adhabu ya viboko
TRANSCRIPT
![Page 1: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/1.jpg)
Je,
Adhabu ya viboko
ina madhara gani?
Vibokohavikubaliki
hapa!
TRV-Bk1
Jishindie kompyuta
Jishindie kompyuta
ndani!ndani!
![Page 2: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/2.jpg)
Adhabu ya kuchapa wanafunzi ni:Adhabu yoyote inayosababisha maumivu ya kimwili.
Kuchapa kwa mikono, vitu, kupiga teke, kuunguza, kusukuma,
ku nya, nk.
Vilevile ni adhabu yoyote ile isiyo ya kimwili ambayo
hudhalilisha, hutishia, huogopesha
na humuaibisha mtoto.
1
![Page 3: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/3.jpg)
Asilimia 98 ya watoto wamedai
kuwa wameshakumbwa
na adhabu hii...
Mtoto mmoja kati ya watatu
hukumbwa na adhabu hii kila wiki.
2
![Page 4: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/4.jpg)
Kwahiyo? Jambo hili lina ubaya gani?
Ni jambo ambalo tumekuwa nalo, hivyo tunadhani ni jambo zuri kwa malezi ya watoto wetu!
Mwalimu wangu alinichapa kwa sababu alitaka nijifunze!
3
![Page 5: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/5.jpg)
Wala hatuwaumizi watoto wetu!
Kweli! Tunawashikisha
adabu!
4
![Page 6: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/6.jpg)
Lakini adhabu ya kuchapa wa
Kimwili
Kihisia
Kimahusiano
Huumiza mwili wangu!
Huumiza moyo wangu!
Inanifanya nisiamini watu!
5
![Page 7: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/7.jpg)
anafunzi ina madhara mengi!
Kitabia
Ugumu wa
kujifunza
Hunisababisha nifanye mambo mabaya!
Hufanya nishindwe kujifunza!
Tazama ninacho maanisha!
6
![Page 8: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/8.jpg)
Madhara ya kimwili
Ninapaswa nichote maji na kusa sha nyumba kabla ya kwenda shule. Mara nyingi ninachelewa ku ka shuleni!
Mara nyingi ninachapwa ninapochelewa. Siku moja niliji cha kichakani mpaka mwisho wa vipindi.
7
![Page 9: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/9.jpg)
Mwalimu alinikamata na akakasirika sana! Alinichapa viboko 20!
Rose, nitakukomesha uache utoro!
Nisame-he!
Alinichapa sana nikaumia, wazazi wangu wakanipeleka hospitali na nilishindwa kwenda shule wiki nzima.
Najisikia maumivu mwilini!
8
![Page 10: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/10.jpg)
Maumivu ya hisia
Stella! Kila siku wewe ni mchafu! Kwanini huwezi kuwa msa kama wanafunzi wengine?
Lakini mwalimu....
9
![Page 11: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/11.jpg)
Naona unataka kujifunza kufua! Sasa, nenda nyumbani kwa matroni ukafue nguo zake zote...
Na ndiyo maana umefeli mtihani wa hisabati, mjinga wewe!
Hakuna anayenijali! Sijui maisha yangu yatakuwaje!
Inaniumiza rohoni!
10
![Page 12: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/12.jpg)
Madhara ya kitabia
Peter, nilikwambia ufagie darasa. Bado tu!
Mwalimu… nita….
Mvivu wewe! kalete fagio na ufagie sasa hivi!
11
![Page 13: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/13.jpg)
Baadaye siku hiyo…
We mpumbavu! Huwezi kucheza, uko legelege!
Embu leta maji yako! Nina kiu!
Kwanini mimi tu? Kosa langu nini?
Inasababisha nifanye mambo
mabaya
12
![Page 14: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/14.jpg)
Madhara ya kimahusiano
Hassan, funga domo lako! Na uache kusukuma kiti cha Hasifa!
Hassan, inatosha! Sasa ngoja nikufundishe adabu! Hebu peleka tofali 100 kule kilimani!
Namchukia! Na nitaendelea kumchokoza kila siku!
13
![Page 15: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/15.jpg)
Wiki iliyofuata…
Hassan, hebu acha kutupa ovyo karatasi! Kumbe hukukoma wiki iliyopita?
Hassan, hebu niambie nini tatizo lako? Kwanini wewe msumbufu?
Ungejua ninavyokuchukia!Sina jinsi tu!
Inanifanya nisiamini watu!
14
![Page 16: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/16.jpg)
Ugumu wa kujifunza
Haya...Fatima, jibu?
Hivi hili darasa lina tatizo gani? Ni mara ngapi nimefundisha jambo hili?
Fatima, njoo hapa! Sasa ninawashikisha adabu muwe wasikivu!
15
![Page 17: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/17.jpg)
Aisee! Fatima naona umelamba viboko!
Yaani, ninajisikia woga darasani! Ninaho a mwalimu ataniuliza swali huku sijui jibu!
Ninasoma kwa bidii, lakini nimekuwa mwoga kuongea darasani!
Ninatamani walimu wangeacha kututisha!
16
![Page 18: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/18.jpg)
WIKI ILIYOFUATA
Nimesoma vya kutosha! Sasa niko tayari kujibu maswali!
Fatima, jibu?
17
![Page 19: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/19.jpg)
We binti mjinga! Unajua kuwa nitakuchapa, na bado hutaki kujibu!
Najua hali hii itaendelea kutokea, sijui nifanyeje?
Inanifanya nishindwe kujifunza.
Ninajihisi mjinga
18
![Page 20: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/20.jpg)
Adhabu ya kupigwa huwafanya watoto kujisikia vibaya…Lakini bado watu wazima wanatoa sababu za kuendelea kutumia adhabu hii.
Sababu
Sababu
Sababu
Sababu Sababu
SababuSababu
Sababu
19
![Page 21: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/21.jpg)
Sababu
Kama mtoto hakuogopi, kamwe hatakuheshimu!
Mshenzi wewe! Jifunze kuheshimu wakubwa!
Lakini huwezi kumlazimisha mtu kukuheshimu!
Hicho kichapo kitakufanya uniheshimu!
20
![Page 22: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/22.jpg)
Heshimu watu! Watakuheshimu pia!
Mwalimu, hii hapa insha yangu ya mashindano.
Sa sana!
Asante! Naona umekusanya mapema!
21
![Page 23: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/23.jpg)
Sababu
Mwalimu mzuri ni yule anayedhibiti tabia ya mwanafunzi.
Nani anapiga kelele? Ninasikia kelele mpaka o sini kwangu!
Siyo mimi! Sielewi somo!
Kimya!
Wanafunzi huweza kukaa kimya kwa kuogopa adhabu…
22
![Page 24: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/24.jpg)
Mara vitisho vinapoondoka
Matokeo ya nidhamu ya woga...
23
![Page 25: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/25.jpg)
Walimu wazuri hawadhibiti tabia za wanafunzi kwa kuwachapa au kuwatukana.
Huwezi kudhibiti ubunifu… bali unaweza kuuchochea tu!
Ninadhani… Wazo zuri!
Na kuhusu hili?
U mbunifu sana!
24
![Page 26: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/26.jpg)
Sababu
Nilikuwa nikichapwa na imenifunza nidhamu nzuri!
SASA:
Lakini…
Hutoweza kuelewa sayansi, mjinga wewe!
Mimi mwenyewe sikuelewa sayansi, wewe mjinga ndo utaelewa!
25
ZAMANI:
![Page 27: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/27.jpg)
ZAMANI:
SASA:
Jaribu kuwaza jinsi ambavyo mafanikio yako yangeweza kuwa!
Sayansi ni ngumu kwako, hebu ngoja nikusaidie!
26
![Page 28: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/28.jpg)
Lakini mchelea mwana kulia, hulia mwenyewe!
Mithali ya biblia kuhusu viboko ilikuwa kwa nyakati zile…
Lakini, Agano Jipya husisitiza upendo na msamaha
Sababu
27
![Page 29: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/29.jpg)
Tunapaswa kubadilika kuendana na wakati.
Kamwe! Dini haiungi mkono kumlea mtoto kwa kumuumiza!
Maonyo huweza kuwa maneno au vitendo elekezi, na si viboko!
Na daima tusiache kuonya!
28
![Page 30: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/30.jpg)
Sababu
Viboko ni mila na desturi zetu! Hatutaki kukumbatia maadili ya nje!
Lakini mila na desturi zetu SIYO kuumiza watoto!
Huzingatia heshima, upendo na maelekezo
29
![Page 31: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/31.jpg)
Tunataka watoto wetu wakue na kupenda mapokeo yao...
...sio kuyaogopa!
30
![Page 32: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/32.jpg)
Sababu
Mtaka cha uvunguni sharti ainame!
Wanafunzi wangu wamefaulu mtihani kwa sababu waliweza kukariri kila kitu kwasababu ya kuogopa viboko!
Kweli? Hivi kweli wanaelewa?
31
![Page 33: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/33.jpg)
Salma, jana ulikariri namna ya kukokotoa hesabu ya eneo la mstatiri. Sasa namna gani unaweza kukokotoa eneo la mcheduara?
Kujifunza kwa viboko kunatulazimu kukariri!
Kweli, hatujifunzi namna ya ku kiri!
Tumekuwa wanafunzi mbumbumbu!
32
![Page 34: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/34.jpg)
Lakini tunatumia adhabu ya viboko kidogo tu inapobidi!
Sababu
33
![Page 35: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/35.jpg)
Jaribu ku kiria iwapo bosi wako atakuchapa ko , hata mara moja tu, kwa kuchelewa kumaliza ripoti. Utajisikiaje?
34
![Page 36: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/36.jpg)
Ninatumia adhabu ya viboko pale inaponilazimu tu!
Aaah...nimesahau homuweki yangu!
Duh! Pole sana Saad, leo utalambwa viboko!
Hapana, mwalimu hatanichapa ataniamini. .
SHULE
Sababu
35
![Page 37: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/37.jpg)
Saad! Umesahau homuweki yako! Hakuna njia nyingine ya kukumbusha!
Lakini nilikuamini! Ulisema hutatuchapa! Sikuelewi!
Alaa! Kumbe adhabu ya kumtandika mwanafunzi hudhoo sha kujiamini kwake!
36
![Page 38: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/38.jpg)
Kila mmoja anakubali, adhabu ya viboko haisaidii!
37
![Page 39: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/39.jpg)
Ulimwenguni kote, watu wameamua kuachana na adhabu ya kuchapa wanafunzi!
38
![Page 40: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/40.jpg)
Sera za kimataifa zinaeleza kuhusu maamuzi hayo ya dhati
Tamko la kimataifa
kuhusu haki za binadamu
Watoto wana haki za kiutu
na usawa wa kimwili.
Azimio la haki za watoto• Watoto wanapaswa
kulindwa dhidi ya
mambo yote ya kuwaumiza.
• Nidhamu shuleni
inapaswa kuzingatia
utu wa watoto.• Watoto hawapaswi
kutendewa vitendo
vya kinyama wala
kunyanyaswa.Kamati ya Haki za
Watoto
Achana na adhabu ya
kuchapa wanafunzi.
39
![Page 41: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/41.jpg)
Sera ya Afrika pia huzungumza kuhusu maamuzi haya thabiti.
Makubaliano ya Umoja wa Afrika
kuhusu haki za watoto na malezi bora.
Watoto wanapaswa kulelewa
kwa heshima na utu pindi
wanapoonywa nyumbani au
shuleni.
Makubaliano ya haki
za binadamu Afrika
• Watoto wana haki ya
utu na kuishi.• Watoto wana haki
ya kulindwa dhidi ya
uonevu.
40
![Page 42: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/42.jpg)
Sera ya Tanzania ina mkanganyiko
Katiba ya Tanzania• Binadamu wote huzaliwa huru, na
wote ni sawa.• Kila mtu anastahili heshima ya kutam-
buliwa na kuthaminiwa utu wake.
• Ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuad-
hibiwa kinyama au kupewa adhabu
zinazomtweza au kumdhalilisha.
Sheria ya Haki za
Mtoto, 2009
• Mtu yeyote hataruhusiwa kumfanya mtoto
apate mateso, au adhabu ya kikatili, au
afanyiwe matendo yenye kumshushia hadhi.
• Hakuna adhabu kwa mtoto inayokubalika am-
bayo haiendani na kiwango cha umri, afya /hali ya
mwili na akili yake. Hakuna adhabu inayokubalika
kwa mtoto mwenye umri mdogo asiyeelewa
kusudio la adhabu hiyo.
41
![Page 43: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/43.jpg)
Waraka wa Elimu, wa Serikali namba
24 wa mwaka 2002 unaruhusu viboko
japo imewekewa masharti:• Viboko ni kwa ajili ya makosa
makubwa tu. • Mwalimu mkuu ndiye mwenye
mamlaka kuruhusu kimaandishi.
• Viboko visizidi vinne na
viandikwe katika kitabu cha
kumbukumbu. • Mwanafunzi wa kike atachapwa
na mwalimu wa kike tu au
Mwalimu mkuu.
Licha ya kuridhia mikataba ya kimataifa ya haki za watoto, Tanzania bado inatumia adhabu hii!Waraka huu unapingana na Katiba na sera ya mtoto.
42
![Page 44: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/44.jpg)
Shule nzuri huzingatia sera za kimataifa, kitaifa na kikanda.
43
![Page 45: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/45.jpg)
Shule nzuri huunda sera inayopinga adhabu ya viboko kwa wanafunzi.
44
![Page 46: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/46.jpg)
Katika shule
Ninajisikia huru na ninalindwa!
Ninajifunza vizuri bila woga!
Ninaheshimiwa na ninaheshimu pia!
Shule nzuri HAINA adhabu ya kuchapa wan
45
![Page 47: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/47.jpg)
nzuri…
nafunzi! Je, shule yako ni nzuri?
Nina watu wazuri wanaonivutia kubadili tabia yangu!
Ninawaamini walimu!
46
![Page 48: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/48.jpg)
Je, unaweza kufanya nini kuhusu adhabu ya kuchapa wanafunzi?
• Amua kuachana na adhabu hii kwa kudhamiria moyoni.
• Jenga mazingira ya kuepuka adhabu hii shuleni.
• Jifunze kuhusu nidhamu isiyo ya uoga na kisha tumia mbinu za kusisitiza nidhamu hiyo.
• Wasikilize wanafunzi na kutatua matatizo yao.
• Jadili na watu wengine kuhusu faida za utulivu.
• Kuwa mbunifu! Jaribu kutumia mbinu mpya darasani.
47
![Page 49: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/49.jpg)
Jinsi ya kutumia kijitabu hiki…
• Soma kijitabu hiki pamoja na wanafunzi au walimu wengine. Kisha jadilini madhara ya adhabu ya viboko.• Fanya uta ti kuhusu sheria na sera zinazoongoza shule, wilaya, mkoa na nchi nzima kwa ujumla. Jadili undani wa sheria na sera hizo.• Fanya mijadala ukitumia sababu watu wanazotoa kuhusu kuendelea kutoa adhabu hii na kisha fafanua madhara yake. • Fanya maigizo kuhusu adhabu hii na kisha onesha jinsi watoto wanavyoadhirika kutokana na adhabu hii.• Shirikisha familia yako kujua athari za adhabu hii. • Tumia sera zinazopaswa kuzingatiwa ili shule iwe nzuri.
48Mchoraji : [email protected]
![Page 50: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/50.jpg)
49
Toa maoni, shiriki na
Kila baada ya miezi mitatu kwa mwaka 2012, maoni ya wanafunzi yatakayo-tumwa kupitia shule zao yatashindanishwa. Maoni kumi bora yatachaguliwa na yatachapishwa kwenye vitabu pamoja na tovuti. Kila shule itakayoshinda itapata kompyuta ndogo mbili (laptops).
Zawadi:
Msomaji, Serikali yako inataka kukusikia! Shiriki kwa kutuma maoni yako. Mawazo yako yanaweza kuboresha huduma kwa jamii na utawala bora. Pia, hii itakuza ushirikiano kati ya wananchi na Serikali. Maoni yako yatahusiana na mafunzo uliyopata kupi-tia kitabu hiki. Kigezo cha kupata washindi ni ubunifu au wazo jipya.
![Page 51: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/51.jpg)
50
jishindie kompyuta!Mwisho wa maoni yako weka taarifa zako:
a) Tareheb) Majina kamili, umri wako na jina la shule/taasisic) Jinsia - Mwanaume/Mwanamked) Anuani (SLP) kamili, makazi (Kata, Wilaya, na Mkoa)e) Simu yako na/au Barua pepe (kama unayo).
Unangoja nini! Shiriki basi kwa njia zifuatazo. Tuma kwa:
• Barua: OGP Ikulu, S.L.P 9120 Dar es Salaam• Barua pepe: [email protected] au [email protected]• Tovuti: www.wananchi.go.tz
Fikiria. Paza Sauti. Twaweza!
![Page 52: Adhabu ya viboko](https://reader031.vdocuments.mx/reader031/viewer/2022012308/588dbd4c1a28abdc4b8b82c6/html5/thumbnails/52.jpg)
Vibokohavifai!
Kuthaminiwa zaidi!
Kitabu hiki kimeandaliwa na:
Jadili na wenzio ulichojifunza humu au shiriki mjadala kupitia:
Twaweza_Nisisi
Twaweza Tanzania
www.twaweza.org www.raisingvoices.org