambapo pepo anaweza akaishi ki-kwelikweli

ndani ya Mkristo aliyezaliwa mara ya pili, aliyeyatoa maisha yake kwa

Bwana Yesu Kristo na anayetamani kumtumikia. Haiwezekani kabisa!

Tunapaswa tuhoji wokovu wa watu waliojitokeza kwenye mikutano

na kuungama sala ya toba, halafu wakaendelea kudhihirisha dalili za

kupagawa mapepo. Katika hali kama hizo, labda tungepaswa kuuliza

swali: ‘Je, toba ya kweli imefanyika mioyoni mwao?’

Lakini cha muhimu zaidi, ni kwamba ninaamini matatizo mengi

yanayosingiziwa pepo ni madhihirisho tu ya mwili. Kwa bahati mbaya,

16

Page 17: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Wakristo wengi wameaminishwa ya kwamba haya madhihirisho ya

mwili ni kazi za Shetani. Jambo ambalo Kanisa linapaswa kujua ni

kwamba, katika hali kama hizi, maombezi ya ‘ukombozi’ sio jawabu.

Maisha yetu yanapooana na mfano wa Yesu Kristo, na tunapouchukua

Msalaba wetu kila siku, na kuifisha miili yetu na kumfuata yeye, suala

la ‘kupagawa pepo’ halitakuwa tatizo maishani mwetu, au kwa Kanisa.

Ulimwengu wa roho upo na unaweza kuwa na nguvu kuliko

tunavyofikiri. Ndio maana Mungu anapogusa maisha yetu tunaweza

kubadilishwa mara moja. Kwa msingi huo huo kuna watu ambao

maisha yao yameathiriwa na mapepo pamoja na roho za kishetani.

Katika vitabu vya injili, Yesu mwenyewe alitoa pepo na kuwaweka watu

huru. Ukweli kwamba watu wanapagawa mapepo upo na hauwezi

kupingwa. Hata hivyo, katika Mathayo 12, Yesu anapozungumza

juu ya kutoa pepo, alizungumza kabla ya Msalaba na alikuwa

akizungumzia kizazi kikaidi, sio Kanisa. Kwa hivyo, swali langu ni hili:

Wakristo waliozaliwa mara ya pili, waliotubu dhambi zao za kale, na

kuyasalimisha maisha yao kwa Yesu, je! bado wanahitaji kufunguliwa

kutoka katika nguvu za mapepo?

Kuzaliwa Mara Ya Pili Au Kutokuzaliwa Kabisa

Sijaona mahali popote kwenye Biblia Wakristo katika Kanisa la

mwanzo wakitolewa mapepo. Ama umezaliwa mara ya pili au la;

17

Sura ya II - Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo?

Page 18: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

hakuna zaidi! Kabla ya kumjua Yesu tulikuwa chini ya mamlaka

ya Shetani. Hatukumjua Mungu; na sisi sote pia tulikuwa chini ya

ushawishi wa roho za kishetani au tulitawaliwa nazo (Waefeso 2:1-5).

Mtu asiyeamini anapotubu dhambi zake na kuamini katika dhabihu

ya Yesu msalabani, Mwenyezi Mungu mwenyewe huja na kuishi

moyoni mwake. Wakolosai 1:13 inaelezea hivi: “Naye alituokoa katika

nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana

wa pendo lake.” Baada ya sisi kuzaliwa upya na Roho Mtakatifu, asili

ya Mungu inachukua nafasi ya asili ya dhambi iliyotutawala mioyoni

mwetu hapo kabla.

Mara nyingi sio lazima hata kuomba ili mtu afunguliwe. Yule

asiyeamini tayari yuko chini ya hukumu kubwa sana na yuko tayari

kuyasalimisha maisha yake kwa Kristo, kiasi kwamba anawekwa

huru kwa wepesi sana kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Mara nyingine

anahitajika kufanyiwa maombi ili afunguliwe. Kutokana na hayo

unaweza ukauliza je, maana yake nini haya madhihirisho ya nguvu

za giza leo hii makanisani? Jawabu ni kwamba watu wengi huja tu

kwa ajili ya kupokea uponyaji na kufunguliwa kutokana na nguvu za

giza, kubarikiwa, na si kumtafuta Mungu kwanza. Na kwa sababu

hawajazaliwa mara ya pili, nguvu za giza huendelea kuyatawala

maisha yao. Lakini haiwezekani kwa Wakristo waliozaliwa mara ya

pili kuendelea kuwa chini ya nguvu za mapepo, isipokuwa wamerudi

nyuma hadi kuvunja kabisa uhusiano wao na Kristo, wamemkataa

Bwana na kuzifungulia mlango kazi za mapepo mioyoni mwao na

18

Page 19: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

maishani mwao. Kwa sababu, inawezekanaje Roho Mtakatifu kuishi

kwenye mwili mmoja na pepo?

Shida nyingi na mambo mengi yanayohusishwa na mapepo yana

mizizi yake kwingineko. Kama hatupo kwenye msingi wa Msalaba

tunajikuta tukipokea kila aina ya mafundisho ya uongo na imani za

kigeni. Kwa kila jambo linaloharibika tunatupia pepo lawama.

Ni Mwili!

Ni lazima ieleweke kwamba ikiwa mimi kama Mkristo nina shida na

mwili wangu, haina maana kwamba kuna pepo ndani yangu… ila ni

kwamba tu nimeziruhusu tamaa za mwili wangu zinitawale.

Ni kweli twaweza kujaribiwa, lakini ni lazima tutofautishe kati ya

kujaribiwa na kumilikiwa na roho chafu. Ni pale tu nitakapojikana

nafsi yangu, kuwa tayari kuziachilia haki zangu na kuyapoteza maisha

yangu kwa kuuchukua msalaba wangu, ndipo nitakapopata ushindi

katika eneo husika. Sihitaji kabisa kukemewa pepo yeyote atoke,

maana tayari niko huru na mapepo!

19

Sura ya II - Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo?

Page 20: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

Maombi ya Kufunguliwa Sio Jawabu

Mungu ametufungulia njia ya kutokushindwa na miili yetu, au

kuzisikiliza tamaa zake. Ni Msalaba. Ndio maana maisha yetu

hayana uhusiano wowote na mapepo. Roho wa Mungu anaishi ndani

yetu. Yeye anatuombea na kutuwezesha, kwa neema ya Mungu,

kuusulubisha huu mwili. Kile Mungu anachotaka kufanya maishani

mwako kwa njia ya utakaso hakiwezi kupatikana kupitia maombezi

ya kutoa pepo.

Usimruhusu mtu yeyote ajaribu kukemea ndani yako pepo wa hasira,

uvivu, wivu na kadhalika. Vivyo hivyo huwezi kutatua tofauti zilizopo

kati yako na mwenzi wako, watoto wako au Mkristo mwenzako kwa

kukemewa pepo... Haya ni madhihirisho ya mwili wako, matokeo ya

maisha ambayo hayajasalimishwa kwa Bwana. Wakristo wengi leo

wamekata tamaa kwa sababu wanafahamu ni aina gani ya watu

wanaopaswa kuwa, lakini wanapoitazama hali halisi ya maisha yao,

wanahisi tu kushindwa na kukata tamaa. Hivyo wanakimbilia kwenye

kutolewa pepo. Ushindi upo katika Msalaba. Hebu kuwa na utayari

wa kuyapoteza maisha yako na utaona matokeo yake... Tunaweza

kuwa dhaifu katika maeneo mengi, lakini bado tukaudhihirisha uzima

wa Kristo. Tumewekwa huru mbali na mapepo na tunaitembelea

hiyo njia ya kuuelekea ukamilifu; Bwana apewe sifa! Kwa maelezo

kuhusiana na kazi za mwili, angalia orodha iliyoko Wagalatia 5:19-21.

Na hebu nikuambie, huhitaji kutolewa pepo ili uweze kutembea katika

ushindi dhidi ya mambo haya. Chukua tu msalaba wako.

20

Page 21: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kujifananisha Na Kristo

Ni muhimu tuweze kuelewa kusudi la ujumbe wa Msalaba kwa

maisha yetu. Ni lazima tuwe tayari kujifananisha na mauti ya Kristo

ili tuweze kuubeba uzima wake na kuwa huru. Mara tu tunapouweka

msalaba kando, tunatafuta njia za mkato, au jambo mbadala kama vile

kukemewa pepo, yaani, aina ya Ukristo wa kubonyeza kitufe. Lakini

katika Wagalatia 2:20, maneno ya Paulo, “Nimesulibiwa pamoja na

Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu;

na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa

Mungu…” ni tamko la ajabu linalodhihirisha aina ya maisha aliyoishi.

Kupitia ufunuo alioupokea, Paulo alijifunza ya kwamba alihitajika

ayafananishe maisha yake na maisha ya Kristo, ajikane nafsi yake,

ausulubishe mwili wake. Aliuishi huo ufunuo na akaweza kuuhubiri;

maisha yake yalikuwa ni ushuhuda wa mabadiliko yanayoletwa na

kazi ya Msalaba. Ujumbe wa Msalaba ni onyo la mara kwa mara na

kumbukumbu inayoufunua udhaifu wa miili yetu, na kutuwezesha

kuona hali halisi ya maisha yetu. Inatuleta kwenye toba, kujikana nafsi

na kurejea Msalabani.

21

Sura ya II - Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo?

Page 22: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

Huru Kweli Kweli!

Kwa hivyo, ndugu au dada mpendwa, ikiwa kutoka katika vina vya

moyo wako umeyasalimisha maisha yako kwa Kristo, tofautisha kati

ya udhaifu wa mwili wako na kupagawa mapepo. Unaweza ukawa

ni Mkristo dhaifu, ila tambua umewekwa huru mbali na mapepo.

Haleluya! Ndio sababu Mtume Paulo alinena sana juu ya hatari za

mwili. Alifahamu fika udhaifu wa mwili. Kumbuka, “Mwana akiwaweka

huru, mtakuwa huru kweli kweli!”

22

Page 23: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

23

Sura ya III

Mkristo na Pesa

Page 24: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

24

Kama kuna eneo ambalo Wakristo leo hii wamelaghaiwa na

kufundishwa mafundisho yenye udanganyifu, hakika ni katika eneo

la fedha na utoaji. Ni aibu kubwa kwa Kanisa kuona wachungaji

wengi wakilikosesha kundi la Mungu kwa kuwapa ahadi za uongo

za mafanikio na baraka; wakiwapotosha kwa kutumia sheria

zinazowashurutisha kutoa.

Mara nyingi nimelishutumu fundisho la mafanikio lililolivamia Kanisa,

kwenye nchi tajiri na nchi maskini. Jumbe zangu zimeelezewa kuwa

zenye utata kwa sababu nimepinga kuhubiriwa fundisho hili la uongo.

Sina tatizo kabisa Wakristo wanapotajirika kwa mali za ulimwengu

huu, na wanapobarikiwa. Lakini ninapingana vikali na mafundisho

ya kwamba ni mapenzi ya Mungu ya kuwa Wakristo wote wameitwa

kuwa matajiri. Hili linapatikana wapi kwenye Biblia? Hata Kanisa la

Mwanzo lilikuwa na Wakristo maskini. Kwa hivyo, ninaamini ni uzushi

kuwaaminisha Wakristo wote ya kwamba ni mapenzi ya Mungu wote

wawe matajiri, wote wamiliki majumba makubwa, magari ya kifahari,

n.k., au ya kwamba wanapoendelea kubaki maskini ni kwa sababu

hawana imani… uzushi kabisa! Katika maeneo kama Afrika na India,

Wakristo wengi wanaishi katika umaskini wa kutisha. Hakuna aibu

katika hilo, na haimaanishi hawana imani. Zaidi ya hilo, katika mahubiri

mengi ya siku hizi, pesa inapewa umuhimu kupita kiasi!

Page 25: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

25

Si kwamba ninalishambulia fundisho la mafanikio, lakini ninaamini

tunahitajika tuangalie Neno la Mungu kuhusu hili suala katika mtazamo

sahihi – katika kuutafuta moyo wa Mungu kwa hili. Kinachonisikitisha

zaidi ni kwamba waumini katika makanisa ambapo injili ya jinsi hii

inahubiriwa, na ambao wengi wao ni maskini, hawafiki mahali pa

kuelewa ya kwamba Mungu ana haja na aina ya moyo tulionao katika

kumtolea. Mungu humpenda mtu anayetoa kwa moyo mkunjufu, si

mtoaji tajiri!

Katika makanisa mengi sana, linapokuja suala la utoaji, watu wanaleta

sadaka zao wakitaraji kurudishiwa kwa wingi ‘walichopanda’, au

kutokana na shinikizo na hofu ya kuonekana wanaenda kinyume na

‘kile Biblia inachosema’! Ila, tunapolitazama Neno la Mungu, je! ni

wapi tunapomuona Yesu au Mitume wakizungumzia mafanikio kwa

mtazamo wa jinsi hii? Jambo lililo wazi ni kwamba Mungu ameahidi

kuyashughulikia maisha yetu (Mathayo 6:25-26); ni udhihirisho wa

moyo wa Mungu kwa watu wake na maono yake kwa ajili ya Ufalme.

Biblia sio kitabu chenye mbinu na kanuni kwa wahubiri kutumia ili

kuwaomba ninyi muwape pesa ili Mungu aweze kuwabariki.

Sura ya III - Mkristo na Pesa

Page 26: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

26

Kumpenda Yesu, Kuupenda Ufalme Wake

Mpango wa Mungu kwa Kanisa lake ni kwamba Wakristo wabebe

moyo wake uwe ushuhuda kwa ulimwengu usioamini. Kwa Mkristo

mwenye shukrani anayejua kuwa Yesu alitoa kila kitu kwa ajili yake,

ambaye moyo wake unamilikiwa na Mungu na ambaye maisha yake

yamebadilishwa na Kristo, kutamani kumtolea Mungu ni asili yake.

Si mtu anayeleta matoleo yake kwa sababu analazimika kufanya

hivyo, au kwa sababu mtu fulani amemwambia atoe kiasi fulani, au

kwa kuwa amefundishwa jinsi ya kumtolea Mungu. Na hakika hatoi

ili abarikiwe. Anatoa kwa sababu anampenda Yesu na Ufalme wa

Mungu; ana shukrani kwa ajili ya wokovu.

Maisha yake yamefananishwa kikamilifu na ya Kristo, na moyo

wake umetolewa kikamilifu katika kuyatumikia maono ya Mungu

kwa Kanisa lake. Hapa yupo mtu mwenye uwezo wa kutoa vyote,

juu sana kuliko asilimia yoyote iliyopangwa au kiwango chochote

kilichowekwa. Yeye hupanda kwa furaha katika Ufalme wa Mungu

kwa kadiri anavyoongozwa na Roho Mtakatifu. Mkristo wa aina hii

anaweza kutoa kwa ukarimu hata katika nyakati za uhitaji mkubwa,

kama tunavyoona Kanisa la Makedonia likifanya katika 2 Wakorintho

8. Anatenda huku akiamini ya kuwa Mungu atashughulikia mahitaji

yake binafsi, kwa sababu anajua moyo wake ni kwa ajili ya Ufalme.

Page 27: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

27

Mungu Anataka Tufanikiwe

Kuna vifungu viwili vya Maandiko ambavyo karibu kila Mkristo

anavijua; kwani, katika nyakati fulani, wengi wetu huenda tumesikia

vikifundishwa kuhusiana na utoaji na mafanikio. Katika maeneo

yote mawili, mafundisho ya uongo yamepenyezwa Kanisani ikiwa ni

matokeo ya wahubiri kuichukua mistari hii kwa maana nyingine…

Katika 3 Yohana 1-8 tunasoma, “Mpenzi, naomba ufanikiwe katika

mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.”

Sote tunafahamu kuwa Mtume Yohana anamsifu Gayo kwa moyo,

upendo, jinsi anavyoujali Ufalme, na ukarimu wake kwa watu wa

Mungu. Je, si ni jambo la kawaida kabisa kwa Yohana kumtaka

Mungu ambariki mtu wa jinsi hii?

Mtume anataka Gayo afanikiwe katika mambo yake yote, kwa sababu

anajua chochote anachopewa na Bwana kitatumika kuwabariki ndugu

wengine na kitakuwa na manufaa katika Ufalme. Sasa, tunarukaje

kutoka kwenye kweli hii hadi kutangaza kuwa ni mapenzi ya Mungu -

ni kusudi lake na mpango wake - kwamba Wakristo wote wafanikiwe

kifedha; kwamba Wakristo wote wanapaswa watarajie kupokea

mara mia kama malipo, endapo watatoa kwa ajili ya mhubiri huyu au

mradi ule? Hili ni kinyume na Maandiko! Tunachoweza kusema bila

shaka yo yote ni kwamba Mungu angependa kumbariki kila Mkristo,

ambaye, kama Gayo, ana moyo kwa ajili ya Ufalme, na ni mkarimu

kwa watu wa Mungu.

Sura ya III - Mkristo na Pesa

Page 28: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

28

Maono Ya Agano Jipya

Tunaposoma maneno ya Yesu katika Luka 6, tunaona roho ile ile na

moyo ule ule aliokuwa nao Yohana na mitume wengine wote. Hapa

(mistari 27-46) Yesu anazungumza na makutano kuhusu kuwa na

moyo mwingine na maono mengine... moyo na maono ya Ufalme.

Anawasihi watu kutoa maisha yao na kumruhusu Mungu awabadilishe

ili waishi sawasawa na Agano Jipya.

Kwamba, katika mtazamo huu anasema katika msitari wa 38: “Wapeni

watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na

kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani

mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”,

si sababu ya mtu kutafsiri kuwa alikuwa akizungumzia utoaji na

mafanikio. Hiki kifungu kinahusu aina ya moyo anaopaswa kuwa nao

Mkristo ambaye daima anashughulishwa na Ufalme wa Mungu. Kwa

msingi huo Yesu anamalizia, katika msitari wa 46 kwa kusema, “Na

kwa nini mnaniita Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?”

Kwa hiyo, hapaswi mtu yeyote kutumia andiko hilo kushawishi watu

ya kuwa wakitoa, bila kujali hali za mioyo yao au nia wanayotoa nayo,

ya kwamba Mungu bado anawajibika kuwabariki. Hii ndiyo maana leo

hii kuna mamilioni ya Wakristo ambao bado wanasubiri baraka zao!

Page 29: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

29

Kwa Kadri Ya Uhuru Wa Moyo Wako

Niruhusu niseme ya kwamba ikiwa bado unaamini kuwa unalazimika

kumtolea Mungu, hujaelewa undani wa kile ambacho Yesu Kristo

alifanya pale msalabani; ukombozi aliotupatia Mwana wa Mungu.

Ametuweka huru. Leo hii tuko huru kutoa kutoka katika ndani ya

mioyo yetu, kwa kadiri tunavyoongozwa na Roho Mtakatifu.

Je, unafahamu ya kuwa kama nitamtegemea mtu au sheria yoyote

katika Agano la Kale iliyo chini ya ukuhani wa ki-Lawi kuniambia ni

kiasi gani ninachotakiwa kutoa, ninaweza nikajikuta nikitoa chini zaidi

ya kiwango nilichodhamiria moyoni kutoa? Sasa katika mtazamo

halisi tunaona moyo wa Mkristo wa Agano Jipya katika tamko la

Mtume Paulo katika 2 Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende kama

alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima;

maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.” Hapa

hatuoni Mkristo mwenye hofu, na mnyimivu, anayelazimika kutoa

kwa sababu anawajibika kutoa, au kwa sababu kila mtu atafahamu

kiasi alichotoa.

Kutumika Katika Uhuru

Makanisa ya Makedonia yalikuwa na uwezo wa kutoa licha ya

umaskini wao mkubwa, ikiwa ni matokeo ya Injili iliyowafanya kukubali

Sura ya III - Mkristo na Pesa

Page 30: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

30

kupoteza maisha yao, kujikana nafsi zao, kuuchukua msalaba kila

siku na kumfuata Yesu. Ukarimu wao ulikuwa ni matunda ya kazi ya

injili, si matokeo ya kulaghaiwa kihisia. Walitamani kutoa kutoka katika

vina vya mioyo yao, na wakasisitiza kutaka kushiriki katika mradi wa

kiroho na wenye manufaa kwa Ufalme na kwa watakatifu wengine.

Tafadhali elewa kuwa sitaki kukufanya uangalie nyuma na uanze

kuhoji ni kwa jinsi gani au ni kwa lipi ulilotolea pesa zako huko nyuma.

Lakini ninaamini kuna Wakristo wengi wanaotafuta kuujua ukweli.

Nami ninachotaka ni kwa Kanisa kuujua moyo wa Mungu kwenye

suala la pesa; fundisho la kweli ni lipi kulingana na Neno lake ili, kwa

neema yake na kwa kuongozwa na Roho wake Mtakatifu, tuweze

kuwa huru kumtumikia Mungu kwa pesa zetu.

Page 31: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

31

Sura ya IV

Mungu na Muziki

Page 32: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

32

Sitakuwa ninatia chumvi nikisema ya kwamba uzi unaotenganisha

muziki wa kidunia na kile kinachoitwa ‘Muziki wa Kikristo wa Kizazi

Kipya’, ni mwembamba kwelikweli. Inasikitisha, lakini uimbaji mwingi

tunaousikia Kanisani siku hizi ni muziki wa kidunia wenye maneno

ya Kikristo.

Kwa kadiri roho wa dunia hii inavyozidi kujipenyeza Kanisani, si ajabu

kuuona muziki wake pia ukiingia Kanisani. Tunapotazama muziki na

uimbaji wa ‘Kikristo’ ulioko sasa hivi, tunapata kuona ni kwa kiasi gani

roho ya ulimwengu ilivyolivamia Kanisa. Kwa kadiri uimbaji Kanisani

unavyozidi kuchukua sura ya kidunia tunaona jinsi hili linavyoleta

kuchanganyikiwa na kumenyana, hasa kwa vijana.

Swali ninalotaka kuuliza ni: ‘Je, kuabudu halisi kuna uhusiano gani na

muziki wa kidunia?’ Ninashindwa kuelewa ni kwa nini tutake na hata

tujaribu kuyachanganya, haya mawili – kumsifu Bwana kwa mdundo

wa kidunia… kwa kweli, haiwezekani! Tunapokuwa tumezaliwa mara

ya pili, tunapaswa tutamani kuabudu kwa mioyo yetu, katika Roho na

Kweli. Jambo lolote nje ya hilo ni kuuburudisha mwili.

Kwa mara nyingine tena, ninaamini ya kwamba katika kuliangalia Neno

la Mungu tutapata ufahamu na ufunuo mpya juu ya moyo wa Mungu

katika suala la sifa na kuabudu. Hebu tuwe makini tusikaribishe kila kitu

kinachobeba nembo ‘Kristo’ ya kwamba kinampatia Mungu utukufu.

Hakuna maelekezo ya wazi katika Biblia kuhusu namna tunavyo-

paswa kumuabudu Mungu. Katika Agano la Kale kuna maagizo

Page 33: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

33

yanayohusiana na muziki, kuabudu, na vyombo vya muziki, pamoja

na mifano ya watu wa Mungu wakimsifu Mungu kwa shangwe na

kucheza; lakini katika Kanisa la Agano Jipya hakuna maelekezo juu

ya aina ya maneno, mapigo, au midundo tunayoweza kutumia; au

hata namna ya kucheza. Kuna sababu nzuri juu ya hili... kumbuka

kuwa sisi ni watu wa Agano Jipya! Kwamba ni weusi au weupe, tajiri

au maskini, wasomi au wasio wasomi, sote tuna vitu viwili vinavyof-

anana: mioyo yetu na Roho Mtakatifu aliyeko ndani yetu. Yeye ni

mwalimu wetu, anatuongoza na kutushuhudia mioyoni mwetu juu ya

nini kinachotokana na Mungu Baba na nini kisichokuwa cha Mungu.

Roho Mtakatifu Ni Mwangalizi Wetu

Katika Yohana 16:13-14, tunasoma, “Lakini yeye atakapokuja, huyo

Roho wa kweli atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana

hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia

atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye

atanitukuza mimi; kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha

habari.” Hakuna kuchanganya hapa: Ni wazi kwamba Roho Mtakatifu

ndiye anayetuelekeza, kutufundisha na kutuongoza katika namna

Yesu anavyonena na namna anavyotenda. Sote tutakubaliana kuwa

kulikuwa na harufu nzuri ya manukato katika yote Yesu aliyosema na

kufanya. Vivyo hivyo, harufu ya manukato ya kumjua Kristo inapaswa

iambatane na yote tunayosema na kufanya. Cho chote kinachotokana

Sura ya IV - Mungu na Muziki

Page 34: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

34

na dunia kina roho nyingine; lakini kwa sababu Mungu ametupa sisi

(Wakristo tuliozaliwa mara ya pili) Roho Mtakatifu kuishi ndani ya

mioyo yetu, tunaweza kupambanua roho ya ulimwengu huu ulioko

chini ya milki ya Shetani.

Mambo Ya Ajabu Yanafanyika

Ninaamini watu wanaelewa ya kuwa hata katika Ukristo kuna mambo

ya misisimko na ya kimwili yanayoendelea. Kwa bahati mbaya si kila

kitu chenye nembo ya ‘Ukristo’ ni kizuri kwa moyo wako au roho

yako. Kama ilivyo kwamba kuna aina ya uimbaji na muziki ambavyo

tunashuhudiwa mioyoni mwetu ya kuwa vinatokana na Bwana, vivyo

hivyo kuna aina ya muziki, uimbaji na kucheza ambavyo vinatoa

harufu kali ya kidunia na ya mwili. Tuwe makini tusibebe Neno la

Mungu katika hali ya maandiko tu. Neno linaposema ‘Msifuni Bwana

kwa vinanda’ au ‘Msifuni kwa kucheza na shangwe’, haina maana

kwamba tunaweza kuleta roho ya dunia Kanisani, kwa kucheza

kwa namna yoyote tunayojisikia, au kwa kutumia vyombo kucheza

midundo au mitindo ambayo huwezi kutofautisha na ile inayochezwa

katika kumbi za muziki.

Kwa kuangalia mifano michache tu ya kucheza na kushangilia katika

Biblia, ninaamini tunaweza kuona tofauti kati ya muziki na kuabudu

kunakompendeza Mungu kwa kuashiria kile kilichomo ndani ya

Page 35: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

35

mioyo yetu, na muziki unaotumbuiza tu na kulisha miili yetu, ambao

mwisho wake ni kutupeleka katika kutenda dhambi. Katika Kitabu cha

2 Samweli 6:12-15, kuhusiana na wakati ambapo Daudi aliporejesha

sanduku la agano, lililowakilisha uwepo wa Mungu katika Yerusalemu,

mistari ya 14-15 inaeleza, “Daudi akacheza mbele za BWANA kwa

nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani. Basi

Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la BWANA kwa

shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.” Daudi pamoja na watu wa

Israeli walikuwa wanasherehekea ushindi mkubwa. Kicho chake

kwa Mungu, unyenyekevu wake, pamoja na furaha ya kweli vilizidi

sana ndani yake kiasi cha kumfanya acheze, licha ya kuwa tendo

lile lilionekana kama la kipuuzi mbele ya mke wake. Watu walifurahia

kile ambacho Mungu alikuwa amefanya, walijua hii haikuwa kazi ya

mwanadamu. Daudi alipomuua Goliathi, watu wale wale waliokuwa

wakitetemeka kwa hofu ghafla walijawa ujasiri wakatoka kwenda

kuwashambulia Wafilisti. Baada ya kuwa wametoka kwenye vita

kama hiyo, tunasoma katika 1 Samweli 18:6-7 kwamba, “wanawake

wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki

Mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda. Nao

wanawake wakaitikiana wakicheza.” Katika Agano Jipya (Matendo

ya Mitume 3) Petro na Yohana walienda hekaluni siku moja, na mtu

mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa akaponywa. Mtu huyu

alishangilia kwa furaha kuu na kucheza ndani ya hekalu akimsifu

Mungu kwa muujiza wake. Hakuweza kujizuia katika furaha yake.

Sura ya IV - Mungu na Muziki

Page 36: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

36

Shangwe Itokayo Moyoni

Katika mifano yote mitatu, tunaona mlipuko wa shukrani na shangwe,

vilivyotokana na moyo wa shukrani uliosababisha kuimba, kucheza

na muziki. Ni suala la Mungu, wala si muziki. Tunaponyenyekezwa

na kile ambacho Mungu ametufanyia, tuko huru kufurahia kwa

kadiri mioyo yetu itakavyotuongoza. Hakuna tatizo juu ya kuimba na

kucheza katika mazingira kama hayo.

Lakini viongozi wa sifa wanapoamua Jumapili asubuhi kwamba

‘sasa’ ni wakati wa kuanza kumsifu Bwana kwa kucheza, au kuabudu

kwa kushawishi hisia za watu, kwa uimbaji ambao si kingine bali

ni maneno ya Kikristo yaliyoambatana na midundo ya kidunia na

yanayotupelekea katika kuigiza, ni lazima tuanze kujiuliza maswali.

Na ni vivyo hivyo kwa ‘Matamasha ya Injili’.

Je, ni nini kinachotokea kwa hawa vijana wa kike na wa kiume ambao

hisia zao na miili yao inakuwa imeamshwa kwa hali ya juu na waimbaji

walioko jukwaani? Yesu anapewaje heshima na utukufu katika

mazingira haya? Wengine wanaweza kusema hiyo ndiyo namna

vijana wa kisasa wanavyoabudu na ni njia ya kuwavuta marafiki zao

kuja kusikiliza habari za Bwana Yesu. Lakini mimi naweza kuuliza

je! ni wangapi katika hawa marafiki wanaofikia kwenye kuzaliwa

mara ya pili kwenye haya matamasha? Na, cha muhimu zaidi, je! ni

idadi gani ya hawa Wakristo vijana wanaojikuta sasa wakiwa katika

barabara ya kurudi nyuma kiroho ikiwa ni matokeo ya kuwasha tamaa

Page 37: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

37

za miili yao kupitia haya matamasha? Mimi binafsi ninapoyasikiliza

au kuyatazama matamasha kama haya, Roho Mtakatifu hushuhudia

ndani yangu kuwa kuna kitu hakiko sawa. Na sote tunajua ni nani

na ni nini kilichoko nyuma ya kila kitu ambacho hakitokani na Roho!

Hatuwezi kujificha nyuma ya ‘muziki wa injili’ unaofurahisha hisia zetu

na kuamsha miili yetu. Mwili hauwezi kutoa uzima wa rohoni, kwa

hiyo, mara tu mwili unaposisimkia aina fulani ya muziki tuko hatarini.

Sisi kama watu wa rohoni ni lazima tuweze kupambanua kati ya

muziki utokanao na Mungu - ibada ya moyoni inayojenga - na muziki

wa kidunia unaoamsha tu miili na hisia zetu.

Muziki Una Vyanzo Viwili

Kama tunavyojua, muziki unatokana na mmojawapo ya vyanzo viwili

tu. Chanzo cha kwanza ni katika moyo wa Mungu - ambapo wanaume

na wanawake, mara nyingi kutokana na kazi ya Mungu waliyoishuhudia

maishani mwao, huongozwa na Roho Mtakatifu kutunga sauti au

kuandika wimbo. Nyingi za tenzi kuu za Kikristo tulizonazo leo hii

zinalishuhudia hili. Mungu ndiye anayeumba huu muziki moyoni mwa

mwanadamu ili amwabudu na kumsifu Yeye, kumpa utukufu wote,

heshima na uweza. Upako wa Mungu unapokuwepo, mioyo yetu

inayeyuka na tunamezwa katika uwepo wake. Chanzo cha pili cha

muziki ni roho inayoutawala ulimwengu - ambapo midundo, vionjo na

miondoko ni ya kimwili na ya kidunia.

Sura ya IV - Mungu na Muziki

Page 38: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

38

Muziki ni eneo lingine la hatari sana kwa Kanisa tunapouweka

kando msingi, yaani, Injili ya Msalaba, ambayo mara zote inatupa

changamoto na kutuleta kwenye utu uzima. Tukikaa kwenye huo

msingi, kwa kadiri tunavyozidi kukua na kufanana zaidi na Kristo,

tutafahamu pasipo na shaka yo yote ni lipi tufanye, wapi pa kwenda,

na kipi cha kusikiliza. Na tutajikuta hatuvutiwi tena na muziki ambao

hauifaidi roho kwa namna yoyote.

Ninataraji ya kuwa maneno haya machache yameleta mwanga na

ufafanuzi zaidi kuhusiana na somo hili; ya kwamba kwa namna fulani

Mungu ameyafungua macho yako na umetiwa moyo

Page 39: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

39

Sura ya V

Vita ya Rohoni

Page 40: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

40

Fundisho lingine ambalo limejipenyeza Kanisani ni lile la ‘vita vya

kiroho’. Wakristo kila mahali wanatilia mkazo katika kutoa pepo na

kudhibiti roho chafu kila mahali wanakokwenda. Ikiwa tunataka kuishi

sawasawa na fundisho la uzima la Kristo, tunapaswa tuyachunguze

Maandiko tuone ni nini kilichomo moyoni mwa Mungu, na katika

mioyo ya Mitume walioandika Nyaraka.

Leo hii katika mengi ya makanisa, kuna lugha nyingi na shughuli nyingi

linapokuja suala la vita ya rohoni, na kifungu cha Biblia kinachotumika

katika hili suala ni Waefeso 6. Hata hivyo, ninapokitazama hiki kifungu,

sioni jambo lolote linazungumzia kuanzisha mapambano dhidi ya

roho wachafu. Ninachoona ni wito halisi wa Mungu juu ya maisha

ya muumini. Mtume Paulo anatuhimiza tujitie nguvu katika Bwana,

ili tuweze kusimama siku ya uovu. Mahali pengine, Mtume Yakobo

anatuagiza ya kwamba adui ashambuliapo: “Mpingeni Shetani naye

atawakimbia.”

Sehemu kubwa ya kile Kanisa linachokiita ‘vita vya kiroho’ si kingine

zaidi ya kupigana na mapepo. Wakristo wanaona hiyo kuwa ndiyo njia

ya kupata ushindi maishani mwao. Lakini, Biblia inasema waziwazi

ya kuwa ikiwa tuko ndani ya Kristo, Shetani hawezi kutugusa. Ikiwa

maisha yetu yako sawa mbele za Mungu , na mioyo yetu ni safi, ni

kwa nini tuyaogope mapepo? Tunapaswa tu kuyapinga. Tumeitwa

tuishi maisha yenye ushindi, na tutaupata huo ushindi na kupinga

mashambulizi ya Shetani tutakapoyafuata maagizo ya Yesu katika

Mathayo 16:24: “Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe,

ajitwike msalaba wake, anifuate.”

Page 41: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

41

Tunapoyaangalia Maandiko katika mtazamo sahihi, na kupata ufahamu

sahihi wa kile kilichofanyika Msalabani, tutaanza kuona nafasi yetu

na msimamo wetu katika Kristo na katika Neno lake. Ninaamini wale

wanaojishughulisha na ‘vita vya kiroho’ wanapaswa wajiulize maswali

matatu… “Vita vya kiroho ni nini hasa?” “Hili limetajwa wapi kwenye

Agano Jipya?” Na, “Je, dhabihu ya Yesu Msalabani haikutosha?”

Katika Waefeso 6, ninaamini Mtume Paulo anazungumzia maisha

ya ushindi pamoja na Bwana, maisha yenye ushindi katika haki na

maisha matakatifu yanayompendeza Mungu. Kwa namna fulani, hii

mistari imetafsiriwa kwa namna isiyo sahihi kuleta maana ya kwamba

vita ya rohoni ni sehemu ya wito wetu. Leo hii, Kanisani kumeingia

uelewa fulani ya kwamba, ikiwa tunataka ushindi, tunahitajika muda

wote kuwa vitani tukipigana na mapepo, roho chafu, na kila nguvu na

mamlaka; kufunga na kufungua roho kila tupatapo nafasi kwa sababu

wametuzunguka kila mahali.

Hebu tuangalie mistari ya 10-11: “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika

Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu,

mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana

kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka,

n.k...” Kusudi la hili andiko sio kutufundisha jinsi ya kupigana vita

ya rohoni. Wito uliopo hapa ni kwamba tuimarike, kwa sababu

adui atashambulia! Paulo anasema, ‘Muimarike katika Kristo kwa

sababu siku ya uovu imewadia.’ Mtume anaelewa fika ya kuwa vita

au mapambano yo yote maishani mwetu hakika ni ya rohoni, na

Sura ya V - Vita ya Rohoni

Page 42: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

42

wala si kitu cha kimwili au cha asili. Anatuonya mapema ya kwamba

tunapaswa kuwa hodari katika Bwana. Kwa maana nyingine, ikiwa tu

imara rohoni hatutashindwa na hila za adui.

Ufunguo wa hili ni shauku yetu ya kutaka kukua, na utayari wa

kuyasalimisha maisha yetu kikamilifu kwa Kristo. Hapo Bwana atatupa

neema ya kusimama, hata kama tu wachanga kiroho, tunapozidi

kumpinga Shetani. Mungu hatamruhusu adui avuke mpaka kwani

yeye ndiye mlinzi wetu; yeye ni ngao na mwokozi wetu. Shauku kuu

ya Paulo ni kwamba tumtumikie Bwana katika hali zote na ya kwamba

adui ashambuliapo, tuwe hodari katika imani ili tuweze kusimama

imara na kuupata ushindi.

Kumtii Mungu

Mtume Yakobo anasema katika waraka wake (4:7-8): “Basi mtiini

Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu,

naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi...”

Roho iliyoko nyuma ya mistari hii ni sawa na ile iliyo kwenye Waefeso

6; mwito ule ule, maisha yale yale, mamlaka ile ile! Anaposema

tuyatiishe maisha yetu kwa Mungu, anamaanisha kujikana nafsi zetu,

kuuchukua msalaba wetu, na hatimaye, kumpinga Shetani.

Page 43: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

43

Tutawezaje kubaki mwilini halafu tuende vitani dhidi ya mapepo, na

falme, na kudai na kufundisha ya kuwa tutapata ushindi dhidi yao?

Huku ni kuyatumia Maandiko kama mbinu, na inakwepa ukweli ya

kwamba Ukristo ni maisha tunayoishi katika roho.

Silaha Zote Za Mungu

Ni vigumu kumshinda Shetani ikiwa hautembei kwenye barabara ya

Msalaba na kumruhusu Mungu akutakase na ashughulike na mwili

wako. Unaweza ukanukuu kila Andiko, ukafunga kila pepo, ukakiri

kila msitari, ukachukua mamlaka dhidi ya kila jambo, na kufunga

na kufungua kwa kadiri upendavyo. Ikiwa maisha yako ya rohoni

yamevurugika, na hayako juu ya msingi wa Kristo aliyesulubiwa,

adui hatakimbia utakapojaribu kumpinga; badala yake, atakuingiza

dhambini na kukushinda.

Jumbe nyingi zimehubiriwa, na vitabu vimeandikwa, juu ya ‘kuvaa

silaha zote za Mungu’. Hakika hii haiwezekani iwe ni kanuni ya kimwili;

wala haihusikani na kuyanukuu Maandiko, kufunga mapepo, n.k. Si

suala la maneno hata kidogo. Silaha yetu ya rohoni inapatikana katika

hali za mioyo yetu, maisha yetu matakatifu, na roho wa maombi.

Mamlaka yetu inapatikana katika utakatifu wa maisha yetu ya rohoni.

Ushindi unapatikana kwenye barabara ya Msalaba!

Sura ya V - Vita ya Rohoni

Page 44: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

44

Kwa hivyo, je! ‘kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu

zake’ inamaanisha nini hasa kwa maisha yetu ya siku kwa siku?

Tukiunganisha yale wanayoyasema Paulo na Yakobo, ni kwamba ni

wakati tunapoyaweka maisha yetu katika mkono hodari wa Bwana.

Ni wakati tunapoifungua mioyo yetu kwa ajili ya kuupokea ufunuo wa

injili na kumruhusu Mungu kutenda kazi ndani yetu, inayotupeleka

kwenye maisha ya imani, haki, maombi, n.k. – kwa maana nyingine,

tunazivaa silaha zote za Mungu. Kwa jinsi hiyo tunaupata ushindi bila

kumenyana na mapepo mchana kutwa.

Na, Shetani anapokuja, tunahitajika tu kumpinga bila kufanya jambo

lingine zaidi. Huo ndio wito, ndugu na dada zangu. Si kuingia kwenye

mapambano ya kiroho dhidi ya mapepo…

Maisha yetu yanapokuwa juu ya msingi sahihi, tunakuwa na mamlaka

ya Mungu katika kumpinga Shetani. Kila anaposhambulia na sisi

kumpinga, Shetani hana budi kukimbia. Sote tunakubali ya kuwa

mapepo na roho chafu wapo, ila Yesu Kristo amewashinda wote

(Wakolosai 2:15). Ndio maana, maisha yetu yanapokuwa yametiishwa

kwa Mungu, hatutaogopa mapepo, wala kuyatafuta kila mahali.

Mamlaka Ya Mungu

Hebu sasa tuangalie Mathayo 16:18-19. Yesu anasema, “Nami

nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga

Page 45: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

45

kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa

wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani

litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utalolifungua duniani,

litakuwa limefunguliwa mbinguni.” Bwana wetu alimpa Petro mamlaka

kuliongoza Kanisa lake. Anamwambia, ‘Lo lote utakaloamua na

kutamka duniani kulingana na mpango wangu na mapenzi yangu, kwa

manufaa ya Ufalme, nitakutetea nikiwa mbinguni na nitalifanikisha.’

Mfano wa hii mamlaka ikitenda kazi unaonekana katika Matendo 5.

Akiwa mtu wa imani na maombi, aliyeishi maisha matakatifu na ya

haki, Petro alivaa silaha za Mungu, na akaongozwa na Roho Mtakatifu

kunena sawasawa na mapenzi ya Mungu. Akafahamu kile Anania

na Safira walichokuwa wamekifanya, na akanena kwa mamlaka ya

Mungu. Alichofunga duniani kikafungwa na mbinguni. Ninamwona

Petro akitekeleza jukumu lake la uongozi, pamoja na mamlaka

aliyopewa na Bwana.

Kumpinga Shetani

Mara nyingine tunahitajika kumpinga Shetani, na kumzuia na

kumsimamisha katika kazi zake. Lakini hii haiwezi kuwa mbinu

tutakayotumia katika maisha yetu ya siku kwa siku. Paulo na Sila

walipowekwa gerezani, hawakuanzisha kipindi cha vita ya rohoni;

Biblia inasema walianza kumtukuza Mungu.

Sura ya V - Vita ya Rohoni

Page 46: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

46

Hawakuhitaji kufunga mapepo au roho yo yote ili wafunguliwe.

Mioyo yao ilikuwa sawa, maisha yao yalikuwa kwenye utaratibu wa

roho na walimwabudu Mungu, huku wakifahamu ya kuwa ukombozi

wao ulikuwa karibu. Muda si mrefu, Mungu akalitikisa gereza na

kuwaokoa. Paulo alipofika Athene, Biblia inasema alichukizwa

na sanamu na miungu waliyoiabudu. Je, Mtume alianza kufunga

mapepo? Hapana! Alinena waziwazi, akiwaambia ya kuwa waliabudu

kila aina ya miungu, ila yeye angewaambia habari za Yule waliyepaswa

kumwabudu. Akanena habari za Mungu wake, na akawahubiria habari

za Yesu Kristo.

Tunaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume, tunaona wanafunzi

walitumia muda wao wakiihubiri Injili. Walipokutana na mazingira

ya kuhitaji kumpinga adui, walifanya hivyo na kuendelea na kazi ya

huduma. Hebu tusitekwe akili na kutumia muda mwingi tukishughulika

na mapepo, badala ya kuiishi na kuishiriki Injili, na kumtumikia Kristo

kwa mioyo yetu yote.

Page 47: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

47

Sura ya VI

Mahusiano Kabla ya Ndoa

Page 48: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

48

Kama kuna eneo Kanisani leo ambapo kuna mkanganyiko mwingi,

na ambapo kuna ushahidi ya kwamba mfumo wa ulimwengu

umejipenyeza tena na kuathiri namna Wakristo wanavyofikiri na

kuenenda, ni katika mahusiano kabla ya ndoa. Ingawa hili somo

linaweza kuonekana kama linawahusu tu vijana wanaotaraji kufunga

ndoa, ukweli ni kwamba ni jambo linalohusika na Wakristo wote.

Katika hili suala, Kanisa linaonekana kuamua kuchukua mitazamo

miwili inayokinzana kabisa. Leo hii tunaona ama sheria au uhuru

usiokuwa na mipaka. Katika baadhi ya makanisa kuna sheria kuhusu

kile watu wanachoruhusiwa kufanya au kutokufanya, ilhali katika

mengine, hilo suala halizungumziwi kabisa. Hakuna mmojawapo ya

hii misimamo ulio sahihi!

Ninaamini kwa dhati ya kwamba Kanisa limeutelekeza wajibu wake

kwa kutokuchukua msimamo wa wazi wa Kibiblia kuhusu namna

Wakristo, na hasa vijana, wanavyopaswa kuishi maisha halisi ya

Ukristo, iwe ni kabla ya au baada ya kufunga ndoa. Katika kukaa kimya

na kuruhusu viwango na fikra za kidunia kuingia Kanisani, tumeacha

kuisimamia Kweli ya Injili, na tumejichanganya. Matokeo yake ni

kwamba Wakristo wanajiingiza kwenye mahusiano yasiyokuwa ya

rohoni na ambayo hayawasaidii kukua na kumtumikia Bwana katika

njia sahihi na mara nyingi yakiwapelekea katika kutenda dhambi na

kuwaondoa mbali na mpango wa Mungu kwa maisha yao.

Page 49: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

49

Kwa ujuzi nilionao ninafahamu ya kwamba Injili inapoyakamata

maisha ya vijana, hawamenyani, au kuhisi kusukumwa au

kuchanganyikiwa juu ya kile kinachoruhusiwa katika mahusiano yao,

au ni wapi wanapaswa kuchora msitari. Kinyume chake, hawahitaji

sheria za kuwaambia ni lipi wafanye na lipi wasifanye. Wanafahamu

waziwazi mpango wa Mungu ni upi juu ya maisha yao na wanatamani

kutenda mapenzi ya Mungu, kubaki wasafi, na kuenenda katika njia

inayompendeza Mungu.

Tunapoliangalia Neno la Mungu katika mtazamo wake, ninashawishiwa

kufikiri ya kwamba dhana zetu kuhusu kuchumbiana, kuwa na marafiki

wa kike na marafiki wa kiume, na mahusiano kwa ujumla zitabadilika!

Ulimwenguni, mahusiano ya karibu ya kimwili kabla na nje ya ndoa

yanakubalika, na hata kushabikiwa. Vipindi vya uchumba vinahesabika

kama nyakati za wahusika hao wawili kuona kama ‘wanafaana’. Hili

mara nyingi linawapelekea katika kuwa na mahusiano ya kimwili kabla

ya ndoa.

Inasikitisha kwamba katika makanisa mengi vijana wanauiga mtindo

huu huu, na wale walio katika nafasi za mamlaka – viongozi wa kanisa,

wazazi, n.k., hawashughuliki na hili suala kwa umakini unaohitajika.

Vijana wanaachiwa kujiamulia wenyewe mipaka katika hili suala nyeti,

badala ya kupewa miongozo ya Kibiblia iliyo wazi.

Hebu tuwe wazi tokea mwanzo ya kwamba Mungu hachanganyikani;

Neno lake halijaficha jambo. Ndani mwake, tunaona maono na

Sura ya VI - Mahusiano Kabla ya Ndoa

Page 50: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

50

mpango wake ulio dhahiri, kwa watu wake na kwa Kanisa lake. Ni

wazi kwamba hataki tujichanganye na ulimwengu na njia zake. Na

wala Mungu hataki sheria na kuhukumiana Kanisani mwake, ambavyo

havina nguvu yoyote ya kumbadilisha mtu. Anachotaka ni Wakristo

wote wahakikishiwe na Roho Mtakatifu kuhusu dhambi kupitia Injili

ya Yesu Kristo ambayo inaweka mpaka ulio wazi na kutuonyesha

tunapaswa tusimame juu ya msingi upi. Hii ndiyo maana ninaamini

tunapaswa kurejea kwenye msingi – Neno la Mungu – ili tuone Mungu

anasemaje juu ya hili suala.

Miili Yetu Ni Viungo Vya Kristo

Hebu tuangalie Mungu anavyoiona ndoa na mahusiano nje ya ndoa,

na tutafahamu ya kwamba uhusiano wowote wa kimwili nje ya ndoa,

uwe wa aina yo yote ile, unahesabika kuwa ni dhambi machoni pa

Mungu. Si suala la ‘Tuweke wapi mipaka?’ kwa sababu tukijaribu

kuweka mipaka ya aina yoyote, tutaivuka tu. Ni kama lile tangazo

la breki za magari lisemalo, “Usianzishe jambo ambalo hutaweza

kulizuilia!”

1 Wakorintho 6:15 inasema: “Je, hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo

vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya

kahaba? Hasha!” Kwa hivyo, si roho zetu tu zilizounganika na Kristo;

nafsi yetu yote ni moja naye. Mistari ya 16 – 17 inasema, “Au hamjui

Page 51: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

51

ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana

asema, ‘Wale wawili watakuwa mwili mmoja.’ Lakini yeye aliyeungwa

na Bwana ni roho moja naye.”

Paulo hapa anasema waziwazi ya kwamba ni lile tendo la ndoa

linalowaunga watu wawili kuwa mwili mmoja, na hili linapaswa

kuchukuliwa kwa uzito. Katu hatupaswi kusahau ya kuwa roho zetu,

nafsi zetu na miili yetu imeungwa pamoja na Kristo. Siku hizi Wakristo

wengi wanafanya wanavyopenda na miili yao, pasipo kutambua

madhara ya rohoni yanayotokana na matendo yao. Kwenye kifungu

hiki Paulo anaweka utofauti kati ya dhambi ya mwili na dhambi

nyingine; katika zinaa unatenda dhambi dhidi ya mwili wako kwa

sababu unafanyika kuwa mmoja na yule mnayeunganika naye

kimwili. Uzinzi ni uhusiano wowote wa kimwili nje ya ndoa. Uongo,

wizi, hasira, n.k., ni tofauti; haya ni matunda ya tamaa zetu za kimwili.

Ikiwa Mungu aliamua kuweka utofauti kati ya dhambi ya mwili na

dhambi nyingine, tunapaswa kuwa makini sana, na kuufahamu moyo

wake katika hili suala. Msitari wa 18 unasema, “Kila dhambi aitendayo

mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda

dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.” Hatupaswi kusahau ya kuwa

miili yetu pamoja na roho zetu vimeungwa na Kristo, na tunapotenda

zinaa ni jambo zito sana machoni pa Mungu. Mistari ya 19-20

inatukumbusha ya kuwa mwili wetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na

tunahimizwa, “mtukuzeni Mungu katika miili yenu.”

Sura ya VI - Mahusiano Kabla ya Ndoa

Page 52: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

52

Mwili Unapaswa Kusulubiwa

Katika Wagalatia 5:24-25, Paulo anasema, “Na hao walio wa Kristo

wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.

Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.” Kila Mkristo ana uelewa

fulani wa maana ya haya Maandiko. Lakini kwa wale wanaotamani

kutembea rohoni, na walio tayari kuoa au kuolewa, yana maana zaidi

maishani mwao.

Tumeitwa kuisulubisha miili yetu na tamaa zake. Hii ndio maana

tunahitajika kuusikia ujumbe wa Msalaba kila wakati kwa sababu

unatukumbusha kujikana nafsi zetu na kuyapoteza maisha. Hakuna

nafasi ya kudanganyana, wala kujaribisha mambo… Sisi ni watu

waliochaguliwa ambao miili yetu ni mali ya Bwana Yesu Kristo.

Iweje, basi, tuwaze ya kuwa ni sahihi kwa watu wawili waliochumbiana

rasmi au vinginevyo, kufanya mambo wanayoruhusiwa kufanya tu

mume na mke, eti kwa kuwa wamefikia uamuzi wa kuwa wenza?

Uamuzi wa watu wawili wa kuoana huko mbeleni unapaswa umaanishe

ya kwamba wataheshiminiana kwa utimilifu mbele za Bwana. Hadi

siku ya kuoana, Bwana anawataka waishi maisha safi na matakatifu.

Vijana, sikilizeni... isipokuwa una uhakika moyoni mwako ya kuwa

uhusiano unaoingia umeanzishwa na Mungu, usithubutu kuuingia.

Ukitaka kuufahamu mpango wake kwako, na mtu aliyekuandalia

kuwa mwenza wako, fahamu ya kuwa atakufunulia.

Page 53: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

53

Mkishafahamu ya kuwa ni mpango wa Mungu muoane, na ikiwa

mnafahamu maisha ya utakatifu mnayopaswa kuishi kabla ya harusi,

hakuna hatari. Mnaweza mkachumbiana na kutiana moyo katika

kuheshimiana, kwa sababu mmehakikishiwa mioyoni mwenu ya

kuwa mnapaswa kuishi maisha matakatifu mbele za Bwana hadi

mtakapooana. Utakuwa na kicho kitakatifu cha uwepo wa Mungu

katika maisha ya mwenza wako na kufanyika kielelezo kwa wengine.

Ndio maana unapaswa uthibitike katika kile Mungu anachosema,

ili pasiwepo na kubahatisha. Je, kuna mahusiano ya aina yoyote ya

kimwili kabla ya ndoa yanayokubalika? Hasha! Neno la Mungu liko

wazi sana juu ya suala hili.

Manukato Ya Uhusiano Safi Na Mtakatifu

Labda tayari uko katika uhusiano wa kimwili nje au kabla ya ndoa, na

Bwana anakunenea ya kwamba si sahihi. Ushauri wangu ni kwamba

utubu na ufanye uamuzi imara wa kuacha mahusiano yote ya

kimwili mara moja; na usigeuke nyuma. Si jambo ambalo linafanyika

kwa awamu, wala si jambo la kuchukulia kwa wepesi. Neema ya

Mungu ipo kukusaidia. Na ikiwa ninyi wawili mnafahamu mioyoni

mwenu ya kuwa mmeandaliwa kuoana, basi jitunzeni hadi siku hiyo,

mheshimiane kama vile ndugu wa kiume anavyomheshimu ndugu

wa kike kanisani, na katika kufanya hivyo muishi maisha matakatifu

Sura ya VI - Mahusiano Kabla ya Ndoa

Page 54: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

54

na safi. Injili ya Msalaba wa Yesu Kristo inaleta jawabu, na kuchora

msitari ulio wazi katika kila jambo tunalokabiliana nalo maishani

mwetu. Inatusaidia kuenenda katika uhakikisho, na kwa maana

hiyo tunatembea katika ushindi. Wakristo wa kila rika, walio kwenye

ndoa na walio bado, wanahitajika wasikilize kwa umakini kile Mungu

anachosema katika Neno lake ili waweze kuishi maisha matakatifu

na kufanyika vielelezo kwa wengine. Je! si ni jambo la utukufu moyo

wako unapokushuhudia ya kuwa kuna hali ya usafi katika uhusiano

wa ndugu wanaotaraji kufunga ndoa? Hili linaleta harufu nzuri ya

manukato inayopendeza. Ni ushuhuda mkuu kiasi gani wa nguvu ya

Injili watu wawili wanapooana juu ya msingi huu!

Ninaamini huu ndio mpango wa Mungu kwa Kanisa lake na kwa

watoto wake. Hakuna haja ya kukata tamaa. Mungu yu hai; anaweza

kuleta watu wawili pamoja. Anajua ya mbeleni. Anajua kila kitu kuhusu

maisha yetu, na shauku yake ni sisi tuishi maisha safi na matakatifu.

Ndio maana ni heri kusubiri, kuliko kujaribisha mambo. Fungua moyo

wako; mwache Mungu azungumze na wewe na akushawishi. Kwa

Yesu Kristo hakuna kuchelewa. Leo inaweza ikawa siku yako ya

kumtangazia Bwana ya kuwa unaenda kuishi maisha yako ya Ukristo

kabla ya ndoa kwa kulifuata Neno lake..

Page 55: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

55

Sura ya VII

Barabara ni Nyembamba

Page 56: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

56

Ni kweli kwamba nimeshutumiwa mara nyingi ya kuwa ninaweka

mkazo kupita kiasi juu ya ujumbe wa Msalaba, na ya kwamba sihubiri

kingine zaidi, wakati ambapo leo hii huu ujumbe unahubiriwa kidogo

sana Kanisani. Lakini, mimi nami ningejibu hili kwa kuuliza swali: “Ni

kwa nini ujumbe wa msingi wa Yesu Kristo – kile mitume wa mwanzo

walichohubiri, na tunachosoma katika nyaraka za Paulo, Yakobo,

Yohana na Petro – ni kwa nini hicho kisihubiriwe katika kila kanisa kila

wakati?” Ujumbe wa Msalaba ndio ujumbe wa msingi wa Ukristo!

Ninaamini kwa moyo wangu wote ya kuwa kila mchungaji angepaswa

atamani kuuleta moyo wa kila Mkristo mahali ambapo ataona hitaji la

kufanyiwa kazi na Bwana moyoni mwake na maishani mwake, na pia

anamruhusu Mungu amfinyange. Kupitia hilo, huyo mtu atakua katika

sura ya Kristo na katika kuyabeba maisha ya Kristo. Hii ndio maana

kuna umuhimu kabisa wa kuuhubiri ujumbe wa Msalaba, ujumbe

wa msingi wa maisha ya Ukristo. Kutokana na kile nilichopitia mimi

mwenyewe ninaamini huwezi kuuhubiri huu ujumbe vya kutosha; kwa

sababu sisi sote kama waamini tunahitaji kukabiliwa kunakoletwa na

hii kweli, kila siku ya maisha yetu.

Page 57: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

57

Kuna Wakristo wengi mno wanaoiacha imani yao kwa kuwa tu

hawaisikii injili sahihi. Kwa kuuangalia mfano wa Kanisa la Mwanzo

katika Neno la Mungu, tunaweza tukaona ya kwamba uwepo wa

Mitume halisi waliokuwa wakihubiri Injili ya kweli kulilifanya Kanisa

liendelee kusimama kwenye msingi sahihi na katika fundisho lenye

uzima. Yesu mwenyewe alitoa tamko lisilokuwa na shaka juu ya

maisha ya Ukristo aliponena kuhusu njia nyembamba. Ni kwa nini

ujumbe wa Msalaba hauhubiriwi Kanisani leo?

“Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni

mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa

mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo

uzimani, nao waionao ni wachache.…” Mathayo 7:13.

Maisha ambayo Yesu anazungumzia katika hiki kifungu ni maisha

ya rohoni. Wakristo wote, basi, wanapaswa wasikilize kwa umakini

mkubwa anachokisema. Bwana wetu anatuonyesha barabara

tunayopaswa kuichukua ikiwa tunataka kuukwepa ‘upotevu’ pamoja

na madhara yote ya kutokumtii. Ikiwa wewe unaamini ya kuwa

maisha ya Ukristo ni ya baraka za mwilini na mafanikio – Ukristo

usiokuwa na maumivu – basi hujayaelewa maneno ya Yesu, na

ushuhuda wa maisha yake. Kitabu cha Matendo na nyaraka za

mitume zinashuhudia Wakristo wa Kanisa la mwanzo wakipita katika

nyakati ngumu, mitihani, majaribu, mateso na adha katika barabara

hii ngumu na nyembamba.

Sura ya VII - Barabara ni Nyembamba

Page 58: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

58

Kuteseka Kwa Ajili Ya Kukua

Ikiwa tunatamani kuyaishi maisha ya ufufuo, maisha ya Kristo, maisha

ya Roho, hatuna budi kukubali ya kwamba tumeitwa tuitembee

barabara inayojumuisha shida; barabara inayojumuisha mateso na

maumivu. Sisemi ya kwamba ni lazima tuyapitie maumivu ya mwilini,

bali nazungumzia maumivu yanayokuja pale Mungu anapoyachukua

maisha yetu na kuanza kuyashughulikia – tabia zetu, miili yetu,

tamaa zetu za kibinafsi na nia zetu – na tunakubali kuvunjwa na

kunyenyekezwa katika ujumla wa maisha yetu; ili, kwa neema yake,

tuanze kukua taratibu na kufananishwa na sura ya Kristo. Katika

Wakolosai 1:24, Mtume Paulo anatudokezea ni kwa nini alikuwa tayari

kulipa gharama ya kuteseka: “Sasa nayafurahia mateso niliyo nayo kwa

ajili yenu; tena nayatimiliza katika mwili wangu yale yaliyopungua ya

mateso ya Kristo, kwa ajili ya mwili wake, yaani, kanisa lake…” Mkristo

anayeikimbia changamoto hii na asiyeikubali kazi ya Kristo maishani

mwake, hawezi kutaraji kukua katika maisha yake ya rohoni. Katika

jinsi ya roho, atabakia kuwa mtoto mchanga.

Kazi Ya Utakaso

Mungu anatusihi tuipitie hii barabara nyembamba kwa sababu hapa

ndipo kazi yake ya utakaso itakapotimilika maishani mwetu. Mateso

tunayoyapata mikononi mwake si kwa ajili ya kutukandamiza au

Page 59: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

59

kutuangamiza. Tukijaribu kuyakwepa maumivu na mateso, matokeo

yake tunaweza kuishia kuangamizwa na hali ile ile tunayojaribu

kuikwepa. Wengi wetu tunataka kumfanyia Mungu mambo makubwa,

ila tunapata shida kukubali ya kwamba, Mungu alilazimika kwanza

kufanya kazi ya ndani na nzito maishani mwa wengi wa wale

aliowatumia kwa namna ya kipekee. Hebu tafakari watu mashuhuri

wa Mungu katika Agano la Kale waliotajwa katika Waebrania 11.

Wote walikabiliwa, walipita katika majaribu, mateso, adha, pamoja

na kurudiwa na Mungu: yaani, kujaribiwa kwa imani yao. Na, je!

matokeo yake yalikuwaje? Walifanyika watu mashuhuri wa rohoni,

mashujaa wa imani. Mungu yule yule anatuita tuipitie barabara ile ile

nyembamba katika siku za leo.

Kulipa Gharama

Je! unaamini ya kuwa Ibrahimu alijawa na furaha alipoamua

kumwamini Mungu na kumtoa mwanawe dhabihu? Atakuwa aliteseka

sana alipokuwa njiani wakielekea mahali pa kutolea dhabihu pamoja

na Isaka; ila aliamua kuutii mpango Mungu aliokuwa nao kwa maisha

yake, na Mungu akamzawadia. Je! Musa alilipa gharama alipoamua

kubeba shutuma ya Kristo na kuteseka pamoja na watu wa Mungu,

badala ya kuzifurahia hazina za Misri? Je! Habili alikuwa na huzuni

alipoelewa ya kuwa alipaswa kumtolea Bwana wazao wake wa kwanza

wa mifugo? Mtafakari Nuhu, je! alikata tamaa kwa sababu hakuna mtu

Sura ya VII - Barabara ni Nyembamba

Page 60: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

60

aliyemjali na wote walimdhihaki? Hapana! Watu hawa walimtii Mungu,

walipita katika mitihani na majaribu; walilipa gharama. Mioyoni mwao,

walikuwa tayari kuipitia barabara nyembamba; imani yao iliimarishwa,

na walipata kibali kwa Bwana. Leo hii, tunayafananisha maisha yetu

na mateso na kifo cha Kristo, kwa sababu tumeitwa kuipita njia hiyo

hiyo ngumu, na hatuwezi kuikwepa.

Mitihani Na Majaribu

Ninaamini hakuna maelezo sahihi kuhusu wito huu kuliko yaliyo

katika Wafilipi 1:29 ambapo Paulo anasema: “Maana mmepewa

kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake…”

Katika 2 Wakorintho 4:8-9, anasema “… Pande zote twadhikika,

bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; twaudhiwa,

bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi.” Kwingineko,

Mtume Yakobo ananena juu ya mitihani na majaribu ya imani

yetu. Hayo ndiyo mambo tunayopaswa kutarajia kwenye barabara

nyembamba. Kama Paulo, sisi pia tunajikuta tumesongwa pande

zote lakini tunasonga mbele; tukitatizwa, lakini tukimtumainia Mungu;

tukikataliwa kwa ajili ya Yesu, lakini tungali wenye furaha. Sisi pia

tunafahamu ya kuwa hatuna budi kuyapitia mambo hayo kama Yesu,

Mitume, na Wakristo wa Kanisa la Mwanzo walivyopitia; hili ndilo

fungu letu. Huu ndio Ukristo halisi! Mara tunapoamua kumfuata Yesu,

tunaitwa tuyafananishe maisha yetu na mateso yake. Yesu alituonya

Page 61: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

61

mapema ya kuwa mambo yangekuwa hivyo. Lakini, wakati kila jambo

linapoonekana kugubikwa na giza na hali inakuwa ya kukatisha tamaa,

hebu tukumbuke ya kuwa kuna kusudi katika hayo yote. Katika hayo

tutauona ukombozi wa Mungu wetu na katika hayo tutakua rohoni.

Kusudi La Mateso

Waebrania 12:4 inasema: “Hamjafanya vita hata kumwagika damu,

mkishindana na dhambi.” Kwa maana nyingine, mioyoni mwenu

hamjafika mahali pa kuchukizwa na dhambi kabisa kabisa. Katika 1

Petro 4:1 tunasoma: “Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake,

ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika

mwili ameachana na dhambi.” Ili kuelewa kinachozungumziwa katika

hii mistari, ni lazima tuikamate roho wa Injili. Vinginevyo, haitakuwa

rahisi kwetu kuelewa ni kwa nini tunaitwa kushiriki katika mateso ya

Kristo. Hakika Yesu hakutaka tu tupite katika mateso na shida bila

sababu.

Ni lazima kutakuwepo na kusudi, lengo, katika haya mambo. Nalo ni

nini? Matunda ya maisha ya jinsi hii ni uzima wa Kristo ndani yetu; ili

tuweze kufanana naye. Paulo anasema katika Wafilipi 2:5, “Iweni na

nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo…”; kwa

maana nyingine, iweni na nia aliyokuwa nayo Yesu, alipojinyenyekeza

na kuonja kifo cha Msalaba. Matokeo yake ni kwamba Mungu

alimwadhimisha mno.

Sura ya VII - Barabara ni Nyembamba

Page 62: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

62

Kufanyika Kielelezo

Hatimaye, hebu tuangalie Waebrania 12:5-6, ambapo tunahimizwa

kutoyadharau marudia ya Bwana, kwani anatutendea kama wana,

wa kike na wa kiume... Ikiwa tunatamani kuhesabika kama wana

nyumbani mwa Mungu Baba yetu na kupata kibali kwake, ni lazima

tumruhusu atufinyange na kuturudi. Mwandishi anamalizia hiyo

sura kwa kuzungumzia maumivu yatokanayo na marudia; si wakati

wa furaha, tunateseka Mungu anapotuvunja na kutufinyanga,

anapofanya kazi maishani mwetu, lakini hili huleta matunda ya haki,

maisha matakatifu; matunda ya utakaso. Katika kuichukua barabara

nyembamba, hatuna budi kukubali ya kuwa ni jambo ambalo Mungu

ametuandalia, ili tuwe mifano, na vielelezo kwa ulimwengu.

Barabara Ya Utakaso

Hii ndiyo barabara ya utakaso. Tunatakaswa, na kufanyika zaidi na

zaidi kama Kristo. Kwenye hii barabara nyembamba, pamoja na

makemeo, marudia na maonyo yake – yanayoelezewa kuwa ni ‘kwa

faida yenu’ – ndipo tunapoandaliwa “tuushiriki utukufu wake”, na

kuleta “matunda ya haki yenye amani” Waebrania 12:10-11.

Hakuna njia nyingine ya kushughulika na dhambi yetu isipokuwa ni

kuyafananisha maisha yetu na mateso ya Kristo. Tunaweza kuwa na

Page 63: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

63

uhakika wa kukua katika Ukristo wetu na kufanyika watu wa rohoni

pale tu tutakapoichukua barabara nyembamba, na kudumu juu yake.

Hii ndiyo siri ya maisha yenye ushindi.

Sisi watu wa Kanisa tunapaswa kubadili mtazamo wetu, na tuache

kuendelea kuikwepa barabara nyembamba. Ni sehemu ya mpango

maridadi kabisa Mungu alionao kwa ajili yetu. Na hapo, kama wale

mashujaa wa imani waliotajwa katika Waebrania 11, tutakuwa na

uhakika wa kusimama imara, na kuzikamilisha mbio zetu. Kamwe

tusisahau ya kwamba barabara nyembamba ndiyo iendayo uzimani!

Sura ya VII - Barabara ni Nyembamba

Page 64: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

64

Page 65: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

65

Sura ya VIII

Kanisa Litakabiliwa

Page 66: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

66

Ninapoiangalia hali ya Kanisa la leo, nina hakika Wakristo wengi

wanahuzunishwa na kile wanachokiona. Kwa namna nyingi hakuna

utofauti kati ya mwenendo wa Wakristo wa karne ya 21 na maisha

waliyoishi wana wa Israeli enzi za Yeremia na manabii wengine wa

Agano la Kale. Katika siku za leo inaonekana ya kwamba, mara

nyingine tena, watu wa Mungu wanaelekezwa katika kufukuzia

mambo yasiyowafaidi.

Siku hizo, kutokana na upendo wake kwa watu wake, Mungu alituma

watu kuwaonya juu ya hatari za yale waliyokuwa wakifanya na athari

za kuendelea kumpinga. Leo tumebarikiwa kwa kuwa na Neno la

Mungu, Biblia, inayotuonya, kutuhimiza na kututia moyo. Zaidi ya

hayo, tunayo mifano ya Yesu Kristo, pamoja na Kanisa la Mwanzo,

inayotutia nguvu kubaki kwenye hiyo ‘barabara nyembamba’.

Zaidi ya hayo pia, tuna ujumbe wa Msalaba – nguvu ya Mungu –

unaotuwezesha kuishi maisha yenye ushindi na kulinda fundisho

la uzima. Kutokana na hilo, hakika inasikitisha kuona Wakristo

wakitafuta baraka ‘zinazopita’ ilhali ‘nguvu ya Mungu’ ipo kwa ajili

yao. Ushuhuda wa Kanisa dhaifu, na lililojaa migawanyiko, hakika

hauwezi kumfurahisha Mungu. Isipokuwa Kanisa liurudie ujumbe wa

msingi wa Ukristo, litaendelea kupeperushwa na kila upepo wa elimu

unaojitokeza.

Nina hakika ya kwamba Mungu anataka kutuonya juu ya baadhi

ya mambo yanayoendelea Kanisani katika siku za leo. Katika siku

Page 67: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

67

tunazoishi Kanisa litakabiliwa: katika mwenendo wake, katika mahubiri

na mafundisho yake, na katika namna Wakristo wanavyohimizwa

kuyaishi maisha yao. Imani yangu ni kwamba kupitia kuhubiriwa kwa

ujumbe wa Msalaba, watu wa Mungu watakabiliwa.

Katika siku zake, nabii Yeremia, kupitia maagizo aliopewa na Mungu,

hakuacha kuwaonya Waisraeli juu ya kile ambacho kingewapata

kama wangeendelea katika njia zao zenye uovu. Wakati ule walikuwa

wakifukuzia vitu vingine vingi badala ya Mungu. Yeremia 1:9-10

inasema, “...Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;

angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa,

na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.”

Sote tutakubaliana ya kuwa mara nyingi maonyo huja wakati mambo

yanahitajika kubadilika. Katika siku hizi za mwisho, ninaamini Kanisa

litakabiliwa katika namna linavyomtumikia Mungu, na katika mambo

yanayoivuta mioyo ya watu wa Mungu!

Neno la Mungu linasema ya kuwa mambo yaliyofanyika katika vizazi

vya nyuma yalikuwa ni mifano kuvionya vizazi vya mbeleni. Kwa mfano,

katika 1 Wakorintho 10:11 tunamwoma Mtume Paulo akitamka ya

kuwa mambo yote yaliyowapata Waisraeli jangwani yaliandikwa kwa

ajili yetu, sisi waamini wa Agano Jipya; “Basi mambo hayo yaliwapata

kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na

miisho ya zamani.” Tunaishi katika nyakati ambapo maisha ya juu juu,

au ya kurushwa huku na huku na kila aina ya upepo, hayana nafasi

tena. Vinginevyo tutajikuta tukivutwa na ulimwengu haraka sana,

Sura ya VIII - Kanisa Litakabiliwa

Page 68: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

68

pamoja na mafundisho ya uongo, na hatimaye kunaswa katika mtego

wa adui.

Tunafahamu kilichowapata wana wa Israeli kutokana na kutotii kwao

na uasi wao. Lakini hata hivyo wao, pamoja na viongozi wao wa

kiroho, walipewa onyo baada ya jingine. Katika Yeremia 2:8 Mungu

anawakemea waziwazi kwa kutafuta mambo ambayo hayatawafaidia:

“Makuhani hawakusema, Yuko wapi BWANA? Wala wana-sheria

hawakunijua; wachungaji nao waliniasi, nao manabii walitoa unabii

kwa Baali, wakafuata mambo yasiyofaidia kitu.” Mungu anarudia tena

kemeo lake katika msitari wa 11, “Je! taifa wamebadili miungu yao,

ingawa si miungu? lakini watu wangu wameubadili utukufu wao kwa

ajili ya kitu kisichofaidia.” Nina hakika unatambua ya kuwa mali ya

kidunia haiwezi kutuletea badiliko la rohoni, au kutuleta katika utu

uzima rohoni na ukamilifu katika Kristo! Ndio maana wakati umefika

Kanisa likabiliwe na ujumbe wa Msalaba wa Yesu Kristo; injili pekee

inayoshughulika na mwili, inayokabili maisha yetu na hali za mioyo

yetu; na inayotupa kuyatamani mambo ya Roho yatakayotufaidia.

Katika msitari wa 13 Mungu anawakemea watu wake: “Kwa maana

watu wangu hawa wametenda maovu mawili; wameniacha mimi,

niliye chemichemi ya maji ya uzima, wamejichimbia mabirika,

mabirika yavujayo, yasiyoweza kuweka maji.” Birika linalovuja halina

kazi yoyote. Vivyo hivyo na sisi leo, tunajenga maisha ya ubatili kwa

kutafuta vitu ambavyo tumeaminishwa Kristo atatupatia, badala

ya kuutafuta uzima wake; uzima wa ufufuo, uzima wa Roho. Mimi

Page 69: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

69

sina neno na wale Mungu mwenyewe anaoamua kuwabariki na

kuwafanikisha, hasa ninapofahamu ya kuwa shauku ya mioyo yao

ni kuubariki Ufalme. Lakini, ninapata shida Wakristo wanapohimizwa

kutafuta mali ya ulimwengu huu badala ya uzima wa Roho. Hata hivyo,

hakuna mahali kwenye Biblia tunapohimizwa kutafuta mali ya dunia;

kinyume chake, katika Wakolosai 3:1-2 Paulo anatuagiza waziwazi,

“Basi ikiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo

aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Yafikirini yaliyo juu, siyo

yaliyo katika nchi.”

Kukemewa Na Kukabiliwa

Ni wazi kwamba si kila mtu atakayepokea makemeo kwa moyo wa

toba. Mungu alimtahadharisha Yeremia kwamba ujumbe aliokuwa

awaletee watu ungezua upinzani mkubwa. Yeremia 1:19 inasema,

“Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo

pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe.” Waisraeli walikuja kinyume

na kile alichokuwa akisema; hasa kauli yake ya kuwa alichokuwa

akisema kilitoka kwa Mungu. Kwa sababu mioyo yao ilikuwa mbali

na Mungu, Waisraeli walikataa kusikiliza; walifurahia kukimbizana na

mambo yaliyoiridhisha miili yao. Matokeo yake ni kwamba walimpinga

Yeremia kwa muda wa miaka 40! Kanisa la Yesu Kristo la mwaka 2010

lina hali inayofanana na hiyo: watu wa Mungu wanahimizwa kutafuta

vitu visivyoweza kuwatosheleza kiroho. Wakati huo huo, Msalaba wa

Sura ya VIII - Kanisa Litakabiliwa

Page 70: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

70

Yesu unapohubiriwa leo hii, unaleta mwanga Kanisani; unakemea; na

ndio maana, si ajabu, watu wengi hawaupendi.

Msalaba Ndio Msingi

Wahubiri wanapounda fundisho kutokana na vitu vya juujuu,

wanaondoa hamu ya kukua kiroho mioyoni mwa Wakristo.

Msalaba wa Yesu Kristo unapaswa uwe sehemu ya maisha ya wale

wanaosimama madhabahuni. Na Wakristo wanapaswa kulishuhudia

hilo; ya kwamba hawa watu wamevunjwa, na wanaendelea kuvunjwa

na Mungu; ya kwamba wamefanyika mifano, vielelezo; na ya kwamba

hawaneni tu elimu ya kibiblia. Hii ndio maana ujumbe wa Msalaba

unapaswa kurudi Kanisani sasa, ili mioyo ya Wakristo irejeshwe kwa

Kristo; hadi kuyafananisha maisha yao naye katika kuteswa kwake na

kifo chake. Hii ndiyo njia pekee ya kuushiriki uzima wa ufufuo, ambao

ni maisha ya Kristo anayoyaishi ndani yako na ndani yangu… tumaini

la utukufu!

Kuna hicho kipengele cha mateso na kifo ambacho kwa kiasi kikubwa

kimepotea Kanisani; huo ndio ujumbe wa Msalaba. Hatuwezi

kuukimbia. Ukristo unaotosheka tu na kuja kanisani, kubarikiwa, na

‘kuwa na wakati mzuri’ na wenzako kabla ya kutoa sadaka yako, kwa

kweli hii ni dini tu! Inanihuzunisha, ila ninaamini ya kuwa mengi ya

mambo yanayoendelea Kanisani leo hii ni dini tu; mikakati, kanuni,

Page 71: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

71

mbinu, vyote vikiwa vimetokana na hekima ya mwanadamu…

kinachosikitisha zaidi ni kwamba katika mengi ya makanisa, pesa

ndio msingi wa kila kitu. Biblia inatamka waziwazi ya kwamba ujumbe

wa Msalaba ndio msingi wa maisha yetu ya Ukristo. Neno la Mungu

lina mengi zaidi kwa ajili ya roho zetu badala ya kuhubiri mfululizo

kuhusu mafanikio, pesa, kutoa na baraka.

Waalimu Kumi Elfu…

Katika 1 Wakorintho 4:14-15 Paulo ananena na Wakorintho wa mwilini

waliokuwa wamerudi nyuma katika kuwakumbusha na kuwaonya:

“Siyaandiki hayo ili kuwatahayarisha; bali kuwaonya kama watoto

niwapendao. Kwa maana ijapokuwa mna waalimu kumi elfu katika

Kristo, walakini hamna baba wengi. Maana mimi ndiye niliyewazaa

katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili.” Kila mahali alikokwenda aliweka

msingi mmoja tu na alihubiri injili moja katika makanisa yote: Injili ya

Msalaba. Hawa Wakorintho walifahamu fika kile Mungu alichotaraji

kutoka kwao, na kazi aliyohitaji kufanya ndani yao, ili wafanyike

wanafunzi, watumishi, na vielelezo kwa ulimwengu uliowazunguka.

Msalaba unapokosekana, mlango unakuwa wazi kwa mioyo yetu

kuvutwa na mambo yasiyokuwa na faida. Hilo ndilo lililowapata

Wakorintho. Walisikiliza injili nyingi. “Mnaweza kuwa na waalimu kumi

elfu.” Katika msitari wa 15 Paulo alikuwa anamaanisha: ‘Mmesikiliza

wahubiri wengi, mmesikiliza imani nyingi, mmejifunza mbinu nyingi;

Sura ya VIII - Kanisa Litakabiliwa

Page 72: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

72

lakini angalieni hali yenu… kuna vita, wivu, na zinaa kati yenu!’

Mara tu unapouondoa msingi wa msalaba, matokeo ni Wakristo

wanaoenenda mwilini; waliorudi nyuma na walioshindwa!

Ikiwa hujazaliwa katika Injili ya Msalaba, utaitafsiri Biblia kwa manufaa

yako binafsi. Hautataka kusikia juu ya mitihani na majaribu, adha, na

mateso; juu ya kukemewa, kuonywa na kutubu; juu ya kuifia nafsi.

Mfano mzuri wa hili ni wakati Wakristo wanaponukuu Wafilipi 4:13,

“Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” Wanachokazia

tu ni ile sehemu ya kwanza ya hili andiko: ‘Nayaweza mambo

yote.’ Lakini hebu tuangalie andiko zima tukianzia msitari wa 10…

”Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha

tena fikra zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali

yangu; lakini hamkupata nafasi. Si kwamba nasema haya kwa kuwa

nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo

nayo. Najua kudhiliwa tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na

katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa

na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye

nguvu.” Katika kuliangalia kwa ukaribu, tunaona kitu tofauti kabisa,

linazungumza habari za Paulo alivyoubeba msalaba wake. Mazingira

yo yote kwake – wingi au uchache – na kwa moyo mnyenyekevu,

neema ya Mungu na nguvu za Mungu vilimpitisha katika hayo yote.

Hii neema itakuwepo katika hali zote, nzuri au mbaya. Hiyo ndiyo

roho, ndio moyo, ambao Paulo anawasilisha hapa; huu ndio moyo wa

Kristo, roho wa Injili.

Page 73: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

73

Kumfahamu Kristo

Usipozaliwa katika Injili ya kweli, utapata shida kukubali kile Mungu

anachotaka kwako. Mwili wako utang’ang’ania vitu vya mwilini, na

utakuzuia katika kuyafananisha maisha yako kikamilifu na Kristo.

Katika Wafilipi 3:10-11 Paulo anasema, “…ili nimjue yeye, na uweza

wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa

na kufa kwake; ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.”

Tunawezaje kusema, sisi kama Wakristo, ya kuwa tunataka kumjua

Kristo pasipo kuwa tayari kuyafananisha maisha yetu na maisha

yake? Kama ilivyokuwa kwa Paulo, vivyo hivyo na sisi pia, tunaitwa

katika ushirika wa mateso yake, ili tuweze kuushiriki uzima wa ufufuo.

Vinginevyo, tutakuwa tunanena tu juu ya kule kuzaliwa mara ya pili.

Lakini, hatuwezi kuishia tu hapo… kwani katika msitari wa 15 Paulo

ananena zaidi ya kuzaliwa mara ya pili. Anatuhimiza kuwa na hali ya

moyo ambapo, hata kama hatuelewi sana au kukubaliana na ufunuo

wa Kristo na namna tulivyoitwa kujifananisha na yeye katika mateso

yake, kifo chake na kufufuka kwake, bado tunaweza kumwamini

Mungu kwamba atatufunulia anachohitaji kutufunulia.

Sura ya VIII - Kanisa Litakabiliwa

Page 74: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

74

Msalaba Ndio Uzima Wako

Ninakutia moyo, mpe Mungu nafasi, kwa njia ya Yesu Kristo,

aidhihirishe nafasi stahili ya Msalaba wake maishani mwako, kama

anavyosema katika Mathayo 16:24: “Mtu yeyote akitaka kunifuata,

na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.” Maisha yetu

ya Ukristo yanapaswa kuwa na msingi mmoja tu: “Yesu Kristo naye

amesulubiwa!”

Page 75: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

75

Sura ya IX

Yesu Anaita Tena

Page 76: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

76

Ni jambo la kawaida kwa mwanadamu kutaka starehe na utoshelevu,

na kutotaka mabadiliko. Sisi kama Wakristo tunaweza tukawa na hali

iyo hiyo kuhusu mwenendo wetu na Mungu; watu waliotosheka na

wanaoishi maisha mepesi katika mfumo wa Ukristo uliozoeleka.

Ninaamini kwa dhati kabisa ya kuwa wimbi lingine la Mungu linakuja

hivi karibuni na ya kwamba Wakristo wanapaswa wafahamu mambo

yaliyoko mbeleni. Ni lazima tuelewe pia ya kuwa kila wimbi la Mungu

huambatana na kutetemeshwa. Mwanzoni miili yetu itataka kulipinga

jambo hili. Lakini wale wanaotamani kwa dhati kumtumikia Mungu na

kumfuata, watakuwa tayari kukubali chochote atakachotaka kwao.

Ni lazima tuhakikishe ya kuwa kwamba tu wachungaji, viongozi au

Wakristo ‘wa kawaida’, tunamtafuta Bwana na kutaka kujua kile Roho

Mtakatifu anacholiambia Kanisa leo.

Bila shaka, Mungu anatuita tulete ujumbe utakaowalisha watu wake;

utakaowafikisha katika utu uzima na uhuru katika Kristo. Ikiwa Yesu

anarudi hivi punde, hatakuja kulichukua Kanisa lisilokuwa na nguvu

wala utakatifu. Ujumbe wa Msalaba ndiyo Injili pekee yenye nguvu

ya kulibadilisha Kanisa na maisha ya Wakristo; na kuwaleta katika

kuichukua sura ya Kristo.

Katika historia ya Kanisa, zimekuwepo nyakati na majira ambapo

Mungu aliwaita wanaume na wanawake kwa makusudi mbalimbali

ili kutekeleza mapenzi yake hapa duniani. Nina hakika ya kwamba

huu sasa ni wakati ambapo Yesu anawaita wanaume na wanawake

kuupokea ujumbe mahsusi, ufunuo: injili ya Msalaba, fundisho la

msingi la Ukristo.

Page 77: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

77

Yesu ana mpango na maono kwa Kanisa lake, na anataka yatimizwe.

Kwa bahati mbaya, anapoita, si kila mtu anayesikiliza au kujali…

Lakini hili halimzuilii, kwa sababu mipango yake ni lazima itekelezwe.

Haiyumkiniki kwamba Yesu atalijia Kanisa butu lisilokuwa na

uhai; na, zaidi ya hapo, Kanisa lililostarehe, lililojitosheleza, lililojaa

udini. Atachagua wanaume na wanawake; atawaita, na kuwapa

changamoto, vile vile kama alivyowachagua wanafunzi 12 waanzishe

Kanisa. Alimwita pia Mtume Paulo kwa kusudi maalum: “Lakini

Mungu…akaniita kwa neema yake…ili niwahubiri Mataifa habari

zake…” Tazama Wagalatia 1:15.

Muda wa Mungu wa kufanya jambo unapowadia, hulifanya. Katika

miaka 40 au 50 iliyopita, Mungu alileta ufunuo mpya kwa Kanisa;

ulikuwa mzuri nasi tunamsifu kwa huo. Lakini, je! tunaona nini leo?

Tunaona Kanisa lililopoteza nguvu yake, utakatifu, na kutengwa

kwake na ulimwengu. Ni nini kilichochukua nafasi? Kuchanganyikana,

dhambi, mafundisho ya uongo, na misisimko! Lakini, tena, Yesu

anawaita wanaume na wanawake ambao atawafunulia ujumbe wa

kweli wa Msalaba, ili waweze kuishi maisha halisi yenye ushindi, na

watakaoihubiri hiyo injili na kuitetea. Si kwa bahati mbaya, basi, ikiwa

wewe binafsi unahisi ya kwamba maisha ya Ukristo si tu kustarehe na

kukubaliana na kila jambo linalofanyika Kanisani siku hizi.

Sura ya IX - Yesu Anaita Tena

Page 78: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

78

Jambo Jipya

Roho Mtakatifu anabisha kwenye mioyo ya Wakristo wengi; viongozi

wa makanisa, wanaume na wanawake, duniani kote; watu waliochoka

na ambao hawakubali ya kuwa Kanisa la Yesu Kristo halina zaidi ya

hiki wanachokiona. Ninaamini kwa moyo wangu wote ya kuwa kuna

jambo jipya, jambo zuri, ambalo Roho Mtakatifu anajiandaa kuinenea

mioyo ya hawa Wakristo. Tayari yuko kazini, akiandaa mioyo kuipokea

Injili ya Msalaba wa Yesu Kristo, hata kama tunaweza tusiione hiyo

kazi. Nina hakika ya kuwa Wakristo wengi wanahisi mioyoni mwao ya

kuwa kuna jambo jipya, jambo tofauti, linalokuja.

Wengine wenu mnaweza kuwa hata mmewaza ya kuwa haya mawazo

yanatokana na uasi ndani yenu, au ya kwamba mna uhuru binafsi katika

kutokukubaliana na mengi ya yale yanayohubiriwa madhabahuni leo

hii. Unajiuliza maswali... juu ya maisha yako ya Ukristo, na hali ya

moyo wako. Huyu ni Yesu anayeita! Hapa hatuzungumzii wito kwa

ajili ya huduma, bali ni Yesu anayekuita kama Mkristo uishi maisha ya

injili ya kweli, umruhusu Mungu kuikamilisha kazi ile njema aliyoianza

ndani yako.

Page 79: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

79

Adui Za Msalaba

Lakini, kama ilivyokuwa siku za Mtume Paulo, wengi watasikia na

kupinga mahubiri ya ujumbe huu na watakuwa ni adui za Msalaba;

tazama Wafilipi 3:18: “Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni

mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi kuwa

ni adui za msalaba wa Kristo…” Inasikitisha kwamba si wahubiri

au Wakristo wote walio tayari kuupokea ujumbe wa Msalaba na

changamoto inayoletwa na maisha ya Ukristo.

Daima kutakuwepo na watu ndani ya Kanisa watakaoinuka na

kupingana na kile Mungu anachotaka kufanya. Kuanzia enzi za

Luther wakati wa Matengenezo hadi leo upinzani umekuwepo ndani

ya Kanisa; maadui wamepingana na kile Mungu anachotaka kufanya

Kanisani mwake. Matokeo yake, tutakutana na wale wanaoamini ni

jukumu lao ki-imani kuyapinga mahubiri ya injili ya Msalaba.

Msalaba Pekee

Paulo anasema katika 1 Wakorintho 2:2, “Maana naliazimu nisijue

neno lo lote kwenu, ila Yesu Kristo, naye amesulubiwa.” Injili ya

Msalaba ndio msingi wa Ukristo; hii Injili ndiyo iliyowapa changamoto

Wakristo katika Kitabu cha Matendo. Leo, Yesu anaita tena. Vile

vile kama Paulo anavyonena katika Wagalatia 1:11 jinsi alivyopokea

Sura ya IX - Yesu Anaita Tena

Page 80: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

80

ufunuo moja kwa moja kutoka kwa Yesu Kristo, ninaamini Bwana

anachagua wanaume na wanawake, anawatenga, anaiandaa mioyo

yao na kuwafunulia ujumbe wa Msalaba.

Huu ujumbe ndio ufunuo ule ule uliokuwepo katika Kanisa la

Mwanzo; unawaalika Wakristo kuitika na kujisalimisha; kujihesabu ya

kuwa wamepoteza maisha yao na kutoshikilia kitu cho chote. Huu

ushawishi wa moyoni unatokana tu na injili ya Msalaba. Wanaume

na wanawake wataanza kusoma Maandiko na kuyafananisha maisha

yao na kile wanachokisoma. Viongozi wa makanisa watayadhihirisha

maisha yao madhabahuni, na kuikiri kazi ambayo Mungu anahitaji

kufanya maishani mwao. Wakristo kutoka kila rika na kabila wataanza

kufahamu ya kuwa Ukristo wa kweli unahusu kupoteza maisha yetu

ili Yesu aishi ndani yetu. Zaidi na zaidi wachungaji na washirika

watakubali ya kwamba injili hii ndiyo iliyokosekana Kanisani leo hii.

Si Ujumbe Mpya

Yesu alifundisha ya kwamba barabara ni nyembamba na ya kwamba

kuna gharama katika kumfuata, inayojumuisha kujikana nafsi, mateso,

adha, na kuyapoteza maisha yako. Wakristo wanapoanza kufahamu

ya kwamba Mungu anataka kuwaumba katika sura ya Mwanawe

watakuwa tayari kuikubali kazi anayotaka kufanya maishani mwao.

Kama Kanisa tutatambua ya kuwa mwenendo wetu hauna uhusiano

Page 81: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

81

na sisi, bali yeye – Yesu akiishi ndani yetu; ni kujifananisha na yeye

kikamilifu. Katika Warumi 6:3-4, Paulo anasema ya kuwa tulizikwa

pamoja na Kristo kwa njia ya ubatizo, na ya kwamba tunapaswa

tuenende katika upya wa uzima, kama Kristo alivyofufuliwa kutoka

kwa wafu. Tunaposhiriki mauti yake, tunashiriki pia katika uzima

wake. Huu ndio upya wa uzima; huu ndio uzima wa Kristo! Haya ndiyo

maisha ya ushindi ambayo Yesu anatuitia… utimilifu wa Kristo ndani

yetu! Huu ndio ujumbe waliohubiri Mitume wa kwanza, na ambao ndio

Kanisa la Kwanza lililouishi. Ujumbe huu si mgeni; utaukuta kwenye

kila tafsiri ya Biblia.

Kufanya Uamuzi

Watu wengi wataanza kuusikia wito na watakabiliwa na uamuzi.

Wengine watasikia na kuupinga wito, lakini wengi watasikia na

kuuitikia. Kwa hao ataifunua injili ya kweli na hitaji lao la kujifananisha na

Kristo. Pamoja na upinzani na adha zitakazowakabili, watakapoanza

kuhisi Yesu akiita, watajawa na shauku ya kuyaishi hayo maisha.

Fahamu zao zinaweza zikataka kujadiliana, lakini mioyo yao itasema,

‘Ndiyo, Bwana. Niko tayari kulipa gharama ya kukufuata, kuiishi hii

injili; kufanyika udongo mikononi mwa mfinyanzi; kubadilishwa,

kutetemeshwa, kugeuzwa; kufanyika kama wewe, Bwana Yesu.’

Watawatafuta wale wanaoishi na kuihubiri Injili. Wataona utofauti ulio

Sura ya IX - Yesu Anaita Tena

Page 82: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji Kujua

82

wazi kati ya injili ya kweli ya Yesu Kristo na injili nyingine zote watu

wanazohubiri na kuziishi.

Katika Wafilipi 1, Mtume Paulo anasema aliitwa aitetee injili. Katika

kuuitikia wito wa Yesu, wewe pia utalazimika kuweka msimamo

na kusema: ‘Hiki si sahihi; yale siyo mafundisho yenye uzima!’

Utakabiliana na watesi na upinzani, lakini kwa neema ya Mungu

utashinda. Hivyo ndivyo Paulo alivyoweza kusema: “Lakini kwa neema

ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo… bali nalizidi sana kufanya kazi kupita

wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.”

Kuuitikia Wito Wake

Yesu anaita tena leo. Anabisha kwenye mlango wa moyo wako na

anakuandaa uwe tayari kuuitikia huo wito. Ni upendeleo wa jinsi gani

huo, ni heshima kuu kiasi gani! Je! uko tayari kuitikia wito wake?

Page 83: Kanisa Linahitaji Kujua (Swahili)

Kanisa Linahitaji KujuaM

iki Hardy

Kanisa Linahitaji Kujua

Hebu sote tukubaliane ya kwamba kwa namna moja au nyingine Kanisa

limeliacha fundisho la uzima, na matokeo yake yanaonekana katika

maisha ya watu wa Mungu.

Viongozi wengi wameathiriwa na mafundisho ya mafanikio ya miaka ya

hivi karibuni, na wanatafuta kujinufaisha wenyewe. Wengine hawatambui

ya kwamba injili ya Msalaba ndiyo nguvu ya Mungu itakayowafikisha

Wakristo katika utu uzima rohoni.

Umefika wakati tuyazungumzie mambo fulani ya msingi waziwazi, ili

Wakristo watambue ya kwamba Bwana ana mambo mazuri zaidi kwa ajili

yao, makusudi watembee katika uhuru na katika ushindi!

9 789994 901814

ISBN 978-99949-0-181-4

Church Team Ministries International | Trianon, Mauritius(230) 403 4500 | [email protected] | www.ctmi.org

CTMI ni mtandao wa Kikristo usio rasmi ulioanzishwa mwaka 2001 na timu ya viongozi kutoka nchi mbalimbali barani Afrika waliounganishwa pamoja na ujumbe wa msalaba na kazi ya Mungu maishani mwao.