jamhuri ya muungano ya tanzania ofisi ya rais tawala … ya ukaguzi wa... · v) ujenzi wa vyumba 8...

104
JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA MKOA WA DAR ES SALAAM TAARIFA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZWA NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA HADI KUFIKIA ROBO YA TATU KWA KIPINDI CHA MWAKA 2016/17 Imetayarishwa na: Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 3 Barabara ya Rashid Kawawa, S. L. P. 5429 12880 DAR ES SALAAM. Mei, 2017

Upload: others

Post on 09-Jan-2020

23 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MKOA WA DAR ES SALAAM

TAARIFA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZWA NA MAMLAKA

ZA SERIKALI ZA MITAA HADI KUFIKIA ROBO YA TATU KWA KIPINDI CHA MWAKA

2016/17

Imetayarishwa na:

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,

3 Barabara ya Rashid Kawawa,

S. L. P. 5429

12880 DAR ES SALAAM. Mei, 2017

YALIYOMO UK.

1. UTANGULIZI: … … … … …… … … … … … 1

2. TAARIFA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI

ZA MKOA WA DAR ES SALAAM … … … … … … … 1

3. CHANGAMOTO ZA JUMLA ZILIZOJITOKEZA WAKATI WA UKAGUZI WA

MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI NA USHAURI ULIOTOLEWA … 4

4. VIAMBATISHO: … … … … … … … … … 8

4.1 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA KINONDONI … … … … … … 8

4.2 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA UBUNGO … … … … … … … 25

4.3 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA ILALA … … … … … … … 50

4.4 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA TEMEKE … … … … … … … 92

4.5 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA KIGAMBONI … … … … … … 106

4.6 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

JIJI LA DAR ES SALAAM … … … … … … … 131

4.7 ORODHA YA WALIOSHIRIKI KATIKA UKAGUZI WA MIRADI YA

MAENDELEO … … … … … … … … 136

1.0 UTANGULIZI

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ilifanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo

inayotekelezwa na Halmashauri za Manispaa zote za mkoa hadi kufikia robo ya tatu kwa

kipindi cha mwaka 2016/2017. Ukaguzi huo ulianza tarehe 25 Aprili hadi tarehe 25 Mei,

2017. Jumla ya miradi 62 ilitembelewa kwa mchanganuo ufuatao: Kinondoni miradi 15,

Ubungo miradi 11, Ilala miradi 15, Temeke miradi 11, Kigamboni miradi 8 na Halmashauri

ya Jiji miradi 2. Miradi iliyotembelewa katika Halmashauri ni pamoja na miradi ya sekta za

Barabara, Maji, Elimu, Afya, Usafi/Usafishaji, Ukarabati wa majengo ya Serikali na Masoko.

Katika kutembelea miradi hiyo, Timu ya Ukaguzi iliongozana na Katibu Tawala wa Mkoa na

shughuli zote za ukaguzi ziliratibiwa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na

Uratibu.

Nyaraka zilizohitajika wakati wa ukaguzi ni pamoja na:-

a) Mpango wa bajeti na Mpango Kazi (Action Plan) ya Halmashauri kwa mwaka

2016/2017,

b) Mkataba na michoro kwa kila miradi iliyokaguliwa,

c) Taarifa za utekelezaji kwa mwaka 2016/2017 hadi kufikia Machi, 2017 kwa kila

miradi (Physical & Financial), na

d) Historia ya mradi husika kutoka kwa msimamizi.

Ukaguzi wa miradi ya maendeleo ulianza katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

tarehe 25 Aprili, 2017 na kumalizika katika Halmashauriya ya Jiji la Dar es Salaam tarehe

25 Mei, 2017. Tarehe za ukaguzi kwa kila Halmashauri zipo kwenye maelezo ya kila

Halmashauri husika.

2.0 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA KINONDONI

Utangulizi.

Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri hii ulianza tarehe 25 hadi 27 Aprili,

2017. Shughuli za Ukaguzi zilianza kwa Mchumi wa Manispaa kutoa taarifa kwa ufupi ya

miradi itakayotembelewa kwa kuelezea lengo la kila mradi, tarehe ya kuanza na

kukamilisha mradi, gharama za mradi na fedha zilizotolewa na zilizotumika. Jumla ya miradi

15 ya maendeleo ilitembelewa ambayo ni kama ifuatavyo:-

i) Ujenzi wa mradi wa Maji Makongo Mbuyuni

ii) Ujenzi wa madarasa 12 Shule ya Sekondari Mivumoni Kata ya Wazo

iii) Ujenzi wa vyumba 6 vya madarasa Shule ya Sekondari Kondo Kata ya Kunduchi

iv) Upanuzi wa wadi ya Wazazi katika Zahanati ya Kijitonyama katika Kata ya

Kijitonyama

v) Ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa Shule ya Msingi Bunju A katika Kata ya Bunju

vi) Ujenzi wa machinjio ya Kuku awamu ya pili katika Kata ya Kawe

vii) Ukamilishaji wa ujenzi wa Soko la Kisiwani katika Kata ya Makumbusho

viii) Ujenzi wa vyumba 4 vya madarasa Shule ya Sekondari ya Salma Kikwete katika

Kata ya Kijitonyama

ix) Ujenzi wa Wodi ya Wazazi Hospitali ya Mabwepande awamu ya kwanza

x) Ujenzi wa Tanuru ya kuchomea taka katika Zahanati ya Boko

xi) Ujenzi wa jengo la upasuaji katika Hospitali ya Mwananyamala

xii) Ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa Shule ya Sekondari ya Mzimuni awamu ya

kwanza katika Kata ya Mzimuni

xiii) Ukaguzi wa barabara ya Arsenal kwa magoti

xiv) Ukaguzi wa barabara ya Polisi Mabatini

xv) Ukaguzi wa barabara ya Magomeni – Sinza

2.1 Ujenzi wa Tanki la Maji Makongo Juu - Mtaa wa Mbuyuni

Utangulizi

Mradi wa Maji Makongo Mbuyuni upo katika Kata ya Makongo Juu Mtaa wa Mbuyuni.

Lengo la mradi ni kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa Makongo

Mbuyuni. Mradi ulianza Februari, 2016 na ulikamilika Agosti, 2016. Mkandarasi aliyejenga

mradi huu ni M/S EDGE POINT Company Ltd na JV REMO (T) Ltd. Kiasi kilichotengwa kwa

ajili ya ujenzi wa mradi ni Tsh. 195,980,000 183 na kiasi kilichotolewa ni Tsh.

183,190,068.00.

a) Utekelezaji

Mradi umekamilika na unatoa huduma ya maji kwa Wananchi wa Makongo Mbuyuni.Awali

kilichimbwa kisima chenye urefu wa mita 100.Ujenzi umejumuisha Tanki lenye ujazo wa lita

40,000 lenye uwezo wa kuhudumia watu 7,200, vituo vya kuchotea maji (DP’s) 14,ufungaji

wa Pampu na mtandao wa mabomba yenye urefu wa Km 2.567. Aidha, kuna Kamati ya

maji yenye wajumbe wanane (8)

b) Changamoto

Changamoto zinazokabili mradi huu ni upatikanaji wa maeneo ya ujenzi wa miundombinu

ya maji.

c) Maoni

Hatua stahiki ya kuchukua ni kushirikisha wananchi katika hatua zote za mradi kuanzia

wakati wa kubuni mradi, kuandaa mpango wa utekelezaji na ujenzi wa mradi na usimamizi

wa matumizi ya mradi.

Picha Na.1: Ujenzi wa Tanki la Maji lenye ujazo wa lita 40,000 katika mradi wa maji Makongo- Mbuyuni

2.2 UJENZI WA VYUMBA VINNE VYA MADARASA SHULE YA SEKONDARI

SALMA KIKWETE.

Utangulizi:

Mradi huu wa ujenzi wa madarasa unajengwa kwa thamani

ya Sh. 68,000,000 sawa na sh. 17,000,000 kwa chumba. Mpaka sasa ujenzi umefikia hatua

za ukamilishaji (rangi, sakafu na vyumba vya usalama).

Ujenzi huu ni mpango wa kupunguza uhaba wa vyumba 10 vinavyotakiwa hapa shuleni

a) Utekelezaji:

Mkataba wa ujenzi kati ya shule na ‘local fundi’ ulifanyika mnamo tarehe 24/01/2017 na

ujenzi ulianza mara moja. Ujenzi ulitakiwa uwe umekamilika majuma matano baada ya

kusainiwa mkataba 28/02/2017). Uongozi wa shule unamshukuru Mkuu wa Wilaya,

Mkurugenzi na uongozi wa Halmashauri kwa ujumla kwa kuwaletea mradi huu. Hata hivyo

mradi ulishindwa kukamilika kwa wakati kutokana na changamoto mbalimbali lakini kubwa

ikiwa ni ucheleweshaji wa idhini ya malipo. Fundi aliomba muda wa nyongeza mpaka

tarehe 20/04/2017 ingawa bado hajaweza kukamilisha ulipaji kutokana na changamoto za

kitaalam zinazokwamisha ulipwaji wa fedha kulingana na mahitaji halisi ya kazi. Mnamo

tarehe 25/4/2017 kamati ya ujenzi ilikutana kwa dharura kujadili changamoto hizo na kuja

na mapendekezo halisi ya kuwezesha kukamilisha mradi.

- Kupitia upya BOQ ili kufanya marekebisho kulingana na hali halisi iliyojitokeza kazini

(omition or addition)

- Kupewa BOQ ya bei elekezi ili iweze kukwamua tatizo hilo.

Ujenzi utaendelea pindi mambo hayo mawili yatakapofanyiwa kazi.

Mpaka sasa ujenzi umefanyika kwa viwango vilivyowekwa na Idara ya Ujenzi.

b) Changamoto:

Changamoto tulizokutana nazo mpaka sasa ni mbili;

i) Maelezo yasiyokamilika toka idara ya ujenzi hasa katika suala la ujazaji wa gharama

katika BOQ hali ambayo imesababisa upotevu wa muda.

ii) Ucheleweshwaji wa idhini ya malipo (certificate) hali ambayo imesababisha usubufu

mkubwa na upotevu wa muda.

c) Maoni

Ushauri uliotolewa na Timu ya Mkoa ni kuwa wasimamizi (Idara ya Elimu na Uhandisi)

kufanya kazi kwa uwazi na ushirikiano ili kwa pamoja waweze kufikia malengo kwa wakati

na kiwango kilichokusudiwa.

1.3 MRADI WA UJENZI WA JENGO LA WAZAZI (MARTENITY BLOCK) KATA YA

MABWEPANDE.

Utangulizi

Mradi huu ulianza rasmi tarehe 04/8/2016 ukilenga kujenga Jengo la Wazazi na Hospitali

ya Kanda (Zonal Hospital) ikitarajiwa kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD),

wagonjwa wa kulazwa na huduma zote zitakiwazo katika ngazi ya Hospitali.

Mradi huu ulipangwa kugharamia kiasi cha Tshs. 974,997,704.40 ili kuweza

kukamilika kwa kuanza kutoa huduma zote kwa wananchi.

a) Utekelezaji

i) Ujenzi wa mradi wa Jengo la Wazazi Kata ya Mabwepande.

kwa Awamu ya kwanza umekamilika.

ii) Wakati mradi huu ukiendelea kutekelezwa, huduma zinaendelea kutolewa kwenye jengo

la zamani ambalo hutoa huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD) ambapo Wananchi

wapatao 19,234 kutoka sehemu mbalimbali za Kata ya Mabwepande pamoja na

wananchi waliopata mafuriko mwaka 2011-2012 hupata huduma katika Hospitali hii.

b) Changamoto.

i) Stoo ya dawa inahitajika kufanyiwa mgawanyo (partition) ili kupata chumba cha

kuhifadhi dawa na kutolea dawa.

ii) Hakuna chumba cha mapokezi na kuchukulia kadi kwa wagonjwa.

iii) Hakuna sehemu ya kupimia watoto.

iv) Hakuna “Incinerator” ya kuchomea taka

v) Ukosefu wa chumba cha kujifungulia katika jengo hili.

c) Maoni

Mradi huu ni muhimu sana, hivyo Halmashauri iukamilishe haraka ili wananchi wapate

huduma zote za afya zilizopo katika hadhi ya Hospitali

Picha Na.2: Jengo la linalojengwa la Wazazi (Martenity Block) Kata ya Mabwepande.

Picha Na.3: Sehemu ya kupandia (ramp) kwa kutumia “wheel chair” wodi ya wazazi katika Hospitali ya

Mabwepande

1.4. MRADI WA UJENZI WA WODI YA WAZAZI KATIKA ZAHANATI YA

KIJITONYAMA

Utangulizi

Zahanati ya Kijitonyama ilianza kujengwa rasmi mnamo mwaka 1978 na kuanza kutoa

huduma mwaka 1979 chini ya ufadhili wa Serikali ya Canada.

Kutokana na ongezeko la mahitaji ya huduma za Afya katika katika eneo hili, Zahanati ya

Kijitonyama ilipata mfadhili ambaye MDH (Management and Development of Health), na

alikubali kusaidia kufanya ukarabati mkubwa na upanuzi wa wodi ya jengo la wazazi

kituoni. Mradi ulianza Mwezi Machi 2016, na kukamilika mwezi Juni 2016.

Jengo hili la wazazi lina sehemu kuu tatu:-

i) Sehemu ya wajawazito kusubiri kabla ya kujifungua (Ante Natal Care)

ii) Chumba cha kujifungulia (Labour Room)

iii) Chumba cha uangalizi baada ya kujifungua (Post Natal Care)

Jengo hili la kisasa la wazazi limegharimu kiasi cha Tshs. 155,700,000 (Milioni Mia Moja

hamsini na tano na laki saba), ambapo MDH wamechangia Tsh. 120,000,000/= kwa ajili ya

ukarabati na Halmashauri imechangia Tsh. 35,700,000/= kwa ajili ya ununuzi wa vifa tiba.

Jengo lilikabidhiwa kwa Manispaa rasmi Desemba 2016. Huduma katika jengo hili lilianza

kutolewa mwezi Desemba 2016, ambapo Jumla ya wajawazito 73 wamepokelewa na

kupata huduma salama ya kujifungua pasipo na matatizo yoyote hadi sasa.

a) Utekelezaji

i) Manispaa kwa kushirikiana na wadau ina mpango wa kuiendeleza zahanati hii

kupanda hadhi na kuwa kituo cha afya (Urban Health Center)

ii) Kujenga chumba cha upasuaji ili kuweza kutoa huduma za upasuaji wa dharura kwa

kina mama wanaoshindwa kujifungua kwa njia ya kawaida.

b) Changamoto

i) Hakuna tanuru yenye vigezo vinavyotakiwa ya kuchomea taka “Incinerator”

ii) Hakuna chumba cha upasuaji “Theatre”

iii) Idadi ya Vitanda kwa kinamama wajawazito havitoshi

c) Maoni

i) Manispaa wajenge tanuru ya kuchomea taka “Incinerator” kwani iliyopo haifai na

haikidhi vigezo.

ii) Kujenga chumba cha upasuaji “theatre” kwa ajili ya kusaidia upasuaji wa dharura.

iii) Kuingiza kwenye bajeti ujenzi wa Hospitali ya Kisasa kwa usanifu wa ghorofa.

Picha Na.4: ujenzi wa Wodi ya Wazai katika Zahanati ya Kijitonyama

1.4. MRADI WA UJENZI WA JENGO LA UPASUAJI KWA WAZAZI KATIKA

HOSPITALI YA MWANANYAMALA

Utangulizi

Hospitali ya Mwananyamala ilianza kama kituo cha kutolea huduma za afya ya mama na

mtoto (MCH) mwezi Julai 1973. Na kupandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa

Novemba, 2010. Kwa sasa Hospitali hii inahudumia wakazi wa Manispaa ya Kinondoni na

Manispaa zingine ikiwemo Manispaa ya Ubungo pamoja na wale wanaotoka Wilaya

nyingine za Tanzania. Kwa wiki wanatibu takribani wagonjwa 15,000.

Hospitali inatoa huduma za uzazi kwa akina mama kati ya 100 hadi 120 kwa siku, kati yao

akinamama 8-10 wanahitaji huduma za upasuaji wa dharura kila siku, na kwa wiki idadi ya

akinamama wanaohitaji huduma za upasuaji ni kati ya 58 hadi 60.

Jengo hili la upasuaji ni sehemu ya utatuzi wa changamoto za ufinyu wa nafasi za kulaza

wagonjwa pamoja na uchache wa vyumba vya upasuaji, lakini pia lina mazingira mazuri na

ya kisasa kwa ajili ya kutolea huduma kwa mama na watoto.

a) Utekelezaji

i) Ujenzi wa jengo umekamilika na Idara ya Afya ya Manispaa tayari imekwisha agiza

vifaa vya upasuaji kutoka Bohari Kuu ya Dawa na malipo yamekwisha fanyika

ambapo baadhi vimeletwa na vingine wanatarajia kuvipokea mwanzoni mwa mwezi

Juni, 2017. Vifaa hivi vimegharimu kiasi cha Tshs.182, 691,344/=.

ii) Ujenzi wa jengo hili umegharimu Tsh. 302,128,001/= kwa ufadhili wa GSM kupitia

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul C. Makonda. Jengo hili linatarajia

kuanza kutumika kuanzia mwezi Juni, 2017 wakati vifaa vyote vitakapofika.

iii) Ujenzi wa jengo hili umefanyika kwa takribani miezi kumi, kuanzia tarehe 13 Machi,

2016 na kukamilika mwishoni mwa mwaka 2016 na kuzinduliwa tarehe 29 Januari,

2017.

Picha Na.5: Kibao kinachoonesha ujenzi wa jengo la upasuaji katika Hospitali ya Mwananyamala

Picha Na.6: Jengo la upasuaji katika hospiatali ya Mwananyamala

b) Changamoto

i) Jengo halina viyoyozi

ii) Jengo halina Masinki ya kunawia na kufulia na kuoshea vifaa

iii) Pia hakuna makabati ya kutunzia vifaa

iv) Hakuna Meza

c) Maoni

i) Mkurugenzi ajitahidi kununua vifaa vyote ambavyo havipo katika jengo la upasuaji

(theatre).

ii) Hospitali ianzishe “fast track” kwa wagonjwa ambao wanapenda kutibiwa kwa

uchangiaji kwani inaweza kuongeza mapato ya Hospitali.

1.5 MRADI WA UJENZI WA VYUMBA 5 VYA MADARASA SHULE YA SEKONDARI

MZIMUNI

Utangulizi

Mradi wa ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa Shule ya Sekondari Mzimuni ni utekelezaji wa mradi

huu awamu ya pili. Mradi ulifunguliwa kwa uwekaji wa jiwe la msingi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es

Salaam ambapo wakati huo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni tarehe 10 Januari, 2016. Lengo

la mradi huu ni kuwa na Shule ya Sekondari katika Kata ya Mzimuni. Kata ya Mzimuni itaweza

kupata shule ya Sekondari ambayo itaondoa usumbufu wa Wanafunzi wanaomaliza shule za msingi

na kwenda kusoma Kata za mbali.

a) Utekelezaji

Mkataba wa ujenzi ulisainiwa mwezi Desemba, 2016 na makubaliano ya mkataba ni kuanza kazi

tarehe 06 Desemba, 2016. Ujenzi ulitarajiwa kukamilishwa tarehe 07 Aprili, 2017. Mkandarasi

aliyepewa kazi ya ujenzi ni Nyakwe Constuction kwa gharama ya Sh. 246,621,740.00. Hadi siku ya

ukaguzi fedha aliyolipwa ni Sh. 104,000,000. Ujenzi umefikia hatua ya kumimina zege katika

ghorofa ya kwanza.

b) Changamoto

Ujenzi umesimama kutokana na nyaya za umeme kupia katika eneo la ujenzi ambapo mwendelezo

wa ujenzi wa kuta utakwamishwa na nyaya hizo.

c) Maoni

i) Mwalimu Mkuu wa Shule kuwasiliana na TANESCO ili kuondoa nguzo ya umeme

inayokwamisha ujenzi.

ii) Mkurugenzi wa Halmashauri awezeshe kufanyika kwa haraka kuhamisha nguzo ya

umeme ili ujenzi uweze kuendelea

Picha Na.7: Ujenzi wa Shule ya Sekondari Mzimuni iliyozinduliwa na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

tangu Januari, 2016.

Picha Na.8: Ujenzi wa Shule ya Sekondari Mzimuni ikionesha nyaya za umeme zilizokatisha katika eneo la

ujenzi.

1.6 MRADI WA KUBORESHA MIUNDOMBINU KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA KINONDONI - DMDP

Utangulizi

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ni miongoni mwa Halmashauri za Manispaa tatu za

Mkoa wa Dar es Salaam zinazotekeleza Mradi wa kuboresha Miundombinu katika Jiji la Dar

es Salaam kupitia fedha za Serikali kupitia mkopo wa Benki ya Dunia ujulikanao kama “Dar

es Salaam Metropolitan Development Project – DMDP). Halmashauri za Manispaa nyingine

zinazotekeleza mradi huu wa DMDP ni Ilala na Kinondoni.

Mpango huu una maeneo makuu manne ambayo ni:

i) Ukosefu wa Miundombinu

ii) Kuinua makazi ya watu wenye vipato vidogo (upgrading in low income

communities)

iii) Kujenga uwezo (Institutional Strengthening and Capacity Building)

iv) Kusaidia usimamizi katika utekelezaji na Tathmini (Implementation Support and

Monitoriong & Evaluation)

a) Utekelezaji

Mtaalam Mshauri M/S Guff Engineering amekamilisha mapitio ya usanifu na kutengeneza

nyaraka za zabuni kwa miradi ya mafungu matatu (3 package):-

Fungu la I: Barabara za Sokoni – Makumbusho - Km. 1.45, MMK – Km. 0.9, Nzasa – Km.

1.25, Viwandani – Km. 1.68, TANESCO – Soko la Samaki – Km. 1.58.

Fungu la II: Barabara za Makanya – Km.5.1, Tandale –Kisiwa – Km 0.8, Kilimani – Km.1.3,

Simu 2000 – Km. 1.3, Kilongawima Km. 1.8 na Makumbusho CBD) – Km. 0.9.

Fungu la III: Barabara za External Km. 1,65, Kisukuru Km. 1.9, Korogwe – Kilungule – Km.

2.88, Maji ya Chumvi – Kilungule Km. 2.85.

Katika utekelezaji wa kazi hizi, fungu la kwanza ambalo halikuwa na ulipaji wa fidia

linaendelela na ujenzi, ambapo Manispaa ya Kinondoni iliingia Mkataba na Kampuni ya

Estim kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha lami kuanzia tarehe

18/01/2017 kwa muda wa mwaka mmoja. Kazi ambayo imefanyika ni uwekaji wa lami

barabara ya Sokoni – Makumbusho uumbaji wa tuta kwa barabara za viwandani Km. 1.68

na TANESCO Soko la Samaki Km. 1.58. Aidha, fungu la II na III linahitaji fidia.

b) Changamoto

Kuchelewa ulipaji wa fidia kwa baadhi ya nyumba ili kupisha mradi kuanza.

C) Maoni

Halmashauri kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya kulipia fidia kwa maeneo ambayo mradi

unapita ili mradi uweze kuanza.

2.0 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA UBUNGO .

UTANGULIZI.

Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Ubungo ulianza tarehe 03 hadi 05 Mei,

2017 ambapo jumla ya miradi 11 ilitembelewa. Ifuatayo ni taarifa ya kila mradi uliotembelewa

ikiwa inaonesha utangulizi, utekelezaji, mafanikio, changamoto na maoni.

2.1. Mradi wa ujenzi wa Barabara ya Riverside – Kibangu kwa kiwango cha lami

Utangulizi.

Mradi upo katika Kata ya Ubungo Mtaa wa Kibangu. Mradi huu ni utekelezaji wa ahadi ya Mhe.

John Joseph Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati

alipotembelea eneo hilo na kukuta hali mbaya ya barabara katika Kata hii. Kukamilika kwa

barabara hii kutaondoa tatizo la usafiri na kuboresha miundombinu ya barabara.

a) Utekelezaji

Kipande cha barabara kilichotengenezwa kwa kiwango cha lami kina urefu Km. 1. Mradi

umekamilika kwa asilimia 100. Kiasi cha fedha kilichotengwa na kutumika ni Sh.

1,200,000,000.00 fedha ambazo ni msaada wa Mhe. John Joseph Pombe Magufuli, Rais wa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, Halmashauri imetenga katika bajeti ya mwaka

2017/18 kiasi cha Sh. 600,000,000.00 kwa ajili ya kuendeleza kujenga barabara hiyo (km 0.5)

likiwa ni ombi la wananchi wa maeneo hayo.

b) Mafanikio

Kukamilika kwa mradi huu wa barabara yenye urefu wa Km 1 kumerahisisha shughuli za

usafiri na usafirishaji kwa wakazi wa maeneo ya Kibangu, Riverside, Makoka n.k. Pia usumbufu

wa kuharibikiwa na vyombo vya usafiri kwa sababu ya ubovu wa barabara umepungua.

c) Changamoto

i) Maji ya mvua yanayokusanywa kwenye mifereji iliyotengenezwa kando ya barabara

yameelekezwa kwenye makazi ya watu.

ii) Uwepo wa nyumba za wakazi kwenye eneo la barabara ambao inatarajiwa

kuendelezwa.

d) Maoni

i) Timu ya ukaguzi ilishauri Mkurugenzi wa Halmashauri kuwapongeza wakazi wa

Kibangu ambao walitoa maeneo yao wakati wa kupanua barabara bila kulipwa fidia

ii) Mkurugenzi atume wataalam kufanya tathmini ya nyumba mbili kwa ajili ya kulipa fidia

ili ujenzi wa kipande cha Km 0.5 uweze kufanyika.

Picha Na.1: Ujenzi wa Mradi wa Barabara ya Riverside Kibangu (1 Km) – Kata ya Ubungo

Picha Na. 2: Nyumba zinazotakiwa kufanyiwa tathmini na kulipwa fidia ili kukamilisha

ujenzi wa barabara ya (River side – Kibangu yenye urefu wa 0.5 Km)

2.2 Ujenzi wa Choo Matundu 12 Shule ya Sekondari Saranga Kata ya Saranga

Utangulizi

Katika kuimarisha suala la usafi katika Kata ya Saranga hasa kwenye shule ya sekondari

ya Saranga, Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo iliazimia kujenga matundu 12 ya vyoo

yaliyogharimu kiasi cha sh. Milioni 32

a) Utekelezaji

Ujenzi wa choo hicho umekamilika lakini usanifu uliotumika ni mbovu kwa sababu vyoo

vya desin ya kuchimba shimo chini na kuta kujengwa juu, vimekuwa vikibomoka kwa

kutitia chini. Mfano wa vyoo hivi vilivyotitia vipo katika shule za msingi za

Malambamawili na Bunju ‘B’ (katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni).

b) Mafanikio

Ujenzi wa vyoo hivyo umekamilika na vinatumika.

c) Changamoto

i) Hakuna milango kwa ajili ya kuimarisha ulinzi pindi wanafunzi wanapokuwa

nyumbani

ii) Choo kimejengwa kwa usanifu ambao si salama sana kwa mipango ya muda mrefu

(Vyoo vingi vinavyojengwa kama hivi huwa vinadidimia mfano wa vyoo

vilivyobomoka ni pamoja na choo cha shule ya msingi Malambamawili (Picha Uk .

iii) Hakuna chumba cha kubadilishia nguo/pedi kwa wasichana wanapokuwa hedhi

iv) Hakuna sehemu ya kunawia mikono kwa wanafunzi baada ya kutoka chooni.

d) Maoni

i) Usanifu wa ujenzi wa vyoo ubadilishwe ili kuepusha madhara pindi choo hicho

kitakapotitia pamoja na kuokoa gharama zisizo za lazima

ii) Walimu wahusika na suala la afya na mazingira shuleni wahakikishe shule inakuwa

na vibuyu mchirizi au waige “best practice” ya shule ya msingi Kibamba, pamoja na

kuweka mazingira kwa ajili ya wanafunzi wa kike kubadilishia pedi.

Picha Na. 3.Ujenzi wa matundu 12 ya choo katika shule ya Sekondari Saranga

Picha Na. 4: Ujenzi wa matundu 12 ya choo katika shule ya Sekondari Saranga

2.3 Ujenzi vyumba 8 vya madarasa katika Shule ya Msingi Temboni

Utangulizi

Katika shule ya Msingi Temboni upo uhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa. Lengo

la mradi huu wa Ujenzi vyumba 8 vya madarasa ni kupunguza msongamano wa

wanafunzi madarasani ambao wanakaa takribani 130 hadi 170 katika darasa moja.

a) Utekelezaji

Ujenzi wa vyumba vitano (5) umekamilika na ujenzi wa vyumba vitatu (3) haujaanza

mpaka wakazi wa eneo hilo walipwe fidia

b) Mafanikio

Wanafunzi wameanza kutumia vyumba vya madarasa 5 yaliyokamilika hivyo kupunguza

msongamano wa wanafuzni hadi kufikia wanafunzi 70 – 80 kwa darasa.

c) Changamoto

i) Mwinuko wa eneo la mwisho wa veranda ambao hauna vyuma vya vizuizi.

ii) Sakafu ya darasa moja haitoi maji nje kwa kutiririsha.

iii) Mbao za kuandikia baadhi haziko katika ubora unaostahili na pia Ash-board haipo.

iv) Vyoo vinajengwa kwa usanifu wa “ shimo chini Jengo juu”- vyoo hivi mara nyingi

vinaleta athari na havidumu kwa muda mrefu (Mfano choo cha shule ya msingi

Malambamawili)

d) Maoni

i) Vizuizi viwekwe ili wanafunzi wasianguke.

ii) Kuboresha sakafu na mbao za kuandikia pamoja na marekebisho mengine.

Picha Na. 5: Ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa katika shule ya Msingi Temboni

Picha Na. 6: Ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa katika shule ya Msingi Temboni

34

Picha Na. 7: Ujenzi wa matundu ya choo unaoendelea katika shule ya Msingi Temboni

Picha Na. 7: Ujenzi wa matundu ya choo unaoendelea katika shule ya Msingi Temboni

35

2.4 Ujenzi vyumba 8 vya madarasa katika Shule ya Msingi Malambamawili

Utangulizi

Kufuatia tatizo la uhaba wa madarasa katika shule msingi Malambamawili

kutokana na wingi wa wanafunzi katika eneo hilo, Halmashauri Mama ya

Manispaa ya Ubungo ambayo ni Kinondoni ilikuja na mpango wa kuanzisha

shule mpya ambapo madarasa 8 kati ya 10 yaliyopangwa kujengwa

yamekamilika. Mpango huu ulianza katika kipindi cha mwaka wa fedha

2015/16 na kukamilika mwaka 2016/17 kwa jumla ya Sh. Milioni 178. Aidha,

shule hiyo inapendekezwa kuitwa shule ya msingi Bwawani kulingana na

mazingira ya ki-jiografia ya mahali ilipo.

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika lakini madarasa hayana ‘ceilingboard’ na vyoo pia hakuna

b) Mafanikio

i) Ujenzi umekamilika na unatumika vile vile inatarajiwa kuwa shule mpya

mara baada ya taratibu za usajili zitakapokamilika. Imependekezwa iitwe

shule ya msingi Bwawani kulingana na hali ya ki-jiografia ya mahali

ilipojengwa.

ii) Kukamilika kwa madarasa hayo kumesaidia kupunguza idadi kubwa ya wanafunzi waliopo katika shule hiyo wanaofikia 3,754 (Darasa la I-VII).

c) Changamoto

i) Uhaba mkubwa wa vyoo kwa kuwa Matundu 8 kati ya 12 yametitia. ii) Ceiling board hakuna na “ash chalk” haikuwekwa. iii) Hakuna sehemu ya kunawia mikono wanafunzi baada ya kutoka chooni.

d) Maoni

i) Itengwe bajeti ya choo kabla shule haijaanza. ii) Ujenzi wa vyoo uzingatie miundombinu ya wasichana waliopevuka na

walemavu

iii) Mbao za kuandikia ziwekewe “ash chalks” na madarasa hayo yawekewe

dari ili usikivu uwepo kati ya mwalimu na mwanafunzi pindi hata mvua

itakapokuwa inanyesha.

iv) Usanifu wa ujenzi wa vyoo ubadilishwe tunapendekeza ujenzi huo uwe

unatenganisha shimo na mahali vyoo vilipo (Shimo liwe mbali na jengo la

vyoo). Mfano mzuri (Best practice) ni vyoo vya shule ya msingi

Lubakaya Kata ya Msongola katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

36

Picha Na. 8: inaonesha hali halisi ya choo kilichotitia katika shule ya Msingi Malambamawili

Picha Na. 9: Mfano wa Usanifu wa ujenzi wa vyoo ukionesha jengo lenye matundu ya vyoo

kujengwa mbali na shimo (Septic tank) - katika shule ya Msingi Lubakaya- Ilala

37

Picha Na. 10: Ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa katika shule ya Msingi Malambamawili

2.5 Ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya Ubungo

Utangulizi

Kuanzishwa kwa maeneo mapya ya kiutawala kumeupa msukumo mkoa

wa Dar es Salaam kufanya jitihada za kupata maeneo kwa ajili ya ujenzi

wa Ofisi za Wakuu wa Wilaya. Hivyo, Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

imekwishatwaa eneo Mbezi Ruguruni kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Mkuu

wa Wilaya ili kurahisisha shughuli za kiutendaji na pia kuepusha gharama

za kupanga/ kukodi ofisi zinazofanyika sasa.

a) Utekelezaji

i) Eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 3,509 limepatikana lakini ujenzi

bado haujaanza

ii) Eneo hilo lipo Mbezi Ruguruni Block (A) 341.

iii) Yamefanyika maandalizi ya Hati kwenye Wizara ya Ardhi, Nyumba na

Maendeleo ya Makazi kwa gharama za Sh. 480,000.

b) Mafanikio

i) Kutwaa eneo na kulipa fidia kwa wakazi.

ii) Kuna fedha kiasi cha Sh. Milioni 500 zimekwishapatikana kwa ajili ya

kuanza hatua za awali za ujenzi.

38

c) Changamoto

Wananchi kuendelea kuwepo katika eneo la mradi licha ya kuwa fidia

walikwishalipwa.

d) Maoni

i) Halmashauri ihakikishe wananchi waliolipwa fidia wanapewa taarifa

mapema waondoke kabla ujenzi haujaanza ili kuondoa usumbufu.

ii) Fedha zilizokwishapatikana zitumike kwa shughuli iliyopangwa na

thamani yake ionekane.

Picha Na. 11: inaonesha ramani (Hati) ya eneo ambalo Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya

Manispaa ya Ubungo itajengwa

39

Picha Na. 12: inaonesha mkazi aliyelipwa fidia katika eneo ambalo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo lakini

bado hajapewa taarifa ya kuondoka.

2.6 Ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya

Ubungo

Utangulizi

Uhitaji wa kujenga Ofisi za Wakurugenzi kwa lengo la kusogeza huduma

kwa jamii kumefuatia baada ya kuanzishwa kwa maeneo mapya ya

kiutawala katika Mkoa wa Dar es Salaam. Ili kutekeleza azma hiyo

Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imefanikiwa kutwaa ardhi yenye

ukubwa wa Hekta 1.64 sawa na ekari 4 ambayo imekwishapimwa na

uondoshwaji wa vichaka katika eneo hilo umefanyika. Eneo hilo lipo katika

Kitalu Na.1 (A) 348. Mbezi Luguluni.

a) Utekelezaji

Eneo limepatikana lakini ujenzi bado haujaanza

b) Mafanikio

i) Eneo limepatikana kwenye Kitalu Na.1 (A) 348, na limekwishapimwa

na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

ii) Maandalizi ya hati yamefanyika kwa gharama za sh. milioni 1.9

iii) Zoezi la kuondoa vichaka katika eneo la mradi limefanyika.

iv) Halmashauri kufanikiwa kutenga kiasi cha Sh. billion 2 kwa bajeti ya

mwaka 2017/18 kwa ajili ya ujenzi huo, ambapo kati ya hizo Sh. bilioni

40

1.2 zinatokana na mapato ya ndani na Sh. milioni 800 ni za Ruzuku

kutoka Serikali Kuu.

c) Changamoto

Kuchelewa kupata hati kwa kuwa utaratibu wa ujenzi hauwezi kuanza

kabla ya kupata hati.

d) Maoni

Kwa kuwa Hati imekwishapatikana Mkurugenzi ahakikishe Michoro ya

ujenzi inapatikana haraka ili ujenzi uanze kwa sababu kukamilika kwa

Mradi huu, kutasaidia kuimarisha utendaji kazi wa Watumishi katika kutoa

huduma kwa jamii pamoja na kuokoa gharama kubwa zinazotumika sasa

hivi kwa kukodi/kupanga ofisi.

2.7 Ujenzi vyumba 3 vya madarasa katika Shule ya Msingi Msakuzi

Utangulizi

Katika kuongeza miundombinu ya kusomea na kupunguza tatizo la uhaba wa

vyumba vya madarasa, Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imeendelea na

ufuatiliaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule mbalimbali

(zilizoanzishwa na Halmashauri ya Kinondoni) ikiwemo hii ya Msakuzi. Ujenzi

huo ulianza katika mwaka wa fedha 2015/16 na kukamilika mwaka 2016/17

na umegharimu kiasi cha Sh. milioni 63.

a) Utekelezaji

Mradi umekamilika na umekabidhiwa kwa Mkurugenzi tarehe 04/04/2017 na

Mkandarasi aliyejenga ni M/S Kachima Limited

b) mafanikio

i) Kukamilika kwa madarasa hayo kumesaidia kupunguza msongamano wa

wanafunzi 829 waliokuwa wanatumia vyumba vinne (4) tu vya madarasa.

ii) Kukamilika kwa mradi huo kumewezesha shule kuwa na vyumba saba (7)

vya madarasa.

iii) Wanafunzi wa masomo ya awali nao wamepata darasa la kujifunzia.

c) Changamoto

i) Mradi hauridhishi kwa kuwa una mapungufu mengi ikiwemo rangi

iliyopakwa ukutani ikiguswa inafutika,

ii) Madirisha hayana nyavu kwa ajili ya ulinzi

iii) Sakafu iliyowekwa haiko kwenye kiwango kinachotakiwa, iliyowekwa ni

rafu na siyo ya kioo

iv) Sehemu ya kuwekea chaki (Ashboard) katika mbao haipo

41

v) Choo chenye jumla ya matundu 12 kinachotumika ni chakavu hasa

sehemu ya velanda

vi) Hakuna huduma ya kunawa mikono wanafunzi wanapotoka chooni.

d) Maoni

Halmashauri ihakikishe Mkandarasi kabla hajamalizia kasoro zilizojitokeza asilipwe fedha zake za “rentantion”, malipo yafanyike baada ya kukamilisha kazi.

Picha Na. 13: Ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa katika shule ya Msingi Msakuzi

2.8 Ujenzi wa vyumba sita (6) na kimoja cha walimu wa shule ya

Sekondari Matosa

Utangulizi

Madarasa hayo yamejengwa kwa lengo lile lile la kukabiliana na uhaba wa

vyumba vya madarasa. Ujenzi huu wa kama ilivyo miradi mingi katika

Halmashauri ya Ubungo ilianzishwa na Halmashauri mama ya Kinondoni.

Ujenzi huu uligharimu kiasi cha Sh. milioni 150 kikiwa kimehusisha ujenzi wa

chumba kimoja ambacho kitatumika kama ofisi ya walimu.

a) Utekelezaji

42

Ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa umekamilika (kwa mujibu wa

Mkandarasi wa Halmashauri) kwa sababu siku hiyo ya Ukaguzi timu ya Mkoa

haikuweza kufika katika eneo la mradi kutokana na changamoto ya barabara

kuharibiwa na mvua.

b) Mafanikio

Wanafunzi kupata madarasa ya kujifunzia

c) Changamoto

Kutokana na changamoto ya barabara, timu ya ukaguzi haikuweza kufika

kuona hali halisi ya ujenzi wa nyumba hiyo.

d) Maoni

i) Miundombinu ya barabara hiyo iboreshwe ili iwe inapitika hata kipindi cha

mvua

ii) Halmashauri ipitie maoni yaliyotolewa kwenye kaguzi zingine za miradi ya

shule ili kuona kama na shule hiyo ya Matosa ina mapungufu ya namna

hiyo, na endapo yatakuwepo basi yafanyiwe kazi.

iii) Timu ya Mkoa itahakikisha inatoa kipaumbele kwa kufanya ukaguzi

kwenye miradi ambayo haikuweza kukaguliwa kwa kipindi hiki kutokana

na sababu ambazo hazikuweza kuzuilika.

2.9 Mradi wa Soko la Mabibo (Mahakama ya ndizi) Kata ya Mabibo

Utangulizi

Soko la Mabibo linalojulikana kwa jina la “Mahakama ya ndizi” lililopo katika

Kata ya Mabibo kwa muda mrefu limekuwa likisimamiwa na Kampuni binafsi

ya “Maji moto” kabla ya Wilaya ya Ubungo haijaanzishwa. Hata hivyo, wazo

la kutaka soko hilo lisimamiwe na Serikali lilikuja baada ya kuanzishwa kwa

Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ambapo kwa uongozi wao kupitia kwa

aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo (Mh. Hamphrey Polepole ambaye kwa sasa ni

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Taifa) ulifanya

juhudi ambazo zilisaidia soko hilo kuwa chini ya usimamizi wa Manispaa. Vile

vile umiliki wa eneo la soko hilo haujawa chini ya Manispaa kwa sababu eneo

hili ni la Kiwanda cha nguo cha Urafiki. Hapo awali Halmashauri ilikuwa

ikipata takribani kiasi cha sh. milioni 3 kama mapato yanayotokana na soko

hili kila mwezi tofauti na sasa hivi pato la mwezi ni kati ya Sh. Milioni 70-80

kwa mwezi.

43

a) Utekelezaji

Juhudi zilizofanyika ni pamoja na kuhakikisha Soko linasimamiwa na

Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, jambo ambalo limefanikiwa.

b) Mafanikio

i) Kufanikiwa kudhibiti suala la upotevu wa mapato

ii) Kuongeza mapato ya Halmashauri kutoka wastani wa shilingi milioni 3

hadi shilingi milioni 70 au 80 kwa mwezi.

iii) Kufanikiwa kusisitiza matumizi ya mashine za ki-ilektroniki katika

kukusanya mapato

c) Changamoto

i) Bado eneo la soko lipo kwenye umiliki wa kiwanda cha nguo cha Urafiki.

ii) Miundombinu ya soko hilo ni mibovu mfano kipindi cha mvua kunakuwa

na matope hali inayosababisha kuongezeka kwa uchafu na hivyo

kutowavutia wateja.

iii) Maji bado ni kero kwa kuwa eneo hili linahitaji maji kwa ajili ya kuimarisha

hali ya usafi

d) Maoni

i) Miundombinu ya soko hilo iboreshwe ili kuongeza tija kwa watumiaji kwa

vipindi vyote vya misimu ya mwaka.

ii) Wakati Mkoa unachukua wazo la kufanya mazungumzo na uongozi wa

Kiwanda cha Urafiki, pia Halmashauri ihakikishe inamkumbusha suala hilo

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mh. Hamphrey

Polepole kwa kuwa aliahidi kufuatilia suala hili hata baada ya kupewa

Wadhifa huo wa ngazi ya Kitaifa.

iii) Halmashauri isijihusishe na masuala ya kamati za masoko kwa sababu

zimekuwa ndicho chanzo cha migogoro, rushwa na hata ubadhilifu wa

mapato.

44

Picha Na. 14: inaonesha hali halisi ya miundombinu katika soko la Mabibo (Mahakama ya ndizi)

2.10 Ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa katika Shule ya Msingi

Kawawa

Utangulizi

Shule ya msingi Kawawa ina jumla ya wanafunzi wapatao 3,000 ambao wamekuwa wakisoma kwa shida sana kutokana na uchache wa vyumba vya madarasa. Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ilipanga kujenga madarasa 5 ili kupunguza kero hiyo. Hata hivyo, kuanzishwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kumesaidia kusimamia kwa ukaribu miradi iliyoanzishwa na Halmashauri ya Kinondoni ambayo sasa imo ndani ya Manispaa ya Ubungo ukimwemo mradi huu wa madarasa 5. Ujenzi wa madarasa hayo ulijengwa na Local fundi kwa gharama ya sh. Milioni 85. Mradi ulianzishwa kipindi cha bajeti ya mwaka 2015/2016 na kukamilika mwaka 2016/17.

a) Utekelezaji Maradasa manne (4) kati ya matano (5) yaliyokuwepo kwenye mpango yamekamilika na yanaridhisha.

b) Mafanikio Kukamilika kwa vyumba 4 vya madarasa kumesaidia wanafunzi kupata mahali pa kusomea na hivyo kupunguza msongamano madarasani

c) Changamoto Mapungufu yaliyopo ni kutokuwepo kwa wavu ‘wire mesh’ madirishani na ‘Ashboard’

d) Maoni

Mapungufu yaliyojitokeza yanatakiwa yarekebishwe haraka kabla tatizo

halijawa kubwa

45

Picha Na. 15: inaonesha ujenzi vyumba 5 vya madarasa katika shule ya Msingi Kawawa

2.11 Ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa shule ya Msingi

Kibamba

Utangulizi

Shule ya msingi Kibamba ipo katika Kata ya Kibamba katika Halmashauri

ya Manispaa ya Ubungo. Ujenzi wa madarasa 2 shule ya hiyo ni

mwendelezo wa juhudi za kukabiliana na tatizo la uhaba wa madarasa ili

kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira stahiki. Mradi huu wa

madarasa mawili (2) ulianza kipindi cha mwaka 2015/16 na kukamilika

kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17 kwa kutumia mapato ya ndani ya

Halmashauri.

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na jumla ya sh. milioni 34 zilitumika kwa ujenzi huo.

b) Mafanikio

Vyumba hivyo vya madarasa vimesaidia kupunguza msongamano wa

wanafuzi japo si kwa kiwango kinachotakiwa.

c) Changamoto

i) Kuna mapungufu ya paa pamoja na sakafu kutokuwa imara.

ii) Ofisi ya walimu iliyojengwa kwa nguvu za kamati ya shule na walimu

haijakamilika kwa kuwa haina choo.

d) Maoni

i) Mapungufu yaliyojitokeza yarekekebishwe.

ii) Maelekezo yametolewa kuwa ofisi ikamilishwe kwa kutumia fedha za

Malipo ya Halmashauri.

46

Picha Na. 16: inaonesha ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa katika shule ya Msingi Kibamba

Picha Na. 17: inaonesha vibuyu chirizi na hatua za kunawa mikono baada ya kutoka chooni

katika shule ya Msingi Kibamba.

47

4.0 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

MANISPAA YA ILALA

UTANGULIZI

Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Ilala ulianza tarehe 09 hadi 11

Mei, 2017. Hata hivyo, pamoja na miradi 12 iliyopendekezwa na Halmashauri kuikagua,

Sekretarieti ya Mkoa ilipendekeza mradi mwingine wa ujenzi wa shule ya msingi

Magorofani iliyopo Gongo la Mboto Jeshini na hivyo kufanya jumla ya miradi

iliyokaguliwa kufikia 13. Ifuatayo ni taarifa ya kila mradi uliotembelewa ikiwa inaonesha

mafanikio, changamoto na mapendekezo ya utatuzi wa changamoto hizo.

4.1 Ujenzi wa Shule Mpya ya Yangeyange (Vyumba 10 vya Madarasa na

Matundu 10 Ya Vyoo)

Utangulizi

Shule ya Msingi Yangeyange ilianzishwa mahsusi kwa ajili ya kukabiliana na

tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa. Mradi huo unahusisha pia

ujenzi wa matundu 10 ya vyoo kwa gharama ya Sh. Milioni 190 ambazo ni

fedha za ndani za Halmashauri.

a) Utekelezaji

Ujenzi wa vyumba 8 umekamilika chini ya usimamizi wa uongozi wa shule ya

msingi Msongola na ujenzi wa vyumba 2 upo katika hatua za awali za

mandalizi.

b) Mafanikio

Kukamilika kwa ujenzi wa madarasa 8 ya shule hiyo kumesaidia sana

wanafunzi wengi kupata mahali pa kujifunzia ikiwa ni pamoja na kuipunguzia

mzigo shule ya msingi ya Msongola. Hadi sasa mradi unahudumia wanafunzi

1,544 wa darasa la I-VI, na walimu wapo 23. Pia shule ilipata msaada wa

kuchimbiwa kisima cha maji kwa ufadhili wa Ubalozi wa Kuwait.

c) Changamoto

Pamoja na mafanikio hayo pia kuna kasoro zifuatazo katika shule hiyo:- i) Sakafu imeonekana kutokuwa imara kwani imeanza kulika. ii) Huduma ya kunawa mikono haitoshelezi kwani lipo ‘sink’ moja tu la

kunawia mikono wakati wanafunzi wanapotoka chooni. iii) Hakuna chumba maalum cha kubadilishia nguo/pedi wasichana hasa wale

waliokwisha vunja ungo. iv) Eneo la shule lipo katika hatari ya kuvamiwa na majirani, eneo lipimwe na

kuwekewa mipaka v) Mbao za kufundishia ni ndogo na hazina ‘ash board’.

48

vi) Usimamizi wa ujenzi wa mradi huo ulikuwa si wa kuridhisha.

d) Maoni

i) Mapungufu yaliyoonekana yafanyiwe kazi haraka kabla tatizo halijawa

kubwa ili kuepusha gharama za ziada za ukarabati.

ii) Wahandisi wafuatilie utekelezaji unaofanyika mashuleni

iii) Kuwe na mawasiliano baina ya Idara ya Mipango na Uhandisi ili kujua

fedha zinazotengwa kwenye miradi ya shule

iv) Maafisa elimu wa Manispaa wahakikishe Walimu wa shule hiyo

wanazingatia suala la usafi shuleni hapo ikiwa ni pamoja na uwekaji wa

vibuyu chirizi kwa ajili ya kunawia mikono wanafunzi ili kuepuka

magonjwa ya mlipuko kama vile kuhara na kipindupindu.

Picha Na. 1: Moja ya jengo la vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Yangeyange.

49

Picha Na. 2: Choo chenye matundu 10 kilichojengwa katika shule ya msingi Yangeyange

4.2 Ujenzi wa Shule ya Msingi Ukonga (Magorofani) Utangulizi Mradi wa ujenzi wa shule ya msingi Magorofani ulianzishwa ili kuweza

kukabililiana na tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa katika shule ya

msingi Gongo la Mboto Jeshini. Ujenzi huo uligharimu jumla ya Sh. Milioni

323.

a) Utekelezaji

Madarasa yamekamilika na yalianza kutumika kuanzia mwezi Januari, 2017

ambapo hadi sasa jumla ya wanafunzi 1,583 wa darasa la I-VII wanayatumia.

Awali wanafunzi hao walikuwa katika shule nyingine ya Gongo la Mboto

Jeshini. Aidha, katika shule hiyo kuna kisima cha maji ambacho kinasaidia

kuyafanya mazingira ya shule hiyo kuwa mazuri.

b) Mafanikio

Mradi unaridhisha na ulianza kutumika kuanzia Januari, 2017 hadi sasa kuna

jumla ya wanafunzi 1,583 wa darasa la I-VII.

Pia kuna kisima cha maji ambacho kinasaidia kuweka mazingira ya shule kuwa mazuri.

c) Changamoto i) Kuna kasoro ndogo ndogo tu za kiujenzi kama vile mwinuko mkukwa

kwenye kingo za madarasa ambazo zinaweza kusababisha wanafunzi

kuanguka

ii) Mbao za kufundishia hazina kiwekeo cha chaki “ash board”

50

d) Maoni

Sehemu zilizoinuka ziwekewe kingo za kuzuia wanafunzi/walimu kuanguka

pamoja na kuweka “ash board” kwenye madarasa yasiyonazo.

Picha Na. 4: Sehemu ya baraza la shule ya msingi magorofani ambayo imeinuka kupita kiasi

51

Picha Na. 5: Vyumba vya madarasa vilivyojengwa katika shule ya msingi Magorofani

4.3 Ujenzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto Chanika

a) Utangulizi

Ujenzi wa Hospitali ya mama na mtoto katika Kituo cha Afya cha Chanika katika

kata ya Chanika unafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa Korea Kusini

kupitia Shirika la Koica. Mradi huo unahusisha ujenzi wa wodi zenye vitanda 160

ikiwemo antenatal (kabla ya kujifungua), labour ward (chumba cha kujifungulia),

postnatal (baada ya kujifungua) vyumba vya upasuaji viwili, vyumba vya

uangalizi maalum vitatu (intensive care units), chumba cha uangalizi wa watoto

(neonatal care room) vyumba kwa ajili ya uchunguzi na vipimo mbali mbali vya X

ray, ultra sound na maabara. Sambamba na hilo, kuna ujenzi wa nyumba za

watumishi 12 katika jengo ghorofa 3 ambapo watakaa watumishi muhimu

wanaohitajika muda wote katika kutoa huduma, kutakuwa na ununuzi wa gari la

wagonjwa (Ambulance) ili kuimarisha huduma ya rufaa kwa wagonjwa. Ujenzi

wa Mradi ulianza mwezi wa Februari 2016 na unakabidhiwa June 2017 na mradi

una thamani ya shillingi Billioni 8.8

b) Utekelezaji

i) Ujenzi wa Hospitali umekamilika kwa asilimia 96%, ikiwa ni pamoja na

ujenzi wa majengo na kuweka sakafu, kuunganisha mifumo ya umeme,

maji safi na maji taka pia kazi ya ufungaji wa vifaa tiba ikiwemo x-ray,

ultra sound, vifaa vya maabara, theatre, mashine za kufua na masinki ya

vyoo. Aidha, ununuzi wa samani za Hospitali kama meza, kabati, na viti

52

unaendelea. Pia kazi ya kusafisha na kuweka sakafu eneo la maegesho ya

magari inaendelea.

ii) Ujenzi wa nyumba 12 za watumishi katika jengo la ghorofa la sakafu 3

umekamilika na ununuzi wa samani za nyumba unaendelea.

c) Mafanikio:

i) Kukamilika kwa hospitali hiyo kutasaidia sana kutoa huduma za afya kwa

akina Mama na Watoto waliopo maeneo ya jirani na kata ya Chanika na

hivyo kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa kiasi kikubwa.

ii) Hospitali hiyo itasaidia kupunguza msongamano wa akina mama

wanaokwenda kupata huduma za afya katika hospitali zingine za Mkoa wa

Dar es Salaam hasa katika hospitali ya Amana.

iii) Huduma za upasuaji zitafanyika kwa wakati hivyo kupunguza maumivu na

vifo vilivyokuwa vinatokea kwa wajawazito na watoto wenye matatizo

iv) kutoa huduma katika mazingira bora na vifaa bora kutaongeza ari na

motisha kwa watoa huduma hivyo kuleta ufanisi na maboresho katika

huduma

v) Halmashauri imekwishapata eneo kwa ajili ya ujenzi wa Maegesho ya

Magari na fidia tayari imekwishalipwa.

d) Changamoto

i) Kuna ufinyu wa eneo la kuegeshea magari na kukosekana kwa uzio

ii) Samani za hospitali hiyo hazijakamilika ili ianze kutoa huduma.

e) Maoni

i) Halmashauri iweke mpango wa kujenga uzio pamoja na kuharakisha zoezi

la ununuzi wa samani za hospitali hiyo ili huduma zianze kutolewa.

ii) Pia Halmashauri ijenge maeneo ya maegesho ya magari kwenye eneo

lililokwishapatikana.

53

.

Picha Na. 8: Katibu Tawala wa Mkoa akikagua jinsi vifaa vya Hospitali ya Mama na Mtoto-Chanika

vinavyofanya kazi.

Picha Na.6: Eneo mojawapo la wazi

(Corridow) katika hospitali ya

‘Mama na Mtoto Chanika’

Picha Na. 7: Hiki ni chumba mojawapo cha kuhudumia

wagonjwa/wajawazito

54

Picha Na. 11: Hili ni Wodi litakalotumika kuwalaza wagonjwa (Mama na Mtoto) katika Hospitali ya

Chanika.

Picha Na. 9: Hiki ni moja kati ya vifaa

ambavyo vitatumika kutoa huduma

maalumu kwa watoto wanaozaliwa kabla ya

wakati “Pre-mature babies”

Picha Na. 10: Hii ni moja kati sehemu ambazo

mgonjwa anafanyiwa uchunguzi kwa njia za kisasa

55

4.4 Ujenzi wa Vyumba 10 vya Madarasa Ya Shule Ya Msingi Mafanikio

Utangulizi

Ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Mafanikio ulianza

kipindi cha mwaka wa fedha 2015/2016 na kukamilika 2016/2017 lengo likiwa

la kukabiliana na tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa katika

Halmashauri.

a) Utekelezaji

Jumla ya vyumba vya madarasa 10 vimekamilika na vimegharimu kiasi

cha Sh. Milioni 210.

b) Mafanikio:

Mradi unatumika na unawahudumia wanafunzi 1,208 kuanzia darasa la I-

VII na kuna walimu 15.

c) Changamoto

i) Kuna mgogoro wa ardhi na hivyo inahitajika fidia kwa baadhi ya

watu/majirani.

ii) Mapungufu ya ubao wa kufundishia (ash board, na ubao kuwa mdogo) na

sakafu siyo imara

iii) Kutokuwepo huduma ya umeme kwa ajili ya kusukuma maji.

d) Maoni

i) Kupima ardhi na kutoa fidia zinazohitajika.

ii) Kufuatilia umeme ili utumike katika huduma mbalimbali shuleni.

iii) Kufanya maboresho ya mbao za kufundishia.

56

Picha Na.12: inaonesha jengo mojawapo la vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi

Mafanikio

4.5 Ujenzi wa Mradi na Usambazaji wa Maji Pugu- Bangulo

Utangulizi

Ujenzi wa Mradi wa maji Pugu- Bangulo ulianza 1/08/2015 na kukamilika

8/05/2017. Mkandarasi aliyejenga mradi huo ni MS Gwantwa Contractors Ltd.

Mradi huo haukukamilika mapema kwasababu ya umeme kuchelewa

kuunganishwa katika eneo la mradi.

a) Utekelezaji

Mradi umekamilika ingawaje bado kuna mapungufu ya rangi ya nyumba ya

pampu ambayo yanahitaji marekebisho. Mradi umegharimu kiasi cha Sh.

152,929,000.00

57

b) Mafanikio

Kukamilika kwa mradi huu kunanufaisha wananchi wapatao 1,800 wa Mtaa

wa Pugu-Bangulo kupata maji safi na salama kwa wastani wa kuchota ndoo 3

za lita 20 kwa siku.

c) Changamoto

i) Mradi ulichelewa kwa umeme kukamilika kwa sababu ya kuchelewa

kuunganishiwa umeme kutoka TANESCO,

ii) Kusimamishwa kwa ujenzi wa nyumba ya kuwashia pampu ya maji “Pump

House”na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwa eneo hilo ni la Wizara

hiyo.

iii) Rangi iliyotumika kwenye uzio wa ‘pump house’ haina kiwango cha

kuridhisha. Aidha rangi haiendani na rangi inayotumika katika masuala ya

maji ambayo ni blue na nyeupe

d) Maoni

i) Changamoto ya umeme na kibali cha kuomba eneo la nyumba ya pampu

zilikwishatatuliwa

ii) Rangi irudiwe (ibadilishwe) na pia pawepo na mipango ya kupata nishati

mbadala kama vile jenereta ili wananchi wasikose huduma hiyo muhimu

pindi umeme wa TANESCO unapokatika.

iii) Kuwepo na kamati ya maji ili kuufanya mradi uwe endelevu.

Picha Na. 13: Marekebisho ya ukuta/uzio wa ‘pump house’ katika kisima cha maji Pugu-Bangulo

58

Picha Na. 14: Tanki la maji la ujazo wa lita 50,000 eneo la Pugu-Bangulo katika Kata ya Pugu.

4.6 Matengenezo ya Barabara ya Mombasa Moshi- Bar kwa Kiwango

cha Lami

Utangulizi

Matengenezo ya barabara hii yalifanyika mahsusi kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya barabara na kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa wakazi wa Majohe, Kipunguni, Kivule na maeneo mengine ya jimbo la Ukonga kuingia barabara kuu ya Pugu. Mradi huu ulianza 22/02/2016 na kukamilika 21/01/2017.

a) Utekelezaji

Mradi haujakamilika kwa sababu bado vituo vya kupakilia na kushushia abiria

“Bus bays” havijakamilika

59

b) Mafanikio

Kukamilika kwa barabara hii kumerahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa wakazi wa Majohe, Kipunguni, Kivule na maeneo mengine ya Jimbo la Ukonga kuingia barabara kuu ya Pugu

c) Changamoto

i) Kuchelewa kuondoa miundombinu ya mawasiliano (nguzo za simu na umeme),

mabomba ya maji na ndani ya eneo la mradi.

ii) Uhamishwaji wa miundombinu hiyo ulihitaji gharama ambazo hazikutengwa na

Halmashauri

iii) Hakuna vituo vya kushushia/kupakilia abiria “Bus Bays”

d) Maoni

i) Ni vyema kuwe na upembuzi yakinifu kwanza kabla ya mradi kuanza ili

kuondoa tatizo la kazi za ziada “additional works.”

ii) Wahandisi wametakiwa kuhakikisha “Bus Bays” zinajengwa haraka.

60

Picha Na. 15 : Hii ni barabara ya Mombasa –Moshibar

iliyojengwa kwa kiwango cha lami.

Picha Na. 16: Mfereji wa maji ya mvua uliojengwa kwenye

barabara ya Mombasa-Moshibar

61

4.7 UJENZI WA VYUMBA 5 VYA MADARASA –KIMANGA SEKONDARI

Utangulizi

Uamuzi wa kujenga vyumba 5 vya madarasa ni juhudi za Halmashauri katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa. Mradi huo ulienda sambamba na ujenzi wa matundu 27 ya vyoo na Mjenzi ni ‘Local Fundi’ na gharama za mradi ni Sh. Milioni 120.

a) Utekelezaji

Ujenzi wa vyumba vya madarasa 5 pamoja na samani tayari vimekamilika

ispokuwa vyoo vipo kwenye hatua ya umaliziaji.

b) Mafanikio

Shule inatarajiwa kuchukua wanafunzi 200 wa kidato cha kwanza kutoka

katika shule waliyokuwa wanasoma kwa muda. Mradi unatarajiwa

kukamilishwa tarehe 28/5/2017. Viti na meza 200 vipo tayari kwa ajili ya

wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na shule hiyo.

c) Changamoto

i) Ubao wa kuandikia kutokuwa na urefu wa kutosha pamoja na ‘Ash board’ ii) Hakuna nyumba ya Mkuu wa shule atakayeteuliwa ikizingatiwa kuwa ni

shule mpya. iii) Shule bado haina hati – hiyo iliyopo ni ya Bodi ya Wakandarasi iv) Vyoo havijakamilika

d) Maoni

Halmashauri ifanye yafuatayo:- i) Maboresho ya ubao, ukamilishaji wa vyoo, kufanya tathmini ya nyumba

iliyopo shuleni kwa ajili ya makazi ya atakayekuwa Mkuu wa shule , au endapo ukarabati utakuwa na gharama kubwa, ushauri ni kuijenga upya

ii) Kufuatilia hati ya kiwanja kutoka bodi ya wakandarasi na kuibadilisha.

62

Picha Na. 17: Huu ni mwonekano wa Jengo la vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari

Kimanga

4.8 UJENZI WA BARABARA YA TABATA ST. MARY’S KWA KIWANGO

CHA LAMI

Utangulizi

Ujenzi wa barabara hii ya Tabata St.Mary’s ni marudio ya ujenzi wa awali

ambao haukuwa imara na hivyo kusababisha barabara hiyo kutodumu

kwa muda mrefu kwa sababu ya kukosa usimamizi thabiti. Mradi huu

ulianza tarehe 28/11/2012 na kukamilika tarehe 13/03/2017 na

umetekelezwa kwa muda mrefu kutokana na sababu iliyoelezwa.

a) Utekelezaji

Matengenezo ya barabara hiyo yamekamilika kwa kiwango cha zege na

lami ngumu pia ujenzi umehusisha Culvert pamoja na mifereji ya

kuondolea maji ya mvua.

b) Mafanikio

Kuimarika kwa miundombinu ya barabara ili kurahisisha shughuli za usafiri

na usafirishaji kwa wakazi wa Tabata, Segerea, Kisukuru na maeneo

mengine kuingia barabara ya Mandela.

63

c) Changamoto

i) Kuna changamoto ya mifereji kuziba kutokana na uchafu pamoja na nyasi zilizoota ndani na pembezoni mwa mifereji hiyo

ii) Road shoulder hazijawekewa lami, zimebaki udongo hivyo kuweza kuchimbika kwa sababu ya maji ya mvua.

d) Maoni

i) Halmashauri kwa kutumia sheria ndogo ndogo (by-laws) za usafi inatakiwa iwahamasishe viongozi wa Serikali za Mitaa kuhimiza suala la usafi katika maeneo hayo

ii) Mkandarasi aweke lami katika road shoulder kama ilivyo katika mkataba

Picha Na. 19: Barabara ya Tabata St. Mary’s iliyojengwa

kwa kiwango cha lami

Picha Na. 18: Nyasi zilizoota kwenye

Mfereji wa maji katika barabara ya

Tabata St. Mary’s

64

4.9 Matengenezo ya barabara ya Vingunguti –Barakuda kwa kiwango

cha lami

Utangulizi

Kama ilivyo kwa barabara ya Tabata St.Mary’s, barabara hii ya Vingunguti –Barakuda imerudiwa baada ya ujenzi wa awali kutokuwa wa ufanisi. Ujenzi huo awali ulitekelezwa na Mkandarasi Patty Enterplan Ltd na baadaye alisimamishwa na akapewa Mkandarasi Del Monte (T) Ltd.

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na gharama za mradi zilikuwa Sh. 1,478,757,133.33 na mpaka mradi unakamilika kiasi cha Sh. 1,333,421,118.00 kilitumika.

b) Mafanikio

Kuimarisha miundombinu ya barabara ili kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa wananchi na vilevile kupunguza msongamano wa magari katika barabara kuu ya Nyerere kwa Wakazi wa Segerea, Tabata, Kimara, Mbezi na sehemu zinginezo.

c) Changamoto

Kiwango cha maji ya ardhini (under ground water table) katika eneo hilo kuwa juu. Hali hiyo ilisababisha barabara hiyo kuharibika mapema baada ya Mkandarasi wa mwanzo kumaliza kazi yake.

d) Maoni

i) Halmashauri ione umuhimu wa kufanya upembuzi yakinifu (feasibility study) kabla ujenzi haujafanyika pamoja na kuwa na Washauri katika ujenzi.

ii) Usanifu ‘Design” uliotumika kujenga mahali pengine ukafanikiwa usitumike kila mahali bila kufanya upembuzi yakinifu kwa kuwa hali ya ki-jiografia hutofautiana kutoka eneo moja na jingine.

65

Picha Na. 20: Ujenzi wa barabara ya Vingunguti – Barakuda kwa kiwango cha lami.

4.10 Ujenzi wa Culvert–Barabaray Kinyerezi- Bonyokwa.

Utangulizi:

Mradi huu wa Ujenzi wa Culvert katika barabara ya Kinyerezi- Bonyokwa ulianza tarehe 18/03/2015 na kukamilika 02/02/2017.Ucheleweshwaji wa kukamilika kwa ujenzi huo ni kutokana na TANROADS kuchelewa kutoa michoro, na vile vile vifaa vya ujenzi kutoka kwa Mkandarasi M/S Engineering & Construction Co. Ltd vilicheleweshwa.

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na unatumika pia ujenzi umehusisha (box culvert) daraja la chuma lenye uwezo wa kuhimili uzito wa tani 7

66

b) Mafanikio

Kuimarisha miundombinu ya barabara kumesaidia kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji hasa kwa wakazi wa Kinyerezi, Bonyokwa, Kimara, Mbezi na sehemu nyingine

c) Changamoto

i) Wizi wa sehemu za vyuma vilivyounganishwa katika daraja hilo

ii) Magari yasiyotakiwa (yenye zaidi ya uzito wa tani 7) kupita katika daraja

hilo.

d) Maoni

i) Pawepo na usimamizi madhubuti pamoja kutoa elimu kwa wakazi wa eneo

hilo juu ya umuhimu wa daraja hilo

ii) Kutoza faini kwa watakaothubutu kupitisha magari na mitambo yoyote

isiyoruhusiwa kisheria.

Picha Na. 21: Hii ni alama inayoonesha uzito

sahihi wa magari yanayotakiwa kupita

katika daraja la Kinyerezi-Bonyokwa

Picha Na. 22: Hili ni box culvert

(daraja la chuma) barabara ya

Kinyerezi -Bonyokwa

67

4.11 Ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi (Madarasa 16) Lubakaya na

Matundu 31 ya Vyoo

Utangulizi

Kimsingi shule ya msingi Lubakaya ilianzishwa kwa lengo la kuimarisha

miundombinu ya sekta ya elimu katika Kata ya Msongola. Ujenzi huo

ulianza na kukamilika ndani ya kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17.

Ujenzi huo ulienda sambamba na ujenzi wa matundu ya vyoo 31 ambapo

mradi wote uligharimu kiasi cha sh. Milioni 374. Kati ya madarasa hayo

16, madarasa 8 yalijengwa kwa Mpango wa Performance for Results (P4R)

na 8 yalijengwa kwa fedha za makusanyo ya ndani ya Halmashauri.

a) Utekelezaji

Ujenzi wa mradi huu umekamilika ukiwa umetekelezwa na Local Fundi’s –

wanaounda umoja wao unaoitwa (Kijiji Construction).

b) Mafanikio

i) Kukamilika kwa shule hiyo kumeimarisha miundombinu ya Sekta ya Elimu pamoja na kuwawezesha wanafunzi wapatao 1,316 kupata madarasa ya kusomea, na hivyo kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule ya msingi Msongola.

ii) Vyoo vilivyojengwa katika shule hiyo vinaridhisha kwa sababu vimejengwa kwa usanifu kuchimba shimo pembeni na jengo.

c) Changamoto

i) Shule haina maji kwa sababu ya kukosa umeme licha ya kuwa ilipata msaada wa kisima kutoka kwa Wafadhili wa Kuwait. Hali hii inapelekea wanafunzi wa shule hiyo kuja na maji yao kutoka kwenye makazi yao bila kujua hali halisi ya usalama wake.

ii) Shule hiyo haina uzio hali ambayo itasababisha uvamizi wa eneo na wizi wa vifaa.

d) Maoni

i) Utatuzi wa muda mrefu ni kuweka umeme katika shule hiyo kwa kuwa tatizo ni kupatikana kwa gharama za kununulia transfoma.

ii) Utatuzi wa muda mfupi imeshauriwa uongozi wa shule hiyo kufanya utaratibu wa kuvuna maji ya mvua ambayo yangeweza kusaidia katika kuboresha shughuli za usafi wa mazingira pamoja na watoto kunawa. wanavyotoka chooni.

iii) Eneo la shule lipimwe na mipango ya kuweka uzio ifanyike ili kuepuka migogoro inayojitokeza.

68

Picha Na. 23: Hili ni jengo mojawapo la vyumba vya madarasa katika shule ya

msingi Lubakaya

69

Picha Na. 24: Haya ni majengo ya vyoo yaliyojengwa katika

shule ya msingi Lubakaya

Picha Na. 25: Hili ni moja kati ya mashimo ya

vyoo katika shule ya Msingi Lubakaya

70

4.12 Ukarabati wa Soko la Buguruni

Utangulizi

Kwa kifupi Soko la Buguruni lilianzishwa mnamo mwaka 1978 likiwa lina

wafanyabiashara takribani 500 ambao walikuwa wauzaji wa rejareja. Kadri

miaka ilivyozidi kwenda na kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu

yamekuwa yakifanyika maboresho mbalimbali ya kupandisha hadhi ya soko ili

kukidhi mahitaji na ubora kwa watumiaji.Adiha, Halmashauri katika

kutekeleza agizo la Serikali lilitolewa na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala

za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Suleiman Jaffo (MB.) lililohusu

ujenzi/uboreshaji wa masoko nchini, walianza kutekeleza agizo hilo kwa

kuhakikisha masoko yanapimwa na kufanya maboresho yanayostahili.

a) Utekelezaji

i. Zoezi la upimaji wa Soko limefanyika na hatua za ujenzi wa mabanda

umekamilika kwa hatua za upauaji.

ii. Hati bado haijapatikana

iii. Bado ile dhana ya kuondoa bidhaa kutoka chini ya ardhi na kuziweka

juu ya vizimba/ meza haijafanyika.

b) Mafanikio

i) Eneo la soko tayari limepimwa jambo ambalo litasaidia Halmashauri kujua mipaka na uhalali wa umiliki wake.

ii) Halmashauri kuweka kipaumbele cha kuboresha masoko yake likiwemo soko la Buguruni ambalo litakuwa la kisasa zaidi.

c) Changamoto

i) Kiasi cha makusanyo kwa mwezi ni Sh. 34,910,000, (milioni thelathini na nne laki tisa na kumi elfu) kilichotajwa hakilingani na ukubwa wa soko hilo kwa maana ya makadirio ya idadi ya wauzaji na wanunuzi wanaokuwepo katika soko hilo kila siku. Wastani wa wafanyabiashara kwa siku ni 3,000 na kiwango cha chini ni Tshs. 500/=

ii) Takwimu ya wauzaji wa bidhaa iliyotajwa kuwepo sokoni hapo hailingani na hali halisi iliyoonekana sokoni hapo.

iii) Hakuna maeneo ya maegesho ya magari. iv) Miundombinu ya vyoo ni mibovu licha ya kuwa inaingiza makusanyo

mengi.

71

d) Maoni

Halmashauri ihakikishe kwamba:-

i) Inasimamia masoko yenyewe kwa kuingia mkataba na wafanyabiashara

moja kwa moja bila kuruhusu mambo ya kamati za masoko. Mfano mzuri

ni kutoka katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kupitia soko

linalojulikana kama mahakama ya ndizi (Mabibo) ambapo wakati

lilipokuwa linaendeshwa na watu binafsi, Halmashauri ya Manispaa ya

Kinondoni (kwa kipindi hicho) ilikuwa ikipata takribani Sh. milioni 3 kwa

mwezi. Kwa sasa lipo chini ya usimamizi wa Halmashauri ya Manispaa ya

Ubungo na makusanyo kwa mwezi ni kati ya Sh. Milioni 70 hadi 80 kwa

mwezi.

ii) Inahimiza matumizi ya Electronic Fiscal Devices (EFDs) katika

ukusanyaji wa mapato.

iii) Inafanya sensa ili kupata takwimu sahihi ya wafanyabiashara pamoja na

kufanya tathimini ya viwango vyao vya ushuru katika soko hilo.

iv) Inaimarisha usafi na mazingira hususan suala la vyoo kwa usalama wa

afya za watu waliopo katika soko hilo lakini pia kwa wakazi wote wa Jiji la

Dar es Salaam.

v) Inafuatilia hati ya eneo la soko hilo.

72

Picha Na.26: Inaonesha maboresho yaliyofanyika katika soko la Buguruni

73

Picha Na. 27: Hapa ni moja kati ya sehemu za kuingilia na kutokea katika soko la Buguruni

74

4.13 UJENZI WA MRADI WA MAJI KIPUNGUNI ‘B’

Utangulizi

i) Ujenzi wa mradi wa maji katika eneo la Kata ya Kipunguni ulianza tarehe 14/07/2014 na kukamilika tarehe 10/05/2017. Kama ilivyo miradi mingine, ujenzi huo pia haukukamilika kwa wakati kutokana na kuchelewa kupata msamaha wa kodi ya vifaa kutoka TRA na ucheleweshwaji wa kuondosha miundombinu iliyokuwepo awali na taasisi husika.

a) Utekelezaji

i) Ujenzi umekamilika isipokuwa Kamati ya maji bado. ii) Ujenzi umejumuisha kisima cha maji chenye urefu wa mita 120, Tanki la

lita 250,000, vituo vya kuchotea maji (DP's) 12, nyumba ya Pampu (Pump house), ufungaji wa Pampu, matenki 3 ya kuvuna maji ya mvua (rain water harvesting tanks) na mtanadao wa mabomba yenye urefu wa Km 9.057 na kufunga transfoma.

b) Mafanikio

i) Mradi umekamilika na hivyo utasaidia wakazi wa Mitaa ya Kipunguni ‘B’ na Mji Mpya na maeneo mengine kupata maji safi na salama (zaidi ya 6000 watapata huduma ya maji)

ii) Kufanikiwa kutatua changamoto zilizokuwa zikichelewesha ujenzi wa mradi kama vile kuchelewa kupewa msamaha wa kodi kutoka TRA na uondoshwaji wa miundombinu ya mabomba iliyokuwepo awali.

c) Changamoto

i) Umeme mdogo unaotokana na kuchelewa kuunganishiwa Umeme na TANESCO licha ya kuwa Mkandarasi alikwishalipia Transfoma ya kuongeza nguvu ya umeme.

ii) Kuchelewa kuunda Kamati ya maji.

d) Maoni

i) Ufuatiliaji wa upatikanaji wa umeme wa kutosha ufanyike. ii) Uundaji wa Kamati za maji uwe unafuata utaratibu yaani miezi 6 kabla ya

mradi kukamilika. iii) Uundaji wa Kamati hiyo ufanyike haraka ili mradi huu uanze kuwanufaisha

wananchi kwa usimamizi thabiti.

75

76

75

5. 0 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA TEMEKE

UTANGULIZI

Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya

Temeke ulianza tarehe 16 hadi 17 Mei, 2017. Shughuli za ukaguzi zilianza

kwa kujitambulisha kwa Mkurugenzi wa Halmashauri na baada ya hapo

kupata taarifa kwa ufupi ya miradi itakayotembelewa. Mchumi wa

Manispaa alielezea miradi ambayo itatembelewa, lengo la kila mradi,

tarehe ya kuanza na kukamilisha mradi, gharama za mradi, fedha

zilizotolewa na zilizotumika. Jumla ya miradi 11 ya maendeleo

ilitembelewa ambayo imeorodheshwa hapo chini:-

i) Ujenzi wa Jengo la ghorofa 1 kwa ajili ya Ofisi ya DMDP Manispaa ya Temeke

ii) Ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa shule ya sekondari Kibasila iii) Ujenzi wa vyumba 15 vya madarasa katika shule ya Msingi Rufu iv) Ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa katika shule ya Msingi Mbande Kata

ya Chamazi v) Ujenzi wa vyumba 10 vya madarasa katika shule ya Msingi Majimatitu

Kata ya Chamazi vi) Ujenzi wa Zahanati charambe iliyopo Kata ya Charambe vii) Ujenzi wa Shule ya Sekondari kidato cha V-VI katika Kata ya Kibonde

Maji. viii) Ujenzi wa barabara ya Kijichi- Nasaco yenye KM 1.2 ix) Ujenzi wa choo matundu 3 katika eneo la soka la buza lililopo Kata ya

Buza x) Ukarabati wa mfereji wa Evareti Chang’ombe Polisi kata ya

Temeke. xi) Ujenzi wa Mabanda 4 (manne) ya biashara katika soko la Temeke

Stereo

76

4.1: Ujenzi wa Jengo la Ghorofa Moja kwa Ajili ya Ofisi ya Dar

es Salaam Metropolitian Development Programme (DMDP)

Manispaa ya Temeke

Utangulizi

Mradi huu umeanza tarehe 15 Februari, 2017 na unatarajia kukamilika

tarehe14 Februari, 2018 lengo la Mradi ni kuimarisha miundombinu hasa

ujenzi wa barabara.

a) Utekelezaji

Mpaka sasa ujenzi wa Fremu, Bimu, nguzo na Slabu vimekamilika na

sasa jengo lipo hatua za umaliziaji.

b) Changamoto

- Manispaa haina Wataalam wa maabara hiyo

c) Maoni

i) Halmashauri ifundishe Wataalam wa Maabara ili pindi hao

Wafadhili wakiondoka halmashauri iweze kuendelea na kazi

hiyo.

ii) Maabara hiyo itangazwe ili ijulikane

iii) Halmashauri inashauriwa kumalizia Maghorofa mawili

yaliyobaki kwani Wafadhili hao wanajenga ghorofa 1

wakati msingi wake ni ya ghoropha 3

Picha Na.1 Mradi wa ujenzi wa ofisi ya DMDP ghorofa 1

77

4.2 Ujenzi wa Vyumba Vinne vya Madarasa Shule ya Sekondari Kibasila

Utangulizi

Ujenzi wa majengo hayo umelenga kuboresha elimu na kupunguza

uhaba wa madarasa shuleni hapo ambapo shule ina jumla ya

wanafunzi 1,343 kuanzia kidato cha I-VI na walimu 86.

a) Utekezaji

i) Vyumba vinne vimejengwa na vimepauliwa

ii) Huduma ya maji ipo na watoto wananawa mikono

b) Changamoto

i) Mradi bado haujapigwa plasta,

ii) ubao wa kufundishia haujawekwa, silling board, milango, sakafu na

wiremesh za madirishani hazijawekwa

iii) Malipo yamefanyika kwa asilimia 25 tu ya mradi inayogharimu sh. Milioni

themanini

(80,000,000/=).

iv) Miti ya miarobaini imepandwa mingi ambayo inahatarisha majengo

kuharibiwa na mizizi

c) Maoni

i) Malipo yafanyike kwa asilimia 100 ya mradi inayogharimu Sh.

Milioni themanini (80,000,000/=) ili madarasa yaanze

kutumika.

ii) Maelekezo yametolewa kuhakikisha kuwa ukamilishaji unafuata

vigezo

iii) Miti hiyo ya miarobaini iondolewe inaweza kuharibu miundo

mbinu ya majengo.

78

Picha na.2: Mradi wa ujenzi wa Madarasa manne shule ya Sekondari Kibasila

4.3 Ujenzi wa Vyumba 15 vya Madarasa Katika Shule ya Msingi Rufu

Utangulizi

Shule hii ni mpya ina darasa la Awali, la Kwanza, na la Pili ikiwa na jumla ya wanafunzi 741 na walimu 13. Ujenzi wa vyumba 15 vya madarasa katika shule ya msingi Rufu unaendelea (5 vinajengwa na Halmashauri na 10 vinajengwa na TATOA (Tanzania Truck Owners Associations) iliyokuwa imetafutwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick. a) Utekelezaji

i) Kwa sasa vyumba 3 tu vimekamilika na vinatumika. ii) Mradi unaotekelezwa na TATOA umesimama kwa kukosa

mawasiliano na wafadhili. Aidha, mradi upo katika hatua tofauti, vyumba 4 vimepauliwa, 3 havijapauliwa lakini vimepigwa plasta na 3 havijapauliwa wala havina plasta.

iii) Mradi wa ujenzi wa vyumba 5 wa Halmashauri vipo katika hatua za mwisho za ukamilishaji.

iv) Shule ina maji yaliyofadhiliwa na shirika la UNICEF

b) Changamoto

i) Vyumba vilivyopauliwa vinazidi kuharibika wakati mahitaji yangalipo

ii) Ash board hazijawekwa katika vyumba 5 vinavyokamilishwa.

79

iii) Hakuna huduma ya kunawa mikono japo maji yapo iv) Vyoo havina milango na vipo barabarani Walimu hawana Ofisi

c) Maoni

i) Halmashauri imeelekezwa na timu ya ukaguzi ya Mkoa kufuata utaratibu wa ujenzi kwa kufuata vigezo sahihi.

ii) Kufanya mawasiliano na TATOA ili ikiwezekana wamalizie majengo hayo.

iii) Halmashauri ikamilishe majengo hayo kwa kipato cha ndani (Own Source)

iv) Huduma ya wanafunzi kunawa mikono baada ya kutoka chooni izingatiwe.

v) Vyoo vitengenezewe milango

Picha na.4: Mradi wa madarasa 5 yanayofadhiliwa na Manispaa, Shule Msingi Rufu

80

Picha na.5: Mradi wa madarasa 10 Shule ya Msingi Rufu yaliyojengwa na shirika la TATOA ambayo

hayajakamilika

4.4 Ujenzi wa Vyumba 5 vya Madarasa Katika Shule ya Msingi Mbande Kata ya Chamazi

Utangulizi

Mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Mbande upo katika kata ya Chamazi kweye mtaa wa Mbande. Kutekelezwa kwa mradi huu ni juhudi za Halmashauri katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa vyumba vya vya madarasa linalosababisha msongamano wa wanafunzi kwenye vyumba vichache vilivyopo. Shule ina wanafunzi 6,274 kuanzia darasa la I-VII. na Walimu 90, vyumba vya madarasa ni 38, matundu ya vyoo 20 yanayotumika na 20 yanayojengwa.

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika ila bado rangi,wiremesh na sakafu

b) Changamoto

i) Ukamilishaji umesisitizwa

ii) Bado fedha za kukamilisha ujenzi

iii) Hakuna Ofisi ya Walimu

iv) Vyoo vya Walemavu ni vya kizamani

c) Maoni

i) Marekebisho yafanywe kwenye ubao

ii) Pia fedha zilizopelekwa shuleni zifuatiliwe

81

iii) Ofisi ya Walimu ijengwe ili kuboresha ufanisi wa kufundisha ili

kupata ubora wa elimu

iv) Vyoo vya Walemavu viboreshwe.

4.5 Ujenzi wa Vyumba Kumi vya Madarasa Katika Shule ya Msingi Majimatitu Iliyopo Kata ya Chamazi.

Utangulizi

Ujenzi wa vyumba 11 shule ya msingi Maji matitu umesaidia kupunguza uhaba wa madarasa kwani shule ina jumla ya wanafunzi 6,798 , Walimu 98 , madarasa 42 na matundu ya vyoo 42. Shule ina kisima cha DAWASCO.

a) Utekelezaji

-Ujenzi umekamilika

b) Changamoto

i) Madirisha hayana “wire mesh”

ii) Hakuna maji kwa sababu shule haina umeme wa kutosha

kupandisha maji

iii) Hakuna ofisi ya Walimu

iv) Walimu hawatoshi ni wachache

c) Maoni

i) Madirisha yawekewe nyavu

ii) Idara ya Mipango kwa kushirikiana na TANESCO itatue tatizo kwa

kuipatia shule umeme wa kutosha kusukuma maji

iii) Ofisi ijengwe na Halmashauri iongeze idadi ya Waalimu

82

Picha na.7: Mradi wa ujenzi wa madarasa 10 S/M Majimatitu

4.6 Ujenzi wa Zahanati Charambe Iliyopo Kata ya Charambe

Utangulizi

Katika kuboresha huduma za afya hasa kwa wakazi wa kata ya

Charambe, Halmashauri ilipanga kuanzisha ujenzi wa Zahanati katika

Kata hiyo. Mpango huu unatekelezwa kwa mapato ya ndani (Own source)

ya Halmashauri. Ujenzi wa Zahanati hiyo utasaidia kuhudumia wananchi

wa Charambe wanaosafiri umbali mrefu kutafuta huduma ya Afya.

a) Utekelezaji

Mradi upo katika hatua ya ukamilishaji

b) Changamoto

i) “Ramp” kwa ajili ya walemavu hazijawekwa

ii) Eneo halijapimwa

iii) hakuna maji

iv) Eneo halina uzio

v) Hakuna mfereji wa kutoa maji ya mvua nje ya zahanati

c) Maoni

i) “Ramp” za walemavu zijengwe

ii) Eneo lipimwe

iii) Eneo liwekewe uzio

iv) Manispaa ifanye utaratibu wa kuvuta maji hadi kwenye

zahanati hiyo.

83

v) Ghata ziwekwe kwa ajili ya kuvuna maji

vi) Mfereji wa kutoa maji nje uwekwe.

Picha Na 8: Mradi wa ujenzi wa Zahanati Charambe

4.7 Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kidato Cha V-VI Katika Kata

ya Kibonde Maji.

Utangulizi

Ujenzi wa vyumba 14 vya shule ya A level Mbagala sekondari unaendelea

ambapo mradi ulianza 2014/2015. Hii ni shule ya ghorofa 2, itakamilika

Septemba 2017 na itakuwa na maabara 2. Mkandarasi wa kwanza

alikuwa Mchina wakavunja mkataba akapatikana mkandarasi mwingine

ambaye anaendelea kujenga ambapo gharama za Mradi ni billion 1.2 na

amelipwa milioni 120 kama malipo ya gharama za awali.

a) Utekelezaji Hardcore, groundbeam na slabu ya chini vimekamilika. Column zote zimemiminwa kwa sasa kazi ya block work kwa sakafu ya chini inaendelea na inakadiriwa kufika asilimia 50. b) Changamoto

i) Ujenzi bado unaendelea kutokana na mvua kuwa nyingi magari

hayafiki eneo la mradi kupeleka vifaa vya ujenzi hasa mchanga na kokoto.

ii) Eneo halijapimwa na hakuna maji.

84

iii) Maabara 2 hazitoshi kwa wanafunzi wa mchepuo wa sayansi. iv) Mkondo wa maji unahitaji kutafutiwa njia muafaka, v) Eneo halijapimwa. vi) Mkandarasi anasuasua.

C) Maoni

i) Manispaa kwa kutumia idara ya ardhi ipime eneo hilo. ii) Manispaa kuongeza maabara moja zaidi

iii) Kuondoa mkondo wa maji unaopita eneo la ujenzi wa shule ili

kuepuka uharibifu wa miundo mbinu ya shule.

iv) Mkandarasi aonyeshe Mpango kazi wake ili kuondokana na

kusuasua kwake

Picha na. 9: Mradi wa ujenzi wa S/Sekondari Mbagala

8. Ujenzi wa barabara ya Kijichi - NASACO yenye KM 1.2 Utangulizi

Mradi huu ulianza kujengwa Julai 2015 na ulitarajiwa kukamilika Disemba 2015 na Mkandarasi anayetekeleza mradi huu ni CASCO. Mradi huu unajengwa kupitia fedha za ndani za Halmashauri (Own Source), ulichelewa kukamilika kutokana na upatikanaji wa fedha.Barabara ina jumla ya urefu wa Km 1.2, urefu wa awali ukiwa mita 905. Gharama ya jumla ya mradi ni Tsh. 904,000,000/-. Kuna nyongeza ya mita 300 anazoendelea kujenga Mkandarasi itakayogharimu Tsh. 330,000,000/- . a) Utekelezaji

i) Ujenzi umekamilika mita 905 kiwango cha lami na mitaro pande zote

85

ii) Kazi ya nyongeza inaendelea b) Changamoto

i) Kipande kilichoongezewa hakijakamilika ili barabara ianze kutumika

ii) Mabega (shoulders) za barabara ukamilishaji wake hayajajengwa vizuri kwanio zinamomonyoka.

iii) Wananchi wanaendelea na shughuli ya uchimbaji mchanga katika sehemu ya Karavati la juu hali itakayopelekea kuleta uharibifu katika barabara hiyo

iv) Maji yametuama katika mtaro kutokana na kuingiliwa na taka mbalimbali na nyingi.

d) Maoni

i) Wahandisi waendelee kusimamia kwa ukaribu ilikukamilisha sehemu iliyobaki

ii) Mabega (sholders) za barabara zimaliziwe vizuri kuweka uimara wa barabara

iii) Mifereji isafishwe mara kwa mara kuepusha maji kuingia barabarani na kuharibu barabara (Watendaji wa mtaa watumike)

iv) Wanaochimba mchanga wasitishwe na kufuatiliwa v) Mwenyekiti wa Mtaa aweke ulinzi kwa ajili ya wachafuzi wa

mifereji na wachimba mchanga pia waweke Sheria ndogo ili kuwezesha utekelezaji.

86

Picha na.10: Ujenzi wa Mradi wa barabara ya Kijichi –Nasaco ambayo shoulder zake ukamilishaji wake hazijajengwa vizuri

4.9 UJENZI WA CHOO MATUNDU 3 KATIKA ENEO LA SOKA LA BUZA LILILOPO KATA YA BUZA Utangulizi

Choo hicho kitasaidia kutoa huduma kwa wafanya biashara na kimejengwa na fedha za Halmashauri pia kitaongeza pato la Taifa na Halmashauri kwani kitakuwa choo cha kulipia. a) Utekelezaji

i) Ujenzi wa choo cha Buza kipo hatua ya ukamilishaji ii) Taratibu za malipo ya mwisho zinaendelea

b) Changamoto

i) Choo hakina ”ceiling board” ii) Choo hakijakamilika kwa wakati kwani kilitakiwa kikamilike

Septemba, 2016 sasa kinatarajiwa kuisha Julai 2017 iii) Soko halina wafanya biashara wa kutosha

87

c) Maoni

i) Kutafuta fedha kwa ajili ya ceiling board ii) Itafutwe mbinu ya kuhakikisha watu/Wafanyabiashara wanaenda

kufanyia biashara zao sokoni badala ya pembezoni mwa barabara

Picha na.11: Mradi wa ujenzi wa choo soko la Buza

4.10. UKARABATI WA MFEREJI WA EVARETI CHANG’OMBE POLISI KATA YA TEMEKE Utangulizi

Mfereji huo umekarabatiwa ili kupitisha maji sehemu moja yaliyokuwa yanatawanyika.

a) Utekelezaji i) Mfereji umekarabatiwa ii) Ujenzi wa mfereji wa maji ya mvua kwa kuchimba, kufunga waya,

kuweka changarawe, kujenga mfereji, kusuka vikapu vya mawe, kujenga kalvati na kazi ya ujenzi umekamilika.

b) Changamoto i. Barabara ya juu ya karavati hilo halijajengwa vizuri ii. Mkandarasi hajalipwa mpaka leo na anaendelea kudai fedha zake

c) Maoni i) Barabara iwekewe karavati na ijengwe kwa fedha za ndani za

Halmashauri.

ii) Mkandarasi alipwe fedha zake baada ya kukamilisha kazi.

88

Picha na.12: Mradi wa ukarabati wa mfereji Chang’ombe Polisi

4.11. UJENZI WA MABANDA MANNE YA BIASHARA KATIKA SOKO LA TEMEKE STEREO Utangulizi

Lengo la mradi ni upanuaji wa biashara ili kuongeza kipato cha wafanya biashara na Serikali. Mradi huu umeanza tarehe 17 Machi, 2016 na utakamilika tarehe 17 Juni, 2016 na mkandarasi ni MASUFIN'S GENERAL CO. LTD

a) Utekelezaji i) Mabanda 3 ya kuuza bidhaa yamekamilika na banda 1 la

machinjio ya kuku limekamilika ii) Mabanda yanatumika

b) Changamoto i) Hakuna sakafu kwenye mabanda hayo ii) Biashara nyingi zinauziwa chini iii) Takwimu sahihi za wafanyabiashara hazipo kwani wamiliki

wanaofahamika ni wale wapangishaji wa zamani.

c) Maoni i. Kutafuta fedha kwa ajili kwa kuweka sakafu ya zege ii. Wauzaji wa Chakula watafutiwe meza na mabanda ya kuuzia iii. Manispaa iepuke uwepo wa kamati ya soko ili kuepuka matumizi

mabaya ya fedha. iv. Utafiti wa kupata takwimu sahihi za wafanyabiashara ufanyike ili

kujua ni kiasi gan cha fedha kwa siku na kwa mwezi kitakusanywa.

89

Picha na.13: Mradi wa ujenzi wa mabanda 4 ya biashara soko la Temeke Stereo

Maoni ya jumla ya ufuatiliaji yaliyotolewa ya miradi ya Temeke

Timu ya ukaguzi ilitoa maoni ya jumla kama ifuatavyo:-

i) Fedha zinapotumwa shuleni, taarifa itolewe katika idara zote ili miradi

ifuatiliwe kwa utaratibu na kwa viwango vinavyotakiwa.

ii) Ujenzi wa vyumba vya madarasa uendane na ujenzi wa vyoo na Ofisi za

Walimu.

iii) Suala la afya na usafi wa mazingira shuleni hasa maeneo ya kunawa

mikono lipewe kipaumbele.

iv) Kupima maeneo ya shule ili kuepusha migogoro.

v) Kuanza utaratibu wa kuchimba kisima na kutengeneza mifumo ya

kukusanya/kuvunia maji ya mvua shuleni.

vi) Wakandarasi ambao hawajalipwa fedha zao walipwe kwa wakati.

vii) Kugawa shule zenye idadi kubwa ya wanafunzi na kuzisajili

viii) Miradi ya shule inayojengwa na Local fundi Wahandisi wa

Halmashauri waisimamie kwa umakini maana wanapojenga

wakikosea wahandisi ndio watakaowajibika kwani hawana mikataba

nao kama ya Wakandarasi.

90

TAARIFA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

UTANGULIZI

Ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni

ulifanyika tarehe 23 na 24 Mei, 2017. Jumla ya miradi nane ya maendeleo

ilikaguliwa. Ifuatayo ni taarifa ya kila mradi.

5.1 Ujenzi wa Vyumba 3 vya Madarasa Shule ya Msingi Bohari

Utangulizi

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni inaendelea kutekeleza Miradi ambayo

ilianzishwa na Halmashauri mama ya Temeke ukiwemo mradi huu wa ujenzi wa

vyumba 3 vya madarasa. Shule ina jumla ya wanafunzi 413 wa kuanzia darasa

la I hadi VII. Ujenzi umekemilka na madarasa yanatumika. Fedha hizi imetolewa

kwa msaada (Mfuko) wa Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

ambapo Mkandarasi ni ‘Local Fundi’

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na unatumika.

b) Changamoto i) Eneo la shule halijapimwa

ii) Ngazi za kuingia na kutokea madarasani zipo sehemu moja tu hivyo

kusababisha msongamano wa wanafunzi

iii) Ukubwa wa ubao hauridhishi (ni mdogo)

iv) Darasa la awali wanasomea nje

v) Vyoo vinavyotumika vimeanza vinaonesha kuanza kutitia

vi) Kuna mgogoro wa mipaka ya shule kati ya Wananchi na uongozi wa

shule

vii) Sakafu siyo imara hali inayopelekea kuanza kubomoka

viii) Vitasa na milango iliyowekwa siyo imara (sub standard)

c) Maoni i) Halmashauri ijitahidi kupima eneo la shule haraka na kuonesha

mchoro wa madarasa ya shule

ii) Kujenga ngazi upande wa pili kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji

maalum

iii) Kuongeza ukubwa wa ubao

iv) Kuongeza ujenzi wa madarasa ili darasa la awali wapate chumba cha

kusomea

91

v) Kufanya ukarabati vyooni na kutenga choo maalumu kwa wasichana

wenye uhitaji.

vi) Halmashauri ijitahidi Kutatua mgogogro wa ardhi uliopo kati ya

mwananchi na Shule

vii) Kufanya ukarabati wa baadhi ya madarasa

5.2 UJENZI WA VYUMBA 2 VYA MADARASA SHULE YA MSINGI

MWONGOZO

Utangulizi

a) Utekelezaji

Shule ina jumla ya wanafunzi 11,235. Ujenzi wa vyumba 2 vya

madarasa umekamilika na vinatumika.

b) Changamoto

i) Kutokuwapo kwa ngazi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum (ramp)

ii) Wavu uliowekwa kwenye madirisha ni dhaifu (sub-standard) iii) Shule haina madarasa ya kutosha iv) Kuwapo kwa nyumba ya mwalimu ambayo haijamaliziwa kwa muda

mrefu tangu mwaka 2012 v) Kutokuwapo kwa “Ash board” kwa ajili ya kuweka/kupokea unga wa

chaki vi) Kutofanya ukarabati vyooni na uchache wa matundu ya vyoo vii) Eneo la shule bado halijapimwa viii) Ushirikishwaji wa mradi ni mdogo kwani walimu wengine hawaujui mradi. Mradi unajulikana na Mwalimu Mkuu.

c) Maoni

i) Kujenga ngazi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum ii) Kurekebisha waya kwenye madirisha. Uliowekwa ni dhaifu. iii) Kujenga madarasa mengine ili kuweza kuchukua madawati yaliyopo nje

ya madarasa iv) Kumalizia ujenzi wa nyuma za walimu zilizojengwa mwaka 2012 bila

kukamilika. v) Kujenga Ash board kwa ajili ya kupokea chaki vi) Kufanya ukarabati vyooni na kujenga matundu mengine ya vyoo

ambavyo vitatenganisha matundu ya vyoo na mashimo yake vii) Kufanya upimaji wa eneo la shule ili kuondoa migogoro. viii) Kufanya ushirikishwaji wa miradi ya maendeleo kati ya Halmashauri na

wanufaika

92

5.3 UJENZI WA SHULE MPYA YA MSINGI MIKENGE KATA YA

KIMBIJI

a) Utekelezaji

Shule ina jumla ya wanafunzi 69. Mradi unafadhiliwa na Mdau (Abdallah

Salim) pamoja na nguvu za wananchi. Ujenzi wa madarasa matatu na

ofisi moja ya mwalimu upo hatua ya umaliziaji bado kuweka Ceiling

Board, milango, mbao za kuandikia na kupaka rangi.

b) Changamoto

i) Eneo la shule halijapimwa japo lilitolewa na mdau. ii) Hakuna mkataba wowote kati ya Mfadhili na Halmashauri iii) Hakuna mchoro wa kusaidia ujenzi wa madarasa yatakayoendelea

kujengwa iv) Hakuna jenereta kwa ajili ya kusukuma maji pamoja na kwamba maji

yapo shuleni. v) Shule bado haijapatiwa usajili japo Serikali imepeleka walimu vi) Kutokuwapo kwa ngazi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum vii) Hakuna milango kwenye vyoo 4

c) Maoni

i) Halmashauri kupima eneo la shule ii) Kuwapo Mkataba kati ya Mfadhili na Halmashauri iii) Kuwapo kwa michoro ya majengo ya Elimu inayokubalika iv) Kuweka “Ceilinga board”, milango, mbao za kuandikia na kupaka rangi ili

kuwapo na mazingira mazuri ya kujifunzia v) Kununua jenereta kwa ajili ya kusukuma maji shuleni vi) Kujenga ngazi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum vii) Kuweka milango kwenye vyoo 4

5.4 Ujenzi wa mradi wa Maji kisarawe II - Mwasonga

a) Utekelezaji

Ujenzi wa ‘Riser’ ya mita sita kwa ajili ya kuweka tanki lenye ujazo wa lita

elfu ishirini, ujenzi wa vituo 15 vya kuchotea maji, kukarabati nyumba na

kununua pump zimeshakamilika. Mradi huu bado haujaanza kutumika

kutokana na kutoshirikiana kati ya Halmashauri, Kamati ya Maji na

Mkandarasi. Aidha, huu ni mradi mmojawapo ya miradi iliyokuwa

inatekelezwa na Halmashauri ya manispaa ya Temeke na kuhamishiwa

Kigamboni bila fedha.

b) Changamoto

i) Kutokamilika kwa mradi kwa wakati. Mradi huu una kipindi kirefu ambacho ni zaidi ya miaka mitatu;

93

ii) Kuna Ushirikiano mdogo uliopo kati ya kamati ya Maji, Wataalam wa Halmshauri na Mkandarasi

iii) Baadhi ya vituo vya kuchotea maji kutotoa maji na kusababisha wananchi kukataa kuupokea mradi.

c) Maoni

i) Halmshauri kuakikisha mradi unakamilika haraka iwezekanavyo ii) Ushirikiano na uwazi kati ya kamati ya maji, wataalam wa Halmashauri

na Mkandarasi uharakishwe ili kumaliza tofauti zilizopo. iii) Kuhakikisha vituo vya kuchotea maji (DPs) 15 zinatoa maji kama mradi

ulivyosanifiwa iv) Pawepo ushirikiano wa kutosha kati ya Halmashauri ya Manispaa ya

Temeke na Kigamboni ili kuhakikisha mradi unakamilika. Makabithiano yawe bayana.

5.5 Ujenzi wa jengo la wazazi zahanati ya kisarawe II

a) Utekelezaji

Mradi huu ulianza rasmi mwaka 2012 na jengo kukamilika mwaka 2016

na vifaa tiba vilipatikana mwaka 2017. Ujenzi huu umefadhiliwa na Water

Com (Said Munifu). Jengo hili ni kwa ajili ya wodi ya wazazi, kuhudumia

mama waja wazito katika kata ya Kisarawe II ili kuwapunguzia akina

mama umbali mrefu kwenda kujifungua katika vituo vya mbali. Jengo

limegawanywa katika vyumba vitatu ambapo chumba I ni Wodi ya waja

wazito (Antenatal ward), chumba II ni Wodi ya kujifungulia (Labour

ward) na chumba cha III ni Wodi ya waliojifungua (Post Natal)

b) Changamoto

i) Shimo dogo maalum (Placenta pit) kwa ajili ya kuweka kondo la uzazi

baada ya mama kujifungua ni dogo sana kwani lililopo harufu inaweza

kurudi ndani.

ii) Hakuna “incinerator” za kuchomea taka ngumu iii) Vitanda havitoshelezi kulala wazazi masaaa 24 ya uangalizi. iv) Kutokuwapo kwa “heater” kwa ajili ya mama wajawazito kupata maji ya

moto ya kuoga kabla na baada ya kujifungua. v) Usafi wa wodi hauridhishi vi) Waya wa kutolea umeme kutoka kwenye jengo la zahanati kuingia

kwenye wodi ya wazazi ni mdogo sana (hauna kiwango).

c) Maoni

i. Kuongeza ukubwa wa ‘Placenta Pit’ ii. Kujenga incinerator za kuchomea taka ngumu iii. Kuongeza vitanda viwili na vifaa tiba k.m. tray maalum za kujifungulia. iv. Kufanya uangalizi wa mama na mtoto kwa masaa 24 v. Kufanya usafi wa labour word na itumike ipasanyo vi. Kuweka heater kwa ajili ya mama wajawazito kupata maji ya moto ya

kuoga kabla na baada ya kujifungua.

94

vii. Kutumia condwit kuingiza umeme wa uhakika katika jengo la wazazi viii. Utaratibu wa makabidhiano kati ta Mdau na Halmashauri ufanyike ix. Kufanya ushirikiano kati ya Mfadhili na Halmashauri ili kuwepo kwa

ubora wa miradi

5.6 Ujenzi wa madarasa 2 Shule ya msingi Kisiwani

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na madarasa yanatumika. Ujenzi umefanywa kwa

nguvu za wananchi kwa kushirikiana na Halmashauri

b) Changamoto

i. Kutokuwapo kwa waya kwenye madirisha yaliyojengwa na wananchi

ii. Kutokuwapo Ash board kwenye mbao za madarasa

iii. Ufinyu wa matundu ya vyoo

iv. Upungufu wa madarasa

v. Kutokuwapo ofisi ya waalimu ambao kwa sasa wanatumia darasa

vi. Baadhi ya maeneo rangi haijamaliziwa inavyotakiwa

vii. Kuwapo kwa nyumba za walimu mbili ambazo hazijamaliziwa kwa muda

mrefu (nyumba zilijengwa mwaka 2012)

viii. Kutokuwapo kwa ngazi (ramph) kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji

maalum

ix. Hakuna vyoo kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum

c) Maoni

i. Kuweka waya kwenye madirisha yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi ii. Kuweka Ash board kwa ajili ya kupokea chaki iii. Kuongeza matundu ya vyoo ili kukabiliana na uhaba uliopo iv. Kujenga madarasa mengine ili kutatua upungufu wa madarasa uliopo v. Kujenga Ofisi ya Waalimu ambao wanatumia darasa kama Ofisi vi. Kumalizia kupaka rangi katika sehemu ya juu ya madarasa vii. Kumalizia ujenzi wa nyumba za waalimu mbili za muda mrefu viii. Kujenga ngazi (ramph) vyooni kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji

maalum

5.7 Ujenzi wa mfereji wa dharura wa maji na

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na mradi unatumika

b) Changamoto

i. Baadhi ya maeneo ya mradi kutitia

ii. Kutokuwapo kingo zinazoweza kusaidia usalama wa wananchi (mfefreji

una kina kifefu kiasi kwamba mtu akitumbukia kwa bahati mbaya

atavunjika vibaya).

95

iii. Kuwapo kwa nyufa katika baadhi ya maeneo ndani ya mfereji.

iv. Kutokuwapo kwa sehemu ambazo wananchi wanaiweza kupita (mfereji

umejengwa bila kuzingatia kuwa kuna watu wenye nyumba na

wanafanya biashara pembeni.

c) Maoni

i) Kufanya marekebisho ya sehemu zinazotitia

ii) Kujenga kingo ili kuimarisha usalama wa wananchi

iii) Kufanya ukarabati katika mfereji (kuziba nyufa)

iv) Kujenga sehemu za kupitia wananchi/ wafanya biashara.

5.8 Mradi wa Maji katika Shule ya Msingi Kijaka

a) Utekelezaji.

Mradi umetekelezwa na Ufadhili wa Watu wa Kuwait. Aidha, mradi huo

umeshaanza kutumika

b) Changamoto

i) Wataalam wa Halmashauri kutoshiriki katika utekelezaji;

ii) Kutokuwepo (distribution point) katika eneo la shule. Maji hayafiki chooni

iii) Kuwapo kwa tanki dogo la lita 2000 ambalo halikidhi mahitaji ya shule

iv) Kuwapo kwa matundu machache ya vyoo. Lipo tundu moja tu la choo

v) Uhaba wa vyumba vya madarasa hali inayopelekea darasa la tatu na la

tano kutumia chumba kimoja

c) Maoni

i) Wataalam wa Halmashauri kushiriki kikamilifu katika Utekelezaji wa Miradi ya

maendeleo;

ii) Kujenga (distribution point) katika eneo la shule

iii) Kujenga tanki kubwa ili kukidhi mahitaji ya shule na majirani

iv) Kujenga matundu ya vyoo ili kukabiliana na upungufu uliopo

v) Kujenga vyumba vya madarasa ili kila darasa liwe na chumba cha kujifunzia

vi) Halmashauri kufanya usimammizi wa miradi ya wafadhili na kutoa ushauri

wa kitaalam

vii) Idara ya Elimu ishirikiane na idara ya Maji katika ujenzi wa miradi ya maji ya

wafadhili mbalimbali ili kujenga mradi bora.

96

TAARIFA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

UTANGULIZI

Ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya

Kigamboni ulifanyika tarehe 23 na 24 Mei, 2017. Jumla ya miradi nane ya

maendeleo ilikaguliwa. Ifuatayo ni taarifa ya kila mradi.

5.9 UJENZI WA VYUMBA 3 VYA MADARASA SHULE YA MSINGI

BOHARI

Utangulizi

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni inaendelea kutekeleza Miradi

ambayo ilianzishwa na Halmashauri mama ya Temeke ukiwemo mradi

huu wa ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa. Shule ina jumla ya wanafunzi

413 wa kuanzia darasa la I hadi VII. Ujenzi umekemilka na madarasa

yanatumika. Fedha hizi imetolewa kwa msaada (Mfuko) wa Mh. Rais wa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Mkandarasi ni ‘Local Fundi’

d) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na unatumika.

e) Changamoto

ix) Eneo la shule halijapimwa

x) Ngazi za kuingia na kutokea madarasani zipo sehemu moja tu hivyo

kusababisha msongamano wa wanafunzi

xi) Ukubwa wa ubao hauridhishi (ni mdogo)

xii) Darasa la awali wanasomea nje

xiii) Vyoo vinavyotumika vimeanza vinaonesha kuanza kutitia

xiv) Kuna mgogoro wa mipaka ya shule kati ya Wananchi na uongozi wa

shule

xv) Sakafu siyo imara hali inayopelekea kuanza kubomoka

xvi) Vitasa na milango iliyowekwa siyo imara (sub standard)

b) Maoni

i. Halmashauri ijitahidi kupima eneo la shule haraka na kuonesha mchoro

wa madarasa ya shule

ii. Kujenga ngazi upande wa pili kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji

maalum

iii. Kuongeza ukubwa wa ubao

iv. Kuongeza ujenzi wa madarasa ili darasa la awali wapate chumba cha

kusomea

97

v. Kufanya ukarabati vyooni na kutenga choo maalumu kwa wasichana

wenye uhitaji.

vi. Halmashauri ijitahidi kutatua mgogogro wa ardhi uliopo kati ya

mwananchi na Shule

vii. Kufanya ukarabati wa baadhi ya madarasa

5.10 UJENZI WA VYUMBA 2 VYA MADARASA SHULE YA MSINGI

MWONGOZO

d) Utekelezaji

Shule ina jumla ya wanafunzi 11,235. Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa

umekamilika na vinatumika.

e) Changamoto

ix) Kutokuwapo kwa ngazi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum (ramp)

x) Wavu uliowekwa kwenye madirisha ni dhaifu (sub-standard) xi) Shule haina madarasa ya kutosha xii) Kuwapo kwa nyumba ya mwalimu ambayo haijamaliziwa kwa muda

mrefu tangu mwaka 2012 xiii) Kutokuwapo kwa “Ash board” kwa ajili ya kuweka/kupokea unga wa

chaki xiv) Kutofanya ukarabati vyooni na uchache wa matundu ya vyoo xv) Eneo la shule bado halijapimwa

Ushirikishwaji wa mradi ni mdogo kwani walimu wengine hawaujui mradi. Mradi unajulikana na Mwalimu Mkuu.

f) Maoni

ix) Kujenga ngazi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum x) Kurekebisha waya kwenye madirisha. Uliowekwa ni dhaifu. xi) Kujenga madarasa mengine ili kuweza kuchukua madawati yaliyopo nje

ya madarasa xii) Kumalizia ujenzi wa nyuma za walimu zilizojengwa mwaka 2012 bila

kukamilika. xiii) Kujenga Ash board kwa ajili ya kupokea chaki

xiv) Kufanya ukarabati vyooni na kujenga matundu mengine ya vyoo ambavyo vitatenganisha matundu ya vyoo na mashimo yake

xv) Kufanya upimaji wa eneo la shule ili kuondoa migogoro. xvi) Kufanya ushirikishwaji wa miradi ya maendeleo kati ya Halmashauri na

wanufaika

98

5.11 UJENZI WA SHULE MPYA YA MSINGI MIKENGE KATA YA

KIMBIJI

a) Utekelezaji

Shule ina jumla ya wanafunzi 69. Mradi unafadhiliwa na Mdau (Abdallah

Salim) pamoja na nguvu za wananchi. Ujenzi wa madarasa matatu na

ofisi moja ya mwalimu upo hatua ya umaliziaji bado kuweka Ceiling

Board, milango, mbao za kuandikia na kupaka rangi.

b) Changamoto

viii) Eneo la shule halijapimwa japo lilitolewa na mdau. ix) Hakuna mkataba wowote kati ya Mfadhili na Halmashauri x) Hakuna mchoro wa kusaidia ujenzi wa madarasa yatakayoendelea

kujengwa xi) Hakuna jenereta kwa ajili ya kusukuma maji pamoja na kwamba maji

yapo shuleni. xii) Shule bado haijapatiwa usajili japo Serikali imepeleka walimu xiii) Kutokuwapo kwa ngazi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum xiv) Hakuna milango kwenye vyoo 4

c) Maoni

viii) Halmashauri kupima eneo la shule ix) Kuwapo Mkataba kati ya Mfadhili na Halmashauri x) Kuwapo kwa michoro ya majengo ya Elimu inayokubalika xi) Kuweka “Ceilinga board”, milango, mbao za kuandikia na kupaka rangi ili

kuwapo na mazingira mazuri ya kujifunzia xii) Kununua jenereta kwa ajili ya kusukuma maji shuleni xiii) Kujenga ngazi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum xiv) Kuweka milango kwenye vyoo 4

5.12 Ujenzi wa mradi wa Maji kisarawe II - Mwasonga

d) Utekelezaji

Ujenzi wa ‘Riser’ ya mita sita kwa ajili ya kuweka tanki lenye ujazo wa lita

elfu ishirini, ujenzi wa vituo 15 vya kuchotea maji, kukarabati nyumba na

kununua pump zimeshakamilika. Mradi huu bado haujaanza kutumika

kutokana na kutoshirikiana kati ya Halmashauri, Kamati ya Maji na

Mkandarasi. Aidha, huu ni mradi mmojawapo ya miradi iliyokuwa

inatekelezwa na Halmashauri ya manispaa ya Temeke na kuhamishiwa

Kigamboni bila fedha.

99

e) Changamoto

j) Kutokamilika kwa mradi kwa wakati. Mradi huu una kipindi kirefu ambacho ni zaidi ya miaka mitatu;

vii) Kuna Ushirikiano mdogo uliopo kati ya kamati ya Maji, Wataalam wa Halmshauri na Mkandarasi

viii) Baadhi ya vituo vya kuchotea maji kutotoa maji na kusababisha wananchi kukataa kuupokea mradi.

f) Maoni

v) Halmshauri kuakikisha mradi unakamilika haraka iwezekanavyo vi) Ushirikiano na uwazi kati ya kamati ya maji, wataalam wa Halmashauri

na Mkandarasi uharakishwe ili kumaliza tofauti zilizopo. vii) Kuhakikisha vituo vya kuchotea maji (DPs) 15 zinatoa maji kama mradi

ulivyosanifiwa viii) Pawepo ushirikiano wa kutosha kati ya Halmashauri ya Manispaa

ya Temeke na Kigamboni ili kuhakikisha mradi unakamilika. Makabithiano

yawe bayana.

5.13 Ujenzi wa jengo la wazazi zahanati ya kisarawe II

a) Utekelezaji

Mradi huu ulianza rasmi mwaka 2012 na jengo kukamilika mwaka 2016

na vifaa tiba vilipatikana mwaka 2017. Ujenzi huu umefadhiliwa na Water

Com (Said Munifu). Jengo hili ni kwa ajili ya wodi ya wazazi, kuhudumia

mama waja wazito katika kata ya Kisarawe II ili kuwapunguzia akina

mama umbali mrefu kwenda kujifungua katika vituo vya mbali. Jengo

limegawanywa katika vyumba vitatu ambapo chumba I ni Wodi ya waja

wazito(Antenatal ward), chumba II ni Wodi ya kujifungulia (Labour ward)

na chumba cha III ni Wodi ya waliojifungua (Post Natal)

b) Changamoto

ii) Shimo dogo maalum (Placenta pit) kwa ajili ya kuweka kondo la uzazi

baada ya mama kujifungua ni dogo sana kwani lililopo harufu inaweza

kurudi ndani.

ii) Hakuna “incinerator” za kuchomea taka ngumu iii) Vitanda havitoshelezi kulala wazazi masaaa 24 ya uangalizi.

ix) Kutokuwapo kwa “heater” kwa ajili ya mama wajawazito kupata maji ya moto ya kuoga kabla na baada ya kujifungua.

x) Usafi wa wodi hauridhishi xi) Waya wa kutolea umeme kutoka kwenye jengo la zahanati kuingia

kwenye wodi ya wazazi ni mdogo sana (hauna kiwango).

100

c) Maoni

i. Kuongeza ukubwa wa ‘Placenta Pit’ ii. Kujenga incinerator za kuchomea taka ngumu iii. Kuongeza vitanda viwili na vifaa tiba k.m. tray maalum za kujifungulia.

iv. Kufanya uangalizi wa mama na mtoto kwa masaa 24 v. Kufanya usafi wa labour word na itumike ipasanyo vi. Kuweka heater kwa ajili ya mama wajawazito kupata maji ya moto ya

kuoga kabla na baada ya kujifungua.

vii. Kutumia condwit kuingiza umeme wa uhakika katika jengo la wazazi

viii. Utaratibu wa makabidhiano kati ta Mdau na Halmashauri ufanyike

ix. Kufanya ushirikiano kati ya Mfadhili na Halmashauri ili kuwepo kwa ubora

wa miradi

5.14 Ujenzi wa madarasa 2 Shule ya msingi Kisiwani

a) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na madarasa yanatumika. Ujenzi umefanywa kwa

nguvu za wananchi kwa kushirikiana na Halmashauri

b) Changamoto

x. Kutokuwapo kwa waya kwenye madirisha yaliyojengwa na wananchi

xi. Kutokuwapo Ash board kwenye mbao za madarasa

xii. Ufinyu wa matundu ya vyoo

xiii. Upungufu wa madarasa

xiv. Kutokuwapo ofisi ya waalimu ambao kwa sasa wanatumia darasa

xv. Baadhi ya maeneo rangi haijamaliziwa inavyotakiwa

xvi. Kuwapo kwa nyumba za walimu mbili ambazo hazijamaliziwa kwa muda

mrefu (nyumba zilijengwa mwaka 2012)

xvii. Kutokuwapo kwa ngazi (ramph) kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji

maalum

xviii. Hakuna vyoo kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum

c) Maoni

ix. Kuweka waya kwenye madirisha yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi

x. Kuweka Ash board kwa ajili ya kupokea chaki

xi. Kuongeza matundu ya vyoo ili kukabiliana na uhaba uliopo

xii. Kujenga madarasa mengine ili kutatua upungufu wa madarasa uliopo

xiii. Kujenga Ofisi ya Waalimu ambao wanatumia darasa kama Ofisi

101

xiv. Kumalizia kupaka rangi katika sehemu ya juu ya madarasa

xv. Kumalizia ujenzi wa nyumba za waalimu mbili za muda mrefu

xvi. Kujenga ngazi (ramph) vyooni kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji

maalum

5.15 Ujenzi wa mfereji wa dharura wa maji na

d) Utekelezaji

Ujenzi umekamilika na mradi unatumika

e) Changamoto

v. Baadhi ya maeneo ya mradi kutitia

vi. Kutokuwapo kingo zinazoweza kusaidia usalama wa wananchi (mfefreji

una kina kifefu kiasi kwamba mtu akitumbukia kwa bahati mbaya

atavunjika vibaya).

vii. Kuwapo kwa nyufa katika baadhi ya maeneo ndani ya mfereji.

viii. Kutokuwapo kwa sehemu ambazo wananchi wanaiweza kupita (mfereji

umejengwa bila kuzingatia kuwa kuna watu wenye nyumba na

wanafanya biashara pembeni.

f) Maoni

v) Kufanya marekebisho ya sehemu zinazotitia

vi) Kujenga kingo ili kuimarisha usalama wa wananchi

vii) Kufanya ukarabati katika mfereji (kuziba nyufa)

viii) Kujenga sehemu za kupitia wananchi/ wafanya biashara.

5.16 Mradi wa Maji katika Shule ya Msingi Kijaka

a) Utekelezaji.

Mradi umetekelezwa na Ufadhili wa Watu wa Kuwait. Aidha, mradi huo

umeshaanza kutumika

b) Changamoto

vi) Wataalam wa Halmashauri kutoshiriki katika utekelezaji;

vii) Kutokuwepo (distribution point) katika eneo la shule. Maji hayafiki chooni

viii) Kuwapo kwa tanki dogo la lita 2000 ambalo halikidhi mahitaji ya shule

ix) Kuwapo kwa matundu machache ya vyoo. Lipo tundu moja tu la choo

x) Uhaba wa vyumba vya madarasa hali inayopelekea darasa la tatu na la

tano kutumia chumba kimoja

102

c) Maoni

viii) Wataalam wa Halmashauri kushiriki kikamilifu katika Utekelezaji

wa Miradi ya maendeleo;

ix) Kujenga (distribution point) katika eneo la shule

x) Kujenga tanki kubwa ili kukidhi mahitaji ya shule na majirani

xi) Kujenga matundu ya vyoo ili kukabiliana na upungufu uliopo

xii) Kujenga vyumba vya madarasa ili kila darasa liwe na chumba cha

kujifunzia

xiii) Halmashauri kufanya usimammizi wa miradi ya wafadhili na kutoa

ushauri wa kitaalam

xiv) Idara ya Elimu ishirikiane na idara ya Maji katika ujenzi wa miradi

ya maji ya wafadhili mbalimbali ili kujenga mradi bora.

103

Ujenzi wa jengo la wazazi zahanati ya kisarawe II.

Vitanda vya kujifungulia kina mama katika zahanati ya kisarawe II.

104

Ujenzi wa Mradi wa Maji Kisarawe II

105

Kisima na Pump za Mradi wa maji wa Kisarawe II

Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya msingi Kisiwani

106

Boma la nyumba ya mwalimu katika shule ya Msingi Kisiwani

Ujenzi wa mfereji wa dharura wa maji

107

Ujenzi wa shule ya mpya ya msingi Mikenge Kata ya Kimbiji

Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa shule ya msingi Mwongozo

108

6.0 UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA

JIJI LA DAR ES SALAAM

5.1 Ukarabati wa ukumbi wa Karimjee:

Utangulizi:

Timu ya ukaguzi ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilitembelea miradi ya

maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

tarehe 26 Mei, 2017. Miradi iliyotembelewa ilikuwa ni ukarabati wa

ukumbi wa Karimjee na Ukarabati wa Miundombinu wa Kituo Kikuu cha

mabasi Ubungo.

a) Utekelezaji:

Shughuli zilizofanyika katika ukarabati wa ukumbi wa Karimjee zilikuwa ni

kubomoa, kujenga na kurekebisha sehemu zote chakavu kama vile

madirisha, milango kuziba sehemu za bati zinazovuja, kuweka celling

zilizoharibika, kukarabati mfumo wa maji, kukarabati mfumo wa vyoo,

kufunga viti vya kukalia na kuweka zulia jekundu na kupaka kuta rangi.

Kazi ya ukarabati ipo hatua ya mwisho kukamilika.

b) Changamoto

Maeneo mengine ambayo hayakuwa katika makisio ambayo ni

machakavu kujitokeza kwa ajili ya ukarabati hivyo kuongeza gharama za

ziada na muda wa ukarabati.

c) Maoni

i) Upembuzi yakinifu uwe unafanyika kabla ya kufanya makisio ili

kuepuka gharama za ziada.

ii) Umaliziaji wa maeneo mengine ufanyike kwa umakini ili kuhakikisha

upakaji rangi hauathiri maeneo ambayo hayatakiwi kuchafuliwa na rangi

mfano vishikio vya taa, matundu ya kutolea hewa na nakshi iliyowekwa

kwenye madirisha.

iii) Maamuzi ya kulipa gharama za ziada yafanyike haraka ilikukamilisha

mradi kwa wakati.

109

Picha Na.1: Upakaji rangi, uwekaji wa viti vya kukalia na karpeti katika

ukumbi wa mikutano Karimjee.

6.2 Ukarabati wa maegesho ya mabasi katika kituo cha Ubungo

a) Utekelezaji

Kituo kikuu cha mabasi cha Ubungo kinahudumia wasafiri wa kuingia na

kutoka mikoani na nchi za jirani ya Tanzania. Inakadiriwa zaidi ya watu

500 wanaingia na kutoka kila siku, hivyo wanahitaji kupata huduma

mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu rafiki ya maegesho ya

mabasi, sehemu za kupumzikia abiria, huduma za vyoo na huduma za

afya.

i) Ukarabati unaendelea kufanyika katika baadhi ya maeneo ya

maegesho. Nusu ya sehemu ya maegesho imekamilika

ii) Taa za usalama ndani ya Kituo zimewekwa

iii) Ukarabati wa vyoo vya umma umefanyika

b) Changamoto

i) Eneo kuwa na uwanda wa maji (water table) ulio wa juu na kufanya ukarabati kuwa ngumu.

ii) Mvua zinazoendelea kunyesha zimefanya ujenzi kuchelewa kukamilika kwa wakati

110

iii) Bado maeneo mengi ya ukarabati hayajafanyiwa ukarabati iv) Kuwepo kwa mashimo katika njia za maegesho ya magari hivyo

kusababaisha kutuama kwa maji.

c) Maoni

i) Ukarabati uharakishwe kwani wingi wa magari yanayotumia

maegesho haya yatasababisha uharibifu wa kuwa mkubwa zaidi

hivyo kuongeza gharama.

Picha Na.2: Maeneo ambayo bado hayajakarabatiwa eneo la maegesho

ya mabasi kituo kikuu cha Ubungo.

ii) Kituo kina sehemu ambayo inaweza kutumika kuweka Zahanati.

Halmashauri ya Jiji na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo wakae

wazungumze wajue namna ya kuanzisha Zahanati katika kituo cha

Mabasi Ubungo

iii) Huduma ya choo iboreshwe ili pawepona vyoo vingi zaidi

111

iv) Halmashauri ifanye maamuzi haraka na kutoa fedha kwa kazi

zilizoongezeka

Picha Na.3: Maeneo ambayo bado hayajakarabatiwa eneo la maegesho ya mabasi

kituoni.

63

ORODHA YA WALIOSHIRIKI KATIKA UGAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOTEKELEZWA NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA ZA MKOA WA DAR ES SALAAM HADI KUFIKIA ROBO YA TATU YA

MWAKA 2016/17

NA. JINA CHEO

1. Theresia Mmbando Katibu Tawala wa Mkoa

2. Yokobety N. Malisa Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu

3. Edward A. Otieno Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji

4. Mary P. Assey Katibu Tawala Msaidizi Huduma za Serikali za Mitaa

5. Michael Ole Mungaya Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu

6. Lawrence Malangwa Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu

7. Eng. Elizabet Kingu Katibu Tawala Msaidizi Maji

8. Mbaraka M. Kumenya Afisa Ugavi Mkuu

9. Rogasian E. Kimaryo Mchumi Mkuu

10. Upendo Charles Afisa TEHAMA Mwandamizi

11. Athumani Mayunga Mchumi

12. Oble F. Mongi Mtakwimu

13. Given Sure Afisa Maendeleo ya Jamii

14. Esterine Sephania Afisa Maendeleo ya Jamii

15. Issaya Mngurumi Mshauri Sekretarieti Ya Mkoa

16. Josephat N. Shehemba Mhandisi Ujenzi

17. Gilbert Bakula Mkadiriaji Majengo

18. Gratius Haule Mhandisi Maji

19. Eng. Mussa Natty Mshauri Sekretarieti Ya Mkoa

20. Bernadetha Thomas Afisa Elimu Mkuu

21. Jumanne Ndaigeze Afisa Biashara Mkuu

22. Hilda Kigoda Msanifu Ramani

23. Vicenti Mseti Mhasibu

24. Forunatus M. Kagoro Mshauri Sekretarieti ya Mkoa

25. Sister Mathew Katibu wa Afya Mkoa

26. Ackim Mwaikasu Afisa Afya

27. Mussa B. Abdallah Mhandisi Maji

28. Mambo Gunze Afisa Ugavi

29. Damsoni Mlashani Afisa Ugavi

64

30. Benedict Tesha Mkaguzi wa Ndani

31. Atupele J. Mwaipasi Mkaguzi wa Ndani

32. Diana Lema Afisa TEHAMA