fataawa za wanachuoni (30)

39
1 علماء ال فتاوىFataawa Za Wanachuoni [30] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Upload: wanachuoni

Post on 13-Apr-2015

272 views

Category:

Documents


6 download

DESCRIPTION

Fataawa Za Wanachuoni (30)

TRANSCRIPT

Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (30)

1

فتاوى العلماءFataawa Za Wanachuoni

[30]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (30)

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (30)

3

Fataawa zilizomo:

1) Mwanamke Anataka Kufunza Kidogo Alichokipata Kwa Wanazuoni

2) Wanyama Wangapi Mtu Atachinja Akipata Watoto Mapacha?

3) Masharti Ya Mwanamke Kutoka Na Kwenda Sokoni

4) Lipi Lakufanya Fataawa Mbili Zikigongana?

5) Lipi Lakufanya Fataawa Mbili Zikigongana?

6) Kusoma Kiarabu Katika Madrasah Ya Mchanganyiko

7) Kununua Au Kuuza Simu Za Camera

8) Kumsomea Mtu Ruqyah Kwa Kitabu Cha Aayah Na Hadiyth

9) Kufanya Kazi Kwenye Mgawaha Wanapohudumia Nguruwe Na Pombe

10) Kuashiria Mkono Anapotoa Mtu Salaam Na Uko Unaswali

11) Khawaarij Wanaokufurisha Watawala

12) Je Kusoma Kwa Kupangilia Suurah Ni Wajibu?

13) Hukumu Ya Mahram Kafiri Kwa Mke Wangu

14) Hukumu Ya Swawm Ya Pamoja (Kundi)

15) Hukumu Kwa Anaemtetea Abu Ishaaq al-Huwayniy

16) Shaykh Dr. as-Suhaymiy Kuhusu ´Aliy al-Halabiy Kuipiga Radd al-Lajnah ad-

Daa´imah

17) ´Allaamah Shaykh Rabiy´ Kuhusu Usaamah al-Quusiy Na Abul-Hasan

18) Kunyoa Ndevu Ni Kujifananisha Na Wanawake Na Ni Laana

19) Vitabu Vinasomwa Kwa Wanachuoni

20) Vipi Mzazi Afanye Uadilifu Kati Ya Mtoto Wa Kiume Na Wa Kike?

21) Wanaume Waliolaaniwa Wanaojifananisha Na Wanawake Na Makafiri

22) Upi Wajibu Wetu Kwa Aliyekataa Kutoa Zakaah?

23) Umekumbusha Yatosha!

24) Swali Lako Halina Faida Kwa Sasa!

25) Swalah Ya Usiku Ina Idadi Rakaa Maalumu?

26) Hukumu Ya Kula Nyama Ya Mtu Asiyeswali

27) Aliyeacha Swalah Ni Lazima Atoe Shahaadah Atapoanza?

28) Unyenyekevu Wa Shaykh ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad

29) Ni Wajibu Kutahadharisha Dhidi Ya Watu Wa Bid´ah

30) Mkutano Wa Shaykh al-Albaaniy Na Shaykh Ibn ´Uthamiyn

31) Hukumu Ya Kumpa Zakaah Mume Wako

32) Je Mwanamke Anaweza Kumuomba Mwanaume Kumuoa?

33) Iko Wapi Demokrasia Ya Hawa Makafiri?

34) Hili Ni Swali La Ajabu Sijawahi Kusikia Maishani

35) Dalili Ya Qur-aan Inayofuta Vitabu Vilivyotangulia

36) Je, al-Ikhwaan al-Muslimuun Ni Katika Ahl-us-Sunnah?

37) Hukumu Ya Mwanamke Kuzuru Makaburi -1-

38) Baina Yetu Sisi Na Nyinyi Ni Vitabu Vya Salaf

39) Sifa Na Tabia Za Mja Zimeumba Na Allaah

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (30)

4

40) Ni Lazima Kwa Muadhini Awe Twahara

41) Mume Ana Wake Wawili Kumuacha Mmoja

42) Madhehebu Manne Ni Katika Makundi 72 Ya Motoni?

43) Kupigana Jihaad Pamoja Na Ahl-ul-Bid´ah

44) Kuweka Mlio Wa Simu Wa Adhaana, Qur-aan Au Dhikr

45) Kupiga Radd Watu Wa Bid´ah Ambao Wanalingania Watu Katika Bid´ah Zao

46) Kumsimamishia Mtu Hoja Kabla Ya Kumhukumu Kuwa Ni Mtu Wa Bid´ah

Wanachuoni waliomo:

1) Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

2) Imaam Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy

3) Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

4) ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy

5) ´Allaamah Ahmad bin Yayhaa an-Najmiy

6) ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

7) ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy

8) ´Allaamah Zayd bin Haadiy al-Madkhaliy

9) ´Allaamah ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad

10) Shaykh Muhammad bin Haadiy al-Madkhaliy

11) Shaykh Swaalih bin Sa´iyd as-Suhaymiy

12) Shaykh Abu ´Abdul-Haaliym ´Abdul-Haadiy

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (30)

5

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1) Mwanamke Anataka Kufunza Kidogo Alichokipata Kwa Wanazuoni

Swali:

Naishi Uingereza na nimekwishasoma baadhi ya vitabu vya wanachuoni, je

naweza kuwafunza watu kiasi hichi kidogo ambacho nimepata katika kusoma

vitabu hivyo?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Ni wajibu kwanza kunibainishia uliyoyaandika na ukayapata kwa baadhi ya

hao wanachuoni ambao yawezekana kweli ulipata kwao, likidhihirika kwako

hilo - ni wajibu kwako kufunza hichi ambacho ulipata kwao - namna hii,

kidogo kidogo.

Chanzo: http://youtu.be/hwoIo0Pra8M

2) Wanyama Wangapi Mtu Atachinja Akipata Watoto Mapacha?

Swali:

Ni wangapi itachinjwa kwa mapacha wawili?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Ikiwa ni mapacha wakiume, ni minyama minne. Na ikiwa ni wakike minyama

itakuwa ni miwili. Na ikiwa ni wakiume na wakike minyama itakuwa mitatu;

mwanamume miwili na wakike mmoja. Lakini huenda baadhi ya watu

wakafikiria kuwa kufanya 'Aqiyqah ni wajibu na sivyo, ´Aqiyqah ni Sunnah

mustahaba na sio wajibu.

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (30)

6

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=109

3) Masharti Ya Mwanamke Kutoka Na Kwenda Sokoni

Swali:

Yapi masharti ya mwanamke kutoka [kwenda] sokoni?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Atoke na Mahram ambaye ni mkubwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) kasema kuwa Shaytwaan huyaweka macho yake kwa mwanamke

anapotoka. Inatakiwa kwa Muislamu (mume) kutomsikiliza mke wake kutoka

kwenda sokoni isipokuwa awe pamoja naye Mahram. Na awe amejisitiri na

ajiepushe na mahala ambapo kumejaa watu wengi.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=6

4) Lipi Lakufanya Fataawa Mbili Zikigongana?

Swali:

Je inajuzu kwa wanawake kuswali mbele ya safu ambayo Imamu anaswali

ikiwa Msikiti umejaa na hawawezi kuswali sehemu ya wanawake, wanaswali

nje ya Msikiti na wakifanya hivyo itakuwa safu yao mbele ya Imaau?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Hili ni kosa wala haifai. Ima wawe nyuma ya wanawake au waswali

majumbani kwao. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kakataza na

kwamba bora ya Swalah ya mwanamke ni katika nyumba yake.

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (30)

7

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=108

5) Lipi Lakufanya Fataawa Mbili Zikigongana?

Swali:

Upi msimamo wa mtafutaji elimu (wanafunzi) anayeanza kwa Fataawa

ambazo zinatofautiana?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Aulize wanachuoni wa Sunnah na awaombe kutoka kwao dalili, ataekuwa na

dalili kwa kauli yake huyu ndiye ambaye inafaa kuchukua [kauli yake].

Chanzo: http://youtu.be/yEvubNcN3_0

6) Kusoma Kiarabu Katika Madrasah Ya Mchanganyiko

Swali:

Kuna dada anasoma lugha ya kiarabu katika Madrasah mchanganyiko na

ndio Madrasah yalioko karibu yake. Je, inajuzu kwake kusoma katika

Madrasah haya mpaka atapopata njia ingine ajifunze lugha?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Uhakika ni kwamba Madrasah mchanganyiko ni fitina sawa kwa vijana na

wasiokuwa vijana. Kusoma kwake kwa haya Madrasah ni makosa na Mtume

kakataza hili.

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (30)

8

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=110

7) Kununua Au Kuuza Simu Za Camera

Swali:

Ipi hukumu ya kuuza simu za Camera na Bluetooth? Na ipi hukumu ya

kununua pia ikiwa mtu huyo haitumii Camera hii kwa kupiga picha viumbe

vyenye roho?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Haijuzu kuziuza wala kuzinunua. Hata yule mwenye anaziuza hana uhakika

kwa yule anayezitumia, huenda ni mmoja katika watu wake wa nyumbani

akapiga nazo picha.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=186

8) Kumsomea Mtu Ruqyah Kwa Kitabu Cha Aayah Na Hadiyth

Swali:

Muulizaji kutoka Ufaransa, mke wangu ni mgonjwa sana kwa majini na

uchawi, inajuzu kwangu kumsomea Matn ya al-Uswuul ath-Thalaathah kwa

kuwa iko na Aaayah na Hadiyth?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Ruqyah inakuwa kwa Aayah za Qur-aan na Sunnah ambazo ziko na dawa.

Msomee al-Faatihah, al-Kursiy, Aayah mbili za mwisho katika Suurat-ul-

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (30)

9

Baqarah na Aayah za wachawi, na Qul-HuwaLlaahu Ahad, na

A´udhubiLlaahi KalimaatiLlaahi at-Tammah, min kulli Shaytwaani

wahammah, wamin kulli ´aynin lammah. Haya ndo yanayopasa.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=180

9) Kufanya Kazi Kwenye Mgawaha Wanapohudumia Nguruwe Na

Pombe

Swali:

Nafanya kazi katika mgahawa ambapo mmiliki wake ni kafiri, kunapikwa

vyakula vya Haramu - kama vile pombe na nyama ya nguruwe. Ipi hukumu

ya kazi hii?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Tunachokunasihi ewe Muislamu ambaye unashahidilia ya kwamba hapana

Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah na kwamba Muhammad ni

Mtume wa Allaah, pamoja na hayo unafanya kazi ya kuhudumia nyama ya

nguruwe na pombe n.k. Najikinga kwa Allaah kutokana na hilo. Je

humuogopi kweli Allaah katika nafsi yako? Na ukawa mwenye kutafuta riziki

kwa njia nzuri na kujiweka mbali na mfano [wa kazi] kama hizi. Haikustahiki

[kazi] kama hii ewe Muislamu.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=855

10) Kuashiria Mkono Anapotoa Mtu Salaam Na Uko Unaswali

Swali:

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (30)

10

Hukumu ya kurudisha Salaam kwa ishara kwa mwenye kuswali ni khaswa

katika Swalah ya mwenye kuswali peke yake au Swalah ya Jamaa´ah? Na je

hukumu inabadilika wakati [Swalah] ya Naafil [Sunnah] na faradhi?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Yote hayo yanajuzu na wala hukumu zake hazibadiliki. Hukumu ya faradhi

na Naafil, zole mbili [zajuzu]. Akitoa Salaam mtu, atafanya namna hii [ishara]

na mkono wake.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=3

11) Khawaarij Wanaokufurisha Watawala

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kuwakufurisha watawala wa kiarabu katika wakati

huu?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Hii ndo hali ya Khawaarij ambao wanawakufurisha watu kwa madhambi.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=190

12) Je Kusoma Kwa Kupangilia Suurah Ni Wajibu?

Swali:

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (30)

11

Je ni sharti unaposoma Suurah iwe kwa mpangilio katika kukhatimu Qur-aan

au hapana?

Muulizaji:

Shaykh anamaanisha mpangilio.

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Kusoma kwa mpangilio ndio bora zaidi, na ikiwa hakufanya hivyo hakuna

ubaya. Mpangilio wa Suurah si lazima. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) aliwahi kuswali Swalah ya usiku akasoma al-Baqarah,

kisha an-Nisaa kisha al-´Imraan.

Chanzo: http://youtu.be/lOgpcjTWgpU

13) Hukumu Ya Swawm Ya Pamoja (Kundi)

Swali:

Ipi hukumu ya Swawm ya kundi? Kama kukusanyika kundi la watu na

kukubaliana kufunga masiku maalumu kama Jumatatu na alkhamisi na hivyo

kwa jili ya kusaidizana katika wema na taqwa; kwa kuwa mtu ni dhaifu katika

nafsi yake anapata nguvu kwa ndugu zake. Ipi hukumu ya hilo?

Imaam Ibn ´Uthaymyniyn:

Naona kuwa si katika Sunnah na ni aina ya Bid´ah, ikiwa watakubaliana hilo.

Kwa kuwa ikiwa tunakataa Takbiyra za pamoja au Dhikr za pamoja kwa

mfano, hii pia ni Swawm na Swawm ni ´Ibaadah. Haifai kuwa pamoja (kundi).

Lakini ikiwa bila ya makubaliano hakuna neno. Kwa mfano imetokea

tumefunga siku ya Jumatatu hivyo wakasema baadhi yetu kuwaambia

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (30)

12

wengine, waliofunga futari itakuwa kwa fulani na tunakubaliana kufuturu

kwake hili halina neno; kwa kuwa si jambo lililopangwa na mkusanyiko wetu

sio ´Ibaadah. Kukusanyika kwa ajili ´Ibaadah au kuwa pekee ni katika jambo

yaliyo katika Shari´ah. Na kwa hili lau kama Allaah Asingetuwekea Shari´ah

kuswali Jamaa´ah, tusingeliswali Jamaa´ah, ingekuwa kuswali Jamaa´ah ni

Bid´ah. Lakini Allaah Katuwekea hilo katika Shari´ah. Hali kadhalika Swawm

ya pamoja (kundi) na kukubaliana hilo kabla, ni aina katika Bid´ah. Baadhi

ya watu wanaweza kuuliza kuhusu Swawm ya Ramadhaan, je situnafunga

pamoja? Ni kweli, lakini hivyo ndivyo ilivofaradhishwa. Imefaradhishwa

kufunga watu wote katika mwezi huu. Mimi naona mtu aache njia hii na mtu

awe mwenye kumuomba Allaah (´Azza wa Jalla) na ajihesabu nafsi yake. Na

ikiwa mtu hawezi kufanya ´Ibaadah ila mpaka apate msaada katika fimbo -

yaani mpaka waifanye wengine - azima yake itakuwa dhaifu.

Chanzo: http://youtu.be/uG05kNiMttU

14) Hukumu Ya Mahram Kafiri Kwa Mke Wangu

Swali:

Je, inajuzu kwa mke wangu kujidhihirisha mbele ya baba yangu kafiri? Na ni

hukumu inayotumika kwa kila Mahram ambaye ni kafiri?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Anasema:

"Au wanawake wenzao". (33:55)

Yaani haijuzu kuonesha mapambo yao isipokuwa kwa wanawake Waislamu,

ama wanawake ambao si wa kiislamu haijuzu kwao kuonesha mapambo yao.

Hali kadhalika kwa baba ambaye ni kafiri, haifai kudhihirisha mapambao

mbele yake. Lakini kama kuacha wazi uso wake, mikono yake; ilimradi tu

hajiachii moja kwa moja mbele yake hili halijuzu.

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (30)

13

Chanzo: http://youtu.be/ypuLD4v0gfQ

15) Hukumu Kwa Anaemtetea Abu Ishaaq al-Huwayniy

Swali:

Ipi rai yako kwa yule anayemtakasa Abu Ishaaq al-Huwayniy na anamtetea?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Abu Ishaaq al-Huwayniy ana changanya, na yule anayemtakasa huenda

hajafikiwa na mchanganyiko huu. Akhabarishwe.

Chanzo: http://youtu.be/2evKwYL7zs8

16) Shaykh Dr. as-Suhaymiy Kuhusu ´Aliy al-Halabiy Kuipiga Radd al-

Lajnah ad-Daa´imah

Shaykh Dr. Swaalih bin Sa´iyd as-Suhaymiy:

Wenye haki ni al-Lajnah ad-Daa´imah. Na ´Aliy [bin] Hassan katika qadhiya

hii alichanganya mambo. Alikosea kuipiga Radd al-Lajnah. Kwa kuwa

hakuyafahamu maneno ya al-Lajnah, kamwe. Alikosea kupiga Radd al-

Lajnah. Alikosea. Na kaidhulumu nafsi yake. Kafungua njia ya kuikashifu al-

Lajnah bila ya kujua. Kafanya kosa, kafanya kosa, kafanya kosa, kosa mara

elfu. Na yuko na msemo ambao wanaingia humo Murji-ah. Yuko na msemo

ambao kunakhofiwa kuutumia Murji-ah. Mfano kwa kusema kwake wakati

fulani kuwa kuna kufuru ya matendo na Itikadi na mtu hakufuru ila

akianguka tu katika kufuru ya Itikadi. Hili si sahihi. Hata Shaykh wake,

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (30)

14

Shaykh [Muhammad] Naaswir-ud-Diyn [al-Albaaniy] kwa fadhila zake na

cheo chake, hatukubaliani nae katika qadhiya hii. Kuna kufuru ya matendo

ambayo inamtoa mtu katika Uilsamu. Kama kumtukana Allaah na Mtume

Wake, kusujudia sanamu, kukejeli Sunnah. Yote haya ni kufuru inayomtoa

mtu katika Uislamu.

Chanzo: http://youtu.be/mgnF8jnDuWw

17) Allaamah Shaykh Rabiy´ Kuhusu Usaamah al-Quusiy Na Abul-

Hasan

´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy:

Usaamah al-Quusiy kama mnavyojua, alikuwa Salafiy wa kweli In Shaa

Allaah. Kisha kulipokuja fitina za Abul-Hasan, akatumbukia humo. Kisha

akaendelea kuathirika na fitina hizi, mpaka akafikia katika daraja ambayo -

tunamuomba Allaah Awakinge Waislamu nayo na yeye pia. Na mimi

siwanasihi kudhudhuria mihadhara na duruus zake, mpaka atubie kwa

Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala) katika aliyotumbukia humo. Hakika ni katika

aliyeathirika na fitina za Abul-Hasan, na alisaidia fitina zake na kufanya

mambo ya kuipatia nguvu. Na mfano wa hilo ni ziara yake katika shirika hii

na mialiko yao kwake. Haya ni mambo nimeona na kuzama kwake zaidi

katika fitina. Na jitihada katika njama zao (za kuwadanganya watu) kuwa

mbali na Rabiy´ na ndugu zake (katika Wanachuoni), bali hata katika Manhaj

yenyewe ya Salaf. Abul-Hasan kazua misingi mingi na yote ni batili, na Abuu

Haatim (Usaamah al-Quusiy) hajakosoa katika hayo lolote. Isitoshe kwa sasa

anatakasa, kutetea na kuwasifia watu wa Bid´ah - kwa masikitiko makubwa.

Kaenda mbali zaidi katika fitina, hii imekuja kuwa kama ilivyokuwa tabia

yake. Tunamuomba Allaah Tawfiyq na tunamuomba Atusamehe sote. Kwa

hali yoyote jiwekeni mbali naye na mihadhara yake mpaka atubie kwa Allaah

na arudi katika Manhaj Salaf.

Chanzo: http://youtu.be/xghBDNTEUJA

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (30)

15

18) Kunyoa Ndevu Ni Kujifananisha Na Wanawake Na Ni Laana

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kwa mwanaume kujifananisha na wanawake katika mavazi yao,

kutembea kwao, kuongea kwao, kujipendezesha kwao wanawake. Haijuzu

kwake hilo kwa kuwa yeye ni mwanamume. Yahitajika kwake nguvu na

ukakamavu, hakuhitajiki kwake ulaini na kujiachia achia hivi ilihali ni

mwanamume. Asifike kwa sifa za wanaume. Kadhalika katika kujifananisha

na wanawake ni kunyoa ndevu, hii ni aina kubwa katika aina za kujifananisha

na wanawake. Kunyoa ndevu akawa mwanaume kama mwanamke. Kitu

kinachomtofautisha mwanaume na mwanamke ni ndevu. Hivyo [mwanaume]

akinyoa ndevu zake huwezi kutofautisha kati ya uso wa mwanamke na uso

wa mwanamume. Inatoweka alama inayowapambanua. Huku ni

kujifananisha wanaume kwa wanawake. Kamuumba nazo mwanaume na

kumnyima nazo mwanamke. Hivyo kamlaani Mtume ( وسلم ليهع هللا صلي )

anayelifanya. Na laana ni dalili ya kuonesha kuwa ni dhambi kubwa katika

madhambi makubwa. Ni wajibu kwa wanaume kujitofautisha na wanawake,

na ni wajibu kwa wanawake kujitofautisha na wanaume. Huu ndo wajibu.

كر وليس كاأل نثى الذ

“Na mwanamume si sawa na mwanamke.” (al-´Imraan 03:36)

Ama akiwa mwanamume kama mwanamke au mwanamke kama

mwanamume, hali itabadilika, laa hawla walaa Quwwata illa biLlaah. Na yeye

kajifananisha na sifa ya wanawake. Lakini ukimwambia wewe [unafanana] ni

kama mwanamke atakukasirikia au anaweza hata kukuua, ukimwambia

[mnyoa ndevu] wewe ni kama mwanamke, atakuua au atakupiga. Ilihali yeye

mwenyewe ndo anafanya jambo hili, anakuwa kama mwanamke.

Chanzo: http://youtu.be/hmwTFUaAgvM

19) Vitabu Vinasomwa Kwa Wanachuoni

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (30)

16

Swali:

Mwanafunzi anaeanza [kusoma] unamnasihi nini kwa vitabu katika elimu ya

tafsiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni kama tulivyosema tatizo si vitabu, vitabu vipo vingi wa Alhamdulillaah.

Lakini tatizo ni kupatikana mwanachuoni ambae utasoma kwake kitabu hiki.

Ukipata mwanachuoni ambae utasoma kwake, kitabu kitakuwa sahali. Ni juu

yake kushikamana na vitabu vyenye tafsiri ya zamani; tafsiri ya Ibnu-Jariyr,

tafsiri ya Ibnu-Kathiyr, tafsiri ya al-Baghawiy. Tafsiri za zamani ambazo

zimeegemea nususi [dalili] za kuaminika. Tafsiri ya Qur-aan kwa Qur-aan,

tafsiri ya Qur-aan kwa Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam),

tafsiri ya Qur-aan kwa tafsiri ya Maswahabah, tasfiri ya Qur-aan kwa kauli za

Taabi´iyn, tafsiri ya Qur-aan kwa lugha yake ilivyoteremka. Na haya

yanapatikana katika [vitabu vya] tafsiri ambazo nimewatajia.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13840

20) Vipi Mzazi Afanye Uadilifu Kati Ya Mtoto Wa Kiume Na Wa Kike?

Swali:

Vipi kwa mzazi afanye uadilifu katika matumizi baina ya watoto, je kijana

apewe zaidi kuliko msichana?

´Allaamah al-Fawzaan:

Matumizi baina ya watoto kwa uadilifu ni kumpa kila mmoja kile

anachokihitaji. Mtoto wa kike utampa kile anachokihitaji na wa kiume

anachokihitaji katika matumizi. Si kwamba kuwapa sawa, hapana! Kila mmoja

ana haja [mahitajio] yake. Matumizi ya mkubwa si kama matumizi ya mtoto

mdogo. Mtoto matumizi yake huwa madogo, lakini mkubwa huwa zaidi.

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (30)

17

Atapewa kila mmoja kile anachokihitaji katika fungu, nyumba na

anayoyahitaji katika mambo yake na kazi zake.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13840

21) Wanaume Waliolaaniwa Wanaojifananisha Na Wanawake Na

Makafiri

Swali:

Yaliyopokelewa kwa Mtume ( وسلم عليه هللا صلي ) kulaani wanaume

wanaojifananisha na wanawake, je anaingia katika laana yule anayenyoa

ndevu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni kila sampuli ya kujifananisha. Huku [kunyoa ndevu] ni kujifananisha kwa

sampuli mbili:

- Mtume ( وسلم عليه هللا صلي ) kasema "Wakhalifuni wamajusi, zirefusheni ndevu

na punguzeni masharubu.

- Na ni kujifananisha na wanawake pia. Kwa hiyo kuna kujifananisha namna

mbili. Ni kujifananisha na wanawake na kujifananisha na makafiri.

Chanzo: http://youtu.be/iUyYPwZ8pQI

22) Upi Wajibu Wetu Kwa Aliyekataa Kutoa Zakaah?

Swali:

Ipi dhambi kwa yule anayechukulia sahali suala la kutoa Zakaah?

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (30)

18

´Allaamah al-Fawzaan:

Ichukuliwe kutoka kwake. Akikataa kuitoa kwa khiyari ichukuliwe kutoka

kwake kwa nguvu, hata ikifikia hii katika kupigana. Ikiwa atahitaji kupigana.

Kama walivyopigana Maswahabah na waliokataa kutoa Zakaah. Ama

akikataa na kusema hakuna uwajibu wa kutoa Zakaah mtu ana khiyari, huyu

karitadi na kutoka katika Dini ya Kiislamu. Kwa kuwa kamkadhibisha Allaah,

na Mtume Wake na Ijmaa´ ya Waislamu. Aliyekataa uwajibu wa kutoa Zakaah

karitadi, na anayekubali uwajibu wake lakini kakataa [kutoa] kwa ubakhili

huyu atalazimishwa kutoa hata kama itakuwa kwa nguvu.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13840

23) Umekumbusha Yatosha!

Swali:

Mimi daima huwanasihi watu kutosengenya na huwatakaza, ninapomnasihi

mtu mara moja mpaka mbili. Je, inajuzu kwangu kukariri nasaha kutokana na

kwamba kuna mtu aliyenambia: Umeshawanasihi mara mbili yatosha.

ما ولنا على فإن بين البلغ رس الم

“Basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha (Ujumbe wake) kwa uwazi tu.”

(64:12) Ipi rai yako kwa hili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio lakini usikae nao. Ukiwanasihi na wasikubali usikae nao. Kwa kuwa

ukikaa nao huku ni kuwasapoti.

Chanzo: http://youtu.be/ENGZ8fbqv6M

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (30)

19

24) Swali Lako Halina Faida Kwa Sasa!

Swali:

Nilimtaliki mke wangu kwa sababu alitoka nyumbani kwa kuvaa vibaya, je

nimekosea katika hili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wewe umeshamtaliki, maadamu umeshamtaliki mambo yamekwisha. Ilikuwa

uulize tangu mwanzo. Kwa sasa swali hili halina faida.

Chanzo: http://youtu.be/iJspPajK9pU

25) Swalah Ya Usiku Ina Idadi Rakaa Maalumu?

Swali:

Swalah ya usiku ina idadi Rakaa ngapi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haina idadi, unaswali [Rakaa] utazoweza kisha utahitimu kwa kuswali Witr.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13840

26) Hukumu Ya Kula Nyama Ya Mtu Asiyeswali

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (30)

20

Swali:

Mimi baba yangu haswali na anatuchinjia siku ya ´Iyd, ipi hukumu ya uchinjo

huu akichinja yeye au akimpa mwengine achinje?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Akichija yeye itakuwa Haramu kutokana na kauli sahihi ya wanachuoni. Kwa

kuwa mwenye kuacha Swalah huchukuliwa ni kafiri, kutokana na Hadiyth:

"Ahadi iliyopo baina yetu sisi na wao [makafiri] ni Swalah, atakayeiacha

amekufuru.

"Hakuna baina ya mja na kufuru na Shirki ila ni mtu kuacha Swalah."

Kaipokea Hadiyth hii Muslim. Kutoka Hadiyth ya nani? Jaabir. Na wakichinja

wengine katika wanaoswali, hakuna ubaya In Shaa Allaah.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=pXOBiW2zkC4

27) Aliyeacha Swalah Ni Lazima Atoe Shahaadah Atapoanza?

Swali:

Akitubia mtu na kurejea kwa Mola Wake kwa kuwa alikuwa haswali, je ni

lazima atamke Shahaadah mbili na kufanya ghusl [kukoga]?

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Akitubia mtu ambaye alikuwa haswali kwa Allaah (´Azza wa Jalla) na

akaanza kuswali, atakuwa Muislamu kwa Swalah yake. Kwa kuwa mwenye

kukufuru kwa kuacha kitu fulani, anakuwa Muislamu kwa kufanya kitu

hicho. Na katika kila Swalah hio, atakuwa akisema "ash-Hadu an laa ilaaha

illa Allaah wa ash-Hadu anna Muhammad ´abduhu wa Rasuuluh". Ama

kufanya Ghusl, msingi wake umejengeka katika uwajibu wa Ghusl wakati

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (30)

21

anasilimu kafiri. Na wanaosema kwamba kafiri anaesilimu si wajibu kufanya

Ghusl, hivyo itakuwa si wajibu kwa mtu huyu kufanya Glusl. Na bila shaka ni

bora zaidi kufanya Ghusl ili atoke katika Khilaaf hii [ya wanachuoni] na awe

katika usalama.

Chanzo: http://youtu.be/PNfsXRKm_9M

28) Unyenyekevu Wa Shaykh ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad

Swali:

Hii ni bishara njema. Shaykh wetu nimeona usingizini kuwa naingia

nyumbani, nikamuona Shaykh al-Albaaniy kajinyoosha nikamuuliza:

"Shaykh wetu, nani wa kurejea kwake baada yako?"

Akasimama na kwenda kwenye mlango na akafungua mlango na akaashiria

kwa mkono wake wa kulia na akanyoosha kidole chake cha shahada na

kuashiria mahala, na akasema:

"al-´Abbaad, al-´Abbaad."

Akaendelea kukariri mpaka nikashtuka na mimi nikafurahi.

´Allaamah al-´Abbaad:

Allaahu Musta´aan. Ninasema Allaahu Musta´aan mimi sistahiki nafasi kama

hii, mimi siwezi kusimama nafasi kama hii. Ndoto hii inaweza kuwa na taabiri

(maana) nyingine.

Chanzo: http://youtu.be/sYIjpAVD3MY

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (30)

22

29) Ni Wajibu Kutahadharisha Dhidi Ya Watu Wa Bid´ah

Shaykh Abu ´Abdul-Haaliym ´Abdul-Haadiy:

Kama alivyosema al-´Allaamah Ibn al-Qayyim (Rahimahu Allaah) na Salaf na

maimamu kuhusu kutahadharisha watu na Bid´ah. Kwa nini? Kwa kuwa

madhara ya Bid´ah na kuiharibu Dini ni mabaya na ni jambo la wajibu katika

mambo ya uwajibu mkubwa na ni Jihaad kubwa. Kasema Shaykh-ul-Islaam

Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah):

“Hakika kutahadharisha watu na maimamu wa Bid´ah kwa watu wakukhalifu

Qur-aan na Sunnah au ´Ibaadah zinazokhalifu Qur-aan na Sunnah, kubainisha

hali zao na kutahadharisha Ummah dhidi yao ni wajibu kutahadharisha watu

na Ahl-ul-Bid´ah.”

Ni wajibu juu yako ewe mja wa Allaah kutadharisha watu dhidi ya watu wa

Bid´ah. Anasema Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah):

"Hakika kubainisha hali zao, na kuhadharisha Ummah dhidi yao ni wajibu

kwa makubaliano ya wanachuoni."

Kulisemwa kuambiwa Ahmad bin Hanbal:

"Mtu anafunga, anaswali na kufanya I´tikaaf - yaani anafunga Swawm za

Sunnah, Swalah za Sunnah na kufanya I´tikaaf. Je ni bora au [mtu mwenye]

kuwaongelea watu wa Bid´ah?

Akasema: "Akisimama na kuswali na kufanya I´tikaaf ni faida yake

mwenyewe, na akiongelea watu wa Bid´ah faida ni ya Waislamu na hili ndio

bora zaidi."

Na ni wajibu kwa maulamaa wa Ummah kutahadharisha watu dhidi ya watu

wa Bid´ah na watu wa Ahwaa (matamanio), kwa kuwa ni Jihaad enyi waja

wa Allaah, bali ni katika aina bora ya Jihaad katika njia ya Allaah (Jalla wa

´Alaa). Kasema Imaam al-Baghawiy katika Sharh-us-Sunnah:

"Katwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu mgawanyiko

wa Ummah huu na kujitokeza Ahwaa na Bid´ah na kuokoka kwa yule

atayefuata Sunnah zake na Sunnah za Maswahabah wake (Radhiya Allaahu

´anhum)".

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (30)

23

Waislamu wajue wakimuona mtu kashikamana na kitu katika Ahwaa na

Bid´ah au anachukia kitu katika Sunnah huku akiamini hivyo, mtu huyo

inatakiwa kumhama [kumsusa] na kujiweka nae mbali kabisa na amuache yu

hai au maiti, asimtolee Salaam atapokutana nae wala asimjibu atapoanza

[kukutolea yeye], mpaka hapo atapoacha Bid´ah zake na kurejea katika haki...

Na makatazo ya kumsusa ndugu yako zaidi ya siku tatu katika yaliyotokea

baina ya watu wawili, hili halihusiana na mambo ya haki ya Dini. Watu wengi

wanadhani kuwa kumhama mtu hata ikiwa kwa watu wa Bid´ah, isizidi siku

tatu. Maana ya Hadiyth si hii, fahamu Hadiyth hii vizuri. Makusudio ya

Hadiyth hii:

"Si halali kwa muumini kumhama ndugu yake zaidi ya siku tatu."

Hili si kwa watu wa Bid´ah na Ahwaa. Bali hili linahusiana wakati watu

wawili wanapokwaruzana katika mambo ya kidunia au ya kawaida tu... Baina

yako wewe na yeye. Ama watu wa Bid´ah na watu wa Ahwaa, wanasusiwa

sawa waliohai na waliokufa mpaka watubie kwa Allaah (Jalla wa ´Alaa). Na

kwa hili anasema Imaam al-Baghawiy:

"Kuwasusia watu wa Bid´ah na matamanio ni jambo la daima (milele) mpaka

hapo watapotubia."

Na si kwamba ni siku tatu, mambo gani siku tatu? Bali ni wajibu kwako

kuwahama [kuwasusia] daima mpaka watapotubie, khaswa ikiwa ni wale

vigogo wa Bid´ah na Ahwaa. Hapa enyi ndugu, lazima tutanabahishe mambo

mawili. Tusiwabadiy´ na kutafsiyq khaswa kama wafanyavyo baadhi ya

vijana wanapoona mtu katika Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah kaanguka katika

Bid´ah moja kwa moja wanamhukumu kuwa ni mtu wa Bid´ah na yuko hivi

na vile, na unamsafiki, na kumbadiy´ na kumsusa, hapana ewe mja wa Allaah.

Si kila mwenye kutumbukia katika Bid´ah, Bid´ah huanguka juu yake.

Anaweza kutumbukia katika Bid´ah naye ni mjinga hajui, anaweza

kutumbukia katika Bid´ah naye kalazimishwa hilo, kama jinsi baadhi ya vijana

wamenguka na Jamaa´at-ut-Tabliygh, al-Ikhwaan al-Muslimuun

wakawadanganya huku wakidhani kuwa wako katika haki. Ni juu yako

kuwabainishia kuwa wako katika Bid´ah, na kwamba kitendo ambacho

wakoemo ni Bid´ah. Uwabainishie kwa dalili katika Qur-aan na Sunnah za

Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ama (baada ya

kumfikishia haki) akaleta kiburi na ukaidi, huyu ndiye Mubtadiy´ (mtu wa

Bid´ah). Mtu wa Bid´ah ni mtu ambaye kaanguka katika Bid´ah akanasihiwa

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (30)

24

lakini akaleta kiburi na ukaidi. Na si (kumhukumu) kabla hujamsimamishia

haki ewe mja wa Allaah. Ama kwa yule anayekubali haki, tutamshika mkono

na Dini ni nasaha kama ilivokuja katika Hadiyth kutoka kwa Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam). Na anasema Imaam ash-Shawkaaniy katika

Fathiyl Qadiyr katika tafsiri Kauli ya Allaah (Jalla wa ´Alaa):

ون الذين رأيت وإذا وض وا حتى عنه م فأعرض آياتنا في يخ وض ا غيره حديث في يخ د فل ياان الش ي نسينك وإم تقع

كرى المين القوم مع بعد الذ الظ

“Na unapowaona wanaoziingilia Aayah zetu, basi jitenge nao mpaka

waingilie mazungumzo mengine. Nakama Shaytwaan akikusahaulisha, basi

baada yakutanabahi usikae pamoja na watu madhaalimu.” (06:68)

Anasema (Rahimahu Allaah) - fahamu Aayah hii vizuri na uzingatie maana

yake nayo ni Aayah kubwa. Anasema Imaam ash-Shawkaaniy (Rahimahu

Allaah) kama ilivo katika kitabu Fathiyl Qadiyr:

"Katika Aayah hii kuna mawaidha makubwa kwa yule mwenye kukaa na

watu wa Bid´ah."

Kama wasemavyo baadhi ya vijana leo, tunaangalia maslahi na madhara

(kabla ya kuwasusa watu wa Bid´ah). Yako wapi maslahi? Je ni wewe mwenye

kujua maslahi na madhara? Mwenye kujua maslahi na madhara ni maulamaa

ewe mja wa Allaah, ewe mja wa Allaah acha kucheza, acha kucheza ewe mja

wa Allaah. Vijana wengi wanasema, tunaangalia maslahi na madhara - anakaa

na watu wa Bid´ah, anatembea na watu wa Bid´ah, anacheka na watu wa

Bid´ah na anasema:

"Ni kwa ajili ya maslahi na madhara"

Maslahi na madhara hayakadiriwi na wewe?? Ni maulamaa wangapi

waliokuwa katika Sunnah, kwa kukaa kwao na watu wa Bid´ah na Hawaa

wamepotea na hili lipo ewe mja wa Allaah. Ni watu wangapi katika wale

wanaodai kuwa wana elimu walipoanza kukaa na watu wa Hawaa na

wakajichanga nao wamepotea, kama ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq,

Adnaan ´Ar´uur na wengine wengi katika makundi haya na katika watu hawa

wanaodai kuwa wana elimu - wamepotea katika Manhaj kwa kukaa nao na

watu wa Bid´ah na wamekuwa na wao sasa wanalingania watu katika Bid´ah.

Hivyo ni lazima tufahamu Aayah hii kuna mawaidha makubwa kwa ambaye

anakaa na watu wa Bid´ah ambao wanageuza Maneno ya Allaah na

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (30)

25

wanafanya mchezo na Kitabu Chake na Sunnah za Mtume na wanazikejeli

kwa matamanio yao ya kipotofu na Bid´ah zao chafu. Basi ikiwa mtu hawezi

kuwakataza na kubadilisha walioemo, basi angalau kwa uchache mtu aache

kukaa nao na hilo ni jambo rahisi kwako, jiweke mbali na watu wa Bid´ah na

hilo ni rahisi kwako na si gumu.

Chanzo: http://youtu.be/4VaMwbrbfDY

30) Mkutano Wa Shaykh al-Albaaniy Na Shaykh Ibn ´Uthamiyn

Swali:

Mmeshawahi kukutana na Shaykh Muhammad bin ´Uthaymiyn katika

mkutano wa kielimu au wa kawaida?

Imaam al-Albaaniy:

Nilipata heshima kwa kupata mgeni wake nyumbani kwa mkwe wangu Dr.

Ridhwaa Na´saan Makkah. Nadhani ilikuwa wakati wa Hajj.

Muulizaji:

Hamjawahi kukutana wakati mwingine tena?

Imaam al-Albaaniy:

Siwezi kukumbuka zaidi ya mara hii.

Muulizaji:

Kama kwamba nadhani alinambia ni wakati ulipita ´Unayzah na Buraydah...

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (30)

26

Imaam al-Albaaniy:

Ni kweli. Ila sidhani kama nilikutana nae.

Muulizaji:

Nadhani hata mlikunywa kahawa nyumbani kwake.

Imaam al-Albaaniy:

Sikumbuki. Yeye ndiye aliyekwambia?

Muulizaji:

Ndio na alinambia kuwa ulikuwa na Zuhayr ash-Shaawaysh.

Imaam al-Albaaniy:

Ndio ni kweli nilikuwa kule na Zuhayr ash-Shaawaysh. Inawezekana ilikuwa

ni wakati sijamjui Shaykh vizuri. Inawezekana ndio maana sikuweza

kumkumbuka, tofauti wakati alinizuru Makkah. Mimi nakumbuka hilo vizuri.

Alikuwa na wanafunzi wawili. Mmoja wao aliniuliza swali kuhusiana na

elimu ya Hadiyth. Kwa kweli napenda tabia ya Shaykh, urafiki wake, maadili

yake na jinsi anavyofanya awezavyo kwa kuepuka Taqliyd [kufuata kichwa

mchunga] tofauti na maulamaa wengi katika miji yote.

Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy

Källa: Silsilat-ul-Hudaa wan-Nuur (301)

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (30)

27

31) Hukumu Ya Kumpa Zakaah Mume Wako

Swali:

Kuna mwanamke ambaye anamiliki dhahabu na zimefika niswaab, je inajuzu

kwake kuwapa Zakaah dada zake au kwa mume wake kwa kuzingatia ya

kwamba hamiliki mali yoyote zaidi ya dhahabu hii anayoimiliki ?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio, inajuzu kwake kulipa Zakaah kuwapa dada zake ikiwa ni mafakiri.

Umaskini wa kuhitajia, yaani ikiwa hawana kile cha kuwatosheleza. Inajuzu

pia kulipa Zakaah kumpa mume wake ikiwa ni fakiri kama alivyosema

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa Zaynab mke wa ´Abdullaah

bin Mas´uud: Aliposema je inajuzu kumpa (mume wangu) Zakaah? Akasema

"Na´am."

Chanzo: http://youtu.be/4j-DmV2wYzY

32) Je Mwanamke Anaweza Kumuomba Mwanaume Kumuoa?

Swali:

Je inajuzu kwa mwanamke akimpata mwanaume mwenye msimamo katika

Manhaj ya Salaf-us-Swaalih kuiwasilisha nafsi yake kwake kwa ajili ya ndoa,

na ipi nasaha yako?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kwa hakika, kutafuta mwanaume mzuri ni jambo ambalo Shari´ah yalisisitiza,

kwa kuwa maisha ya ndoa yana umuhimu na athari yake, kutafuta kwake

mwanamke mwanaume mwema ni dalili ya wema wake. Mwanamke huyu,

kama kuna uwezekano maneno yakawa baina ya walii wake na baina ya huyo

anayetaka kumchumbia hili ni bora. Atamwachia jambo hili msimamizi wake.

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (30)

28

Na ikiwa hawezi kuongea na msimamizi wake, atamtumia dada yake

mkubwa kama mama au dada na mfano wa hao, kisha anaweza kuwakilisha

qadhiya hii na lengo (la ndoa) ili asije kumkosa mwanaume mzuri. Hili halina

makosa. Ama ikiwa makusudio ya yeye kujiwasilisha, ni mazungumzo, au

kwa uhusiano ambao unajulikana hivi leo, kama kuoneshana mapicha,

kupeana mapicha, na kupigiana masimu; hili madhara yake yako wazi kwa

watu. Muhimu ni kuwa, ombi lake ni zuri lakini inatakiwa iwe kwa sura nzuri

na ya heshima. Si kwa maana ambayo imezoeleka leo kama kwa intanet na

simu n.k. Ikiwa itatokea kuongea nae kwa njia ya simu lengo lake la ndoa,

hivyo inatakiwa iwe neno moja tu. Nako ni kuwakilisha ombi la ndoa na

inatosha hivo. Ama kukalia mazungumzo, hili halijuzu mpaka hapo

atapokuwa mke wake.

Chanzo: http://youtu.be/1LFJ8HjGHsg

33) Iko Wapi Demokrasia Ya Hawa Makafiri?

Swali:

Ipi hukumu kwa anayesema kuweka demokrasia ni katika dharurah na

mambo ya muhimu katika zama hizi, la sivyo tutafikwa na yaliyoifika Iraaq?

´Allaamah al-Fawzaan:

Demokrasia ni madhehebu ya makafiri. Na Waislamu Allaah Hakuwapa haja

ya kitu kama hichi. Wao wako na uadilifu, uadilifu wa Kiungu. Wana uadilifu

wa Kiungu. Hawana haja ya "demokrasia" kama wasemavyo. Wanadanganya,

hakuna demokrasia. Hawana ila chuma na moto (unyama). Hawana

demokrasia. Huu ni uongo mtupu. Katika Uislamu kuna kitu kinachoitwa

uadilifu. Alhamdulillaah. Ama wanayodai na kujivunia, si sahihi. Hawana

chochote ila chuma na moto, na kushambulia manyumba na kushambulia

wale wasioafikiana na matakwa yao. Tunawaambia wale wanaosema kuna

"demokrasia", iko wapi demokrasia Afghanistan? Iko wapi demokrasia

Palestina? Iko wapi demokrasia mnayosema? Iko wapi demokrasia

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (30)

29

Chechenia? Iko wapi? Iko wapi demokrasia? Mnashambulia miji yote na watu

wake. Mnaua watoto, wanawake, wazee na watu wote wanapokhalifu amri

zenu. Iko wapi Demokrasia?

Chanzo: http://youtu.be/PHdRay1KTKw

34) Hili Ni Swali La Ajabu Sijawahi Kusikia Maishani

´Allaamah Muhammad bin Haadiy al-Madkhaliy:

Hili ni swali la ajabu sana sijawahi kusikia maishani mwangu, anasema:

Imaam Msikitini kwetu anasema kuwa al-Albaniy ni myahudi.

Mimi nadhani mtu huyu ni mmoja katika watu wawili:

- Ima hamjui ni nani al-Albaaniy

- Na ima ni Shaytwaan mgonjwa.

Hatoki katika watu hawa wawili. Muinuko wa al-Albaaniy haukuinuka kwa

kuwa ni al-Albaaniy tu, hapana. Kainuka kwa na kupanda daraja, na dunia

kukithiri kumtaja, kwa kulinda kwake Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Wallaahi, kisha wallaahi, kisha wallaahi, hata mapua yetu

yakishindiliwa katika vumbi, sijui katika zama hizi aliyezilinda Sunnah za al-

Mustwafaa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hata kwa 1/10

kwa juhudi alizoweka. Ni ushahidi nitaoulizwa mbele ya Allaah (Tabaaraka

wa Ta´ala). Mtu huyu aliishi karibu miaka tisini. Miaka yote hii alikuwa ni

mwenye kuzilinda Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Allaah Akanyanyua utajo wake katika Athaar, na katika minbar, minbar ya

Msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kunasemwa: "[Hadiyth

hii] kaisahihisha al-Albaaniy, kaidhoofisha al-Albaaniy na pia kasema ni

hasan." Tunamshukuru Allaah (Subhaahahu wa Ta´ala) kwa fadhila hii

ambayo Allaah Katuneemesha kwa huduma hii ya kulinda Sunnah za Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika zama hizi ambazo wamekuwa

wachache wenye kujishughulisha na fani hii, fani ya Hadiyth za Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Tunamuombea Allaah (Subhaanahu wa

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (30)

30

Ta´ala) kwa Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) msamaha mkubwa kwa

Mola Wake (Tabaaraka wa Ta´ala). Na mtu huyu atakutana na Mola Wake na

atakutana na malipo yake kwa Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala) ikiwa hatotubia

kwa hili.

Chanzo: http://youtu.be/Uj6oXO9wjQk

35) Dalili Ya Qur-aan Inayofuta Vitabu Vilivyotangulia

Swali:

Je kuna dalili katika Kitabu inayothibitisha kuwa Qur-aan imevifuta vitabu

vilivyotangulia?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili linahitajia dalili katika Qur-aan. Je, hujasoma Kauli ya Allaah:

ها يا ق ل ول إني الناس أي م هللا رس لك له الذي جميعا إليك ماوات م و إال إلـه ال واألرض الس فآمن وا وي ميت ي حيـي ه

وله ي النبي بالل ورس األ م

“Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliyetumwa

na Allaah Mwenye Ufalme wa mbingu na ardhi. Hapana mungu ila Yeye

anayehuisha na anayefisha. Basi muaminini Allaah na Mtume wake asiyejua

kusoma na kuandika. (07:158)

Ni nani Mtume asiyejua kusoma na kuandika? Ni Muhammad (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam).

ون م تهتد وه لعلك بع ي الذي ي ؤمن بالل وكلماته وات األ م

“Ambaye anamuamini Allaah na maneno Yake. Na mfuateni yeye ili mpate

kuongoka.” (07:158)

Angalia.

ي وه وكلماته بالل ي ؤمن الذي األ م بع م وات ون لعلك تهتد

Page 31: Fataawa Za Wanachuoni (30)

31

“Ambaye anamuamini Allaah na maneno Yake. Na mfuateni yeye ili mpate

kuongoka.” (07:158)

Ni dalili ya kwamba ambaye hamuamini hatoongoka na kuwa ni kafiri na

mpotofu. Je, hii haifuti yaliyotangulia?

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2515

36) Je, al-Ikhwaan al-Muslimuun Ni Katika Ahl-us-Sunnah?

Imaam Muhammad Naaswirud-Diyn al-Albaaniy:

Hivyo mimi nikasema hakuna mtu awezae kusema kuwa al-Ikhwaan al-

Muslimuun ni katika Ahl-us-Sunnan, kwa kuwa wanaiharibu Sunnah.

Chanzo: http://youtu.be/U6hPdNVqc6w

37) Hukumu Ya Mwanamke Kuzuru Makaburi -1-

Swali:

Huyu dada anauliza, je inajuzu kwangu kuzuru makaburi - yaani kumzuru

kaka yangu (Rahimahu Allaah)? Tangu kaka yangu afe huwa nikienda daima

kumzuru, napeleka uvumba na humaliza muda mrefu niko nae, humrehemu

na humuombea daima kuingia Peponi. Je hili linajuzu?

Imaam Ibn Baaz:

Hili halijuzu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kawalaani wanawake

wenye kuzuru makaburi, wanawake hawazuru makaburi. Hali kadhalika

Page 32: Fataawa Za Wanachuoni (30)

32

kwenda makaburini na manukato, yote haya ni munkari. Lakini muombee

nyumbani, muombee nyumbani kwako unaposujudu. Muombe Allaah

Amrehemu, mtolee Swadaqah. Ama kwenda kumzuru hapana, wanawake

hawazuru makaburi. Ni juu yako kuomba Tawbah kwa uliyoyafanya, ni juu

yako kuomba Tawbah kwa uliyoyafanya kabla. Na kumuombea Du´aa

itakuwa nyumbani Alhamduli Allaah.

Chanzo: http://youtu.be/9TgK44ou16I

38) Baina Yetu Sisi Na Nyinyi Ni Vitabu Vya Salaf

´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy:

Shikamaneni nyote katika kamba ya Allaah na itawasaidia katika hili, na

itawafanya kuwa kama jua, kwa kurejea katika ufahamu wa Salaf-us-Swaalih,

na (ufahamu wao) kama nilivyowaambia umeenea na upo mbele yenu (katika

Kitabu cha Allaah, Sunnah, duruus za wanachuoni). Na hii ni changamoto

kwa yule atayekengeuka hili, sisi tunawapa changamoto watu wa Bid´ah na

watu wa matamanio; watu wa Bid´ah wa kiitikadi, na watu wa Bid´ah wa

kisiasa. Tunasema:

"Baina yetu sisi na nyinyi ni Salaf, baina yetu sisi na nyinyi ni Vitabu (vya

Salaf).

Alikuwa Ahmad akisema kuwaambia watu wa bid´ah:

"Baina yetu sisi na nyinyi ni Swalah ya janaza (yaani kifo).”

Na sisi tunasema hali kadhalika:

"Baina yetu sisi na nyinyi ni vitabu.”

Vitabu vipo. Allaah Alimwambia Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam):

وراة فأت وا ق ل نت م إن فاتل وها بالت صادقين ك

“Leteni Tawrat muisome ikiwa nyinyi ni wasema kweli.” (03:93)

Page 33: Fataawa Za Wanachuoni (30)

33

Hivyo (Mayahudi) walikuwa wakileta Tawrat na ilikuwa ni yenye

kuwadhalilisha. Na kwa hawa (watu wa Bid´ah), tutaleta vitabu vya Salaf,

Qur-aan na Sunnah, tunaleta vitabu vya al-Bukhaariy, Muslim, Abuu

Daawuud, at-Tirmidhiy, an-Nasaa´iy, na alivyoandika Ahmad na wengineo.

Tutavileta (na kuona) ni nani aliye katika njia ya watu hawa, na ni nani

aliyeitupa na kuwakhalifu? Kama Allaah Alivyowapa changamoto Mayahudi

walete Tawrat, na wakati Tawrat ililetwa ikawafedhehesha. Sisi tunawapa

hawa watu (wa Bid´ah) walete vitabu vya Salaf, ili tumuweke wazi nani mtu

wa Bid´ah ni sisi au wao, na kubainisha ni nani mpotofu ni sisi au wao. Je wao

wanaweza kweli kutupa changamoto? Je wao wanaweza kufungua midomo

yao kwa kuthubutu kusema hivi? Sisi tunafungua midomo yetu kwa ushujaa

mkubwa, tunampa changamoto kila anayesema sisi hatuko katika Manhaj ya

Salaf-us-Swaalih. Sisi wallaahi tunalingania katika Manhaj ya Salaf-us-

Swaalih, katika Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) na tunawaleta katika ´Aqiydah yetu, ´Ibaadah yetu

na msimamo wetu (kuhusiana kati ya) viongozi, makundi, mapote katika

Kitabu cha Allaah na katika Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Ama kwa wengine (watu wa Bid´ah) wako katika hila na

upambaji. Wallaahi hukuti kwao isipokuwa hila tu na michezo kama ya

watoto.

Chanzo: http://youtu.be/HEs47e56TTA

39) Sifa Na Tabia Za Mja Zimeumba Na Allaah

Swali:

Ipi rai yako kwa anayesema kuwa sifa ya ukarimu anayosifika nayo

mwanaadamu imeumbwa?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye Aliyemuumba binaadamu na tabia

yake. Ukarimu, ushujaa n.k. [sifa] hizi zimeumba Allaah kwa waja Wake.

Page 34: Fataawa Za Wanachuoni (30)

34

Chanzo: http://youtu.be/QN188c3AVAs

40) Ni Lazima Kwa Muadhini Awe Twahara

Swali:

Je ni lazima kwa mwenye kutoa adhaana asiwe na hadathi kubwa wala

ndogo?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Ama hadathi kubwa ni sharti [mtu awe Twahara], lakini hadathi ndogo si

lazima. Inajuzu kuadhini bila ya kuwa na Twahara [Wudhuu].

Chanzo: http://youtu.be/6RacSh4v6wE

41) Mume Ana Wake Wawili Kumuacha Mmoja

Swali:

Akimtaliki mwanamume mmoja katika wake zake, ni wajibu kwake

kuheshimu haki za kitandani kwake mpaka itapoisha eda yake?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Hapana! Hapana!

Chanzo: http://youtu.be/9EpD2KvFZTo

Page 35: Fataawa Za Wanachuoni (30)

35

42) Madhehebu Manne Ni Katika Makundi 72 Ya Motoni?

Swali:

Imethibiti kwa Mtume ( وسلم عليه هللا صلي ) kuwa amesema:

"Wamegawanyika Wakristo katika mapote 72 na Ummah wangu

utagawanyika mapote 73. Yote hayo yataingia motoni ila moja tu".

Je, anaingia katika tishio hili mtu ambaye atajinasibisha na madhehebu

maalum, kwa mfano madhehebu mane?

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Hapana, hawatoingia humo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

alimaanisha ni yale makundi ambayo yatawapoteza wengine. Na madhehebu

mane hayawapotezi wengine.

Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

Chanzo: Liqaa' al-Baab al-Maftuuh (129 B)

Tarehe: 1417-02-11/1996-06-27

43) Kupigana Jihaad Pamoja Na Ahl-ul-Bid´ah

Swali:

Muislamu akiwa katika safu ya vita baina ya makafiri - mayahudi, manaswara

na washirikina na baina ya wanaouwakilisha Uislamu, lakini hao

wanaouwakilisha Uislamu ni katika makundi potofu. Upi msimamo wa

Muislamu katika vita hivi ?

Page 36: Fataawa Za Wanachuoni (30)

36

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Ni wajibu apigane. Akiwepo katika safu ni lazima apigane.

Muulizaji:

Hata kama atakuwa na kundi potofu?

Imaam Ibn ´Uthamiyn:

Anapigana kwa ajili ya Uislamu na si kwa ajili ya kundi hili potofu. Si hivyo?

Ni wajibu kwake kupigana, kutokan na kauli ya Allaah:

"Enyi mlioamini! Mkikutana na jeshi, basi kueni imara, na mkumbukeni

Allaah sana ili mpate kufanikiwa". (08:45)

Na Anasema tena Allaah (´Azza wa Jalla):

"Enyi Mlioamini! Mkikutana na waliokufuru vitani msiwageuzie mgongo. Na

atakaye wageuzia mgongo wake siku hiyo - isipokuwa kwa mbinu za vita au

kuungana na kikosi - basi atakuwa amestahiki ghadhabu ya Allaah. Na pahala

pake ni Jahannamu, na huo ni mwisho muovu". (08:15-16)

Isitoshe kasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kukimbia siku ya

mapigano ni katika madhami ya kuangamiza.

Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

Liqaa' al-Baab al-Maftuuh (128 B)

Tarehe: 1417-02-04/1996-06-20

44) Kuweka Mlio Wa Simu Wa Adhaana, Qur-aan Au Dhikr

Swali:

Page 37: Fataawa Za Wanachuoni (30)

37

Je inajuzu kuweka mlio wa simu sauti ya adhaana au Aaayah tukufu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana! Zisitumiwe Adhkaar katika simu kwa ajili ya tanbihi ya maongezi.

Huu ni mtihani kwa Dhikr, mtihani kwa Qur-aan. Weka mlio usiokuwa na ala

wala muziki wala, kwa jili tu ya kukushtua [kuwa kuna mtu anapiga].

Chanzo: http://youtu.be/M072XtKRRXc

45) Kupiga Radd Watu Wa Bid´ah Ambao Wanalingania Watu Katika

Bid´ah Zao

Swali:

Kuhusiana na Radd, baadhi ya watu wanasema asipigwe Radd kila mtu,

akasema:

"Huyu akipigwa Radd na huyu, yupi atakayebaki?"

Je, hili ni sahihi?

Imaam Ibn ´Uthamiyn:

Hapana, makusudio si haya. Ni masuala tu ya Ijtihaad ndo watu haifai

wapigane Radd wao kwa wao. Kwa mfano mmoja anasema nyama ya ngamia

inavunja Wudhuu na mwingine haoni hivyo. Hapa hapahitajiki kupigana

Radd. Lakini masuala ya Fiqh ambayo msingi wake watu wametofautiana na

ni sehemu ya Ijtihaad za wanachuoni, hatuwezi kusema kila mwenye

kukhalifu rai fulani apigwe Radd. Kama tulivyosema tukifungua mlango huu,

kila mtu anapiga na kupigwa Radd.

Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

Page 38: Fataawa Za Wanachuoni (30)

38

Liqaa' al-Baab al-Maftuuh (127 B)

Tarehe: 1417-01-27/1996-06-13

46) Kumsimamishia Mtu Hoja Kabla Ya Kumhukumu Kuwa Ni Mtu Wa

Bid´ah

Swali:

Masuala ya Tabdiy´ [kumtia mtu katika Bid´ah] ni sharti kwanza

kumsimamishia mtu hoja, kwa kuwa kuna watu wanatoa dalili kwa maneno

ya Shayk-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) katika Minhaj-us-

Sunnah an-Nabawiyyah isemayo hapewi hukumu ya Tabdiy´ kwa mtu ila

baada ya kutimia masharti na kutokuwepo vikwazo. Kwa mtazamo mwingine

ana maneno mengine ambayo wanayatolea dalili ambao hawakubaliani na

kauli hii. Je, maneno haya ni kweli kwa Shaykh-ul-Islaam na ipi kauli yenye

nguvu kwa masuala ya Tabdiy´? Ni lazima kwanza kumsimamishia mtu hoja

ili mtu achukuliwe kweli kuwa ni Mubtadiy´?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Kumekithiri maongezi kuhusiana na hili. Tabdiy´ haitokani na Iqaamat-ul-

Hujjah. Bali anasihiwe. Ikiwa Bid´ah zake ziko wazi, anasihiwe mtu wa

Bid´ah. Na wala hakusemwi nimemsimamishia hoja. Kumsimamishia mtu

hoja inahitajika wakati tu wa Takfiyr [kumkufurisha mtu], ama Tabdiy´

hapana. Na wakati Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) alipomuuliza mtu

akasema Ibn Abiy Qutaylah Makkah kasema watu wa Hadiyth ni watu

wabaya, akasema:

"Zindiyq (mnafiki)! Zindiyq! Zindiy!".

Alitoa vumbi kwenye nguo yake na mikono yake na kusema:

"Zindiyq! Zindiyq! Zindiy!".

Hakusema kwanza itabidi nimsimamishie hoja [Iqaamat-ul-Hujjah].

Kumfanyia mtu Tabdiy´ si sharti kwanza kumsimamishia mtu hoja.

Page 39: Fataawa Za Wanachuoni (30)

39

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127300

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.