dola ya kiislamu - hizbhizb.or.tz/wp-content/uploads/2018/08/5.dolayakiislamu.pdf · "dhihirisha...

125
Page 1 of 125 ﺑﺴﻢ ﷲ ﺍﻟﺮﺣﻤﻦ ﺍﻟﺮﺣﻴﻢDOLA YA KIISLAMU Amesema Mtume rehma na amani ziwe juu yake na aali zake, » ﺗﻜﻮﻥ ﺍﻟﻨﺒﻮﺓ ﻓﻴﻜﻢ ﻣﺎ ﺷﺎء ﷲ ﺃﻥ ﺗﻜﻮﻥ, ﺛﻢ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ ﷲ ﺇﺫﺍ ﺷﺎء ﺃﻥ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ. ﺛﻢ ﺗﻜﻮﻥ ﺍﻟﺨﻼﻓﺔ ﻋﻠﻰ ﻋﻠﻰ ﻣﻨﻬﺎﺝ ﺍﻟﻨﺒﻮﺓ, ﻓﺘﻜﻮﻥ ﻣﺎ ﺷﺎء ﷲ ﺃﻥ ﺗﻜﻮﻥ, ﺛﻢ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ ﺇﺫﺍ ﺷﺎء ﺃ , ﻓﻴﻜﻮﻥ ﻣﺎ ﺷﺎء ﷲ ﺃﻥ ﺗﻜﻮﻥ, ﺛﻢ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ ﺇﺫﺍ ﺷﺎء ﷲ ﺃﻥ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ. ﺛﻢ ﺗﻜﻮﻥً ﻋﺎﺿﺎً ﻥ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ. ﺛﻢ ﺗﻜﻮﻥ ﻣﻠﻜﺎ , ﻓﺘﻜﻮﻥ ﻣﺎ ﺷﺎء ﷲ ﺃﻥ ﺗﻜﻮﻥ, ﺛﻢ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ ﺇﺫﺍ ﺷﺎء ﷲ ﺃﻥ ﻳﺮﻓﻌﻬﺎ.ً ﺟﺒﺮﻳﺎً ﻣﻠﻜﺎ ﺗﻜﻮ ﺛﻢ ﻥ ﺍﻟﺨﻼﻓﺔ ﻋﻠﻰ ﻋﻠﻰ ﻣﻨﻬﺎﺝ ﺍﻟﻨﺒﻮﺓ« . "Utume utakuwepo kati yenu kwa muda anaotaka Allah uwepo, kisha Allah atauondosha pindi anapotaka kuondosha, kisha kutakuwepo na Khilafa juu ya mfumo wa utume, utakuwepo muda anaotaka Allah uwepo, kisha atauondosha pindi anapotaka kuondosha. Kisha kutakua na ufalme wa kunyanyasa utakuwepo kwa muda Allah anaotaka uwepo, kisha Allah atauondosha pindi Allah anapotaka kuuondosha. Kisha kutakuwepo na ufalme wa kilazima, utakuwepo kwa muda Allah anaotaka uwepo, kisha atauondosha pindi anapotaka kuuondosha, kisha kutakua na Khilafa juu ya mfumo wa Utume" UTANGULIZI Kizazi kilichoko hakitambui serikali ya Kiislamu ambayo inaotabikisha Uislamu, na wale ambao wameishi mwisho wa serikali ya Kiislamu (dola ya kiuthmani) ambayo ilimalizwa na umagharibi walioona tu humo mabaki ya utawala wa Uislamu, na kwa sababu hiyo Muislamu hupata shida zaidi ya kuiweka karibu picha ya utawala wa Kiislamu katika bongo ambalo limetawaliwa na waqiah, na wala haliwezi (bongo) kutafakari utawala isipokuwa katika vipimo vya kile kinachoona katika nidhamu ya kidemokrasia iliyo fisidifu, iliyolazimishwa juu ya biladi ya Kiislamu kiulazima. Na wala ugumu sio katika hilo pekee, bali lilio gumu zaidi ni katika kuyabadilisha mabongo hayo (yaliochorwa) kwa thaqafa ya kimagharibi. Bila shaka thaqafa hii ya kimagharibi imekua ni silaha ambayo mmagharibi alioitumia katika uso wa serikali ya Kiislamu, na akaidunga mdungo ambao ulimaliza uhai wake, na akaibeba kuwapelekea watoto wa serikali silaha yake hiyo ikitona damu ya mama yao alieuwawa, na akasema kuwaambia huku anajigamba: "nimemuua mama yenu, mzee ambae alikuwa anastahiki kuuwawa kwa uovu wa malezi yake kwenu, na nimewafungulia malezi kwangu ambayo mutapata ndani yake maisha mazuri na neema za milele) na wakanyosha mikono yao wakimkumbatia katili, huku bado silaha inatona damu ya mama yao, hakika amewatendea kitendo cha fisi katika wanaoyaona wakati anapokifanya kiwinja chake kinasepetuka na hakiridhiki illa kukutana nae, na hakikubali illa kipigo kitakacho toa damu yake, au fisi kumfikisha katika bonde na kuumla. Basi ni kina nani kati ya watu hawa walio na mabongo yaliochorwa kuwa wajue kuwa silaha hii ilioua sumu ndio ambayo imeangusha serikali yao ya Kiislamu, ndio hiyo hiyo daima inaomaliza (muda watakao shikamana nayo) uhai wao na mipaka yao, na kua fikra hizi wanazozibeba za kizalendo na kutengamanisha dini na serikali na baadhi za rai za kuutukana Uislamu, ndizo baadhi za sumu ambazo zimeletwa kwao na thaqafa hii, na (uvamizi wa kikiristo) kifungu cha kitabu hiki serikali ya Kiislamu na yote hayo ya kihakika na hisabu za wazi zinatuonyesha katili muovu, na zinatuonyesha sababu ambazo zilimfanya atekeleze maovu haya, na zinatuonyesha mbinu ambazo alizozitumia kutekeleza ukatili huu, na hamna

Upload: others

Post on 03-Feb-2021

21 views

Category:

Documents


2 download

TRANSCRIPT

  • Page 1 of 125

    بسم هللا الرحمن الرحيمDOLA YA KIISLAMU

    Amesema Mtume rehma na amani ziwe juu yake na aali zake, تكون النبوة فيكم ما شاء هللا أن تكون, ثم يرفعها هللا إذا شاء أن يرفعها. ثم تكون الخالفة على على منهاج النبوة, فتكون ما شاء هللا «

    ن يرفعها. ثم تكون ملكاً عاضاً, فيكون ما شاء هللا أن تكون, ثم يرفعها إذا شاء هللا أن يرفعها. ثم تكون أن تكون, ثم يرفعها إذا شاء أ ملكاً جبرياً, فتكون ما شاء هللا أن تكون, ثم يرفعها إذا شاء هللا أن يرفعها.

    .»ن الخالفة على على منهاج النبوة ثم تكو"Utume utakuwepo kati yenu kwa muda anaotaka Allah uwepo, kisha Allah atauondosha

    pindi anapotaka kuondosha, kisha kutakuwepo na Khilafa juu ya mfumo wa utume,

    utakuwepo muda anaotaka Allah uwepo, kisha atauondosha pindi anapotaka kuondosha.

    Kisha kutakua na ufalme wa kunyanyasa utakuwepo kwa muda Allah anaotaka uwepo,

    kisha Allah atauondosha pindi Allah anapotaka kuuondosha. Kisha kutakuwepo na ufalme

    wa kilazima, utakuwepo kwa muda Allah anaotaka uwepo, kisha atauondosha pindi

    anapotaka kuuondosha,

    kisha kutakua na Khilafa juu ya mfumo wa Utume"

    UTANGULIZI

    Kizazi kilichoko hakitambui serikali ya Kiislamu ambayo inaotabikisha Uislamu, na wale

    ambao wameishi mwisho wa serikali ya Kiislamu (dola ya kiuthmani) ambayo ilimalizwa na

    umagharibi walioona tu humo mabaki ya utawala wa Uislamu, na kwa sababu hiyo Muislamu

    hupata shida zaidi ya kuiweka karibu picha ya utawala wa Kiislamu katika bongo ambalo

    limetawaliwa na waqiah, na wala haliwezi (bongo) kutafakari utawala isipokuwa katika

    vipimo vya kile kinachoona katika nidhamu ya kidemokrasia iliyo fisidifu, iliyolazimishwa juu

    ya biladi ya Kiislamu kiulazima. Na wala ugumu sio katika hilo pekee, bali lilio gumu zaidi ni

    katika kuyabadilisha mabongo hayo (yaliochorwa) kwa thaqafa ya kimagharibi. Bila shaka

    thaqafa hii ya kimagharibi imekua ni silaha ambayo mmagharibi alioitumia katika uso wa

    serikali ya Kiislamu, na akaidunga mdungo ambao ulimaliza uhai wake, na akaibeba

    kuwapelekea watoto wa serikali silaha yake hiyo ikitona damu ya mama yao alieuwawa, na

    akasema kuwaambia huku anajigamba: "nimemuua mama yenu, mzee ambae alikuwa

    anastahiki kuuwawa kwa uovu wa malezi yake kwenu, na nimewafungulia malezi kwangu

    ambayo mutapata ndani yake maisha mazuri na neema za milele) na wakanyosha mikono yao

    wakimkumbatia katili, huku bado silaha inatona damu ya mama yao, hakika amewatendea

    kitendo cha fisi katika wanaoyaona wakati anapokifanya kiwinja chake kinasepetuka na

    hakiridhiki illa kukutana nae, na hakikubali illa kipigo kitakacho toa damu yake, au fisi

    kumfikisha katika bonde na kuumla.

    Basi ni kina nani kati ya watu hawa walio na mabongo yaliochorwa kuwa wajue kuwa silaha

    hii ilioua sumu ndio ambayo imeangusha serikali yao ya Kiislamu, ndio hiyo hiyo daima

    inaomaliza (muda watakao shikamana nayo) uhai wao na mipaka yao, na kua fikra hizi

    wanazozibeba za kizalendo na kutengamanisha dini na serikali na baadhi za rai za kuutukana

    Uislamu, ndizo baadhi za sumu ambazo zimeletwa kwao na thaqafa hii, na (uvamizi wa

    kikiristo) kifungu cha kitabu hiki serikali ya Kiislamu na yote hayo ya kihakika na hisabu za

    wazi zinatuonyesha katili muovu, na zinatuonyesha sababu ambazo zilimfanya atekeleze

    maovu haya, na zinatuonyesha mbinu ambazo alizozitumia kutekeleza ukatili huu, na hamna

  • Page 2 of 125

    sababu isipokuwa alikusudia kuumaliza Uislamu, na hamna mbinu kuu illa thaqafa hii

    ambayo imekuja na uvamizi wa kimishenari.

    Hakika Waislamu wameghafilika na hatari ya thaqafa hii, na wamekuwa wanapigana na

    mkoloni na huku wanachukua kutoka kwake thaqafa yake, pamoja na kuomba ndio sababu ya

    kukoloniwa kwao, na kwao anakita mkoloni katika biladi yao, na watizame baada ya hayo

    vipi utakuwa mwelekeo wao unaogongana mgongano wa pamoja na wakuchekesha, na huku

    wanataka kumshinda mgeni wanadai kumpiga vita na huku wanaomnyoshea mikono yao

    kwa nyuma wakichukua kwa mikono miwili sumu yake inaouwa na kuigugumia, na

    waanguka mbele yake wakiangania, mjinga atawadhania ni mashahidi. Sio chochote

    isipokuwa ni kisunzi cha kughafilika na upofu.

    Ni kipi wanacho Kitaka? Je, wanataka serikali juu ya msingi usiokuwa wa Kiislamu? Au

    wanataka vijiserikali vingi katika biladi ya Kiislamu? Basi bila shaka mmagharibi amewapatia

    hilo tangu mambo yameingia katika mikono yake, vijidola vingi, ili atekeleze mipango yake ya

    kuuepusha Uislamu na utawala, na katika kuigawa biladi ya Waislamu, na katika

    kuwalewesha na utawala, na bado anawapatia kila wakati serikali ili aendelee katika

    kuwapotosha na azidi kuwagawanya, na huku amejitayarisha kuwapatia zaidi kwa sababu ni

    wafuasi wake.

    Suala lenyewe sio kusimamisha vijidola, bali ni kusimamisha serikali moja katika ulimwengu

    mzima wa Kiislamu, na wala sio kusimamisha serikali yoyote, na wala sio kusimamisha

    serikali inaoitwa serikali ya Kiislamu na inahukumu kinyume na aliyoyateremsha Allah, na

    wala sio katika kusimamisha serikali inaoitwa serikali ya Kiislamu inaohukumu kwa kanuni

    za Kiislamu tu, bila ya kuubeba Uislamu kama fikra kiongozi. Hakika suala lenyewe sio tu

    kusimamisha serikali, bali ni kusimamisha serikali itakaoyarudisha maisha ya Kiislamu

    kutokamana na aqeeda yake na kuutabiikisha Uislamu katika mujtama, baada ya kuwa

    unatokota katika wafusi uliomakinika katika akili na kuubeba ujumbe wa Kiislamu

    ulimwenguni.

    Na dola ya Kiislamu sio tu ni mawazo ya kindoto, kwani historia yake imeenea kwa muda wa

    karne kumi na tatu, hivyo basi ni uhakika. Ilikuwepo masiku ya kale, na itakuwepo hivi

    karibuni, kwani sababu za kuwepo kwake ni zenye nguvu zaidi kuliko zama kuikataa, au

    kutilia nguvu, na leo hii imejaa katika akili zinazo nawiri, nao ni ummah wa Kiislamu ulio na

    kiu ya utukufu wa Uislamu.

    Na dola ya Kiislamu sio mapenzi yanaoathiri hawa za nafsi, bali ni faradhi alioifaradhisha

    Allah juu ya Wasilamu, kua akawaamrisha waisimamishe, na akawatahadharisha na adhabu

    yake iwapo watadharau katika utekelezaji wake. Na atawakuwa vipi radhi Mola juu yao ilihali

    izzah katika biladi zao sio kwa Allah na wala sio kwa Mtume wake na wala sio kwa waumini,

    na watawezaje kuiepuka adhabu yake na huku wao hawaisimamishi dola inayoandaa jeshi na

    kulinda mipaka, na kutekeleza hudud za Allah, na kuhukumu na kile alichokiteremsha Allah?

    Hivyo basi imekua ni wajibu juu ya Waislamu kusimamisha serikali ya Kiislamu, kwani

    Uislamu hautakua na athari isipokuwa kupitia serikali, na kwa sababu biladi yao haizingatiwi

  • Page 3 of 125

    kuwa ni Darul-Islam isipkuwa tu itakopohukumiwa na dola ya Uislamu. Na dola ya Kiislamu

    – pamoja na hayo - sio sahali kwa namna wataikejeli wanaofanya kejeli iwe ni watu binafsi au

    vyama, na wakawa ni mawaziri wamekaa kukunja miguu katika viti vya utawala. Hakika njia

    yake imejawa na miba, imezungukwa na hatari, iliojawa na vizuizi na matatizo. Mbali na

    ugumu wa thaqafa isiokuwa ya Kiislamu, na mawazo hayo, na kwa tawala hatari zinazo

    nyenyekea umagharibi.

    Hakika wanoichukua njia ya ulinganizi wa Kiislamu ili kurudisha serikali ya Kiislamu, hakika

    wao wanafanya kazi ya kufikia utawala ili waifanye kuwa ndio njia ya kuyarudisha maisha ya

    Kiislamu katika biladi ya Kiislamu, ya kuubeba ujumbe wa Kiislamu katika ulimwengu, hivyo

    basi utawakuta hawakubali utawala kipande hata kama zitatofautiana mbinu za kughuri, na

    wala hawa kubali utawala kamili Isipokuwa iwapo watakua n aimani nayo ya kutabikisha

    Uislamu utabikisha wa kimapinduzi.

    Na baada yahayo hakika kitabu (serikali ya Kiislamu) hiki hakikusudii kuelezea historia ya

    serikali ya Kiislamu, bali imekusudiwa kuwaonyesha watu vipi Mtume alivyosimamisha

    serikali ya Kiislamu, na vipi kafiri mkoloni alivyoivunja serikali ya Kiislamu na namna gain

    Wasilamu wataisimamisha serikali ya Kiislamu, ili ulimwengu urudi na nuru itakao mulika

    njia ya uongofu katika giza lilioenea.

    NUKTA YA KIANZIO

    Pindi alipotumwa Mtume (SAW) alimlingania mkewe Khadija naye akaamini, kisha

    akamlingania mototo wa ammi yake Ali nae akaamini, na akamlingania aliekuwa mtumwa

    wake Zeid nae pia akaamini, na akamlingania rafiki yake Abubakar nae akaamini, kisha

    akawa anawalingania watu akaamini alieamini na akakanausha aliyekanusha. Na pindi

    aliposilimu Abubakar (ra) alidhihirisha Uislamu wake kwa yule alie na imani nae na

    akaligania kwa Allah na Mtume wake. Na Abubakar alikua ni mtu mwenye ushirikiano na

    kipenzi kwa watu wake na ahli, na watu wake walikuwa wanakuja kwake kwa kutaka ushauri

    katika zaidi ya jambo moja, kwa sababu ya ujuzi wake na biashara yake na uzuri wake na

    kukaa na watu, wakasilimu kupitia mkono wake Athman bin Affan, Zubeir bin Al-Awam,

    Abdurahman bin Auf, Saad bin Waqqas na Twalha bin UbeidAllah, na akawaleta kwa Mtume

    (SAW) wakti walipomkubalia na wakasilimu na wakaswali kisha akasilimu Abu Ubeidah na

    jina lake ni Amir bin Al-Jarrah, Abu salama na jina lake ni Abdallah bin Abu Asad, na Arqam

    bin Al-Arqam, Athman bin Madhu'un na wengineo, kisha watu wakawa wanaingia katika

    Uislamu wake kwa waume, mpaka ikaenea habari za Uislamu katika Makkah na watu

    wakawa waizungumza. Na alikuwa Mtume (SAW) anawazungukia watu katika mwanzo

    majumba yao akiwaambia: Hakika Allah amewaamrisha mumabudu yeye na wala

    musimshirikishe na chochote" na alikuwa anawalingania watu katika Uislamu katika

    Makkah wazi akitekeleza amri ya Allah, amesema Ta'ala: ثُِّر قُْم َفأَنِذْر } -{ يَاأَيَُّها اْلُمدَّ

    "Ewe uliejifunika funika - simama uonye" [TMQ Al-Muddathir: 1-2] na alikuwa analingnia watu

    akiwaeleza dini yake na anawaunganisha nae juu ya msingi wa dini hii kwa siri, na

    maswahaba na Mtume (SAW) wakijificha na watu wao. Na Mtume (SAW) alikuwa anatuma

    mtu aliyesilimu mbeleni kuenda kuwafundisha waliosilimu karibuni Quran na dini, kwani

    alimtuma Khabbab bin Al-Arat akawafunze Quran Zeinab bint Al- Khattab na mumewe Said,

  • Page 4 of 125

    Khabbab aliwafunza Quran, na akasilimu Umar kupitia halaqa hiyo. Na wala hakusimama

    hapo bali alijiwekea nyumba akiwafundisha watu Uislamu na akaifanya kama kitovu cha

    kikundi hiki cha waumini, na madrasa ya ulinganizi huu mpya, nyumba yenyewe ikiwa ni

    nyumba ya Al-Arqam bin Abi Al-Arqam, kwani alikuwa anawakusanya Waislamu ndani yake

    akiwasomesha Quran na akiwabainishia, na akiwaamrisha kuidhirisha na kuifahamu, na kila

    anaposilimu mtu anamuunganisha na nyumba ya Al-Arqam. Na akakaa miaka mitatu huku

    anawajenga Waislamu hawa, na akiwasalisha na akiswali Tahajjud, na akiweka mazingara ya

    kiroho kupitia swala na kusoma, na akiwapatia fikra ya kuzingatia juu ya aya ya Allah na

    kuzingatia juu ya viumbe vyake, na akiwajenga akili zao kwa maana ya Quran na matamshi

    yake, na ufahamu wa Uislamu na fikra zake na kuwahimiza kusubiria maudhio, na kuwajenga

    katika kumtii Allah na kuwa wanyenyekevu, ili wamtakasie Allah alie tukuka mweza. Na

    Mtume akaendelea kuficha yeye na Waislamu katika nyumba ya Al-Arqam na hatimae

    ikashuka kauli yake Allah Ta'ala: }اْصَدْع ِبَما تُْؤَمُر َوأَْعِرْض َعِن اْلُمْشِرِكيَن َف {

    "Dhihirisha yale ulioamrishwa nayo na wapuuze washirikina" [TMQ Al-Hijr: 94]

    MSHIKAMANO WA MASWAHABA

    Na alikuwa rehma na amani ziwe juu yake mwanzo mwanzo alimlingania yule aliye na

    matumaini nae kuwa yupo tayari kuukubali ujumbe huu bila ya kujali umri wake na nafasi

    yake, na bila ya kujali jinsi yake na asili yake. Na wala hakuwa anabagua watu ambao

    anaowalingania katika Uislamu kiubaguzi, bali alikuwa anawalingania watu wote, na

    anafuatilia utayarisho wao wa kukubali, na wengi wakasilimu. Na alikuwa na pupa ya

    kuwajenga wote ambao wanaoingia Uislamu na hukmu za dini na anawahifadhisha Quran.

    Na akawa anashikamanisha hawa na akawabebesha ujumbe, (na ilifika idadi yao tangu

    kutumilizwa kwake Mtume (SAW) mpaka alipoamrisha kudhihirisha ujumbe wake kiasi cha

    watu arubaini) wakiwemo waume na wake wa mazingara tofauti na miaka, wengi wao

    wakiwa ni mashabbab wadogo, na kati yao walikuwemo dhaifu na mwenye nguvu, tajiri na

    masikini. Na katika waliomuamini (SAW) na kuwa nae na Kubeba ujumbe pamoja nae

    walikuwa ni: -

    1:- Ali bin Abi Talib na umri wake ulikuwa ni miaka 8

    2:- Zubeir bin Al-Awwam umri wake ulikuwa ni miaka 8

    3:- Twalha bin Ubeid Allah nae alikuwa ni mtoto wa miaka 11

    4:- Al-Arqam bin Abi Al-Arqam alikuwa ni mtoto wa miaka 12

    5:- Abdalla bin Masoud alikuwa ni mtoto wa miaka 14

    6:- Said bin Zeid alikuwa chini ya miaka 20

    7:- Saad bin Abi Waqqas alikuwa na miaka 17

    8:- Masoud bin Rabiah alikuwa na miaka 10

    9:- Jaafar bin Abi Twalib alikuwa chini ya miaka 18

    10:-Zeid bin Harith akiwa na miaka 20

    11:-Athman bin Affan takriban miaka 20

    12:- Tuleib bin Umeir takriban miaka 20

    13:- Khabbab bin Al-Arat takriban miaka 20

    14:- Amir bin Fuheirah akiwa ni mtoto wa miaka 20

    15:- Musa'ab bin Umeir akiwa na miaka 23

    16:- Musaab bin Umeir akiwa na miaka 24

  • Page 5 of 125

    17:- Miqdad bin Al-Aswad akiwa na miaka 24

    18:-Abdallah bin Jahash akiwa na miaka 25

    19:- Umar bin Al- khatab akiwa na miaka 26

    20:- Abu Ubeida bin al-jarrah akiwa na miaka 27

    21:- Utbah bin Ghazwan akiwa na miaka 27

    22:- Abu Hudhaifa bin Utbah akiwa takriban miaka 30

    23:- Bilal bin Rabah takriban miaka 30

    24:- Ayyash bin Rabiah takriban miaka 30

    25:- Amir bin Rabiah takriban miaka 30

    26:- Naim bin Abdallah katika miaka ya 30

    27:- Athman takriban miaka 30

    28:- Abdallah takriban miaka 17

    29:- Qudama takriban miaka 19

    30:- As-saib mtoto wa Madhuun bin Habib miaka 20

    31:- Abu salama Abdallah bin Abdul Asad al Makhzumiy katika miaka ya 30

    32:- Abdurrahman bin Auf takriban miaka 30

    33:- Ammar binYassir takriban miaka 30

    34:- Abubakar As-Siddiq akiwa na miaka 37

    35:- Hamza bin abdul Muttalib akiwa na miaka 42

    36:- Ubeida bin al Harith akiwa na miaka 50

    Vilevile waliamini wanawake kadhaa, na pindi walipoiva hawa maswahaba katika kuwajenga,

    na akliya zao kuwa ni akliya za Kiislamu na nafsiyah zao kuwa ni nafsiyah za Kiislamu kwa

    muda wa miaka mitatu, Mtume akaweka matumaini yake juu yao na kuwa na yakini katika

    kuiva kwao katika akili zao, na katika kunyanyuka katika nafsiyah zao na akaona kudiriki

    kwao na mafungmano na Allah ni yenye kuonekanwa athari yake katika matangamano yao,

    nafsi yake ikatulia sana kwa hilo, na kukifanya kikundi cha Waislamu wote hapo

    akadhihirisha pindi Allah alipomuamrisha.

    KUJITOKEZA KWA ULINGANIZI

    Ulinganizi wa Kiislamu ulikuwa wazi tangu siku ya kwanza ya kutumilizwa kwake (SAW) na

    katika Makkah watu walikuwa wanajua kua Mohammad analinganiya dini mpya, na wanajua

    kua wamesilimu wengi pamoja nae, na wanajua kua Mohammad anawajumuisha maswahaba

    wake na kukesha nao, na wanajua kua na kuingia kwao katika dini mpya, yote haya yalikuwa

    yanafanya watu walihisi kua kuna ulinganizi mpya na wanahisi kuwepo wanaoamini,

    ingawaje walikuwa hawajui ni wapi wanakutana na ni kina nani hao wanaokutana katika

    waumini hivyo basi kujitokeza wazi kwa Mtume (SAW) kwa Uislamu haikua ni kitu geni kwa

    makafiri wa Makkah, bali kitu kipya kilikuwa ni kudhihirika kwa hichi kikundi cha waumini.

    Kwani alisilimu Hamza bin Abdulmuttalib kisha akasilimu Umar bin Al-Khattab, baada ya

    kusilimu Hamza kwa masiku tatu, nguvu za Waislamu zikaongezeka na ikamshukia Mtume

    (SAW) Kauli Yake Ta'ala: } الَِّذيَن يَْجَعلُوَن َمَع هللاِ إَِلًها آَخَر َفَسْوَف َيْعَلُمونَ - إِنَّا َكفَْيَناَك اْلُمْستَْهِزئِينَ - فَاْصَدْع ِبَما تُْؤَمُر َوأَْعِرْض َعِن اْلُمْشِرِكينَ {

    "Dhihirisha yale ulioamrishwa nayo na wapuuze washirikina, bila shaka sisi Tutakutosheleza na wale

    wanao kukejeli, wale ambao wanaweka kijungu mwengine pamoja na Allah bila shaka watakuja kujua"

    [TMQ Al-Hijr: 92-94]. Hapo Mtume (SAW) akadhihirisha amri ya Allah, na akadhihirisha wazi

  • Page 6 of 125

    kikundi kwa watu wote, ingawaje baadhi ya Waislamu walibakia wamejificha, kati yao kuna

    waliojificha mpaka Fathi Makkah. Na mbinu ya Mtume (SAW) ya kudhihirisha muungane

    huu ni kuwa alitoka na maswahaba wake katika vikundi viwili cha kwanza kikiongozwa n

    Hamza bin Abdulmuttalib na cha pii kikiongozwa na Umao bin Al-Khattab, na Mtume

    akaenda nao mpaka Al-Kaaba kwa nidhamu ya hali ya juu ambayo waarabu hawajawahi

    kuona kabla ya hapo, na akatufu nao Al-Kaaba, na kupitia hilo Mtume (SAW) alihama na

    maswahaba wake katika hali ya kujitokeza na katika hali ya maiingiliano ya yule amabaye alie

    na matumaini nae kuingia katika hali ya kuwazungumzia watu wote, hapo ikaanaza

    mgongano kati ya imani na ukafiri katika mujtama na yakaanza malumbano kati ya fikra

    swahihi na fikra fisidifu, na ikaanza safari ya pili nao ni safari ya mvutano na mapambano. Na

    makafiri wakaanza kupinga ulinganizi na kumuudhi Mtume (SAW) na maswahaba wake kwa

    kila aina ya udhia. Na kipindi hiki kipindi cha mvutano na mapambano ndicho kipindi

    kigumu zaidi kinacho julikana katika zama zote, kwani nyumba ya Mtume (SAW) ilipigwa

    mawe, na Umm Jamil mke wa Abu Lahab alikuwa anaweka najisi Mbele ya nyumba yake, na

    Abu Jahal alikuwa anaweka utumbo wa Mbuzi aliechinjwa kwa ajiliya masanamu na alikuwa

    anavumilia udhia na akienda kwa binti yake Fatima alimsafisha na kumtahirisha, hayo

    hayakumzidishia ila subra na kudumu katika ulinganizi, na Waislamu walikua wanatishiwa

    maisha na kuudhiwa, kwani imethubutu kuwa kila kabila wakiwaadhibu na wakiwafitinisha

    Waislamu katika dini yao miongoni mwao, kiasi ambacho mmoja wao alimuweka mtumwa

    wake wa kihabashi Bilal juu ya mchanga kwenye jua linalochoma na akaweka jiwe juu ya

    kifua chake na kumuacha ili afe sio kwa jingine isipokua kwa sababu alidumu juu ya uislamu,

    na katika hali hii haikumzidishia kitu Bilal isipokua ni kukariri neno ahad (mmoja) huku

    akisubiria adhabu hiyo katika njia ya Mola wake, na akaadhibiwa mwanamke kwa sababu

    hakuridhia kuacha Uislamu kurudia dini ya mababa zake, na walikua Waislamu kwa jumla

    wanapigwa na wanaelekezwa njia mbaya zaidi ya unyonge, na walikua wanasubiri yote hayo

    kwa ajili ya kutaka radhi za Allah Taala.

    KUUPINGA ULINGANIZI

    Pindi alipotumilizwa (SAW) na Uislamu watu wakaanza kumzungumza yeye na kuhusu

    ulinganizi wake, na makureishi walikua ndio wachache wao katika kuzungumzia, kwa sababu

    hawakuwa wanajali ulinganizi na wakidhania kuwa mazungumzo yake hayatazidi

    mazungumzo ya makasisi na wasimulizi, na kuwa watuwatairudia dini ya mababa zao na

    mababu za, hivyo basi hawakumkimbia na wala hawakumkataza, na pindi alipokua anapita

    katika katika mikao yao walikua wanasema kijana huyu wa Abdul Muttalib anazungumziwa

    kutoka mbinguni, na akiendelea hivyo, isipokua baada ya kupita muda mchache wa ulinganizi

    wake na wakaanza kuhisi khatari ya hunu ulinganizi walikubaliana wote juu ya kumpinga na

    kumfanyia uadui na kumpiga vita, na mwanzoni walonelea akumpiga vita kwa kupinga tu

    ulinganizi wake juu ya kile anacho dai kuhusu utume wake, baadae wakamuendea kumulizia

    miujiza yake ambayo kwayo atathibishia utume wake, na walikua wanasema ni kwa nini

    Muhammad haigeuzi milima ya Swafaa na Marwa kuwa ni dhahabu, na wala haiteremshi

    kitabu kilicho andikwa kutoka mbinguni kinachozungumza kuhusu yeye, na ni kwa nini Jibril

    hajitokezi ili awazungumzie wao kuhusu Muhammad, na ni kwanini hafufui wafu,na wala

    hayapeperushi majabali ili Makkah isiwe ni yenye kuzingirwa nayo, na ni kwanini hapasui

    maji ya chemchem yaliyo matamu kuliko maji ya zamzam ilhali yeye anajua watu wa mji

    wanavyohitajia maji, na ni kwanini Mola wake hamfunulii yeye bei za bidhaa ili tuzikimbilie

  • Page 7 of 125

    siku za usoni, na hivi ndivyo wakawa wanampiga mtume na ulinganizi wake kwa mbinu za

    kijinga, na hali ikaendelea hivyo, lakini hilo halikumzuia Mtume (SAW) kuendelea na

    ulinganizi wake bali aliendelea kuwalingania watu katika dini ya Allah na huku anayakashifu

    masanamu kuyaaibisha na kuyakejeli kuzisafihi akili za wanavoviabudu na ndoto zao

    wanaoyatukuza, ikawa zito juu yao hilo na hivyo basi wakatumia mbinu zote ili wamzuie na

    ulinganizi wake na wala hawakufaulu, na miongoni mwa mbinu muhimu walizozitumia za

    kupambana na ulinganizi huu ni mbinu tatu;

    1) Kuadhibu 2) Uvumi wa kindani na wa kiinje 3) Vikwazo

    Aina za adhabu zilikuwa zikimfikia Mtume rehma na amani ziwe juu yake pamoja na kwamba

    ameshikamana na kaumu yake, na juu ya Waislamu wote, kwani zilizotofautiana na mbinu za

    kuwaadhibu lakini waliwaadhibu vikali ili waiache dini yao lakini hilo halikuwazidishia ila

    uthabiti na imani, na Mtume (SAW) alipita na huku wanaadhibiwa na akawaambiya »يئاً صبراً آل ياسر فإن موعدكم الجنة إني ال أملك لكم من هللا ش «

    "Subirini jamii ya Yassir hakika makao yenu ni peponi mimi similiki chochote kutoka kwa

    Allah" na hakika jawabu yoyote kutoka kwa Sumayya mke wa Yassir pindi alipowaambiya

    hakika makao yenu ni peponi, isipokuwa alisema: "Mimi naiona mbele yangu, ewe Mtume wa

    Allah." Na hivi ndivyo makureshi waliendelea kumuadhibu Mtume na maswahaba wake.

    Makureishi walipoona kuwa hilo halikufaa wakatumia silaha nyengine nao ni silaha ya

    propaganda ya dhidi ya Uislamu dhidi ya Waislamu katika kila sehemu, katika mji wa Makaa

    kindani na katika mji wa Habashi kiinje, na wakatumia propaganda katika kila sehemu na kwa

    kila kinacho hitajika nacho kama mjadala na huja na kueneza uvumi, na wakatumia

    propaganda dhidi ya aqeeda, na kumtuhumu nayo na kuituhumu dhati yake, na wakawa

    wanakanusha Mtume, na wakawa wanajiandaa na kila propaganda watakuitumia dhisi ya

    Muhammad katika mji wa Makka na nje ya Makka na khususan propaganda katika msimu wa

    hijja na makuireishi waliona umuhimu wa kupanga propaganda dhidi ya Mtume (SAW) kiasi

    ya kuwa walikusnayika kikundi cha makuresihi kwa Walid bin Mughaira wakishauriana ni

    yapi watakaoyasema kuhusu Muhammad kuwaambia waarabu wanao kuja Makkah katika

    msimu wa hiujja, baadhi yao wakashauri kuwa waeme kuhusu yeye kua ni kuhani, Al-Walid

    akaipinga rai hiyo kuwa anaoyasema Muhammad hayana mfanano wa kuhani, wakashauri

    baadhi yao wengine wadai kua Muhammad ni mwandazimu, Al-Walid pia akapinga rai hiyo

    kwa sababu hamna ishara kuwa Muhammad anaonyesha ishara ya uendawazimu wake, na

    wengine wakaonelea kuwa wamtuhumu Muhammad na uchawi Al-Walid akaipinga rai hiyo

    kwa kusema kuwa Muhammad hapigi ramli na wala hafanyi jambo lolote linalihusiana na

    uchawi. Na baada ya majadiliano na mvutano, walikubaliana kumtuhumu Muhammad (SAW)

    juu ya sihr ul-bayan (uchawi wa maneno). Kisha wakatawanyika katika makundi ya mahujaji

    waarabu wakiwatahadharisha kumsikiza Mtume (SAW) kwa sababu yeye ni mchawi wa

    maneno na anayosema ni uchawi unaomtenganisha mtu na kakake na mamake, na babake na

    familia yake, na inaogopewa kwa yoyote atakae msikiza kurogwa na akatengana na watu

    wake. Lakini uvumi huu haukufaa, na wala haikuwa ni kizuizi kati ya watu na ulinganizi wa

    Uislamu. Kisha wakamuendea An-Nadhr akawa killa alipokuwa amekaa Mtume (SAW) katika

  • Page 8 of 125

    kikao anapolinganiwa katika dini ya Allah nae huja akisimuliya hekaya za mafursi na dini yao,

    na anasema, ni kwa lipi Muhammad awe na hadithi nzuri zaidi kuliko mimi. Si yeye anasoma

    maandiko ya kale kama ninayosema mimi? Na makuresihi walikuwa wakizichukua hadithi

    hizo na kuzieneza kwa watu, vile vile walikuwa wakiyasambaza anayosema Muhammad

    kuwa yeye (Muhammad) anafundishwa na kijana wa kinasara aliyekuwa akiitwa Jabr na kua

    hayatoki kwa Allah, na wakaeneza sana uvumi huo mpaka Allah akawarudi kwa kusema: } ولُوَن إِنََّما يُعَّلُِمهُ َبَشٌر ِلَساُن الَِّذي يُْلِحُدوَن إِلَْيِه أَْعَجِميٌّ َوَهذَا ِلَساٌن َعَرِبيٌّ ُمبِينٌ َولَقَْد َنْعَلُم أَنَُّهْم يَقُ {

    "Hakika Tunajua kuwa wao wanasema:'Yeye anafundishwa na mwanadam'. Ulimi wa yule

    wanaemsingizia ni wa kiajemi na huu ni ulimi wazi wa kiarabu" [TMQ An-Nahl 103] na hivyo

    ndivyo uliendelea uvumi wa makureishi ndani ya bara arabu. Na wala hawakukoma hapo bali

    wakti waliposikia kuwa Waislamu wamegura kwenda Habash waliwatuma wajumbe wao

    wawili ili waeneze uvumi dhidi ya Waislamu kwa Najashi ili awatoe katika biladi yake. Na

    wajumbe hao wawili walikuwa ni Amru bin Al-Aas na Abdallah bin Rabiah. Hivyo basi

    walifika Habash na wakampelekea zawadi generali wa Najash ili awasaidie kuwarudisha

    Waislamu Makka, na wakakutana na Najashi na wakamwambia, " Ewe mfalme wamekuja

    katika biladi yako vijana masafihi kutoka kwetu waliojitenga na dini yao ya kaumu yao na

    wala hawakuingia katika dini yako na wamekuja na dini waliozusha, hatuijui sisi wala wewe,

    na tumekuja kwako na watu wao watukufu miongoni mwao mababa zao maami zao na

    familia zao ili uwarudishe kwani sisi tutawaangalia wao zaidi na twaelewa zaidi kasoro yao".

    Najashi akataka kuwasikia Waislamu wanaoyasema kuhusiana na hayo, na akutamana

    wakaitwe na walipoitwa aliwaulizwa, "Ni dini ipo hiyo amabo mumetengana na kaumu yenu

    na wala hamukuingia katika dini yangu wala katika dini nyengineo"? Akajibu Jaafar bin Abi

    Twalib, akaielezea hali zao katika zama za kijahiliyya na tabia walizo kuwa nazo, na kisha

    akaelezea uongofu ambao Uislamu umekuja nao, na hali ilivyogeuka baada ya kusilimu kwao,

    kisha akaeleza kuadhibiwa kwao na makureshi (na walipo tushinda nguvu na kutudhulumu

    na kututia dhiki na wakawa ni kizuizi kati yetu na dini yetu, tukatoka kuja katika biladi yako,

    na tukakuchagua wewe na kuwawacha wengine na tukapendelea kuwa jirani yako na

    tukatarajia tusiwe ni wenye kudhulumiwa hapa kwako) Najashi akasema kumuambia Jaafar,

    "Je, kuna kitu alichokuja nacho mjumbe wenu kutoka kwa Allah unisomee? Jaafar akasema,

    "Ndio" Jaafar akasoma sura ya Maryam kwanzia mwanzo wake mpaka katika kauli yake

    Ta'ala ]ُم َم]ْن َك]اَن ِف]ي اْلَمْه]ِد َص]بِيZا{ َوَجعَلَِن]ي ُمبَاَرًك]ا أَْي]َن َم]ا ُكن]ُت -َق]اَل إِّنِ]ي َعْب]ُد اَل]ِه آتَ]اِنَي اْلِكتَ]اَب َوَجعَلَِن]ي نَبِيZ]ا - فَأََشاَرْت إِلَْيِه قَالُوا َكْي]َف نَُكّلِ

    َكاِة َما ُدْمُت َحيZا الَِة َوالزَّ }َوالسَّالَُم َعَليَّ يَْوَم ُوِلْدُت َويَْوَم أَُموُت َويَْوَم أُْبَعُث َحيZا -ا بَِواِلَدِتي َوَلْم يَْجعَْلِني َجبَّاًرا َشِقيZا َوبَرZ -?َوأَْوَصاِني بِالصَّ"Maryam akaashiria kwake (Motot) wakasema itawezekanaje kuzungumzia na mtoto mchanga-akasema

    (motto) hakika mimi ni mja wa Allah amenipatia Kitabu na akanijaalia Utume na akanijaalie ni mwenye

    popote ulipo na akanuusia na swala na zake madamu ni hai na nimtendee wema mamangu na wala

    hakunifanyia jabari muovu na amani iwe juu yangu siku siku nilio zaliwa na siku nitakao kufa na siku

    nitakaofufuliwa kuwa hai" (TMQ Maryam 29:33) Na aliposikia generali haya maneno, alisema

    "maneno haya yanatoka katika chimbuko lile ambalo yalipotoka maneno ya bwana wetu yesu

    masihi na Najashi akasema: "Haya na hayo aliokuja nayo Issa yanatoka mshumaa mmoja."

    Kisha akawaelekea wajumbe wawili wa kikureishi na kuwaambia: "Nendeni, Wallahi

    sitowasalimisha kwenu." Na wakaondoka wajumbe wawili katika ikulu ya Najashi na wakawa

    wanafikiria njia nyengine, na ilipofika siku ya pili Amru bin Al-Aaas alirudi kwa Najahi na

    akawambia: "Waislamu wanasema maneno maovu kuhusu Issa mwana wa Maryam". Najashi

    akatumana Waislamu waitwe na kuwauliza, Jaafar akasema: "Tutasema kuhusu yeye yale

    aliokuja nayo Mtume wetu, anasema: "Mja wa Allah na Mtume wake na roho yake na neno

  • Page 9 of 125

    lake aliyoiweka kwa Maryam bikira aliebarikiwa." Najashi akaishika fimbo na akachora nayo

    mstari juu ya ardhi na kumwambia Jaafar "Hapana kati ya dini yenu na dini yetu zaidi ya

    mstari huu." Na wakaondoka wajumbe wa kikureishi na wakarudi kwao mikono mitupu.

    Hivyo ndvyo zilivyoanguka propaganda na nguvu ya haki ambayo Mtume rehma na amani

    zimshukie anailingania ilikuwa katika sura ya wazi ambayo inaotoka katika ulimi wake

    inaolea juu ya uvumi wote, na nuru ya Uislamu inaoaangaza inazima diaya zote na uvumi. Na

    wakaanza makuresihi kutumia silaha ya tatu nao ni silaha ya vikwazo, na wote

    wakakubaliana kumwekea vikwazo Mtume (SAW) na familia yake na wakaandika mkataba

    waliokubaliana ndani yake juu ya kuiweka vikwazo baina Hashim na Banu Abdul-Muttalib

    kuwatenga kamili wasiolewe wala wasiozeshwe kusinunuliwe kwao na wala wasiuziwe. Na

    wakabandika mkataba huo kwenye ukuta wa Kaaba, kwa kusisitizia na kuwakumbusha, na

    wakadhania kua siasa hii ya vikwazo itakuwa ni yenye athari zaidi kuliko ya kuadhibu na

    uvumi. Na wakaendelea vikwazo hivyo kwa muda wa miaka miwili au miaka matatu, na

    huku wakiwa wanangoja banu Hashim na Banu Abdul-Muttalib wamwache Muhammad

    (SAW) na Waislamu wauuache Uislamu wao ili Muhammad (SAW) abakie pekee, nae imma

    arudi nyuma na ulinganizi wake au kusiwe na tishio lolote la ulinganizi wake juu ya

    makureshi na juu ya dini zao, na hili halikumzidishia Mtume (SAW). Isipokuwa ni mwenye

    kushikamana na kamba ya Allah na ni menye kushikamana na dini ya Allah na kumzidishia

    hamasa katika njia ya ulinganizi kwa Allah, na wala hawakuzidi waumini walio kuwa pamoja

    nae Isipokuwa ukakamavu na nguvu na wala hawakuwa ndio kizuizi cha kuenea ulinganizi

    wa Uislamu katika Makka na nje ya Makka, na habari ya vikwazo vya makuresihi kumuekea

    Muhammad ikawafikia waarabu nje ya Makka na habari ya ulinganizi ikaenea kwa makabila,

    na habari ya Uislamu ukawa unaenea katika bara arabu. Na wasafiri wakawa wanazungumza,

    Isipokuwa vikwazo viliendelea na maumivu ya njaa iliendelea, na mkataba ambao uliowekwa

    na makureshi ni wenye kuendelea. Na akabakia na watu wake katika vichaka vya Makka

    wakiwa wanumizwa na njaa na ukosefu na ufukara. Na mara nyingi hawakuwa ni wenye

    kupata kinacho tosheleza mahitaji yao, vile vile hawakuwa na fursa ya kutangamana na watu

    na wenye kuwazungumzisha, isipokuwa katika miezi mitukufu Mtume (SAW) alikuwa

    anakwenda upande wa Al-Kaaba akiwalingania katika dini ya Allah na kuwapa biashara ya

    thawabu zake na kuwaonya na adhabu zake, kisha anarudi vichakani. Na hili lilikuwa likileta

    sikitiko kwa waarabu juu yao na miongoni mwao walikuwa wakikubali ujumbe wake, na

    miongoni mwao walikuwa wakiwapeleka chakula na kinywaji kwa kujificha, Hisham bin

    Amru alikuwa anachukua ngamia aliebebeshwa chakula na ngano na anakwenda nae kati kati

    ya usiku mpaka anapofika vichakani, hapo anawachilia kamba yake kisha anampiga ubavuni

    mwake ili aende vichakani na wanachukua alichobeba, na kumchinja na kula nyama yake, na

    wakendelea katika hali hiyo kwa muda wa miaka matatu mfufulizo mpaka dunia ikawa ni

    dhiki kwao mpaka Allah alipoileta faraja yake na vikwazo vikaisha. Na hayo ni kutokamana

    na vijana watano wa kikureshi nao ni Zubeir bin Abi Umayya na Hisham bin Amru na Mutim

    bin Adiq na Abu Bukhtiriy bin Hisham na Zama'a bin Al-Aswad walikusanyika na

    kuzungumzia kuhusu mkataba na suala la kikwazo, na miongoni mwao wakalipinga na

    kudhihirisha chuki zao kwa baadhi yao, na wakakubaliana na kuweka ahadi ya kufanya jambo

    ambalo litapeleka kuvunjika kwa mkataba na kuurarua, siku ya pili walikwenda hadi Al-

    Kaaba akaja Zuheir akatufu mara saba kisha akawaita watu "Enyi watu wa Makka sisi

    tunakula na tunavaa na huku Banu Hashim wanaangamia hawauzi wala hawauziwi, wallahi

  • Page 10 of 125

    sitokaa mpaka uraruliwe huu mkataba wa vikwazo wa kidhalimu. Hakuwacha kusema mpaka

    Abu Jahl akasikia na akampigia mayowe" Umedanganya wallahi usirarue, kwa upande wa pili

    Kaaba walikuwepo Zama'a na Abu Al-Bukhtiriy na Mutim na Hisham wote hawa wakapiga

    makelele huku wakimghadhabisha Abu Jahl na kumtia nguvu Zuheir. Abu Jahl akafahamu

    kuwa hili limepangwa usiku na kuwa watu wanakubaliana nao na kuwa khalifu kwaweza

    kuzua shari hivyo basi nafsi yake ikaingiwa na uoga na hapo akarudi nyuma. Na Mutim

    akasonga Mbele ili auraruwe mkataba, na akaupata kuwa umeliwa na mchwa isipokuwa

    ufunuzi wake (Kwa jina lako ewe Mola – Bismika Allahumma) na hilo likampatia nafsi Mtume

    (SAW) na maswahaba wake warudi Makka kutoka vichakani na vikwazo visitishwe, hapo

    wakarudi na Mtume akaendelea na ulinganizi wake, hivi ndivyo zilivyo anguka mbinu za

    makureishi katika kuadhibu na uvumi na vikwazo na wala hazikuweza kufitini Waislamu na

    dini yao, wala kumrudisha Mtume na ulinganizi wake na hatimae Allah Ta'ala akaifanya ni

    yenye kudhihiri pamoja na vizuizi vyote na vizingiti.

    MAINGILIANO YA ULINGANIZI

    Mapambano ya makureishi na ulinganizi wa Kiislamu ilikuwa ni jambo la kawaida, kwa

    sababu yeye Mtume (SAW) alibeba ulinganizi na kudhihirisha kikundi ambacho kinabeba

    ulinganizi pamoja nae kwa sura ya mapambano na mvutano, juu ya hayo ulinagnizi wenyewe

    kwa dhati yake ililazimisha kupambana na makuresishi na mujtama katika mji wa Makka kwa

    sababu ilikuwa inalingania kumpwekesha Allah na kumuabudu yeye tu pekee, na kuwacha

    kuabudu masanamu na kuingoa nidhamu fisidifu ambayo wanaishi nayo, hivyo basi

    ikagongana na makureishi mgongano kamili, na jee yawezekana kwa Mtume (SAW) asiwe ni

    mwenye kugongana na makureishi ilhali yeye anazisafihi ndoto zao na kudharau miungu yao

    na kukejeli maisha yao ya kirahisi, na kukashifu njia yao kimaisha ya kidhalimu. Inamshukia

    Quran ikiwahujumu na huku ikiwaambia parwanja: }إِنَُّكْم َوَما تَْعبُُدوَن ِمْن ُدوِن هللاِ َحَصُب َجَهنََّم {

    "Nyinyi na munaoviabudu kinyume na Allah ni kuni za moto" [TMQ Al-Anbiyaa: 98]. Kisha

    anaihujumu riba ambayo kwao wanaishi nayo akiwahujumu kwa ukali kutokamana na msingi

    wake. Amesema Ta'ala katika sura ya Al-Rum: }َوَما آتَْيتُْم ِمْن ِربًا ِليَْربَُوا ِفي أَْمَواِل النَّاِس فَالَ يَْربُوا ِعْنَد هللاِ {

    "Na kile mnacho kitoa ili kuchukua riba katika mali ya watu basi hakiongezeki Mbele ya Allah" [TMQ

    Ar-Rum: 39]. Na anawakemea wale ambao wanaopanga katika uzito na mizani. Amesema

    Ta'ala: َوإِذَا َكالُوُهْم أَْو َوَزنُوُهْم يُْخِسُروَن } -الَِّذيَن إِذَا اْكتَالُوا َعلَى النَّاِس َيْستَْوفُوَن -َوْيٌل ِلْلُمَطّفِِفيَن

    "Ole wao hao wanaopunja ambao wanaponunua kwa watu wanatimiza na wanapopima hupunguza"

    [TMQ Al-Mutafiffin: 1-3]. Na kwa sababu hiyo wakawa wanampinga na wakimuudhi yeye na

    maswahaba wake mara kuwaadhibu, na mara nyengine kuwawekea vikwazo na kwa kueneza

    uvumi dhidi yake na dini yake. Isipokuwa yeye aliendelea kuwahujumu na aliendelea

    kugonga rai potofu, na kuvunja aqeeda fisidifu na kufanya juhudi katika njia ya kueneza

    ujumbe. Na alikuwa anaulingania Uislamu kwa uwazi wala harudi nyuma na wala

    kutaradhilia na wala kuhadaa, juu ya yale yalimkumba aina za adhabu kutoka kwa

    makureishi, pamoja n mashaka yaliomsibu, juu ya kuwa alikuwa ni pekee mnyonge hana

    msaidizi wala mwenye kumnusuru, hana chochote wala silaha kwani yeye alikuja kwa njia

    wazi na mapambano, akilingania dini ya Allah kwa nguvu na Iman, wala hakuingiwa na

    udhaifu wowote wa Kubeba majukumu ya ulinganizi na kutekeleza majukumu makubwa kwa

    ajili yake, yote hayo yakawa ndio sababu kwa ajili yake, hayo yakawa ndio sababu za kuvuka

  • Page 11 of 125

    vizingiti vyote ambavyo makureishi walivyomuekea mbele yake ili kumzuia yeye kuwafikia

    watu. Na Mtume (SAW) aliweza kuwafikia watu na akawafikishia, na wakakaikubali dini ya

    Allah, na nguvu ya haki ikawa ipo juu ya batili, na nuru ya Uislamu ukawa unazidi kila siku

    kuenea kati ya waarabu, wakasilimu wengi waliokuwa wakiabudu masanamu na katika

    manasara, bali mabwenyenye na kikureishi wakawa wanaisikiza Qur'an na mioyo yao

    kuhuzunika.

    Tufail bin Amru Ad-Dawsi alikuja Makka na alikuwa ni mtu mtukufu mwenye akili,

    makureishi wakamuendea kumtahadharisha kuhusu Muhammad na kua maneneo yake ni

    kama uchawi yanyomtenganisha mtu na watu wake na kuwa wao wanamroga na kaumu yake

    mfano ya wale waliowapata wao Makka, na kuwa bora asiwe ni mwenye kumzungumzisha na

    wala asimsikize. Siku moja Tufeil alikwenda katika Al-Kaaba na Mtume (SAW) alikuwa hapo

    na hatimae akasikia maneno yake nayakawa ni maneno mazuri na akaiambia nafsi yake

    "Wallahi mimi ni mtu mwenye akili mshairi, mimi siwezi kuchanganyikiwa na kizuri katika

    kibaya basi ni kipi kinacho nizuia kumsikiza mtu anaoyasema, iwapo ni mabaya nitayawacha"

    na akamfuata Mtume (SAW) mpaka nyumbani kwake kisha akajitambulishe na akaeleza

    yaliomo moyoni mwake, hapo Mtume (SAW) akamuelezea kuhusu Uislamu na akamsomea

    Quran hapo akasilimu na kutammka shahada ya haki, na akarudi kwa kaumu yake

    akiwalingania Uislamu.

    Na Mtume (SAW) alipokuwa Makka alijiwa na watu ishirini wa kinasara wakati walipofikiwa

    na habari zake, na wakakaa nae na wakamsikiza, na wakamuitikia na wakamuamini na

    wakasadiki jambo lililowaudhi makureishi mpaka wakawatukana na kuwaambia: "Allah

    awaangamize ni watu aina gani nyinyi, watu wenu wamewatuma ili muwaletee habari za mtu

    huyu na pindi tu mlipokaa nae mukaiwacha dini yenu na mkayaamini aliyoyasema". Na

    hawakurudishwa nyuma na maneno waliyoyasema makureishi katika kufuata Mtume na wala

    hawakurudi nyuma na Uislamu bali liliwazidishia imani kwa Allah juu ya imani yao. Na

    hivyo ndivyo ilivyo dhihiri ulinganizi wa Mtume na ikazidi shauku ya watu ya kusikiza

    Quran kiasi ambao hata wale ambao ni maadui zaidi wa kikureishi wakawa wanaulizana, "Je,

    ni ukweli analingania dini ilionyoka na anayowaahidi na kuyaonya nayo ni sahihi? Maswali

    haya yakawapelekea kunyanyapa na kuenda kuisikiza Quran. Alitoka usiku mmoja Abu

    Sufyan bin Harb, Abu Jahl, Amri bin Hisham na Akhnas bin Shariq ili wamsikize Muhammad

    (SAW) akiwa nyumbani mwake, na Muhammad (SAW) alikuwa anasimama usiku Isipokuwa

    analala kidogo akisoma Quran huku wakisikia aya za Allah, mioyo yao na nafsi zao

    zikaathrika, na wakawa wamenyamaa mpaka alfajiri, na wakaondoka kurudi nyumbani

    mwao, wakakutana njiani na wakaanza kulaumiana na wakaambiana musirudie kwani

    mukionekanwa na wengine walio wajinga mambo yenu yatadhoofika mbele yao na

    Muhammad atawashinda, na ilipofika usiku wa pili, kila mmoja alijiskia kwenda ile sehemu

    aliukuwepo jana ni kana kwamba miguu yake pasi na yeye kuweza kujizuia kufika pale

    alipokuwepo usiku wa jana, na ili amsikize Muhammad tena upya, na wala haikuwa kizuizi

    kulaumiana kwao ya kuenda usiku wa tatu na walipofahamu udhaifu wao kwa ulinganizi wa

    Muhammad waliahidi wasirudie waliofanya, na wakawacha kwenda kumsikiza Muhammad

    (SAW) lakini walioyasikia usiku tatu yaliwacha athari katika nafsi zao iliwafanya waulizane

    baina yao kuhusu yale walioyasikia, na wote wakaingiwa na wasiwasi katika nafsi, na

    anahofia asije akadhoofika na yeye ni kionozi wa watu wake wakamfuatia Muhammad

  • Page 12 of 125

    (SAW). Na hivi ulienea ujumbe kila sehemu pamoja na kwamba vizingiti walivyoviweka

    mbele yake, hilo liliwaudhi sana makureishi na ikazidi hofu yao ya kuenea ujumbe kati ya

    makabila ya kiaarabu baada ya kuenea Makka, na wakazidi kuwaudhi maswahaba wake, na

    wakawa wanaendelea kuzidi kuwaudhi, na kuongeza hasira zao kwa maswahaba mpaka

    ikawa dhiki kwao. Hapo akatoka kuelekea Taif na kutarajia Uislamu wao, lakini

    wakamrudisha kwa jawabu ilio mbaya zaidi, na wakatoa vijana wao na wandazimu wao na

    kumtukana na wakampiga kwa mawe mpaka miguu yake yakaloa damu, akawatoroka na

    kurudi mpaka alipofika kwenye bustani la zabibu la Utbah na Shaibah watoto wa Rabiah

    akawa anafikiria kuhusu nafsi yake na ulinganizi wake, kwani alikuwa hawezi tena kurudi

    Makka Isipokuwa chini ya ulinzi wa mmoja wa mabwenyenye wa Makka mushrikina, na wala

    hawezi kwenda Taif baada ya mateso yaliomkumba, na wala hawezi kubakia hapo kwa

    sababu bustani ni la watu wawili washirikina, hapo wasiwasi ukazidi na akanyanyua kichwa

    chake mbinguni akimshtakia Allah katika hali ya maumivu makubwa, na katika hali ya imani

    na kutaka radhi zake, na akawa anaomba dua hii: أللهم إليك أشكو ضعف قوتي وقلة حيلتي وهواني على الناس, يا أرح]م ال]راحمين أن]ت رب المستض]عفين وأن]ت رب]ي, إل]ى م]ن تكلن]ى, «

    إن لم يكن بك علي غضب فال أبالي, ولكن عافيتك هي أوس]ع ل]ي. أع]وذ بن]ور وجه]ك أل]ذي إلى بعيد يتجهمني, أم إلى عدو ملكته أمري,ى ترض]ى, وال ح]ول وال ليه أمر الدنيا وآلخرة, من أن تنـزل بي غضبك, أو يحل علي سخطك, لك العتبى حتأشرقت له الظلمات, وصلح ع

    »قوة إال بك "Ewe Mola kwako wewe nalalamikia udhaifu na nguzo zangu na uchache wa maarifa yangu

    na unyonge wangu kwa watu, ewe mwingi wa rehma mwenye kurehemu wewe ndie Mola

    wa wanyonge na wewe ndie Mola wangu, waniegemeza kwa nani, kwa wa mbali, atake

    nihujumu, au kwa adui ulemilikisha mambo yangu, iwapo huna ghadhabu juu yngu basi

    mimi sijali, lakini msamaha wako ndio mkunjufu kwangu. Najilinda kwa nuru ya dhati

    yako ambayo imeangazia kiza, na kutengea kwao mambo ya dunia na akhera isije

    ikanishukia mimi ghadhabu zako au kufikiwa na hasira zako, ni wewe wa kufanyiwa

    mpaka uridhike, wala hamna uwezo wala nguvu Isipokuwa kupitia wewe". Kisha akarudi

    Makka katika ulinzi wa Muti'im bin Adiy, na makureishi walijua yaliyomfikia Muhammad

    katika mji wa Taif, hivyo basi wakazidisha mateso na wakazidisha vitimbi vyao juu yake, na

    wakawa wanawakanya watu kumsikiza, na watu wa Makka wakawa wanajiepusha nae na

    kumpuuza, hilo halikumfanya kuwacha kulingania dini ya Allah, na akawa anazungukia

    makabila ya waarabu katika msimu wa hijja anawlaingania katika Uislamu, na anawaeleza

    kuwa yeye Mtume aliiyetumwa, na kuwataka wamuamini, isipokuwa ammi yake Abdul-

    Uzzah bin Abdul-Muttalib, Abu Lahab hakuwa akimwacha bali alikuwa anamfuata

    anakoenda na akiwahimiza wasiwe ni wenye kumsikiza, hilo likawaathiri na wakawa

    wajiepusha kumsikiza Mtume (SAW) akawa anayaendea makabila katika majumbani mwao,

    na kuwaelezea, na akawaendea Kinda katika majumba yao na akawaendea Kalb katika

    majumba yao na akawaendea Bani Hanifa na Bani Amir bin Saa' saa', hamna kati yao,

    aliemsikiza na wakamrudisha kusiko kuzuri, bali Bani Hanifa walimrudisha kwa ubaya. Ama

    Bani Amir bin Saa' Saa' wakafanya tamaa iwapo atashinda utwala uwe kwao baada yake, na

    pindi alipo waambia, utawala ni wa Allah anauweka anapotaka, wakamgeuzia nyuso zao na

    wakamrudisha kama walivyomrudisha wengine. Na hivi ndivyo Makka ilipuuza Uislamu na

    watu wa Taif kumpuuza Mtume (SAW) na makabila walivyo urudisha ujumbe wa Mtume

    (SAW) na makabila ambayo yanaokuja Makka kuhiji yaliona ule upweke aliokuwa nao

    Muhammad na namna makureishi walivyomzingira na uadui, ilifanya kila msaidizi kuwa ni

    adui kwake na wasaidizi kwao, na wakazidi kumpuuza na hilo lilimzidisha Mtume (SAW)

  • Page 13 of 125

    upweke, na ulinganizi ukwa mgumu katika Makka na pambizoni mwake na kujtamaa wa

    Makka ukajitokeza kwa ukafiri na inadi, jambo ambalo linalofanya matarajio kudhoofika.

    MIZUNGUKO MIWILI KATIKA MIZUNGUKO YA ULINGANIZI.

    Katika mji wa Makka Mtume (SAW) alifuata mizunguko miwili mfululizo, dori ya kwanza ni

    kufundisha na kujenga na matayarisho ya kifikra na ya kiroho, na dori ya pili ikiwa ni dori ya

    kuzihamisha hizi fikra kwa nguvu za msukumo katika mujtama itakao usukuma ili

    wazitabikishe katika nyanja za kimaisha kwa sababu fikra hubakia kuwa ni malumati

    madamu hazijatabikishwa, na hamna tofauti hizi fikra ziwe katika vitabu au katika mabongo

    kwani zitakuwa zimefungika katika sehemu, hivyo basi fikra hazitakuwa na thamani iwapo

    hazitatabikishwa katika maisha. Na fikra ili ziweze kutabikishwa ni lazima zipitie dori ya

    kuzibadilisha kutoka katika fikra na kuingia katika nguvu itakao wasukuma watu, ili watu

    jumla waziamini na kuzifahamu na kuzibeba na kupambana ili zitabikishwe, na wakati huo

    utabikishaji wake itakuwa ni jambo lisilo na shaka na la kikawaida. Na hivi ndivyo Mtume

    (SAW) aliupeleka ujumbe katika Makka katika dori hizi mbili, ama dori ya kwanza ni

    kuwalingania watu katika Uislamu, na kuwajenga kwa fikra na kuwafunza hukmu zake na

    kuunganishwa yule anaeweza kuunganishwa juu ya aqeeda ya Kiislamu na dori hii ni ni dori

    ya kuunganisha kisiri katika dawah. Na hilo ni kwa saabu Mtume (SAW) alikuwa hadharau

    ulinganizi na kuwa na bidii ya kumjenga kifikra kila anaeingia katika Uislamu, na

    anawakusanya katika nyumba ya Al-Arqam, na kumtuma yule aliemjenga kujenga katika

    halaqa, na wakajumuika Waislamu katika majumba yao kisiri na majabalini kwa siri na katika

    nyumba ya Arqam kwa siri na wakajengwa, na kila siku kuzidi imani yao na kuongezeka

    maingiliano yao, na kila siku kuzidi kufahamu umuhimu ambao wanaobeba, na kujitayarisha

    kujitolea katika njia hiyo mpaka dawah ikakita katika nafsi zao, na Uislamu ukawa unatembea

    ndani yao kama damu katika viwiliwili vyao, na wakawa ni Uislamu unatembea katika

    mabarabara. Na kwa ajili hiyo haukuweza ujumbe kubakia umefungwa katika nafsi zao

    pamoja na kujificha kwao pamoja na kujengwa kwa kisiri na kufanya bidii ya kuficha

    kujumuika kwao, na wakawa wanawazungumzia wanaowaamini na kwa kila yule

    wanaomtarajia kuwa yuko tayari kuukubali ujumbe, na kwa sababu hiyo watu walihisi

    ulinganizi wao, na kujua kuwepo kwao, na kwa hila ukatambulika ujumbe kama nukta ya

    kianzio, na ikawa hamna budi kutoka, na yakapatikana majaribio ya kuingiza na

    kuwazungumzia watu wote, na kwa hilo lilimalizika dori ya kwanza ikiwa ni dori ya

    kuwaunganisha kisiri na kuwajenga ambao umejenga muungano huu, na ikawa hamna budi

    kuingia katika dori ya pili ikiwa ni dori ya mapambano na mvutano kwa kuwafahamisha watu

    Uislamu ili waviitikie pamoja nao na kuukubali na kutangamana nao, au waukatae na

    waubebe na kugongana kwa fikra zake, na yatapatikana kwa mgongano huu ni kuwa ukafiri

    na usidifu vishindwe na itulie imani na matengeneo, na fikra sahihi kushinda, kwa sababu

    akili namna zitakavyo kanusha lakini haitoweza kufungika mbele fikra sahihi, wala haziwezi

    kuzikataa, hata kama walijaribu kuzitoroka ili zisiathiriwe. Na hivi ndivyo ilivyoanza dori ya

    mapambano na kwao kuanza mvutano baina ya fikra mbili, baina ya Waislamu na makafiri,

    lilionekana kwa hilo muungano wa kichama pindi alipotoka Mtume (SAW) pamoja na

    maswahaba wake katika mpangilio ambao waarabu hawajauonapo kabla yake, na katika

    mshikamano mmoja, na akatufu nao Al-Kaaba na kudhihirisha ujumbe wake. Na kuanzia

    wakati huo Mtume (SAW) akawa anaeneza ujumbe baina ya watu wote parwanja mchana kwa

    njia ya kupambana na kuwachalenji. Na zikawa aya zinamshukia Mtume (SAW)

  • Page 14 of 125

    zinazolingania Tauhid, na kukanusha masanamu na shirki na kuyahujumu na kukemea

    kufuata mababa na mababu pasi na muelekeo, na zikawa zinashuka kuhujumu maamiliano

    fisidifu na zikihujumu riba, na kuhujumu biashara chafu na kufanya hila katika kupima na

    mizani, na Mtume akawa anawazungumzia watu Uislamu kwa makundi, alikuwa anawaalika

    chakula watu wake nyumbani kwake na akiwazungumzia waote kwa pamoja, na anawataka

    wasilimu na kumuunga mkono na wakamkataa vibaya, kisha wanawakusanya watu juu ya

    safaa na anawazungumzia, na mabwenyenye wa kikureishi wanakasirika na Abu Lahab

    kumrudi vibaya mno, na chuki ya makureishi kuongezeka, na kwa Mtume Muhammad (SAW)

    vile vile kuongezeka chuki baina yake na waarabu wengine wasiokua Makuresihi, na hivi

    ndivyo ulinganizi inavyojumuisha kujenga kupitia halaqa katika majumba na katika majabali

    na katika nyumba ya Al-Aqram kujengwa kijumla, na kutoka kulingania yule anaetarajiwa

    kuwa yuko tayari na kuingia kulingania watu wote, na ulinganizi huu wa jumla na kujenga

    kwa pamoja ulikuwa na athari katika makureishi, kwani ilizidisha chuki yao na kuhisi hatari

    inaokuja, na wakaanza kuchukua hatua mpya Muhammad wala ulinganizi wake, na wakazidi

    kumuudhi na kumkaandamiza Mtume (SAW) na maswahaba wake. Lakini hunu ulinganizi

    wa kijumla ulikuwa na athari katika ulinganizi wenyewe, kwani wote walisikia neno Uislamu

    na ukaenea ulinganizi kwa dini ya Allah kati ya watu wote wa Makka, na wala hamna siku

    isipokuwa alisilimu mmoja wao kwa ajili ya Allah na radhi zake, na akaamini kila maskini na

    kila mnyonge na kila fakiri, na kila ambae habaishwi na biashara wala hababaishwi na kuuza

    na kudhrau kwa anaowalinhania kwao Mtume (SAW), na wakaamini baadhi ya wafanyi

    biashara wa Makka na watukufu wake na viongozi wao, katika wale ambao nafsi zao

    zilitambua usafi, hima na ukweli na kujiepusha na kiburi na kujigamba, hawa walisilimu kwa

    ajili ya Allah kwa ujua tu ukweli wa ulinganizi na ukweli wa mlinganizi, na Uislamu ukaenea

    Makka na watu wakaingia katika Uislamu waume kwa wake. Na ulinganizi wa jumla ulikuwa

    na athari pana, japo liliwapelekea katika mashaka na adhabu na kuwaka katika nafsi za

    mabwenyenye wa kikureishi kwa sababu Mtume kuhujumu dhulma na uovu na kumtenga

    ambao ulikuwa umeenea Makka kukashifu kwake hali za makafiri na mambo yao. Na ikaanza

    baina ya Mtume wa mswahaba wake na baina makafiri wa kikureishi marhala uilio mgumu

    zaidi na dori ilio mbaya zaidi. Japokuwa ilikuwa ni kuingia katika dori ya mapambano kutoka

    kwa dori ya kujenga japo ni dori nyembamba zaidi kwa sababu inahitaji hikma subra na

    umakini wa utekelezaji, hivyo basi dori ya mapambano ndio dori ngumu zaidi kwa sababu

    inahitaji uwazi wa kujitolea bila ya kujali natija na matokeo, kwani itapatikana kufitini kwa

    makafiri kwa Waislamu juu ya dini yao, na pia hudhihirika imani nguvu ya kustahamili na

    kudhihirika yaliomo katika nafsi kama ukweli wa kukutana, na hivi ndivyo alipitia Mtume

    (SAW) katika dori hii yeye pamoja na mswahaba wake wakivumilia aina ya majabali

    makubwa ya dhulma maonevu kunyanyaswa na kukandamizwa, miongoni mwao waliougura

    Habash ili kuhifadhi dini yao, miongoni mwao waliouwawa kwa kuadhibiwa na miongoni

    mwao waliovumilia aina kali za adhabu, na walioendelea hivyo kwa muda mrefu waliokuwa

    unatosha kuathiri mujtama wa Makka kwa nuru ya Uislamu na kuondosha dhulma pamoja n

    akwa Mtume (SAW) alikaa miaka matatu katika nyumba ya Al-Arqam na kumaliza dori ya

    kwanza ikiwa ni dori ya kuunganisha na kujenga kisiri kwa muda wa miaka hii mitatu pia,

    aliishi Mtume (SAW) miaka minane mengine huku anapambana na (miujiza ikiidhihirikia

    watu) juu ya hayo haikusahilisha njama za makureishi za kuadhibu Waislamu wala

    kusahalisha hamasa zao katika kuupinga Uislamu, naam hayo yalikuwa kutokamana na

    Waislamu kuvutana na makureishi mpaka bara arabu nzima ikasikia kuhusu Uislamu, na

  • Page 15 of 125

    mazingira ya dawah yakaenea katika sehemu zote za bara arabu, ilipopelekwa na mahujaji na

    wakawa wanaizungumza, lakini hawa waarabu walikuwa wamesimama msimamo wa

    watazamaji, na wala hawakuchukua hata hatua moja kusongelea iman, bali walikuwa

    hawataki kuwaudhi makureishi, na wajiepushe na Mtume (SAW) ili makuresihi wasikasirike.

    Likawa zito hilo kwa Mtume (SAW) na mswahaba wake na kudhihirika kwa dori ya

    kujitokeza ina dori ya tatu nao ni utabikishaji wa Uislamu hauna budi nao, lakini uovu wa

    mujtama katika Makka hauoneshi dalili ya uwezekano wa kutabikisha, na kuendelea

    maudhuijuu ya Waislamu liliwazuia wao kujitolea kamili kwa ajili ya Dawah bali kuwa

    kizuizi baina yao na baina yake, na watu kupuuza dawah hayo yaliwazidisha maumivu na

    huzuni.

    KUUPANUA UWANJA WA DAWAH

    Yaliongezeka mateso ya makuresihi kwa Mtume (SAW) kwa kuwa Waislamu mpaka ikawa ni

    dhiki kwao, na hapakubakia na matarajio ya makabila kumnusuru yeye baada ya Thaqif

    kumrudisha na majibu mabaya, na baada ya kurudishwa na Kinda na Kalb na Banu Amir na

    Banu Hanifa wakati alipowaendea katika msimu wa hijja, na hapakuwa na matumaini ya

    kuingia katika Uislamu katika makureishi na yaliona makabila yasiokuwa ya kikuresihi

    ambayo wanaishi jirani na Makka na yale ambayo yanaokuja kutoka sehemu tofauti kutoka

    biladi za waarabu ili kuhiji, yale yanaomkumba Muhammad (SAW) kama kutengwa, na

    namna makureishi walivyo mzingira na uadui ilimfanya killa msaidizi kuwa adui juu yake na

    wasaidizi wao, hivyo basi wakazidi kumpuuza. Na Mtume (SAW) akaona ujumbe wa Mola

    wake katika mzunguko kuanzia kufuata kwake mpaka leo, na yakarefuka masiku na Mtume

    (SAW) anazidi kutengwa na watu wake, na makuresihi wanazidisa juu yake chuki, na watu

    wanazidi kumpuuza, Isipokuwa yeye (SAW) pamoja na yote hayo aliendelea yeye na

    maswahaba wake waliokuwa karibu nae katika hali ya imani kali zaidi juu ya nusra ya Allah

    na kunyanyua dini yake juu ya dini zote na akawa anawalingania watu kila anapopata wasaa,

    na msimu wa hijja unapofika wa watu wakikusanyika katika mji wa Makka kutoka bara arabu

    alikuwa anawaendea na kuwalingania katika Uislamu bila ya kujali iwapo makabila hayo

    watapuuza ujumbe wake au kumpuuza au kumrudisha na majibu yasio mazuri. Baadhi ya

    wajinga wa kikureishi walikuwa wanamfuata na kumuudhi wakati aipokuwa anawaendea

    watu kuwafirishia ujumbe wa Mola wake, na wala hayo maudhui hayakumuondoshea

    matamanio na matumaini yake. Hakika Allah ndie aliemtumiliza na Uislamu hivyo basi

    hamna shaka atamnusuru na atamsaidia na mwenye kuifanya dini yake idhihiri. Na akawa

    anasubiri nusra ya Allah hali ya kuwa siku hizo yupo katika maumivu ya kusimama

    ulinganizi wake, na katika shida na dhiki ya makureishi, na wala hakusubirii sana hatimaye

    dalili ya kufuzu ikawa inakuja kutoka Madina, hilo ni kuwa watu katika Khazraj walitoka kuja

    Makka katika msimu wa hijja Mtume (SAW) akakutana nao na akawazungumzia na

    akawauliza kuhusu wao, na akawalingania kwa Allah na wakaanza kuangaliana na

    wakasema: Wallah huyu ni Mtume ambaye mayahudi wanaahidi basi wawatangulia na

    wakakubali ujumbe na Mtume na wakasilimu na wakakuambia: Sisi tumewacha kaumu yetu

    (yaani Aws na Khazraj) na wala hamna watu wenye uadui kati yao kama uliopo baina yao na

    huenda Allah akatuunganisha kupitia wewe na iwapo Allah atatuunganisha kupitia wewe

    basi hamna mtukufu zaidi yako". Na watu hawa wakarudi Madina na wakawaeleza watu wao

    kuhusu kusilimu kwao, na wakaziunganisha mioyo iliyo wazi na nafsi zilizo kunjufu katika

  • Page 16 of 125

    dini mpya, na wala haikubakia nyumba ya Aws wala Khazraj ila kuna utajo wa Muhammad

    (SAW).

    BAYAH YA KWANZA YA AQABAH

    Mwaka ulipozunguka na kuingia msimu wa hijja walikuja watu kumi na mbili mwaka huo

    katika watu wa Madina na wakakutana na Mtume (SAW) katika Aqabah na wakambayiisha

    bayah ya kwanza ya Aqabah, walimbajiisha juu ya asiyemshirikisha Allah na chochote na wala

    assibe wala wasizini na wala asiue watoto wake na wala asieneze uvumi atakautunga Mbele

    ya mikono yake na miguu yake na wala asimuasi katika jema na iwapo atatekeleza hayo basi

    atapata pepo na iwapo atalaghai katika hayo chochote basi mambo yake ni kwa Allah akitaka

    atamuadhibu na akitaka atamsamehe. Na baada ya kuikamilisha bayah na msimu wa hijja

    kumalizika walirudi Madina.

    ULINGANIZI KATIKA MADINA

    Amesema ibn Ishaq: wau walipokuwa wanaondoka, Mtume (SAW) alimtuma Musa'ab bin

    Umeir pamoja nao, na akamuambia awafunze Quran na awafundishe Uislamu na

    awafundishe dini, na Musa'b akawa anaitwa Muqri (msomaji) katika Madina. Na makao yake

    yalikuwa kwa Asaad bin Zurarah. Na akawa anawaendelea watu katika maskani zao na

    makabila yao na kuwalingania katika Uislamu, na anawasomea Quran na anamsilimisha mtu

    na watu wawili mpaka Uislamu ukaenea katika maskani zote za Answar isipokuwa maskani

    ya Khatamah na Wail na Waqif, na Musa'b akawa anawasomea Quran na kuwafundisha, na

    akamuandikia barua Mtume (SAW) kumtaka ruhusa ili awakusanye na akamruhusu na

    akamuandikia: "Ama baad: subiri siku ambayo mayahudi watajitayarisha kwa zaburi kwa

    ajili ya jumamosi yao…mchana unapoingia basi jikurubishe kwa Allah kwa Rakaa mbili na

    uwakhutubie, Musaab bin Umeir akawakusanya katika nyumba ya Saad bin Khaithamah

    wakiwa ni watu kumi na mbili na hakuwachinjia siku hiyo ispokuwa mbuzi mmoja, kwani

    yeye ndie wa kwanza kuanzisha jumaa katika Uislamu. Musa'ab akaendelea kuzunguka

    Madina kuwatembelea watu na akiwalingania katika Uislamu na kuwafundisha. Siku moja

    Asaad bin Zurara alitoka na Mus'ab bin Umeir akiwa amekusudia nyumba ya bani Abdul

    Ashhal na nyumba ni mtoto wa khalati ya Asaad bin Zurarah na akaingia nae kupitia bustani

    katika mabustani ya bani Dhafr karibu na kisima kilichoitwa Marq, na wakakaa katika bustani

    na watu waliokuwa waliosilimu wanaanza kujumuika. Na Saad bin Muadh na Useid bin

    Khudheir siku hizo walikuwa ni mabwana kwa watu wao wakiwa ni bani Abdul Ash-hal, na

    wawili hawa walikuwa wakishirikiana wakifuata dini ya watu wao, wa walipo wasikia Saad

    bin Muadh akimuambia Useid bin Khudeir" Twende kwa watu wale wawili ambao wamekuja

    kwetu kuwasafihi wajinga tuwafukuze na tuwakataze wasije kwetu, kwani lau kama Asaad

    bin Zurarah hahusiani na mimi na mimi basi wajua mimi natosheleza, yeye ni motto wa

    khalati yangu na mimi siwezi kumfanya lolote, Useid bin Khudheir akachukua mkuki wake

    kisha akamwendea na pindi Asaad bin Zurarah alipomuona alimuambia Musa'ab bin Umeir

    huyu anakujilia ni bwana kwa watu wake hivyo basi kuwa mkweli kwa Allah Mbele yake,

    Musa'ab akasema "Iwapo atakaa nitazungumza naye" akasema: akawasimamia kwa ukali na

    akasema "ni yapi ywaletani kuja kusafihi wajinga. Ondokeni iwapo mwazithamini nafsi zenu"

    hapo Musa'ab akasema "Hukai ili usikie iwapo utaridhika utayakubalina iwapo utayachukia

    tutawacha yanaokuudhi" akasema "umefanya uadilifu" kisha akakita mkuki wake na akakaa,

    Musa'ab akamzungumzia kuhusu Uislamu na akamsomea Quran wakasema kulingania na

  • Page 17 of 125

    waliyosema wallahi tuuliona Uislamu katika uso wake kabla hajazungumza kwa amani yake

    kuunga kwake. Kisha akasema: "ni mazuri yalioje maneno haya, ni yapi munaoyafanya iwapo

    munataka kuingia katika dini hii?" wakamuambia: "utaoga, ujitahirishe nguo zako kisha

    utapiga shahada ya haki kisha utasali rakaa mbili. Akasimama na akaswali Rakaa mbili kisha

    akawaambia "nyuma yangu kuna mtu iwapo atawafuata hamna hata mmmoja atakae

    mkhalifu katika watu wake na nitawaletea sasa hivi Saad bin Muadh kisha akauchukua mkuki

    wake na akaenda kwa Saad na watu wake wakiwa wamekaa na watu maskani yao, pindi Saad

    bin Muadh alipomuona anavyokuja akasema "Naapa kwa Allah Useid bin Khudheir

    anawajilia na sura taofauti na ile aliowaondokea nayo, na walipo simama katika maskani Saad

    akamuambia" Umefanya nini" akasema "Nimezungumza na watu wawili na wallahi sikuona

    ubaya wowote kwao na niliwakataza na wakasema tutafanya unachokipenda. Na

    nimeambiwa kua bani Harith wametoka kuenda kwa Asaad bin Zurarah ili wamvuwe, na hilo

    ni kuwa wamejua kuwa yeye ni mototo wa khalati yako ili wakuchimbe, Saad akasimama kwa

    hasira na haraka kwa huku alioelezwa kuhusu basi Harith akashika mkuki mkononi mwake

    kisha akasema: "Walla nimekuona hutoshi" kisha akawatokea na Saad alipomwona makini

    alijua kuwa Useid alichotaka ni yeye awasikie na akawasimamia kwa hasira kisha

    akamuambia Asaad bin Zurakah "Ewe Aba Umamah lau kama hamna kilichoko baina yangu

    na yako uhusiano usingelinifanyia hayo, munatulaghai hapa kwetu kwa yale

    yanayotuchukiza, na Asaad ameshangulia kumuambia Musa'ab, yaani Musa'ab amekujilia

    mtu Wallah ni bwana wa watu wake iwapo atakufuata hamna atakaye kuenda kinyume yako

    wawili wao. Musa'ab akamuambia: "Kwani hukutusikia iwapo utadhihirika na utapendelea

    utayakubali, na iwapo utayechukia tutayawacha yanaokuchukiza." Saad akasema: "Umefanya

    uadilifu" kisha akaukita mkuki wake na akakaa. Akaanza Musa'ab na kumueleza Uislamu na

    akamsomea Quran, wakasema"Tukaona Uislamu usoni mwake kabla hajasema kwa sababu ya

    kungaa kwake na amani yake, kisha akawaambia" munafanya nini iwapo mutasilimu na

    kuingia katika dini hii?" wakasema"utajitahirisha na kutahirisha nguo zako kisha utapiga

    shahada kisha utaswali rakaa mbili." Kisha akauchukua mkuki wake akaondoka kuelekea

    maskani na watu wake wakiwa na Useid bin Khubeir na watu wake walipomuona anakuja

    wakasema: "Tunaapa kwa Allah Saad anawarudia na sura tofauti na ile ambayo

    amewaondokea nayo" na akawasimamia na akasema: "Enyi bani Abdul Ash-hal nyinyi

    munachukulia vipi kwenu?' Wakasema Kiongozi wetu na mwenye ushauri bora zaidi kwetu

    na kiongozi shupavu" akasema "maneno ya wanaume wenu na wanawake wenu ni haramu

    mpaka mutakapo amini Allah na Mtume wake" wakasema"Basi wallah hakukutwa katika

    nyumba ya bani Abdul Ashhal mwanamume na mwanamke illa Muislamu." Musa'ab akarudi

    nyumbani kwa Asaad in Zurarah na akaishi kwake akiwalingania watu katika Uislamu, hata

    ikafikia haikubakia nyumba katika majumba ya Answar isipokuwa wanaume na wanawake

    Waislam. Musa'ab akakaa Madina pamoja na Aws na Khazraj kwa muda wa mwaka

    anawafundisha dini yao huku anaangalia kwa furaha kuongezeka kwa watakao nusuru dini

    ya Allah na neno la haki na alikuwa radhi za Allah zimshukie Musa'ab anawabishia milangoni

    watu kwa kumkimbilia ili kuwalingania nao na akawafikishia ulinganizi wa Allah, na alikuwa

    anaingia mashambani ili kuingilia na wakulima na katika shughuli yao akiwalingania katika

    Uislamu, na alikuwa anakutana na viongozi anawalingania katika dini ya Allah, na alikuwa

    anafanya mambo aliyokusudia kama alivyofanya pamoja Asaad bin Zurarah katika kutumia

    mbinu ya kuwafikia watu ili waweze kuwasikilizisha sauti ya haki mpaka mji wa Madina

    kutoka kwa ushirikina, upotofu na kutoka katika miito miovu (kuwapeleka katika tauhid na

  • Page 18 of 125

    imani na miito ya Kiislamu) iliojengwa juu ya shirki na kunguza katika uzito na uzani. Hivyo

    ndivyo ulivyokuwa ukakamavu wa Musa'ab na ulivyokuwa ukakamavu ya wale ambao

    waliosilimu pamoja mpaka waliweza Kuibadilisha Madina katika mwaka mmoja kutoka hali

    ya ushirikina mpaka katika hali ya Uislamu.

    BAY'AH YA PILI YA AQABAH

    Bay'ah ya kwanza ya Aqabah ilikuwa ni kheri na baraka, kwani waliosilimu juu ya uchache

    wa idadi yao walitosheka na mtu mmoja miongoni mwa maswahaba wa Mtume nae ni

    Mus'aab kuweza kuiadilisha Madina na kugeuza mawazo na miito iliokuwepo katika mujtama

    wao, pamoja na kwamba kuwa jumla ya watu wamejitenga nao hivyo basi jumla

    hawakuamini, na mujtama usiweze kuathirika kwa fikra na miito ya Kiislamu, kinyume na

    Madina kwani waliuingia katika Uislamu jumla ya watu, na mujtama ukaathiri na miito

    ikaathiri na hii ni dalili wazi imani ya watu fulani waliotengwa na mujtama waliotengwa na

    jumla ya watu haikuathiri katika mujtama wala katika watu jumla namna iwavyo uwezo wa

    watu hawa kadha. Na kwa mahusiano yaliopo kati ya watu iwapo zitaathiri kwa kuathiri fikra

    na miito mageuzi yatapatikana na mapenduzi namna iwavyo uchache wa idadi ya wanaobeba

    ulinganizi. Na yaonyesha pia kuwa mujtama pindi utakuwa umeganda juu ya ukafiri kama

    mujtama wa Makka inakuwa ni vigumu zaidi kuliko mujtama ambao haujaongozwa na rai

    fisidifu mfano wa mujtama wa Madina hata kama zipo rai hizo ndani yake, kwa sababu hiyo

    uliathiri mujtama katika Madina kwa Uislamu kuliko wa Makaa, kwani watu wa Madina

    walikuwa wanahisi upotofu wa fikra ambazo wanazozibeba na walikuwa wanatafuta fikra

    nyengine na nidhamu nyengine kwa ajili ya maisha yao, ilhali mujtama na Makka ulikuwa

    umetulia kwa yale waliokuwa nayo, na kuwa hamu ya kuendeleza hasa mabwenyenye wa

    ukafiri mfano wa Abu Lahab na Abu Jahl na Abu Sufyan, kuwa sababu hiyo hakukawia

    Mus'aab katika Madina muda mfupi hatimae kulipatikana mageuzi ya ulinganizi na kuweza

    kuitikiwa kwa haraka na akashuhudia kukubali kwa watu Uislamu na kukubali kujifunza

    hukmu zake na kumfurahisha sana, na anaona kuongzeka idadi ya Waislamu na Uislamu

    kuenea Madina, anafurahishwa kwa hila na inaongezeka uchangamfu katika kufundisha na

    kueneaza ujumbe, na ulipoingia msimu wa hijja alirudi Makka na akamueleza Mtume (SAW)

    habari za Waislamu na nguvu zao na habari za Uislamu na kuzidi kuenea kwake, na

    akamuelezea namna mujtama wa Madina umekuwa hazungumzi isipokuwa Uislamu, na

    kuwa nguvu za Waislamu na uwezo wao huko una taathira na kuufanya Uislamu ndio ambao

    unaolea juu ya kila kitu, na kua mwaka huu watakuja baadhi ya Waislamu walio na imani

    kubwa zaidi kwa Allah na wako tayari Kubeba ujumbe wa Allah na kuihami dini ya Allah,

    akafurahia sana Mtume (SAW) habari ya Mus'aab akawa anafikiria kwa urefu na akawa

    analinganisha kati ya mujtamaa wa Makka na mujtama wa Madina, kwani Makka amelingania

    watu kwa Allah kwa muda wa miaka kumi na mbili mfululizo na watu hakuchoka kufanya

    daw'ah na wala hakuacha fursa isipokuwa alitumia kila anachoweza kama juhudi na

    kuvumilia killa aina za adhabu, pamoja na hayo mujtama umejifunga na iimekosekana njia ya

    kuupenyeza ujumbe kutokamana na uovu uliopo katika mioyo ya watu wa Makaa na ugumu

    uliopo katika nafsi zao, na mgando wa kale uliopo katika akili zao, na kwa sababu hiyo

    mujtama wa Makka muovu na dhaifu wa kukabili daw'ah kutokamana na ushirikina wa

    masanamu uliokita katika nafsi za wakazi wake ambao Makka ilikuwa kama kitovu chake.

    Ama mujtama wa Madina baada ya kupita mwaka ilikuwa ni kusilimu kwa watu wachache na

    Khazraj, kisha bay'ah ya watu kumi na mbili na juhudi ya Mus'aab bin Umeir kwa muda wa

  • Page 19 of 125

    mwaka mwengine, hayo yalikuwa yanatosha kuleta mazingara ya Kiislamu katika Madina na

    watu kuingia katika dini ya Allah kwa haraka hii ya kushangaza, na iwapo Makka ujumbe

    umesimama kwa wale ambao tu waliosilimu pamoja na yanaowakumba Waislamu katika

    mateso na maudhi ya makureshi, basi Madina ujumbe wa Allah umeanza kuenea haraka

    hivyo na wala mateso ya washirikina na hayo ni katika yanaoumakinisha Uislamu katika nafsi,

    na kuwafungulia njia Waislamu, hivyo ndivyo ilivyo bainika kwa Mtume (SAW) kuwa

    Madina inafaa zaidi kwa daw'ah ya Uislamu kuliko makaa na mujtama wa Madina unafaa

    zaidi kueneza nuru ya Uislamu kuliko wa Makka. Na kwa sababu hiyo akafikiria kuguria na

    wakagura maswahaba wake kwenda kwa ndugu zao Waislamu ili wapate amani kwao na ili

    wasalimike na mateso ya makureshi na ili wajitolee kwa ajili ya daw'ah kuiingiza katika

    marhala ya kivitendo nao ni utabikishaji wa Uislamu na Kuubeba ujumbe wake na nguvu za

    serikali na utawala wake, hiyo ndio sababu pekee ya kuguria na wala sio nyengine.

    Na ni lazima ieleweke kuwa Mtume (SAW) hakufikiria kugura Makka kwa sababu ya vizuizi

    vilivyo kuwepo Mbele ya daw'ah pasi na kusubiria au ili aviepuke vizuizi hivi, kwani yeye

    Mtume (SAW) alisubiri miaka kumi katika Makka, na wala haipurukushi daw'ah na alikuwa

    anafikwa mateso katika njia ya daw'ah yeye na wafuasi wake na wala mateso ya makureshi

    hayakudhoofisha chochote katika nafsi yake na kudhoofisha azma yake ya mapambano yao,

    bali yalimzidisha mani katika daw'ah ambayo kwao imeleta utukufu kuto kwa Allah, na

    kumzidisha yakini kwa nusra ya Allah kumzidisha umakinifu na uthabiti, lakini aliona baada

    ya majaribio hayo uovu ulio katika mujtama wa Makka kama fikra finyo na ugumu na upotofu

    mambo yanaodhoofisha matarajio na kuendeleza ujumbe inahitajia juhudi zaidi, ndio ikawa

    hamna budi kutoka mujtama huo na kuingia katika mujtama mwengine na ndio maana

    akafikiria kuigura Makka, na hilo ndilo ambalo limempeleka kufikiria kuguria Madina, na

    wala sio mateso yaliomfikia yeye na yaliowafikia maswahaba wake. Ndio tume (SAW)

    aliamrisha maswahaba wake wagurie habasha kukimbia mateso, kwani inajuzu kwa waumini

    kugura sehemu za fitna kuhifadhi dini yao, japo mateso yanaongeza imani kukandamizwa

    kuzidisha ikhlasi na mapambano yanalenga matarajio, na imani humpelekea alie nayo

    kupuuza kila kitu na kujitolea katika njia yake kwa mali, cheo, raha na maisha, ndio hata kama

    imani juu ya Allah humfanya muumin aitangulize nafsi yake katika hatari kwa ajili ya Allah

    lakini kuendelea kwa mateso na kudumu katika kujitolea humfanya muumin kujishughulisha

    na subra juu ya mateso na kuzidi kujitolea kutampuepusha kutafakari jambo ambalo

    litamzidisha muumin upana wa kudiriki haki, hivyo basi imekuwa namna budi kwa muumin

    kugura sehemu za fitna. Isipokuwa hilo linalingania na kugura kwa aislamu na kwenda

    habash. Ama kuguria kwa Madina ilikuwa ni kwa ajili waweze kumakinika kuugurisha

    ujumbe wao katika hali ambayo ni hai katika mujtama wao mpya, na kuueneza katika

    ulimwengu ili wanyanyue neno la Allah. Na hapa ndipo Mtume (SAW) aliamrisha

    maswahaba wake kiasi hicho. Na kabla hajawaarimsha kuguria Yathrib na kabla hajaamua

    kuguria ni lazima aonane na mchujaji kutoka Madina, na akutane na Waislamu waliokuja

    kuhiji na kujionea upeo wa maandalizi yao ya kuhifadhi ujumbe na upeo wa maandalizi ya

    kujitolea kwa ajili ya Uislamu na kuona iwapo watambayiisha yeye bay'ah ya vita, bay'ah ya

    vita ndio jiwe msingi ya kusimamisha serikali ya iislamu na akasubiria kuingia kwa mahujaji,

    na hiyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na mbili ya kutumilizwa sawa na 622 miladi na

    mahujaji walikuwa ni wengi na miongoni mwao walikuwa Waislamu sabiini na tano: sabiini

    na tatu wanaume na wanawake wawili wakiwa ni Nuseibah bint Kaab Umm Ammarah

  • Page 20 of 125

    mmoja kati ya wanawake wa bani Maziu bin Najjar na Asmaa bint Amru bin Adiy kati ya

    wanawake wa bani Salamah nae ni Umm Mani'i, Mtume (SAW) akakutana nao kwa siri na

    akawazungumzia katika bay'ah ya pili kuwa haimaliziki katika ujumbe tu na kusubiria bali

    inapita hayo inasonga mbele kiasi hawezi kuwapitia nguvu Waislamu kujihami nafsi zao, bali

    inakwenda mbali zaidi ya hayo pia kiasi ya kuweka kiungoambacho kitakuwa jiwe msingi la

    kusimamisha serikali ya Kiislamu, ambayo utatabikishwa katika mujtama na kuubeba ujumbe

    wake kiulimwengu kwa watu wote, na Kubeba pamoja nao nguvu ambazo zitauhami na

    kuondosha njiani mwaka kila kizuizi inaosimama katika njia ya kuweza kwake na utabikishaji

    wake. Aliwazungumzia hayo na akatambua uzuri wa maandalizi yao na akaagana nao

    wakutane nae Aqabah usiku wa manane katikati ya siku za Tashriq. Na akawaambia

    wasimwamshe alielala, wala musimngoje asiekuwepo. Na siku ya maagano maalum baada

    kupita thuluthi ya kwanza wa usiku wakaanza safari yao wakinyapanyapa na wakijificha,

    wakiogopea kujulikanwa na yeyote na wakaenda Aqabah na wote wakapanda jabali na

    wakapnda wanawake wawili pamoja nao na wakawa wanamsubiri Mtume (SAW) na akawajia

    akiwa na Abbas na wakati huo hakuwa amesilimu bali amekuja kumpa nguvu motto wa

    kakake. Na ndie aliekuwa wa kwanza kuzungumzia akasema: "Enyi kongamano la Khazraj,

    bila shaka mwajua hali ya Muhammad hapa mwetu, na tumemhifadhi kutokamana na watu

    wetu ni kama hivi tumuonavyo, yeye ni mtukufu kwa watu wake na amehifadhiwa katika mji

    wake na yeye hataki illa kuungana na nyinyi na kuwa pamoja na nyinyi na iwapo mwaona

    mutatekeleza munayomuahidi na kumhifadhi na maadui wake basi nyinyi na mlioyabeba na

    iwapo mwaona mutamsalimisha na kumuuza baada ya kutoka kuja kwenu basi muachane

    hivi sasa". Na pindi waliposikia maneno ya Abbas walimuambia "tumesikia uliyoyasema"

    Kisha wakasema "Zungumza ewe Mtume wa Allah tumia ulimi wako kuizungumzia nafsi

    yako na Mola wako unaoyapenda". Mtume (SAW) akajibu baada ya kusoma Quran na kutia

    motisha katika Uislamu »مما تمنعون منه نساءكم وأبناءكم يعكم على أن تنمنعوني أبا «

    "Nawabayiisha juu ya kunihifadhi mimi kama munavyohifadhi wake zenu na watoto

    wenu". Baraa akaunyosha mkono wake ili ambayiishe kwa hayo akasema "Tumekubayiisha

    ewe Mtume wa Allah wallahi sisi ni watu wa vita na watu wa silaha na tumezirithi kutoka

    kwa mababu na mababu". Na kabla Barra hajamaliza maneno yake, Abu Haitham bin Tayhan

    akamkatiza kwa kusema "Ewe Mtume wa Allah kati yetu na watu (yaani mayahudi) kuna

    mkataba na sisi tutauvunja, na iwapo sisi tutafanya hilo na kisha Allah akakupa ushindi

    utarudi kwa watu wako na kutuacha? Mtume (SAW) akatabasamu na akasema: »رب من حاربتم, وأسالم من سالمتمبل الدم الدم, والهدم الهدم أنا منكم, وأنتم مني, أحا «

    "Bali damu yenu ni damu yangu na kitukufu chenu ni kitukufu kwangu mimi ni katika

    nyinyi na nyingi katika mimi, utapigana na yeyote mutake pigana nae na nitaweka amani

    na yule mulieweka nae amani". Na watu wakataka kufanya bay'ah Abbas bin Ubada

    akawakatiza kwa kusema "Enyi Khazraj mwajua ni kuwa lipi munalo mbayiisha nalo mtu

    huyu nyinyi muambayiisha juu ya kupigana na watu wekundu na weusi iwapo nyinyi

    mwaona mutapoteza mali yenu na watukufu wenu kuuwawa na baadae kumsalimisha basi

    bora sasa, kwani mukifanya basi hizaya ya dunia na akhera itawafika, na iwapo mwaona

    mutatimiza kwa yale munaomwtia nayo ya kuharibu mali na watukufu kuuwawa basi

    mchukuweni kwani wallah yeye ni kheri ya dunia na akhera. Watu wakajibu sisi tutamchukua

    juu ya mali kuaribiwa na watukufu kuuwawa, kisha wakasema "Tutapata nini ewe Mtume wa

    Allah iwapo tutatimiza hayo". Mtume akawajibu huku ametulia kwa kusema: »الجنة «

  • Page 21 of 125

    "Pepo" Wakainyosha mikono yao nae akawanyoshea mkono wake na wakambayiisha huku

    wakisema: بايعنا رسول هللا صلى هللا عليه وسلم على السمع والطاعة في عسرنا, ويس]رنا, ومنش]طنا, ومكرهن]ا وأث]رة علين]ا وأن ال نن]ازع األم]ر «

    »كنا, ال نخاف في هللا لومة الئم أهله, وأن نقول بالحق أينما "Tulimbayiisha Mtume (SAW) juu ya kusikiza na kutii katika mazito yetu na mepesi yetu

    na yanayotuchangamsha na yanaotuchukiza na tusiwe ni wenye kujipendelea na wala

    tusizozane kuhusu utawala na wanao husika, na tuwe tunazungumza ukweli popote

    tutakapo kuwepo tusiogope katika njia ya Allah lawama za mwenye kulaumu" na walipo

    maliza Mtume (SAW) akasema: »كونوا على قومهم بما فيهم كفالء اثني عشر نقيباً, لي أخرجوا إلي منكم «

    "Nitoleeni watu kumi na mbili kati yenu ili wawe ni wasimamizi juu ya watu wao" watu

    wakachagua watu tisa kutoka Khazraj na watatu kutoka Aws, na Mtume akawaambia hawa

    Manaqibu: »سى بن مريم, وأنا كفيل على قومي لى قومكم بما فيهم كفالء, ككفالة الحواريين لعيأنتم ع «

    "Nyinyi ni wasimamizi wa watu wenu mfano wa wanafunzi wa Issa ibn Maryam na mimi

    ni msimamizi juu ya watu wangu" wakasema "Ndio". Kisha wakarudi katika malazi yao, na

    wakabeba mizigo yao na kurudi Madina. Na baada ya hayo Mtume (SAW) aliwaamrisha

    Waislamu wakaamua kugura mmoja au vikundi vidogo, na makureshi walikuwa washajua

    kuhusu bay'ah na ndio maana walijaribu kumrudisha Makaa wanaemweza. Na wakawa ni

    pingamizi kwa Waislamu kugura mpaka kuwa pingamizi kati ya mtu na mkewe. Na wala hilo

    halikuathiri katika Hijra bali Waislamu waliendelea kuguria Madina na huku Mtume (SAW)

    bado anaishi Makka, na wala hamna ajuwae kama ameazimia kuguria Madina au ameamua

    kubakia Makka? Lakini lile ambalo linaonekana ni kua anataka kuguria Madina, kwani

    Abubakar alimtaka ruhusa ili agurie Madina na akasema Mtume (SAW): » تعجل لعل هللا يجعل لك صاحباً ال «

    "Usifanye pupa huenda Allah akakujaalia rafiki" Abubakar akajua kuwa anataka kugura. Na

    makureshi walikuwa wnaipigia mahisabu Hijra ya Mtume (SAW) kuenda Madina mahisabu

    elfu baada ya kukithiri Waislamu huko uwingi ambao umewafanya kuwa na mkono wa juu

    katika Madina na imewapatia wao nguvu kubwa pamoja na wale waliogura kutoka Makka, na

    iwapo Mtume atakuwa pamoja nao wakiwa katika nguvu hizi, basi hilo litakuwa maangamizo

    kwao. Hivyo basi wakafikiria kumzuia Mtume (SAW) kuguria Madina na wakati huo huo

    wakiogopea kubakia kwake Makka hilo litawaudhi Waislamu katika Madina na kuja kumaliza

    baada ya kupata nguvu hizo na watakuja kumkinga Mtume (SAW) wale waliomuamini yeye.

    Hivyo basi wakafikiria kumuua ili asikutane na Waislamu Madina ili kusiwepo kile kitakacho

    sababisha wao kupambana na watu wa Madina kwa ajili ya Uislamu na kwa ajili ya

    Mohammad (SAW). Na imekuja katika kitabu cha sera imepokewa kutoka hadithi ya Aisha na

    Abi Umamah bin Salmi "Na wakati walipoondoka watu sabiini nafsi yake ilitulia kwani Allah

    amemjaalia nusra kutoka kwa watu wa vita na nguvu". Na mateso yakawa yanaongezeka juu

    ya Waislamu kutoka kwa makafiri kwa kudhihirisha kwao kutoka na wawadhiki maswahaba

    wake na wafuasi wake na akifikiwa yale ambayo hawajawahi kufikiwa katika matusi na

    mateso kutoka kwa makureishi, na wakamlalamikia Mtume (SAW) na akasema: »ة قد أريت دار هجرتكم سبح «

    "Nimeonyeshwa nyumba yenu mutakaohamia" Kisha akakaa masiku kisha akatoka akiwa na

    furaha na kusema: »راد منكم أن يخرج فليخريج إليها قد أخبرت بدار هجرتكم وهي يثرب, فمن أ «

  • Page 22 of 125

    "Nimejulishwa nyumba yenu mutakaoihamia nayo ni Yathrib, kwa hivyo yoyote anaetaka

    kwenda basi aende huko". Na wakawa wanajitayarisha na kusuhubiana na kukutana na

    wanaotoka na wakajificha, walitoka vipute na vikundi vidogo vidogo, huku Mtume (SAW)

    bado yupo Makka akisubiria kupewa ruhusa ya kutoka, na Siddiq mara nyingi alikuwa

    anamuomba ruhusa Mtume (SAW) ili agurie Madina baada ya kua Waislamu wameanza

    kuguria na akimuambia: » تعجل لعل هللا يجعل لك صاحباً ال «

    "Usifanye pupa huenda Allah akakujaalie rafiki" Abubakar akawa anatarajia kuwa atakuwa

    ni yeye. Na pindi makureishi walipoona kugura kwa maswahaba na kujua katika Dar An-

    Nadwah wakashauriana kile watakachofanya kuhusu Mtume (SAW) na wakakubaliana

    wamuue na wakatawanyika juu ya uamuzi huo. Kisha Jibril akamjia Mtume akamuamrisha

    asilale kwenye kitanda chake anachokilalia na akamuelezea kuhusu vitimbi vya watu, usiku

    huo hakulala nyumbani kwake na hapo Allah akamruhusu atoke.

    Juu ya hayo kuwepo kwa nguvu za Kiislamu katika Madina, Madina kuandaa kumpokea

    Mtume (SAW) na kuisimamisha serikali ya Kiislamu huko ndio mambo ambayo yalimpeleka

    Mtume (SAW) kugura, na hiyo ndio sababu za moja kwa moja za kugura. Hivyo basi

    amekosea kila anayedhania kua Mtume (SAW) aliguria Madina kwa sababu ya uoga na

    kuogopa makureishi wasije wakamuua, na kutoroka. Kwani yeye Mtume (SAW) hakuyapigia

    mateso hisabu yoyote, na wala hakuwa akiyajali mauti katika njia ya kulingania Uislamu na

    wala haikumshughulisha nafsi yake wala uhai wake, na wala haikuwa kuguria Madina

    Isipokuwa kwa ajili ya ulinganizi wa Kiislamu na kwa ajili ya kusimamisha serikali ya

    Kiislamu. Bali makureishi walipanga njama ya kumuua kwa kuogopea kuguria kwake

    Madina, na kupata nguvu, lakini Mtume (SAW) akawashinda na akaguria Madina pamoja na

    kuchukiwa kwao, na wala wasiweze kumzuia pamoja na njama walizomfanyia. Hivyo basi

    Hijra imekuwa ndio kipambanuo katika Uislamu baina dori ya kulingania na kuhamisha

    mujtama na serikali itakao hukumu na kuitabikisha, na kulingania kwa hijja na dalili, na kwa

    nguvu ambazo itaohifadhi hunu ujumbe kutokamana na nguvu za shari na upotofu.

    KUSIMAMA KWA SERIKALI YA KIISLAMU

    Mtume (SAW) aliwasili Madina na akapokelewa na idadi kubwa ya wakaazi wake, wakiwemo

    Waislamu na mushrikina na mayahudi, na Waislamu wakawa wamemzunguka. Na wote

    walikuwa na hamu ya kumtumikia na kumfurahisha, wana hamu ya kuitolea nafsi zao kwa

    ajili ya ujumbe wa Kiislamu. Na kila mmoja wao alikuwa na hamu ya kumweka Mtume

    nyumbani mwake, lakini Mtume (SAW) aliachia kamba ya ngamia wake na hatimae akapiga

    magoti katika kiwanja cha Sahl na Suheil watoto wa Amru, na akakinunua na akajenga msikiti

    juu yake na ubavuni mwake akasimamisha nyumba yake. Na ujenzi wa msikiti na nyumba

    haikua ni ya kumumiza yeyote kwani ulikuwa ni wa sahali kiasi ambacho haikuhitajika

    mapesa mengi wala kazi kubwa. Msikiti ulikuwa ni ukumbi, kuta nne zilizojengwa na matofali

    na udongo, na sehemu ya sakafu ilikuwa imefinikwa na matawi ya mitende na sehemu

    maalum ya mafuqara ambao hawakuwa na makao na msikiti haukuwa ukiwaka mataa

    Isipokuwa wakati wa suala ya ishaa, kwani ilikuwa unang'arishwa na nyasi kavu

    zilizochomwa kando kando, na nyumba ya Mtume (SAW) haikuwa zaidi ya msikiti kiujuzi

    isipokuwa ilikuwa inamuangaza zaidi kuliko misikiti mengine. Na Mtume (SAW) alikaa

    katika nyumba ya Abu Ayyub Khalid bin Zeid Al-Answariy wakati wa ujenzi wa msikiti na

  • Page 23 of 125

    nyumba mpaka ilipomalizika kujengwa kwake, na akahamia na kutulia Mtume (SAW) na

    huku anatafakari kuhusu maisha mapya alioyafungua na ambayo yamemhamisha yeye na

    kuhamisha ujumbe wake katika uwanja mpana kutoka katika dori moja hadi dori nyengine,

    imetoka kutoka katika dori ya kujenga na katika dori ya mapambano na kuingia katika dori

    kutabikisha hukumu za Uislamu juu ya watu katika mahusiano yao. Na kutoka katika dori ya

    kulinganiwa isitoshe na kusubiria mateso kwa ajili yake na kuingia katika dori ya utawala na

    uongozi na nguvu ambazo zitaihami ujumbe huu. Kwani Mtume (SAW) pindi alipowasioli

    Madina aliamrisha kujengwa kwa msikiti kama sehemu ya kuswali kukutana na kushauriana

    na kusimamia mambo ya Waislamu na kuhukumu baina yao, na akamfanya Abubakar na

    Umar kama wasaidizi wake, amesema Mtume (SAW): »وزيراي في األرض أبو بكر وعمر «

    "Mawaziri wangu katika ardhi ni Abubakar na Umar" na Waislamu wakawa

    wamemzunguka na kumrudilia na akawa anatekeleza shughuli za kiongozi wa serikali na

    hakimu na amiri jeshi, na yeye Mtume (SAW) alikuwa anachunga mambo ya Waislamu na

    kuondosha husuma baina yao, na alikuwa anaviweka vikosi nje ya Madina. Na kwa hayo

    alisimamisha serikali katika Madina kuanzia siku ya kwanza alioingia, na akawa

    anaimaikinisha serikali hiyo kwa kujenga mujtama juu ya msingi thabiti, na kuandaa nguvu za

    kutosha zitakazoweza kulinda serikali na kueneza ujumbe. Na baada ya kuwa na matumaini

    na hayo yote alianza kuondosha vizuizi vya kimada ambayo vinasimama katika njia ya

    kueneza Uislamu.

    KUUJENGA MUJTAMAA

    Allah amemuumba mwanadamu na umbile la kuhifadhi maisha na katika madhihirisho yake

    kujumuika mwanadamu, hivyo basi ni jambo la kimaumbile kukutana kwa watu wao kwa

    wao, na kuwepo mujtama baina yao ni jambo la kimaumbile, isipokuwa kukutana tu kwa

    watu hakuwafanya kuwa ni mujtama, bali inawafanya wao kama kundi, na watabakia kundi

    iwapo watakomea juu ya kukutana tu kwao na iwapo yataanza baina yao mahusiano ya

    kupata maslahi yao na kujiondosha madhara, basi mahusiano hayo yatakifanya kikundi hicho

    kuwa ni mujtama, isipokuwa mahusiano hayo haitawafanya wao ni mujtama moja isipokuwa

    iwapo mitazamo yao itaungana wa kuunganisha fikra zao, kuungana mapenzi yao na

    machukivu yao kwa kuunganisha hisia zao, na kuungana utatuzi wa mahusiano hayo kwa

    kuunganisha nidhamu ambayo itakaotatua, hivyo basi hamna budi ya mtazamo wa fikra na

    hisia na nidhamu wakati wa kuangalia mujtama, kwa sababu ndio jambo ambalo linaofanya

    kuwa ni mujtama maalum ulio na rangi maalum. Na juu ya msingi huu tutauangalia mujtama

    katika Madina wakati wa kuingia kwake Mtume (SAW) ili tujue mwelekeo wake.

    Wakati huo Madina ilikuwa kunaishi vikundi vitatu: cha kwanza Waislamu wakiwemo

    Muhajirun Answar na walikuwa ni wengi. La pili mushrikina katika Aws na Kazraj ambao

    bado hawajasilimu na hawa walikuwa wachache. Na la tatu ni mayahudi nao ni vigawanyiko

    vinne: kimojawapo wanaishi ndani ya Madina na vitatu nje ya Madina. Ama wale waliokuwa

    ndani ya Madina walikuwa ni Banu Qainuqa'a na wale waliokuwa nje ni Banu adhir na

    mayahudi wa Khaibar na Banu Qureidhah. Na mayahudi kabla ya Uislamu walikuwa ni

    mujtama mbali na mujtama wa Madina, kwani fikra zao zilikuwa ni tofauti na hisia zao tofauti

    na utatuzi, hivyo basi mayahudi hawachukuliwi kuwa ni sehemu